expedition
JF-Expert Member
- Jul 16, 2016
- 935
- 2,995
Kwako mbunge wangu Mh Medard Matogoro Kalemani na waziri kamili wizara ya nishati, kwa niaba ya wanachato wapenda CCM tunakuomba tu upumzike siasa na uwaachie wengine watakao weza kuleta maendeleo chanya jimboni kwetu.
Kwa muda wa miaka yako mitano kama mbunge wa jimbo letu pendwa naomba nikiri wazi hujafanya lolote wewe kama mbunge.
Shida za wanachato bado ni nyingi sana licha ya kwamba zinaweza kupatiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi tu.
Tukiacha miradi yenye ufadhili wa serikali kuu moja kwa moja kama vile ujenzi/uboreshaji wa hospitali ya wilaya pamoja na vituo na zahanati mbali mbali, uboreshaji wa shule, ujenzi wa chuo cha VETA na usambazi wa umeme vijijini wacha tuongeze na shule ya Nyabilezi inayojengwa kwa ufadhili wa Yoweli Museveni unaweza kutuambia wewe kama mbunge ni kipi hasa umefanya?
Sehemu nyingi za jimbo lako bado kuna shida kubwa sana ya maji ukianzia maeneo ya Buseresere, Bwanga, Njoo mpaka Mkungo na buzirayombo, Nyamirembe, Kibehe mpaka Muganza hadi Bwongera huku kote upatikanaji wa maji safi na salama bado ni shida kubwa sana licha ya kwamba tupo kando kando ya ziwa victoria linalohudumia mikoa ya shinyanga na Tabora.
Tuachane na suala la ajira maana hili ni janga la kitaifa na kwa nchi yoyote inayopitia kipindi cha mpito ili kuyafikia maendeleo ni lazima tu kundi fulani liumie ili badae wengi waje wafurahie ila sasa ni aibu sana kwa kushindwa ata kuweka barabara za mitaa jimboni kwako yaani pako zig zag tu. Hapa sisemie Chato mjini nazungumzia kata zote zilizo nje ya mji wa Chato.
Bado huduma ni mbovu sana katika hospitali yetu ya wilaya kwani watoa huduma hawako na spidi kubwa yaani unaweza wahi mapema asubuhi ila ukaondoka jioni saa kumi na moja bila kupata majibu ya vipimo ulivyopima.
wacha tu niishie hapa kwa leo ila ni mengi sana bado hujayafanya.
TUPISHE TU MHESHIMIWA.
UPDATES.
Hongera Dr Kalemani kwa ushindi wa kura za maoni ulioupata.
To be honest, binafsi sikupendi kabisa ila tu nakuunga mkono kwa maslahi ya Chama, Chama kwanza mtu badae.
Ushauri wangu hakikisha unatatua changamoto za jimbo letu hasa hasa suala la maji japo kuna watu wanasema eti Chato tuna maji ila ukweli tunaujua sisi wana Chato hasa tulio pembezoni mwa you wilaya yetu. Shida ya maji ni kubwa sana hakikisha unaitatua.
TUPO PAMOJA KWA MASLAHI YA CHAMA.
Kwa muda wa miaka yako mitano kama mbunge wa jimbo letu pendwa naomba nikiri wazi hujafanya lolote wewe kama mbunge.
Shida za wanachato bado ni nyingi sana licha ya kwamba zinaweza kupatiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi tu.
Tukiacha miradi yenye ufadhili wa serikali kuu moja kwa moja kama vile ujenzi/uboreshaji wa hospitali ya wilaya pamoja na vituo na zahanati mbali mbali, uboreshaji wa shule, ujenzi wa chuo cha VETA na usambazi wa umeme vijijini wacha tuongeze na shule ya Nyabilezi inayojengwa kwa ufadhili wa Yoweli Museveni unaweza kutuambia wewe kama mbunge ni kipi hasa umefanya?
Sehemu nyingi za jimbo lako bado kuna shida kubwa sana ya maji ukianzia maeneo ya Buseresere, Bwanga, Njoo mpaka Mkungo na buzirayombo, Nyamirembe, Kibehe mpaka Muganza hadi Bwongera huku kote upatikanaji wa maji safi na salama bado ni shida kubwa sana licha ya kwamba tupo kando kando ya ziwa victoria linalohudumia mikoa ya shinyanga na Tabora.
Tuachane na suala la ajira maana hili ni janga la kitaifa na kwa nchi yoyote inayopitia kipindi cha mpito ili kuyafikia maendeleo ni lazima tu kundi fulani liumie ili badae wengi waje wafurahie ila sasa ni aibu sana kwa kushindwa ata kuweka barabara za mitaa jimboni kwako yaani pako zig zag tu. Hapa sisemie Chato mjini nazungumzia kata zote zilizo nje ya mji wa Chato.
Bado huduma ni mbovu sana katika hospitali yetu ya wilaya kwani watoa huduma hawako na spidi kubwa yaani unaweza wahi mapema asubuhi ila ukaondoka jioni saa kumi na moja bila kupata majibu ya vipimo ulivyopima.
wacha tu niishie hapa kwa leo ila ni mengi sana bado hujayafanya.
TUPISHE TU MHESHIMIWA.
UPDATES.
Hongera Dr Kalemani kwa ushindi wa kura za maoni ulioupata.
To be honest, binafsi sikupendi kabisa ila tu nakuunga mkono kwa maslahi ya Chama, Chama kwanza mtu badae.
Ushauri wangu hakikisha unatatua changamoto za jimbo letu hasa hasa suala la maji japo kuna watu wanasema eti Chato tuna maji ila ukweli tunaujua sisi wana Chato hasa tulio pembezoni mwa you wilaya yetu. Shida ya maji ni kubwa sana hakikisha unaitatua.
TUPO PAMOJA KWA MASLAHI YA CHAMA.