Uchaguzi 2020 Dr. Kalemani pumzika tu, Ukweli Jimbo la Chato hujafanya chochote

Uchaguzi 2020 Dr. Kalemani pumzika tu, Ukweli Jimbo la Chato hujafanya chochote

Kwako mbunge wangu Mh Medard Matogoro Kalemani na waziri kamili wizara ya nishati, kwa niaba ya wanachato wapenda CCM tunakuomba tu upumzike siasa na uwaachie wengine watakao weza kuleta maendeleo chanya jimboni kwetu. Kwa muda wa miaka yako mitano kama mbunge wa jimbo letu pendwa naomba nikiri wazi hujafanya lolote wewe kama mbunge. Shida za wanachato bado ni nyingi sana licha ya kwamba zinaweza kupatiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi tu. Tukiacha miradi yenye ufadhili wa serikali kuu moja kwa moja kama vile ujenzi/uboreshaji wa hospitali ya wilaya pamoja na vituo na zahanati mbali mbali, uboreshaji wa shule, ujenzi wa chuo cha VETA na usambazi wa umeme vijijini wacha tuongeze na shule ya Nyabilezi inayojengwa kwa ufadhili wa Yoweli Museveni unaweza kutuambia wewe kama mbunge ni kipi hasa umefanya? Sehemu nyingi za jimbo lako bado kuna shida kubwa sana ya maji ukianzia maeneo ya Buseresere, Bwanga, Njoo mpaka Mkungo na buzirayombo, Nyamirembe, Kibehe mpaka Muganza hadi Bwongera huku kote upatikanaji wa maji safi na salama bado ni shida kubwa sana licha ya kwamba tupo kando kando ya ziwa victoria linalohudumia mikoa ya shinyanga na Tabora. Tuachane na suala la ajira maana hili ni janga la kitaifa na kwa nchi yoyote inayopitia kipindi cha mpito ili kuyafikia maendeleo ni lazima tu kundi fulani liumie ili badae wengi waje wafurahie ila sasa ni aibu sana kwa kushindwa ata kuweka barabara za mitaa jimboni kwako yaani pako zig zag tu. Hapa sisemie Chato mjini nazungumzia kata zote zilizo nje ya mji wa Chato. Bado huduma ni mbovu sana katika hospitali yetu ya wilaya kwani watoa huduma hawako na spidi kubwa yaani unaweza wahi mapema asubuhi ila ukaondoka jioni saa kumi na moja bila kupata majibu ya vipimo ulivyopima. wacha tu niishie hapa kwa leo ila ni mengi sana bado hujayafanya. TUPISHE TU MHESHIMIWA.
Kwako mbunge wangu Mh Medard Matogoro Kalemani na waziri kamili wizara ya nishati, kwa niaba ya wanachato wapenda CCM tunakuomba tu upumzike siasa na uwaachie wengine watakao weza kuleta maendeleo chanya jimboni kwetu.

Kwa muda wa miaka yako mitano kama mbunge wa jimbo letu pendwa naomba nikiri wazi hujafanya lolote wewe kama mbunge.

Shida za wanachato bado ni nyingi sana licha ya kwamba zinaweza kupatiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi tu.

Tukiacha miradi yenye ufadhili wa serikali kuu moja kwa moja kama vile ujenzi/uboreshaji wa hospitali ya wilaya pamoja na vituo na zahanati mbali mbali, uboreshaji wa shule, ujenzi wa chuo cha VETA na usambazi wa umeme vijijini wacha tuongeze na shule ya Nyabilezi inayojengwa kwa ufadhili wa Yoweli Museveni unaweza kutuambia wewe kama mbunge ni kipi hasa umefanya?

Sehemu nyingi za jimbo lako bado kuna shida kubwa sana ya maji ukianzia maeneo ya Buseresere, Bwanga, Njoo mpaka Mkungo na buzirayombo, Nyamirembe, Kibehe mpaka Muganza hadi Bwongera huku kote upatikanaji wa maji safi na salama bado ni shida kubwa sana licha ya kwamba tupo kando kando ya ziwa victoria linalohudumia mikoa ya shinyanga na Tabora.

Tuachane na suala la ajira maana hili ni janga la kitaifa na kwa nchi yoyote inayopitia kipindi cha mpito ili kuyafikia maendeleo ni lazima tu kundi fulani liumie ili badae wengi waje wafurahie ila sasa ni aibu sana kwa kushindwa ata kuweka barabara za mitaa jimboni kwako yaani pako zig zag tu. Hapa sisemie Chato mjini nazungumzia kata zote zilizo nje ya mji wa Chato.

Bado huduma ni mbovu sana katika hospitali yetu ya wilaya kwani watoa huduma hawako na spidi kubwa yaani unaweza wahi mapema asubuhi ila ukaondoka jioni saa kumi na moja bila kupata majibu ya vipimo ulivyopima.

wacha tu niishie hapa kwa leo ila ni mengi sana bado hujayafanya.
TUPISHE TU MHESHIMIWA.
Ungeeleweka kama ungemtaka mtangulizi wake awapishe kwa kutofanya lolote miaka 20 akiwa Mbunge na Waziri na miaka 5 akiwa Rais akizunguka na mabulungutu ya fedha akigawa kama njugu kwa watu wasio wa nyumbani. Mpeni huyo miaka mingine 5 atawafanyia maajabu ikiwa ni pamoja na flyover kama Ulaya mkimtupilia mbali mtangulizi wake aliyeahidi kuwatua ndoo ya maji wanawake kumbe ana maana ndoo tupu.
 
ila naweza kusema watanzania hawariziki,,imagine mwananchi wa chato nae analalamika hawajafanyiwa maendeleo jimboni kwao,,,,
Aisee na mimi nimestuka sana, hawa watu wa chato ndo watu wamepata neema kuliko majimbo yoote hapa Tanzania kwa hawamu hii, suala la umeme wamesambaziwa hadi kwenye vibanda vya nguruwe, mbuzi, ng'ombe na kuku huku majimbo mengine tukiendelea kusalia kwenye giza, sasa huyu naona anakufuru maana kumbe wamejengewa na hospital, Veta nk
 
Wewe umeshawahi kumiliki kibanda hata cha Room 1?je matumizi ya manunuzi ya umeme unayajua?kila mteja anayenunua umeme anakatwa asilimia ambazo zinaenda kuingia kwenye umeme wa Rea,umeme wote unaouona WANANCHI ndiyo wamewasambazia wanyonge wa vijijini, Serikali haijatoa hata Senti, na Rea haijaanzia awamu ya tano.
ACHA ujinga mdudu wewe, umeme hauvuki 10,000. kwa mita moja kwa mwezi iwe Mjini au vijijini
unakumbuka majenereta yalivyounguruma mijini? je yale yaliyokamatwa na JPM
ulichangia nini Tanesco au maisha yako yote wakati Herbiner Sigh na Ruge waliimaliza Tanesco?
wako waliochota mabilioni Benki ya Standard kwa canter kw nini hayakujenga kwenu hiyo REA hizo awamu nyingine
Tunazungumzia Dr Kalemani, anaitumikia Tanzania sio Chato, kamuulize Prof Muhongo na wenzake km waliiweza Wizara hiyo
 
Aisee na mimi nimestuka sana, hawa watu wa chato ndo watu wamepata neema kuliko majimbo yoote hapa Tanzania kwa hawamu hii, suala la umeme wamesambaziwa hadi kwenye vibanda vya nguruwe, mbuzi, ng'ombe na kuku huku majimbo mengine tukiendelea kusalia kwenye giza, sasa huyu naona anakufuru maana kumbe wamejengewa na hospital, Veta nk
yaani kuna mijitu mijinga sana YANAPINGA KILA KITU mpaka wanataka kuondoa neema Jimboni kwao
wamepewa mpaka Traffic Light, magari hakuna wamepewa Mabenki hawaweki pesa humo, barabara za taa, uwanja wa ndege, Kiwanja cha mpira kikubwa kuliko vyote.
Eti Mbunge Dr Kalimani hafanyi kazi hatuna maji, aache kuzunguka Tanzania
Wakaangalie Majimbo km Hai, Vunjo, Rombo hata taa za barabarani hawana, traffic light hakuna vichochoro vya lami, kiwanja tu cha mpira wanatumia cha Chuo cha Ushirika Mkoa hauna
Leo mnamsumbua Dr Kalemani
 
Na hatorudi hapo chato jinga Sana kashindwa kumtumia Magufuli kuleta maendeleo jimboni kwake,, naona watu wanaing'ong'a chato na wakazi wake Ni wivu tu endeleeni kuumia na kupata vidonda vya tumbo
 
Hongera Dr Kalemani kwa ushindi wa kura za maoni ulioupata.
To be honest, binafsi sikupendi kabisa ila tu nakuunga mkono kwa maslahi ya Chama, Chama kwanza mtu badae.

Ushauri wangu hakikisha unatatua changamoto za jimbo letu hasa hasa suala la maji japo kuna watu wanasema eti Chato tuna maji ila ukweli tunaujua sisi wana Chato hasa tulio pembezoni mwa you wilaya yetu. Shida ya maji ni kubwa sana hakikisha unaitatua.

TUPO PAMOJA KWA MASLAHI YA CHAMA.
 
Back
Top Bottom