Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
- Thread starter
- #21
😋😋😋😋😋acheni kutishana tuendelee kujadili mada, muda unakwenda.hahahaha noma sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😋😋😋😋😋acheni kutishana tuendelee kujadili mada, muda unakwenda.hahahaha noma sana
Mkuu umeelezea vitu vidogo sana, umesahau kuwaelezea wale wenye uwezo lakini bado hawawezi kufanya vumbuzi wala tafiti zozote."Repetion is a mother of learning and a father action." Tuache vingizio, elimu ya nchi hii imevurugwa na mikono ya wanasiasa, ni siyo suala lugha. Mwafrika anao uwezo mkubwa sana wa kujifunza kwa lugha yoyote ile, bila tatizo. Elimu yetu ya GPA za hongo ndiyo kansa inayotutafuna taratibu.
😁😁😁😁😁😁🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌madawati sio tatizo mkuu, watu wazamani walisoma bila madawati."Tatizo sio madawati Kama wasemavyo wanasiasa, tatizo sio vitabu Kama wasevyo wa-Dodoma tatizo elimu mbovu kama mfumo wa TFF"Bonta maarifa
Wamefanya mengi ila mikono yao hao wanasiasa, imeyaweka kapuni hautokaa uyaone, Afrika ni zaidi ya uidhanivyo katika, ulingo wa kisiasa, katika siasa za kutembeza bakuli la kuomba misaada ugenini, wakati mali tunazo tumezikalia hapa nyumbani, tukilala wanachukua, wanawapelekea, asante kwa kupewa mikopo ya mashangingi yao ya kutembelea.Mkuu umeelezea vitu vidogo sana, umesahau kuwaelezea wale wenye uwezo lakini bado hawawezi kufanya vumbuzi wala tafiti zozote.
Lowasa alisema Elimu Elimu Elimu[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]madawati sio tatizo mkuu, watu wazamani walisoma bila madawati.
Vumbuzi na tafiti zinaenda sambamba na funding, serikali imetenga bajeti kiasi gani kwa ajili ya hawa wasomi wetu kufanya tafiti ? Ni kawaida sana kumkuta PhD holder kwenye field ya Telcom au Mechanical engineering etc. anakimbizana kwenye mabanda ya nguruwe ili apate additional income.Mkuu umeelezea vitu vidogo sana, umesahau kuwaelezea wale wenye uwezo lakini bado hawawezi kufanya vumbuzi wala tafiti zozote.
Hivi wewe ni mwlimu wa kiswahili nini,usilazimisge wenzio wasiotaka upumbavuTatizo la elimu ya Tanzania sio kukariri bali ni ugumu wa lugha inayotumika bila kuwekewa msingi mzuri katika lugha hiyo.
Kila kitu huja kwa kukariri lol. Bila kukariri huwezi kuelewa. Bila kukariri huwezi kujua kusoma na kuandika, bila kukariri huwezi kushika verbs, bila kukariri huwezi kuhesabu, bila kukariri huwezi kushika table ya kuzidisha. Bila kukariri huwezi kushika kanuni za kufanyia hesabu.
Hata calculator imekaririshwa kanuni.
Hata computer imekaririswa kanuni.
Hata roboti linakaririshwa kanuni.
Hata sofwares, programes zinazakaririshwa kanuni na definition.
Hata translator zanakaririshwa pia maana za maneno.
Ni hivyo tu. Tatizo la elimu yetu ni lugha tu.
Haya anazungumza Dr. Meneja wa makampuni.
Elimu ya Tanzania inajengwa kwa msingi wa lugha ya Kiswahili baadaye inachanganywa na lugha ya kiingereza.
Nirudie tena, elimu yetu inajengwa kwa msingi wa lugha ya Kiswahili baadaye inachanganywa na lugha ya kiingereza.
Wakuu naomba tusaidiane, hii sentensi inamaana gani? Yaani nikiwa naama kwamba wewe umeilewaje?
Kama tunapenda maendeleo ya kiuchumi kupitia elimu yetu tunapaswa kufanya jambo katika elimu yetu.
Pamekua na minong'ong'ono mingi kwamba elimu yetu ni ya vyeti tu ikiwa naama kwamba watu wanakariri tu na wala hawaelewi.
Maswali
Je, ni kwanini elimu yetu ni ya vyeti?
Je, ni kwanini wanafunzi hawaelewi?
Je, ni kwanini wanafunzi wanakariri?
Je, Wanakariri ili waweze kukuhifadhi kichwani walichofundishwa?
Je, Wanakariri ili waweze kuelezea wakipewa maswali kasababu tu hawawezi kuelezea kwa maneno yao wenyewe kwa kutumia lugha wanayotumia?
Je, ukiwambia waeleze kwa lugha ya kiswahili wataweza?
Tufanye nini katika elimu yetu, tutumie lugha ipi, tuanze kuitumia wapi ili kuweka msingi imara kwenye lugha ya kujifunzia.
Karibuni
Wao wana ukabila, na kinachowaunganisha wakiwa nje ya vijiji vyao ni lugha ya Kiingereza sisi ni Kiswahili. Kwa maana hiyo wao wanapokwenda vyuoni wanafahamu zaidi Kiingeza na maeneo yote wanatumia Kiingereza, vinginevyo hawataelewana. Tofauti na sisi ambapo mwanafunzi akitoka shuleni au chuoni Kiingereza anakiacha huko huko zaidi ya zile familia zenye uzungu uzungu. Ziko familia zenye uwezo wanapeleka watoto wao katika English medium schools, lakini wazazi wenyewe hawajui Kiingereza, unadhani pale nyumbani itatumika lugha gani?Mbona Kenya na Uganda wanatumia Kingereza hicho hicho elimu zao ni bora zaidi ya kwetu?
Wao wana tofauti gani na sisi?
Nchi zao ni kama sisi,tunafanana fanana....inakuaje wao wafanikiwe zaidi yetu?
Una hoja ya hili?
Usilete matusi lakini