Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU


That is my point exactly... Mwakyembe ... supastaa wa Bongo... kwikwikwi.....
 
Ni jambo zuri kudhihirisha u msafi.Ishu ni kwamba na wenyewe wanaotaka kuwahoji wenzao ku-prove usafi wao nao je ni wasafi? kazi ipo
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 52 (16 members and 36 guests)
Susuviri, Arnold, Buchanan, Edson, herikujua, Hofstede, Hujale, Jmpambije, JS, Kibunango, Limbani, Mfunyukuzi, Pilato2006, Shishye, Watu, Zitto
Time: 11.00 AM - Thursday

Namwona Mh yupo humu ndani... hivi mheshimiwa uko bungeni au? Maana naona you are surfing the internet saa za kazi.... tehehehe...hiyo nayo siyo kosa?
But seriously, kuna misdemeanor na makosa mengine ambayo yanaweza kushughulikiwa within the structure of the parlament, lakini ni uwendawazimu kuishikilia bango TAKUKURU kuhoji na kumkamata Mwakyembe kwa kosa la kupokea posho mara mbili.
 
kwani kuna tatizo gani kwenda kuwasikiliza, hofu ya nini?
jamani hawa wanasiasa wanatuchanganya sana ni wala rushwa sana , hakuna cha wapambanaji wa ufisadi hapa ni wote mafisadi kwa ujumla wao
ningewaelewa hapo bungeni kama wangekomaa na hata kujiuzulu kama alivyofanya mrema , serikali chafu na wabunge hatuna kabisa , nadhani hawafiki watano wenye moyo wa dhati kutetea umma wa tanzania
 
sio uchunguzi huu tu ambao unafanywa na takukuru. kesi ya liyumba pia ilichunguzwa nao ingawaje "kutumia madaraka vibaya" sio rushwa.inaonekana kuna matatizo ya kunyanganyana kazi za uchunguzi siku hizi, bado kidogo usalama wa taifa watakuwa wanafanya kazi hizi pia.

macinkus
 
Ukisoma thread hii unagundua wengi wetu hapa hatujui sheria hata zile za msingi.

Kwanza TAKUKURU hawashitaki case mahakami na hiyo ni kazi ya idara ya mashitaki, sijui jina wanaitwaje. Kazi ya Takukuru ni kuchunguza na kisha kuipeleka case kwa prosecutor. Kama kuna malalamiko au wasiwasi wa kosa kutendeka ni lazima polisi au hao Takukuru wakuhoji kwanza kabla ya kupeleka case kwa prosecutor.

Pili kuna hili suala la kuitwa kwa simu, sijui kwa TZ lakini kwa nchi zingine za Common Wealth kama UK ni mtindo wa kawaida mno (Mara nyingi kwenye sheria nchi zote za commonwealth hufuata taratibu zinazofanana). Unapigiwa simu na kuambiwa uende kituoni, mtu ukipata ujumbe kama huo unakimbia haraka kuongea na mwanasheria wako na kisha kwenda. Ukichelewa, wanaenda kuomba kibali cha kukukamata na wakipata, wanakuja kukuchomoa saa 11 asubuhi ukiwa kwenye mashuka na si ajabu wanawatonya na waandishi wa habari ili uumbuke zaidi. Ndio maana walio wengi wanaenda wenye haraka ili kuondoa madhara ya wao kukufuata kuja kukuchukua.

Dr. Mwakyembe ni mwanasheria kwahiyo huenda kuna mambo anayajua zaidi ya sisi tusiojua kitu. Wacha tuendelee kufaidi hii sinema mpaka mwisho wake tutajua ukweli wake.

Ila kama sio mjuzi wa sheria usije ukafanya huo mchezo wa Mwakyembe maana utakuja kukuweka pabaya. Polisi wana madudu yao mengi sana, wanaweza kukukamata Ijumaa jioni ili tu usipate dhamani mpaka Jumatatu na uwe umeonja karaha za mahabausu. Kinachotakiwa ni kujua haki zako lakini pia kutokubishana na polisi pasipo na msingi. Ikiwezekana mwachie mwanasheria wako ndio afanye hiyo kazi.
 

Susuviri,

Jina kuonyesha yupo kwenye active user haina maana kwamba yupo actively aki surf net au akisoma thread husika. Kwa mtu mkongwe JF kama wewe unatakiwa ulijue hili.

Kama hujui nafikiri unahitaji tuition toka kwa Invisible.

Kama huja log out jina lako linaendelea kuonekana. Pia kuna watu wengine hasa nje ya TZ ambao PC zao muda wote zinakuwa on na wao kama haja log out jina lake linaendelea kuonyesha hata kama yeye kasafiri.
 
mimi ambacho kinanishangaza, si hoja ya kukamatwa Mwakyembe. ila ni vile gazeti la Mtazania lilivyogeuka kuwa jukwaa na PCCB , kutolea taarifa, ni kwanini habari hizi zinafika kwanza Mtanzania kisha kusambaa kwa magazeti mengine, ? ooh sorry kumbe hili gazeti linamilikiwa na watuhumiwa wa Ufisadi, kwa hiyo ipo mikakati kati ya Hosea, RA, NA mzee wa Monduli.
 
Mheshimiwa Zitto anachosema ni sawa kabisa. Dr.Mwakyembe kama kiongozi wa juu nchini kwetu angefanya busara kwa kwenda Takukuru na kuhojiwa hata kama Takukuru walikuwa na hila ndani yao. Hata kama Mwakyembe ana haki ya kutokwenda kuhojiwa iwapo anafikiri hatotendewa haki angeitikia wito na kuweka bayana kwamba anakwenda shingo upande ( under protest). Nchi itaendeshwaje iwapo kila mtu atasema "siendi kuhojiwa maana nahisi sitatendewa haki na chombo husika". Dr. Mwakyembe ni mtu mahiri na angekubali kuhojiwa nafikiri Takukuru wangeondoka kwenye mahojiano wakishika pua zao! Tena tusisahau EL alimlalamikia Dr. Mwakyembe kwa kutomwita kumhoji wakati wa uchunguzi wa Richmond! Hivyo kuhojiwa ni kitu muhimu sana hata kama kuna hila. Tunaongoza kwa kuonyesha mfano tena ulio mzuri and I do not believe this was done by the honourable MP this time around.
 
.

Pasco.

soma taarifa zote za nyuma na ndipo uandike hivyo.bunge lilitaarifiwa kuhojiwa kwa wabunge na barua zipo.lakini sitta anasema alikuwa hajui.sasa kama barua zipo,ambazo zinataka wabunge wahojiwe na zimejibiwa na katibu wa bunge,sasa wewe unataka taarifa gani?
 

Mkuu majibu unayo, karata zinachezwa na pengine mwakyembe akalamba dume!

Wakati JF tunaringia uhuru wa kuzungumza freely, EL, RA na washabiki wao wanaringia uwezo wao wa fedha kufanya kazi.
 

Vipi na zile taarifa zinazoyafikia haraka sana yale magazeti ya yule fisadi nyangumi(mengi)?.Utasikia ohoo mwakyembe aliatakuchomwa kisu,mwakyembe ni mti mkavu hauchimbwi dawa?. hiyo yote nini bwana.wewe chapa kazi wananchi watakurudisha jimboni na sio media.
 
Huyu Hosea ndio aliwasafisha wale matapeli wa Richmond then akawa busted lakini cha ajabu hakuna chochote kilichomtokea,huyu anatakiwa kuwa jela sasa hivi ,wapuuzi kama hawa ndio wanatumaliza na hakuna chochote wanafanya zaidi ya kugeuza chombo muhimu kama PCCB/TAKURURU kuwa cha kisiasa na revenge kwa wote wanaoonekana kama ni hatari kwa serikali yao...kuna rushwa za mabilioni kila siku lakini hakuna prosecution yeyote kila siku ni kanyaboya tuu hawa matapeli wa TAKURURU,huyu Hosea lazima aondoke!
 


kila mtu anakimbilia kwenye nafuu anakoona anakubalika, haiwezekani Mwakyembe aitishe press conferess bila ya ITV na washirika wake. Mwakyembe, Mengi, Kimaro, Selelii, Sendeka wooote kundi moja. Serukamba na wenzie utawaona huko kwingine. . . ..

Ndo mchezo huo, Marando anauita Media politics!
 
Hivi mtu yeyote akihisi hatatendewa haki na vyombo vya dola km Polisi, PCCB, Mahakama, etc ndio usiende ukiitwa? Kama kasheria hako kapo Msomi Mwakyembe atujulishe na sisi tuwe na uchaguzi wa vyombo vya kutushughulikia! Nikihisi Mahakama haitanitendea haki hakuna haja ya kupata shida, unawaarifu tu kwamba huendi, waendelee na shughuli zao! Life made simple!
 

Akawasikilize kina nani? Kwani wao PCCB rushwa wanazopokea nani huwa anawahoji? The point ni kuwa yeye Hosea,uchafu wake kausafisha lini,na kama kupokea posho mara mbili ni rushwa,vipi wao PCCB wanapojaza Imprest za uongo na wanajidai kwenda kukamata watuhumiwa wa rushwa,kisha wanaishia kwenye mabaa kubwia maji ya Ilala (beer) nani huwa anawahoji? Tunaishi nao,na tunawafahamu vizuri sana.
 

Masikini Tanzania....na huyu naye atakuja hapa kukaripia ufisadi....kweli ufisadi ni kansa ya akili iliyosambaa kila pande ya nchi yetu

omarilyas
 
Masikini Tanzania....na huyu naye atakuja hapa kukaripia ufisadi....kweli ufisadi ni kansa ya akili iliyosambaa kila pande ya nchi yetu

omarilyas

Mkuu wangu,pana pending issues ngapi ambazo ni serious PCCB hawajazishughulikia? Badala yake wanakimbilia kwenye issue za posho? What about Richmond,EPA et al,wao kama PCCB wamefanya nini mpaka sasa?
 
Nasubiri nione video yenyewe, sidhani kama Stering atakufa ili kuharibu picha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…