Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Hivi kwa nini Dkt Mwakyembe amesikia maumivu zaidi (hata kutetemeka wakati anaongea na waandishi wa habari) kuliko Wabunge wenzake waliohojiwa? Au yeye (Dkt Mwakyembe) alikwapua nyingi zaidi ukichanganya na zile fedha za matibabu hewa alizotia ndani?
 

Wewe nawewe nimbunge au? nawewe unapokeaga bahasha (posho) marambili kwa kazi moja? Hapa nikuwapongeza hao TAKUKURU kwakutake initiative za kutokomeza hayo 'mazoea' ya wabunge kufanya mambo kinyume na sheria, Pili nadhani huo nimwanzo mzuri wa TAKUKURU kutekeleza majukumu yake ya kusafisha hali ya rushwa ambayo nimbaya sana Tanzania, wabunge hawalioni hili kwasababu linawagusa wao moja kwa moja
 
Hao TAKUKURU....do they really mean business? Or something is to happen at the background?
 
Hao TAKUKURU....do they really mean business? Or something is to happen at the background?

Nafikiri angalia uhalali wa hizo posho zaidi! Otherwise, jiulize pia kama "wapambanaji" nao wako serious kwa kupokea malipo zaidi ya mara moja kwa kazi moja! Ni sawa na kulipwa mishahara miwili kwa kazi ile ile! Kanchi ketu kazuri jamani, wakati kuna watu wanapokea malipo mara mbili kuna wengine hawana uhakika na mlo mmoja kwa siku! Ukitaka kuwajua wabunge wetu gusa maslahi yao! Tunakumbuka juu ya hoja ya Dkt Slaa juu ya kupunguziwa posho zao! Hapa hakukuwa na Kilango, Seleli, Mwakyembe au nani! They were totally against the idea! Kaazi kweli kweli!
 
Unamkumbuka Dr. Masumbuko Lamwai- unakumbuka alivyokuwa anatesa na Sheria zake za Kidokta yuko wapi.

.
Huo sasa ni uonevu kwa kuwataka watu wasiseme hata kama ni sheria. sasa tutaendekeza hali ya kuogopa mpka lini?
 
Hawa MPs bado hawajakoma kuimba wimbo wa takrima? Wameuhamisha toka kwenye uchaguzi wameuingiza kwenye vikao ili kupata posho mara mbili kwa kazi moja? Ndio maana vikao vinaendeshwa kila siku: too much talking for Tanzanians! Kaazi kweli kweli!
 
Kwenye gazeti la Mtanzania leo kuna habari kwamba Mbunge wa Kyela atakamatwa na TAKUKURU ambayo imesema kwamba mbunge huyo hayuko juu ya Sheria! Kwa kuwa habari niliyo nayo ni ya kusikia toka kwenye Redio (RFA) naomba mwenye nakala ya gazeti hilo amwage data zaidi!
 

Du! kazi kwelikweli, PCCB wameanza kuonekana wanajua kazi kwa kuanzia bungeni!! mangapi yamelala pale............. majibu hakuna.
 
Kwa maoni yangu, Mwakiembe hakamatiki kwa ajili ya matamshi yake ya Dodoma, unless PCCB walimtaarifu spika kwa maandishi kuwa wanamuhitaji Mwakiembe kwa mahojiano, huku Mwakiembe mwenyewe amepelekewa samansi ya PCCB kuitwa kwa mahojiano,akakaidi, ni kweli anakamatika.
 
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA IMEFIKIA UAMUZI WA KUMKAMATA MH Dr H. MWAKYEMBE KWA KUKAIDI WITO WA KWENDA KUOJIWA KWA KUPOKEA POSHO MARA MBILI KWA KAZI MOJA.... DUH KAMA NI KWELI BASI MWAKYEMBE HATA JIMBO UTAKOSA SASA
 

Can you revisit my posting?
Nilisema nilitegemea zoezi liwe random. Majibu yako yanonekana kama umeelewa kinyume cha mambo.

Uchunguzi ulianza February, OK! Kwa nini? Utasema PCCB wanaruhusiwa kisheria, Fine! But what a coincidence in its happening?

You are possibly right, hebu niambie tangu waanze wamekwisha muhoji waziri yupi?

Lakini pia bila kujali kisingizio cha uchunguzi unaoendelea, unaweza kutueleza ni kwa nini kulipwa posho hizi imekuwa ni notorious habit among the so called waheshimiwa?
Tusitetee uzembe wowote hata kama tumeshaukubali. iwe ni kupokea posho za ziada au hata kutojua na kujukuta ukihojiwa kwa kudhalilishwa.

Ni tabia mbaya na hasa ukizingatia kwamba mashirika na ofisi zinazotoa posho hizo, zinawategemea hao hao wabunge kuweza kupata utetezi bungeni.

Hata hivyo tatizo langu hukulieleza. Kwa nini sasa? Kwa nini kwa wabunge baada ya kuwa na mijadala ya RICHMOND? Baada ya kuitaka mara nyingi serikali ichukuwe hatua juu ya tabia ya PCCB over Richmond. Whatever sense you may make out of the exercise, it can’t defeat a normal human common sense.
 
Nami nimeona katika star tv magazeti. Pccb katika hili la kumkamata wamechemsha. Kwanza wabunge tuna kinga katika tunayosema si tu ndani ya ukumbi bali pia katika viunga vya bunge. Takukuru hawana mamlaka ya kumkamata mbunge kwa matamshi aliyoyatoa kwenye press conf iliyofanyika kwenye viunga vya Bunge. Wanajimwambafy tu, hawana uwezo huo. Jambo la msingi ni wao kuhakikisha wito wao unaitikiwa na wabunge na kupata maelezo yao. Ni muhimu wabunge kuonyesha jamii kuwa hatuna mawaa katika mienendo yetu. Kuhojiwa na kutoa ushirikiano ni hatua mojawapo ya kuithibitishia jamii kuwa tu wasafi.
 
RA yeye huwa hasaini "viposho" hivi. Alishajizolea zake nyingi mapema. Zitto msiwaache MAWAZIRI wetu. Wao wanachota nyingi zaidi. Ni kufuru!
 


Mkuu Zitto nimekupata hapa, lakini pia hili linawezekana tu pale PCCB watapofuata utaratibu unaokubalika sio kukurupuka tu kwamba leo tunamtaka fulani basi wanapiga simu kumuita.

Nina amini msimamo wa Mwakyembe kukataa kuhojiwa ni sahihi na kwamba utafungua njia mpya ya hawa watu kuacha kutaka kunyamazisha watu fulani eti kuwa tu wana mamlaka ya kuwanyamazisha
 
Mawaziri wanaongoza kuchukua posho mara mbili. Kama mnabisha nendeni halmashauri mkaulize.
 
Naombeni kuuliza vipi kuhusu ile tume/kamati aliyounda Mh Mwakyembe ya sakata la rushwa la Richmond???iliishia wapi?nadhani siko off point sana wadau mnisamehe kama niko off point.
 
muda si mrefu wataanzisha kyelastan hawa ... teh teh teh teh
mzee kyela haiwezi fika uko, we subiri hio 2010 utaprove kuwa Mwakyembe ni simba wa kyela.
Hivi tangu lini mtu mwizi, huyo aliyeshindwa kuchunguza richmond leo aje awachunguze wale waliomgundua kuwa yeye ni mwizi na mbabaishaji. Hapa ndio utangundua jinsi viongozi wetu walivyowasanii, unaona kuwa mambo ya richmond kimya sasa yameanza ya akinamwakyembe. nafikiri tumalize kwanza richmond halafu mengine yaje yafuate. halafu hata mawaziri pia wahojiwe maana nao ni wabunge. hapa waanzie kwa pinda mwenyewe.
 
Mawaziri wanaongoza kuchukua posho mara mbili. Kama mnabisha nendeni halmashauri mkaulize.
Nakumbuka hili lilitokea Karatu (ambako Halmashauri inaongozwa na Chadema) madiwani walikataa kulipia malazi ya ujumbe wa Makamu wa Rais kwa vile tayari walisha lipwa posho na ofisi zao walikotoka.
 
nilijua kuwa lazima roho itakuuma kuona mwakyembe anasimama yeye kama yeye na kuonyesha njia, huo ndio uongozi na sio kufuata mkumbo tu. Tungekuwa na rais kama mwakyembe tungekuwa mbali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…