Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Nami nimeona katika star tv magazeti. Pccb katika hili la kumkamata wamechemsha. Kwanza wabunge tuna kinga katika tunayosema si tu ndani ya ukumbi bali pia katika viunga vya bunge. Takukuru hawana mamlaka ya kumkamata mbunge kwa matamshi aliyoyatoa kwenye press conf iliyofanyika kwenye viunga vya Bunge. Wanajimwambafy tu, hawana uwezo huo. Jambo la msingi ni wao kuhakikisha wito wao unaitikiwa na wabunge na kupata maelezo yao. Ni muhimu wabunge kuonyesha jamii kuwa hatuna mawaa katika mienendo yetu. Kuhojiwa na kutoa ushirikiano ni hatua mojawapo ya kuithibitishia jamii kuwa tu wasafi.

Mheshimiwa Zitto tunaomba vifungu (kanuni za bunge, katiba au sheria nyingine yoyote) vinavyotoa hiyo kinga maana hapa kidogo mnatuchanganya, hasa mnapozungumzia kinga sasa hivi, huku hamkusema chochote kuhusu kinga ya mbunge hasa pale Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba (kesi ya misamaha ya kodi) na Mheshimiwa Andrew Chenge (kesi ya kusababisha ajali) walipohojiwa na kesi zao kwa sasa ziko mahakamani!
 
Naombeni kuuliza vipi kuhusu ile tume/kamati aliyounda Mh Mwakyembe ya sakata la rushwa la Richmond???iliishia wapi?nadhani siko off point sana wadau mnisamehe kama niko off point.
na mie pia nasubiri kusikia majibu katika hili swali lako
 
Mheshimiwa Zitto tunaomba vifungu (kanuni za bunge, katiba au sheria nyingine yoyote) vinavyotoa hiyo kinga maana hapa kidogo mnatuchanganya, hasa mnapozungumzia kinga sasa hivi, huku hamkusema chochote kuhusu kinga ya mbunge hasa pale Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba (kesi ya misamaha ya kodi) na Mheshimiwa Andrew Chenge (kesi ya kusababisha ajali) walipohojiwa na kesi zao kwa sasa ziko mahakamani!

Kuhusu kinga ya mbunge, mkuu, mi nakubaliana nalo kwani linamkinga mbunge awe huru kufanya maamuzi na kuongea kwa uwazi, sasa kama tayari tunaona kuwa TAKUKURU imetumika kutishia na kunyamazisha baadhi ya wabunge kama akina Mwakyembe, kama sheria ingeruhusu ingekuwa ni standard practice.

Mh Zitto, kutoa ushirikiano ni sawa, ila kumbuka kwamba inabidi kupima kama wito ni wa maana au la, vinginevyo unaweza kujikuta unaenda kwa ushirikiano, alafu ukakuta wapiga picha wakikutoa na kifulana na jeans wakidai "Mh akamatwa na TAKUKURU" Nadhani we unaelewa fika kwamba hapa kuna mchezo mchafu na kila hatua unayopiga kama mbunge ni lazima upime.

Nilishasema kwenye thread nyingine, wakijaribu kumkamata Mwakyembe, watakuwa wanajenga sifa na carrier ya Mwakyembe, na atakuwa ni STAR! Tehehehe. Mi ningekuwa Mh Mwakyembe ningewasubiri kwa hamu na kuwaita waandishi.... it is a great oportunity kuonekana kama mpiganaji...... nadhnai Mh Zitto knows what I mean..... he seized that opportunity kujijengea sifa kubwa na jina.... that is the game....
 
Nami nimeona katika star tv magazeti. Pccb katika hili la kumkamata wamechemsha. Kwanza wabunge tuna kinga katika tunayosema si tu ndani ya ukumbi bali pia katika viunga vya bunge. Takukuru hawana mamlaka ya kumkamata mbunge kwa matamshi aliyoyatoa kwenye press conf iliyofanyika kwenye viunga vya Bunge. Wanajimwambafy tu, hawana uwezo huo. Jambo la msingi ni wao kuhakikisha wito wao unaitikiwa na wabunge na kupata maelezo yao. Ni muhimu wabunge kuonyesha jamii kuwa hatuna mawaa katika mienendo yetu. Kuhojiwa na kutoa ushirikiano ni hatua mojawapo ya kuithibitishia jamii kuwa tu wasafi.

Mh Zitto, naomba utufumbue macho kidogo. Hawa jamaa wa PCCB wanahoji nini? Maana sioni kama suala la kuchukua posho mara mbili linahitaji mahojiano ili kulithibitisha! Wabunge wanapochukuwa posho hizi huwa wanasaini? Haya mashirika ambayo yamekuwa yakitoa posho hizo, huwa zinatoka kwenye fungu gani? Auditors wamewahi kuzihoji?
 
Wanajamii,
Kwa mtazamo wangu bila kupendelea upande wowote, nafikiri TAKUKURU itakuwa inachemka. Ki sheria nafikiri haina haki ya kukamata bali kama ina kitu chochote cha kushitaki ni kupeleka mahakamani, labda kama ni "sheria ya siasa".
Pili, Mhe. Mwakyembe hakukufanya uchunguzi peke yake na hakujiteua. Hii ina maana huwezi kumwita Mhe. Mwakyembe kana kwamba ni "Mwakyembe" kama mtu au Mbunge, inabidi uombe Mhe. Spika kutaka kuhoji Kamati (ingawa imekuwa hivyo tangu zamani) na si mtu.
Tatu, sheria hii haizingatii immunity ya mtu?
Nafikiri kuna maswali mengi kuliko majibu.
Uchambuzi mwema!
 
Mi naona ili falsafa ya utawala bora iwe kweli utawala bora basi lazima wabunge na wanasiasa wajue kuwa kuutumikia umma sio kujilimbikizia mali kwa ujanja ujanja. Hii move iendelee mpaka mwisho maana ndo njia ya kujifunza nini mtu anaweza kufanya na nini usithubutu.
 
Kuhusu kinga ya mbunge, mkuu, mi nakubaliana nalo kwani linamkinga mbunge awe huru kufanya maamuzi na kuongea kwa uwazi, sasa kama tayari tunaona kuwa TAKUKURU imetumika kutishia na kunyamazisha baadhi ya wabunge kama akina Mwakyembe, kama sheria ingeruhusu ingekuwa ni standard practice.

Mh Zitto, kutoa ushirikiano ni sawa, ila kumbuka kwamba inabidi kupima kama wito ni wa maana au la, vinginevyo unaweza kujikuta unaenda kwa ushirikiano, alafu ukakuta wapiga picha wakikutoa na kifulana na jeans wakidai "Mh akamatwa na TAKUKURU" Nadhani we unaelewa fika kwamba hapa kuna mchezo mchafu na kila hatua unayopiga kama mbunge ni lazima upime.

Nilishasema kwenye thread nyingine, wakijaribu kumkamata Mwakyembe, watakuwa wanajenga sifa na carrier ya Mwakyembe, na atakuwa ni STAR! Tehehehe. Mi ningekuwa Mh Mwakyembe ningewasubiri kwa hamu na kuwaita waandishi.... it is a great oportunity kuonekana kama mpiganaji...... nadhnai Mh Zitto knows what I mean..... he seized that opportunity kujijengea sifa kubwa na jina.... that is the game....

SLOWLY BUT SURELY, nimeanza kupoteza imani yangu kwa Zitto: He can do anything to make ends meet, and this is really dangerous! Zitto, come back we need you. After all bado ni kijana, una nafasi ya kujisahihisha....ila maamuzi yako hivi karibuni yananitia shaka kwamba wewe ni kashushu ka kila upande (as long as you get paid)....BUT ask yourself, "FOR HOW LONG YOU WILL BE SAFE?" doing this kind of Hipocrity?
 
pccb bana,yaani wanaamka tu bila kupiga mswaki!!!!
 
Kwa kuwa kadhia hii ya Mwakyemebe imeshakuwa public intereset,nafikiri TAKUKURU watalishughulikia suala hili kwa uangalifu sana tofauti na wengi tunavyo fikiria!Kwanza TAKUKURU wanajua Mwakyembe ni Mwanasheria,pili Mbunge!Hawawezi kukulupuka na Kumkamata Mwakyembe kama anavyo kamatwa afisa mtendaji kwa kula rushwa ya shs 2000 pamoja na kuwa raia wote kisheria wapo sawa!
TAKUKURU ina wansheria wengi waliyobobea watakaa na kuchambua taratibu zote kupambana na "mkubwa"huyo !
 
Ni muhimu sana Mwakyembe akikubali kuhojiwa na kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU. Matumaini yetu ni kuwa TAKUKURU itakwenda mbali zaidi na kuhoji watu wengi zaidi katika Serikali na taasisi zake na kuhakikisha kuwa tabia ya watu kupokea Posho mara mbili au zaidi inakufa.
 
Hivi ni vita vya Hosea na Mwakyembe. Credibility ya uongozi nchi hii imepotea. For as long as Hosea ni head of PCCB, Hosea ni PCCB. Hao vijana wake wachapa kazi wanaotumwa naye hata wangekuwa wazuri vipi, lazima watekeleze matakwa ya bosi wao. Itakuwa ngumu kwa wabunge kufanya kazi na hii taasisi kwa moyo mweupe unless ni wanafiki, kwamba hawako 100% committed na maamuzi ya kamati ya Mwakyembe. Hali kadhalika uwazi wa Hosea na Wabunge lazima uwe na walakini. Ndio maana kajambo kadogo kama haka katakuzwa sana kutokana na historia hii.
 
imani na takukuru imekwisha kabisa, hata hii ya uwezekano wa kukamatwa kwa Mwakyembe inawezekana na mizengwe tuu time will tell, huwa wanajifanya wakali kama mbogo, lakini nyuma ya pazia ni something else

watu wanakamatwa wanahojiwa na kuachiwa na wengine wanafunguliwa mashtaka kwenye mahakama zilizojaa rushwa wakati wenyewe ndio chombo cha kuzuia rushwa. hatusikii mtu wa ngazi za juu kafungwa..

kama kweli wamejisafisha na wako serious watuonyeshe basi kwa vitendo,
 
Mheshimiwa Zitto tunaomba vifungu (kanuni za bunge, katiba au sheria nyingine yoyote) vinavyotoa hiyo kinga maana hapa kidogo mnatuchanganya, hasa mnapozungumzia kinga sasa hivi, huku hamkusema chochote kuhusu kinga ya mbunge hasa pale Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba (kesi ya misamaha ya kodi) na Mheshimiwa Andrew Chenge (kesi ya kusababisha ajali) walipohojiwa na kesi zao kwa sasa ziko mahakamani!
Buchanan, nadhani hapa wewe ndio umechanganya mambo mawili tofauti.

Mimi nimemuelewa Zitto. Kasema wabunge wana immunity kwa yale yote wanayozungumza ndani au nje katika viunga vya bunge.

Kesi za wakina Pesambili Mramba ni ya jinai na haihusikani kwa namna yoyote na masuala ya Bunge.
Ni kama vile ukiua mtu kama alivyofanya Dito na wewe ni mbunge usitegemee kupata immunity. Au ukivunja nyumba ya jirani yako hata kama wewe ni mbunge usitegemee kupata immunity.

Unakumbuka kesi ya wale wabunge wa Zanzibar walioghushi nyaraka za uhamiaji? ( ingawa sielewi ziliishaje mahakamani)? hapo hakuna cha immunity kaka/dada.
 
hii nchi ndugu zangu inamaajabu sana .
sasa wanataka kuwahoji wakina mwakyembe ili waweze kuwatisha wabadilishe misimamo
juu ya swala la richmond.
huyo hosea ni mtuhumiwa wa kuisafisha kutokana na rushwa sasa yeye anawatuma vijana wake ambao walishirikiana nae kuisafisha richmod kutoka katika swala la rushwa.
na wanawahoji watu waliowaona kua wao takukuru ni wachafu na wao leo wanasema eti wabunge ni wachafu.
mimi sioni mantiki hapo kwani wanaotoa hizo posho ni nani si serikali????!!!
sasa kama wabunge wanakula rushwa ya hizo posho ni sawa . na sheria ya rushwa inasema MTOA RUSHWA NA MPOKEA RUSHWA WOTE WANAHATIA. naomba takukuru waanze kuwahoji serikali wakisema kweli walitoa ni rushwa basi ndipo wawafate wabunge tena kutakua hakuna hata haja ya kuhojiana kwani mtoa rushwa anavidhibitishao mpokeaji hawezi kukataa.
hawa takukuru watakua hawana kazi za kufanya ndio maana wanaamua kupoteza muda kwenye swala la kuwahoji wabunge wakati wanajua mtoa rushwa ni nani kama kweli ni rushwa .
 
Buchanan, nadhani hapa wewe ndio umechanganya mambo mawili tofauti.

Mimi nimemuelewa Zitto. Kasema wabunge wana immunity kwa yale yote wanayozungumza ndani au nje katika viunga vya bunge.

Kesi za wakina Pesambili Mramba ni ya jinai na haihusikani kwa namna yoyote na masuala ya Bunge.
Ni kama vile ukiua mtu kama alivyofanya Dito na wewe ni mbunge usitegemee kupata immunity. Au ukivunja nyumba ya jirani yako hata kama wewe ni mbunge usitegemee kupata immunity.

Unakumbuka kesi ya wale wabunge wa Zanzibar walioghushi nyaraka za uhamiaji? ( ingawa sielewi ziliishaje mahakamani)? hapo hakuna cha immunity kaka/dada.

Yaani watu humu wanachekesha kweli mkuu wangu MF..Eti wanalinganisha ishu ya Mramba na ya Mwakyembe,ni kitu cha ajabu kweli aisee
 
SLOWLY BUT SURELY, nimeanza kupoteza imani yangu kwa Zitto: He can do anything to make ends meet, and this is really dangerous! Zitto, come back we need you. After all bado ni kijana, una nafasi ya kujisahihisha....ila maamuzi yako hivi karibuni yananitia shaka kwamba wewe ni kashushu ka kila upande (as long as you get paid)....BUT ask yourself, "FOR HOW LONG YOU WILL BE SAFE?" doing this kind of Hipocrity?
Duh! wewe unachemka big time, Zitto amekuwa akijaribu kuweka mambo wazi kadiri ya ufahamu wake. Anajitolea sana kuhakikisha kuwa wana jamvi wa hapa wanapata kujua kuhusu upande wa pili wa mambo mengi yanayohusu bunge.

Ni nadra sana kuwa na mtu kama huyu, ambae ameweza kuwa kiunganishi. Sijaona sehemu yoyote katika michango yake hapa ambayo inatia shaka kiasi cha wewe kuishiwa imani nae.

Ni vema ukawa unasoma mabandiko yake kwa umakini ili uweze kumfahamu, na sio kukurupuka na kuja na madai hewa hapa!
 
Duh! wewe unachemka big time, Zitto amekuwa akijaribu kuweka mambo wazi kadiri ya ufahamu wake. Anajitolea sana kuhakikisha kuwa wana jamvi wa hapa wanapata kujua kuhusu upande wa pili wa mambo mengi yanayohusu bunge.

Ni nadra sana kuwa na mtu kama huyu, ambae ameweza kuwa kiunganishi. Sijaona sehemu yoyote katika michango yake hapa ambayo inatia shaka kiasi cha wewe kuishiwa imani nae.

Ni vema ukawa unasoma mabandiko yake kwa umakini ili uweze kumfahamu, na sio kukurupuka na kuja na madai hewa hapa!

Ndhani mkuu ni ishu kama hii ya we mshabiki wa CCM kumtetea Zitto ndo inatufanya tukose naye imani... ghafla amekuwa msemaji wa TANESCO, Dr Rashid, Dowans na TAKUKURU... strange coming from an opposition MP.... don't ya think?
 
Hili la kumkamata nafikiri ndiyo Mwakyembe alikuwa analiomba kwa udi na uvumba, kwani kumkamata tu haitoshi jibu ni je wataweza kumhoji?, akikataa kuongea watakaa naye kwa muda gani?, watamfunga nyaya za umeme mpaka aongee?. Hii sasa ni starting point nzuri sana kwa wapiga vita ufisadi. Nadhani wakimkamata huyu bwana watakuwa wamefungua njia ya kumkamata EL, RA, Hosea et al. Otherwise watakuwa wamemtengeneza Mwakyembe kuwa Mandela wa Bongo.
 
Ndhani mkuu ni ishu kama hii ya we mshabiki wa CCM kumtetea Zitto ndo inatufanya tukose naye imani... ghafla amekuwa msemaji wa TANESCO, Dr Rashid, Dowans na TAKUKURU... strange coming from an opposition MP.... don't ya think?
Naona bado unakuwa mgumu wa kufahamu, wengi wa watu hapa wamekuwa wakijadili issue pasipo kujua hali halisi ipo vipi.

Anapotokea mtu ambae yupo jikoni na kuweka mambo sawa ili mjadala uende katika mstari, sio vema kumbeza. Hii sio sahihi hata kidogo. Hatuwezi kujadili mambo hewani kama kweli tunataka kuona nchi hii inakwenda kwa mujibu wa sheria na katiba.
 
Back
Top Bottom