Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Mkuu Zitto nimekupata hapa, lakini pia hili linawezekana tu pale PCCB watapofuata utaratibu unaokubalika sio kukurupuka tu kwamba leo tunamtaka fulani basi wanapiga simu kumuita.

Nina amini msimamo wa Mwakyembe kukataa kuhojiwa ni sahihi na kwamba utafungua njia mpya ya hawa watu kuacha kutaka kunyamazisha watu fulani eti kuwa tu wana mamlaka ya kuwanyamazisha

"Hawana lolote PCCB, wanaangaika tu mkuu wao atakoma mwezi huu hata afanyeje, Oseaaaaa kwishaa.Tena walitakiwa wawe na adhabu ya kunyongwa, osea,mwanyika,mwakapugi Lowasa,Jeetu na wengine wote bila kumsahau mramba na yona.
 
Mwakyembe anaweza kukamatwa kama alipewa wito na kukaidi kwenda. Wala si mazungumzo aliyotoa viunga vya bunge.
 
Akawasikilize kina nani? Kwani wao PCCB rushwa wanazopokea nani huwa anawahoji? The point ni kuwa yeye Hosea,uchafu wake kausafisha lini,na kama kupokea posho mara mbili ni rushwa,vipi wao PCCB wanapojaza Imprest za uongo na wanajidai kwenda kukamata watuhumiwa wa rushwa,kisha wanaishia kwenye mabaa kubwia maji ya Ilala (beer) nani huwa anawahoji? Tunaishi nao,na tunawafahamu vizuri sana.
.

mkuu nyamizi.

sasa kama hakuna haja ya kuhojiana,hiyo richmond ya nini?
 
Tupende, tusipende Imani kwa Wapiganaji (kama wapo anyway) itaanza kushuka taratibu kama mambo yenyewe ndio haya! Mbunge mpokea posho mbili kwa kazi moja ana tofauti gani na mtu anayechukua mshahara wa marehemu wakati na yeye ana wa kwake?
 
Hivi imekuwaje hawa wapiganaji wakachukua posho sehemu mbili tofauti kwa kazi ileile.
Kwa hakika hii inaondoa their sense of partiality na vilevile watu kuhoji sincirety yao katika kupambana na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Kwa upande wao damage has been done na wote wanaonekana kuwa walaji tu!
 
Mimi nadhani kwenye hili la kuitwa PCCB na kukataa kwa msomi mwakyembe ni uchemfu. kasheria kapya ka PCCB ambacho wabunge hawa hawa walikapitisha kako wazi kuhusu wito chini ya "special powers of investigation" kama ilivyo hapa chini.

"10 (1)Special Power of Investigation
An officer of the Bureau investigating an offence under this Act may
a) Order any person to attend before him for the purpose of being interviewed orally or in writing in relation to any matter which may assist investigation of the offence."

Kwa wale wenye interest ya kusoma vizuri hii sheria nimeiattach. Kiukweli haijakaa vizuri na PCCB wana nguvu kubwa mno ila wabunge wetu wakati wanaipitisha hawakuona hilo na leo hii inakula kwao.
 

Attachments

Kama ni mimi, hata kama ningelipwa posho mara 10, ningechukua. POSHO si rushwa. Kwani waliiomba au walipewa? Kama kuna watu ambao posho inawafunga mdomo, basi poleni sana...hamfai!
 
mheshimiwa zitto tunaomba vifungu (kanuni za bunge, katiba au sheria nyingine yoyote) vinavyotoa hiyo kinga maana hapa kidogo mnatuchanganya, hasa mnapozungumzia kinga sasa hivi, huku hamkusema chochote kuhusu kinga ya mbunge hasa pale mheshimiwa basil pesambili mramba (kesi ya misamaha ya kodi) na mheshimiwa andrew chenge (kesi ya kusababisha ajali) walipohojiwa na kesi zao kwa sasa ziko mahakamani!

kwani takukuru imeundwa ili kuchunguza wananchi pekee au ? Kwani wao hawaoni jinsi umasikini ulivyo hapa nchini mwetu? Kila siku bajeti yetu ya nchi inategemea nje ya nchi kumbe hii yote ni kwa ajili ya kulipana posho? Mimi binafsi nampongeza sana raisi jakaya mrisho kikwete kwa kuruhusu hili.....na hili analofanya mheshimiwa sasa baadae watanzania tutalikumbuka hata kama litamkuta na yeye mwenyewe.
 
"10 (1)Special Power of Investigation
An officer of the Bureau investigating an offence under this Act may
a) Order any person to attend before him for the purpose of being interviewed orally or in writing in relation to any matter which may assist investigation of the offence."

Na hiyo ndio nguvu ya kweli kwenye chombo cha uchunguzi amna wa kuachwa, sawa sawa hata kama wengine bado hawajafikiwa huu ni mwanzo mwenye kosa na asie na influence ndio aanziwe awe Mwakyembe sijui nani. Cha muhimu hapa ni kuanza kumaliza huu utamaduni wa hizi tabia zao mbaya ambazo zimekuwa ignored for too long.
 
Na hiyo ndio nguvu ya kweli kwenye chombo cha uchunguzi amna wa kuachwa, sawa sawa hata kama wengine bado hawajafikiwa huu ni mwanzo mwenye kosa na asie na influence ndio aanziwe awe Mwakyembe sijui nani. Cha muhimu hapa ni kuanza kumaliza huu utamaduni wa hizi tabia zao mbaya ambazo zimekuwa ignored for too long.

safi sana mtu wangu......vijana tunakosa ajira kwa ajili yao, na hii yote ni ufisadi uliokithiri.......
 
Wakuu zangu,
Mimi nilikaa pembeni kusikiliza wachangiaji lakini kuna maswali ambayo nashindwa kuyajibu ikiwa kweli tutatafsiri hizi sheria kwa jinsi tunavyojisikia..

Ningependa kujua ni wakati gani TAKUKURU wanaruhusiwa kuwahoji Wabunge?..Mathlna Takukuru wamewahi kufanya uchunguzi wa Richmond kabla ya kamati ya Mwayembe (kama Mnakumbuka) Je, ni Mawaziri ganmi waliohojiwa na TAKUKURU kama sio hao hao Wabunge!..

Pili tusichanganye makosa ya mbunge ktk utendaji akiwa nje ya Bunge, mathlan Mbunge ambaye ni waziri akifanya wizi wizarani sidhani kama sheria inakataza asihojiwe kwa wizi huo kwa sababu ni Mbunge hilo moja, ila sheria inakataza Mbunge asihojiwe maswala yoyote yanayohusiana na BUNGE..(kama sikosei).
Mfano ni kuhojiwa kwa Mramba, huyu kweli aliikuwa Mbunge lakini kesi yake ilihusioana na utendaji kazi wake akiwa waziri wa wizara na sii Mbunge.. hivyo inakubalika kisheria..Tukipinga hili ni lazima tujiuliza je ni wakati gani wabunge wanaweza kuhojiwa.. mathlan kina Rostam, who's to question them..maanake hata Rostam ni mbunge!


Swala la Mwakyembe kuhojiwa lipo wazi kabisa kuwa ni makosa...kwa sababu lipo ktk kifungu cha pili..Kazi zote za kamati za Bunge zilipewa baraka za Bunge pamoja na rais mwenyewe..sote tunakumbuka hili, hivyo kama kulikuwepo na malipo ya posho mbili -mara zote sheria za uhasibu mkosa ni yule aliyelipa posho hizo kinyume cha sheria..iwe ni muidhinishaji wa malipo ya posho za Bunge, shirika, wizara au taasisi husika kwa sababu kabla hujalipa poshi au fedha zozote ni lazima kuwepo na suppoting document ambayo huidhinishwa kulingana na tumizi tarajiwa..Ni kazi ya Auditors kufanya uchunguzi huo na kuwakilisha mahesabu yao, kulipwa posho mara mbili sii kosa la kukihusisha chombo kikubwa kama TAKUKURU kama vile wamekosa kazi..
Hao waliolipa waliweka mahesabu ya posho hizo ktk kifungu gani na iliidhinishwa na nani?..Na ikiwa sehemu zote za kikazi ziliidhinisha posho hizo kimakosa hili sii kosa linalotakiwa kufikishwa mahakamani isipokuwa ni chombo husika (i.e Bunge) kukata (as a refund) fedha zote walizolipa kwa mbunge huyo kama ziada ya malipo.. Unless Bunge lenyewe ndilo lipeleke malalamiko haya TAKUKURU na kuomba uchunguzi ufanyike.
 
Wakuu zangu,
Mimi nilikaa pembeni kusikiliza wachangiaji lakini kuna maswali ambayo nashindwa kuyajibu ikiwa kweli tutatafsiri hizi sheria kwa jinsi tunavyojisikia..

Ningependa kujua ni wakati gani TAKUKURU wanaruhusiwa kuwahoji Wabunge?..Mathlna Takukuru wamewahi kufanya uchunguzi wa Richmond kabla ya kamati ya Mwayembe (kama Mnakumbuka) Je, ni Mawaziri ganmi waliohojiwa na TAKUKURU kama sio hao hao Wabunge!..

Pili tusichanganye makosa ya mbunge ktk utendaji akiwa nje ya Bunge, mathlan Mbunge ambaye ni waziri akifanya wizi wizarani sidhani kama sheria inakataza asihojiwe kwa wizi huo kwa sababu ni Mbunge hilo moja, ila sheria inakataza Mbunge asihojiwe maswala yoyote yanayohusiana na BUNGE..(kama sikosei).
Mfano ni kuhojiwa kwa Mramba, huyu kweli aliikuwa Mbunge lakini kesi yake ilihusioana na utendaji kazi wake akiwa waziri wa wizara na sii Mbunge.. hivyo inakubalika kisheria..Tukipinga hili ni lazima tujiuliza je ni wakati gani wabunge wanaweza kuhojiwa.. mathlan kina Rostam, who's to question them..maanake hata Rostam ni mbunge!


Swala la Mwakyembe kuhojiwa lipo wazi kabisa kuwa ni makosa...kwa sababu lipo ktk kifungu cha pili..Kazi zote za kamati za Bunge zilipewa baraka za Bunge pamoja na rais mwenyewe..sote tunakumbuka hili, hivyo kama kulikuwepo na malipo ya posho mbili -mara zote sheria za uhasibu mkosa ni yule aliyelipa posho hizo kinyume cha sheria..iwe ni muidhinishaji wa malipo ya posho za Bunge, shirika, wizara au taasisi husika kwa sababu kabla hujalipa poshi au fedha zozote ni lazima kuwepo na suppoting document ambayo huidhinishwa kulingana na tumizi tarajiwa..Ni kazi ya Auditors kufanya uchunguzi huo na kuwakilisha mahesabu yao, kulipwa posho mara mbili sii kosa la kukihusisha chombo kikubwa kama TAKUKURU kama vile wamekosa kazi..
Hao waliolipa waliweka mahesabu ya posho hizo ktk kifungu gani na iliidhinishwa na nani?..Na ikiwa sehemu zote za kikazi ziliidhinisha posho hizo kimakosa hili sii kosa linalotakiwa kufikishwa mahakamani isipokuwa ni chombo husika (i.e Bunge) kukata (as a refund) fedha zote walizolipa kwa mbunge huyo kama ziada ya malipo.. Unless Bunge lenyewe ndilo lipeleke malalamiko haya TAKUKURU na kuomba uchunguzi ufanyike.

sasa hapa mkuu umenielewesha vyema........ila wasipinge takukuru kuwahoji....mimi nionavyo ni kwamba Takukuru wanafanya uchunguzi kwanza...na kuhojiwa si kosa kabisa
 
yaani hunigusi hata kidogo na hoja yako. kumbuka mtu unapoitwa kwa mahojiano njia moja tu ndio inayokubalika nayo ni kwa njia ya Summons tena ya maandishi. niambie ni lini umewahi kuona summons ya simu??ndugu yangu hiyo haipo hata mie ningeitwa kwa staili hiyo nisingekwenda.
Mind you tena PCCB wanafanya kazi yao kienyeji tena kwa dharau kubwa sana hebu fikiri anamuita Mbunge akamhoji halafu anamuuliza summons iko wapi anamwambia we njoo tu utakuta barua yako getini. je ndo hivi tunavyotakiwa kufanya kazi kwa dharau na kujidai hata pale tunapokuwa tunashughulikia wakubwa. si hivyo hata kidogo. mwacheni Mwakyembe atajipanaga aende akiitwa kiustaarabu na sio kwa njia waliyotumia kumuita NASEMA HAIPO KISHERIA HATA UENDE WAPI. "Government works with Papers" bwana na hapa naongelea summons ya maandishi ndugu yangu na sio mtu alete upuuzi wake wa kupiga simu.
Tukirudi kwenye issue ya PCCB kudai wabunge wamepokea posho mara mbili ni posho gani hiyo unayoingelea. hivi ofisi yako ikikulipa posho ya kikao halafu ikaja ofisi ya waziri Mkuu ikakulipa posho ya chakula je posho hizo zinafanana?? tazama kwanza hayo ni majina mawili tofauti hata uende wapi. sasa huyo PCCB anayeitafuta posho ya mara ya pili ni ipi. PPC kama umekosa kazi za kufanya kaa chini ukapambane na ma rushwa makubwa unataka tukuandikie hapa na hasa tukianza na wewe mwenyewe HOSEA una uozo mwingi wa kwako mwenyewe sasa sijui tukuundie TUME??? tukufichue ngoja nipe muda
 
sasa hapa mkuu umenielewesha vyema........ila wasipinge takukuru kuwahoji....mimi nionavyo ni kwamba Takukuru wanafanya uchunguzi kwanza...na kuhojiwa si kosa kabisa
Mkuu kwa mtazamo wangu Takukuru wana makosa ikiwa BUnge au rais hakutoa amri hiyo... Sii kazi yao kuchunguza posho na malipo ya wabunge ktk kazi za bunge..
 
Hawa wabunge wachunguzwe tena kwa saana. Wasijifiche katika kivuli cha Richmond na kusema timing mbovu na blablaa ningi tu. Tena wakimaliza kuchunguza posho wacghunguze vyeti vya elimu zao feki, mali walizoandikisha bungeni nk. lways the guilty are afraid!!
 
chuki binafsi tu ndio zinawasumbua pccb....kweli kwa akili zao ndogo wanachunguza tuposho wakati tuna mikataba mibovu na wao wanaridhia kuwa iko safi........pccb kuwachunguza wabunge na hasa mwakyembe ni jitihada za takukuru kuficha ukweli kuwa hawawezi kufanya kazi ya kuchunguza........wamechukia sana ripoti kamati teule iliyoonyesha udhaifu mkubwa wa tume hii udhaifu ambao tungekuwa na uongozi wa kweli na unaojali maslahi ya taifa na kama viongozi wa juu wa nchi wasingekuwa wamehusika kwa makusudi kuupigia chapuo mkataba huu wa kinyonyaji basi kwenye tume hii mpaka sasa asingebakia.....nashangaa watanzaia tumetulia tuli wakati tumeunda taasisi kubwa inayolipwa vinoti kibao ifanye kazi hizi za kiuchunguzi lakini cha ajabu wanachezea ofisi kwa maslahi ya akina lowasa,roatam na ndugu zao.ndio maana watz waliofikia hatua ya kukata tamaa wanafikia mahali wanasema ingekuwa nchi za watu tungekuwa tuliisha andamana kuwafukuza waajiliwa wote wa pccb kwani hawapo kwa kazi tuliyo watuma.......ki ukweli pccb iliyopo hawana haki ya kuwahoji wabunge kwani wamefanya kazi ambayo wao kama taasisi maalum wameshindwa......nalaani sana kitendo cha takukuru kutumia rungu lao kuwanyamazisha wabunge..TUNAJUA WANAONGOZWA NA KUCHOCHOWA NA EDWARD HOSEA,,,,,,,,HOSEA tumekuona ila kuwa macho tumechoka na upuuzi wa kutufanya sisi mbumbumbu.....
 
Ndugu yangu Buchanan kama hujui vitu ni bora usipoteze muda wako kuandika kutupotosha na hoja zisizoeleweka. tafuta ukweli wa jambo chambua tujadiliane vizuri au sio ndugu yangu. PCCB wametumwa kufanya kazi hiyo na mamlaka ya Juu tena kwa kulazimishwa walikuwa wapi siku zote na hali jambo walikuwa wanalijua tena wamelianza kwa papara bila research. walitakiwa kwanza kuidadisi hiyo posho ya mara ya pili then ndo waanze kazi. na kwa mamlaka waliyonayo wangerudi kwa aliyewatuma na kumueleza bwana ee hapa hatuoni hoja. na kwa taarifa yako wako maafisa wa PCCB ambao wamewahoji Wabunge ktk issue hii na wao weneywe wamekiri du hapa hakuna hoja wanajipotezea muda kwa sababu kila kitu kipo wazi ndugu yangu labda wa badilishe kesi kama wanavyofanyaga polisi.poa mtu wangu kwa leo niliona nikupe dondoo hizi uzitafakari na malizia kwa kusema PCCB wenyewe kazi hii ya mahojianao na wabunge inawachosha maana hakuna jibu jipya wanalolipata kutoka kwao ikilinganishwa na documents walizonazo kuwahojia wabunge zikiwa na uhalali. WAMELAZIMISHWA, HAWASEMI ACHA WAJICHOSHE
 
naamini tungekuwa na uongozi wa kweli wala mpaka sasa tusingekuwa tunazungumzia akina hosea tungelikuwa tumewafukuza na wala hawatakiwi kujiuzuru...........''URAFIKI WANGU NA KIKWETE HAUKUANZIA BARABARANI'' hili ndio tatizo kubwa...lowasa na rostam wanaendesha nchi..lowasa na rostam wanampiga mkwara jk kutomchukulia hatua za kumfukuza na za kisheria kisheria hosea kwa sababu wanataka watz tuendelee kuamini report ya pccb kuwa richmond ilikuwa kampuni safi kwa hiyo rostam na lowasa hawahusiki......tumechoka jamani
Huyu Hosea ndio aliwasafisha wale matapeli wa Richmond then akawa busted lakini cha ajabu hakuna chochote kilichomtokea,huyu anatakiwa kuwa jela sasa hivi ,wapuuzi kama hawa ndio wanatumaliza na hakuna chochote wanafanya zaidi ya kugeuza chombo muhimu kama PCCB/TAKURURU kuwa cha kisiasa na revenge kwa wote wanaoonekana kama ni hatari kwa serikali yao...kuna rushwa za mabilioni kila siku lakini hakuna prosecution yeyote kila siku ni kanyaboya tuu hawa matapeli wa TAKURURU,huyu Hosea lazima aondoke!
 
hii kitu haiwezekani kabisa, eti akamatwe kisa kagoma kwenda. hii janja ya nyani
 
yaani hunigusi hata kidogo na hoja yako. kumbuka mtu unapoitwa kwa mahojiano njia moja tu ndio inayokubalika nayo ni kwa njia ya Summons tena ya maandishi. niambie ni lini umewahi kuona summons ya simu??ndugu yangu hiyo haipo hata mie ningeitwa kwa staili hiyo nisingekwenda.
Mind you tena PCCB wanafanya kazi yao kienyeji tena kwa dharau kubwa sana hebu fikiri anamuita Mbunge akamhoji halafu anamuuliza summons iko wapi anamwambia we njoo tu utakuta barua yako getini. je ndo hivi tunavyotakiwa kufanya kazi kwa dharau na kujidai hata pale tunapokuwa tunashughulikia wakubwa. si hivyo hata kidogo. mwacheni Mwakyembe atajipanaga aende akiitwa kiustaarabu na sio kwa njia waliyotumia kumuita NASEMA HAIPO KISHERIA HATA UENDE WAPI. "Government works with Papers" bwana na hapa naongelea summons ya maandishi ndugu yangu na sio mtu alete upuuzi wake wa kupiga simu.
Tukirudi kwenye issue ya PCCB kudai wabunge wamepokea posho mara mbili ni posho gani hiyo unayoingelea. hivi ofisi yako ikikulipa posho ya kikao halafu ikaja ofisi ya waziri Mkuu ikakulipa posho ya chakula je posho hizo zinafanana?? tazama kwanza hayo ni majina mawili tofauti hata uende wapi. sasa huyo PCCB anayeitafuta posho ya mara ya pili ni ipi. PPC kama umekosa kazi za kufanya kaa chini ukapambane na ma rushwa makubwa unataka tukuandikie hapa na hasa tukianza na wewe mwenyewe HOSEA una uozo mwingi wa kwako mwenyewe sasa sijui tukuundie TUME??? tukufichue ngoja nipe muda

Kumbuka malipo ya posho yamefanywa kupitia Serikali ile ile moja, hata kama Idara ni tofauti! Wewe jiulize, kwa nini Mbunge anapoondoka kwenda kwenye shughuli fulani analipwa? Si ili akajikimu wakati yuko nje ya ofisi kikazi? Kumbuka kuwa kuna rate kulingana na stahili ya mtumishi! Sasa kwa nini anaenda kudai posho nyingine nje ya stahili yake? Kwani hizo fedha hazina kazi nyingine ya kufanyia? Halafu juu ya Summons, Mwakyembe hakulalamika kwamba kaitwa kwa simu, bali yeye HATAKI KUITWA NA TAKUKURU kwa kuwa hana imani nayo! Kama mimi sina imani na mahakama ambazo zinanuka rushwa ina maana sitashtakiwa? Au chombo rahisi kukigomea ni TAKUKURU tu?
 
Back
Top Bottom