Dr. Slaa amsimamisha kazi Katibu wa CHADEMA Nzega

Dr. Slaa amsimamisha kazi Katibu wa CHADEMA Nzega

Katika nchi zenye democrasia changa kama Tanzania na nchi nyingine nyingi za Africa, maamuzi kama hayo ni muhimu sana kufanyika kwa haraka kama kuna ushahidi wa kutosha wa tuhuma na wenye kuridhisha. Ni vizuri sana kuwa na uwazi kwa mambo yanayohusu uwajibikaji kwa wananchi au wanachama pia. Mkimsoma vizuri Dr. Slaa kwa maelezo yake yuko sahihi kwa nafasi aliyonayo kufikia maamuzi kama hayo ili kuepusha hali ya mashaka na sintohamau kwa uma. Huyo katibu hajavuliwa madaraka bali amesimamishwa kwa muda ili uchunguzi ufanyike na haki itendeke, na kama akionekana hana hatia basi chama kitamsafisha kwa njia hiyohiyo iliyotumika kumsimamisha.

Tukumbuke pia kuwa uimara wa serikali ya ccm chini ya Mwalimu Nyerere mambo kama hayo alikuwa akiyafanya sana yeye pamoja na Hayati Sokoine, na hiyo ilisaidia sana kuleta nidhamu ya utendaji na kuepusha ubadhilifu wa mali na madaraka pia. Maamuzi kama hayo pia yanasaidia sana kuchuja wale mamluki walioingia katika chama ili kutumiwa kukiua chama kujiondoa wenyewe kama siyo kuogopa kabisa kujiingiza katika chama.

Nashauri sana chama kizingatie umuhimu wa kuendesha semina za mara kwa mara kwa viongozi wa kazi zote kuanzia mashina juu ya uwajibikaji na uadilifu katika uongozi ili kuzidi kukiimarisha chama na kukijengea uaminifu kwa wananchi.
 
Naweza kuwa na fikra tofauti kidogo na uamuzi wa Katibu Mkuu wa Chadema kumsimamisha Katibu wa Chadema wa wilaya ya Nzega. Si vizuri kutumia jukwaa kutolea maamuzi mazito ni hatari kwa uhai wa wanachana na viongozi wao. Bora angetulia na kuvumilia kidogo hadi ujumbe wa kitaifa kuja kufanya uchunguzi na kumpa nafasi ya kujitetea. Sina maana ya chama kufuga wabadhilifu wa mali za chama au wanaoweka mipasuko ndani ya chama, bali kutumia taratibu nzuri za kisheria zinazokubalika na kulinda heshimna ya mtu.

Kuna matukio kadhaa hata kipindi cha kampeni alifanya hivyo kutolea maamuzi jukwaani kitu ambacho kisaikoloji inaweza kumharibu mhusika hata kabla ya kufanya uchunguzi kwa taratibu za kichama. Katika hilo Katibu Mkuu Dr. Slaa anatakiwa kuwa mwangalifu maana busara inatakiwa kutumika zaidi katika nafasi kama hiyo. Na tujue binadamu si 100% ni kamili la hasha, kila mtu ana mapungufu yake, na kwa hilo mimi namshauri kuwa mwangalifu kadiri ya mtazamo wangu.




Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko

Sera za CCM kungoja viongozi wa juu wafanye uchunguzi as if they are angels. Sera ya CDM weka pembeni ndipo uchunguzi ufanywe ukiwa nje. Ukibainika huna hatia utarudishwa. Big UP Dr. wa ukweli
 
Candid, ukifikilia siasa za namna hii utaona kazi ya kuchukua nchi ilivyokuwa ngumu. Yaani hawataki wao kuwa ni alternative. Hivi ni demokrasia gani ipo hivyo? Wapi duniani kuna vituko vya hivi? Hapa wanataka gavana au watendaji wengine wathibitishwe na bunge ili kumpunguzia madaraka Rais lakini vitendo wafanyavyo ni vya kujilimbikizia madaraka.
Kuna haja ya kunijanusua katika baadhi ya vitanzi, kwamba wenye maamuzi katika chama ni watu wachache. Kesho akisafiri Mbowe au Arfi na yeye anaweza kufanya hivyo? Hivi ziko wapi taratibu na kanuni za CHAMA. Kule Nzega hakuna uongozi kabisa. Yaani kesi inasikilizwa hapo na utetezi unafanyiwa tathmini kisha maamuzi. Huyu bwana angekuwa hakimu huenda wengi hata wasio na hatia wangejaa magerezani na kinyume chake.


Kule Nzega hakuna uongozi wa Chadema ya wilaya na hakuna uongozi wa Chachema wa Mkoa wa Tabora, vinginevyo hao wangekaa kikao na kutathmini yaliyojilia na kutolea uamuzi au mapendekezo badala ya hatua ya kusikiliza watu kwenye mkutano wa hadhara na kutolea uamuzi bila upembuzi yakinifu.
Kama ni ubadhilifu wa mali za chama ni mhasabu gani aliyeoditi mahesabu na kuonyesha kwamba kumekuwa na ubadhilifu wa matumizi?

Mimi ni mpenda mageuzi lakini tuende kwa system isiwe hoja ya kwamba chama kinaendeshwa kama kampuni ikashika kasi, bora kutoa ushauri wa kufaa.

Chama Cha CCM lengo la kuwaondoa matajiri ni la Kikwete na alishalitamka kule Dodoma katika sherehe za chama. Lakini kwa busara alisubiri kikao cha chama na hivyo uzito wa suala lote la kuondolea akila Lowasa, Chenge na Rostam ni Kikao cha Chama na wala si Kikwete. Tuna mambo ya kujifunza katika tukio hili.

Viongozi wa Chadema wafungue macho na masikio kwa tunayoongelea ni kwa ajili ya kujenga chama si vinginevyo. Wengine hapa ni kushabikia tu cho chote kinachofanyika bila kuangalia athari zake kwa siku za usoni. Na pengine watu hawa tunaowaona hawafai huenda wanahitaji tu darasa na baadaye wakawa watu wa kufaa zaidi.
 
Hiyo ni zaidi ya gamba alilovaa kikwete.............hiyo ni fagia fagia....safisha safisha ambay7o ccm hawaiwezi
 
mbona hatujaelewa hapa au watu hawasomi? Kilichofanyika hapa ni kumsimamisha kwa muda hadi uchunguzi utakapokamilika. Uchunguzi ukifanyika akiwa madarakani anaweza kuupindisha. kama itaonekana hana kosa atarudishwa hivyo ndivyo nilivyoelewa na ndivyo alivyofanya Slaa
 
Jile79. Huwezi mfananisha JK na Slaa. Mmemfanya Mzee wa Watu awajengee Chama kwa ahadi ya pipi na kuwafukuza kazi wadogo. Zitto aliyewazidi nguvu Bungeni mmemshindwa hata kumpa onyo. Kweli hicho c Chama cha Demokrasia ila CHAUMA - Chama Cha UBABE na Maendeleo.
 
Sera za CCM kungoja viongozi wa juu wafanye uchunguzi as if they are angels. Sera ya CDM weka pembeni ndipo uchunguzi ufanywe ukiwa nje. Ukibainika huna hatia utarudishwa. Big UP Dr. wa ukweli

Kumbuka kumdhalilisha mtu mbele ya halaiki ni kinyume cha haki za binadamu na haki za msingi za kila raia. Yule katibu baada ya kudhalilishwa hadharani pale anajisikiaje? Heshima na haki za mtu zilindwe na utaratibu mzuri unaofaa utumike badala ya mapigo ya papo kwa papo kuwafurahisha wananchi lakini ni jeraha linalokua ndani ya chama. Hayo yanaakiwa yasitishwe na mambo yafanywe systematically.

Tunasoma kwenye misahafu kuwa kijana mdogo Daniel aliweza kuwaaibishwa wazee waliomzulia jambo msichana waliyemtaka kimapenzi na kisha kawatolea nje. Wakamsingizia amekutwa anafanya mapenzi na mtu na hivyo anastahili kuuawa kwa kurushiwa mawe. Kijana akauliza wazee moja baada ya mwingi, je ulimwona chini ya mti gani, mwingine kasema mpera, na mwingine msandarusi, na mwingine mwembe nk, ushahidi wao ulihitilafiana na watu wakamshukuru sana kijana Daniel kumnusuru yule dada asiuawe kwa mawe kwa hila ya wale wazee. Mambo haya yamekuwepo miaka nenda rudi, ila burasa inatakiwa ichukue nafasi na mfumo wa utendaji wenye kujenga umoja na mshikamano ndani ya chama ni muhimu.
 
Candid Scope,
Leo tunamtuhumu JK kwa kuwataka watuhumiwa wa ufisadi wajivue magamba ndani ya siku 90. Ni kushindwa kwa uongozi kuwa na uamuzi. Yaani ufisadi ufanyike mbele yangu, licha ya tuhumu zilizoelezwa na waliolaklamika. Kisha nimwache aendelee kuua chama? Uongozi ni kufanya maamuzi kwa wakati kuepuka mdhara zaidi au kulenga manufaa ya uamuzi huo. Ndivyo nilivyofundishwa uongozi. Uongozi legelege usio na maamuzi ndio uliotufikisha hapa tulipo. Mhusika alipata nafasi ya kujieleza hapo hapo, lakini maelezo yake hayakuridhisha hasa kwa kuwa ufisadi ni "documentary" na kwa kawaida kwa documentary evidence huhitaji ushahidi zaidi.

Daktari wa ukweli,hapo umepotoka na umekiuka katiba,hata kama umefundishwa uongozi naamini waliokufundisha walitaka ufuate sheria na katiba.

Katiba ya CHADEMA 6.3.6(b) insema:-Kiongozi alieteuliwa na vikao vya uongozi ataweza kusimamishwa au kuachishwa uongozi na kikao kilichomteua Period!

Kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA,katibu huyo alipaswa kushughulikiwa na kamati kuu,
Kama katiba ya CHADEMA unapindisha,itakua vipi ukipewa dola
 
Kiongozi mzuri ni yule anayetoa maamuzi yake kwa uwazi, ukweli na kufuata utawala wa sheria bila kumwonea mtu wala kumpendelea kwa dhana kwamba ni mwenzetu. Naamini taratibu zote muhimu zilifuatwa katika kumtimua huyo katibu
 
That is great action! Commendable job!!!!!!!!!
 
Kiongozi mzuri ni yule anayetoa maamuzi yake kwa uwazi, ukweli na kufuata utawala wa sheria bila kumwonea mtu wala kumpendelea kwa dhana kwamba ni mwenzetu. Naamini taratibu zote muhimu zilifuatwa katika kumtimua huyo katibu

Kasome katiba ya CHADEMA.
 
Candid, ukifikilia siasa za namna hii utaona kazi ya kuchukua nchi ilivyokuwa ngumu. Yaani hawataki wao kuwa ni alternative. Hivi ni demokrasia gani ipo hivyo? Wapi duniani kuna vituko vya hivi? Hapa wanataka gavana au watendaji wengine wathibitishwe na bunge ili kumpunguzia madaraka Rais lakini vitendo wafanyavyo ni vya kujilimbikizia madaraka.
Kuna haja ya kunijanusua katika baadhi ya vitanzi, kwamba wenye maamuzi katika chama ni watu wachache. Kesho akisafiri Mbowe au Arfi na yeye anaweza kufanya hivyo? Hivi ziko wapi taratibu na kanuni za CHAMA. Kule Nzega hakuna uongozi kabisa. Yaani kesi inasikilizwa hapo na utetezi unafanyiwa tathmini kisha maamuzi. Huyu bwana angekuwa hakimu huenda wengi hata wasio na hatia wangejaa magerezani na kinyume chake.

Yaani nyinyi Anfaal na Candid hamjui mlinenalo. Hivi nchi hii changa na maskini mnadhani inahitaji diplomacy katika mambo ya msingi ya kuitoa nchi katika janga la Umasikini. Nyie mnadhani time is on our side!! Ni heri mtu 1 avunjiwe heshima (ambayo badae anaweza regain even in bulky eg. Mwinyi resignation) kuliko wengi wadidimie katika janga la ufukara. uongozi ni misimamo, misimamo ni kuchagua fungu lililo bora ili kufikia uamuzi, uamuzi ni utekelezaji na ndio maendeleo yanapatikana hivyo. Ndo mana twasema JK ni dhaifu, coz hana msimamo wa wazi. Uongozi si lelemama,huwezi furahisha wengi na sifa ya uongozi inakuja baada ya maamuzi. Mwache Dr. apige kazi, Chama kikue, kikamate dola, maendeleo yaje hata kwa wachache kuumia. The end justifies the means. Sasahivi nchi yetu ina umaskini na maendeleo duni (end) japo kuna utawala wa sheria na Uungwana wa kiutawala(means), Useless!!!!!
 
Wakuu,

Niweke mambo sawa.
  • Matatizo ya Nzega katika ngazi ya wilaya hayakuanza leo wala jana yalikuwepo muda tu mrefu. Mojawapo ambapo mimi nilishiriki ni wakati wa uchaguzi mkuu. Just imagine nguvu kubwa tuliotumia lakini mpaka ninaandika hivi sina ushahidi wa matokeo ya uraisi kutoka kwa kiongozi wangu. Baada ya kuona mchezo mchafu, mgombea wetu wa ubunge alikataa kusaini. Ok, alisaini yeye. Copy ya matokeo ipo wapi?
  • Maandalizi ya mkutano wa jumatatu ule wa hadhara, wanachama wenyewe pale walichanga pesa kugharamia mambo mengine kama vipaza sauti vya kuvuta watu kabla gari ya CDM haijaja, vitu vya kukalia na maji ya kunywa. Cha kushangaza gharama ya kukodi ile gari kwa ajili ya matangazo hayo ililipiwa jumla ya tshs 120,000 na alijua kabisa na hakuna aliesema zitarudisha kwa kuwa haikuwa mkopo kwa chama ila yeye bila aibu akazidai. Gharama ya kukodi kiti ni shs 1000 kwa siku, mgombea ubunge alitoa viti 30 bure kabisa.
  • Katibu yule hakutolewa mkuku hadharani, kikao hiki kilikuwa cha ndani.
 
Wakuu,

Niweke mambo sawa.

  • Matatizo ya Nzega katika ngazi ya wilaya hayakuanza leo wala jana yalikuwepo muda tu mrefu. Mojawapo ambapo mimi nilishiriki ni wakati wa uchaguzi mkuu. Just imagine nguvu kubwa tuliotumia lakini mpaka ninaandika hivi sina ushahidi wa matokeo ya uraisi kutoka kwa kiongozi wangu. Baada ya kuona mchezo mchafu, mgombea wetu wa ubunge alikataa kusaini. Ok, alisaini yeye. Copy ya matokeo ipo wapi?
  • Maandalizi ya mkutano wa jumatatu ule wa hadhara, wanachama wenyewe pale walichanga pesa kugharamia mambo mengine kama vipaza sauti vya kuvuta watu kabla gari ya CDM haijaja, vitu vya kukalia na maji ya kunywa. Cha kushangaza gharama ya kukodi ile gari kwa ajili ya matangazo hayo ililipiwa jumla ya tshs 120,000 na alijua kabisa na hakuna aliesema zitarudisha kwa kuwa haikuwa mkopo kwa chama ila yeye bila aibu akazidai. Gharama ya kukodi kiti ni shs 1000 kwa siku, mgombea ubunge alitoa viti 30 bure kabisa.
  • Katibu yule hakutolewa mkuku hadharani, kikao hiki kilikuwa cha ndani.
Kaka pamoja na kuremba koote ili ionekane katiba imefuatwa bado,hujaweza kutoa maelezo yakinifu.
Elezea jinsi katiba ya CHADEMA inavyoelekeza kama kuna tatizo kama hili likitokoea,ukileta story ya bili za viti na maji ya kunywa,hizi ndio standards za CDM,kwani hata viongozi wa kitaifa,wanajilipa tu madeni bila idhini ya kamati kuu
 
Yaani nyinyi Anfaal na Candid hamjui mlinenalo. Hivi nchi hii changa na maskini mnadhani inahitaji diplomacy katika mambo ya msingi ya kuitoa nchi katika janga la Umasikini. Nyie mnadhani time is on our side!! Ni heri mtu 1 avunjiwe heshima (ambayo badae anaweza regain even in bulky eg. Mwinyi resignation) kuliko wengi wadidimie katika janga la ufukara. uongozi ni misimamo, misimamo ni kuchagua fungu lililo bora ili kufikia uamuzi, uamuzi ni utekelezaji na ndio maendeleo yanapatikana hivyo. Ndo mana twasema JK ni dhaifu, coz hana msimamo wa wazi. Uongozi si lelemama,huwezi furahisha wengi na sifa ya uongozi inakuja baada ya maamuzi. Mwache Dr. apige kazi, Chama kikue, kikamate dola, maendeleo yaje hata kwa wachache kuumia. The end justifies the means. Sasahivi nchi yetu ina umaskini na maendeleo duni (end) japo kuna utawala wa sheria na Uungwana wa kiutawala(means), Useless!!!!!

Kumbuka Katibu wa Chadema wa Nzega ni tuhuma tu na utaratibu unatakiwa ufuatwe kadiri ya Katiba ya Chadema kama mdau alivyoainisha hapo juu kama ifuatavyo: Katiba ya CHADEMA 6.3.6(b) inasema:-Kiongozi alieteuliwa na vikao vya uongozi ataweza kusimamishwa au kuachishwa uongozi na kikao kilichomteua Period! Kwa maana hiyo. Kwa hoja hiyo Katibu Mkuu Dr. Slaa amekiuka katiba ya Chama kwa kumsimamisha Katibu wa wilaya Nzega nje u utaratibu wa kikao. Inawezekana kuna kipengile kingine aliposimama Dr. lakini busara, subira na uvumilivu ni nguzo muhimu.

Ndio maana nasema busara na subira ni muhimu vinginevyo kunaweza tokea mkorogano. Kwa misingi hiyo ndio maana kuna kamati mbalimbali za uongozi na maadili ili kuweka mambo sawa, vinginevyo utaratibu wa papo kwa papo unasabisha nyufa kuongezeka.

Wanamageuzi tuwe na jicho la kuona pande zote za sarafu vinginevyo hii fukia fukia italeta madhara, bora kuwa wakweli ili kuokoa jahazi lisizame. Hakuna aliyemkamilifu, kila mtu ana kasoro zake, hivyo kwenye kasoro turekebishane hata awe aliye juu yetu kama binadamu ana mapungufu.
 
Candid Scope,
Leo tunamtuhumu JK kwa kuwataka watuhumiwa wa ufisadi wajivue magamba ndani ya siku 90. Ni kushindwa kwa uongozi kuwa na uamuzi. Yaani ufisadi ufanyike mbele yangu, licha ya tuhumu zilizoelezwa na waliolaklamika. Kisha nimwache aendelee kuua chama? Uongozi ni kufanya maamuzi kwa wakati kuepuka mdhara zaidi au kulenga manufaa ya uamuzi huo. Ndivyo nilivyofundishwa uongozi. Uongozi legelege usio na maamuzi ndio uliotufikisha hapa tulipo. Mhusika alipata nafasi ya kujieleza hapo hapo, lakini maelezo yake hayakuridhisha hasa kwa kuwa ufisadi ni "documentary" na kwa kawaida kwa documentary evidence huhitaji ushahidi zaidi.

Labda Dr. atuambie amekuwa akipata past records za huyu Bwana hivyo hakuhitaji ushahidi mwingine.Otherwise good governance ambayo inasisitiza utatuzi wa matatizo kisayansi itakuwa imewekwa kando.Si kwamba natetea uovu huo,ila point ya Dr. kuwa ndivyo alivyofundishwa uongozi ni deadly wrong.Mahakama haiwezi kutoa haki ama kumnyima haki mtu kwa documentary evidence pekee tena papo kwa hapo.Dr. alipaswa kufuata utaratibu wa kawaida ili kumpa Mtuhumiwa nafasi ya kujitetea akiwa katika free mind na si kwa undue influence.Ni dhahiri hapa Mtuhumiwa pamoja na kupewa "natural justice" hakuwa katika free mind.

Any way kwakuwa hakufukuzwa,nadhani haki itatendeka baada ya hiyo tume kuja,japo kama ni issue ya fedha tena vijicenti vya chama ndio tume inakuja kufanyia kazi huu utakuwa ufisadi mwingine (kesi ya kuku,unauza ng'ombe).
 
haya mambo magamba hawayawezi hawako serious maana mpaka sasa chadema wako poa lakini magamba wanatafuta cheap popularity
 
[/B][/COLOR]

Kule Nzega hakuna uongozi wa Chadema ya wilaya na hakuna uongozi wa Chachema wa Mkoa wa Tabora, vinginevyo hao wangekaa kikao na kutathmini yaliyojilia na kutolea uamuzi au mapendekezo badala ya hatua ya kusikiliza watu kwenye mkutano wa hadhara na kutolea uamuzi bila upembuzi yakinifu.
Kama ni ubadhilifu wa mali za chama ni mhasabu gani aliyeoditi mahesabu na kuonyesha kwamba kumekuwa na ubadhilifu wa matumizi?

Mimi ni mpenda mageuzi lakini tuende kwa system isiwe hoja ya kwamba chama kinaendeshwa kama kampuni ikashika kasi, bora kutoa ushauri wa kufaa.

Chama Cha CCM lengo la kuwaondoa matajiri ni la Kikwete na alishalitamka kule Dodoma katika sherehe za chama. Lakini kwa busara alisubiri kikao cha chama na hivyo uzito wa suala lote la kuondolea akila Lowasa, Chenge na Rostam ni Kikao cha Chama na wala si Kikwete. Tuna mambo ya kujifunza katika tukio hili.

Viongozi wa Chadema wafungue macho na masikio kwa tunayoongelea ni kwa ajili ya kujenga chama si vinginevyo. Wengine hapa ni kushabikia tu cho chote kinachofanyika bila kuangalia athari zake kwa siku za usoni. Na pengine watu hawa tunaowaona hawafai huenda wanahitaji tu darasa na baadaye wakawa watu wa kufaa zaidi.
Mkuu heshima mbele! Nikisoma hii thread inaonyesha ilikuwa kikao ndani ya ukumbi, na nikisoma hoja zako naona unataja mkutano wa hadhara na kuna sehemu unataja jukwaa. Je, kuna sehemu umepotoka hukuelewa vizuri au unajaribu kupotosha?!
 
Mkuu heshima mbele! Nikisoma hii thread inaonyesha ilikuwa kikao ndani ya ukumbi, na nikisoma hoja zako naona unataja mkutano wa hadhara na kuna sehemu unataja jukwaa. Je, kuna sehemu umepotoka hukuelewa vizuri au unajaribu kupotosha?!

Kilikuwa kikao cha wanachana wa chama cha Chadema, hakikuwa kikao cha uongozi au kamati za uongozi na maadili kichama, kwa maana hiyo ulikuwa ni mkutano wa wanachama. Kusema maana ya jukwaa kwa hali ya mkutano ilivyokuwa ni sawa
 
Back
Top Bottom