The Supreme Conqueror
JF-Expert Member
- Feb 13, 2017
- 458
- 1,280
Kada na kiongozi muandamizi wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa, ameshutumu vikali chama hicho kwa kushindwa kujiandaa kikamilifu kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji, na vijiji.
Katika kauli yake isiyo na kificho, Slaa amewapa somo Chadema, akiwataka wafahamu kwamba kwenda kulalamika kwa mataifa ya Magharibi kuhusu mchakato na matokeo ya uchaguzi kutawafanya wajiulize maswali magumu kuhusu maandalizi yao hafifu.
Slaa pia amemkosoa vikali Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, kwa kushindwa kutoa maelekezo ya wazi kwa viongozi wa ngazi za chini na wadau wa chama, jambo ambalo limesababisha kukwama kwa maandalizi ya uchaguzi huo.
Kutokana na hali hii, ni dhahiri kwamba Chadema wanajua wazi kuwa wanakabiliwa na kushindwa vibaya kwenye uchaguzi ujao, na karata pekee waliyobakiwa nayo ni kutoa visingizio vya mchakato wa uchaguzi ili kuficha udhaifu wao mkubwa wa kutokujiandaa ipasavyo.
Katika mazungumzo yake, Dkt. Slaa alitilia mkazo umuhimu wa chama kuwa na mikakati ya kuwajengea uwezo wananchi, akieleza kuwa kwa muda mrefu wananchi wa Tanzania hawajawahi kupewa mwongozo madhubuti wa kujitegemea katika harakati za kisiasa.
"Usitegemee wananchi wawe mstari wa mbele, wanahitaji kuongozwa... CHADEMA mliwajengea uwezo? Upi? Kama mliwajengea uwezo wamefika wakashindwa kutekeleza, wananchi wajibu wao nini?" alihoji Dkt. Slaa, akisisitiza kuwa ni jukumu la viongozi wa kisiasa kuwaongoza wananchi na kuwapa moyo wa kusimama kidete kwa ajili ya haki zao.
Dkt. Slaa alitoa mfano wa matukio mbalimbali ya siku za karibuni likiwamo tukio la Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) kuchoma vitenge vilivyokuwa vimetolewa kama zawadi na Rais Samia Suluhu Hassan. Tukio kama hilo ni ishara ya namna chama kimeshindwa kuleta ushawishi wa kutosha kwa wananchi.
“Kwenye suala hili kwa mfano la kuchoma kanga na vitenge, wananchi hawakumualika Rais Samia, nyinyi ndiyo viongozi mliomualika, mlikwenda kama chama kwenda kumbana Samia kwamba ulitupa zawadi, sasa leo tunataka kuchoma hizi zawadi na mkachoma mbele yake? Wananchi mtawaingiza kwenye matatizo tu bila sababu”, amesema Dkt. Slaa na kuongeza,
Katika kauli yake isiyo na kificho, Slaa amewapa somo Chadema, akiwataka wafahamu kwamba kwenda kulalamika kwa mataifa ya Magharibi kuhusu mchakato na matokeo ya uchaguzi kutawafanya wajiulize maswali magumu kuhusu maandalizi yao hafifu.
Slaa pia amemkosoa vikali Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, kwa kushindwa kutoa maelekezo ya wazi kwa viongozi wa ngazi za chini na wadau wa chama, jambo ambalo limesababisha kukwama kwa maandalizi ya uchaguzi huo.
Kutokana na hali hii, ni dhahiri kwamba Chadema wanajua wazi kuwa wanakabiliwa na kushindwa vibaya kwenye uchaguzi ujao, na karata pekee waliyobakiwa nayo ni kutoa visingizio vya mchakato wa uchaguzi ili kuficha udhaifu wao mkubwa wa kutokujiandaa ipasavyo.
Katika mazungumzo yake, Dkt. Slaa alitilia mkazo umuhimu wa chama kuwa na mikakati ya kuwajengea uwezo wananchi, akieleza kuwa kwa muda mrefu wananchi wa Tanzania hawajawahi kupewa mwongozo madhubuti wa kujitegemea katika harakati za kisiasa.
"Usitegemee wananchi wawe mstari wa mbele, wanahitaji kuongozwa... CHADEMA mliwajengea uwezo? Upi? Kama mliwajengea uwezo wamefika wakashindwa kutekeleza, wananchi wajibu wao nini?" alihoji Dkt. Slaa, akisisitiza kuwa ni jukumu la viongozi wa kisiasa kuwaongoza wananchi na kuwapa moyo wa kusimama kidete kwa ajili ya haki zao.
Dkt. Slaa alitoa mfano wa matukio mbalimbali ya siku za karibuni likiwamo tukio la Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) kuchoma vitenge vilivyokuwa vimetolewa kama zawadi na Rais Samia Suluhu Hassan. Tukio kama hilo ni ishara ya namna chama kimeshindwa kuleta ushawishi wa kutosha kwa wananchi.
“Kwenye suala hili kwa mfano la kuchoma kanga na vitenge, wananchi hawakumualika Rais Samia, nyinyi ndiyo viongozi mliomualika, mlikwenda kama chama kwenda kumbana Samia kwamba ulitupa zawadi, sasa leo tunataka kuchoma hizi zawadi na mkachoma mbele yake? Wananchi mtawaingiza kwenye matatizo tu bila sababu”, amesema Dkt. Slaa na kuongeza,