Dr. Slaa: Kikwete mmiliki wa DOWANS...

Dr. Slaa: Kikwete mmiliki wa DOWANS...

Watazungukaaaaaa kuficha ukweli,ila mwisho wa siku Dowans ni ya kikwete
 
dowanmmilikisuleiman_thumb.jpg
Mmiliki Dowans akagua mitambo Send to a friend Tuesday, 22 February 2011 21:21

dowanmmilikisuleiman.jpg
Miliki wa Dowans, Suleiman Al Adawi akikagua mitambo yake Ubungo Dar es Salaam juzi.
 
Mgawo sasa swali gumu


*TANESCO, wabunge wakosa majawabu
*Wagonganisha vichwa nini kifanywe


Na Tumaini Makene

HATMA ya mgawo wa umeme unaoendelea nchini kwa takribani miezi mitatu sasa bado ni kizungumkuti, huku
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ikikutana na watendaji wa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) kwa saa tano bila suluhisho mwafaka.

Wakati kamati hiyo pamoja na watendaji wa TANESCO wakizungumzia kuwasha mitambo ya kampuni tata ya Dowans kama moja ya njia ya dharura ya kupunguza ama kumaliza tatizo la mgawo wa umeme, Majira limeelezwa kuwa iwapo hatua hiyo itafanyika bila ruksa ya bunge, itakuwa na sawa na kudharau mhimili huo wa dola, kutokana na azimio lake miaka mitatu iliyopita.

Mmoja wa wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini, ambaye alizungumza na Majira katika hali ya kutoandikwa jina lake gazetini, alisema kuwa mbali ya kuweza kulidharau bunge, kuwasha mitambo ya Dowans kama moja ya suluhisho, ina lengo la kutaka kuisafisha kampuni hiyo ionekane kuwa haina tatizo, hivyo kuondoa utata wake uliosababisha mkataba wake na TANESCO wa kuzalisha umeme, ukavunjwa mwaka 2008.

Wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini, chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Bumbuli (CCM), Bw. January Makamba jana kabla ya kukutana na watendaji wa TANESCO, ilikuwa na kikao kifupi kilichoonekana kuwa ni cha maandalizi katika ofisi ndogo za Bunge Dar es Salaam, kabla ya kuanza safari kwenda makao makuu ya shirika hilo.

Wakiwa makao makuu ya shirika hilo, ndani ya kikao baada ya kuwaomba waandishi wa habari wapishe, wajumbe wa kamati na watendaji wa TANESCO walitumia takribani saa tano, kuanzia saa tano asubuhi mpaka saa 10 jioni kupata mapumziko ya muda mfupi kwa chakula cha mchana, huku mambo yakionekana kuwa moto.

Mara kadhaa, watendaji wa TANESCO na wabunge walikuwa wakitengana kwa muda kisha kukutana tena, hali ambayo ilielezewa baadaye na Bw. Makamba kuwa wakati mwingine ililazimika kamati hiyo kuendesha vikao vyake kwa mujibu wa kanuni na taratibu za kibunge na watendaji nao kwenda kujadili pembeni masuala yaliyoibuka katika kikao, kisha pande mbili hizo kukutana tena kuendeleza mjadala kikaoni.

"Ndani tumepokea na kujadili taarifa ya watendaji wa TANESCO ambayo kwa kweli ukiachilia mbali usahihi, ina mambo mengi ikielezea kwa kina sana, wametoa taarifa yao juu ya hali ya mgawo wa umeme, nasi tumeuliza maswali na kutoa ushauri namna gani hatua za kusaidia ziwe za haraka zaidi, kwa sababu TANESCO ina biashara ya kuwasha umeme si kuzuia umeme.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari juu ya mipango ya dharura ya kupunguza au kumaliza mgawo wa umeme, iliyojadiliwa katika kikao hicho Bw. Makamba alisema;

"Ndiyo suala la kuwasha mitambo ya Dowans imejadiliwa ikiwa ni moja ya hatua ya dharura, na wenye mitambo walikuwa hapa nchini na walizungumza na TANESCO, lakini imeshauriwa kuwa suala hilo liangaliwe vizuri, lizungumzwe bila kuathiri kesi iliyoko mahakamani...maana suala hili lina mambo mengi ndani yake;

"Kuna masuala ya kisheria, kisiasa na kiuchumi...mipango mingine iliyojadiliwa ni kuhusu ununuzi wa majenereta ya diseli ambayo yanaweza kuzalisha megawati 260, ambayo yanaweza kupatikana mwezi Juni au Julai. Pia kuna mpango wa kuzalisha megawati 100 kwa gesi hapa Dar es Salaam na megawati 60 kwa mafuta huko Mwanza," alisema Bw. Makamba kabla ya kuendelea na kikao baada ya mapumziko.

Mapema wakati akifungua kikao cha jana, Bw. Makamba alisema kuwa mbali ya kutambuana, kutaka kujua namna shirika hilo linavyoendeshwa, hali ya uzalishaji wa umeme nchini, suala la muhimu ambalo wajumbe wa kikao walipaswa kujikita kujadili ni 'kwa taarifa sahihi, za ukweli na uwazi, namna gani na lini mgawo wa umeme utamalizika nchini'.

Lakini akizungumza na waandishi wa habari, Bw. Makamba alisema kuwa mpaka wanafikia mapumziko, baada ya kuwa wamesikiliza taarifa hiyo aliyoita ya kina kutoka TANESCO na kujadiliana kwa saa tano, kikao hicho kilikuwa bado hakijafikia suluhisho mwafaka hasa juu ya namna gani na lini, mgawo wa umeme unaoendelea kuathiri uchumi na maisha ya kila siku ya Watanzania, utamalizika.

Mpaka Majira linaondoka eneo la kikao, makao makuu ya TANESCO, wajumbe walikuwa wakiendelea na mjadala, ambao mmoja wa maofisa wa bunge wanaohusika katika kamati hiyo ilithibitisha kuwa 'kikao kilikuwa moto kweli'.
 
Nitarudia kusema tena kwamba, sisi wananchi tutaendelea kulaani mbunge au wabunge wanaotetea ununuzi au mkataba wowote na Dowans iwe kwa sababu yeyote ile. Tulikwisha sema serikali ina uwezo wa kununue mtambo mpya kutoka GE au mashirika mengineyo yanayotengeneza ua kuuza genereta kama hiyo. Na sasa Imepita miaka mitatu tunajizungusha tuu na uswahili wa Dowans kana kwamba umeme duniani unazalishwa na mtambo wa Dowans pekee. Hawa wabunge wote watetezi wa Dowans watueleze wazi wanashindwa nini kuagiza genereta nyingine mpya yenya guarantee ya miaka sii chini ya mitano badala yake wanataka tuumize vichwa na Dowans. Madai yao ya awali ilikuwa kwamba itachua miezi 12 kwa genereta mpya kuagizwa hadi ianze kuzalisha umeme, wananchi tulikubali kukaa kizani kwa muda zaidi ya huo waliodai, Leo tena wanakuja na story mpya ati wanaimiza vichwa hali uchumi wa nchi unazidi kudidimia siku hadi siku.. Tuna zaidi ya miaka miwili tunabishana tuu juu ya swala hili pasipo ufumbuzi, hii ni dalili tosha ya kuonyesha mapungufu ya vionozi wetu ktk maamuzi mazito..Dowans imekuwa Dowans...Tunaumiza vichwa kiasi kwa hatuna tena uwezo wa kufikiri nje ya mashine moja ya Dowans
 
Dowans bado kaa la moto Send to a friend Wednesday, 23 February 2011 21:00 0diggsdigg

NAFASI ZA AJIRA KWA VIGOGO ZATANGAZWA

Ramadhan Semtawa na Exuper Kachenje
dowanssite.jpg
KAMATI ya Bunge ya Nishati na Madini jana ilichukua zaidi ya saa tano kukutana na uongozi wa Tanesco kujadili na kutafuta ufumbuzi kuhusu mgawo wa umeme unaoendelea, huku taarifa zikionyesha kuwepo mvutano mkubwa baina ya pande hizo na Tanesco kukataa kujadili suala la Dowans.

Hali hiyo inaonyesha kuwa Dowans bado ni kaa la moto kwa Tanesco na Kamati ya Nishati na Madini inayoongozwa na January Makamba, ambaye ni mbunge wa Bumbuli.

Awali akizungumza katika utambulisho, Makamba alisema dhumuni la ziara ya kamati yake pamoja na mambo mengine ni kutaka kujua mgawo wa umeme utaisha lini na wao kusaidia mawazo katika kutatua tatizo hilo.

"...Tunataka kujua mgawo wa umeme utaisha lini na utaishaje? Na katika hili muwe wazi na sisi tuweze kusaidia mawazo yetu kuondoa tatizo, pia tujue mnaendeshaje Tanesco, matatizo ili tusaidie kwa manufaa ya Watanzania," alisema Makamba.

Mvutano ndani ya kikao
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa ulizuka mvutano mkubwa baina ya wabunge na viongozi wa Tanesco huku ikielezwa kwamba shirika hilo limeshindwa kutoa kwa kamati hiyo mikakati yake ya kumaliza mgawo wa umeme.

Tanesco pia ilidaiwa kukataa kuzungumzia suala la Dowans nje ya Mahakama na kuwashwa kwa mitambo hiyo ili itoe megawati100 za umeme kwa lengo la kupunguza makali ya mgawo wa umeme unaondelea sasa.

"Mvutano mkubwa humo ndani, moto unawaka, Tanesco hawataki hata kuzungumzia suala la Dowans, mvutano unaendelea. Nimechoka maana huku ni kupoteza muda, hatuelewani ili kutatua tatizo," alisema mmoja wa wabunge ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini na kuongeza:

"Tumeomba mikakati yao (Tanesco) katika kumaliza mgawo wameshindwa, wamesema eti bado ipo katika Bodi yao ya Wakurugenzi".

Tanesco wakaa faragha
Ujumbe wa Tanesco ulitoka nje ya ukumbi wa mkutano saa 8:51 mchana na kufanya kikao cha faragha huku baadhi ya wajumbe wake wakionekana kuhaha kuweka sawa mambo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Makamba alikiri kugawanyika kwa pande hizo, lakini akasema kulifuata kanuni.

"Kutoka nje si tatizo, sisi tumefanya kikao kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, inaruhusiwa na imetokana na mwenendo wa mjadala," Makamba alisema.

Alisema kamati yake imepokea taarifa ya Tanesco na kwamba wao wamejikita katika hatua za dharura.

Kuhusu Dowans, alisema kama taarifa zilizokuwepo, wamiliki wa Dowans walikuwepo nchini na wameanza mazungumzo na Tanesco ambapo mazungumzo na taratibu zinaendelea bila kuathiri kesi iliyo mahakamani ili mitambo hiyo itumike.

Hata hivyo, alikiri kuwapo kwa mvutano katika suala hilo na kwamba kazi ya kamati yake ni kushauri hatua za haraka kumaliza mgawo, pia kuishauri Tanesco waingie biashara ya kuwasha umeme na siyo kuzima.

Alisema Jumatatu ijayo kamati yake itakuwa na taarifa na mapendekezo ya kumaliza mgao wa umeme.

Majumuisho ya Kamati
Jana jioni, Makamba alizungumzia majumuisho ya kikao hicho ambapo alisema kuwa wameihimiza Tanesco waharakishe utekelezaji wa miradi ya umeme.

Miongoni mwa miradi hiyo ni ule wa wa megawati 260 kwa njia ya gesi unaotakiwa kukamilika Juni mwaka huu na mingine ambapo alisema tayari Tanesco imeipa kamati hatua zilizofikiwa na wadau wa miradi husika.

Makamba alisema kazi ya kamati yake sasa ni kuisukuma Serikali itoe fedha haraka kukamilisha miradi iliyopo kwenye hatua nzuri ili iweze kukamilika katika muda uliopangwa na kuondoa kabisa tatizo la umeme.

Kuhusu Dowans, Makamba alisema Kamati yake imeiagiza Tanesco kuhakikisha hakuna utata wowote wa kisheria na kwamba iwapo wataingia mkataba na kampuni hiyo basi mkataba huo uwe mfupi na usivuke mwezi Juni mwaka huu.


Nafasi za vigogo wazi
Wakati hayo yakiendelea shirika hilo la umma linajipanga kuwabadili wakuu wote wa vitengo vinavyounda menejimenti yake.

Uamuzi huo wa kuifumua Tanesco pamoja na mambo mengine, umekuja kipindi ambacho shirika hilo limepigwa mawimbi mazito huku wimbi la Dowans, likionekana kutikisa zaidi.

Katika tangazo lake lililotolewa jana kwenye vyombo vya habari, lenye Kichwa cha habari, '' Ajira kwa Nafasi Nyeti za Uongozi,'' Tanesco imeweka bayana kuwa nafasi zote za wakuu wa vitengo ziko wazi na zinahitaji kujazwa.

Nafasi hizo ni pamoja na Meneja Rasilimali Watu, Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Meneja Mwandamizi wa Mipango Mikakati, Meneja Mwandamizi wa Utafiti na Meneja Mwandamizi wa Miradi.

Nafasi zingine zilizotangazwa katika tangazo hilo ni Meneja Mwandamizi wa Uangalizi wa Mfumo na Meneja Mwandamizi Mfumo wa Usambazaji.

Zingine ni Meneja wa Uzalishaji Umeme kwa kutumia Maji, Meneja Mwandamizi Uzalishaji Nishati na Meneja wa Mauzo na Masoko.

Pia anatafutwa mtu wa kujaza nafasi ya Meneja Mwandamizi Usambazaji, na nafasi ya Meneja Uhusiano wa shirika hilo.Mwisho wa kutuma maombi ya kujaza nafasi hizo ni Machi 8, mwaka huu 2011.

Tanesco imekuwa ikitajwa kukabiliwa na matatizo ya menejimenti kwa muda mrefu, hali inayotajwa kama moja ya chanzo cha kuzorota kwa utendaji wa shirika hilo nyeti la umma.

Matatizo mengine yanayoikabili Tanesco ni mikataba mibovu kama ule ulioingiwa kati yake na Richmond ambao baadaye ulirithiwa na Dowans Tanzania Ltd, ambayo sasa inaidai Tanesco Sh94 bilioni kwa kukatisha mkataba kinyume cha taratibu.

Jana Makamba alisema ukaimu wa nafasi mbalimbali ndani ya Shirika hilo kuwa moja ya tatizo la kiutendaji linaloliyumbisha.Makamba alitoa kauli hiyo katika utambulisho wakati kamati yake ilipofanya ziara Makao Makuu ya Tanesco, Ubungo Dar es Salaam."Kaimu wengi, inawezekana hili ni moja ya matatizo,"alisema Makamba.

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Nishati na Madini, alijikuta akitoa kauli hiyo ghafla baada ya mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando, kujitambulisha na kutoa nafasi kwa ujumbe wake kujitambulisha.

Katika utambulisho huo zaidi ya nusu ya wakuu wa idara na vitengo vya Tanesco, walijitambulisha kuwa ni makaimu.
Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Last Updated on Thursday, 24 February 2011 09:02 Comments




0 #11 issa moshi 2011-02-24 11:11 sisi tunaomba mkuu wa police kumkamata huyu adawi afikiswe mahakamani awataje wenzie kwa makosa ya kuhujumu nchi huyu si muoman ni mtanzania anae tumia pasport ya oman huyu adawi anatumiwa na baadhi ya watu nchini
Quote









0 #10 Honorable 2011-02-24 10:48 Hapa kuna ujanja makamba anaucheza wa kiintejensia, anataka kuliingiza Bunge kubarika ufisadi wa Dowans, napenda kuwaonya wabunge walioko kwenye kamati ya makamba, wawe makini hasa wabunge wa Upinzani rasmi Bungeni wasikubali ukuwadi wa makamba wa kutaka mitambo ya dowans iwashwe, Dowans ni wahujumu uchumi, tuwaacheni watanzania tukae gizani hata kwa mwaka mzima lakini tupiganie heshima yetu, na wabunge wetu tafuteni utatuzi endelevu wa maswala ya umeme nchini, nampogeza ztto kabwe kwa kuanza kujadili suluhisho endelevu la umeme, na kuachana na kujadili wahalifu dowans! Kwani Dowans ina uchumi kuliko Tanzania? Hiyo mitambo ya Dowans inagarama kiasi gani kiasi kwamba Tanzania kama nchi haiwezi kumiliki? Kwanini Makamba hujadili umiliki wa Mitambo yetu hata kwa dharura, kwanini unajadili Dowans kila wakati au ndo ulivyo tumwa na chama chako? Hatutaki kusikia mitambo ya Dowans imewashwa! Heri tukae gizani kipindi chote cha utawala wa Kikwete na CCM, kwani ni miaka 5 imebaki! Tutoe hukumu yetu kwenu kwa hasira!
Quote









0 #9 TZA. HATUWAJIBIKI 2011-02-24 10:39 Pigo la TANESCO lina liza umma mzima.
pigo la ATCL lina liza umma mzima.
pigo la Rites RELI lina liza umma mzima.
Looh wenzangu tumebakia na nini? vishindo vilviyo enea humu ni ufisadi mtupu. sioni laa maana kabisa kama kunakuwajibka. Makosa ya poor GOVERNESS.
Je wenzangu hamuoni kuwa tunahujumiwa na nchi jirani? maana kila tukinyanyua kichwa tuna kandamizwa na kila tukianza shughuli/miradi tunazi zoretesha au kupoteza dira na hatimaye kufiya mbali. WHATs going on??
Quote









0 #8 Wakudata 2011-02-24 10:25 Dowans SA wameishitaki Tanesco, kwa kuvunja mkataba kutokana na hiyo mitambo ya Dowans. Ni ajabu na kweli Kamati ya Bunge chini ya January Makamba Mbunge kupitia CCM wanailazimisha Tanesco kuwasha mitambo ya Dowans, Tanesco ndiyo watakaolipa deni hilo la Dowans pesa ya walipakodi ndiyo maana gharama za nishati ya umeme imepanda ili kufidia hasara. Hiyo mitambo isiwashwe hadi kesi imekwisha. Je kuna kibali chochote cha kutoka mahakamani kinachoruhusu kuwashwa mitambo hiyo. Je ni nani anapaswa kukiomba ni Tanesco au Kamati ya Bunge. Tunajua Makamba anapigania maamuzi yaliyopitishwa na Kamati kuu ya CCM kulipwa kwa Dowans SA, ndiyo maana anaipigia debe ili kuihalalisha kiujanja ili baadaye waseme Bunge ndilo limehalalisha uhalali wa Dowans. Sisi Watanzania tunasema hakuna kuwasha mitambo hiyo hadi kieleweke.
Quote









+1 #7 MKWELI 2011-02-24 10:10 Ndugu GILLIARD tATIZO LA UONGOZI WA TANESCO ULIKUWA UNAINGILIWA SANA NA MAFISADI WENGI WAO WALIPEWA HIZO KAZI KWA VIMEMI. HAWAKUAJILI WATU KULINGANA NA SIFA NDIO MAANA UNAYUMBA, HAWAKUWA HURU KUFANYA KAZI ZAO. VIGOGO WALIWAPA KAZI WATU WAO ILI KUHUJUMU NCHI NA LEO NDIO HAPO TULIPOFIKA. USIONE WAMETOA NAFASI ZA KAZI KWA MKUPUO ILI NI KWA AJILI TU MAFISADI ISWAKUTE KASHFA KWANI AJIRA ZA UONGOZI WA TANESCO ULIJAA MIZENGWE SIKU NYINGI. WA KULAUMIWA NI MAFISADI AMBAO WANAJULIKANA.Quoting GILLIARD:
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete acha kuwa Rais Bubu hatujakuchagua uwe kivuli Ikulu.
Vunjilia mbali uongozi mzima wa Tanesco ndio unahujumu uchumi wa Taifa.Anzia Tanesco makao makuu hadi mikoani.Uchumi wa nchi ukiharibika kwa ajili ya uongozi mbovu wa Tanesco wananchi wanajua wewe ndio umeshindwa uongozi.Fumba macho tumia fyagio la chuma.​
Quote









+1 #6 BENSON 2011-02-24 10:09 HIVI, IMEKUWAJE HATA KUFIKIA HAPO? BADO MIMI HAIINGII AKILINI KWA NINI SERIKALI IMESHINDWA KUNUNUA MITAMBO YAKE YENYEWE. KAMATI YA MAKAMBA WALISEMEE NA HILI. TUMECHOSHWA NA HADITHI ZISIZOISHA ZA DOWANS. LEO ANAFIKA MAHALI ATI ANATAKA KUTUWEKEA MASHARTI, SASA HII NI NCHI YENYE RAIS WAKE AU NI KAMPUNI YA [NENO BAYA] FULANI TU? TUTADHALILIKA HIVI MPAKA LINI?
MIAKA NENDA RUDI TUNAHANGAIKA NA VINA VYA MAJI NA MGAO WA UMEME, HIVI NI KWA NINI SERIKALI IMESHINDWA KULIMALIZA HILI? HILI LIPO KILA MWAKA KILA KIANGAZI, TUNASHINDWAJE KULIMALIZA? WAKO WAPI WASOMI WA NCHI HII? HEBU TUFIKE MAHALI TUACHE HUU U[NENO BAYA] UNAOITWA SIASA, UMEPITWA NA WAKATI. TUNAKUWA KAMA HATUAMINI KUWA TULIKWISHA PATA UHURU, TUNATAKA WENGINE WATUSAIDIE HATA PALE AMBAPO UWEZO TUNAO? HESHIMA YETU IKO WAPI?
Quote









+1 #5 JOHN 2011-02-24 09:49 Sikirizeni bwana mm naona hapa kuna sumu hata hawa Tanesco wamelishwa na yawezekana ikawa wanamjua mmiliki halisi wa mitambo hiyo ndio maana hawakutaka kuzungumzia hizo habari wakihofia kufukuzwa kazi mm naiomba hiyo kamati ya nishati ya bunge itafute njia mbadala yakuweza kafanya kazi zake vizuri kwa manufaa ya watanzania,tofa uti na hivyo hawatafanikisha lolote.
Quote









-1 #4 Zanzibari Mtanzania 2011-02-24 09:35 Ukeli umejulikana na haki isemwe wazi
Maoni mengi jana tuliyasikia na kusoma kwa kumsakama Mwarabu/mOmani eeti alikuwa anafuata nini. Ngoma ipo kwa wanaSIASA kutuuza bei ndogo. Huyu mmiliki wa DOWANZ anafuatilia kazi na miliki yake kama alivyo ahidi huko alipozitoa ULAYA/UMERKANI/SINGAPORE /popte, wenye mali wamemuamrisha kufuata malipo na hatma ya mitambo, sivyo tunavyo dhania Watanzania. Ikiwa humu ndani Tunatapeliwa na wana Siasa wetu au Viongozi mafisadi. Basi ujuwe mwarabu naye kesha chapwa vibaya, Ndiyo maana ameamua kujitosa na kugaragara hapa na kutupiwa lawama na kupigwa chenga za Wabongo. Sura yote utaielewa hivi sii punde.
Quote









+1 #3 Modern Day 2011-02-24 09:22 Shukrani Kwa Gzti.Mwananchi kutuletea habri nzito na moto za Dowans. Ukweli umejulikana kuwa kuna mvutano baina ya Kamati v/s Utendaji. yaani kwa kifupi baina ya siasa na uongzi.Ukitafakari utaona kuwa kuna uhondo wa mambo wenye lengo la kuhujumu uchumi na uzalishaji nchini, Kwani yote hayo tuna shuhudia upungufu mkubwa kapata umeme kukimu kazi na maendeleo ya viwanda vidogo na vya kati. Je Wa Tanzania hamuoni hapo kuna utata fulani, Wapo tayari kuzorotesha uchumi wetu humu ili mambo (agenda) zao zipite na kusambaza mali na biashara zao zichanganye faida na sisi watuachie Siasa na malumbano baina yetu WaTZA.(hiyo ni sabotage ndogo tu).Nina Amini kuna watu wanalipwa na nchi jirani.(pelelezni kuna payroll kwa kundi moja).
La pili inafahamika sasa kuwa " Wahusika wana uza TIME ".
hayo utayajua kama una miliki mradi au kazi,Biashara,h ata workshop ndogo tu utaona taathira zake na hasara zake.
Quote









-2 #2 GILLIARD 2011-02-24 09:16 Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete acha kuwa Rais Bubu hatujakuchagua uwe kivuli Ikulu.
Vunjilia mbali uongozi mzima wa Tanesco ndio unahujumu uchumi wa Taifa.Anzia Tanesco makao makuu hadi mikoani.Uchumi wa nchi ukiharibika kwa ajili ya uongozi mbovu wa Tanesco wananchi wanajua wewe ndio umeshindwa uongozi.Fumba macho tumia fyagio la chuma.
Quote









0 #1 MKWELI 2011-02-24 09:11 NAWAPONGEZA TANESCO KWA KUKATAA MAADHIMIO YA MAFISADI, HAIWEZEKANI WEWE TANESCO UMEFIKISHWA MAHAKAMANI KAMA MUHARIFU. KWA HIYO USIKUBARI KUJADILI NJE YA MAHAKAMA, HUYO MAKAMBA ANATUMIWA TU!. HIYO NIJANJA YAO MAFISADI KUTUCHINJA KIMYAKIMYA. TANESCO MKISHINDWA TUAMBIENI WANANCHI!
Quote
 
MWANGAZA NILISHAWAHI KUANGAZA HII:



Jk, rex na downs ni kitu kimoja !!
Wadau hivi hamjiuliza kwanini serikali ilitumia kampuni ya sheria ya REX kwenye mktaba wa Richmond na baade DOWANS. REX iliishauri serikali ililipe DOWANS mabiliaoni ya shilingi bila kukata rufaa ikingali inajua kukata rufaa inawezekana,

Kwa mazingila hayo tunzaidi kutilia shaka utendaji kazi wa REX na uhusiano wake na JK. Kwa mfano angalia baadhi ya watendaji wa REX na uhusiano wao na JK.

1. Arafa Mohamed (Mrs. Ridhiwani JK)

Huyu ni mke wa mtoto wa JK (Ridhiwani kikwete) na ni mfanyakazi wa REX Attorney. Uhusiano wake kikazi nawa familia ya JK unatilia mashaka ushirikishwaji wa JK na DOWANS. Arafa anakihisiwa kulinda maslahi ya babamkwe (JK) ktk DOWANS akiwa REX.

2. Mwanaidi Sinare Maajar

Huyu ni mmoja wa wanahisa wakubwa wa REX na nani balozi wa Tanzania nchin Marekani. Huyu mama amekuwa balozi wa TZ nnchi UK kwa mda mrefu kabla ya kuteuliwa kwenda USA juz juz na JK. Ukaribu wake kikazi na JK unatia mashaka kulinda maslahi binafsi ya JK ktk DOWANS.


3. Mr. Sinare Zaharan na Dr. Eve Hawa Sinare

Hawa ni wanahisa wengine wa REX na wanaundugu wa karibu sana na Balozi Maajar.
undugu huu na Balozi maajar unazidi unatilia mashaka utendaji wa REX na maslahi binafsi ya JK ktk DOWANS

4. Dr. Alex Thomas NgulumaHuyu ni mwanahisa wa REX na wakili maarufu wa mahakama kuu ya TZ na ZNZ. Akiwa wakili mzoefu tena wa mahakama kuu inashangaza alishaurije DOWANS walipwe tena kabla hata kesi haijasijiliwa na mahakama kuu.Hapa inatutia shaka hata utendaji wa haki ktk kesi iliyofunguliwa na wanaharakati kupinga ulipaji wa DOWANs kama mahakama kuu kuna watu kama hawa wanotumia sheria kupindisha haki kwa maslahi ya wachache.

UHUSIANO WA REX NA ROSTAM

Rostam Aziz aliyemilikishwa kisheria kushughulikia shughuli za DOWANS Tanzania, ana ukaribu wa karibu sana na REX ambayo imekuwa ikshughulkia shughuli zake mbalimbali kisheria hasa kampuni yake ya CASPIAN Construction iliyokuwa imepanga jengo moja na REX kwenye gholofa moja la NIC mitaa ya posta, kabla REX hawajaa mia kwenye jengo lao mitaa ya Upanga. Inasemekana pia kwamba JK na Lowassa walikwa wanaenda mara kwa mara CASPIAN mwaka 2005 kabla hajagombea urais 2005. Tetesi zisema walikuwa wanaenda kupata support ya kifedha..ndo maana JK anashindwa kumgusa mfadhili wake wa muda mrefu (RA)​
 
Ipo mkala nyingine ya mchango ya Ridhiwani kwenye JF Jukwaa la siasa ambayo inaonyeoshe jinsi ukoo wa kifalme wa Jk unavyojihusisha moja kwa moja na uendeshaji wa Kampuni ya kifisadi ya DOWANS.......................
 
Chadema waiteka Mwanza Send to a friend Thursday, 24 February 2011 21:39

WAMTAKA JK KUTOA TAMKO KUHUSU UFISADI, DOWANS NA HALI YA NGUMU YA MAISHA
Frederick Katulanda na Sheila Seizzy, Mwanza
_dk%20wilbord%20slaa.jpg
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana kililiteka Jiji la Mwanza, pale viongozi wake wa kitaifa walipoongoza maelfu ya waandamanaji katika Jiji hilo.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa na wabunge kadhaa waliowaongoza maelefu ya wandamanaji katika kile walichosema kuwa ni kupinga kupanda kwa gharama za maisha, malipo kwa Kampuni ya Dowans na kupanda kwa gharama za umeme.

Katika mkututano wa hadhara uliohitimishwa katika Viwanja vya Furahisha, Dk Slaa alitoa siku tisa kwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli kuhusu kushamiri kwa vietndo vya ufisadi, malipo ya Dowans na suluhisho la kupanda kwa gharama za maisha kwa Watanzania.

Dk Slaa alisema iwapo Serikali itakaa kimya basi Chadema kitaitisha maandamano ya nchi nzima ili kushinikiza mabadiko kama ilivyo katika nchi za Misri na Tunisia.

Alisema kitendo cha Rais Kikwete kuendelea kukaa kimya kitasababisha Chadema kuchukua hatua ya pili ambayo wataitisha maandamano nchi nzima.

Kabla ya mkutano huo, kulikuwa na maandamano yaliyoanzia katika Uwanja wa Shule ya Msingi Buzuruga na kupita katika Barabara za Nyerere, Pamba na kuingia Barabara ya Kenyatta na ile ya Uwanja wa Ndege na kuhitimishwa katika Uwanja wa Furahisha.

Wakipita katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza, waandamanaji walikuwa na mabango wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa kuilaumu Serikali kutokana na kile walichosema kuwa ni kufumbia macho ufisadi.

Aidha, akizungumzia suala la Dowans, Dk Slaa alisema kamwe kodi ya wananchi haitotumika kuilipa kampuni hiyo na kwamba kama wanataka kampuni hiyo kulipwa basi zitumike fedha za Rais Kikwete,Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Alisema ujio wa mmiliki wa Dowans, Suleyiman Al Adawi ni mbinu za kutaka kuwahadaa Watanzania.

"Dowans haiwezi kulipwa kwa kodi za wananchi kutokana na kampuni hiyo kuwa mtoto haramu, mama na baba yake ni Richmond na hayo yote yanayofanyika Rais Kikwete anayajua sababu yanafanyikia katika Serikali ya Tanzania, "alisema Dk Slaa.

Alisema Rais Kikwete ana maswali mengi ya kujibu kutokana na Dowans kwa sababu Serikali ilitoa fedha nyingi za wananchi za kuleta mitambo hiyo ya umeme na kununua vifaa ili Dowans izalishe umeme, lakini leo nchi ipo gizani.

Kupanda kwa gharama za maisha
Katika hatua nyingine, Dk Slaa alisema kupanda kwa gharama za maisha kunatokana na kupanda kwa umeme pia kukatika kwa umeme ambapo uzalishaji haufanyiki kama inavyotakiwa.

Alisema tabia ya wabunge wa CCM kuwazomea na kuwatisha wabunge wa Chadema wasiongee bungeni ni kazi bure na kusema kuwa kama hawatojirekebisha kwa hilo watawahamasisha wananchi kuwazomeoa wabunge hao majimboni kwao kama ilivyokuwa kipindi kile cha EPA.

Dk Slaa pia alimtahadharisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro kutokuingilia mamlaka ya Halmashauri ya Jiji na badala yake amuachie Meya wa Jiji hilo ambaye ni kutoka Chadema afanye kazi kwani yeye ndiye aliye na mamlaka hayo.

Alisema kwa mujibu wa sheria namba 19 ya mwaka 1999 inamtaka Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya kuwa wawezeshaji na sio watu wa kuingilia mamlaka ya Halmashauri ya Jiji.

Mbowe aonya Serikali kuhusu ufisadi
Kwa upande wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kama Serikali haitaweze kuinua maisha ya Watanzania kwa kuwaondolea ugumu wa maisha, wananchi wanaweza kutumia nguvu kukabiliana na mafisadi.

Wakatia akihutubia adhara hiyo ya watu waliokusanyika katika mkutano huo, Mbowe aliwaomba wananchi hao kuelezea Serikali kuwa wapo tayari kudai haki zao na kusema kuwa viongozi wa Chadema wakiongea CCM wanasema kuwa wanawaongopea wananchi kuwa hawajawatuma.

"Tumenyanyaswa, tumetishwa sasa tunasema kuwa tumechoshwa na tunasonga mbele kudai haki pamoja na uhuru na kama hawatoweza kutupatia nguvu zetu zitakuwa zaidi ya Libya," alisema Mbowe.

"Mnataka na Kikwete ajiuzulu pia," wananchi walimjibu kwa sauti "Ndiyo" Mbowe aliendela na kusema, "Sawa nimewaelewa kumbe mnataka Rais Kikwete naye ajiuzulu pamoja na Ngeleja na Waziri Mwinyi (Hussein) pia ajiuzulu..ahaa ngojeni kwanza Kikwete tunataka kwanza tumalize kupita mahali pote na kuzunguka yeye inakuja yake babu kubwa kama ya Misri na Tunisia," alieleza Mbowe.

Alisema Serikali ipo katika mpango wa kukodisha umeme kwa muda wa miezi minne na katika kipindi hicho wanazalisha umeme kwa kutumia kodi za Watanzania Sh 400 bilioni kulipa kampuni inayokodisha mitambo hiyo ya umeme.

Alisema Serikali kukubali kulipa Sh 300 bilioni za kunulia mafuta ni wizi mkubwa na kwamba uvumilivu wa Watanzania umefikia ukomo hivi sasa.

"Tumevumilia vya kutosha, safari hii ni ama zao ama zetu. Hatuwezi kukubali nchi imekaa miaka minne hakuna ufumbuzi wa umeme, taifa linalipa fedha za ajabu, hakuna anayejiuzulu na safari hii hatukubali,"alisema Mbowe na kuongeza:

"Mkuu wa Mkoa anatumia jenereta, Waziri Ngeleja, Waziri Mkuu wote hawa hawajui shida ya umeme, shida iko kwetu wananchi hivyo wananchi lazima tuchukue hatua".

Baada ya hapo aliwauliza wananchi iwapo wanataka Waziri Ngeleja ajiuzulu, wananchi walijibu ajiuzulu na kumtaja Rais Kikwete pia kujiuzulu.

Katiba ya nchi

Mbowe alisema aliwaongoza wabunge kutoka nje kumfikishia Rais Kikwete kutaka mabadiliko na kwamba hatua ile ilibezwa na viongozi wa CCM ambao leo hii wanaushangaza umma kwa kujadili mabadiliko ya Katiba.

Alisema baada ya hatua hiyo, mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika aliwasilisha bungeni hoja kuhusu suala hilo, lakini haikuweza kujadiliwa na hivyo kuwataka wananchi kuvumilia kwa vile sasa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya utaanzia bungeni Aprili mwaka huu.

Joseph Mbilinyi na Halma Mdee
Kwa upande wake, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi alisema kuwa Tanzania haina amani kama Serikali ya CCM inavyowatangazia wananchi.Alisema anashangaa hata wabunge wakiingia bungeni wanakaguliwa, sasa je wananchi wa mitaani.


Jonh Mnyika na Godbless Lema
Pamoja na kuambiwa kumuobaa radhi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisisitiza kauli yake kuwa alidanganya na kusema kuwa kamwe hawezi kuomba radhi.

Alisema Jeshi la Polisi mkoani Arusha liliomba siku 60 kufanya upelelezi wa mauaji yaliyotokea jimboni kwake, inakuwaje leo anasimama na kuwadanganya wananchi kuwa Chadema ndiyo waliofanya mauaji hayo wakati hata upelelezi haujakamilika.

Kwa upande wake, Mnyika alisema kupanda kwa gharama za maisha ni matokeo ya mafisadi.

Alisema kuwa anashangazwa na agizo la Serikali kushusha bei ya sukari nchini ambayo imepanda mpaka kufikia Sh 2000 kwa kilo moja kutoka katika bei ya kawaida iliyokuwapo ya Sh 1600.

"Watanzania agizo hilo la Serikali limetokana na maandamano ya leo waliposikia tuna andamana kupinga mfumuko wa bei pamoja na Dowans kutokulipwa kwa kodi za wananchi na wao wakajifanya kutoa agizo hilo, "alisema Mnyika.

Wabunge wa Mwanza
Kwa upande wa wabunge hao wa Chadema mkoani Mwanza waliohudhuria mkutano huo walisema kuwa watahakikisha wanainua maisha ya wana-Mwanza kwa kusimamia rasirimali zilizopo mkoani hapa na kuifanya wilaya ya Bunda ambayo ndiyo ya kwanza kwa umasikini kuondoka kwenye nafasi hiyo .

Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje alisema kuwa ni aibu kwa wana-Mwanza kuchachuka na maisha wakati mkoa huu uonaongoza kwa kuwa na rasilimali nyingi ambazo kama zitasimamiwa ipasavyo zitawakomboa wananchi wake.

Maandamano ya Mwanza yamefanyika takribani miezi miwili tangu kutokee mauaji ya raia waliopigwa risasi na polisi mkoani Arusha, wakati walipokuwa wakizuia maandamano ya Chadema mkoani humo.

Katika tukio hilo la Januari 6, mwaka huu polisi wa Arusha walimwaga damu za watu kadhaa na wengine zaidi ya 30 walijeruhiwa miongoni mwao wakiwamo walioshiriki na wasioshiriki maandamano yaliyoandaliwa na Chadema.

Risasi za moto na mabomu ya machozi vilitumika katika jitihada za polisi kuzima maandamano hayo, wakitekeleza amri ya Mkuu wa Jeshi hilo, Ispekta Jenerali Said Mwema ambaye awali aliyapiga marufuku baada ya awali kuwa yameruhisiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Last Updated on Friday, 25 February 2011 08:49 Comments




0 #12 Kimweri ye Nyumbai 2011-02-25 09:48 Imefika mahali Watanzania lazima wajuwe haki zao za msingi kama wazawa na watu wanaostahili kula vizuri,kulala mahali pazuri,kupata afya na elimu bora na kuwa na uhuru na ardhi yao.Wakubwa wetu akiwemu Rais tuliyempa dhamana ya kutuongoza,wame kuwa watu wakujimegea mkate na kupaka siagi huku wakimezea na chai ya maziwa wakituacha Watanzania wengi tukinywa chai ya rangi isiyo na kitafunwa(instr umental)matokeo yake tunapata vidonda vya tumbo,ndiyo shida tunayoipata sasa ambapo wakubwa hawaioni wala kusikia kwasababu hawashindi njaa,hawakosi wala kulipia umeme,hawaendi sokoni kununua nyanya,watoto wao wanasoma kwa raha,lini watamkumbuka Mtanzania wa kawaida.

Yote haya ni matokeo ambayo Watz tumejitafutia katika uchaguzi mkuu uliopita.Viongozi wa vyama vya upinzani hasa CHADEMA wamezunguka kila mahali kuwaelimisha watu lakini wananchi wakaamua kuwarudisha bungeni wanafiki wa ccm,wakashangil ia JK kurudi Ikulu,haya leo mtasema nini?Mafuta ya kupikia,unga wa mahindi,sukari vyote bei juu na mishahara haipandi.Hainingii akilini kumuona Mtz wakawaida anaishabikia ccm tena amevaa t-shirt na kofia,hamna aibu?

Watanzania amkeni acheni kulala Tanzania bilA ccm na JK inawezekana.Raisi nchi inamshinda,alow aweka madarakani(masw ahiba)wamemgeuk a,hawatendi kazi walopewa.

Hongera sana Wanamwanza na CHADEMA,CCM NI DUDU LIUMALO BILA HURUMA LAZIMA TULITWANGE RUNGU LA KICHWA LISITUAMBUKIZE MAGONJWA.

Quote









0 #11 Junior 2011-02-25 09:40 wewe Sawia ni mpuuuuzi mkubwa. Hapa tunaongelea maandamano ya Mwanza na madai yake hatuongelei ni kabila gani limefanya nn. Hebu nipe jina moja la Mchaga ambaye ni Fisadi na useme ufisadi wake ni nn. Tatizo kwako ni wachaga kusoma au? nani alikataza kabila lako wasisome? Badala ya kuongea matatizo yetu na uozo wa serikali ww unaturudisha kwenye ukabila!.Mshenziiii sana we
Quote









+1 #10 MKWELI 2011-02-25 09:26 kwa hali hii, naishauri serikali ya CCM ichukue hatua za haraka. lakini watanzania nawaonya tusitegemee hali ikawa kama TUNISIA au EGYPT, zile nchi ni tofauti ni nchi za kiarabu. nakumbuka hata aliyekuwa rais wa Tunisia BIN ALLY aliambiwa na mfalme wa SAUDIA kuwa "ondoka haraka hapo TUNIS usije ukasababisha umwagaji damu kwa ndugu zetu wa kiarabu, hatutaki kuona kabisa waarabu wenzetu wakiuwana" ndio maana mapinduzi yalikuwa ya Amani. kadhalika na EGYPT JESHI LILIKATAA AMRI KUTOKA KWA HUSSEIN MUBARAKA KUDHIBITI MAANDAMANO NCHINI EGYPT.jeshi lilisema "hatutoweza kuingilia kati kwani tutasababisha umwagaji mkubwa wa damu dhidi ya waarabu wenzetu". KWA HIYO NCHI HIZI ZISICHUKULIWE KAMA MFANO HAWA NI WAARABU WANAPENDANA WENYEWE. LAKINI IKITOKEA HAPA KWETU HISTORIA ITAKUWA TOFAUTI KABISA. YATAJIRI YA RWANDA GENOSIDE 1994.HALI ITAKUWA TOFAUTI. HIVYO WADAU TUSITEGEE HILO TUJIPANAGENI MPAKA 2015 CCM TUTAIONDOA KWA AMANI NA SALAMA.
Quote









0 #9 Al-Dowans 2011-02-25 09:26 Jambo ambalo bado nazidi kulitafakuri lakini sioni mwelekeo wa kupata jibu ni; Inakuwaje Mmiliki wa Richmond, Mohamed Gire aletwe na Rostam Aziz (Kama alivyokiri Salva Rweyemamu kwamba alitambulishwa kwake na Rostam), pia Mmiliki wa Dowans, kampuni ambayo haikuwahi kuwa na uhusiano wa kibiashara na Richmond, aletwe tena na Rostam!
Wabongo hapa ni AKILI KUMKICHWA.

Quote









0 #8 mwanamaendeleo 2011-02-25 09:20 hiyo ni rasharasha mvua kamili yenye ngurumo na radi inakuja
PEOPLES POWER

Quote









0 #7 sawia 2011-02-25 09:19 Naomba tuelewe kuwa mafisadi tanzania siyo wako CCm tu wapo wengi ukiwa pamoja na mbowe, umasikini wa kitanzania mwingi umeletwa na ninyi mliosoma mwazo (wachaga na wahaya) wengi wenu mliliibia taifa sana. BISHENI! (sisemi wote kwani wapo watakatifu).
Wewe mbowe lini umelala na giza? Tukianza maandamano kama tunisia je wewe utakufa au sisi ndo tufe?
Watanzania: moja tutoe kikwete aondoke pili mbowe na mafisadi wengine. Msiandamane pupa tumieni vichwa kabla ya maandamano,ukio na kuna dalili ya kifo acha! angalieni kibaki na Laila wanakula kuku jamaa wameondoka. Akiingia mchaga ikulu mamayangu nchi itauzwa mara mbili. Karibuni kwa majibu wenye uchungu na niliyosema. na toeni facts. NB siyo wachaga wote wezi ila wengi wametufikisha hapa tulipo. vupumba! tembelea tovuti yangu: www.factscorruption.tz

Quote









0 #6 Geoffrey 2011-02-25 09:19 Safi sana Kamanda Sirro unastahili kuwa IGP unajua kazi siyo kama Mwema na Andengenye umeonyesha ukomavu wa hali ya juu hauchangani utendaji na siasa unastahili tuzo kumbe polisi ndiyo waanzishaji wa vurugu mbona maandamano na mkutano umeisha salama Mwema watanzania tu wastaarabu muda wa
Quote









+1 #5 Mchungu wa Bongo 2011-02-25 09:11 Na bado, hongereni Chadema, hongereni wana wa Mwanza, hongereni Watanzania wote wenye moyo wa kishujaa mlioi-support Chadema pale Mwanza, Mungu ibariki Chadema, Mungu wabariki Watanzania wanaonyonywa na serikali ya JK, na kama serikali hiihaitasoma alama za nyakati, basi utafika wakati nguvu ya umma itaamua maamuzi magumu kama Tunisia, Misri na Egypt, mkifikiri kwamba haya hayawezi kutokea Tanzania endeleeni na kuwanyonya Watanzania na kuwafanya [NENO BAYA], mtaisoma namba ya kiatu aliyoiva Hosni Mubaraki na aliyeivaa Gaddafi, asomaye na afahamu
Quote









+2 #4 JUMA ABDU 2011-02-25 08:59 Napongeza maandamano ya chadema huko MWANZA
Quote









+1 #3 wabogojo 2011-02-25 08:58 ee Mwenyezi Mungu wasaidie wananchi wa Tanzania.. nina swali rahisi sana kwa wananchi wenzangu kama tuunauwezo wa kukodisha hio mitambo ya dowans kwa miezi 4 kwanini tusinunue serikali na Tanesco wasinunue mitambo yao wenyewe? sababu kuu kama wakikodisha kwa miezi minne je mwaka mwingine ikitokea shida ya umeme tu[NENO BAYA]disha tena. na kama hatuna hela hautwezi nunua kwa installment kuliko kukodisha hii mitambo ya ROSTAM? hili swala linadhihirisha wazi kuwa ni mradi wa mtu wa ccm na huyu JK najua wazi kabisa..! anaenda sulhisha mambo ya nchi nyingine wakati nchini kwake kuna shida kubwa kuliko hizo nchii..! ee bwna Mungu wasaidie hawa CCM walipotufikisha inatosha..! si lengo letu wala furaha yetu kutokea mabo ya Libya, Tunisia na Libya hapa nchini ila inafikia sehemu tufanye kwa faida ya kizazi kinachokuja..! Ngeleja hana uwezo kuwa hata mkuu wa shule ya primary jamani..!
Quote









+4 #2 fredy chokela 2011-02-25 07:37 Mwenye macho haambiwi tazama, hivi nyie mliooona kuwa JK anauwezo wa kutuongoza na mkampa kura zenu na leo yanawatokea puani, najua walioandamana jana siyo wafuasi wa Chadema tu kwani nafsi zao zinawasuta baada ya kuona maisha yamekuwa magumu..Mie ningependa kuuliza swali, Je nyie mliowapigia kura hawa viongozi wa ccm huu mgao wa umeme nyie hammo?? Je hizi bei kubwa za vitu hizo kadi zenu za ccm huwa mkizionyesha kwa wauza bidhaa huwa mnapunguziwa bei ya bidhaa??
Watanzania nawaomba mbadilike kifikrakwani hawa viongozi wa Chadema hawawezi kusema kitu bila uhakika, huuu ni mwanzo tu baada ya uchaguzi kuisha je hiyo bajeti itakuwaje, ooohhh mungu wasaidie hawa ccm kwa hata chembe ya huruma hawana....

Quote









0 #1 Amanda 2011-02-24 22:07 Jamani naomba kujua hapa kwetu Tanzania utasikia barabara ya Kenyatta sijui Kwame nkuruma na majina kibao hivi na nchi nyingine kama Kenya nako kuna barabara kama ya Nyerere, Mkapa au Mwinyi?? Msaada tutani tafadhali
 
Chadema waiteka Mwanza Send to a friend Thursday, 24 February 2011 21:39

WAMTAKA JK KUTOA TAMKO KUHUSU UFISADI, DOWANS NA HALI YA NGUMU YA MAISHA
Frederick Katulanda na Sheila Seizzy, Mwanza
_dk%20wilbord%20slaa.jpg
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana kililiteka Jiji la Mwanza, pale viongozi wake wa kitaifa walipoongoza maelfu ya waandamanaji katika Jiji hilo.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa na wabunge kadhaa waliowaongoza maelefu ya wandamanaji katika kile walichosema kuwa ni kupinga kupanda kwa gharama za maisha, malipo kwa Kampuni ya Dowans na kupanda kwa gharama za umeme.

Katika mkututano wa hadhara uliohitimishwa katika Viwanja vya Furahisha, Dk Slaa alitoa siku tisa kwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli kuhusu kushamiri kwa vietndo vya ufisadi, malipo ya Dowans na suluhisho la kupanda kwa gharama za maisha kwa Watanzania.

Dk Slaa alisema iwapo Serikali itakaa kimya basi Chadema kitaitisha maandamano ya nchi nzima ili kushinikiza mabadiko kama ilivyo katika nchi za Misri na Tunisia.

Alisema kitendo cha Rais Kikwete kuendelea kukaa kimya kitasababisha Chadema kuchukua hatua ya pili ambayo wataitisha maandamano nchi nzima.

Kabla ya mkutano huo, kulikuwa na maandamano yaliyoanzia katika Uwanja wa Shule ya Msingi Buzuruga na kupita katika Barabara za Nyerere, Pamba na kuingia Barabara ya Kenyatta na ile ya Uwanja wa Ndege na kuhitimishwa katika Uwanja wa Furahisha.

Wakipita katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza, waandamanaji walikuwa na mabango wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa kuilaumu Serikali kutokana na kile walichosema kuwa ni kufumbia macho ufisadi.

Aidha, akizungumzia suala la Dowans, Dk Slaa alisema kamwe kodi ya wananchi haitotumika kuilipa kampuni hiyo na kwamba kama wanataka kampuni hiyo kulipwa basi zitumike fedha za Rais Kikwete,Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Alisema ujio wa mmiliki wa Dowans, Suleyiman Al Adawi ni mbinu za kutaka kuwahadaa Watanzania.

“Dowans haiwezi kulipwa kwa kodi za wananchi kutokana na kampuni hiyo kuwa mtoto haramu, mama na baba yake ni Richmond na hayo yote yanayofanyika Rais Kikwete anayajua sababu yanafanyikia katika Serikali ya Tanzania, ”alisema Dk Slaa.

Alisema Rais Kikwete ana maswali mengi ya kujibu kutokana na Dowans kwa sababu Serikali ilitoa fedha nyingi za wananchi za kuleta mitambo hiyo ya umeme na kununua vifaa ili Dowans izalishe umeme, lakini leo nchi ipo gizani.

Kupanda kwa gharama za maisha
Katika hatua nyingine, Dk Slaa alisema kupanda kwa gharama za maisha kunatokana na kupanda kwa umeme pia kukatika kwa umeme ambapo uzalishaji haufanyiki kama inavyotakiwa.

Alisema tabia ya wabunge wa CCM kuwazomea na kuwatisha wabunge wa Chadema wasiongee bungeni ni kazi bure na kusema kuwa kama hawatojirekebisha kwa hilo watawahamasisha wananchi kuwazomeoa wabunge hao majimboni kwao kama ilivyokuwa kipindi kile cha EPA.

Dk Slaa pia alimtahadharisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro kutokuingilia mamlaka ya Halmashauri ya Jiji na badala yake amuachie Meya wa Jiji hilo ambaye ni kutoka Chadema afanye kazi kwani yeye ndiye aliye na mamlaka hayo.

Alisema kwa mujibu wa sheria namba 19 ya mwaka 1999 inamtaka Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya kuwa wawezeshaji na sio watu wa kuingilia mamlaka ya Halmashauri ya Jiji.

Mbowe aonya Serikali kuhusu ufisadi
Kwa upande wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kama Serikali haitaweze kuinua maisha ya Watanzania kwa kuwaondolea ugumu wa maisha, wananchi wanaweza kutumia nguvu kukabiliana na mafisadi.

Wakatia akihutubia adhara hiyo ya watu waliokusanyika katika mkutano huo, Mbowe aliwaomba wananchi hao kuelezea Serikali kuwa wapo tayari kudai haki zao na kusema kuwa viongozi wa Chadema wakiongea CCM wanasema kuwa wanawaongopea wananchi kuwa hawajawatuma.

“Tumenyanyaswa, tumetishwa sasa tunasema kuwa tumechoshwa na tunasonga mbele kudai haki pamoja na uhuru na kama hawatoweza kutupatia nguvu zetu zitakuwa zaidi ya Libya," alisema Mbowe.

“Mnataka na Kikwete ajiuzulu pia,” wananchi walimjibu kwa sauti “Ndiyo” Mbowe aliendela na kusema, “Sawa nimewaelewa kumbe mnataka Rais Kikwete naye ajiuzulu pamoja na Ngeleja na Waziri Mwinyi (Hussein) pia ajiuzulu..ahaa ngojeni kwanza Kikwete tunataka kwanza tumalize kupita mahali pote na kuzunguka yeye inakuja yake babu kubwa kama ya Misri na Tunisia,” alieleza Mbowe.

Alisema Serikali ipo katika mpango wa kukodisha umeme kwa muda wa miezi minne na katika kipindi hicho wanazalisha umeme kwa kutumia kodi za Watanzania Sh 400 bilioni kulipa kampuni inayokodisha mitambo hiyo ya umeme.

Alisema Serikali kukubali kulipa Sh 300 bilioni za kunulia mafuta ni wizi mkubwa na kwamba uvumilivu wa Watanzania umefikia ukomo hivi sasa.

"Tumevumilia vya kutosha, safari hii ni ama zao ama zetu. Hatuwezi kukubali nchi imekaa miaka minne hakuna ufumbuzi wa umeme, taifa linalipa fedha za ajabu, hakuna anayejiuzulu na safari hii hatukubali,"alisema Mbowe na kuongeza:

"Mkuu wa Mkoa anatumia jenereta, Waziri Ngeleja, Waziri Mkuu wote hawa hawajui shida ya umeme, shida iko kwetu wananchi hivyo wananchi lazima tuchukue hatua".

Baada ya hapo aliwauliza wananchi iwapo wanataka Waziri Ngeleja ajiuzulu, wananchi walijibu ajiuzulu na kumtaja Rais Kikwete pia kujiuzulu.

Katiba ya nchi

Mbowe alisema aliwaongoza wabunge kutoka nje kumfikishia Rais Kikwete kutaka mabadiliko na kwamba hatua ile ilibezwa na viongozi wa CCM ambao leo hii wanaushangaza umma kwa kujadili mabadiliko ya Katiba.

Alisema baada ya hatua hiyo, mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika aliwasilisha bungeni hoja kuhusu suala hilo, lakini haikuweza kujadiliwa na hivyo kuwataka wananchi kuvumilia kwa vile sasa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya utaanzia bungeni Aprili mwaka huu.

Joseph Mbilinyi na Halma Mdee
Kwa upande wake, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi alisema kuwa Tanzania haina amani kama Serikali ya CCM inavyowatangazia wananchi.Alisema anashangaa hata wabunge wakiingia bungeni wanakaguliwa, sasa je wananchi wa mitaani.


Jonh Mnyika na Godbless Lema
Pamoja na kuambiwa kumuobaa radhi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisisitiza kauli yake kuwa alidanganya na kusema kuwa kamwe hawezi kuomba radhi.

Alisema Jeshi la Polisi mkoani Arusha liliomba siku 60 kufanya upelelezi wa mauaji yaliyotokea jimboni kwake, inakuwaje leo anasimama na kuwadanganya wananchi kuwa Chadema ndiyo waliofanya mauaji hayo wakati hata upelelezi haujakamilika.

Kwa upande wake, Mnyika alisema kupanda kwa gharama za maisha ni matokeo ya mafisadi.

Alisema kuwa anashangazwa na agizo la Serikali kushusha bei ya sukari nchini ambayo imepanda mpaka kufikia Sh 2000 kwa kilo moja kutoka katika bei ya kawaida iliyokuwapo ya Sh 1600.

“Watanzania agizo hilo la Serikali limetokana na maandamano ya leo waliposikia tuna andamana kupinga mfumuko wa bei pamoja na Dowans kutokulipwa kwa kodi za wananchi na wao wakajifanya kutoa agizo hilo, ”alisema Mnyika.

Wabunge wa Mwanza
Kwa upande wa wabunge hao wa Chadema mkoani Mwanza waliohudhuria mkutano huo walisema kuwa watahakikisha wanainua maisha ya wana-Mwanza kwa kusimamia rasirimali zilizopo mkoani hapa na kuifanya wilaya ya Bunda ambayo ndiyo ya kwanza kwa umasikini kuondoka kwenye nafasi hiyo .

Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje alisema kuwa ni aibu kwa wana-Mwanza kuchachuka na maisha wakati mkoa huu uonaongoza kwa kuwa na rasilimali nyingi ambazo kama zitasimamiwa ipasavyo zitawakomboa wananchi wake.

Maandamano ya Mwanza yamefanyika takribani miezi miwili tangu kutokee mauaji ya raia waliopigwa risasi na polisi mkoani Arusha, wakati walipokuwa wakizuia maandamano ya Chadema mkoani humo.

Katika tukio hilo la Januari 6, mwaka huu polisi wa Arusha walimwaga damu za watu kadhaa na wengine zaidi ya 30 walijeruhiwa miongoni mwao wakiwamo walioshiriki na wasioshiriki maandamano yaliyoandaliwa na Chadema.

Risasi za moto na mabomu ya machozi vilitumika katika jitihada za polisi kuzima maandamano hayo, wakitekeleza amri ya Mkuu wa Jeshi hilo, Ispekta Jenerali Said Mwema ambaye awali aliyapiga marufuku baada ya awali kuwa yameruhisiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Last Updated on Friday, 25 February 2011 08:49 Comments




0 #12 Kimweri ye Nyumbai 2011-02-25 09:48 Imefika mahali Watanzania lazima wajuwe haki zao za msingi kama wazawa na watu wanaostahili kula vizuri,kulala mahali pazuri,kupata afya na elimu bora na kuwa na uhuru na ardhi yao.Wakubwa wetu akiwemu Rais tuliyempa dhamana ya kutuongoza,wame kuwa watu wakujimegea mkate na kupaka siagi huku wakimezea na chai ya maziwa wakituacha Watanzania wengi tukinywa chai ya rangi isiyo na kitafunwa(instr umental)matokeo yake tunapata vidonda vya tumbo,ndiyo shida tunayoipata sasa ambapo wakubwa hawaioni wala kusikia kwasababu hawashindi njaa,hawakosi wala kulipia umeme,hawaendi sokoni kununua nyanya,watoto wao wanasoma kwa raha,lini watamkumbuka Mtanzania wa kawaida.

Yote haya ni matokeo ambayo Watz tumejitafutia katika uchaguzi mkuu uliopita.Viongozi wa vyama vya upinzani hasa CHADEMA wamezunguka kila mahali kuwaelimisha watu lakini wananchi wakaamua kuwarudisha bungeni wanafiki wa ccm,wakashangil ia JK kurudi Ikulu,haya leo mtasema nini?Mafuta ya kupikia,unga wa mahindi,sukari vyote bei juu na mishahara haipandi.Hainingii akilini kumuona Mtz wakawaida anaishabikia ccm tena amevaa t-shirt na kofia,hamna aibu?

Watanzania amkeni acheni kulala Tanzania bilA ccm na JK inawezekana.Raisi nchi inamshinda,alow aweka madarakani(masw ahiba)wamemgeuk a,hawatendi kazi walopewa.

Hongera sana Wanamwanza na CHADEMA,CCM NI DUDU LIUMALO BILA HURUMA LAZIMA TULITWANGE RUNGU LA KICHWA LISITUAMBUKIZE MAGONJWA.

Quote









0 #11 Junior 2011-02-25 09:40 wewe Sawia ni mpuuuuzi mkubwa. Hapa tunaongelea maandamano ya Mwanza na madai yake hatuongelei ni kabila gani limefanya nn. Hebu nipe jina moja la Mchaga ambaye ni Fisadi na useme ufisadi wake ni nn. Tatizo kwako ni wachaga kusoma au? nani alikataza kabila lako wasisome? Badala ya kuongea matatizo yetu na uozo wa serikali ww unaturudisha kwenye ukabila!.Mshenziiii sana we
Quote









+1 #10 MKWELI 2011-02-25 09:26 kwa hali hii, naishauri serikali ya CCM ichukue hatua za haraka. lakini watanzania nawaonya tusitegemee hali ikawa kama TUNISIA au EGYPT, zile nchi ni tofauti ni nchi za kiarabu. nakumbuka hata aliyekuwa rais wa Tunisia BIN ALLY aliambiwa na mfalme wa SAUDIA kuwa "ondoka haraka hapo TUNIS usije ukasababisha umwagaji damu kwa ndugu zetu wa kiarabu, hatutaki kuona kabisa waarabu wenzetu wakiuwana" ndio maana mapinduzi yalikuwa ya Amani. kadhalika na EGYPT JESHI LILIKATAA AMRI KUTOKA KWA HUSSEIN MUBARAKA KUDHIBITI MAANDAMANO NCHINI EGYPT.jeshi lilisema "hatutoweza kuingilia kati kwani tutasababisha umwagaji mkubwa wa damu dhidi ya waarabu wenzetu". KWA HIYO NCHI HIZI ZISICHUKULIWE KAMA MFANO HAWA NI WAARABU WANAPENDANA WENYEWE. LAKINI IKITOKEA HAPA KWETU HISTORIA ITAKUWA TOFAUTI KABISA. YATAJIRI YA RWANDA GENOSIDE 1994.HALI ITAKUWA TOFAUTI. HIVYO WADAU TUSITEGEE HILO TUJIPANAGENI MPAKA 2015 CCM TUTAIONDOA KWA AMANI NA SALAMA.
Quote









0 #9 Al-Dowans 2011-02-25 09:26 Jambo ambalo bado nazidi kulitafakuri lakini sioni mwelekeo wa kupata jibu ni; Inakuwaje Mmiliki wa Richmond, Mohamed Gire aletwe na Rostam Aziz (Kama alivyokiri Salva Rweyemamu kwamba alitambulishwa kwake na Rostam), pia Mmiliki wa Dowans, kampuni ambayo haikuwahi kuwa na uhusiano wa kibiashara na Richmond, aletwe tena na Rostam!
Wabongo hapa ni AKILI KUMKICHWA.

Quote









0 #8 mwanamaendeleo 2011-02-25 09:20 hiyo ni rasharasha mvua kamili yenye ngurumo na radi inakuja
PEOPLES POWER

Quote









0 #7 sawia 2011-02-25 09:19 Naomba tuelewe kuwa mafisadi tanzania siyo wako CCm tu wapo wengi ukiwa pamoja na mbowe, umasikini wa kitanzania mwingi umeletwa na ninyi mliosoma mwazo (wachaga na wahaya) wengi wenu mliliibia taifa sana. BISHENI! (sisemi wote kwani wapo watakatifu).
Wewe mbowe lini umelala na giza? Tukianza maandamano kama tunisia je wewe utakufa au sisi ndo tufe?
Watanzania: moja tutoe kikwete aondoke pili mbowe na mafisadi wengine. Msiandamane pupa tumieni vichwa kabla ya maandamano,ukio na kuna dalili ya kifo acha! angalieni kibaki na Laila wanakula kuku jamaa wameondoka. Akiingia mchaga ikulu mamayangu nchi itauzwa mara mbili. Karibuni kwa majibu wenye uchungu na niliyosema. na toeni facts. NB siyo wachaga wote wezi ila wengi wametufikisha hapa tulipo. vupumba! tembelea tovuti yangu: www.factscorruption.tz

Quote









0 #6 Geoffrey 2011-02-25 09:19 Safi sana Kamanda Sirro unastahili kuwa IGP unajua kazi siyo kama Mwema na Andengenye umeonyesha ukomavu wa hali ya juu hauchangani utendaji na siasa unastahili tuzo kumbe polisi ndiyo waanzishaji wa vurugu mbona maandamano na mkutano umeisha salama Mwema watanzania tu wastaarabu muda wa
Quote









+1 #5 Mchungu wa Bongo 2011-02-25 09:11 Na bado, hongereni Chadema, hongereni wana wa Mwanza, hongereni Watanzania wote wenye moyo wa kishujaa mlioi-support Chadema pale Mwanza, Mungu ibariki Chadema, Mungu wabariki Watanzania wanaonyonywa na serikali ya JK, na kama serikali hiihaitasoma alama za nyakati, basi utafika wakati nguvu ya umma itaamua maamuzi magumu kama Tunisia, Misri na Egypt, mkifikiri kwamba haya hayawezi kutokea Tanzania endeleeni na kuwanyonya Watanzania na kuwafanya [NENO BAYA], mtaisoma namba ya kiatu aliyoiva Hosni Mubaraki na aliyeivaa Gaddafi, asomaye na afahamu
Quote









+2 #4 JUMA ABDU 2011-02-25 08:59 Napongeza maandamano ya chadema huko MWANZA
Quote









+1 #3 wabogojo 2011-02-25 08:58 ee Mwenyezi Mungu wasaidie wananchi wa Tanzania.. nina swali rahisi sana kwa wananchi wenzangu kama tuunauwezo wa kukodisha hio mitambo ya dowans kwa miezi 4 kwanini tusinunue serikali na Tanesco wasinunue mitambo yao wenyewe? sababu kuu kama wakikodisha kwa miezi minne je mwaka mwingine ikitokea shida ya umeme tu[NENO BAYA]disha tena. na kama hatuna hela hautwezi nunua kwa installment kuliko kukodisha hii mitambo ya ROSTAM? hili swala linadhihirisha wazi kuwa ni mradi wa mtu wa ccm na huyu JK najua wazi kabisa..! anaenda sulhisha mambo ya nchi nyingine wakati nchini kwake kuna shida kubwa kuliko hizo nchii..! ee bwna Mungu wasaidie hawa CCM walipotufikisha inatosha..! si lengo letu wala furaha yetu kutokea mabo ya Libya, Tunisia na Libya hapa nchini ila inafikia sehemu tufanye kwa faida ya kizazi kinachokuja..! Ngeleja hana uwezo kuwa hata mkuu wa shule ya primary jamani..!
Quote









+4 #2 fredy chokela 2011-02-25 07:37 Mwenye macho haambiwi tazama, hivi nyie mliooona kuwa JK anauwezo wa kutuongoza na mkampa kura zenu na leo yanawatokea puani, najua walioandamana jana siyo wafuasi wa Chadema tu kwani nafsi zao zinawasuta baada ya kuona maisha yamekuwa magumu..Mie ningependa kuuliza swali, Je nyie mliowapigia kura hawa viongozi wa ccm huu mgao wa umeme nyie hammo?? Je hizi bei kubwa za vitu hizo kadi zenu za ccm huwa mkizionyesha kwa wauza bidhaa huwa mnapunguziwa bei ya bidhaa??
Watanzania nawaomba mbadilike kifikrakwani hawa viongozi wa Chadema hawawezi kusema kitu bila uhakika, huuu ni mwanzo tu baada ya uchaguzi kuisha je hiyo bajeti itakuwaje, ooohhh mungu wasaidie hawa ccm kwa hata chembe ya huruma hawana....

Quote









0 #1 Amanda 2011-02-24 22:07 Jamani naomba kujua hapa kwetu Tanzania utasikia barabara ya Kenyatta sijui Kwame nkuruma na majina kibao hivi na nchi nyingine kama Kenya nako kuna barabara kama ya Nyerere, Mkapa au Mwinyi?? Msaada tutani tafadhali
 
CHADEMA inatisha
• Wafanya maandamano makubwa ya kihistoria jijini Mwanza

na Sitta Tumma, Mwanza


amka2.gif
MAELFU ya wakazi wa jiji la Mwanza na viunga vyake, jana walilazimika kusimamisha shughuli zao na kujiunga katika maandamano makubwa na ya kihistoria, yaliyoongozwa na viongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA, huku mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, akitoa msimamo mkali kuwa chama chake sasa kimedhamiria kuwakomboa Watanzania kutoka katika hali ngumu ya maisha na mgawo wa umeme, ikiwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete haitachukua hatua za dharura kulinusuru taifa.
Maandamano hayo yaliyoongozwa na Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willbrod Slaa, yalianzia katika shule ya Nyakato Buzuruga na kupita barabara za Pamba, Kenyatta, na Makongoro zilizo katikati ya jiji hili na kuhitimishwa katika viwanja vya Furahisha kulikofanyika mkutano mkubwa wa hadhara.
Mbowe alipata wakati mgumu kutoa hotuba yake kutokana na maelfu ya watu kumkatisha mara kwa mara wakitaka Rais Jakaya Kikwete ajiuzulu pamoja na mawaziri wake wa Ulinzi, Dk. Hussein Mwinyi, na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kwa sababu ya kushindwa kusimamia majukumu yao vizuri.
Alisema uzembe na ufisadi ndio uliolifikisha taifa katika mgawo wa umeme na hali ngumu ya maisha kwamba hivi sasa Watanzania wameingizwa kwenye ufisadi mpya kutokana na serikali kuamua kutenga sh bilioni 400 kwa ajili ya kukodi mitambo ya kuzalishia umeme.
"Bilioni 400 zimepangwa na serikali ya Kikwete kwa ajili ya kukodi mitambo ya kuzalisha umeme na kila mwezi sh bilioni 23 zitalipwa...huu ni ufisadi mkubwa na mauaji kwa Watanzania," alisema Mbowe.
Akiwageukia polisi na maofisa wa usalama wa taifa walioamiminika uwanjani hapo, Mbowe aliwataka wakafikishe salamu kwa Rais Kikwete na CCM yake, kwamba CHADEMA sasa imedhamiria kulikomboa taifa kutoka kwenye makali ya maisha.
Alionya kuwa kama Rais Kikwete hatachukua hatua za dharura kulinusuru taifa basi yaliyotokea katika nchi za Misri, Tunisia na Libya kwa wananchi wenyewe kuamka na kuing'oa serikali madarakani, yanaweza pia kutokea Tanzania.
Wakati wakitoa msimamo huo, umati ulisikika ukisema "tufanye sasa hivi, tuko tayari kwenda Ikulu hata sasa hivi" lakini alisema wataendelea kuwasha moto wa mabadiliko nchi nzima na kwamba Rais Kikwete wataenda naye hatua kwa hatua kuangalia kama anachukua hatua za kunusuru nchi au la.
"Rais Kikwete tunakwenda naye kwa stepu, tutawasha moto wa maandamano nchi nzima, tukimaliza tutaangalia kama atakuwa amechukua hatua. Tunampa siku tisa," alisema Mbowe na kushangiliwa.
Dk. Slaa aliyekuwa wa kwanza kuhutubia katika mkutano huo, alisisitiza sana msimamo wa chama hicho kumpa Rais Kikwete siku tisa za kuhakikisha anaondoa kodi kwenye maeneo yote yaliyosababisha bei za vyakula na bidhaa mbalimbali kupanda na kufanya maisha ya wananchi kuwa magumu.
Katibu Mkuu huyo aliyekuwa pia mgombea urais kupitia uchaguzi mkuu uliopita hakusahau kuzungumza makovu ya uchaguzi huo ambapo alisisitiza kuwa kura zake zilichakachuliwa.
"Tunajua walichakachua kura zangu, ila hatupotezi muda kwa sasa, twende kwenye kazi hadi kieleweke," ambapo wananchi waliitikia tena wakisema "iwe kama Misri, Libya" na kusisitiza kuwa wako tayari kwa hilo muda wowote wakati huo.
Aidha, katika hotuba yake hiyo iliyotumia takriban dakika 45 hivi jukwaani, Dk. Slaa alisisitiza kuwa Rais Kikwete aliwajua vizuri sana wamiliki wa kampuni ya Dowans tangu awali.
Alisema kama Rais Kikwete, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Rostam wanataka Dowans ilipwe basi watoe fedha zao mifukoni na sio kutumia fedha za umma kujilipa wenyewe kupitia kampuni ya Dowans.
Aidha, Dk. Slaa aliwaambia wananchi waliofurika katika viwanja hivyo kuwa mmiliki wa Dowans ni Rostam Aziz kwani ndiye aliyehusika kubadili mkataba wa kampuni tata ya Richmond, kwa kuwatuma watu wawili Marekani kubadili mkataba huo ili uweze kumilikiwa na Dowans. Majina ya waliotajwa tunayahifadhi.
"Rostam Aziz alifanya mawasiliano yote na serikali katika hatua za kubadilisha mkataba wa Richmond kuwa wa Dowans, sasa Kikwete atakataaje na atakwepaje kwamba haijui Dowans na mmiliki wake? Ina maana Rostam alifanya mawasiliano haya na serikali ya nani kama si ya Kikwete?"
"Rostam alituma watu wawili ambao ni (….) kwenda Marekani kubadili mkataba wa Richmond kwenda Dowans...na ujanja huu umekuwa ukifanywa sana katika nchi na Kisiwa cha Costa Rica ambako huwa wanauza makampuni kwa mtu yeyote anayehitaji kumiliki kampuni! Tuliambiwa na kamati ya kina Mwakyembe kwamba kampuni ya Richmond inafanya kazi ya Stationary," alisema Dk. Slaa.
Wabunge wa CHADEMA nao waliwasha moto
Mbunge wa Jimbo la Ubunge, John Mnyika, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Nishati na Madini alisema kupanda kwa gharama za bidhaa kumesababishwa na tatizo la mgawo wa umeme unaoendelea ambao kwa namna moja ama nyingine unawanufaisha wakubwa wachache ndani ya serikali.

Aidha, Mnyika aliwakumbusha wananchi wakumbuke kauli za wakubwa akiwemo Rais Kikwete kuhusu ujio wa kampuni ya Dowans kwamba hawamfahamu mmiliki na hapahapo aliwataka viongozi hao sasa watoe maelezo baada ya kumwona.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee alisema kuwa wakati wa CCM kutawala umefika mwisho na kuwataka kuwapisha ili waweze kufanya kazi.
"Kama wananchi mtakubali mabadiliko yanawezekana …leo hii tuko Mwanza kwa ajili ya kuiondoa CCM madarakani pamoja na kudai kuwa kufanya kwetu maandamano kuna maana kuwa hatuna kazi," alisema Mdee.
Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje alisema kama mikoa ya Kanda ya Ziwa, ndiyo yenye rasilimali na utajili mkubwa kwa nini wananchi wake wapigike kimaisha, aliwataka wananchi hao kuanza mapambano ya kuhakikisha wanauaga umaskini.
"Kama dhahabu, almasi, samaki na malighafi nyingine zinapatikana katika ukanda wetu na kuchukuliwa na watu wachache …kwa nini tusibadilike na kuwa na nguvu moja ya kukataa, sasa tuanze kazi ya kujikomboa," alisema Wenje.
Mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia, aliwataka wananchi hao kutoa wasiwasi kuhusu hatma ya mgogoro wa ardhi ambao unaendelea na kuahidi kuwa Waziri wa Ardhi na Makazi, Anna Tibaijuka, atalitatua mwezi Mei mwaka huu.
Alisema ingawa CCM mkoa wa Mwanza umemfungulia mashtaka kuwa alishinda kwa wizi wa kura, nguvu ile ile iliyompa ushindi wa kishindo, ndiyo itakayoleta maendeleo ndani ya miaka mitano.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, alimtaka Rais Kikwete kuchukua tahadhari kutokana na mwenendo mzima wa mambo unavyoendeshwa ndani ya serikali yake.
Akisisitiza kauli hiyo, Lema alisema kama jiji la Mwanza limeweza kufanya mkutano na maandamano ya amani, kwa nini katika jiji la Arusha, hali ya hewa ilichafuliwa na viongozi wake?
Alisema, "JK akiona wenzake wananyolewa , yeye atie maji ..ndugu zangu, namaanisha kuwa JK anatakiwa kuwaangalia viongozi wenzake kule Misri, Tunisia na sasa Libya wanavyofanywa na nguvu ya umma."
Aidha, Lema aliendelea kusisitisa kauli yake aliyoitoa bungeni kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema uongo kuhusu tukio la Januari 5 mwaka huu kule Arusha na kwamba ukweli upo.
Huku akishangiliwa kwa kuongea kwa lugha ya kisanii, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Mr. Sugu, alisema kama jimboni kwake, Manzese, Nyamagana na kwingineko wanalia njaa, kwa nini CCM isiondoke?
 
Dowans yatikisa maandamano CHADEMA


*Slaa asema kuilipa ni kuiba fedha za walalahoi
*Mbowe ataka Rais Kikwete achue hatua, la sivyo...


Na Suleiman Abeid, Mwanza

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilifanya maandamano ya amani na mkutano wa
hadhara huku kikiwataka viongozi wa serikali kushughulikia wahusika katika suala la malipo ya Dowans na ukosefu wa umeme nchini.

Moja ya maazimio yaliyotolewa jana na viongozi hao na kuungwa mkono na maelfu ya wananchi waliokuwa wamehudhuria mkutano huo uliofanyika jana katika viwanja vya Furahisha mjini Mwanza ni kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwawajibisha wote walioisababishia hasara nchi kwa kuingia mikataba yenye utata katika masuala ya umeme.

Akihutubia katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe alisema umefika wakati hivi sasa kwa Rais Kikwete kuwawajibisha watendaji wake wote ambao wamebainika kuwa ndiyo chanzo cha matatizo ya umeme katika nchi hii.

Bw. Mbowe alisema baada ya CHADEMA kuanzisha maandamano ya nchi nzima, chama hicho kinataka mara baada ya kumalizika kwa mzunguko huo katika mikoa yote, Rais Kikwete naye awe amechukua hatua dhidi ya wahusika wote vinginevyo wananchi watahamasishwa ili wamchukulie hatua yeye.

Bw. Mbowe alimtaka Waziri wa Nishati na Madini, Bw. William Ngeleja kujiuzulu mara moja katika wadhifa wake kutokana na kushindwa kuisimamia vyema wizara hiyo na kwamba amekuwa akitoa maelezo tofauti kuhusiana na suala zima la umeme hapa nchini.

"Watanzania tunasema tumechoka sasa, tunahitaji ukombozi wa mara ya pili haraka, tatizo la umeme hapa nchini limegeuka kuwa ‘dili' la kuvuta fedha kwa viongozi wetu, hapana Watanzania tunasema tumechoka, hatuwezi kukubali kuendelea na mateso tunayoyapata hivi sasa ya mgao wa umeme.

"Rais Kikwete na mawaziri wake wote hawajawahi kuonja makali ya mgao wa umeme kwa vile wao wana majenereta majumbani kwao ambayo yanalipiwa mafuta kwa kodi za wananchi, sasa tunasema awashughulike wale wote waliohusika na matatizo haya, vinginevyo tutawaaambia wananchi na yeye wamwajibishe," alieleza.

Akizungumza suala la milipuko ya mabomu yaliyolipuka hivi karibuni kule Gongolamboto alisema tukio hilo siyo la bahati mbaya kama ilivyoelezwa na Rais Kikwete alipowatembelea wahanga wa mabomu hayo hivi karibuni na kwamba limesababishwa na uzembe.

Alisema jambo la ajabu, Rais Kikwete alidai kuwa tukio hilo limetokana na mapenzi ya Mwenyezi Mungu, lakini siku ya pili yake badala ya kushiriki mazishi ya watu waliopoteza maisha kutokana na mabomu hayo alipanda ndege na kwenda Mauritania kusuluhisha mgogoro wa Ivory Cost.

"Kwa kweli Rais wetu ametushangaza sana, anadai kuwa tukio la milipuko ya mabomu kule Gongolamboto ni tukio lilitokana na mapenzi ya Mwenyezi Mungu, na kwamba halitatokea tena, lakini cha kusikitisha, rais anaacha kuzika watu wake anapanda ndege kwenda Mauritania, inasikitisha," alieleza Bw. Mbowe.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Bw. Mbowe alisema iwapo serikali haitokubali kujirekebisha na kuwasikiliza wananchi kwa kutekeleza yale wanayoyasema, Rais Kikwete asishangae kuona yanatokea maandamano makubwa mengine ya nchi nzima ya kumuondoa katika madaraka kama ilivyotokea katika nchi za Tunisia na Misri.

Awali akizungumza katika mkutano huo katibu mkuu wa CHADEMA Taifa, Dkt. Willibrod Slaa aliwashukuru wakazi wa jiji la Mwanza kukipigua kura chama hicho na kuwachagua wabunge wanaotokana na CHADEMA pamoja na madiwani wengi na hivyo kuweza kuunda serikali.

Dkt. Slaa alikemea kitendo cha kunyanyaswa kwa machinga waliokuwa wakifanya biashara zao mitaani ambapo aliutaka uongozi wa Jiji la Mwanza kuwashirikisha machinga hao katika kupanga na kuona ni maeneo yapi yanayowastahili wao kuendeshea biashara zao.

Hatua hiyo ilitokana na kelele za wananchi waliokuwa wamehudhuria mkutano huo kumkataa kwa nguvu Meya wa Jiji la Mwanza, Bw. Josephat Kanyonyi Manyerere kwa madai aliwasaliti baada ya uchaguzi .

Kutokana na hali hiyo, Dkt. Slaa aliwaagiza madiwani wote katika halmashauri zote nchini zinazoongozwa na CHADEMA kuwa wahakikishe machinga hawanyanyaswi, na badala ya kufukuzana nao mitaani wakae pamoja na kupanga maeneo muafaka kwa ajili ya kuendeshea biashara zao.

"Ndugu zangu naomba muwe na subira, nimewasikia kilio chenu cha kumkataa meya wenu, na yeye nafikiri amesikia, lakini la muhimu ambalo napenda nilitolee agizo ni kwamba tangu sasa viongozi wa halmashauri acheni kuwasumbua ndugu zetu hawa wamachinga, walalahoi, hawa ndiyo wenye nchi.

"Ninasikitishwa sana ninaposikia viongozi wa serikali kuu wanapoingia mitaani kukimbizana na machinga, akiwemo Mkuu wa Mkoa ndugu yangu Bw. Abbas Kandoro, hii siyo kazi yako, wewe siyo mtawala, wewe ni ‘facilitator (mwezeshaji)' siyo mtawala, hatutaki mkuu wa mkoa aingilie mambo ya jiji," alisema.

Akizungumza suala la malipo ya Dowans alisema serikali haipaswi kulipa na kwamba kama ni lazima kulipwa, basi watakaopaswa kutoa fedha zao mfukoni ni Rais Kikwete na waziri wake Ngeleja.

Dkt. Slaa alisema tangu awali alikwisha sema suala la Dowans ni kiini macho, na mhusika mkuu ni mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz na kwamba hata huyo Brigedia aliyekuja nchini juzi, Brigedia Sulaiman Al- Adawi ni wa kuchongwa si muhusika mkuu.

Alisema Bw. Rostam anaelewa kila kitu, hivyo kulipa fedha hizo ni kuiba fedha za walalahoi wa Tanzania waziwazi na kwamba hata kamati ya Bw. Harrison Mwakyembe ilibaini kuwa kampuni ya Richmond ilikuwa kampuni ya kitapeli, hivyo hata Dowans aliyerithi naye ni tapeli.

"Sisi CHADEMA tunasema serikali ya CCM haipaswi kulipa fedha hizi kwa kampuni hii ya kitapeli, ushahidi wote unaonesha kuwa ni mchezo wa kuigiza lakini bado wanang'ang'ania kutaka kulipa, hata kamati ya bunge ilibaini hilo , tuelezwe iwapo akina Mwakyembe (Harrison) walisema uongo, basi tuwawajibishe wao," alieleza Dkt. Slaa.

Viongozi hao wa CHADEMA leo wanatarajiwa kufanya mikutano katika wilaya zote za mkoa wa Mwanza ambapo kesho watakuwa mkoani Mara kabla ya kuelekea mkoani Shinyanga Jumatatu ijayo.

Amani yatawala maandamano

Kabla ya mkutano huo chama hicho kilifanya maandamano makubwa ya amani nchini yaliyoanzia katika viwanja vya Shule ya Msingi Buzuruga nje kidogo ya Jiji la Mwanza na kuishia katika viwanja vya Furahisha katikati ya mji yaliongozwa na viongozi wakuu wa kitaifa wa CHADEMA wakiwemo Mwenyekiti, Bw. Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Willibrod Slaa na wabunge kadhaa wa chama hicho.

Wananchi wengi waliohudhuria maandamano hayo walionesha utulivu wa hali ya juu kwa kuandamana kwa amani huku wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa kwa kuzunguka mitaa mbalimbali kabla ya kuingia katika viwanja vya Furahisha.

Nyimbo nyingi zilikuwa zikipinga uamuzi wa serikali kutaka kuilipa kampuni ya Dowans, kupanda kwa gharama za umeme, kulaani mauaji ya wananchi mkoani Arusha na milipuko ya mabomu ya Gongolamboto jijini Dar es Salaam iliyotokea hivi karibuni.

Baadhi ya nyimbo hizo pia zilikuwa zikidai kuwa wananchi wamechoshwa na serikali ya CCM iliyopo madarakani ambayo walisema kila siku zinavyozidi kwenda mbele ndivyo maisha yanavyozidi kuwa magumu kwa wananchi wengi wenye vipato vya chini.

Mbali ya hali ya utulivu katika maandamano hayo pia wananchi wengi walifunga shughuli zao za biashara na kujipanga kando kando ya barabara kutoka eneo la Buzuruga hadi viwanja vya Furahisha hali iliyosababishwa kufungwa kwa muda kwa baadhi ya barabara zikiwemo za Nyerere na Pamba.

CHADEMA imeamua kuendesha maandamano ya amani kwa nchi nzima kupinga mambo manne makuu ambayo ni fujo zilizotokea mkoani Arusha na kusababisha vifo vya Watanzania wawili na raia moja wa Kenya ambapo serikali ya CCM imekuwa ikidai fujo hizo zilisababishwa na wana CHADEMA wenyewe madai ambayo viongozi wa CHADEMA wanayakanusha, wakisema zilisababishwa na polisi.

Pili kupinga kitendo cha serikali ya CCM cha kutaka kuilipa kampuni ya Dowans, ambapo CHADEMA inataka fedha hizo kama zipo zielekezwe katika huduma nyingine muhimu za kijamii ikiwemo elimu na afya.

Tatu, maandamano hayo yana lengo la kuwahamasisha wananchi kupinga kwa nguvu zote ongezeko la bei ya umeme nchini ambao umeongezwa kuanzia Januari Mosi mwaka huu kwa kiwango cha asilimia 18.5 hali ambayo CHADEMA wanadai ni kuwaongezea mzigo wa maisha magumu Watanzania, na kusababisha mfumuko wa bei kwa bidhaa zote muhimu.

Na mwisho maandamano hayo yatatumika kushinikiza kumtaka Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa nchini, Dkt. Hussein Mwinyi kujiuzulu katika wadhifa wake kutokana na tukio la milipuko ya mabomu huko Gongolamboto jijini Dar es Salaam, na kwamba ni tukio la pili kutokea nchini akiwa waziri wa wizara hiyo.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na Majira jana katika eneo la Buzuruga muda mfupi kabla ya kuanza kwa maandamano hayo, walisema pamoja na kwamba viongozi wa CCM wamekuwa wakidai chama hicho hakiwezi kuondolewa madarakani hivi sasa, lakini muda wao wa kuondoka umefika.

"Kwa hali hii kwa kweli siku za CCM kuendelea kubaki madarakani zinahesabika, wananchi tumechoshwa na hali ya ugumu wa maisha, na serikali haioneshi harakati zozote za kutaka kuwasaidia wananchi wake kuondokana na hali hiyo.

Mapema, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Bw. Erasto Tumbo aliwaeleza waandishi wa habari kuwa maandamano kama hayo yataendelea kufanyika leo (Ijumaa) katika wilaya zote za mkoa wa Mwanza, ambapo Februari 26, yatahamia Mara na wilaya zake zote kabla ya kuelekea mkoani Shinyanga Februari, 28 na Machi Mosi mwaka huu.

Bw. Tumbo alisema Februari 2, mwaka huu maandamano hayo yatafanyika mkoani Kagera na siku ya pili yake yatafanyika katika wilaya zote za mkoa huo ambapo itakuwa ndiyo mwisho wa maandamano hayo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

 
Dowans yaibua mapya TANESCO


Na Rabia Bakari

KAMPUNI ya Mawakili ya Rex iliyoiwakilisha TANESCO katika kesi dhidi ya Dowans imetajwa mbele ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kuwa
ilihusika katika kesi hiyo ikiwa na mgongano wa kimaslahi.

Hayo yalifahamika jana baada ya kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Bw. Januari Makamba ilipotembelea mitambo ya Dowans, na katika maelezo ya mmoja wa wanahisa na Mkurugenzi wa Fedha wa Dowans Tanzania Limited, Bw. Stanley Munai ilibainika kuwa kampuni ya REX ilikuwa inatoa msaada wa kisheria kwa pande mbili katika kesi hiyo.

Maelezo hayo yalijitokezo wakati Bw. Munai akijibu maswali kuhusu madeni yanayikali kampuni hiyo ambayo imekuwa gumzo la muda mrefu hapa nchini.

Bw. Munai alisema kuhusu madeni hawana cha kuficha, kwamba wanadaiwa dola milioni mbili na benki ya Barclays, na kabla ya deni hilo na benki hiyo, walikuwa wamechukua mkopo katika benki ya Stanbic wa dola milioni 20 ambako walihamishia deni hilo Barclays kutokana na makato ya Stanbic kuwa makubwa.

Alisema wakati wa kuchukua mkopo Stanbic, benki hiyo iliwaonesha orodha ya kampuni za mawakili na kuwataka kuchagua mojawapo kwa ajili ya kuwakagua na kuwathibitisha ili waweze kupata mkopo ambapo walichagua Kampuni ya Mawakili ya REX, ambayo iliwaandikia maoni 'mazuri' na kuwathitisha wapate mkopo huo.

Kauli hiyo ilisababisha baadhi ya wabunge wahoji, iweje mawakili hao wa REX wawathibitishe Dowans kupata mkopo, wakati huo huo ndio walikuwa wawakilishi wa wapinzani wao TANESCO katika kesi iliyokuwa ikisikilizwa ICC.

Akijibu hilo, Bw. Munai alidai kuwa hofu hiyo hata wao aliiona mapema na kwa ushauri waliwaandikia barua TANESCO kuwajulisha kuwa mawakili hao wana mgongano wa kimaslahi na kuwa haitakuwa vizuri kuwawakilisha TANESCO, lakini hawakuji na matokeo yake mawakili waliendelea kusimamia kesi hiyo, huku akidai kuwa hawakujua kwa nini TANESCO waliamua kukaa kimya.

Kauli hiyo iliwafanya wabunge wengi kutingisha kishwa na kumwambia mkurugenzi huyo kuwa wameshaelewa, na hilo si la kwake yeye.

Akiendelea kubanwa na maswali ya papo hapo kwa hapo ya wabunge hao, ambapo kwa kiasi kikubwa Bw. Makamba ndio alikuwa akiuliza maswali mfululizo, pia alitaka kufahamu sababu kubwa iliyofanya mmiliki wa Dowans, Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi kuja nchini na kutaka kuzungumza na TANESCO.

"Alikuja nchini (Al Adawi) baada ya kusikia malalamiko ya Watanzania kuwa fedha tunazodai ni nyingi, na lengo likiwa ni kuzungumza na TANESCO ili kukubaliana gharama za kupunguza na hatimaye kama inawezekana tuendelee kutoa huduma, lakini hata hivyo TNAESCO hawajajibu barua hiyo ya kutaka tuonane nao na wala hawataki kukaa pamoja nasi," aliongeza Bw. Munai.

Alisema kuwa Bw. Al Adawi alikuwa tayari kupata hasara na kusamehe mambo mengi, lakini TANESCO hawaoneshi ushirikiano katika hilo.

Bw. Mkamba alitaka kujua hasara gani ambayo Bw. Al Adawi yupo tayari
kuipata na kuwasaidia Watanzania, na Bw. Munai alijibu kuwa "Yeye
amewekeza mitambo yake ipo hapa, na inawashwa ili isioze, kuna umeme tunatumia, bima ya tahadhari inalipwa, tunalipa watu wanaokuja kufanya kazi, ni gharama kubwa tunatumia, lakini yupo tayari kupata hasara kwa hilo."

Baada ya wanakamati kuondoka waandishi walimganda Bw. Munai kutaka kujua mambo kadhaa ikiwemo uhalali wa deni na gharama halisi wanazodai kwa TANESCO, ambapo alijibu kuwa ni nyingi mno, kwani hata hizo bilioni 94 zinazosemwa ni nyuma kabla ya hukumu kutoka, ambapo kwa makubaliano TANESCO walitakiwa kuwalipa dola 11,800 kila siku na fedha hizo zilianza kuhesabika kuanzia Juni 14, mwaka jana hadi leo.

Katika hatua nyingine, Dowans imeitupia lawama TANESCO kuwa ndio chanzo cha matatizo baada ya kutotaka kujibu barua mbalimbali walizoandikiwa wala kutotaka kukaa mezani kwa ajili ya kushauriana kuwapa 'unafuu' Watanzania.

Awali, baada ya kamati hiyo kuingia katika eneo la mitambo ya Dowans, Mkurugenzi wa Uzalishaji wa TANESCO, Bw. Moses Mwandenga alianza kutoa maelezo ya mitambo hiyo jinsi inavyowashwa na kufanya kazi, ambapo alielezea uwezo wa kuzalisha umeme na jinsi unavyoingia katika gridi ya taifa.

Mtaalamu huyo alieleza kuwa tangu mkataba wao na TANESCO uvunjwe, ili
kudhibiti uharibifu wa vifaa mitambo hiyo huwashwa na kila baada ya wiki mbili ili kuhakikisha inafanya kazi lakini bila kuzalisha umeme.

Baadhi ya wanakamati walitaka kujua hali ya mitambo wakati inaingizwa nchini ambapo, Bw. Munai alijibu kuwa ilikuwa mipya, na kuonesha kuchukizwa na kauli za baadhi ya watu wanaodai kuwa mitambo hiyo ni chakavu.

Alisema mitambo yote iliingia nchini ikiwa mipya isipokuwa mmoja, uliokuwa umetumika kwa saa 5,000, muda ambao alidai ni mfupi kwa kifaa kipya.

Baada ya maswali ya kitaalamu ndipo, Bw. Makamba alimpotaka mkurugenzi huyo kueleza ni kwanini hawataki kuondoa mitambo yao ilihali haifanyi kazi yoyote na kung'ang'ania kubaki nchini.

"Hatujang'ang'ania, isipokuwa baada ya TANESCO kuvunja mtakaba, tulitaka kuondoa mitambo, wao wakatuzuia kuwa mpaka kesi iliyopo ICC itakapomalizika ndipo tunaweza kuondoka," alisema Bw. Munai.

Aliendelea kujitetea kuwa kesi hiyo imeisha muda si mrefu, lakini ni mapema mno kwao kueleza hatua za kuondoka kwa sasa.

Baada ya ziara, waandishi walimgeukia Bw. Makamba kutaka maoni yake, ambapo alikiri kuona matatizo mengi, na kudai kuwa hawezi kuongea hapo isipokuwa leo ambapo kamati itakutana na wadau wote wanaozalisha umeme.

"Nadhani ndugu waandishi na nyie mmejionea kila kitu, sasa mimi sina cha kusema kwa leo, isipokuwa kesho tutazungumza baada ya kukutana na wadu wote wakiwemo Songas, Dowans, TANESCO na wengineo," alijibu.




1 Maoni:

blank.gif

Anonymous said... ukweli utajulikana tuu. mambo yanaanza kidogo kidogo kufunguka. waandishi tunawaomba wasilalie upande mmoja endeleeni kutupa ukweli kadri unavyojitokeza. maana tumedanganywa sana mpaka kufika mahala wananchi kiuona Dowans kama vile adui mkubwa wa watanzania. kumbe kikulacho kinguoni mwako. huu ni wakati wa watanzania kuzipa akili zetu nafasi badala ya kukurupuka na kujaa jazba zenye maslahi ya kisiasa ya baadhi ya watu. Mh. Makamba endelea na shughuli za kamati yako, nadhani sasa tumeanza kuona ukweli wa jambo hili. unaelekea kuzuri. ukweli utajulikana tuu. kama kosa ni la Dowans,Tanesco au bunge lililopita?
February 24, 2011 10:36 PM
 
Ufisadi mpya wawashtua wabunge
• Wabaini ulaji kwenye mikataba ya nishati ya umeme

na Betty Kangonga


amka2.gif
KAMATI ya Nishati na Madini imedai kupatiwa mikataba yote iliyoingiwa na serikali na kampuni zinazozalisha nishati ya gesi baada ya kubaini kuwapo kwa mapungufu makubwa kwenye mkataba mmoja ambao umeelezwa kumpa nguvu muuzaji kuuza nishati hiyo kwa Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO) kwa bei ya dola za Kimarekani badala ya shilingi za Kitanzania.
Kwa hali hiyo, imeelezwa kuwa TANESCO imekuwa ikipata hasara na kushindwa kujiendesha; huuza umeme kwa bei ya shilingi za Kitanzania lakini huuziwa gharama kubwa ya dola za Kimarekani.
Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, ndiye aliyeonekana kuishawishi kamati hiyo kupitia mikataba yote iliyoingiwa na serikali kwa sababu ya kile alichokieleza kuwa "haiwezekani gesi iwe yetu halafu kampuni iliyopewa zabuni kuisafirisha kutoka Songosongo iuze gesi hiyo kwa TANESCO kwa bei ya dola za Kimarekani."
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba (CCM), kufanya ziara ya kutembelea mitambo mbalimbali ya kuzalisha umeme, Meneja Mkuu wa kitengo cha Theo Generation kinachosimamia uzalishaji wa umeme gesi, Gregory Chegele, alisema yote hayo yanatokana na mikataba iliyoingiwa na serikali.
Alisema Kampuni ya Pan Afrika ndiyo iliyopata zabuni ya kuuza gesi hivyo gharama za uendeshaji inategemea bei ya gesi ilivyo katika soko la dunia.
"Aliyepata hiyo tenda hana uwezo wa kuzalisha megawatts 120 bali umeme unaokwenda katika gridi ya taifa kutokana na gesi ni megawats 80 pekee," alisema.
Alisema kuna kipindi uzalishaji ulipungua baada ya kutokea tatizo katika kisima cha Songosongo hali iliyoathiri utendaji.
Chegele alisema kuwa pamoja na mabadiliko ya bei bado tatizo la utengenezaji wa vipuri na mafuta ya uendeshaji wa mitambo vinachangia katika kuathiri uzalishaji wa umeme huo.
"Unajua sisi tunaponunua gesi kutoka kwa Pan Afrika tunauziwa kwa bei ya dola tena inategemea bei ilivyo kwa wakati huo katika soko la dunia…lakini tunapozalisha umeme tunauza kwa shilingi," alisema.
Hatua hiyo iliwafanya baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo kuhoji maswali mbalimbali huku Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akisisitiza kuwa kamati hiyo inahitaji kupata taarifa zaidi pamoja na kukutana na wahusika hao.
Alisema wakati wa majadiliano hayo ni bora kamati ikajiridhisha kwa kupitia mkataba huo maana haiwezekani gesi iwe ya kwetu halafu kampuni hiyo iuze gesi hiyo kwa bei ya dola.
"Mwenyekiti naomba kama hiyo kesho tunakutana na kuzungumzia masuala haya ni bora tukakutana na wadau wote na pia tukaletewa mkataba huo kwa kuwa hauna siri ili tuuone ukoje," alisema.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati hiyo Makamba alisema kutokana na taarifa hiyo ni vyema kamati ikaangalia na kujadili kwa kina kuhusu jambo hilo maana hatua hiyo imeashiria kuna "katatizo" mahali.
Kauli ya Makamba kuliita suala hilo kuwa ni "katatizo" ilipingwa vikali na mjumbe Sendeka, ambaye alimjibu akisema, "Hapa sio katatizo mwenyekiti, hapa inaonekana wazi kuna tatizo kubwa katika mkataba huo, hivyo ni lazima kamati yetu ilijadili hili kesho."
Wakati huo huo kamati hiyo ilikagua mtambo wa kuzalisha umeme wa kampuni ya Dowans na kukutana na mkurugenzi wa kampuni hiyo, Stanley Munai ambapo alisema mitambo hiyo imekuwa ikiwashwa kwa muda wote lakini haipeleki umeme katika gridi ya taifa.
"Kila kitu kimeunganishwa; hakijazimwa kitu chochote lakini kila baada ya wiki mbili tunawasha mashine hizo ili zisiharibike," alisema.
Alisema ni neno baya kuita mitambo hiyo ni chakavu maana hakuna mashine iliyo mbovu kwani zote zina uwezo wa kufanyakazi kwa muda wa miaka 50.
"Mashine hizo zililetwa hapa zikiwa hazijatumika na hata ile kubwa inayozalisha megawats 40 ilifika hapa ikiwa katika namba sifuri, haijawahi kutumika mahali popote," alisema.
Makamba alihoji sababu za mitambo hiyo kuendelea kuwepo wakati imesimamisha uzalishaji kwa kipindi kirefu.
Akijibu hoja hiyo, Munai alisema walitegemea kuondoa mitambo hiyo mwaka 2008 lakini kutokana na kuwa na kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC Court) iliwaweka katika wakati mgumu kuondoa mitambo hiyo.
Alisema taratibu za uwekezaji wa kampuni hiyo uliipa kodi ya kawaida kama kampuni nyingine ndiyo maana Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) haikuendelea kudai fedha kwa Dowans.
"Taratibu za uwekezaji tunatakiwa kufanya kazi kwa miaka mitatu au minne bila kulipa kodi hivyo hatujavunja sheria ya aina yoyote katika suala hilo; tumekuwa tukitimiza wajibu wetu kulipa mapato kama wengine," alisema.
Alisema mmiliki wa mitambo hiyo Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi alifika nchini ili kusikiliza kilio cha Watanzania ndiyo maana akafikia hatua ya kuiandikia TANESCO barua ili kuweza kukaa katika meza ya majadiliano.
Alisema iwapo TANESCO watakataa kujibu barua hiyo basi kampuni hiyo itaacha suala hilo lifanyike mahakamani kama walivyoamua kusajili tozo ya hukumu hiyo.
"Unajua mmiliki hatataka wajadiliane kuhusu kutumika kwa umeme wa kipindi cha nyuma kama miezi 10 ambapo wananchi walitumia umeme uliozalishwa na dowans pasipo kulipwa," alisema.
Alisema walizalisha umeme na kudai kiasi cha dola milioni 24 ambazo serikali haijalipa hadi sasa.
Munai alisema benki pekee inayoidai kampuni ya Dowans ni ya Baclays ambayo inaidai kampuni hiyo kiasi cha dola milioni mbili.
"Tuliwahi kukopa huko nyuma benki ya Stanbic ambapo mawakili wa Rex Attorney ndiyo waliotusimamia na tukaweza kupata mkopo lakini kama unavyojua mfanyabiashara anaangalia riba tulipoona Barclays wana riba ya chini tukaamua kuchukua mkopo huko," alisema.
Alisema mmiliki huyo alifika nchini kutokana na yeye kuwa anamiliki hisa nyingi katika kampuni hiyo kuliko wengine.
Munai alisema ikiwa serikali itahitaji kuuziwa mitambo hiyo kampuni hiyo haitakuwa na pingamizi iwapo itakataa itauza mitambo hiyo kwa watu wengine wanaohitaji.
Alisema hadi sasa fedha inayohitajika kulipwa kwa kampuni hiyo si bilioni 94 kama wengine wanavyofikiri bali kiwango hicho kilianza kupanda tangu Juni 15 mwaka jana.
 
Makamba atoboa siri ya mgawo
• Dowans yawekewa ngumu TANESCO, LHRC

na Betty Kangonga na Bakari Kimwanga


amka2.gif
IMEBAINIKA kuwa makali ya mgawo wa umeme yamekuwa yakichangiwa na serikali kushindwa kutoa mafuta ya kuzalishia umeme katika mtambo wa IPTL.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini na Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba (CCM) alisema kuwa kukosekana kwa mafuta hayo kumesababisha mtambo huo kuzalisha chini ya kiwango.
Alisema serikali kupitia hazina haina budi kutoa fedha kwa ajili ya kuagiza mafuta ya kuzalishia umeme ili kuwezesha mtambo huo kuzalisha megawati 100 ili kupunguza tatizo la mgawo wa umeme.
Makamba alisema kupatikana mafuta kidogo kumesababisha IPTL kwa sasa kuzalisha kati ya megawati 10 mpaka 50 zinazopelekwa katika gridi ya taifa kwa siku.
"Kuna mafuta yapo eneo la Kurasini ambapo yanahitajika kubebwa na kusafirishwa hadi katika mitambo hiyo …bado Hazina inahitajika kuhakikisha inatoa fedha kwa ajili ya kupata mafuta ili mitambo hiyo iweze kuzalisha megawati 100," alisema.
Alisema kutokana na serikali kushindwa kutoa mafuta kwa kiwango halisi mitambo hiyo ya IPTL imeshindwa kuzalisha umeme ambao ungesaidia kupunguza tatizo lililopo sasa.
Makamba alisema kwa mwezi mitambo hiyo inatumia mita za ujazo elfu 15 ambapo hadi kufikia juzi ilizalisha megawati zipatazo 50.
Wakati huo huo, mwenyekiti huyo alisema walikutana na wadau mbalimbali wa masuala ya gesi ambapo pamoja na majadiliano bado kamati hiyo imeombwa kupatiwa taarifa za bei ya gesi kwa maandishi ili kuweza kulitazama suala hilo kwa upana zaidi.
Alisema ni kweli wadau hao walikiri kuuza gesi hiyo kwa dola za Marekani lakini kamati imehitaji kupatiwa taarifa hiyo kwa maandishi.
Makamba alisema walijadili pia tatizo lililojitokeza ambapo kuna mashaka na mtambo wa bomba la kusafisha na kusafirisha gesi inayodaiwa kuwa imefikia mwisho wa uwezo wake.
"Tumeliangalia pia tatizo lililojitokeza la kuwepo kwa matatizo katika mtambo wa bomba la gesi kutokana na kuongezeka kwa matumizi ambapo kwa hivi sasa kuna viwanda kama vitatu vikubwa vinavyotumia gesi kuzalisha umeme," alisema.
Alisema pia mitambo ya mabomba hayo ilijengwa miaka 15 iliyopita na mahitaji ya gesi yameongezeka hivyo wamejitahidi kuliangalia hilo na wadau wote na taarifa yote itatolewa wiki ijayo.
Wakati huo huo, siku moja baada ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, kutangaza kuwa iko tayari kusamehe deni la sh bilioni 94 kadhalika kukiwa na msukumo wa kulitaka Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kuingia mkataba nao ili kupunguza makali ya mgawo wa umeme, hatua hiyo imeonekana kutiliwa shaka.
Hivyo TANESCO imesema inahitaji kutafakari juu ya hatua hiyo ya Dowans kuwafutia deni kwani jambo hilo ni la kisheria na si la makubaliano ya kawaida.
Uamuzi wa Dowans kuifutia deni TANESCO, ulitangazwa juzi na Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Stanley Munai, ambaye alisema kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya kusikia kilio cha Watanzania, lakini TANESCO imeshindwa kuitikia wito huo wa kusamehewa.
Akizungumza na Tanzania Daima, kuhusu kauli hiyo ya Dowans, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Wiliam Mhando, alisema ni muhimu kwa sasa kuzingatia masuala ya kisheria kuliko kukurupuka na kuonekana wao ndio waliovunja sheria na kusababisha kuibuka kwa mjadala mpya.
"Hili suala linazungumzika lakini kinachosababisha haya ni kauli za kisiasa, jambo la kisheria huenda kisheria ni muhimu kwanza tukae na timu yetu ya wataalamu kuliko kukubali na kukurupuka, ni mchakato kufikia makubaliano nao na tunahitaji ufafanuzi wa kina," alisema Mhando.
Juzi, Munai alisema kuwa licha ya kutoa msamaha huo, TANESCO bado walishindwa kujibu kama imeukubali au la ili mazungumzo yaanze.
Akifafanua zaidi kuhusu ombi la Dowans kutaka kukutana na TANESCO, Mhando aliwataka Watanzania kuvuta subira ili kuona juhudi zinazofanywa na TANESCO katika kukabiliana na hali ya mgao wa umeme nchini na hata kuondokana nao kabisa.
Dowans ilishinda kesi dhidi ya TANESCO katika Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), na hivyo kuamriwa ilipwe shilingi bilioni 94, uamuzi ambao ulizusha malumbano makubwa nchini na kusababisha Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Nchini (LHRC)
kuwasilisha pingamizi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, kupinga usajili wa tuzo iliyotolewa na Mahakama ya ICC.

Hata hivyo, uamuzi wa Dowans kutaka kuifutia deni TANESCO haujaweza kubadilisha mawazo ya LHRC ambao wameapa kuendelea na msimamo wao mahakamani.
Tanzania Daima iliwasiliana na mkurugenzi mkuu wa kituo cha sheria na haki za binaadamu nchini (LHRC), Francis Kiwanga, kuhusu uamuzi wa kuendelea na kesi hiyo au la, alisema ni vizuri mahakama ikaheshimiwa kwani ndicho chombo muhimu katika kusimamia na kutafsiri sheria.
"Kimsingi hebu tuheshimu mahakama suala la kufuta kesi au vinginevyo mahakama ndiyo yenye uwezo wa kuamua lakini sisi bado tutaendelea na kesi yetu ya msingi," alisema Kiwanga.
Januari mwaka huu kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kwa kushirikiana na wanaharakati wa haki za kijinsia nchini waliwasilisha pingamizi Mahakama Kuu kupinga serikali kuilipa kampuni ya Dowans sh bil. 94.
Mahakama hiyo ya kimataifa ilikuwa imesikiliza malalamiko ya Dowans dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kuamua iilipe fidia kampuni hiyo baada ya kubaini kuwa ilivunja mkataba kinyume cha taratibu.
Hata hivyo Februari 22, mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania ilipokea na kusajili kesi nyingine ya kikatiba kupinga malipo ya kampuni ya umeme ya Dowans.
Kesi hiyo ya kikatiba ilifunguliwa mahakamani hapo na Watanzania saba wakiwemo wabunge watatu na kupewa namba tano ya mwaka 2011 chini ya Kampuni ya Mawakili ya Mpoki na Lukwaro.
Msingi wa kesi hiyo ni kwamba malipo ya Dowans ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 sehemu ya tatu kifungu cha 27 Ibara ya kwanza na ya pili. Hivyo katika kesi hiyo Watanzania hao wanaiomba Mahakama Kuu kutengua uamuzi wa malipo hayo kwa kuwa yanakwenda kinyume na katiba ya nchi.
Hali kadhalika, deni ambalo Dowans wanaidai TANESCO hivi sasa limeongezeka na kufikia sh bilioni 99 badala ya sh bilioni 94 za mwaka jana.
Kwa mujibu wa maelezo ya Dowans wenyewe, ongozeko hilo linatokana na kampuni ya Dowans kuitoza TANESCO kila siku Dola za Marekani 11,800 (ambazo ni sawa na sh milioni 15.3) kama gharama za uzalishaji umeme ambapo nyongeza hiyo ilianza kutozwa kila siku tangu Januari 15, mwaka 2010 hadi sasa.
 
Tanesco, Dowans bado hakieleweki Send to a friend Friday, 25 February 2011 21:42

mhando%20tanesco2.jpg
Mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando

Mpira watupwa kwa serikali yenyewe yaurudisha kwa Tanesco
Waandishi Wetu
HATUA ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kukataa kuzungumza chochote kuhusu kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans katika kikao chake na Kamati ya Nishati na Madini, pamoja na kukaa kimya bila kujibu hoja na barua za Dowans kutaka wakae mezani, imedaiwa ni kutokana na shirika hilo kutojua, wala kuhusika na ujio wa kampuni hiyo nchini.Habari za kiuchunguzi ambazo zilithibitishwa na baadhi ya watendaji ndani ya Tanesco zinaeleza kuwa shirika hilo lilifanya makusudi kutozungumzia Dowans kwa kuwa halijawahi kukutana wala kuingia mkataba wowote na kampuni hiyo ya uzalishaji umeme wa dharura, inayomilikiwa na mfanyabiashara wa Oman, Suleyman Al Adawi.

Kwa mujibu wa habari hizo, uongozi wa Tanesco chini ya Mkurugenzi wake, William Mhando uligoma kuzungumzia Dowans ukidai kuwa hauna mkataba wowote na kampuni hiyo.

Taarifa za msimamo huo wa Tanesco zimekuja siku moja tangu kampuni ya Dowans Tanzania, kupitia kwa mkurugenzi wake wa Fedha, Stanley Munai kuilaumu hadharani Tanesco, kwa kile alichodai kuwa ni uongozi wa shirika hilo kukataa kufanya mazungumzo ambayo yangeweza kuondoa sintofahamu iliyopo baina ya pande hizo.

Munai alisema Tanesco wanapaswa kulaumiwa kwa kuchangia tatizo la mgawo wa umeme nchini kwani Dowans mara kadhaa wametaka mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mivutano iliyopo ikiwa ni pamoja na deni la Sh94 bilioni ambalo linatokana na tuzo iliyopewa Dowans katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiashara, ICC.

Mmiliki wa Dowans, Al Adawi alikuwepo nchini siku chache zilizopita ambapo alikutana na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari nchini, na kueleza nia yake ya kukutana na Serikali ili kujadili mvutano kuhusu malipo ya tuzo ya Sh94 bilioni anazotakiwa kulipwa baada ya kushinda kesi ICC.

Hata hivyo, kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya kuaminika toka ndani ya Tanesco, msimamo wa menejimenti ya shirika hilo ni kutowasha mitambo ya Dowans na kwamba kwao ni bora kuongeza mafuta katika mitambo ya IPTL iliyopo Tegeta ili iongeze uzalishaji toka megawati 10 za sasa.

"Tanesco haipo tayari kuwasha mitambo ya Dowans wala kuzunguza nao kwani haijawahi kukutana, kuzungumza wala kuingia mkataba wowote na Dowans. Ni bora kuongeza mafuta mitambo ya IPTL izalishe umeme zaidi ya megawati 10 za sasa, " alisema mmoja wa watendaji wa Tanesco aliyeomba kuhifadhiwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa shirika hilo.

Suala la IPTL kufanya kazi chini ya uwezo wake wa kawaida lilithibitishwa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba alipozungumza na waandishi wa habari huku akiitaka Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kununua mafuta yatakayowezesha mitambo hiyo kuzalisha kiasi kikubwa zaidi cha umeme.

Kadhalika Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) katika taarifa iliyotolewa jana na mwenyekiti wake, Felix Mosha, wameitaka serikali kufanya mazungumzo na kampuni ya IPTL ili izalishe umeme kwa kiwango cha juu kama moja ya njia ya kusaidia pia kutatua tatizo lililopo.

Habari zinasema Tanesco inadai kuwa mitambo hiyo ilifikishwa ilipo sasa na serikali ambayo iliielekeza tu kuanza kuitumia hivyo kwa hali ya sasa anayepaswa kuzungumza na Dowans ni serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini.

"Msimamo wa Tanesco ni kuwa serikali au Wizara ya Nishati na Madini ndiyo izungumze na Dowans kwa kuwa ndiyo walioileta mitambo Ubungo,Tanesco haihusiki, vinginevyo suala hilo lirejeshwe Bungeni likajadiliwe na kutolewa uamuzi," kinaeleza chanzo chetu ndani ya Tanesco.

Kilisema kwa Tanesco, Dowans ni kama mwanamke aliyefumaniwa, mumewe akamtembeza mitaani utupu na kumuacha hivyo hawezi kumrudia au mtu wa jamii husika kumuoa tena.

"Kuna kabila moja kanda ya ziwa mwanaume akimfumania mkewe, humtembeza mitaani akiwa utupu na kumuacha hivyo hawezi kumrudia, ndivyo ilivyo kwa Tanesco, Dowans ni kama mwanamke wa aina hiyo utamuoaje?, serikali yenyewe ndiyo inayoweza kuamua siyo Tanesco," alisema.

Aliongeza, "Serikali ndiyo izungumze na Dowans na kuamua kwani ndiyo iliyoingia mkataba na Dowans na kuileta nchini siyo Tanesco."

Mwananchi ilimtafuta mkurugenzi wa Tanesco William Mhando ili atoe ufafanuzi wa taarifa hizo lakini alipopatikana alisema," Ahh Mwananchi, unaweza kunipa muda nakula kwanza."

Alipoulizwa baada ya muda gani atakuwa tayari alisema, "Nipe nusu saa hivi."

Maelezo ya Tanesco
Hata hivyo Mhando alipopigiwa simu mara kadhaa iliita bila kupokelewa ambapo baadaye Meneja Mahusiano wa shirika hilo Badra Masoud alilipigia simu gazeti hili ili kujua shida yake, lakini naye baada ya kuulizwa kuhusu taarifa hizo alionyesha msimamo huo.

"Kuhusu Dowans kwa sasa hatuzungumzi chochote, tutakapokuwa tayari tutazungumza kwani hakuna cha kuficha," alisema Badra na kuongeza:

"Hawa watu (Dowans) bado tuna kesi nao, ninyi mnataka tuzungumze nao nini?, subirini tu tutakapomalizana nao mahakamani tunatunguza na kila kitu kitawekwa wazi".

Hata hivyo, habari zaidi zinasema kuwa menejimenti ya Tanesco imeshindwa kuweka wazi ukweli huo mbele ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Januari Makamba mbunge wa Bumbuli kwa kuwa kila inapotaka kufanya hivyo anakuwepo Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja hivyo kukosa uhuru wa kweli kuzungumza.

Jumatano wiki hii Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ikiongozwa na Makamba ilikutana kwa zaidi ya saa tano na uongozi wa Tanesco huku kukiripotiwa kuwapo kwa mvutano mkubwa baina ya pande hizo ambapo Tanesco walidaiwa kukataa kujadili suala la Dowans.

Tanesco ilidaiwa kukataa kuzungumzia suala la Dowans nje ya Mahakama, pia suala la kuwashwa kwa mitambo ya kampuni hiyo ili itoe megawati 100 za umeme kwa lengo la kupunguza makali ya mgao wa nishati hiyo unaondelea sasa.

Hata hivyo, akizungumzia hitimisho la kikao baina yao na Tanesco Makamba alisema suala la kuamua kuwasha mitambo au la, ni la shirika hilo na wao ni washauri tu wa namna ya kuondoa mgao wa umeme nchini.

Alisema wameliagiza shirika hilo kuhakikisha hakuna utata wowote wa kisheria iwapo wataamua kuingia mkataba na kampuni hiyo na kushauri uwe wa muda mfupi usiozidi miezi minne.

Juzi kamati hiyo ya makamba ilitembelea mitambo ya kuzalisha umeme jijini Dar es Salaam ikiwemo wa Dowans, Songas, IPTL na mtambo wa Tanesco wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Ubungo.

Hata hivyo, habari za uhakika zinasema kuwa serikali ipo katika harakati za kumaliza utata baina Tanesco na Dowans ambapo juzi iliwakutanisha Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhando, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, Gavana wa Benki Kuu, Beno Ndullu na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo.

Kwa mujibu wa habari hizo watendaji hao walikutana usiku katika ofisi za Wizara ya Fedha ambapo uchunguzi unaonyesha kuwa kikao chao kilianza majira ya saa moja usiku.

Badra mbali ya kukiri kuwepo kwa kikao hicho, alisema ni mapema mno kueleza kilichojadiliwa akidai kilikuwa kikao cha kawaida, lakini akasema kwamba wakati ukifika yatokanayo na kikao hicho yatatolewa kwa umma.

"Kikao cha jana (juzi) ni cha kawaida na si mara ya kwanza kufanyika, vikao kama hivyo hufanyika mara kwa mara na hujadili mambo ya kawaida ya kiutendaji, kwa sasa yaliyojadiliwa siwezi kuyaweka wazi ila wakati ukifika tutawataarifu kwani hakuna cha kuficha,"alisema Masoud.

Kauli ya Ngeleja
Jana gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza kwa simu na Waziri Ngeleja ambaye alisema "hata ukinibana vipi mimi siwezi kuzungumzia masuala haya, utanichinja tu rafiki yangu".

Ngeleja alisema Tanesco wanapaswa kutoa ufafanuzi wa masuala yote kuhusu umeme kwa sababu wana bodi na menejimenti inayojitegemea.

Kuhusu Dowans Ngeleja alisema pia yeye hawezi kulizungumzia suala hilo kutokana na kesi iliyopo mahakamani. "Tanesco wana uamuzi, wakitaka kuingia mkataba mfupi au wa aina yoyote ni uamuzi wao maana vyombo vyote vya uamuzi vipo," alisema Waziri huyo na kuongeza:

"Nadhani watazungumza tu kama walivyoahidi pengine kwa sasa hawajajipanga na kama unavyojua pressure kutoka kwenye public (msukumo wa umma) ni mkubwa sana kutokana na matatizo haya ya Nishati ya umeme".

Akizungumzia suala la kuwa kikwazo kwa Tanesco pale walipokutana na kamati ya bunge ya Nishati na Madini, Ngeleja alisema kwa mujibu wa Kanuni za bunge toleo la mwaka 2007 kila waziri wa kisekta ni mjumbe katika kamati husika.

"Mimi sikuvamia kamati kama inavyodaiwa, wala sikwenda wa lengo lolote baya bali mimi ni mjumbe wa kamati ile kama kanuni zetu za bunge zinavyosomeka, tena bora umeniuliza hili maana wapo watu wanaweza kudhani mimi ni mvamizi wa vikao vya kamati,"alifafanua.

Waziri huyo akizungumzia suala la IPTL alisema yeye hawezi kufahamu sababu za kampuni hiyo kutozalisha umeme kwa kiwango cha juu cha uwezo wake, lakini akabainisha kuwa inawezekana ni kutokana na mahitaji waliyopewa na Tanesco.

"Mimi niko ofisini ndugu yangu, mambo mengine siwezi kuyaelewa maana inawezekana mahitaji ya Tanesco kutoka IPTL ni kiasi hicho kinachozalishwa ama pengine kuna hitilafu kwenye mitambo huwezi jua,"alisema Ngeleja huku akilishauri gazeti hili kuwasiliana na mfilisi wa IPTL aliyemtaja kwa jina moja la Rugonzibwa ili kupata ufafanuzi wa kina.

CTI nao waitaka Dowans
Naye Mwandishi Leon Bahati, anaripoti kuwa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) limetoa msimamo wake likisema kwamba suluhisho la haraka la kuokoa uchumi wa nchi usiendelee kuteketea ni kuruhusu mitambo ya kampuni ya Dowans iwashwe na kupunguza tatizo la uhaba wa umeme unaolikumba Taifa kwa sasa.

CTI imeitaka serikali pia kufanya mazungumzo na kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ili izalishe umeme kwa kiwango cha juu kama moja ya njia ya kusaidia pia kutatua tatizo lililopo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa CTI, Felix Mosha katika taarifa yake iliyotoa msimamo wa shirikisho hilo baada ya kutafakari kwa kina tatizo la umeme nchini.

"Tumetafakari kwa kina na kutambua kuwa pamoja na suala la Dowans kuingiliana na misimamo ya kisiasa, njia pekee na ya busara inayofaa kwa sasa kutatua tatizo hili la umeme ni kuruhusiwa kwa mitambo ya Dowans kufanya kazi," alisema Mosha kupitia taarifa hiyo aliyoitoa jana.

Alisema watumiaji wakubwa wa umeme kupitia CTI wapo tayari kufanya mazungumzo na Tanesco ili kuangalia namna watakavyoshirikiana kukabiliana na gharama za wazalishaji wa nishati hiyo muhimu kwa uchumi.

Mosha alielezea kilio cha wenye viwanda nchini ambacho kiliwasilishwa kwa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kwamba tatizo la umeme nchini limewasababishia hasara kubwa ambayo inatishia kusimamisha uzalishaji.

"Viongozi pamoja na baadhi ya wanachama wa CTI Februari 21, mwaka huu walikutana na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kuwaelezea kwa kina jinsi wanavyopata hasara na kutishia kuviua," alisema Mosha.

Kwa sababu hiyo akasema ni jambo la busara kutumia mitambo ya Dowans na IPTL kwa kuwa tayari ipo nchini na ndio suluhisho la haraka linaloweza kuchukuliwa kwa sasasa.

Mgawo wa Umeme kuendelea
Wakati hayo yakijiri, imebainishwa kuwa mgao wa umeme utaendelea kuwa tishio huku ikielezwa kuwa mitambo ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) haina mafuta ya kutosha kuzalisha kiwango cha umeme kinachotakiwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Makamba iliwaambia waandishi wa habari jana kuwa IPTL inashindwa kuzalisha umeme kwa kiwango kikubwa kinachotakiwa kutokana na kukosa mafuta ya kutosha.

Kutokana na hali hiyo, Makamba aliitaka Wizara ya Fedha (Hazina) kutoa fedha za kutosha kwa Kampuni hiyo ili iweze kununua mafuta ya kutosha kwa ajili ya kuendeshea mitambo hiyo ambayo ina uwezo wa kuzalisha megawati 100.

"Kwa sasa IPTL inazalisha megawati 10 mpaka 50 tu, jambo ambalo halitoshelezi kulingana na uwezo wa kuzalisha umeme katika mitambo hiyo," alisema Makamba.

Alisema kutokana na hali hiyo Hazina inatakiwa kutoa fedha ya kutosha ili uzalishaji huo ufikie angalau megawati 80 na kwamba kama Hazina hawatafanya hivyo machungu ya mgawo wa umeme yataendelea.

Makamba alifafanua hayo muda mfupi baada ya kutoka kuzungumza na wadau mbalimbali wa umeme katika kikao kilichofanyika kwenye ofisi ndogo za bunge.

Makamba pia aliiagiza Shirika la Petroli nchini (TPDC) liipatie Kamati yake bei halisi ya gesi ilivyo nchini kutokana na bei ya nishati hiyo kupanda mara kwa mara.

"Bei ya gesi imekuwa ikipanda mara kwa mara, hivyo nimeiagiza TPDC kutupa maelezo kwa maandishi yanayoeleweka kuhusu bei halisi ya gesi," alisema Makamba.

Alisema kuwa mitambo ya kusafirishia gesi iliyopo nchini imezidiwa uwezo kutokana na kuongezeka kwa viwanda na mashirika mbalimbali ambayo inatumia nishati hiyo, hivyo aliishauri serikali waongeze uwezo wa mitambo hiyo.

"Kwa sasa gesi inayotakiwa nchini ni mita za ujazo 15,000 ambazo ni sawa na megawati 10 kwa mwezi jambo ambalo hatuwezi kulimudu, serikali itoe fedha kwa ajili ya kubadilisha mitambo hii," alisema Makamba.

Kamati hiyo ambayo pia ilipatiwa mikataba ya gesi inatarajiwa kukutana tena Jumatatu ijayo kwa ajili ya kufanya majumuisho.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Last Updated on Saturday, 26 February 2011 08:56 Comments




0 #4 comrade 2011-02-26 08:43 tanesco,wizara, kamati nyinyi wote ni wamoja na kazi yenu kuu ni kuhakikisha unapatiikana umeme wa uhakika embu tafuteni njia mbadala za kuwapatia watanzania umeme wa uhakika sio kutupiana mpira..
Quote









0 #3 Kizingo 2011-02-26 08:21 Kutokana na habari hii kuonyesha maelezo wanayotoa watendaji wa serikali, Tanesco na kamati ya nishati na madini, kuna JAMBO LA SIRI linafichwa! Bado sijapata sababu za msingi wananchi kuendelea kukosa umeme wakati kuna mitambo ya IPTL ambayo kwa sasa inazalisha megawati 10 lakini uwezo wake ni kuzalisha megawati 100! Sababu inayotolewa ni ukosefu wa mafuta! Wakati huohuo waziri husika anapoulizwa kuhusu jambo hilo anajibu, "Mimi niko ofisini ndugu yangu, mambo mengine siwezi kuyaelewa maana inawezekana mahitaji ya Tanesco kutoka IPTL ni kiasi hicho kinachozalishwa ama pengine kuna hitilafu kwenye mitambo huwezi jua,"alisema Ngeleja huku akilishauri gazeti kuwasiliana na mfilisi wa IPTL aliyemtaja kwa jina moja la Rugonzibwa ili kupata ufafanuzi wa kina! Wakati huohuo mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini anajua sababu zilizopelekea IPTL kuzalisha umeme kidogo lakini bado siasa zinaendelea kutawala. Jamani , sisi wananchi tumeathirika na tunaendelea kuathirika na mgao wa umeme.Kwahakika chuki inayoendelea kujengeka ndani ya jamii ni kubwa ambayo madhala yake tutayashuhudia soon.
Quote









0 #2 kidaruini 2011-02-26 08:05 tanesco wanasema hawaifahamu dowans. wanasema serikali ndiyo inayoifahamu. waziri wa nishati na madini mh Ngeleja anasema hawezi kuzungumza mambo yanayuhusu dowans. anayeweza kuzungumza ni tanesco.Jamani mbona mnatuchanganya? Hivi hiyo mitambo serikali haiwezi kununua ya kwake mipya? au wanangoja wawekezaji waliowekeza mabilioni ya fedha katika miradi mingi inayotumia umeme wafilisike na huku serikai imeshachukua kodi zao? ni kwa nini msisimamishe shughuli zote mkaona kwanza hili la umeme? hamjui viwanda vidogo tulivyo navyo vikiacha kuzalisha hamtapata pesa za kuwasomesha watoto wenu nje ya nchi na pesa za kufanya safari kila wiki kwenda nje ya nchi kwenda kuomba pesa za neti za mbu?
Quote









0 #1 Emily Kashingo 2011-02-26 07:26 NGELEJA WIZARA IMEMSHINDA AACHIE NGAZI ASISUBIRI KUTOLEWA NA WANANCHI KWANI HATUMTAKI, LAKINI MKURUGENZI WA TANESCO MHANDO NAYE AACHIE NGAZI,KAMA HAWAWEZI HATA KUTOA UFAFANUZI HAWA SIO VIONGOZI NA HATA KAMA NI VIONGOZI NI MAMBUMBUMBU WA KUSOMA ISHARA NA NYAKATI, WANANCHI WAMECHIKA HAWATAKI SIASA WANATAKA UTEKELEZAJI
Quote
 
Tanesco, Dowans bado hakieleweki Send to a friend Friday, 25 February 2011 21:42

mhando%20tanesco2.jpg
Mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando

Mpira watupwa kwa serikali yenyewe yaurudisha kwa Tanesco
Waandishi Wetu
HATUA ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kukataa kuzungumza chochote kuhusu kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans katika kikao chake na Kamati ya Nishati na Madini, pamoja na kukaa kimya bila kujibu hoja na barua za Dowans kutaka wakae mezani, imedaiwa ni kutokana na shirika hilo kutojua, wala kuhusika na ujio wa kampuni hiyo nchini.Habari za kiuchunguzi ambazo zilithibitishwa na baadhi ya watendaji ndani ya Tanesco zinaeleza kuwa shirika hilo lilifanya makusudi kutozungumzia Dowans kwa kuwa halijawahi kukutana wala kuingia mkataba wowote na kampuni hiyo ya uzalishaji umeme wa dharura, inayomilikiwa na mfanyabiashara wa Oman, Suleyman Al Adawi.

Kwa mujibu wa habari hizo, uongozi wa Tanesco chini ya Mkurugenzi wake, William Mhando uligoma kuzungumzia Dowans ukidai kuwa hauna mkataba wowote na kampuni hiyo.

Taarifa za msimamo huo wa Tanesco zimekuja siku moja tangu kampuni ya Dowans Tanzania, kupitia kwa mkurugenzi wake wa Fedha, Stanley Munai kuilaumu hadharani Tanesco, kwa kile alichodai kuwa ni uongozi wa shirika hilo kukataa kufanya mazungumzo ambayo yangeweza kuondoa sintofahamu iliyopo baina ya pande hizo.

Munai alisema Tanesco wanapaswa kulaumiwa kwa kuchangia tatizo la mgawo wa umeme nchini kwani Dowans mara kadhaa wametaka mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mivutano iliyopo ikiwa ni pamoja na deni la Sh94 bilioni ambalo linatokana na tuzo iliyopewa Dowans katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiashara, ICC.

Mmiliki wa Dowans, Al Adawi alikuwepo nchini siku chache zilizopita ambapo alikutana na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari nchini, na kueleza nia yake ya kukutana na Serikali ili kujadili mvutano kuhusu malipo ya tuzo ya Sh94 bilioni anazotakiwa kulipwa baada ya kushinda kesi ICC.

Hata hivyo, kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya kuaminika toka ndani ya Tanesco, msimamo wa menejimenti ya shirika hilo ni kutowasha mitambo ya Dowans na kwamba kwao ni bora kuongeza mafuta katika mitambo ya IPTL iliyopo Tegeta ili iongeze uzalishaji toka megawati 10 za sasa.

"Tanesco haipo tayari kuwasha mitambo ya Dowans wala kuzunguza nao kwani haijawahi kukutana, kuzungumza wala kuingia mkataba wowote na Dowans. Ni bora kuongeza mafuta mitambo ya IPTL izalishe umeme zaidi ya megawati 10 za sasa, " alisema mmoja wa watendaji wa Tanesco aliyeomba kuhifadhiwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa shirika hilo.

Suala la IPTL kufanya kazi chini ya uwezo wake wa kawaida lilithibitishwa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba alipozungumza na waandishi wa habari huku akiitaka Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kununua mafuta yatakayowezesha mitambo hiyo kuzalisha kiasi kikubwa zaidi cha umeme.

Kadhalika Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) katika taarifa iliyotolewa jana na mwenyekiti wake, Felix Mosha, wameitaka serikali kufanya mazungumzo na kampuni ya IPTL ili izalishe umeme kwa kiwango cha juu kama moja ya njia ya kusaidia pia kutatua tatizo lililopo.

Habari zinasema Tanesco inadai kuwa mitambo hiyo ilifikishwa ilipo sasa na serikali ambayo iliielekeza tu kuanza kuitumia hivyo kwa hali ya sasa anayepaswa kuzungumza na Dowans ni serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini.

"Msimamo wa Tanesco ni kuwa serikali au Wizara ya Nishati na Madini ndiyo izungumze na Dowans kwa kuwa ndiyo walioileta mitambo Ubungo,Tanesco haihusiki, vinginevyo suala hilo lirejeshwe Bungeni likajadiliwe na kutolewa uamuzi," kinaeleza chanzo chetu ndani ya Tanesco.

Kilisema kwa Tanesco, Dowans ni kama mwanamke aliyefumaniwa, mumewe akamtembeza mitaani utupu na kumuacha hivyo hawezi kumrudia au mtu wa jamii husika kumuoa tena.

"Kuna kabila moja kanda ya ziwa mwanaume akimfumania mkewe, humtembeza mitaani akiwa utupu na kumuacha hivyo hawezi kumrudia, ndivyo ilivyo kwa Tanesco, Dowans ni kama mwanamke wa aina hiyo utamuoaje?, serikali yenyewe ndiyo inayoweza kuamua siyo Tanesco," alisema.

Aliongeza, "Serikali ndiyo izungumze na Dowans na kuamua kwani ndiyo iliyoingia mkataba na Dowans na kuileta nchini siyo Tanesco."

Mwananchi ilimtafuta mkurugenzi wa Tanesco William Mhando ili atoe ufafanuzi wa taarifa hizo lakini alipopatikana alisema," Ahh Mwananchi, unaweza kunipa muda nakula kwanza."

Alipoulizwa baada ya muda gani atakuwa tayari alisema, "Nipe nusu saa hivi."

Maelezo ya Tanesco
Hata hivyo Mhando alipopigiwa simu mara kadhaa iliita bila kupokelewa ambapo baadaye Meneja Mahusiano wa shirika hilo Badra Masoud alilipigia simu gazeti hili ili kujua shida yake, lakini naye baada ya kuulizwa kuhusu taarifa hizo alionyesha msimamo huo.

"Kuhusu Dowans kwa sasa hatuzungumzi chochote, tutakapokuwa tayari tutazungumza kwani hakuna cha kuficha," alisema Badra na kuongeza:

"Hawa watu (Dowans) bado tuna kesi nao, ninyi mnataka tuzungumze nao nini?, subirini tu tutakapomalizana nao mahakamani tunatunguza na kila kitu kitawekwa wazi".

Hata hivyo, habari zaidi zinasema kuwa menejimenti ya Tanesco imeshindwa kuweka wazi ukweli huo mbele ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Januari Makamba mbunge wa Bumbuli kwa kuwa kila inapotaka kufanya hivyo anakuwepo Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja hivyo kukosa uhuru wa kweli kuzungumza.

Jumatano wiki hii Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ikiongozwa na Makamba ilikutana kwa zaidi ya saa tano na uongozi wa Tanesco huku kukiripotiwa kuwapo kwa mvutano mkubwa baina ya pande hizo ambapo Tanesco walidaiwa kukataa kujadili suala la Dowans.

Tanesco ilidaiwa kukataa kuzungumzia suala la Dowans nje ya Mahakama, pia suala la kuwashwa kwa mitambo ya kampuni hiyo ili itoe megawati 100 za umeme kwa lengo la kupunguza makali ya mgao wa nishati hiyo unaondelea sasa.

Hata hivyo, akizungumzia hitimisho la kikao baina yao na Tanesco Makamba alisema suala la kuamua kuwasha mitambo au la, ni la shirika hilo na wao ni washauri tu wa namna ya kuondoa mgao wa umeme nchini.

Alisema wameliagiza shirika hilo kuhakikisha hakuna utata wowote wa kisheria iwapo wataamua kuingia mkataba na kampuni hiyo na kushauri uwe wa muda mfupi usiozidi miezi minne.

Juzi kamati hiyo ya makamba ilitembelea mitambo ya kuzalisha umeme jijini Dar es Salaam ikiwemo wa Dowans, Songas, IPTL na mtambo wa Tanesco wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Ubungo.

Hata hivyo, habari za uhakika zinasema kuwa serikali ipo katika harakati za kumaliza utata baina Tanesco na Dowans ambapo juzi iliwakutanisha Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhando, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, Gavana wa Benki Kuu, Beno Ndullu na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo.

Kwa mujibu wa habari hizo watendaji hao walikutana usiku katika ofisi za Wizara ya Fedha ambapo uchunguzi unaonyesha kuwa kikao chao kilianza majira ya saa moja usiku.

Badra mbali ya kukiri kuwepo kwa kikao hicho, alisema ni mapema mno kueleza kilichojadiliwa akidai kilikuwa kikao cha kawaida, lakini akasema kwamba wakati ukifika yatokanayo na kikao hicho yatatolewa kwa umma.

"Kikao cha jana (juzi) ni cha kawaida na si mara ya kwanza kufanyika, vikao kama hivyo hufanyika mara kwa mara na hujadili mambo ya kawaida ya kiutendaji, kwa sasa yaliyojadiliwa siwezi kuyaweka wazi ila wakati ukifika tutawataarifu kwani hakuna cha kuficha,"alisema Masoud.

Kauli ya Ngeleja
Jana gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza kwa simu na Waziri Ngeleja ambaye alisema "hata ukinibana vipi mimi siwezi kuzungumzia masuala haya, utanichinja tu rafiki yangu".

Ngeleja alisema Tanesco wanapaswa kutoa ufafanuzi wa masuala yote kuhusu umeme kwa sababu wana bodi na menejimenti inayojitegemea.

Kuhusu Dowans Ngeleja alisema pia yeye hawezi kulizungumzia suala hilo kutokana na kesi iliyopo mahakamani. "Tanesco wana uamuzi, wakitaka kuingia mkataba mfupi au wa aina yoyote ni uamuzi wao maana vyombo vyote vya uamuzi vipo," alisema Waziri huyo na kuongeza:

"Nadhani watazungumza tu kama walivyoahidi pengine kwa sasa hawajajipanga na kama unavyojua pressure kutoka kwenye public (msukumo wa umma) ni mkubwa sana kutokana na matatizo haya ya Nishati ya umeme".

Akizungumzia suala la kuwa kikwazo kwa Tanesco pale walipokutana na kamati ya bunge ya Nishati na Madini, Ngeleja alisema kwa mujibu wa Kanuni za bunge toleo la mwaka 2007 kila waziri wa kisekta ni mjumbe katika kamati husika.

"Mimi sikuvamia kamati kama inavyodaiwa, wala sikwenda wa lengo lolote baya bali mimi ni mjumbe wa kamati ile kama kanuni zetu za bunge zinavyosomeka, tena bora umeniuliza hili maana wapo watu wanaweza kudhani mimi ni mvamizi wa vikao vya kamati,"alifafanua.

Waziri huyo akizungumzia suala la IPTL alisema yeye hawezi kufahamu sababu za kampuni hiyo kutozalisha umeme kwa kiwango cha juu cha uwezo wake, lakini akabainisha kuwa inawezekana ni kutokana na mahitaji waliyopewa na Tanesco.

"Mimi niko ofisini ndugu yangu, mambo mengine siwezi kuyaelewa maana inawezekana mahitaji ya Tanesco kutoka IPTL ni kiasi hicho kinachozalishwa ama pengine kuna hitilafu kwenye mitambo huwezi jua,"alisema Ngeleja huku akilishauri gazeti hili kuwasiliana na mfilisi wa IPTL aliyemtaja kwa jina moja la Rugonzibwa ili kupata ufafanuzi wa kina.

CTI nao waitaka Dowans
Naye Mwandishi Leon Bahati, anaripoti kuwa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) limetoa msimamo wake likisema kwamba suluhisho la haraka la kuokoa uchumi wa nchi usiendelee kuteketea ni kuruhusu mitambo ya kampuni ya Dowans iwashwe na kupunguza tatizo la uhaba wa umeme unaolikumba Taifa kwa sasa.

CTI imeitaka serikali pia kufanya mazungumzo na kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ili izalishe umeme kwa kiwango cha juu kama moja ya njia ya kusaidia pia kutatua tatizo lililopo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa CTI, Felix Mosha katika taarifa yake iliyotoa msimamo wa shirikisho hilo baada ya kutafakari kwa kina tatizo la umeme nchini.

“Tumetafakari kwa kina na kutambua kuwa pamoja na suala la Dowans kuingiliana na misimamo ya kisiasa, njia pekee na ya busara inayofaa kwa sasa kutatua tatizo hili la umeme ni kuruhusiwa kwa mitambo ya Dowans kufanya kazi,” alisema Mosha kupitia taarifa hiyo aliyoitoa jana.

Alisema watumiaji wakubwa wa umeme kupitia CTI wapo tayari kufanya mazungumzo na Tanesco ili kuangalia namna watakavyoshirikiana kukabiliana na gharama za wazalishaji wa nishati hiyo muhimu kwa uchumi.

Mosha alielezea kilio cha wenye viwanda nchini ambacho kiliwasilishwa kwa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kwamba tatizo la umeme nchini limewasababishia hasara kubwa ambayo inatishia kusimamisha uzalishaji.

“Viongozi pamoja na baadhi ya wanachama wa CTI Februari 21, mwaka huu walikutana na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kuwaelezea kwa kina jinsi wanavyopata hasara na kutishia kuviua,” alisema Mosha.

Kwa sababu hiyo akasema ni jambo la busara kutumia mitambo ya Dowans na IPTL kwa kuwa tayari ipo nchini na ndio suluhisho la haraka linaloweza kuchukuliwa kwa sasasa.

Mgawo wa Umeme kuendelea
Wakati hayo yakijiri, imebainishwa kuwa mgao wa umeme utaendelea kuwa tishio huku ikielezwa kuwa mitambo ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) haina mafuta ya kutosha kuzalisha kiwango cha umeme kinachotakiwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Makamba iliwaambia waandishi wa habari jana kuwa IPTL inashindwa kuzalisha umeme kwa kiwango kikubwa kinachotakiwa kutokana na kukosa mafuta ya kutosha.

Kutokana na hali hiyo, Makamba aliitaka Wizara ya Fedha (Hazina) kutoa fedha za kutosha kwa Kampuni hiyo ili iweze kununua mafuta ya kutosha kwa ajili ya kuendeshea mitambo hiyo ambayo ina uwezo wa kuzalisha megawati 100.

“Kwa sasa IPTL inazalisha megawati 10 mpaka 50 tu, jambo ambalo halitoshelezi kulingana na uwezo wa kuzalisha umeme katika mitambo hiyo,” alisema Makamba.

Alisema kutokana na hali hiyo Hazina inatakiwa kutoa fedha ya kutosha ili uzalishaji huo ufikie angalau megawati 80 na kwamba kama Hazina hawatafanya hivyo machungu ya mgawo wa umeme yataendelea.

Makamba alifafanua hayo muda mfupi baada ya kutoka kuzungumza na wadau mbalimbali wa umeme katika kikao kilichofanyika kwenye ofisi ndogo za bunge.

Makamba pia aliiagiza Shirika la Petroli nchini (TPDC) liipatie Kamati yake bei halisi ya gesi ilivyo nchini kutokana na bei ya nishati hiyo kupanda mara kwa mara.

“Bei ya gesi imekuwa ikipanda mara kwa mara, hivyo nimeiagiza TPDC kutupa maelezo kwa maandishi yanayoeleweka kuhusu bei halisi ya gesi,” alisema Makamba.

Alisema kuwa mitambo ya kusafirishia gesi iliyopo nchini imezidiwa uwezo kutokana na kuongezeka kwa viwanda na mashirika mbalimbali ambayo inatumia nishati hiyo, hivyo aliishauri serikali waongeze uwezo wa mitambo hiyo.

“Kwa sasa gesi inayotakiwa nchini ni mita za ujazo 15,000 ambazo ni sawa na megawati 10 kwa mwezi jambo ambalo hatuwezi kulimudu, serikali itoe fedha kwa ajili ya kubadilisha mitambo hii,” alisema Makamba.

Kamati hiyo ambayo pia ilipatiwa mikataba ya gesi inatarajiwa kukutana tena Jumatatu ijayo kwa ajili ya kufanya majumuisho.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Last Updated on Saturday, 26 February 2011 08:56 Comments




0 #4 comrade 2011-02-26 08:43 tanesco,wizara, kamati nyinyi wote ni wamoja na kazi yenu kuu ni kuhakikisha unapatiikana umeme wa uhakika embu tafuteni njia mbadala za kuwapatia watanzania umeme wa uhakika sio kutupiana mpira..
Quote









0 #3 Kizingo 2011-02-26 08:21 Kutokana na habari hii kuonyesha maelezo wanayotoa watendaji wa serikali, Tanesco na kamati ya nishati na madini, kuna JAMBO LA SIRI linafichwa! Bado sijapata sababu za msingi wananchi kuendelea kukosa umeme wakati kuna mitambo ya IPTL ambayo kwa sasa inazalisha megawati 10 lakini uwezo wake ni kuzalisha megawati 100! Sababu inayotolewa ni ukosefu wa mafuta! Wakati huohuo waziri husika anapoulizwa kuhusu jambo hilo anajibu, "Mimi niko ofisini ndugu yangu, mambo mengine siwezi kuyaelewa maana inawezekana mahitaji ya Tanesco kutoka IPTL ni kiasi hicho kinachozalishwa ama pengine kuna hitilafu kwenye mitambo huwezi jua,"alisema Ngeleja huku akilishauri gazeti kuwasiliana na mfilisi wa IPTL aliyemtaja kwa jina moja la Rugonzibwa ili kupata ufafanuzi wa kina! Wakati huohuo mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini anajua sababu zilizopelekea IPTL kuzalisha umeme kidogo lakini bado siasa zinaendelea kutawala. Jamani , sisi wananchi tumeathirika na tunaendelea kuathirika na mgao wa umeme.Kwahakika chuki inayoendelea kujengeka ndani ya jamii ni kubwa ambayo madhala yake tutayashuhudia soon.
Quote









0 #2 kidaruini 2011-02-26 08:05 tanesco wanasema hawaifahamu dowans. wanasema serikali ndiyo inayoifahamu. waziri wa nishati na madini mh Ngeleja anasema hawezi kuzungumza mambo yanayuhusu dowans. anayeweza kuzungumza ni tanesco.Jamani mbona mnatuchanganya? Hivi hiyo mitambo serikali haiwezi kununua ya kwake mipya? au wanangoja wawekezaji waliowekeza mabilioni ya fedha katika miradi mingi inayotumia umeme wafilisike na huku serikai imeshachukua kodi zao? ni kwa nini msisimamishe shughuli zote mkaona kwanza hili la umeme? hamjui viwanda vidogo tulivyo navyo vikiacha kuzalisha hamtapata pesa za kuwasomesha watoto wenu nje ya nchi na pesa za kufanya safari kila wiki kwenda nje ya nchi kwenda kuomba pesa za neti za mbu?
Quote









0 #1 Emily Kashingo 2011-02-26 07:26 NGELEJA WIZARA IMEMSHINDA AACHIE NGAZI ASISUBIRI KUTOLEWA NA WANANCHI KWANI HATUMTAKI, LAKINI MKURUGENZI WA TANESCO MHANDO NAYE AACHIE NGAZI,KAMA HAWAWEZI HATA KUTOA UFAFANUZI HAWA SIO VIONGOZI NA HATA KAMA NI VIONGOZI NI MAMBUMBUMBU WA KUSOMA ISHARA NA NYAKATI, WANANCHI WAMECHIKA HAWATAKI SIASA WANATAKA UTEKELEZAJI
Quote
 
Dowans yalikoroga taifa
• Wadau sasa wataka mitambo yake iwashwe

na Bakari Kimwanga


amka2.gif
SAKATA la kuwashwa au kutokuwashwa mitambo ya Kampuni ya umeme wa dharura ya Dowans, limechukua sura mpya baada ya wananchi kutaka siasa ziachwe na mitambo hiyo iwashwe kuinusuru nchi katika mgawo wa umeme unaoendelea.
Kilio hicho wamekitoa jana jijini Dar es Salaam katika kikao cha pamoja kilichofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee ambacho kiliitishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambacho kilihudhuriwa pia na watendaji wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO)
Walisema kuwa mgawo wa umeme umeathiri uchumi wa taifa, kwani viwanda vingi vimelazimika kupunguza uzalishaji sambamba na kuwapunguza kazi baadhi ya wafanyakazi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Utafiti na Sera wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Tonedeus Muganyizi, alisema migogoro ya kampuni za kuzalisha umeme za IPTL na Dowans kumesababisha mamlaka hiyo kukosa sh bilioni mbili kila mwezi, ambazo ni kodi zilizokuwa zikitolewa na kampuni husika.
"Serikali ikae na iamue kuwasha mitambo ya Dowans ili tupate fedha za kodi sambamba na kuvihuisha viwanda vinavyosuasua kwa kukosa umeme," alisema.
Alisema umefika wakati wa kumaliza tatizo la mgawo wa umeme kuliko kusubiri hadi Juni mwaka huu kama Mkurugenzi wa TANESCO, William Mhando, alivyobainisha kuwa ndiyo mgawo wa umeme utafikia kikomo.
Alisema kitendo cha kuwaka umeme kutasababisha serikali kupitia TRA kupata trioni 5.6, ambazo wamejiwekea katika malengo yao kwa mwaka huu wa fedha na kuonyesha hofu yake ya kushindwa kufikia malengo waliyowekewa na serikali.
"Wanasiasa wafike mahali waheshimu wataalamu, hasa katika masuala muhimu kwa taifa kuliko hali ilivyo sasa, ambapo siasa zimekuwa na nguvu kuliko utaalamu wa sekta husika," alisema
Mwakilishi wa taasisi za sekta binafsi, Edward Furaha, alisema ili nchi iendelee ni lazima mitambo ya Dowans iwashwe sambamba na kuziweka kando siasa za malumbano na chuki ambazo zimekuwa zikipewa nafasi kubwa hivi sasa.

"Leo mkulima wa mboga mboga anashindwa hata kuzalisha vile inavyotakiwa lakini leo kama mitambo ya Dowans ingewashwa tungeondokana na hali hii, lakini kila eneo siasa zimetawala hata katika mambo ya kitaalamu, sasa mgonjwa anavuja damu na anatakiwa kutibiwa haraka kwa dharura, hebu Dowans iwashwe ili tumalize tatizo kwa dharura," alisema Edward.
Alisema tangu kutungwa sheria ya umeme ya mwaka 2008 na kupitishwa na Bunge lakini hadi sasa hakuna kanuni zinazoendesha sheria hizo zaidi ya Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Maji na Nishati (Ewura) kutangaza kupandisha bei ya umeme kila wakati huku nishati hiyo ikiwa adimu nchini.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwaji Group Works Limited, Alan Mwaigaga, alisema suala la mgawo wa umeme lisichukuliwe kisiasa, ni muhimu wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana na TANESCO ili kumaliza taizo la umeme lililopo sasa.
Mdau mwingine katika mkutano huo ambaye pia ni mwakilishi wa Kampuni ya SD toka nchini Israel, Marick Kasambala, alisema kutowashwa mitambo ya Dowans ni shikizo la kisiasa na kuhoji nini TANESCO wanachoshindwa kukutana na wamiliki wa kampuni hiyo ili wawashwe mitambo hiyo katika kipindi hiki cha hatari ya mgao umeme.
" Mitambo ya IPTL na Dowans iwashwe na kufanya kazi huku TANESCO iachiwe iwe na mikakati ya kuondoa tatizo hili milele kuliko sasa siasa na malumbano ya watu zaidi kuna nini au ndio urasaimu unazongumzwa jamani," alisena na kuhoji Kasambala.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk. Servecius Likwelile, alisema mgawo wa umeme unaoendelea huenda ukasababisha kushuka kwa pato la taifa na wateja wengi kushindwa kulipa kodi.
"Hali hii huenda ikasababisha pato letu likapungua kutoka asimilia saba ya sasa hadi kufikia tano, na kama uzalishaji haupo kwa kukosa umeme huku gharama za pato zinakuwa kubwa na kusababisha ugumu wa maisha, ni vizuri tuwe na bajeti ya dharura hasa katika kukabiliana na hali hii ya mgawo nchini," alisema Dk. Likwelile.
Alisema hali ya mgao inatakiwa kumalizika na hali ya uchumi huenda ikaporomoka kwa mujibu wa pato la taifa kwa mwaka (GDP) ambayo inaonyesha kukosekana kwa umeme hivi sasa serikali inapoteza Trilioni 1.4 na kupoteza lengo la uchumi wa nchi.
Alisema kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni ukweli kuwekwa bayana kwa kuishauri serikali pamoja na Kamati ya Nishati na Madini kuepuka siasa, kutoiingilia TANESCO katika utendaji wa kila siku ili umeme wa uhakika upatikane.
Awali Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Wiliam Mhando, alisema kuna hatari ya kuwa na mgawo ukaenda hadi Julai mwaka huu kutokana na vyanzo vingi vya maji hasa katika mabwawa kukauka na kushindwa kuzalisha umeme.
"Hivi sasa tunapata megawati 540 na mahitaji ya taifa ni megawati 833, lakini bado tuna tatizo la mgawo ambao bado huenda ukalisumbua taifa hadi Julai mwaka huu nasi TANESCO tunajitahidi kuagiza mitambo kutoka nje ya nchi na huenda ikafika mwezi huo" alisema.
Mhando alisema TANESCO imekuwa ikilazimika kuzima mitambo iliyopo kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme kutokana na uhaba huo wa maji huku jenereta za Kampuni ya IPTL nazo zikishindwa kutoa kiwango kilichotarajiwa kutokana na kukosekana kwa mafuta ya uhakika ya kusukuma mitambo hiyo.
"Hivi sasa mchana inazalisha megawati 10, usiku tukiisukuma kwa nguvu hadi kufikia megawati 50 tu, lakini kama tukipata mafuta ya uhakika ina uwezo wa kuzalisha megawati 80," alisema Mhando.
 
Huruma hii ya Dowans inatoka wapi?
ban.nyamaza.jpg

Salehe Mohamed

amka2.gif
KWA takriban miaka mitatu sasa sinema ya mitambo ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Dowans imezidi kushika kasi kwenye macho,vichwa na masikio ya kila mwenye kiu na habari pamoja na nishati ya umeme.
Sinema hii kwangu imeshnichosha licha ya baadhi ya watu wenye kuheshimika hapa nchini kuitumia kwa lengo la kujinufaisha kwa namna wanayoijua wao hasa katika kipindi hiki cha mgawo wa umeme.
Baada ya Dowans na TANESCO kufikishana kwenye mahakama ya kimataifa inayoshughulikia migogoro ya kibiashara na TANESCO kuamriwa kulipa fidia y ash bilioni 94, sasa sinema hiyo imebadili upepo.
Dowans sasa wanaionea huruma Tanzania kwa kukaa gizani wakati mitambo ya kuzalisha umeme ipo, kampuni hiyo inataka kuzungumza na TANESCO ili kuangalia uwezekano wa kupunguza fidia wanayoitaka.
Ili kuwaonyesha kuwa wana huruma zaidi, mmiliki wao Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, anayeishi Oman aliamua kuja hapa nchini, ili kuzungumza na TANESCO namna watakavyoweza kulimaliza skata hilo kwa njia iliyo bora.
Eti mmliki huyo ameguswa na Tanzania kuwa gizani kiasi cha kutuhurumia, anasema aliwaandikia barua TANESCO ili wafanye mazungumzo lakini Shirika hilo mpaka sasa limekaa kimya.
Mkurugenzi wa Fedha wa Dowans, Stanley Munai, anasema wanataka walipwe kiasi cha sh bilioni 36 (dola milioni 24) ambazo ndiyo thamani ya umeme iliyowauzia TANESCO kabla ya mkataba wao kuvunjwa mwaka 2008.
Ni vema kabla ya kuanza kushabikia au kufurahia huruma hii ya Dowans tukajiuliza ni kwa nini imekuja hivi sasa? Kwanini baadhi ya viongozi hasa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba wapo mbele kuuaminisha umma kuwa hatuwezi kuwa na umeme wa uhakika bila Dowans.
Makamba, anashauri TANESCO waingie mkataba wa muda mfupi na Dowans ili umeme upatikane, hazungumzii matokeo ya kesi baina ya pande hizo mbili na wala hazungumzii uzembe wa serikali ambayo kwa takriban miaka minne imeshindwa kununua mitambo kama ya Dowans au kuzidi hiyo.
Mwenyekiti huyo anataka jamii ione TANESCO ndiyo wanaokwamisha mazungumzo na Dowans ili kupata umeme wa uhakika, lakini hazungumzii watu waliotufikisha hapa tulipo, je mtu huyu ana nia njema na taifa?
Hivi ni kweli hatuwezi kuwa na umeme wa uhakika pasipo na Dowans au ndiyo viongozi wetu wanaitumia kampuni hiyo kujinufaisha?
Kimsingi ujio wa mmiliki wa Dowans na kasi ya viongozi wetu vinatia shaka, vinaonyesha wazi kuna ajenda ya siri au ulaji ndani ya sakata hilo, TANESCO wanataka waburuzwe kwa matakwa ya wachache.
Hebu tujiulize Dowans wanatuonea huruma na kusamehe sehemu ya deni wanalotudai bila kutegemea chochote? Jibu ni hapana wanafanya hivyo wakijua fika wataanza kuuza umeme wao kwa shirika hilo muda si mrefu.
Huruma hii ya Dowans ni ya kuogopwa sana, Tunahitaji muda wa kufikiri zaidi juu ya huruma hiyo ambayo inaweza kuwa mzigo mkubwa kwetu kuliko hata ule wa awali tuliouvunja.
Haiingii akilini kuwa Dowans ambayo ni kampuni ya kibiashara ikasamehe zaidi ya mili 55 bila kuwepo mazingira ya kupata fedha hizo kwa mlango wa nyuma kama inavyofanyika katika mikataba mbalimbali ambayo Tanzania huingia na wale tunaowaita kuwa ni wawekezaji.
Tunahitaji umakini mkubwa wa kupokea huruma hii na ikiwezekana kila kitu kiwekwe wazi katika sakata hilo ili TANESCO isije ikatumbukizwa kwenye mtego wa watu wachache ambao kila kukicha hupanga mbinu za kutafuna rasilimali za taifa.
Tunachotakiwa kukifanya hivi sasa ni kuibana serikali itekeleze miradi ya kuzalisha umeme kama walivyoahidi miaka mingi iliyopita na wala si kushabikia umeme wa kampuni za dharura.
Inatia aibu na kusikitisha kuona Tanzania yenye dhahabu, tanzanite, mito, bahari, maziwa, makaa ya mawe, chuma ikiendelea kuwa katika giza ilhali nchi zisizo na vitu hivyo zikiwa na umeme wa uhakika na mwingine zinauuza nje ya nchi zao.
Afrika Kusini ina idadi ya watu milioni 40 kama tulivyo sisi na ina uwezo wa kuzalisha megawati 42,000 lakini sisi hatuna uwezo hata wa kuzalisha megawati 1000, hii ni aibu na kamwe hatuwezi kuendelea kama umeme utaendelea kugawiwa kwa mafungu.
Leo hii uchumi unalega lega kwa sababu ya viwanda vingi vinashindwa kuzalisha kwa kiwango kinachotakiwa na pia vimeshawafukuza kazi baadhi ya watu ili kubana matumizi lakini wananchi wanaendelea kuwa wapole kwa madai kuwa kutopatikana kwa mvua za kuyajaza mabwawa ya kuzalisha maji ni mapenzi ya Mungu.
Hakuna mapenzi ya Mungu hapa, bali ni mipango mibovu na ulaji wa watawala wetu ambao wanajua fika kama nchi itakuwa na umeme wa uhakika hawatoweza kupata tenda za kuuza mafuta au kuingiza majenereta hapa nchini.
Wananchi hivi sasa wamekata tamaa ya maisha, hawajui kesho itafikaje, ahadi ya maisha bora yatapatikana katika Tanzania yenye neema hivi sasa haisikiki tena, porojo za siasa, maneno matamu matamu na matumaini yasiyokamilika ndiyo yanayozungumzwa kila kukicha na wanasiasa wetu.
Mazingira tuliyonayo hivi sasa yanaonyesha wazi kuwa viongozi wetu wameshindwa kubuni mbinu na mikakati imara ya kutuoa kwenye umasikini tulionao, suluhisho la pekee ni kuwawajibisha na tutafute wengine wenye uwezo wa kutukwamua kutoka hapa tulipo.
Kama tutaendelea kuvumilia ngonjera za Dowans, Bajaj kwa wajawazito, meli kubwa na nyinginezo kamwe hatutaweza kuachana na giza linalotukabili pamoja na hali duni ya maisha
 
Maswali 14 kwa Brigedia Al Adawi wa Dowans
ban.tafakuri.jpg

Deogratius Temba

amka2.gif
MTU anayejiita au anayatajwa kuwa ndiye mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya Dowans Tanzania Limited, Brigedia Jenerali (mstaafu), Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi, anayeishi Oman, amefika Tanzania mwishoni mwa wiki iliyopita na kujitambulisha kuwa ndiye mmiliki wa kampuni hiyo.
Binafsi sitaki na wala siwezi kuhalalisha kwa kumtaja kuwa ni mmiliki kwa sababu sina uhakika na umiliki wake kutokana na yeye mwenyewe kujichanganya kimaelezo wakati anajieleza.
Bahati mbaya kabisa, ambayo na yeye ameichangia, ni Watanzania kutokusikia sauti yake kwenye redio au kumuona akizungumza kwenye runinga. Hili limeongeza utata.
Pia waliofanya naye makubaliano hawataki kumkubali kuwa wamemwalika au wanamtambua au wanatambua ujio wake. Hii ni ajabu na mazingaombwe ya mwaka 2011.
Mazingira ya ujio Al Adawi, kama mwekezaji wa mradi mkubwa kiasi hiki unazua utata kwangu binafsi na baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kiuchumi na siasa za hapa Tanzania kuwa hakuna uwazi.
Tunayo maswali mengi ya kumuuliza Al Adawi kutokana na ujio wake na mazingira ya uwekezaji wake ili tuendelee kujishawishi kuwa yeye ndiye mmiliki wa Dowans Tanzania, na pia anastahili kuendelea kutambuliwa na Watanzania wote hivyo. Kwa kuwa ni mtu muhimu sana kwetu anayeweza kumaliza tatizo kubwa la umeme tulilo nalo.
Tatizo letu sisi Watanzania pamoja na matatizo na changamoto zote zilizo kwisha jitokeza kwasasa tunataka suluhisho la tatizo la umeme.
Tunataka mgawo wa umeme umalizike Watanzania tufanye kazi, shuguli zetu zimekwama, uzalishaji umeshuka na maisha yanazidi kuwa magumu.
Mfano, amesema "I am here to find a happy resolution, a business decision. I am ready to offer something nice to TANESCO ……..." Kwa tafsiri isiyo sahihi, "Nipo hapa (Tanzania) kutafuta suluhu ya amani, maamuzi ya kibiashara, nipo tayari kutoa kitu kizuri kwa TANESCO…." Haya ni maneno ya tajiri huyu.
Suala la ujio au kutoka kwa mmiliki wa Dowans bila shaka halina maslahi kwa tajiri huyu wa kiarabu, ila tatizo na wasiwasi wetu ni jinsi alivyokuja au kuingia nchini, na akazungumza na baadaye waliodaiwa kumwalika nchini wakamkana.
Yapo maswali mengi ambayo watu mbalimbali mitaani, na wachambuzi wa mwambo wamejiuliza kuhusu ujio wa Al Adawi. Moja ni kwanini amekataa kupigwa picha na waandishi wa habari? Na ni kwanini amebagua vyombo vya habari katika mkutano wake?
Katika maelezo yake amesema kuwa si kawaida yake kuzungumza na vyombo vya habari, na kwamba hataki kupigwa picha yoyote, kwa sababu yeye ni mfanyabiashara asiyependa makuu na asiye na makeke.
Akasema amewekeza katika nchi 12 duniani, na kwamba katika zote hizo anawakilishwa na rafiki zake; na kwamba hapa nchini aliletwa na Rostam Aziz mwaka 2005 kwa ajili ya mradi wa Fibre Optic. Hiyo si sababu ya kukataa kupigwa picha hasa pale unapojitaja kama mtu maarufu.

  1. Al Adawi haoni au hajui kuwa kuwaita waandishi wa habari wanataaluma wenye maadili ya kazi zao na kuwapangia cha kufanya ni kuingilia uhuru wa habari katika nchi za watu hasa zinazofuata mfumo wa demokrasia na utawala bora?
  2. Je, haoni kuwa tayari amejenga picha na mtazamo hasi miongoni mwa wananchi wa Tanzania kuwa ameteka vyombo vya habari?
  3. Je hawaoni kuwa kubagua vyombo vya habari ni kuwanyima wananchi haki ya habari na kujua kinachoendelea kama ilivyoainishwa katika ibara ya 18(2) ya katiba ya Tanzania? na pia kinyume cha ibara ya 19 ya tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa.
  4. Ni kwanini Al Adawi amekuja katika kipindi hiki ambacho Taifa lipo katika changamoto kubwa kiasi hiki ya nishati ya umeme?
  5. Kwanini Al Adawi hakuja Tanzania katika kipindi kingine mfano mwaka 2007 na 2008 ambapo mjadala mzito ulikuwa umeibuka juu ya uhalali wa kampuni yake na kuihusisha na Richmond?
  6. Al Adawi haoni kuwa ujio wake Tanzania kwa kipindi hiki unaonekana kuwa amekuja kwasababu kuna tatizo kubwa na anataka kulishawishi Taifa kununua mitambo yake?
  7. Ni kwanini ujio wa Al Adawi unarukwa na viongozi waandamizi wa serikali kuwa hawajamwalika wakati yeye anawataja kuwa amealikwa nao?
  8. Al Adawi haoni kuwa kujichanganya huko na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO kukana kumwalika au kumfahamu kunafungu ukurasa mpya katika sakata la Dowans kuwa hakuna uwazi?
  9. Ni kwanini hakuja nchini mapema kuweka mambo sawa wakati Bunge lilipo kuwa likihangaika kuuda kamati teule ya kuchunguza mkataba wa kampuni ya Richmond na kuisaidia kwa kutoa ushahidi kuwa kampuni yake imeridhi mkataba halali na siyo feki kama ilivyoainishwa katika kamati ya Bunge?
  10. Mmiliki huyu wa Dowans kwanini anasema kuwa anataka kufanyia Tanzania kitu kizuri juu ya umeme, wakati anajua kuwa kampuni yake ilishaishtaki Tanzania na hukumu imeshatoa?
  11. Watanzania wanaweza kujiuliza ni kwanini kama kweli alikuwa na huruma na umasikini wetu hakujitokeza mapema na kuomba suluhu ya nje ya mahakama na kuomba mnakubaliano mapya au mkataba ili kuokoa gharama za kesi?
  12. Mmiliki wa Dowans hajui kuwa hukumu ikishatoka mdaiwa atapaswa kulipa? 13. Na kama mmekubaliana vinginevyo ni lazima kuitaarifu mahakama?
  13. Al Adawi una uhakika kuwa unaweza kulifuta deni letu lote kwa kwa huruma bila Watanzania kulazimishwa kufuata masharti yasiyo na faida kwao?
  14. Al Adawi yupo tayari kulifuta deni lote halafu tuachane na yeye kibiashara kabisa? Ili kuonesha kuwa ameona na kukisikia kilio cha Watanzania masikini ambao kodi yao ndio itakayo mlipa?
Maswali haya 14 kwa Brigedia Jenerali (Mstaafu) Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi, ni machache kulingana na mengi ambayo Watanzania wanaulizana ambayo kama angeweza kuyajibu ipasavyo, manung'uniko ya chini chini ya wananchi kuhusu ujio wake yangepungua au kuisha kabisa.
Ni vizuri waliomleta au kumsaidia mtu huyu wakawa makini wakati mwingine, wasiwe wanawaleta wageni halafu wanashindwa kuwaelekeza namna ya kutoa maelezo ya kutosheleza.
Bado Watanazania tunahotaji maelezo ya kina na ya wazi kutoka kwa Al Adawi, kama bado yupo nchini atoe ufafanuzi zaidi.
 
Back
Top Bottom