Elections 2010 Dr. Slaa kumuwekea pingamizi Kikwete!

Elections 2010 Dr. Slaa kumuwekea pingamizi Kikwete!

Hii ni balaaaaa mwenye kitabu cha sheria za uchaguzi atuwekee maana kama bilion 1.5 ni kwenye mabango tu sasa ikija kwenye swala la mavazi yao (mashati,vitenge,kofia,t-shirt) itakuwaje????? :confused2::confused2:
 
Hiyo nyekundu nakuelewesha kuwa, Hao mapadre wanasomea mambo mengi sana na ndiyo maana kuna Madaktari Bingwa wengi sana Masista na mapadre na hata nyanja zingine nyingi tu. Tambua kuwa kuna vyuo, mashule, na vitengo mbalimbali katika kanisa na pia tambua kuwa viongozi wengi wa mwanzo wa nchi hii wenye taaluma maalum wamesoma huko, ila sheria za kuwa mapadre hazikuwaruhusu na wakaja huku katika siasa.
Kanisa ndo lilianza mambo ya upendo, umoja, amani na ndo sera zake ambazo Tz bado inajivunia.
Katiaka Bold; Jamaa kainua kwanza mishahara kimya kimya mara tu alipomsikia DR. wa kweli akinukuu ile hotuba na "wazee wa DAR" Mimi pia nishtuka kuona mshahara umeongezeka ghafla. Hilo ni dili tu na ni rushwa kwa mtu mkubwa kama yeye. Siku ile alidiriki hata kuwatukana wafanyakazi kupitia mwakilishi wetu, leo anakataa eti atatufikiria wapi na wapi.
Dr. slaa na haki ya kupinga. JK katuhonga laivu ni kwa vile tu sisi ni watanzania ingekuwa kwa wenzetu yaani kashatoka saa nyingi!!!
SEMA TU CCM NDO KASHIKA MPINI NA ATAFANYA LOLOTE KUIGEUZA ISHU
kAMA MUONGO KUWA NI WAMAFIA BASI SUBIRI UONE!

Shiiiit, nigga has a PHD in theology and he is treated like he has the real PHD. You know, the ones that you actually have to earn them. Eti Dr. Slaa. Come oon people. He might be a heck of a leader and visionary or whatever you guys want to anoint him to be, but acting like he is a law guru is a stretch.

And its bad politics going after wafanyakazi salaries. The Makambas of the world will spin this around and mtanzania wa kawaida will made it to believe kwamba Chadema is against the salaries. In politics its not about making sense--its about selling it to voters. Whoever has the loudest mouth wins the contests.
 
Hiyo nyekundu ni ungo mkubwa. Dr. Slaa hiyo sheria kaisomea wapi au sheria ya kanisa ndio inamfanya kubobea kitaaluma katika sheria?

Nawasiwasi kama Dr. Slaa hana washauri wa kweli. kwani habari ya mshahara kuongezeka sio ya leo na wala hajaanza baada ya kampeni. watu wamesha kula mishahara miwili mpya na kampeni hazina hata wiki sasa hapo si ukilaza jamani. Hao FOS au FOD wanamshauri nini kama ndio anatuletea hizi pumba hata kabla hajaanza kampeni.

Heri Dr. Slaa amesoma hiyo sheria hata kama ni ya kanisa but amesoma huyo wakwenu amesomea wapi hadi akapata UDOKTA!!!! KUBALINI MATOKEO TU WANA CCM MSIINGIZE MAMBO YA DINI KWENYE MASWALA YA KITAIFA. MKIAANZA MAMBO YA UDINI NCHI ITAELEKEA KUBAYA MAANA KILA MTANZANIA ATATAKA KIONGOZI WADINI YAKE!!!!
 
Nimesoma habari hii kwenye Gazeti la Mwenyekiti wa Chadema Mbowe la leo-Tanzania Daima habari hii ya Padri Slaa ina walakini. na haieleweki anasema kuwa JK anatumia majukwaa ya mikutano yake kueleza mafanikio ya serikali na pale anatakiwa aseme mambo ya chama tu.Jk alipeleka Ilani ya Chama chake kwa wananchi 2005 akawaambia kuwa mkinipa kura zenu kwa kupitia Ilani hii nitaunda serikali kutekeleza ahadi hizi.sasa kwa vile ametekeleza ahadi hizo ni lazima apite tena kwa wananchi na kuwaeleza kuwa tayari ametekeleza ahadi na sasa wampe nafasi afanye mengine.sasa Slaa alitaka JK aseme kitu gani?

kwenye Hili la mishahara Slaa anasema wao yaani yeye na Mgaya walitaka kima cha chini kiwe laki 315,000 na JK ameongeza toka 104,000 hadi 235,000 kama asilimia 126% kama Slaa ana mapenzi na wafanyakazi angesema kuwa asilimia 126% imeongezwa ni jambo zuri.sasa sielewi analalamika kwa vile hazikufika laki tatu na 15 elfu? kama zingefika asingeweka pingamizi? Slaa anajua yeye ni Small Fish in the big sea na shughuli ya Urais ni kubwa hana elimu wala uwezo wa kuifanya anatafuta sababu . source Tanzania Daima - Sauti ya Watu
 
Mimi sikuzungumzia Udaktari wa Slaa, nilichokuwa na pinga ni habari iliyosema Dr. Slaa kabobea katika taaluma ya sheria.

Nimesoma habari hii kwenye Gazeti la Mwenyekiti wa Chadema Mbowe la leo-Tanzania Daima habari hii ya Padri Slaa ina walakini. na haieleweki anasema kuwa JK anatumia majukwaa ya mikutano yake kueleza mafanikio ya serikali na pale anatakiwa aseme mambo ya chama tu.Jk alipeleka Ilani ya Chama chake kwa wananchi 2005 akawaambia kuwa mkinipa kura zenu kwa kupitia Ilani hii nitaunda serikali kutekeleza ahadi hizi.sasa kwa vile ametekeleza ahadi hizo ni lazima apite tena kwa wananchi na kuwaeleza kuwa tayari ametekeleza ahadi na sasa wampe nafasi afanye mengine.sasa Slaa alitaka JK aseme kitu gani?

kwenye Hili la mishahara Slaa anasema wao yaani yeye na Mgaya walitaka kima cha chini kiwe laki 315,000 na JK ameongeza toka 104,000 hadi 235,000 kama asilimia 126% kama Slaa ana mapenzi na wafanyakazi angesema kuwa asilimia 126% imeongezwa ni jambo zuri.sasa sielewi analalamika kwa vile hazikufika laki tatu na 15 elfu? kama zingefika asingeweka pingamizi? Slaa anajua yeye ni Small Fish in the big sea na shughuli ya Urais ni kubwa hana elimu wala uwezo wa kuifanya anatafuta sababu . source Tanzania Daima - Sauti ya Watu


Upupu
 
Hutuba ya bajeti ya mwaka 2010/11 [Wizara ya fedha]
55. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Nne inatambua umuhimu wa kuwa na maslahi bora ya wafanyakazi katika kuongeza ufanisi na tija. Serikali inachukua hatua za kuboresha maslahi ya wafanyakazi katika mwaka 2010/11. Sanjari na hatua hii, utaratibu wa kuhakiki mishahara utaendelea ili kudhibiti malipo kwa wafanyakazi hewa.

(ii) Kupunguza kiwango cha chini cha Kodi ya Mapato kwa wafanyakazi kutoka asilimia 15 hadi asilimia 14 sambamba na nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kitakachotangazwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma. Lengo ni kuwaongezea kipato na kuwapunguzia mzigo wa kodi watumishi wa umma wenye kipato cha chini;

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA:



44. Mheshimiwa Spika
mishahara ya Watumishi wa Umma itaongezwa kwa
kuzingatia makubaliano yaliyofikiwa katika Baraza la Majadiliano ya Pamoja Katika
Utumishi wa Umma. Serikali itaandaa mkakati wa utekelezaji wa Sera ya Malipo ya
Mishahara na Motisha Katika Utumishi wa Umma mara baada ya Sera hiyo
kupitishwa. Aidha, Serikali itakamilisha uanzishaji wa Bodi ya Maslahi na Tija katika
Utumishi wa Umma.


{Kamati ya kujadili bajeti ya wizara ya nchi, ofisi ya rais, menejimenti ya utumishi wa umma}
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani wakati nasoma hotuba yangu nimesema kwamba Serikali imekubali kuongeza kima cha chini sawa na makubaliano yetu na Vyama vya Wafanyakazi. Kwa kufanya hivyo Bajeti ya mishahara mwaka huu imeongezeka kwa shilingi bilioni 558 ukilinganisha na ya mwaka jana

Tuambie wapi mishahara hajapitishwa na bunge?


Wewe pupu msikilize Dr Slaa anavyosema sio unakurupuka kama njugu
 
Shiiiit, nigga has a PHD in theology and he is treated like he has the real PHD. You know, the ones that you actually have to earn them. Eti Dr. Slaa. Come oon people. He might be a heck of a leader and visionary or whatever you guys want to anoint him to be, but acting like he is a law guru is a stretch.

And its bad politics going after wafanyakazi salaries. The Makambas of the world will spin this around and mtanzania wa kawaida will made it to believe kwamba Chadema is against the salaries. In politics its not about making sense--its about selling it to voters. Whoever has the loudest mouth wins the contests.


Jamani dr ya kikwete ni ya nini vile?
 
kuna watu humu jf akiwa na keyboard na mouce bas anaandika upupu tupu

hivi dr wenu kikwete ana phd ya nini

wewe dubo unajua cannon law inacover vitu gani?

ndio maana dr wenu kikwete anasaini sheria bila kusoma!! dr kikwete = dr uchwara
 
jk: hivi ninapoongea watu wananielewa? maana unajua kinana mimi naongea tu lakini sasa mbona ninapoongelea mambo ya wafanya kazi watu wote wanakaa kimya?! hata nilisema kuwa tutaongeza mishara bado walikaa kimya niliona kikundi cha ngoma tu ndo wanashangilia!

kinana: wanaelewa hivyo hivyo ila unapokuwa unaongea usipende kuweka neno TUKTA na viongozi wake pale unawachafua sana watu na hasa wakikumbuka matamshi yako . we kazia kuwa tutaboresha maslahi yao.

jk: hivi nilimtaja mgaya tena? maana unajua najiongelea tu hata ilani ya chama siiangalii

kinana: hujamtaja jina lake ila ukisema neno tukta moja kwa moja watu wanajua unamtaja mgaya?

jk: siku ile niliteleza tu pale unajua tukta nao waliniudhi na nisingekuwa mbishi wale wangegoma halafu ningeaibika sana si unakumbuka kulikiwa na kikao cha WEF ?

kinana: nakumbuka sana ila uliingiwa jazba sana

jk: chupa yangu ya maji iko wapi, hebu angalia upande wako huko, najisikia kuchemka!

kinana: mbona chupa unayo mkononi umeshika!

jk: aisee, kweli. hii kwa sasa tunaelekewa wapi maana huku angani sijui kabisa wapi tunakwenda

kinana: ngara!

jk: hivi una habari na makamba yuko wapi? unajua yule angekuja huku angeharibu sana.yaani sasa hivi tutumie hila na mbinu zote; dr slaa akianza kampeni zake patakuwa hapatoshi. wana sera nzuri sana. ila kinana kusema ukweli miaka mitano iliyopita nimejitahidi sana ila basi tu kulikuwa na matatizo kibao duniani....

kinana: jiandae mkuu tunakaribia kutua ngara

jk. hebu nishikie maji yangu na box langu la biskuti.....
 
Amekurupuka huyo na washauri wake wako kisiasa zaidi badala ya kutafuta ukweli.kura hazitafutwi hivyo .

Hata alipotaja Majina ya wale mafisadi 11 walimwambia kakurupuka, Na hata aliposema kuwa sheria iliyosainiwa kwa mbwembwe pale magogoni imechakachuliwa walimwambia tena kuwa kakurupuka...

Ila wote tunajua in both occasions what followed. Dokta proved them wrong.
 
Kweli sasa naanza kuamini kuwa JK maji yamemfika shingoni ndiyo sababu sasa hajui tena namna ya kuwadanganya Wadanganyika. Lililobakia sasa ni rushwa mbele kwa mbele.

Nafikiri ameshasahau kuwa mwezi wa tano (May) aliwahutubia wazee wa SISIM kwamba hataki kura za wafanyakazi na mishahara hatapandisha kwa kuwa serikali haina uwezo na kuwa hata miika 8 ijayo serikali haitakuwa na uwezo huo. Sasa sijui leo pesa wamezito wapi?? No wonder, Tsh imeshuka value kwa kasi ya ajabu ili kupata pesa za kuwapa rushwa Wadanganyika.

Natabili miika 5 ya maisha magumu kwa Wadanganyika kama JK ataendelea kuwa rais. Utabili kama huu Sheik Yahya hauwezi. Yeye wake ni wa kufa kwa watu.
 
CCM laughs off Chadema claims on JK




By Dominic Nkolimwa



27th August 2010


email.png

Email



printer.png

Print



comment_bubble.png

Comments








SlaaWaandishi.jpg

Chadema presidential candidate Willbrod Slaa



CCM has dismissed as "the expected manifestations of election fever" yesterday's reports of plans by the opposition Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) to file an objection against the ruling party's presidential candidate, President Jakaya Kikwete.
Chadema says it believes that Kikwete has contravened the Election Expenses Act of 2010 by appearing to use his ongoing election campaigns to promise workers pay hikes.
But Capt (rtd) John Chiligati, the CCM publicity secretary, told this paper later in the day that all that their candidate was doing was to elaborate on the extent to which the government he was heading had implemented the ruling party's 2010 Election Manifesto.
"All pronouncements CCM candidates at all levels are making at campaigns rallies elaborates on the contents of our manifesto, which was launched at Jangwani grounds in Dar es Salaam on Saturday (August 21), and not otherwise," he said.
"Among other things, our manifesto addresses the needs to improve the living standards of workers. So what is wrong with a CCM candidate elaborating on such issues," he queried, "advising" all aggrieved parties including Chadema "to play it cool as the election fever takes its toll and wait for polling day – October 31".
Chadema presidential candidate Willbrod Slaa revealed the objection plans at a news conference in Dar es Salaam, saying his CCM counterpart (President Kikwete) had violated Section 21 (1) of the Election Expenses Act "by announcing salary rises for workers at one of his campaign rallies in Mwanza Region".
Dr Slaa argued that the law was categorical that that it was wrong for any aspirants or candidates "to offer or promise to offer cash or anything of value to prospective voters during the nomination or campaign period".
"President Kikwete did exactly that at his campaign rally at Mwanza by telling workers that he has raised the minimum wage, while knowing that saying so could woo the workers to vote for him," he said.
"This amounts to corruptions because the president had previously rejected all pleas from trade unions for the minimum wages to be adjusted upwards to 315,000/-. He even dissolved Parliament declaring that he would not budge," he added.
Dr Slaa announced that he had instructed the Chadema lawyer to make sure that the objection was filed today with the office of the Registrar of Political Parties, "in relation to this breach of the Election Expenses Act".
He admitted that, by virtue of his being the sitting President, the CCM presidential candidate retained "some rights like full escort and security detail at campaign rallies, but not using political platforms to make decisions of far-reaching impact like this one".
"What I know it is only Parliament which has the mandates to adjust workers' wages," he pointed out, adding that it appeared the procedure was being ignored and the timing of the adjustments raised doubts.
Dr Slaa said Chadema would continue fighting for the Tanzanian people's rights "because it sincerely believes that it quite possible for workers to be paid better than is now the case if the government is really keen and serious about it".
"There is unequal distribution of economic gains among our people, with some filthy rich and others dirt poor, a situation we (Chadema) promise to rectify," he noted.




SOURCE: THE GUARDIAN

Hivi hawa jamaa SISIM wameshaanza ku-implement 2010 manifeto!!!!! Kweli sasa hii ni kasi ya ajabu.
 
Kwa mujibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya 2010, kifungu cha 21(1a) kisemacho,

PART V
PROHffiITED PRACTICES
Unfair conducts
21.-(1) During the nomination process, election
campaign or election, an act of prohibited practice shall be
committed by-
(a) every person who, before or during the campaign
period, directly or indirectly, by any other person
on his behalf, gives, lends or agrees to give or to
lend, or offers, promises, or promises to procure or
to endeavor to procure, any money or valuable
consideration to or for any voter or to or for any
person on behalf of any voter or to or for any other
person, in order to induce any voter to vote or to
refrain from voting, or corruptly does any such
act, on account of such voter having voted or
refrained from voting at any nomination process
or election;

Ni kweli Kikwete ametenda kosa,na sio kosa tu, ila kosa la jinai na hivyo hatua za kisheria yeye kama mgombea zinastahili kuchukuliwa dhidi yake,

Hii ni kutokana na ukweli ambao hata yeye mwenyewe hawezi kuupinga kwamba aliwaahidi wafanyakazi nyongeza ya mshahara, nyongeza ambayo haikuwa imejadiliwa awali wala kupitishwa na bunge kama inavyostahili!

Naomba tutofautishe kati ya ahadi za kawaida kwa jamii na ahadi au amri hii Kikwete aliyoitoa kule Mwanza kuhusu wafanyakazi, nyongeza hii kama ingetolewa na mgombea mwingine haingekuwa kosa kwani ingekuwa ni mwendelezo wa ILANI yao, au hata kama Kikwete angesema wanategemea kuongeza ingekuwa tofauti na ilivyotolewa, kwani tayari kulikuwa na mlolongo wa matukio kuhusu mshahara wa wafanyakazi hata kabla ya kampeni na serikali ya Kikwete kupitia maneno yake mwenyewe aliweka msimamo wake, sasa kosa liaanzia pale alipobadilisha msimamo wake na kuongeza mshahara huo wakati huu wa kampeni.

Ni wazi kuwa, mabadiliko hayo ya msimamo wa Kikwete umeletwa na nia ya kutaka kupata kura za wafanyakazi na hivyo hiyo ni rushwa ili apate kura!

Kosa hili la jinai alilolifanya Kikwete, halitakuwa kosa kama ataweza kuudhibitishia umma kuwa, nyongeza hiyo ya mshahara alikuwa ameshaifanya kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uteuzi kama sheria ilivyonukuliwa hapo chini!


"Section 21(3) For the purposes of this section an act or transaction
shall not be deemed to constitute prohibited practice if it is proved
to have been designed to advance the interests of community fund
raising, self-help, self-reliance or social welfare projects within
the constituency and to have been done before the nomination
process or election campaign, as the case may be."

Ila ni ngumu Kikwete kudhibitisha hilo kwani amenukuliwa zaidi ya mara mbili akiwaambia wafanyakazi kuwa nyongeza ya mshahara wanaoutaka haiwezekani. Kama hiyo haitoshi, japo mazungumzo kati ya serikali na TUKTA yalikuwa yanaendelea, mwenendo wa kiongozi wa TUKTA, Bw. Mgaya ulionesha wazi bado hawajakubaliana na maamuzi ya serikali, hivyo iweje leo Kikwete aseme kitu ambacho anaamini kitawaridhisha wafanyakazi kama kitu hicho sio zaidi ya kilichokuwepo kwenye mazungumzo kati ya TUKTA na serikali? Kuwa Kikwete ameivunja sheria na kifungu hicho kidogo cha tatu hakimsaiidii kwani, baada ya kutangaza nyongeza hiyo kule Kirumba, mara moja, Kiongozi wa TUKTA, Bw. Mgaya alimjibu kwa kumwambia AMECHELEWA, hii inamaana kwamba nyongeza hiyo sii ile iliyokuwa imejadiliwa na kufikiwa katika mazungumzo kwani laiti kama wangeiongeza mapema, basi ingekubaliwa. Hivyo Kikwete asijaribu kutumia kifungu hicho kidogo cha TATU!

Hata hivyo, kutokana na taasisi zetu(Haswa Msajili wa Vyama Vya Siasa na NEC) kuwa dhaifu na zenye upendeleo wa wazi, tunaamini kuwa Kikwete hatashughulikiwa ipasavyo na badala yake ukweli utapindishwa kwa kuwabeza watanzania hawaijui sheria hii mpya huku wabezaji wajitutumua kuwa ni manguli wa sheria haswa hii mpaya hivyo wao hawaoni kama Kikwete kakosea,

SISI TUNASEMA, hata kama vyombo husika havitachulua hatua stahiki, kosa hilo limeingia kwenye daftari la kumbukumbu na dhambi hii, na zingine nyingi, zitamtafuna KIkwete na wanaCCM wote na maswahiba wao wote kwa hujuma wanayoifanya kwa taifa hili hadi watakapoiingia kaburini!
 
Niliwahi kusoma mahali kwamba Small Minds discuss People halafu zingne zina-discuss events na zingine bora au kubwa zinadiscuss IDEAS, sasa tuwahurumie hao wanaomwona Slaa ni Padre, ni Mkatoliki baadae watamwona sio handsome, watagundua anakunywa pombe watasema mlevi, watamwona amechukua mke watasema sijui nini, lakini hawaoni kingine, wanaweza hata wakasema akivaa nguo hazimpendezi, ni small minds hawa,

tena mahali pengine waliandika usijibishane na mpungufu maana wote mtaonekana mapunguani, jamani!

Tafadhali sijibu hoja yako na slaa...huko mie siko.
Ila tu hiyo filosofi huwa siielewi kwani events zinafanya na watu that's why watu wanadiscuss watu...sielewi aliyeitunga alimaanisha nini kwani ni ngumu kujadili events bila kujadili wahusika...ni mtazamo wangu tu juu ya philosofi hii...I mean ni ngumu kidogo kutenganisha watu binafsi as agency na events au policy as structure kwa sababu zina affectiana to some extent
mix with yours
 
Hutuba ya bajeti ya mwaka 2010/11 [Wizara ya fedha]
55. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Nne inatambua umuhimu wa kuwa na maslahi bora ya wafanyakazi katika kuongeza ufanisi na tija. Serikali inachukua hatua za kuboresha maslahi ya wafanyakazi katika mwaka 2010/11. Sanjari na hatua hii, utaratibu wa kuhakiki mishahara utaendelea ili kudhibiti malipo kwa wafanyakazi hewa.

(ii) Kupunguza kiwango cha chini cha Kodi ya Mapato kwa wafanyakazi kutoka asilimia 15 hadi asilimia 14 sambamba na nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kitakachotangazwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma. Lengo ni kuwaongezea kipato na kuwapunguzia mzigo wa kodi watumishi wa umma wenye kipato cha chini;

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA:



44. Mheshimiwa Spika
mishahara ya Watumishi wa Umma itaongezwa kwa

kuzingatia makubaliano yaliyofikiwa katika Baraza la Majadiliano ya Pamoja Katika

Utumishi wa Umma. Serikali itaandaa mkakati wa utekelezaji wa Sera ya Malipo ya
Mishahara na Motisha Katika Utumishi wa Umma mara baada ya Sera hiyo
kupitishwa. Aidha, Serikali itakamilisha uanzishaji wa Bodi ya Maslahi na Tija katika




Utumishi wa Umma.



{Kamati ya kujadili bajeti ya wizara ya nchi, ofisi ya rais, menejimenti ya utumishi wa umma}
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani wakati nasoma hotuba yangu nimesema kwamba Serikali imekubali kuongeza kima cha chini sawa na makubaliano yetu na Vyama vya Wafanyakazi. Kwa kufanya hivyo Bajeti ya mishahara mwaka huu imeongezeka kwa shilingi bilioni 558 ukilinganisha na ya mwaka jana​

Tuambie wapi mishahara hajapitishwa na bunge?
Wewe ndio mbumbumbu kabisa mishahara haiongezwi hivyo hizo ulizobandika ni kauli za kisiasa. Mishahara inaongezwa kwa kamati maalum za bunge kukaa, kujadili na kupitisha figures ambacho ndicho anachodai Slaa kamati gani ya bunge ilikaa na kupitisha.

Utaratibu wa bunge wizara au kamati husika inapendekeza kiwango, kamati maalum ya bunge inakaa na inajadili na kujiridhisha, baada ya kujiridhisha inapeleka pendekezo hilo bungeni, bunge linapiga kura ya kulikubali au kulikataa hilo pendekezo huo ndio utaratibu si uliotubandikia eti bumge lilipitisha. Hayo matamko yanaweza kutolewa hata miaka miwili nyuma lakini lazima bunge lipige kura acha hizo wewe unakurupuka tu bila kuelewe kitu.
 
Wafanyakazi wa Tanzania hawako hivyo unavyowafikiria. Hawajui kugoma. Ni watiifu sana. Wengi wao wanaridhika sana anapopewa nafasi inayomwezesha kufanya ubadhirifu. Hawatamwelewa Dr Slaa hasa katika kipindi hiki ambacho CCM inaweza kucheza rafu yoyote ile ikiwemo hiyo nyongeza kinyemela ya mishahara. CCM wanajua marefa wote ni wao. NEC, RPP na vyombo vya DOLA.
Wafanyakazi ni watiifu kwa nani, hilo ni relative term sijui unamaanisha watiifu kwa TUCTA kwa Mwajiri(JK) au kwa Slaa. Ungeniambia ni waoga ningekuelewa lakini waone hivyo hivyo wanaakili sana hao unaweza kuwadanganya wakabaki wanakutizama na usijue wanafikiri nini.

Wengi wetu nafikiri hatujazielewa mbinu wanazotumia Chadema wanataka kuifanya CCM kazi yake iwe kujibu tuhuma counterattach na siyo kurusha makombora, kupeleka mashambulizi golini kwa mpinzani asipate pumzi wala upenyo wa kusogelea goli lako, ndicho Chadema inachokifanya.

Hata kama Msajili au NEC watatupilia mbali pingamizi tayari Chadema watakuwa wameacha damage kubwa kwa NEC, Msajili, CCM na JK mwenyewe, na umesikia Slaa alivyosema hata kama likitupiliwa mbali kama wengi tunavyotarajia Msajili afanye watasonga mbele hiyo tosha ni psychological torture kwa CCM ilitumiwa na CUF zanzibar kama utakumbuka.

Damage ninayoisema kwa NEC na Msajili ni kuonesha watanzania kuwa vyombo tulivyonavyo havifai ni double standard na damage kwa CCM na JK, Chadema wanataka kuonesha watanzania ni kwa kiwango gani sheria zetu zinavunjwa na mtu aliyeapa kuzilinda. Mimi nafikiri hilo ndilo lengo hasa la Chadema kwa vile najua na wao Chadema wanajua itakuwa ngumu sana pingamizi lao kupita.
 
Sasa nyie wasiwasi wa nini? Kama hajavunja sheria, Mahakama itaamua. Itajulikana kama alitoa hongo au laa.

Pia itabidi aseme, pesa ametoa wapi kama bunge halijaidhinisha.

Kazi mnayo mwaka huu......... Kwa mara ya kwanza CCM imeanza kujibu mashambulizi.

Na bado Slaa akianza kurusha mabomu yake 19. Moja limesharushwa.
 
Sasa nyie wasiwasi wa nini? Kama hajavunja sheria, Mahakama itaamua. Itajulikana kama alitoa hongo au laa.

Pia itabidi aseme, pesa ametoa wapi kama bunge halijaidhinisha.

Kazi mnayo mwaka huu......... Kwa mara ya kwanza CCM imeanza kujibu mashambulizi.

Na bado Slaa akianza kurusha mabomu yake 19. Moja limesharushwa.
Haya ndiyo mambo muhimu ya kuongolea, sheria zimevunjwa, pesa za umma kutumiaka bila utaratibu maalum. Masuala kama haya ndiyo yanayogusa moja kwa moja maslahi ya watanzania kuliko kuongelea personal issues za upadri wa Slaa ambao haunisaidii.
 
Nashawishika kuamini kuwa JK amekiuka sheria hii ambayo yeye mwenyewe aliisaini kwa mbwembwe nyingi akiamini kwamba itawabana wapinzani wake tu. Sasa tunataka kuona sheria ikichukua mkondo wake na aadhibiwe accordingly. Kinyume cha hapo tutaandaa maandamano makubwa ya nchi nzima kuikataa serikali hii dhalimu! Tunasubiri. Kitendo alichofanya ni RUSHWA ya waziwazi kabisa, na sasa Slaa amemshika pabaya.
 
Back
Top Bottom