Elections 2010 Dr. Slaa kumuwekea pingamizi Kikwete!

Elections 2010 Dr. Slaa kumuwekea pingamizi Kikwete!

Duh! Jamani sasa habari za chadema tutakuwa tunapata wapi maana naona kuna hatari tv zote zisitangaze hizi habari!! Nakumbuja ofisi ya AG kupitia TBC ilivyokanusha kikwete kufunguliwa kesi ya kupingwa kugombea urais, japo haikutoa maelezo mengi ila walikataa kabisa kuwa hamna kitu cha namna hiyo lakini ukweli kesi ipo na walitaka itupiliwe mbali japo mahakama imekataa! Naona hakuna habari za chadema tutakazo sikia. Chanel ten wameshaanza tayari kwenye taarifa yao kulikuwa na habari za kampeni za kikwete na malalamiko ya makamba nikajua chadema bado wanakula fungate kumbe leo walikuwa moro, napingamizi limewekwa!! Chadema plz tunahitaji altenative hapa hali itakuwa mbaya!

Nipo kwenye msafara i will keep you posted.otherwise contact Ngurumo
 
wakuu wana CHADEMA, kudos kwa kuona mbali ... strategies hizi lazima ccm wataachia ...
 
One step at a time wazee nchi tutaikomboa tu! Swala kubwa ni kuwapa presure nec, msajili na ccm wabanane kwani tunajua hatima ya uamuzi nec watakao toa but this will give chadema kuonyesha kwa wananchi jinsi tume ya uchaguzi ilivyo bias na wananch wataamua
 
Kama kawaida,Tendwa atawatetea mabosi wake wanaomweka mjini (CCM). CHADEMA inaonesha ukomavu wa kidemokrasia.
 
Sasa Tunasubiri Blah Blah zao.....Kama Mgombea binafsi ilivyokuwa au walivyoizima Richmond na walivyoimeza/Kumbatia KAGODA....
 
Ya; nimeona ukombozi unakuja maana watapiga kelele mpaka watachoka; BIG UP CHADEMA kwani unaishi kwa maneno ya kweli
 
Je, hiyo mishahara ilitangazwa lini mara ya kwanza kuongezwa?

Je, makamba hakutoa tamko kuwa safari hii ya uchaguzi mkuu ccm itatumia helikopta?
 
naomba kujua kama nikweli shitambala amekabidhi kadi ya chadema kwa j k leo huko mbalizi
kwa mujibu wa tbc taiafa habari saa 2 usiku
 
naomba kujua kama nikweli shitambala amekabidhi kadi ya chadema kwa j k leo huko mbalizi
kwa mujibu wa tbc taiafa habari saa 2 usiku

liganga4

user-online.png
Junior Member

reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join Date : Sun Aug 2010
Posts 2
Thanks : 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
 
huko ni kupoteza muda wenu wa kampeni na pesa. pole Chadema
 
Mgombea wa CCM kwenye kiti cha urais, Mh JM Kikwete amewekewa pingamizi na Chama cha Demokrasia na maendeleo kwa kukiuka sheria aliyoisaini yeye mwenyewe. Imedaiwa kuwa ameongeza mishahara kwa wafanyakazi kinyume na taratibu za nchi kitu ambacho kisheria kinaonekana ni rushwa. Kwahiyo CHADEMA wamepeleka malalamiko yao kwa tume ya uchaguzi wakiomba jina lake lienguliwe kwenye mbio za kuwania uras wa JMT. Je kweli Tendwa ataweza kusimamia haki?
Sungura


Chadema wanatakiwa wapige kampeni na si kulialia. Hii ni dalili ya kushindwa kabla ya mchezo.
 
Mgombea wa CCM kwenye kiti cha urais, Mh JM Kikwete amewekewa pingamizi na Chama cha Demokrasia na maendeleo kwa kukiuka sheria aliyoisaini yeye mwenyewe. Imedaiwa kuwa ameongeza mishahara kwa wafanyakazi kinyume na taratibu za nchi kitu ambacho kisheria kinaonekana ni rushwa. Kwahiyo CHADEMA wamepeleka malalamiko yao kwa tume ya uchaguzi wakiomba jina lake lienguliwe kwenye mbio za kuwania uras wa JMT. Je kweli Tendwa ataweza kusimamia haki?
Sungura

Jaji Tendwa hawezi kuchukua hatua yoyte dhidi ya CCM. Taarifa nilizopata, baada ya kuvuruga kazi katika moja ya mahakama alizokabidhiwa kuiongoza, walimtema. Ikabidi ahamie kijijini maeneo ya Temboni Kimara.

Ili kupata kzi aliyonayo ilibidi atoe Takrima ya Whisky za aina mbali mbali kwa Mhe Bakari Mwapachu, Mbunge wa Tanga na Waziri wa Wizara ya Sheria wa Serikali ya Benjamin Mkapa ndipo akateuliwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Mara tu alipoteuliwa akahama Temboni na kuhamia Oystebay na kumilikishwa nyumba ya Serikali na utawala wa Mkapa.

Sasa nasikia karejea Temboni, baada ya kupangisha nyumba ya Serikali aliyokatiwa kama fungu lake.

Je kwa msingi huo ataweza kuchukua hatuayoyote dhidi ya Kikwete na CCM. Naye ni FISADI TUU. Hakuna jipya, hawezi kumwambia Kikwete chochote.

Taarifa nilizo nazo hastahili kuitwa Judge, naomba wadau mnihabarishe
 
Hii sio kulialia, without reference kama hizi one can not build his/her case of injustice. Usisahasau reference kama hizi huwa zinatunzwa kwa ajili ya vizazi vijavyo na wanafunzi wa vyuo vikuu.

Hivyo ni kutokuwajibuika kuacha kuchukua administrative procedures kama hivi kwa viongozi wa public instuitution kama CHADEMA. Nashukuru kutambua uwezo wako wa kufikiri.
 
Source please..!

Geofrey Nyang’oro

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeteketeza azma yake ya kumwekea pingamizi mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.

Taarifa zimeeleza kuwa chama hicho kiliwasilisha pingamizi hilo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini jana saa 7:30 mchana.

Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika, ndiye aliyewasilisha pingamizi hilo.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa alipoulizwa hakutaka kukubali au kukataa kuliona pingamizi hilo na akasema atazungumzia suala hilo leo.

Awali Chadema ilipanga kuweka pingamizi hilo la kutaka Kikwete azuiwe kugombea urais, Agosti 27 mwaka huu, lakini, ilisitisha kwa kile ilichoeleza kuwa inasubiri mambo mengi zaidi ambayo wangeyaingiza kwenye pingamizi hilo.

Chama hicho awali kilitaka kuweka pingamizi hilo kwa kile kilichoeleza kuwa Rais Kikwete amekiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa kutangaza nyongeza ya mishahara ya wafanyakazi kwenye kampeni.

"Tulishindwa kupeleka pingamizi hilo jana kwa sababu tumesikia kwamba huku anakoendelea na kampeni zake, mgombea huyo ameendelea kufanya makosa mengine ambayo tutataka tuyaingize kwenye pingamizi hilo," alisema Mnyika mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na gazeti hili jana muda mfupi baada ya kuwasilisha pingamizi hilo, Mnyika alibainisha kuwa mambo mengine mapya yaliyoingizwa kwenye pingamizi hilo ni mgombea huyo wa CCM kuahidi kukilipia Chama cha Ushirika cha Nyanza deni la Sh 5 bilioni na kuahidi kununua meli kwa ajili ya watu wa mikoa ya Kagera na Mwanza.

Mnyika alisema tayari Chadema imewasilisha pingamizi hilo jana lakini, ina mashaka kama ofisi ya msajili itawatendea haki.

“Sisi tumeshawasilisha pingamizi letu kwa msajili wa vyama vya siasa kama Sheria ya Gharama za Uchaguzi zinavyoelekeza, lakini, tuna tumaini lenye shaka ndani yake kama tutatendewa haki,”alisema Mnyika na kuongeza.

“Mheshimiwa Kikwete wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi, moja kwa moja akitumia nafasi yake kama rais, ameongeza na /au kuahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa kupandisha kima cha chini kutoka Sh130,000 hadi Sh235,000,”inasema sehemu ya kwanza ya pingamizi hilo lenye sehemu tatu.

Katika pingamizi hilo, Chadema pia ilieleza kuwa mgombea huyo wa CCM, ameahidi kutoa Sh5 bilioni kwa chama cha Ushirika cha Nyanza ili kilipe madeni yake mbalimbali na kuahidi kuwa serikali itachukua madeni yote ya vyama vya ushirika.

Chadema pia imesema katika sehemu ya tatu ya pingamizi hilo kuwa mgombea Kikwete alitumia nafasi yake kwa kuwaahidi watu wa mkoa wa Kagera kuwa atawanunulia Meli mpya, kubwa na ya kisasa.

"Ahadi hizo ni sehemu ya mambo yaliyokatazwa kwa mujibu wa kifungu cha 21 (1) (a) na (e) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi namba 6 ya mwaka 2010," imeendelea sehemu ya pingamizi hilo.

Mnyika alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria hiyo, vitendo hivyo vilikuwa na nia ya kushawishi wapigakura wampigie kura mgombea huyo wa CCM.

Kuhusu ahadi ya kuchukua madeni ya Chama cha Ushirika cha Nyanza, alisema kitendo hicho nacho kililenga kuwashawishi wananchi wa Mkoa wa Mwanza kumpigia kura.

“Nyongeza ya mishahara, ahadi ya Sh5 bilioni na ahadi ya meli kutumika kama hongo/rushwa kwa hao wote wahusika ili wampigie kura Kikwete," alisema Mnyika na kueleza kifungu kinachozuia mambo hayo kuwa kinasema:

"Mgombea yeyote ambaye yeye mwenyewe, wakala wake au chama chake kitafanya kitendo ambacho kimekatazwa na kama ilivyoelezwa katika sehemu hii, atakuwa, au, kitakuwa kimepoteza sifa za kushiriki katika mchakato wa uteuzi na uchaguzi.”

Wakati huo huo, mgombea urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemshukia Meneja wa Kamati ya Kampeni CCM, Abdulrahman Kinana na kumtaka anyamaze kwani katika orodha ya uchafu wa watuhumiwa wa ufisadi nchini hatoki.

Juzi Kinana aliwaambia waandishi wa habari kwamba, Dk Slaa anawadanganya wananchi kuhusu suala la ufisadi na kumtaka aache kufanya hivyo na anadi sera zake.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara katika Jimbo la Mikumi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro jana, Dk Slaa alisema fisadi ni fisadi tu na hana njia nyingine ya kumpamba kwa maneno mazuri mtu anayeiba mali za umma.

“Namuonya Kinana anyamaze, nisije nikamshukia kwa sababu katika orodha ya wana-CCM waliofanya uchafu hatoki kupitia kampuni zake,” alisema Dk Slaa.

Dk Slaa alimgeukia Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo kwamba pamoja na cheo chake cha uwaziri na ubunge katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, lakini wilaya yake ni moja kati ya tano zilizopata orodha chafu sana .

Dk Slaa anaendelea ziara zake za kampeni na leo anatarajia kufanya mikutano kadhaa katika mkoa wa Dodoma kwa kutumia usafiri wa helikopta.

Source: Mwananchi.

Ulitaka source hiyo!!!!
 
Thanx Mdondoaji. Mimi source yangu ilikuwa reliable lakini verbal source kutoka kwa mtu anayefuatlia mambo hayo kwa karibu ...sikuwa na sababu ya kuexpose jina lake hapa kwa ajili ya usalama wake.. Tuko pamoja mkuu. Sungura
 
nyinyi hamna lolote, maneno yenu humu tu, lakini kwenye uwanja wa mapambano watupu.

na ndio maaana viongozi wenu hawaelewani, na wengine wanaaacha jahazi liende mrama na kurudi CCM.



Chadema inayoongozwa na mkuu wa WAPUKI na ukabila uliosheheni kamwe hakiwezi kuiongoza Tanzania.


chama gani kilichojikita baadhi ya sehemu tu, hata kwenye Nchi ya zanzibar ambayo nimshirika wa Muungano hakijulikani
 
CHADEMA jamani hawana sera na hawajiamini pamoja na mabomu yao yote hayo.
Wanataraji huruma ya Tendwa.Kosa ni la kwao wenyewe kuweka mgombea asiye na elimu inayohitajiwa na watanzania wa sasa.Mgombea wao hakubaliki kabisa hasa miongoni mwa jamii ya waislamu.
Wanalilia na huruma ya Mungu.Ati Kikwete afe,vipi nyinyi!.Kuumwa si kufa.Safari ya Dkt Slaa ni ndefu.Hata ikitokea dharura basi si Chadema watakaochukua nchi bali ni CUF.
 
Jana Kinana alipoulizwa kwa nini hoja za CUF mpaka leo hawajazijibu akasema kuwa wanazifanyia utafiti. Hii inaonyesha jinsi CHADEMA wanavyowatia kiwewe kiasi cha kukosa subira ya kutafakari na badala yake kuja na kisingizio cha "Wanatumia Lugha isiyo ya Kistaarabu".
bila

Hiyo lugha ya kistaarabu ndo imefanya watanzania tumeibiwa kwa miaka mingi sana..

Hiyo lugha haijatusaidia so long yanayosemwa ni ya ukweli...Haya ni mapambano dhidi ya MAFISADI ccm:cheer2:
I wapi kauli ya ccm kuwa CHADEMA ni moto wa mabua?
Huo ni mwanzo tu jamani....Tuko kikazi zaidi
 
Back
Top Bottom