Dr Slaa na Dharau kwa Chuo Kikuu cha Mlimani (UDSM)

Dr Slaa na Dharau kwa Chuo Kikuu cha Mlimani (UDSM)

Acha upumba.vu dogo Udom inaingiaje hapa? Kaanzishe thread ya kuijadili udom sio kujitia kujua kwinhi apa...

Haa haa dogo kumbe upo vp kampango kenu na yule mshamba mwenzako kakutaka yule mbunge wa viti maalum-Iringa CCM awatafutie ajira. Madogo ninyi wajinga sana
 
Dr Slaa.,Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameonyesha dharau kubwa na kukosa kwake imani kwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam maarufu kama UDSM juu ya kiwango cha Elimu kinachotolewa chuoni hapo. Kadhia hiyo imetokea pale Dr Slaa alipokuwa anajibu Post ya Mwigulu Madelu Nchemba Naibu Katibu Mkuu wa CCM ambapo Dr Slaa alisema kuwa kulingana na kauli za Mwigulu anazozitoa ni zao la Elimu aliyoipata chuoni hapo ambapo Mwigulu alipata ufaulu wa first class chuoni hapo...


Je maneno haya ya Dr Slaa yanaukweli wowote kuwa chuo hiko kinatoa mazao yasiyofaa na kwamba anayoyasema na kuyafanya mwigulu yanatokana na Elimu yake aliyoipata Chuoni hapo..???

Ujue kuna kauli na mambo anayoyafanya huyu kiumbe mwingulu mpaka mtu unashindwa kuwa na imani na elimu yake!
 
Dr Slaa.,Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameonyesha dharau kubwa na kukosa kwake imani kwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam maarufu kama UDSM juu ya kiwango cha Elimu kinachotolewa chuoni hapo. Kadhia hiyo imetokea pale Dr Slaa alipokuwa anajibu Post ya Mwigulu Madelu Nchemba Naibu Katibu Mkuu wa CCM ambapo Dr Slaa alisema kuwa kulingana na kauli za Mwigulu anazozitoa ni zao la Elimu aliyoipata chuoni hapo ambapo Mwigulu alipata ufaulu wa first class chuoni hapo...
sina hakika Kama Mwigulu aliwahi kujifunza kitu kinachoitwa logic katika maisha yake. Kuelewa kuwa Kaulinzako zinajikanyaga huhitaji sana kwenda shule kubwa kubwa, unless mnatuambia Chuo Kikuu kilichompa Degree ni hovyo kiasi hicho

Je maneno haya ya Dr Slaa yanaukweli wowote kuwa chuo hiko kinatoa mazao yasiyofaa na kwamba anayoyasema na kuyafanya mwigulu yanatokana na Elimu yake aliyoipata Chuoni hapo..???

Dr.Slaa wala hajakidharau chuo, bali wewe na huyo Mwigulu ndio mnakidharaulisha chuo. Kama mtu umeenda shule mpaka umefika kidato cha pili halafu hujui maana ya neno UNLESS, hivi tuiiteje shule uliyosoma?
 
UDSM si tatizo: tatizo ni mtu mwenyewe binafsi, kama mtu ni kichwa maji hata apige shule Havard hawezi kubadilika!
 
Mbona kama una ka wivu vile, walikupiga chini nini?

haha....hapo ndipo fikra zako zilipoishia.Kujilinda kwa "accusations na kuplay victim" kila kitu mnakizua kisisemwe kwa kisingizio cha wivu
 
Duh huyu jamaa kwanini aliasi upadri?

kwa sababu alikuwa mkweli ..huwezi watumiki mabwana wawili...ama kukomboa kondoo kupitia kanisa ama kukomboa taifa kupitia siasa.

Na hakuasi kwa vile alifuata exit doors kwa taratibu za kanisa..kuasi ni kujitoa kichume cha sheria.
 
Dr.Slaa hapo amezungumzia neno moja tu muhimu "Logic"ambalo linampita kushoto Mwigulu mpaka mleta mada ameshindwa kung'amua, yeye ameng'ang'ania chuo.

Wala siyo bahati mbaya. Hivyo ndivyo CCM wote walivyo. Huwa hawana muda wa kudiscuss point ya msingi, wenyewe wanarukia kujadili vibwagizo vya point. Dr. Slaa aliposema kama Kikwete hachukui serious measures dhidi ya uvunjifu wa sheria unaoendelea, nchi haitatawalika, wao waliacha kujadili hali ya uvunjifu wa sheria ambao Kikwete amepuuza na kukimbilia kujadili nchi haitatawalika.

Juzi Mbowe kasema chadema tunaonewa sana kwa hiyo tutaimarisha kikosi chetu cha ulinzi, rais, polis na hadi msajili wa vyama wamekurupuka utafikiri wamekurupushwa na nyoka shimoni na kutoa matamko kibao ya kuponda mpango wa CHADEMA tena kwa kugeuza kabisa na maana halisi ya kile ambacho chadema ilitangaza kukifanya. Hao ndiyo CCM. Halafu tumewapa dhamana ya kuongoza nchi. Fikiri kama hata katika sentensi aliyoifanyia quotation haelewi ina maana gani, sasa utajiuliza watu wa aina hii wanapokwenda kujaza mikataba huwa wanajaza nini? No wonder nchi ina kila aina ya resources lakini bado ni maskini ya kutupwa.
 
haha....hapo ndipo fikra zako zilipoishia.Kujilinda kwa "accusations na kuplay victim" kila kitu mnakizua kisisemwe kwa kisingizio cha wivu


hapana ni reasonable doubt ,wemgi wa wanaokipaka matope udsm

1)wame disco

2)wameikosa nafsi points zilikuwa almost zitoshe

3) wivu
 
Hapa ndipo tunapojikuta pamoja na utajiri wote wa nchi yetu bado tuko masikini. Tatizo kubwa ni kukataa kujikosoa ama kukosolewa. Hivi anahitajika Dr Slaa kusema kwamba VYUO VYETU na wala sio chuo cha UDSM peke yake, ni vijiwe vya kuzalisha uharo? tazama soko la ajira linajibu vipi huko, ni nani anayeajiri mtu wa chuo cha ndani kama sio wale tu wenye network za ma god father? stupid argument kabisa tena bora hata wakati wa Mwigula labda walikua wanatoka kinafuu kidogo, hebu angalia nani anayeajiri hizo takataka? ni aibu kabisa ku standardize matokeo kwa lengo la kuwahadaa wananchi ili kumlinda home boy Kawambwa. Watanzania sijui tumelaaniwa na nani? mpaka tukorogewe mavi kwenye chungu na kulishwa kwa kijiko bado tutasema asante hiki chakula chetu kitamu sana, angalia the so called walimu wa udsm hata ukiwakuta kwenye mikutano, labda wale wa engineering na kule economics wana tofauti hao wengine choka mbaya, vijana wa jana wamebebwa kwa ukabila na udini ndio wana GPA za kuua hata sentensi moja yenye akili ya kiswahili hawawezi kuitunga. Pelekeni watoto wenu India elimu bei nafuu achaneni na hawa, angalia average time mwanafunzi wa chuo anatumia on the streets kutafuta kazi so far ni 5 years, kama anachosema slaa ni uongo kwa nini wasikimbiliwe na waajiri wakati tunasema mnadai kuna maimilioni ya kazi zilizozalishwa na rais wenu Dhaifu. Nani asiyejua hata Ridhiwani Kikweni alifeli somo raisi kama Sheria, na kupewa na Jaji Juma aliyeishia kuhongwa ujaji leo hii, sasa muonenei leo hii eti wakili ambaye hajawahi kusikiliza kesi Imma walimtumia wakimtuma kupeleka mafailia wizara ya ardhi, tusijidanganye tunaficha ugonjwa kifo kinatuumbua sasa, vijana wetu hawaajiriki
 
Hawa watu wanadharau kila kitu, mwisho watajidharau wenyewe

Wamedharau jeshi la polisi

Wamedharau Jeshi la wananchi

Wamedharau watendaji wote serikalini, hii ikiwa na maana hata walimu

Na sasa wanadharau vyuo vyetu

sasa kwanini watu wa aina yako wasidharauliwe.....
 
dr ni mtanzania ameongea vizuri ila nashangaa watu wanaquote vijimaneno na kuacha lile point of view, lingine udsm will remain the place to be forever.siku nyingine mada hizi za kiumbea pelekeni bamaga kwa shigongo ndio ugali wake.
 
we jamaa mleta uzi unakera kinyama, kwa nini hukuikosoa kauli ya pinda, unajifanya ng'weeh ng'weeh, nyie vijana wa aina hii mnaoendeshwa na mahaba ya siasa ni janga kwa taifa hili! You are just wasting the money of the tax payers, this nation is very unlucky to have the youths of your type!
 
Sitaji kujiingiza kwenye marumbano ya Dr.Slaa na Mwigulu Nchemba lakini hoja yako hii inagota palepale kwenye point aliyokuwa anaisema Dr.Slaa kuhusu somo la LOGIC.

Kabla ya kuleta bandiko lako ulitakiwa kwanza ukipambanue ki-logic hicho alichokisema Mwigulu Nchemba na kukiona kama ni ukweli au siyo ukweli.

Kama alichokisema Mwigulu ni kweli basi hoja ya Dr. Slaa inakuwa ni worthless kuijengea hoja, lakini kama siyo kweli, basi ndipo ungekuja na hoja ya maneno ya Dr.Slaa kutaka yachambuliwe na wanaJF.

So far, kwa kuleta hoja inaonekana unakubaliana na hoja ya Dr. Slaa kwa yale aliyoyasema Mwigulu Nchemba na kwa maana hiyo yatakuwa yamechangiwa na elimu aliyoipata pale UDSM.

Sasa sijui unataka tujadili nini wakati kile alichokisema Dr. Slaa unakubaliana nacho.

Kwani hufahamu kuwa Mwigulu aliongeza elimu na maalifa zaidi pale UDSM na kutunukiwa cheti baada ya kufaulu. Huoni kuwa hoja zake anazijenga kutokana na kupata elimu na maalifa zaidi hapo UDSM.

Point noted.
 
Back
Top Bottom