DRC iwaangukie "mabeberu" wakubwa wa Magharibi kumaliza vita nchini kwake, mabeberu wanahitaji kubembelezwa kidogo tu na kuheshimiwa kumaliza mgogoro

DRC iwaangukie "mabeberu" wakubwa wa Magharibi kumaliza vita nchini kwake, mabeberu wanahitaji kubembelezwa kidogo tu na kuheshimiwa kumaliza mgogoro

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Vita vya muda mrefu na ukosefu wa amani mashariki mwa Congo(DRC) nyakati hizi kwa kiasi kikubwa vinachangiwa na udhaifu wa dola ya DRC kudhibiti nchi pamoja biashara ya madini adimu mbalilmbali yenye mahitaji makubwa duniani kwa sasa. Baada ya Waafrika wenyewe kuushindwa huo mgogoro bila shaka mwenye uvumbuzi wa haya matatizo aliyebaki ni "beberu" Marekani na wenzake wa Ulaya kwa sababu wao ndio wanaoshikilia mpini wa mfumo wa fedha ulimwenguni kwa sasa na ndio wenye uwezo ya kumdhibiti jirani au majirani wanaodaiwa kujinufaisha pia na huo mgogoro.

DRC iwaangukie hawa mabeberu kuiponya nchi yao. SADC, EAC na AU watulie tu wasitoe milio ya kuingiliwa na mabeberu wazee wa kazi watakapoingia mzigoni, zaidi wawape ushirikiano mkamilifu. Pia Wazalendo uchwara waache kelele za kusema West ndio wanawapa silaha waasi kwa sababu ni kuwavunjia heshima "mabeberu" wenye ufunguo wa mgogoro wakati hata hizo tuhuma zenyewe zinaweza kuwa sio za kweli au hazithibitishiki.

Wanachohitaji mabeberu ni sabubu nzito za maslahi ili kuhusika kikamilifu kuumaliza huo mgogoro. DRC wao watalipia gharama kwa kuwapa mabeberu mikataba exclusive na minono ya miaka 30 ya madini adimu na muhimu, faida igawanywe pasu kwa pasu 50/50 kati ya Congo na Mabeberu.
 
Kinachotakiwa Congo ni Dialogue sio mtutu,Dialogue baina ya Mwafrika kwa Mwafrika.
 
Hao wanajua fika kinachotokea Congo kwa kuwa wanakiratibu wao
Media zao zinaongelea hii habari sasa hivi kama breaking news kwa marudio 24/7, lakini hakuna mmoja kajitokeza kusema kitu..
 
Acha kujitoa ufahamu hao ulio wataja ndo wanao endesha mgogoro kwa kujificha nyuma ya mgongo wa kagame.
Nadhani ungesema hivi ,serikali ya Kongo iwagawie hayo madini bure ili wasirazimike kuanzisha makundi ya waasi kuyapora.
 
Kinachotakiwa Congo ni Dialogue sio mtutu,Dialogue baina ya Mwafrika kwa Mwafrika.
CIA wapo mzigoni nyie,hii vita haiishi as long yale madini yapo sehemu zote zenye malighafi wamepatibua ili wabebe kirahisi,it’s their strategy to sell weapons as well kwakua ndio nchi inaongoza Kwa viwanda vya silaha
 
Acha kujitoa ufahamu hao ulio wataja ndo wanao endesha mgogoro kwa kujificha nyuma ya mgongo wa kagame.
Nadhani ungesema hivi ,serikali ya Kongo iwagawie hayo madini bure ili wasirazimike kuanzisha makundi ya waasi kuyapora.
Serikali ya DRC ni ya kizalendo sana kuliko zote Africa kiasi cha kuzuia madini yake kupatikana kwa amani kwa mikataba hadi mabeberu wakaanzisha makundi ya uasi ?
 
CIA wapo mzigoni nyie,hii vita haiishi as long yale madini yapo sehemu zote zenye malighafi wamepatibua ili wabebe kirahisi,it’s their strategy to sell weapons as well kwakua ndio nchi inaongoza Kwa viwanda vya silaha
Ni rahisi kubeba madini katika nchi ya vita kuliko ya amani?
 
Tshekedi anatakiwa amwombe Putin tu awasambaratishe tu hao waasi .lkini kwamataifa ya magharibi ningumu mnooo.russia Hana urafi huo warasilimali
 
Njia ya amani hawapati faida. Hapo wanapta madini na soko la silaha
Mbona makampuni ya mafuta na gas ya Marekani yako Saudi Arabia na Qatar na silaha wanawauzia pia kama wateja wao wakubwa zaidi?

Mbona sisi pia tunanua silaha kwa mabeberu ?
 
Suluhisho la DRC na kugawanya nchi tu. Hizo kivu ziwe nchi zinazojitegemea. Katanga nchi, Maniema nchi nk nk. Watu wako nchi moja lakini hawawezi kuelewana kwa Lugha. Mtu wa Kinshansa, Mbuyi Mayi na Goma wakikaa wanaweza wasielewane kabisa.
 
Suluhisho la DRC na kugawanya nchi tu. Hizo kivu ziwe nchi zinazojitegemea. Katanga nchi, Maniema nchi nk nk. Watu wako nchi moja lakini hawawezi kuelewana kwa Lugha. Mtu wa Kinshansa, Mbuyi Mayi na Goma wakikaa wanaweza wasielewane kabisa.
Hili nalo ni suluhisho pia japo kuna faida nyingi kuliko hasara za kuwa nchi kubwa,
 
Vita vya muda mrefu na ukosefu wa amani mashariki mwa Congo(DRC) nyakati hizi kwa kiasi kikubwa vinachangiwa na udhaifu wa dola ya DRC kudhibiti nchi pamoja biashara ya madini adimu mbalilmbali yenye mahitaji makubwa duniani kwa sasa. Baada ya Waafrika wenyewe kuushindwa huo mgogoro bila shaka mwenye uvumbuzi wa haya matatizo aliyebaki ni "beberu" Marekani na wenzake wa Ulaya kwa sababu wao ndio wanaoshikilia mpini wa mfumo wa fedha ulimwenguni kwa sasa na ndio wenye uwezo ya kumdhibiti jirani au majirani wanaodaiwa kujinufaisha pia na huo mgogoro.

DRC iwaangukie hawa mabeberu kuiponya nchi yao. SADC, EAC na AU watulie tu wasitoe milio ya kuingiliwa na mabeberu wazee wa kazi watakapoingia mzigoni, zaidi wawape ushirikiano mkamilifu. Pia Wazalendo uchwara waache kelele za kusema West ndio wanawapa silaha waasi kwa sababu ni kuwavunjia heshima "mabeberu" wenye ufunguo wa mgogoro wakati hata hizo tuhuma zenyewe zinaweza kuwa sio za kweli au hazithibitishiki.

Wanachohitaji mabeberu ni sabubu nzito za maslahi ili kuhusika kikamilifu kuumaliza huo mgogoro. DRC wao watalipia gharama kwa kuwapa mabeberu mikataba exclusive na minono ya miaka 30 ya madini adimu na muhimu, faida igawanywe pasu kwa pasu 50/50 kati ya Congo na Mabeberu.
DRC inatakiwa kuwapa usawa jamii zote za Wakongomani bila kubagua
 
CIA wapo mzigoni nyie,hii vita haiishi as long yale madini yapo sehemu zote zenye malighafi wamepatibua ili wabebe kirahisi,it’s their strategy to sell weapons as well kwakua ndio nchi inaongoza Kwa viwanda vya silaha
Hizo ni Propaganda.
 
Hao hao ndio wahusika Wa hayo machafuko, wanatumia machafuko nchi isitulie wapate kuiba madini ya kwenda kutengenezea simu laptop na magari ya umeme , washenzi tu hao
 
Back
Top Bottom