DStv badilisheni mtangazaji na utangazaji wa Kiswahili kwenye mechi za Kombe la Dunia

DStv badilisheni mtangazaji na utangazaji wa Kiswahili kwenye mechi za Kombe la Dunia

Kiukweli hawa watangazaji wa kiswahili wa DSTV wanaboa mnoo.
Mapungufu makubwa niliyoyaona.

1. Mtangazaji anakuwa nyuma ya tukio, sisi tunaona tukio kwanza (goli au kosa kosa) halafu mtangazaji ndio anaibuka kusema kwa makeke wakati tukio limepita kwa nusu sekunde. Hiyo kitu inaboa sana. Nadhani ni kwa sababu watangazaji hawako live uwanjani, wanafuatilia sambamba na sisi tunaoangalia kwa Tv, hivyo sauti zao zitachelewa kidogo.

2. Hawako katika uhalisia kabisa, hususani huu utangazaji wa Maulid Kitenge (umejaa mbwembwe zisizo na maana) au ule kina Kibwana (wa Clouds Fm) ambao umejaa blah blah za kuiga uzungu, afadhali hata ule utangazaji wa option nyingine ya kiswahili (sijui jamaa wa RTD wale) ambao umekaa kiuhalisia kiasi.


Binafsi mpaka sasa watangazaji wa kiswahili wa Azam Tv kwenye ligi ya ujerumani ndio nawaelewa vizuri. Wale jamaa nawaelewa sana.
Suala la Mtangazaji kuwa nyuma ya tukio hata mimi nimeliona ila tatizo ni kutokana na kwamba mtangazaji mwenyewe yuko Dar na yeye anaangalia kwa kutumia screen kama wewe unavyoangalia nyumbani kwako alafu inafanyika Sound exchange inazimwa ya mtangazaji wa kiingereza alafu anazungumza yeye kwa kiswahili kisha inarushwa sasa lazima tukio litangulie halafu sauti ndyo ifuate au sauti itangulie halafu tukio ndio lifuate
 
Mtangazaji wa hovyo anamizuka ya kijinga utadhani mtazamaji kumbe ni mtangazaji.

Makelele kama maulid kitenge hayafai kwenye channel tulivu kama zile. Yan nalipia king'amuzi 56k afu napigiwa mayowe badala ya kutabgaziwa burudani
 
Suala la Mtangazaji kuwa nyuma ya tukio hata mimi nimeliona ila tatizo ni kutokana na kwamba mtangazaji mwenyewe yuko Dar na yeye anaangalia kwa kutumia screen kama wewe unavyoangalia nyumbani kwako alafu inafanyika Sound exchange inazimwa ya mtangazaji wa kiingereza alafu anazungumza yeye kwa kiswahili kisha inarushwa sasa lazima tukio litangulie halafu sauti ndyo ifuate au sauti itangulie halafu tukio ndio lifuate
DStv ni brand kubwa sana. Wanachofanya ni kitendo cha kipuuzi hasa ukizingatia tunalipia zaidi ya elfu hamsini.
 
DStv ni brand kubwa sana. Wanachofanya ni kitendo cha kipuuzi hasa ukizingatia tunalipia zaidi ya elfu hamsini.
Walichopaswa kufanya DSTV ni kupeleka mtangazaji Quatar akae kwenye vile vyumba maalum vya watangazaji ili sauti iambatane Moja kwa moja na picha na akijaribu tu kupiga Mayowe wenzake wanamnyamazisha.[emoji23][emoji23]
 
Hahaaaa
Walichopaswa kufanya DSTV ni kupeleka mtangazaji Quatar akae kwenye vile vyumba maalum vya watangazaji ili sauti iambatane Moja kwa moja na picha na akijaribu tu kupiga Mayowe wenzake wanamnyamazisha.[emoji23][emoji23]
 
Kingereza ndo lugha gani hiyo wadau mimi sijawai isikia kabisa.naifurahia kiswahili lugha ya Baba zangu enzi na enzi
 
We unasema ivi...jana kwenye mechi ya saa moja nilikua hoi. Watangazaji walianza kupiga story binafsi. Yani mchezaji kafika kwenye box wao wanapiga story personal. Hasa Maulid siku akiwepo shughuli. Yeye anawarusha watu hewani tu na kusoma message zao....mpira hana muda nao
 
Tatizo la watangazaji wa kiswahili wanafanya kazi kwa mazoea, na sio wataalamu

1. Hawana data!
ukisikiliza matangazo ya wazungu huwa wanatoa data za timu na wachezaji
unaeza pata darasa tosha la mpira
watakuambia rekodi ya timu ya mechi zilizopita
watakupa data za mchezaji mmoja mmoja mfano; idadi ya magoli, club anayocheza, historia yake nk
watakupa uchambuzi juu ya kocha na vikorombwezo vingi vingi vinavokupa burudani

mbongo utasikia tu mbungi inawekwa kati piga moja refuuu kule anapokea namba 23
naona mabaliko namba 10 anatoka anaingia namba 19....utopolo mtupu

hwafanyi research ya timu wanazoenda kutangaza, hata majina ya wachezaji hawayajui wanataja namba

2. Hawana lugha nzuri za kutangaza, zaidi ya kelele za kosakosa na mara chache hukaa kimya bila maneno!
wanajisahau sana
 
Huyu mtangazaji wenu anapayukapayuka na hata haieleweki anaongea nini. Kila wakati anapaza sauti na kuongea vitu visivyoeleweka wala kuhusiana na mechi iliyopo mubashara.
Maulidi kitenge ni mduwanzi Dstv mmekosea sana kumpanga kutangaza mechi za kombe la dunia huyo chizi.
 
Mimi nimeamua ni rudi kwenye comentetor wa kiingereza hao waswahili wenzagu siwawezi kelele tupu stori kujifanya ni wachambuzi, mswahili ni mswahili siku zote hata umpeleke ulaya
Tatizo la waafrika ni janja janja tu wakati hizo ni taaluma za watu wamesomea tena kww kiwango cha juu kabisa,,hapa ukiwa na maneno mengi tu tayari kina MBWIGA WA MBWIGUKE.
 
Tatizo la watangazaji wa kiswahili wanafanya kazi kwa mazoea, na sio wataalamu

1. Hawana data!
ukisikiliza matangazo ya wazungu huwa wanatoa data za timu na wachezaji
unaeza pata darasa tosha la mpira
watakuambia rekodi ya timu ya mechi zilizopita
watakupa data za mchezaji mmoja mmoja mfano; idadi ya magoli, club anayocheza, historia yake nk
watakupa uchambuzi juu ya kocha na vikorombwezo vingi vingi vinavokupa burudani

mbongo utasikia tu mbungi inawekwa kati piga moja refuuu kule anapokea namba 23
naona mabaliko namba 10 anatoka anaingia namba 19....utopolo mtupu

hwafanyi research ya timu wanazoenda kutangaza, hata majina ya wachezaji hawayajui wanataja namba

2. Hawana lugha nzuri za kutangaza, zaidi ya kelele za kosakosa na mara chache hukaa kimya bila maneno!
wanajisahau sana
Afadhari hata DR.LEAKEY yule jamaa huwa ana kuwa na taarifa nyingi za timu na mchezaji mmoja mmoja,hadi una enjoy kumsikiliza.
 
Tatizo la watangazaji wa kiswahili wanafanya kazi kwa mazoea, na sio wataalamu

1. Hawana data!
ukisikiliza matangazo ya wazungu huwa wanatoa data za timu na wachezaji
unaeza pata darasa tosha la mpira
watakuambia rekodi ya timu ya mechi zilizopita
watakupa data za mchezaji mmoja mmoja mfano; idadi ya magoli, club anayocheza, historia yake nk
watakupa uchambuzi juu ya kocha na vikorombwezo vingi vingi vinavokupa burudani

mbongo utasikia tu mbungi inawekwa kati piga moja refuuu kule anapokea namba 23
naona mabaliko namba 10 anatoka anaingia namba 19....utopolo mtupu

hwafanyi research ya timu wanazoenda kutangaza, hata majina ya wachezaji hawayajui wanataja namba

2. Hawana lugha nzuri za kutangaza, zaidi ya kelele za kosakosa na mara chache hukaa kimya bila maneno!
wanajisahau sana
Tatizo hiyo kazi ya utangazaji inachukuliwa poa, unakuta mtu kamaliza kunywa supu na chapati mbili anakimbilia studio kurusha matangazo, wenzao huko nje unakuta mtu ana datasheet itakayomuongoza kwa matukio mbali mbali yanayoweza kutokea uwanjani, angalia jinsi kama huyu mwamba alivyojipanga

 
yah
Tatizo hiyo kazi ya utangazaji inachukuliwa poa, unakuta mtu kamaliza kunywa supu na chapati mbili anakimbilia studio kurusha matangazo, wenzao huko nje unakuta mtu ana datasheet itakayomuongoza kwa matukio mbali mbali yanayoweza kutokea uwanjani, angalia jinsi kama huyu mwamba alivyojipanga


hii ndo professionalism, watangazaji wetu bado sana.. daah1
 
Afadhari hata DR.LEAKEY yule jamaa huwa ana kuwa na taarifa nyingi za timu na mchezaji mmoja mmoja,hadi una enjoy kumsikiliza.
Kwa Sasa Kuna Gharib Mzinga wa azam, yule jamaa anajitahidi
Akiwa anatangaza mechi anakua na taarifa za wechezaji wote, sio kama wale WA TBC hawajui hata mchezaji anaeingia sub, shwaini zao
 
Huyu mtangazaji wenu anapayukapayuka na hata haieleweki anaongea nini. Kila wakati anapaza sauti na kuongea vitu visivyoeleweka wala kuhusiana na mechi iliyopo mubashara.
Angalia supersport channel 222 mkuu, achana na 223
 
Suala la Mtangazaji kuwa nyuma ya tukio hata mimi nimeliona ila tatizo ni kutokana na kwamba mtangazaji mwenyewe yuko Dar na yeye anaangalia kwa kutumia screen kama wewe unavyoangalia nyumbani kwako alafu inafanyika Sound exchange inazimwa ya mtangazaji wa kiingereza alafu anazungumza yeye kwa kiswahili kisha inarushwa sasa lazima tukio litangulie halafu sauti ndyo ifuate au sauti itangulie halafu tukio ndio lifuate
Yaani dstv wameshindwa kuwapeka qatar
 
Back
Top Bottom