DStv wametoa ofa ya chaneli zote bure kuanzia 27 mpaka 29 Desemba hata kama hujalipia

Mimi kwangu wameziacha kabla ya christmas channel karibu zote zilikuwa zinaonyesha wakati kakifurushi kangu ni kale ka 37500
HALAFU inaonyesha wewe BADO hujazijua vizuri channel ZA dstv. Ni BORA uKaPANDISHA kifurushi Chako AU ukakishusha. Uzoefu Wangu umenionyesha KUWA kifurushi CHA 25,000 hakina TOFAUTI kubwa NA HICHO CHA 37500. BORA upandishe kifurushi chako AU ushuke kwenye 25,000. KUNA NAMNA AMBAYO Unaweza KUINGIA kwenye website ya dstv na ukalinganisha vifurushi KUONA NI channel zipi ZIPO KWENYE kifurushi chako, AMbAZO HAZIPO KWENYE kifurushi kingine
 
Wamepiga pesa sana hao acha wanyooshwe tu
 
Mimi si mtu nayetazama sana tv. Nalipia hicho kifurushi kwa sababu watu nnaoishi nao wanapenda channel namba 165 na 168 maisha magic, na 171 ambapo hazipatikani katikq kifurushi cha chini ya hapo. Bila hizo channel wanazopenda ningekuwa nalipia kifurushi cha chini zaidi.
Mimi mambo yote nayopenda nayapata kwenye internet.
 
DSTv walikuwa watamu kuanzia 2015 kurudi nyuma mpaka 2010 huko, kipindi hicho walipiga pesa ndefu kwasababu Afrika ilikua haijaamka bado ndio maana hata channels za Muziki miaka ile zote zilikua za USA

Hongera yao kwa kuosha macho ya wateja wao, hii offer ili iwe tamu wangetoa mwezi mmoja
 
Dstv kila mwaka hua wanahizo offer mtu mmoja mmoja kimya kimya ila hawatangazi hii ya jana wala sio big dili kiivo
 
Mtoa mada sio suala la ushindani na azam, DStv kila mwaka msimu wa sikukuu Huwa wanatoa channels Bure Kwa wateja, sasa hivi huwezi kufikiri yaani watoe channels Bure siku mbili kisa ushindani na azam....hapa bongo hakuna king'amuzi Cha kushindana na DStv...unaweza ukawa na azam lakini ukakosa channels za kuangalia Kwa sababu zinaboa..labda Kwa watu wanaopenda mpira wa kibongo na siku hiyo iwe inacheza yanga au simba, otherwise hakuna Cha maana azam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…