Dstv yangu huu ni mwezi wa 3 nakula maisha

binafsi nilinunua iwe substitute ya azam, lakini nimeona hakuna vipindi vizuri, nimebaki na azam yangu.
 
Hiyo inatokea unapoongeza salio bila ya kusubiria kifurushi kiishe,yani kama imebakia siku moja kwisha unajazia salio,ila ukisubiri mpaka ikakata,hiyo compact huwezi ipata kwa hela ya Bomba...
 
Kirudishe mkuu.Utapewa kesi ya utakatishaji fedha na ugaidi
 
Hapa sijaelewa hebu fafanua zaidi
azam ana vipindi vingi vizuri kuliko dstv, hapo utakuwa umenielewa sasa. na nilinunua dstv makusudi baada ya kuona matamthilia ya kiislam tuu na story za kiislam tuuu hadi nikawa nashindwa kuelewa watoto wangu wakiangalia hiyo tv mbona watakubaliana na uislam? nikanunua dstv, ajabu yake, nimerudi kutumia azam kwasababu dstv hawana vipindi vingi vizuri. wamezidiwa na azam inshort.
 
Kifurushi kizuri dstv ni kuanzia 51000. Hivyo vya 9000 utajuta.
sasa kwanini niende kwenye 50s wakati azam yupo kwenye 20s? kwa maisha haya ya kitanzania ambayo tv kwangu mimi naangalia mara chache sana, ni kwaajili ya watoto tu kwanza.
 
Azam huko watoto si wanakimbilia Tamthilia za wakina kurufii? Sasa pale mtoto anajifunza nini hasa? Mnaharibu watoto kwa ujinga wenu
 
Makampuni ya vipindi ya Television soko lao kubwa ni Africa huku ndo wajinga wamejaa, ndo watu wana muda wa kuangakia Tv, masaa yote.

Wazungu kama wanatazama TV ni nadra sana.
 
Kuna Day nilitembelea Mzungu nmoja Arusha ni Mwanamke wa Kimarekani ila kaolewa na Mmasai, ana watoto wanne, nilishangaa kuto kuona TV sebuleni na vile alivyo na watoto wadogo, ila sikumuuliza.

Siku nyingine nikaenda tena ila siku hio sikuingia ndani niliishia nje kuna kazi nilikuwa nafanya ikabidi nimuulize kwamba Watoto wako hawatazami TV?

Alicho niambia ni kwamba hawezi ruhusu ujinga huo kwa watoto na watoto wanapoteza ile natural cretivity yao na wanajazwa ujinga sana sana wana computa wanacheza games mbalimbali na michezo mingine.

Sasa njoo kwetu Sasa Mtoto anaijua Tamthilia ya Kituruki kuliko kitu chochote kile.

Watoto wanakuwa wajinga lakini wazazi wanaona ni kama ndo malezi Bora ya Watoto.
 
Ngoja kwanza, mzungu wa kimarekani???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…