Dubai: Rais Samia ahudhuria Siku Maalum ya Tanzania (Tanzania Day) ya maonyesho makubwa ya Kimataifa ya Biashara na Uwekezaji ya Dubai Expo 2020

Hakuna kitu kama hicho.
 
Baadae mje mtupe mrejesho wa matajiri waliokuja kuwekeza Tanzania kutokana na hiyo Dubai Expo!
 
Tena tunaomba epitie huko aende kuzindua ile filam ya royal toulsim aliyozunguka mwezi mzima eti anatangaza vivutio vya utalii, Sasahivi mawaziri na mabarozi wako likizo.
 
Wakirudi Kutoka SHOPPING yao huko Dubai, utawasikia jinsi wanavyoongopa kuwa wamepata wawekezaji wengi wanakuja na pia wamepata vijisenti!
 
No serious investor anapatikana kwenye matukio kama hayo.

Tutaishia kupata madalali tu.
weyey jamaa ku invest kwa wengine unapenda ila wakija kwako hutaki mweeee!
 
Umesema sahihi kabisa. Nimewahi kufanya kwenye multinational companies 3, zote zina vigezo vyake wanavyovitazama. Hawaendi mahali popote kuwekeza eti kwa sababu Rais amesema.
 
Safi Kazi iendelee
 
Zingatia alichokwambia mwana hapo.. madalali hujaa kwenye maonyesho hayo.. hutak sawa.. hata wenyew wanasema..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na Bwanku M Bwanku.

Leo Jumapili kwenye Gazeti la MZALENDO Ukurasa wa 4 nimechambua hatua ya nchi yetu kushiriki kwenye maonyesho makubwa ya Kimataifa ya Biashara na Uwekezaji ya Dubai Expo 2020 ambapo Jana Jumamosi Februari 26, 2022 ilikuwa Siku Maalum ya Tanzania (Tanzania Day) kwenye maonyesho hayo ambapo Rais Samia alikuwa Mgeni rasmi na kuieleza Dunia kupitia maonyesho hayo fursa zote za Biashara na Uwekezaji zilizopo Tanzania.

Maonyesho hayo ya Dubai Expo ni makubwa sana Duniani yakishirikisha nchi 192 pamoja na Wafanyabiashara na Wawekezaji wakubwa kutoka kila pembe ya ulimwengu. Hatua yetu kushiriki maonyesho hayo kama Mshiriki rasmi, kuwa na Banda lake na Rais Samia kushiriki kuongoza Taifa letu kueleza kila fursa iliyopo nchini ni hatua kubwa sana ya kushusha Uwekezaji mkubwa sana nchini kutoka Nje. Pata NAKALA sasa ya Gazeti hili la MZALENDO usome Makala yangu hii uone ukubwa wa maonyesho hayo na hatua ya Nchi yetu kushiriki itakavyo-boost Uchumi na Maendeleo yetu.

Bwanku M Bwanku
bwanku55@gmail.com





 
Sure, mtu mwenye akili hawezi kuacha maonyesho haya yenye nchi zaidi ya 192 na Wafanyabiashara na Wawekezaji wote wakubwa. Heko Rais Samia Suluhu Hassan, endelea kuifungua nchi yetu kiuchumi, Kidiplomasia na uwekezaji. Vijana tuko nyuma yako maana haya MATUNDA ya ajira yanakuja kwetu. Heko SSH.
 
Kitabu cha Marketing high technology cha Professor William L. kitatufaa zaidi naona kama kwenye marketing bado tupo analogue...
 
Waziri Mwigulu juzi alikuwa Abuu Dhabi, ziara za Rais zinajibu
 
Tumefungua nchi ambayo milango yake ilifungwa. Ali Hassan Mwinyi alijaribu kuifungua lakini alishindwa kwa upinzani mkubwa wa wafuasi wa Bwana yule mjamaa mkubwa Tanzania.

Hivyo, jitihada zinafanyika lakini kazi ipo, watanzania hawapo tayari kuona nchi inafunguka. Hata baadhi ya mawaziri ni taabu kweli kweli. Hivyo usijali jaribu baada ya miaka 5, maana mfunguaji atakuwa bado ni pilot wa nchi hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ