tuzzo zilkua znaitwaje?bro sikubaliani nawewe diamond hakushiriki tuzo za Eatv coz alikua Na contract Na voda Na ni balozi WA voda kiutaratibu hakupaswa yeye wala timu yake ya Wasafi kiashiriki Ni utaratibu WA kawaida huo.NI Kama coca wakiwa Na bahati nasib zao wanakuambia kabisa wafanyakazi Na familia zao hawapaswi kushiriki,hii Ni kwa uelewa wangu mdogo.Bifu laweza kua Na sabanu nyingi ambazo sisi watazamaji hatuzifaham.
Chuki haikisaidii, pambana na hali yako
Maelezo meengi kama umetumwa, jambo la msingi kama wamedharauliana kwe masuala ya mpunga ili awapawambe je? Najua mleta mada unatumika kama toilet paper tu wakipatana huna dili wakishindwana unadili mmbea.Wasalaam wana jamvi.
Bila shaka hakuna ubishi kabisa moja ya vyombo vya habari ambavyo vimekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha muziki na tasnia ya muziki wa kizazi kipya hatuwezi kivisahau vyombo kama EATV na EARADIO na wala si vya kubezwa...
Pamoja na hivi vyombo kuwa na matatizo na wasanii ambayo kimsingi yanaweza kutokea kwakuwa wanaofanya kazi wote ni binadamu na hawajakamilika kabisa.....lakini tusisahau kuwa vyombo hivi vingi au karibu vyote vina sifa ya kupenda kuabudiwa lakini mara zote matatizo yao na wasanii humalizwa kwa kuongea hasa kwa hawa EARADIO/EATV.
Ni wazi kabisa EARADIO/EATV ndio lilikuwa kimbilio la wasanii wengi maana walijiweka mbali sana na migogoro na wasanii na kwakweli kipindi cha nyuma walijizolea umaarufu mkubwa sana kwa sababu ya utaratibu mzuri wa kutatua migogoro yao na wasanii.......
Hivi karibuni EATV/EARADIO wamekuwa wakilalamikiwa sana tena sana kuwa hawachezi nyimbo za Diamond na wamekwenda mbele zaidi hawachezi nyimbo zote za WCB.... katika ya watu waliokuwa wana watetea hawa EARADIO/EATV mimi nilikuwa mmoja wao kwani niliamini hawana kosa lolotea na wanayo hoja na kuna kipindi walikuwa wanapinga nyimbo za WCB.
Lakini baada ya kufanya utafiti nimejiridhisha kabisa EARADIO/EATV ni chombo kilicho jaa wanafiki waliotukuka kwa sababu pamoja na kuwa na chuki na msanii fulani hawataki kuweka wazi kama wenzao clouds ambao ni wazi kuwa kila mtu anajua kuna wasanii hawapatani nao...
Kibaya zaidi EATV/EARADIO sasa wamekuwa wakiongozwa na fikra na chuki za Abdallah Hamisi Ambua ambaye yeye na kundi lake pale EATV/EARADIO huokoteza vihabari kwenye mitandao ambavyo vinalengo la kumchonganisha Diamond na watu na wao huvifanya topic ili Diamond na wale wanaomzunguka waonekane wabaya na pamoja na watu wa karibu wa Diamond kujaribu kutatua migogoro hiyo lakini Dullah yeye huwa ndio kama mmiliki wa vituo hivyo....
Kwa sasa hawachezi nyimbo za WCB kabisa na hii ni kutokana na chuki za Dullah kwa Diamond...
Dullah anatakiwa kujua kuwa kwa sasa vyombo vya habari ni vingi hata wasipo cheza nyimbo za Diamond na WCB bado zita hit kwani ni ukweli ulio wazi EARADIO kwa sasa haina nguvu kuzidi Clouds fm na E-fm pamoja ina frequency mbili....na uongozi wa Earadio na EATV wasipo angalia Dullah na timu yake watawaharibia biashara kwaajili ya chuki zao binafsi...
Dullah anatakiwa kujua kuwa hata yeye alipo hapo alisaidiwa sana tena kupitia Salama Jabir anatakiwa kujua kama yeye alisaidiwa atumie nafasi yake kusaidia wengine.
Kama ni hoja ya kutoshiriki tunzo zao wanatakiwa kutwambia kama ni WCB peke yao ndio hawakushiriki au lah...lakini bado si hoja ya kumchukia msanii wakati tunzo ilikuwa si lazima au wajitazame upya....
Naamini EATV/EARADIO wanaweza tafuta njia nzuri ya kutatua matatizo yao na wasanii hawa kwa njia nzuri tuu na sio kwa chuki hizi za wazi wazi kwani hazimsaidii yeyote yule na wote wana chakupoteza kwenye hili....Hakuna watu wanaofurahia migogoro bali wengi wanapenda amani.
Wasalaam
Kwan kushiriki izo tunzo ilikuwa lazima maana kwanza zilikuwa za kujipendekeza.,..au ww maana ya neno kujipendekeza hulijui mkuu
Unamaanisha Diamond mkubwa kuliko Mengi? Mengi anauwezo wa kumfanya Diamond houseboy wake na akamlipa pesa ndefu kuliko anayopata kwenye mzikiwapige wasipige diamond bado mkubwa kuliko EATV.
Huyo Domo nyimbo zake zilikuwa hazipigwi hapo kitambo lakini bado anatisha.. Hao wasanii wanaochezwa nyimbo zao huko wamefika wapi kimafanikio ya kimuziki? (harmorapa, baraka da prince n.k)
Ukweli utabaki palepale, kituo chenye nguvu ni clouds pekee maana wale watu msaada wao hauishii kwenye kupiga nyimbo pekee hadi shows, na deals mbalimbali (Mf. Perfume za Chibu limepigwa collable Kusaga na Domo, Usiku wa kuamkia leo Domo kapiga show Rwanda huko iliyoandaliwa na Clouds)
Hao walalanjaa Eatv ni kama kitumbua kikikosekana unakula sambusa ila Clouds ni Chumvi na ndio alikojishkiza huyo Domo, hajatetereka na hawezi kutetereka kisa Eatv..
Sababu ya kutoshiriki Fiesta ilikuwa kampuni ya Tigo ndio ilikuwa inadhamini show na yeye ana mkataba na Voda.Unakumbuka fiesta ya mwaka jana walimchunia kimtindo kupiga nyimbo zake kwa sababu alikataa kushiriki shughuli zao?