Wale ambao hawana dini wanaamini juu ya kila ambacho wanakifanya. Nadhan unajua kabisa kuwa ukijenga iman juu ya kila unachokifanya mara nyingi unafanikiwa na hiyo inatokana na physic power ambayo kila mtu anayo. Kinachotakiwa ni kuweka na kuamini juu ya kile unachokifanya ANY THING IS POSSIBLE.
Wengine wanaenda kuombewa wapate magari....
Nakubaliana na wewe kwamba dini ndio zinawafanya watu wasifikiri kabisa. Ukiangalia nchi maskini utagundua ndio wanapambana na dini kuliko zilizoendelea. Dini zinawafanya watu watumwa wa fikra wasiweze kufikiri zaidi ya kuamini wasichokijua.
Binadamu hajaweza kutumia uwezo wake wa kufikiri kwa sababu mbali mbali ikiwemo dini. Itambulike kwamba fikra ndio kila kitu. Kila kitu duniani kimetokana na fikra au wazo. Dini zitakuambia kuwa kila kitu kimeumbwa na Mungu. Huu sio ukweli. Mungu aliumba mara ya kwanza tena vitu vichache tu, lakini binadamu ndiye amekuwa akiumba vingine hadi leo. Mtoto akizaliwa ni matokeo ya uhai uliwekwa ndani mwanaume ukiunganishwa na mazingira ya uumbaji kwenye tumbo la uzazi la mwanamke na baadae kutokea au kumanifest kama binadamu. Hapa sii Mungu bali binadam wameendeleza uumbaji. Leo hii Mungu haumbi tena. Hii ndio procreation. Ila tukisema Mungu aliumba binadam tuko sahihi.
BTW Mbegu ya mwanume ndiyo yenye uhai tuu. Bahati mbaya hata yai la mwanamke halina uhai.
Najua wengine mtapiga mawe lakini ni kwa sababu ya dini zao.
Kuomba hakuhitaji dini yo yote. Wewe ukitaka cho chote unapata. mfano. "Ninataka kuwa daktari". iwapo utaiweka hii kwenye subconsious mind yako sawa sawa mwisho wa siku utakuwa daktari na sio dereva wa malori. Sasa hapo dini ni ipi?
Katika mkusanyiko wa sayari nyingi na nyota mbalimbali kunauwezekano mkubwa kwenye sayari zingine mamilioni kukawa na viumbe hai.
Kwakutumia formula za kimahesabu uwezekano wa kuwepo viumbe kwenye sayari zingine ni asilimia mia.
Lakini kwa utawala wa sasa wa dunia ni mbovu kiasi cha kufanya watu wasifikiri sana. Dunia imetawaliwa na siasa na dini. Watu wanajificha kwenye mgogo wa dini au siasa na kuacha kabisa kutumia akili zao inavyotakiwa.
Viongozi wa dini wamewapumbaza watu kiasi cha kushindwa kuwaza zaidi ya vitu wajuavyo.
Ningependa sisi GT tujaribu kutoa mawazo yetu na kuruhusu kujifunza zaidi.
Hebu fikiria watu wanauana kwa kigezo cha dini au siasa. Hivi inaingia akilini kweli?