Dunia itakuwaje Trump atakapoapishwa kama Rais wa Marekani hapo mwakani?

Dunia itakuwaje Trump atakapoapishwa kama Rais wa Marekani hapo mwakani?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Kabla ya mdahalo wa urais wa leo Donald Trump alikuwa ameamuacha Joe Biden kwenye kura za maoni. Lakini mdahalo wa huu umefunga kabisa maneno. Ni wazi kuwa Trump sasa njia ya ikulu ni nyeupe kabisa. Biden alikuwa na hoja nzuri na aliandaliwa vyema ila afya yake na uelewa wake sababu ya uzee vimemuangusha. Si mtu fit kushika madaraka ya urais. Sasa tujiandae na dunia ya Rais Trump, itakuwaje?

1. Hoja kubwa ya Trump ambayo aliikazia na kuilazimisha ni juu ya wahamiaji haramu. Bila shaka atakomaa sana na hii ishu, sijui itakuwaje?
2. Trump ana bifu kali la kibiashara na China, ataongeza kodi na vikwazo vya kibiashara kwa China. China atajibuje? Itakuaje kwa dunia?
3. Vita ya Russia na Ukraine. Trump atawezaje kuizima. Alipoulizwa alikazana tu kuwa angekuwa Rais vita isingetokea, lakini hakusema ataizimaje. Atapunguza misaada ya kijeshi kwa Ukraine?
4. Sema wote Biden na Trump wanaiogopa mno Israel.
5. Jamaa anaweza kukuza uchumi wa Marekani na kushusha Inflation?

Naiona Dunia chini ya Trump kama Rais wa Marekani kama Dunia hatari sana
 
Trump anazijua sana siasa kwa kweli nimemnyooshea mikono.

Ingawa simkubali Trump ila jamaa ni fundi sana wa kutumia mdomo na ndio kitu ambacho kimemuangusha Biden.

Trump kiutendaji ni worst leader, Marekani inatakiwa ipate raisi mwenye dira nzuri nje na hao wawili.
 
Uzuri wa Marekani Katiba yao iko vizuri na wabunge wana macho na akiharibu tu anaondoka kwa impeachment. Angalau wenzetu wako vizuri kuliko sisi.
Kwa sasa bunge ni majority republicans, ikiendelea hivi maana yake atakuwa na bunge la ndiyo mzee, na wabunge wa repubicans wanamuabudu balaa. Mahakama Kuu imejaa majudge wa republican. Pia anampango wa kugeuza vyeo vingi vya serikali viwe vya kuteuliwa ili aweke watu wake. Mhula ule wa kwanza alikwamishwa sana na maafisa wa serikali, safari hii amedhamiria kuweka watu wake. Hakutakuwa na wa kumzuia.
 
Uzuri wa Marekani Katiba yao iko vizuri na wabunge wana macho na akiharibu tu anaondoka kwa impeachment. Angalau wenzetu wako vizuri kuliko sisi.
Trump anampa ushindi urusi, halafu anarudi kuwapa sapoti israel kamaliza mchezo.......kosa kubwa kwa rais wa marekani ni kwenda tofauti na matakwa ya wayahudi, mengine wanamezea tu,,,,,Enzi za Trump ndo Jerusalem ilianza kutambuliwa na marekani kama ni mji mkuu wa Israel badala ya Tel aviv ,na hilo jambo ndo myahudi analitaka,,,,jamaa atauma upande huu na kupuliza upande huu kazi kamaliza
 
Trump anazijua sana siasa kwa kweli nimemnyooshea mikono.

Ingawa simkubali Trump ila jamaa ni fundi sana wa kutumia mdomo na ndio kitu ambacho kimemuangusha Biden.

Trump kiutendaji ni worst leader, Marekani inatakiwa ipate raisi mwenye dira nzuri nje na hao wawili.
Ukweli ni kuwa Trump kakutana mshindani dhaifu kupita kiasi.
 
Siasa za Marekani huwa hazitabiriki! Ni pande mbili (Dem n Rep) katika sarafu ya shiling moja Hata aingie Rais gani mf.Putin asitegemee unafuu wo wote katika vita vyake na Ukraine! Akaze buti kikweli kweli.
Iran ijiandae kwa sanctions zaidi
Kwetu sisi Waafrika ambao aliwahi kutuambia kuwa tunatoka kwenye shitholes huenda tusipate misaada zaidi.Aliwahi kusema dawa ya umaskini kwa nchi za kiafrika ni kuzi colonize tena.
Lakini huenda kutakuwa na utulivu duniani. Jamaa hapendi vita.
 
Ikitokea, nasema ikitokea, Trump akachaguliwa urais, lazima Putin ahudhurie uapisho wake pale kwenye mnara wa Washington.

Hawa jamaa wawili huenda ni watoto wa baba mmoja. Ni maswahiba hadi Marekani yenyewe inaogopa.
Jidanganye, usidhani kule mtu anaongiza nchi kwa matakwa yake. Tuliwahi kusema Boris akiondoka ktk ofisi ya PM UK basi UK itaacha kusapoti Ukraine, akaja mmama fulani na sasa hivi ni huyu Mhindi ila moto uko palepale.
 
Siasa za Marekani huwa hazitabiriki! Ni pande mbili (Dem n Rep) katika sarafu ya shiling moja Hata aingie Rais gani mf.Putin asitegemee unafuu wo wote katika vita vyake na Ukraine! Akaze buti kikweli kweli.
Iran ijiandae kwa sanctions zaidi
Kwetu sisi Waafrika ambao aliwahi kutuambia kuwa tunatoka kwenye shitholes huenda tusipate misaada zaidi.Aliwahi kusema dawa ya umaskini kwa nchi za kiafrika ni kuzi colonize tena.
Lakini huenda kutakuwa na utulivu duniani. Jamaa hapendi vita.
Vita ya Ukraine na Russia haina unafuu wowote wa kupoa endapo kama haitaisha kidiplomasia. Kinachoendelea sasa ndicho kitazidi, Ukraine ataendelea kupambana kukomboa ardhi yake huku akipiga ndani ya Russia. Russia naye atapambana zaidi ili kuzima mashambulizi ya Ukraine kukomboa ardhi yake.

Kule uarabuni ndo itakuwa balaa, jamaa atapambana kwelikweli kuwaondoa wahamiaji na wajinga wajinga, Lebanon na Iran ni kama watakalia kuti kavu.
 
Trump anazijua sana siasa kwa kweli nimemnyooshea mikono.

Ingawa simkubali Trump ila jamaa ni fundi sana wa kutumia mdomo na ndio kitu ambacho kimemuangusha Biden.

Trump kiutendaji ni worst leader, Marekani inatakiwa ipate raisi mwenye dira nzuri nje na hao wawili.
Tofauti ya Trump na Biden ni kwamba Joe Biden yeye ana uzoefu mkubwa sana katika medani za siasa na uongozi kuliko watawala wengi sana Marekani.

Ila sasa hana kabisa ile inayoitwa ^honor even among thieves.^

Anatumika tu na wenye nchi ilimradi yeye, Jill na Hunter wake mikono inaenda kinywani.

Kwa upande mwingine, Trump anaweza kufananishwa na jasiri hanibu (brave ignorant) anayependa kujinasibisha kama mzalendo kwa nchi yake.

Ni mtu mwenye uchu na azma thabiti ya kuuthibitishia ulimwengu kwa gharama yoyote kwamba hakuna anayeweza kufanya anachofanya yeye.

Ndiyo maana wakati mwingine amelazimika kung'ang'ania misimamo yake licha ya msukumo mkubwa wa wazee wa meza.

Katika ulimwengu wa Trump, msamiati wa kushindwa ulishafutikaga kitambo sana.

Wakati JB yeye anasaka mkwanja kupitia siasa, kipaumbele kikubwa cha Trump ni kuweka alama ya kudumu ya urathi.
 
Siasa za Marekani huwa hazitabiriki! Ni pande mbili (Dem n Rep) katika sarafu ya shiling moja Hata aingie Rais gani mf.Putin asitegemee unafuu wo wote katika vita vyake na Ukraine! Akaze buti kikweli kweli.
Iran ijiandae kwa sanctions zaidi
Kwetu sisi Waafrika ambao aliwahi kutuambia kuwa tunatoka kwenye shitholes huenda tusipate misaada zaidi.Aliwahi kusema dawa ya umaskini kwa nchi za kiafrika ni kuzi colonize tena.
Lakini huenda kutakuwa na utulivu duniani. Jamaa hapendi vita.
Trump hana interest na mrusi,,,,,.....anajua hawawezi kupiga front zaidi ya 1 na mambo yaende, hapo Ukraine anaenda kubwagwa focus wanahamishia kwa Israel,,kama kweli Israel ataingia kupigana Lebanon lazima mmarekani aachie upande mmoja, na kama akishinda Trump kazi itakua nyepesi kwa Putin ila ngumu kwa Iran na wenzie
 
Vita ya Ukraine na Russia haina unafuu wowote wa kupoa endapo kama haitaisha kidiplomasia. Kinachoendelea sasa ndicho kitazidi, Ukraine ataendelea kupambana kukomboa ardhi yake huku akipiga ndani ya Russia. Russia naye atapambana zaidi ili kuzima mashambulizi ya Ukraine kukomboa ardhi yake.

Kule uarabuni ndo itakuwa balaa, jamaa atapambana kwelikweli kuwaondoa wahamiaji na wajinga wajinga, Lebanon na Iran ni kama watakalia kuti kavu.
Unajua, Trump ni fundi sana wa kuzungumza mduro (double speech).

Anaweza kusema atashughulika na wahamiaji, kumbe kumkichwa anamaanisha kuwaondoa Ukreni wanajeshi na maafisa wote wa Marekani wasijihusishe na vita dhidi ya Putin mdogo wake.

Kwa mujibu wake, usitishaji vita Ukreni utamhitaji apige simu moja tu, inatosha.

Alifanya kwa Watalibani, bila shaka atafanya tena kwa Ukreni. The guy seems to be specialized in the impossible feats.
 
Kwa sasa bunge ni majority republicans, ikiendelea hivi maana yake atakuwa na bunge la ndiyo mzee, na wabunge wa repubicans wanamuabudu balaa. Mahakama Kuu imejaa majudge wa republican. Pia anampango wa kugeuza vyeo vingi vya serikali viwe vya kuteuliwa ili aweke watu wake. Mhula ule wa kwanza alikwamishwa sana na maafisa wa serikali, safari hii amedhamiria kuweka watu wake. Hakutakuwa na wa kumzuia.
Naililia marekani 😭😭😭
 
Back
Top Bottom