Dunia ni uwanja wa vita za hatima

Dunia ni uwanja wa vita za hatima

Thecoder kwa hiyo ukienda labda kwenye interview ya kazi ambayo siyo hatma yako na ukiwa umejiandaa sana kwa kusoma, kusali na kufunga pamoja na kuelewa mkono na watumishi ni rahisi kupigiwa chini na mtu ambaye hajajiandaa, hajasoma, hajasali, hajafunga na hana mkono wa mtumishi, ila kinachokushinda no kwamba eneo ni la hatma yake sio yako japo wewe umeinua nguvu za rohoni, kwa nini inakua hivyo?
 
Thecoder kwa hiyo ukienda labda kwenye interview ya kazi ambayo siyo hatma yako na ukiwa umejiandaa sana kwa kusoma, kusali na kufunga pamoja na kuelewa mkono na watumishi ni rahisi kupigiwa chini na mtu ambaye hajajiandaa, hajasoma, hajasali, hajafunga na hana mkono wa mtumishi, ila kinachokushinda no kwamba eneo ni la hatma yake sio yako japo wewe umeinua nguvu za rohoni, kwa nini inakua hivyo?
Inakua hivyo kwasababu ya hatima.

Hili swali nimelijibu mara nyingi kwamba kinachoombewa si pesa ila ni njia za pesa ambazo zipo ndani ya kila mtu kupitia hatima yake.

Pia nataka ujue ya kwamba duniani si kila jambo huwa linaombewa na mambo yote ambayo yapo ndani ya mtu tangu alipozaliwa huwa hayavutwi kwa maombi ila yanavutwa kwa kuyaendea kwenye njia zake but mambo ambayo huwa yanaombewa ni yale mambo ambayo hayakuwa ndani ya mtu tangu alipozaliwa kwamfano ukiwekewa unajisi ni rahisi sana kutoka kwa njia hizo za maombi.

Skia, ukienda dukani ukawa umenunua shati au tishet nyeupe then ukaivaa ila ikatokea wakati uko kwenye mitikasi yako madoa yakiingia utaenda kununua dawa ya madoa na utayatoa hayo madoa, na kinachotokea ni kwamba hiyo dawa ya madoa itadeal na madoa tu na wala si vitu vingine ambavyo vilikuja na hiyo nguo kutoka kiwandani na hivi ndivyo maombi yanavyofanya kazi.

Kwahiyo unapoombewa kwenye kazi ambayo si ya hatima yako huwa kinachotoea ni kuoverride kwa maana unaongeza baraka kwenye kazi ya hatima ila si kwenye kazi ambayo si ya hatima yako thou kuna baadhi ya sababu za hapa na pale zinaweza kupelekea ukapata hiyo kazi ila si kwasababu ya hayo maombi.

Kubadili asili ya kitu kilichopo ndani ya mtu au ulimwengu na kufanya kifanye kazi kwa namna tofauti hapa huwa tunasema muujiza umetokea au mtu ameamua kufosi hatima ambayo si yake.

Muujiza si kila mtu anaweza kuufanya na Kubadili hatima kuna utaratibu wake na kuihodhi haiwezekani bila kafara.
 
KIPANDE CHA TATU CHA NYONGEZA.

Nadhani hadi sasa wote tunajua kwamba Kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na swala la mafanikio ya kibiashara huwa yanategemea zaidi asili yako na ninaposema asili nadhani kwa sasa wote tunaelewana kwamba nazungumzia lile jambo la msingi ambalo lilizaliwa ile siku ambayo wewe umezaliwa kwa maana ya hatima au uelekeo ongozi ambao wewe unatakiwa uufuate ili uweze kutimiza lile lengo la wewe kuwa hapa duniani.

Sasa kutokana na kwamba biashara huwa inamtindo wa kuchagua watu basi kuwa na uhakika hata hawa mentors ambao huwafunza watu mambo mbalimbali ya kibiashara kwenye mazingatio ya ule upande ambao wao wamefanikiwa nao huwa hawafanikiwi kuwafanya watu wote wanaoenda kwenye madarasa yao wafanikiwe kwenye hizo biashara ambazo wao huzitumia kuwaelekeza na kuwasimamia watu wengine waweze kufanikiwa.

Kwahiyo kuna watu ambao wameshawahi kutoa pesa nyingi sana kuwalipa mentors ili waweze kuwasaidia kuwapa mbinu za kuitoa idea yaani wazo lao la kibiashara hadi kwenda kwenye ile hatua ya biashara kisha kuitoa hiyo biashara kuipeleka kwenye hatua ya biashara inayoleta faida itarajiwayo au zaidi, lakini badala yake wanaishia kupata hasara licha ya kufuata hatua zote na mbinu zote ambazo wamekua wakifundishwa na hao mentors wao.

Sasa basi...

Kama utakua umenisoma vizuri kuanzia mwanzo utaelewa ya kwamba hapa mentor hana kosa ila ni vile tu hajui kwamba biashara ni kama dunia ambayo iko ndani ya dunia kwahiyo iko na sheria zake pamoja na taratibu ambazo mtu ni lazima azifuate ili aweze kuishi na sio tu kuishi bali kuishi na kudumu katika dunia hiyo ya kibiashara.

Yaani ni...

Kwamba biashara ambayo imempa utajiri yeye haiwezi kumpa utajiri huo kila mtu ambae yuko hapa duniani, ndio maana mentors wengi huwa wanakuaga na watu wao kadhaa ambao wanapenda sana kuwatolea mfano kwamba waliwafuata wakiwa hawana kitu ila baada ya kusoma na kutumia mbinu zao watu hao waliweza kufanikiwa sana kibiashara lakini pia ukifuatilia kwa mentors hao hao utakuta kuna wimbi la watu wengi ambao wanawalalamikia kwamba ni matapeli kwa maana wamewalipa pesa nyingi ila wameshindwa kuwapatia yale mafanikio ambayo waliwaahidi kuwapatia kabla ya hayo mafunzo.

Sasa yote haya yanatokana na hatima tulizobeba ndani yetu ndizo zinazoleta huu utofauti wa nani afanikiwe kwenye biashara ipi na nani asifanikiwe na kwa maana hiyo basi kabla hujatafuta mentor hakikisha unajijua kwanza na hii itakusaidia sana kuepukana na hali ya kulaumu watu au kuwaona watu ni matapeli wakati wako kwenye hiko wanachokifanya kwa miaka na wamesaidia watu kufanikiwa katika njia hizo hizo ambazo wewe hazikuweza kukufanikisha.

Nimekua nikisema mara nyingi ila nasisitiza tena kwamba kila mtu anaouwezo wa kuanzisha biashara ila si kila biashara inayoanzishwa na mtu inaouwezo wa kuleta faida mikononi mwa kila mtu ambae ameianzisha.

Na ndio maana siku hizi...

Kuna wimbi la watu wengi ambao wamebobea kwenye maswala haya ya biashara na uchumi na wengi wamekua wakitoa ushauri wa namna tofauti tofauti za kuanzisha na kukuza biashara kuanzia hatua za awali hadi kufikia ile hatua ya ukomavu yaani hatua ambayo biashara inaanza kuleta faida na mbinu hizi huwa hazitofautiani sana kati ya mchumi mmoja na mwingine na huwa zinazoleta bure kabisa kwenye mitandao ya kijamii ila licha ya haya yote bado watu ambao wanawafuatilia watu hawa wanapata tabu sana kwenye maswala haya ya kibiashara, wanatumia kila mbinu inayofundishwa na kufuata hatua zote ila bado mambo ni magumu sana.

Sasa ukichunguza kwa umakini hizi shida na taabu watu wanazozipitia kwenye mambo haya ya kibiashara na katika watu hawa ambao wanapitia hizi shida pia wapo walimu au wakufunzi wanaofundisha watu maswala haya haya ya biashara ila nawao pia wanashindwa kuziendesha biashara zao na kuzifanya ziweze kufikia katika ile hatua ya kuleta faida inayotarajiwa au zaidi. Na hii inaashiria kwamba kuna kitu fulani cha msingi sana huwa kinakosekana kwenye vitabu vingi vya mambo ya biashara (ni kama vitabu vingi vimeruka kurasa yaani zile kurasa za awali zilinyofolewa na kujikuta tunaanzia katikati katika kujifunza mambo haya).

Najua watu ambao tayari mmefanikiwa kibiashara hamuwezi kuelewa hili lakini pia najua nyingi wenyewe licha ya kwamba mmefanikiwa ila huwa hamna maelezo toshelezi ya Kwanini mmefanikiwa katika biashara hizo mnazozifanya na ndio maana kila mara tukiwauliza huwa mnaishia kutupatia majibu yale yale kama tusikate tamaa, kujituma, kuheshinu watu na kadhalika na kusema ule ukweli haya majibu huwa ni mepesi sana kiasi ambacho watu wengi tumeshayazoea na ndio maana wapo watu ambao wanaamini kwamba utajiri ni siri.

Sasa inawezekana mawazo yao yakawa sahihi kwamba utajiri ni siri ila duniani tuko na matajiri kadhaa na ukifuatilia kwenye ile orodha ya matajiri wa dunia halafu ukirudi kwenye ndugu zao wa damu, kwa asilimia kubwa ndugu hao hautawaona hata kwenye orodha ya matajiri 1000 wa dunia, sasa tuseme ni kweli utajiri ni siri ila inamaana matajiri hawa wanafanya siri hadi kwa ndugu zao wa damu? Inamaana hata kuwafunulia kidogo ili na wao wapate hata ule upukupuku wa mwisho mwisho wanashindwa? Hii ukiifikiria ni kama haiingii akilini hivi na inatia mashaka kidogo kuamini kwamba utajiri ni siri ambayo watu wameificha ili wengine wasiijue.

Kwa maana kama nilivyosema hapo awali kwamba ukiwauliza matajiri wenyewe wamefanya fanyaje hadi kufika kwenye hayo maisha ya kitajiri waliyopo au wanayoishi huwa siku zote wanakuambia mambo yale yale, yaani kufanya kazi kwa bidii, kuheshimu watu, kutokukata tamaa na mara chache utawasikia wengine wanaongeza na neno bahati.

Sasa basi, kwakua matajiri wengi wakiulizwa swali hilo moja, huwa wanakua na majibu yale yale mfanano, ambayo siku hizi masikioni mwa watu wengi huwa wanayaona kama ni majibu mepesi mepesi yasiyo na ukweli wowote, kwasababu hivyo vyote vilivyosemwa na hao matajiri hata wao wanavifanya kila siku wanapokua kwenye shughuli zao za kuwaingizia kipato, ila cha ajabu ni kwamba hawakui kiuchumi, lakini ukirudi kwenye huo mfanano wa majibu, tunaona matajiri wachache ambao wao huwa wanaongezea neno la ziada ambalo ni bahati, na hapa ndipo ambapo siri ya utajiri ilipo, kwa maana hawa waliotutajia hili neno la bahati ni kama wametuibia siri kwa njia isiyo ya moja kwa moja.

Kwa maana kama utakua umenifuatilia vizuri kwenye huu uzi kuanzia mwanzo nilikwambia kuhusu maswala ya hatima kwamba nguvu ya umiliki wa fedha na Mali huwa imejificha kwenye huo upande na nikasema tena kwamba kuliko na hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na ndio maana siku zote watu au matajiri wachache husema utajiri ni bahati.

…. Nitarudi tena baadae kidogo kuleta muendelezo wa uzi mama, ila kwenye hiki kipande nimerudia rudia maneno kuweka msisitizo na lengo langu usitoke nje ya haya kwa maana tumeongea mambo mengi na yapo mengi ya kuongea na kuna kitabu kinaitwa vipawa vya hatima unaweza kukitafuta ili uendelee nacho, ni kitabu kidogo na HAKIUZWI.

Lakini pia ipo programme ya VIPAWA VYA HATIMA ikiwa na lengo la kukusaidia wewe kuweza kuijua asili yako na baada ya kuijua hiyo asili yako pia utaweza kujua zile biashara zote ambazo zinafungamana na upande huo, hii programme ni bure kabisa na itakua bure milele so usije ukadhani ni bure kwa sasa ila huko mbele itakua na malipo, HAPANA haitakuwa na malipo milele. Na ukomo wa programme hii yaani kuanzia ule muda wa kuanza kwake hadi kuisha huwa inategemea sana na muhusika kwa maana kadri ambavyo atatoa ushirikiano kwenye kufuata zile taratibu ambazo tutamuelekeza ndivo ambavyo atawahi kupata lile file lake la yeye ni nani na ameletwa hapa kuongeza mitetemo chanya katika upande upi na zipi ni biashara ambazo zinafungamana na yeye moja kwa moja, kwahiyo inaweza ikachukua wiki, mwezi, miezi hadi mwaka.

Kwahiyo kama utahitaji kujiunga na programme hii basi unaweza ukaja PM au ukatuma ujumbe kwenye hii barua pepe vipawavyahatima@gmail.com na moja kwa moja utafanyiwa ule mchakato wa awali ili kwenda kwenye hatua ya kwanza.(HII NI PROGRAMME YA LAZIMA NDIO MAANA NI BURE)

Ila pia ipo programme ya TABSTIP hii ni programme ambayo inachukua ile idea au wazo lako la kibiashara kwenda kwenye biashara na kuitoa hiyo biashara kwenda moja kwa moja kwenye biashara inayoleta faida inayotarajiwa au zaidi. Sasa programme hii inachukua watu ambao wameshapata basic knowledge ya kujitambua Kwanini wako hapa na hatima yao ni ipi na hii knowledge hupatikana katika ile programme mama ya VIPAWA VYA HATIMA kwa maana kuna watu baada ya kuijua hatima yao na zile biashara fungani wanataka waweze kupata ule muongozo wa namna ya kulichukua wazo kulipeleka hadi kwenye biashara iliyokomaa na haya yote hufanyika kwenye TABSTIP na programme hii kuanza hadi kuisha kwake ni miaka 3 ikiwa imegawanyika katika session kuu mbili na kila session huchukua mwaka mmoja na nusu huku zote zikiwa zimegawanyika katika hatua kuu sita na kila hatua itatumika kwenye kufanya transformation yaani mabadiliko ya biashara yako, na hii ndio programme pekee ambayo huwa inahusisha mchango kidogo kwa kila anaetaka kwenda nayo.(HII SIO PROGRAMME YA LAZIMA NDIO MAANA KUNA ADA)
Ngoja niwasaidie ambao wameshindwa kukipata kule telegram
 

Attachments

Mzee umetisha yaani unavyo tirilika nikama vile unanijua aiseee 🤔

This 👇👇 unaweza Vipi kuziepuka Roho hizi !? Au ndio hatima yako so haiepukiki!?
 

Attachments

  • Screenshot_2024-12-20-09-08-31-566_com.quoord.jamiiforums.activity-edit.jpg
    Screenshot_2024-12-20-09-08-31-566_com.quoord.jamiiforums.activity-edit.jpg
    256.3 KB · Views: 11
Ulimwengu wa Roho wa Nuru ndio unaongoza ulimwengu wa mwili.

Hatma yako ili uifikie lazima ushinde vita na vita hiyo ni ya Rohoni ni vita kati ya ulimwengu wa Giza na Nuru, na ukishinda utaiona hatma ila ukishindwa hutaona hatma yako.

Kazi kwako kuchagua ulimwengu wa Giza au Nuru ili uifikie hatma yako...

NB: Dunia hujaja kucheza ni uwanja wa vita ila isiyoonekana.
 
Ulimwengu wa Roho wa Nuru ndio unaongoza ulimwengu wa mwili.
sio watu wote wanaishi kwa uadilifu kwa maana kuuruhusu ule ulimwengu wa kiroho uweze kuuongoza mwili na hata wale ambao waliwahi kufanikiwa hawakuwahi kuishi upande huo kwa asilimia 100 bali walio wengi wanahama na ndio asili ya kila mwanadamu na hili unaweza kuliona hata kwenye manabii na mitume ambao waliaminiwa sana kuishi kwa uadilifu kilichokuja kuwaangusha wengi wao ni kushindwa kuuacha mwili uendelee kuongozwa na roho na badala yake kuna nyakati waliuacha mwili uiongoze roho na ndio maana mwanadamu ni kiumbe ambae haaminiki kwa maana huwa anaswitch kwa haraka sana kwa sababu asili ya ulimwengu inafavor sana upande wa mwili kuliko ule wa kiroho...na huu ndio ugomvi mkubwa kati ya mamlaka za juu na mwanadamu.
 
sio watu wote wanaishi kwa uadilifu kwa maana kuuruhusu ule ulimwengu wa kiroho uweze kuuongoza mwili na hata wale ambao waliwahi kufanikiwa hawakuwahi kuishi upande huo kwa asilimia 100 bali walio wengi wanahama na ndio asili ya kila mwanadamu na hili unaweza kuliona hata kwenye manabii na mitume ambao waliaminiwa sana kuishi kwa uadilifu kilichokuja kuwaangusha wengi wao ni kushindwa kuuacha mwili uendelee kuongozwa na roho na badala yake kuna nyakati waliuacha mwili uiongoze roho na ndio maana mwanadamu ni kiumbe ambae haaminiki kwa maana huwa anaswitch kwa haraka sana kwa sababu asili ya ulimwengu inafavor sana upande wa mwili kuliko ule wa kiroho...na huu ndio ugomvi mkubwa kati ya mamlaka za juu na mwanadamu.
Imani na Toba ya kweli yaani msamaha pekee ndio unafanya Manabii na wanaomuamini Mungu waweze kuendelea kuishi kiroho na kimwili.

Pia kufunga chakula ni njia nzuri ya kujiweka kiroho zaidi.

Ukiwa kiroho zaidi unakuwa na taarifa za mambo yajayo yaani kama Kuna kazi au adui anakujia unapata taarifa..
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...


Cc: Mahondaw
ni asili, kwa maana mtu ni copy ya ukuu halisi kama ilivyo wewe na mwanao, utaweza kumpa maagizo na kuyafuata pale ambapo atakua kwenye ule umri wa kutokujua lipi jema na lipi baya pamoja na kutokuyamaster vizuri mazingira ila akishafikia umri fulani neno lako kwake haliwi na uzito ule wa kama mwanzo na hata yale mambo mengi ambayo ulikua unamkataza asiyafanye atayafanya... kwahiyo utaona hapo kwamba mwanzo alikua anafuata order zako ila anapojitambua anafuata za kwake mwenyewe na kurudi kwako kila anapokwama.
 
Imani na Toba ya kweli yaani msamaha pekee ndio unafanya Manabii na wanaomuamini Mungu waweze kuendelea kuishi kiroho na kimwili.

Pia kufunga chakula ni njia nzuri ya kujiweka kiroho zaidi.

Ukiwa kiroho zaidi unakuwa na taarifa za mambo yajayo yaani kama Kuna kazi au adui anakujia unapata taarifa..
upo sahihi, na hiyo ndio nguvu ya kuishi maisha ya rohoni... kuishi maisha ya rohoni ni kuishi maisha asili ya uumbaji wa ulimwengu, kwa maana hautendi jambo lolote kwa akili za mazoea bali kwa akili halisi ambazo ndizo zilizokuwa sababu ya mtu kuumbwa.
 
Mpaka sasa naamini mimi naishi na roho ambayo iliwahi kuwepo

mimi ni kijana naweza sema ni GEN Z lakini kila nikiwa napiga story na vijana wezangu nahisi kabisa kuna generation gap between me and them

Lakini nikiwa naongea na wazee au watu walionizidi umri wanakuwa wakiniona kama ni genius na muelewa sana pia upendwa na wazee kiufupi ni kwamba.

The more I talk to people of my age I realise I have a generational gap with my own generation

Vipi kuhusu hili mtaalam.

Maana mimi ni moja kati ya vijana ambao napenda sana kufuga ingawa naishi mjini lakini napenda wanyama na nature kwa ujumla mpaka sasa niliona kama maisha yangu yanafaa kuwepo kijijini

Lakini kila nikikaa na vijana wenzangu nikawaambia kuhusu maswala ya nature ufugaji na kadhalika huwa wananiona kama nina akili nyingi lakini mi kama na data




Thecoder
Thecoder
Thecoder
 
upo sahihi, na hiyo ndio nguvu ya kuishi maisha ya rohoni... kuishi maisha ya rohoni ni kuishi maisha asili ya uumbaji wa ulimwengu, kwa maana hautendi jambo lolote kwa akili za mazoea bali kwa akili halisi ambazo ndizo zilizokuwa sababu ya mtu kuumbwa.
Thecoder uko wapi kwani.....
 
Mpaka sasa naamini mimi naishi na roho ambayo iliwahi kuwepo

mimi ni kijana naweza sema ni GEN Z lakini kila nikiwa napiga story na vijana wezangu nahisi kabisa kuna generation gap between me and them

Lakini nikiwa naongea na wazee au watu walionizidi umri wanakuwa wakiniona kama ni genius na muelewa sana pia upendwa na wazee kiufupi ni kwamba.

The more I talk to people of my age I realise I have a generational gap with my own generation

Vipi kuhusu hili mtaalam.

Maana mimi ni moja kati ya vijana ambao napenda sana kufuga ingawa naishi mjini lakini napenda wanyama na nature kwa ujumla mpaka sasa niliona kama maisha yangu yanafaa kuwepo kijijini

Lakini kila nikikaa na vijana wenzangu nikawaambia kuhusu maswala ya nature ufugaji na kadhalika huwa wananiona kama nina akili nyingi lakini mi kama na data




Thecoder
Thecoder
Thecoder
Jitafutie muda wa kukaa mwenyewe katika utulivu wa akili kuna vitu vingi sana utavuvuta ndani yako na huo uwezo ambao wanauona uko nao sasa utaongezeka zaidi.

Kati ya dalili moja wapo ya kugundua kama ulishawahi kuwepo hapa au laa ni hiyo ya kuwa na machaguo ya rika kwamba wewe mwenyewe tu ukikaa na watu wa rika lako unaona kama si watu sahihi ila ukikaa na watu wenye umri mkubwa kuliko wewe unajiona unafurahia sana maongezi lakini pia ukikaa na watu wa rika lako wanakuona kama uko na ukale fulani ambao hauendani na wao so automatic wanakua hawavutiwi sana na wewe.

Jitahidi ufuge.
 
Back
Top Bottom