Thecoder
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,590
- 4,244
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA TANO.
Wakati unaenda kwa mganga au unaenda kuombewa au kupigwa dua kanisani au msikitini, kinachoombewa si hatima ila kinachoombewa ni nyota.
Nyota iko ndani ya nguvu zako za asili, kwahiyo hizi dua au maombi huwa zinanyanyua mitetemo hasi au chanya ya nguvu za asili ambazo ziko ndani yako.
Kwakufanya hivi ni kwamba ulinzi unaongezeka kwako ila sasa ule uwezo wako wa kipato unaweza usiongezeke au ukaongezeka sana na hii hutegemeana na wewe kama umeanza kuifuata ile njia ya hatima yako au bado, kama umeanza kuifuata basi baada ya hayo maombi au dua mambo yako yatakwenda vizuri sana kwa maana ile mitetemo ya mfumo nyota kutoka ulimwengu wa juu inakua iko juu sana na hapa ndio huwa watu wanasema nyota inang'aa. (Nadhani huwa mnawaskiaga watu wakisema ngoja nikasafishe nyota kidogo kwa maana mambo yangu kama yamesimama hivi) ila kama haujaanza kuielekea ile njia ya hatima yako basi kuwa na uhakika watakuombea na kukupiga dua sana ila hautakua na yale mafanikio ambayo wewe unayatarajia.
Sasa kwanini hatima huwa haiombewi au kupigwa dua ni kwamba hatima ni jambo la kiroho ambalo linamuunganiko na dunia hii ya damu na nyama ila nguvu za asili ni jambo la kiroho ambalo linamuunganiko na ulimwengu wa juu, chukulia huu mfano, mwanajeshi aliyevitani akitaka backup kutoka katika nchi yake yaani makao makuu huwa anatumia redio call kuwasiliana na watu wa makao makuu basi na wewe unapotaka backup kutoka kwa malaika walio katika mfumo nyota wako basi utatumia hayo maombi au dua au matambiko au chochote kile ambacho kimefanikiwa kunyanyua nguvu zako za asili na mara tu unavyofanya hivi basi majibu huwa yanarudi kutoka katika huo ulimwengu wa juu hadi upande wako wa kiroho na kutoka upande wako wa kiroho hadi kwenye dunia hii ya damu na nyama kupitia kiunganishi cha umiliki wa fedha na mali ambacho ni hatima, kwahiyo maombi yote ya kiroho huwa yanaishia kwenye ulimwengu wa kiroho na kutokea pale ndio kiunganishi cha kutokea rohoni hadi ulimwenguni hapa cha mahitaji ya hayo maombi kinapokea, kwahiyo mahitaji ya yale maombi ya umiliki wa mali na fadha kiunganishi chake ndio hatima.
Na hapa ndio nilikuambia sasa kwamba unapoomba maombi ya fedha majibu yake huwa yanarudi moja kwa moja kwenye hatima yako na hapa haijarishi wewe upo huko au haupo huko ila yenyewe yanaenda tu moja kwa moja kama vile mtu aliyeagiza bidhaa mtandaoni na akatoa address yake full basi mtu wa delivery atakachofanya ni kuleta mzigo kwenye address husika bila kujali wewe upo au haupo.
Pia naomba niseme hili jambo hapa, kwamba njia ya kusafisha nyota na kuichafua pia inaweza kufanywa na tendo la ndoa.
Tendo la ndoa ni tendo ambalo hufanyika kwa njia ya mwili wa damu na nyama ila liko na muunganiko wa moja kwa moja na upande wako wa kiroho.
Kila nguvu huwa inamiiko na nguvu hii ya asili miiko yake ni moja na tendo la ndoa, naomba nieleweke hapa kwanza, simaanishi kwamba tendo la ndoa ni jambo baya ila namaanisha si kila mtu afaa kukutana na wewe kimwili yaani kufanya tendo hilo la ndoa.
Kiasili mwanamke aliumbwa kuja kuongeza utimilifu kwa mwanaume hapa duniani, na moja kati ya kitu ambacho mwanamke anaweza kuongeza kwa mwanaume ni mitetemo ya mfumo nyota.
Na si tu mwanamke ndio mwenye uwezo huo wa kuongeza hiyo mitetemo ya mfumo nyota bali hata mwanaume anaouwezo wa kumuongezea mwanamke hiyo mitetemo lakini kiasili kwakua mwanaume ndio mtafutaji na ndio provider basi haifai mwanaume amuongezee mwanamke mitetemo ya mfumo nyota bali yafaa mwanamke ndio afanye hivyo kwa mumewe ili azidi kuifanya nyota ya mumewe iwake zaidi.
Sasa kwakua watu tumeundwa kwa mifumo nyota tofauti tofauti basi pia kaa ukijua kuna watu ambao wanazaliwa wakiwa na utimilifu katika mitetemo ya mifumo nyota yao na hawa huwa tunawaita wachangiaji yaani donors au powerbank.
Lakini pia kuna watu wanazaliwa huku mifumo nyota yao ikiwa si mitimilifu na hawa ndio huwa tunawaita wapokeaji yaani receivers au simu, na watu hawa pia huku kukosa utimilifu baina ya mtu na mtu huwa kunatofautiana kwahiyo huyu anaweza akawa na kasoro hii na huyu akawa na kasoro hii.
Na ninaposema utimilifu na kutokua na utimilifu namaanisha kwamba watu ambao wako timilifu kwenye mfumo nyota wao pindi wanapounganisha mitetemo inakua ya hali ya juu hadi kupelekea nyota kung'aa sana kama umeme ambao ulikata halafu ukarudi kwa wingi na wale ambao hawako na utimilifu huwa nyota zao hazing'ai sana ni kama umeme ulikata halafu ukarudi mdogo sana.
Kitu cha ajabu ni kwamba nilikwambia mwanzo kwamba wale timilifu ndio madonor ila pia kuna nyakati hata watu ambao hawako timilifu huwa wanakua madonor hasa wanapokutana na watu ambao si watimilifu pia.
Sasa angalia hapo yaani wewe umenyanyua nyota yako ikawa inang'aa japo kwa kufifia fifia halafu katika huo huo mfifio anakuja mtu anazidi kukunyonya ili nyota yako izidi kufifia zaidi.
Anyway turudi kwenye mada, kwamba kwakua watu ambao sio watimilifu huwa wanakuja na kasoro za aina tofauti tofauti basi pia hata wale watu wakuwapa huo utimilifu huwa wanakuja wakiwa wa aina tofauti tofauti.
Kwahiyo provider mwenzangu nakuasa hapa kwamba kutokana na jambo hilo ni kwamba si kila mwanamke hapa duniani amekuja kwaajiri ya kukupa utimilifu wewe kwahiyo unatakiwa kuwa makini sana na mwanamke ambae unashiriki nae tendo (hii nitailetea kipande chake cha ziada kwa maana nikiiweka hapa kwa upana itafanya hili andiko liwe refu sana na litakuchosha ila nimeweka hapa kwa uchache ili uelewe kwamba tendo la ndoa laweza kuwa njia mbadala ya kusafisha nyota).
Ila kwa sasa niseme tu kwamba...
Mifumo nyota huwa inatofautiana baina ya mtu na mtu hasa kulingana na nguvu ya asili iliyopo ndani mwake, kwahiyo basi hii inamaanisha kwamba hata njia za kufanikiwa kwenye kuzinyanyua hizi nguvu ili nyota ing'ae huwa hazifanani, sasa how? Soma hapo chini.
Chukulia mfano wewe unataka kupika ugali, ukaenda kununua unga robo na wakati huo huo jikoni umebandika sufuria ya kilo kumi niambie hapa ugali utapatikana? Jibu ni hapana na inawezekana hata uji usipatikane pia, basi hivyo ndivyo ilivyo hata kwenye hizi nguvu, nilikuambia nguvu chanya inawakilisha nuru na nguvu hasi inawakilisha giza. Sasa ikitokea mtu wa nuru akaenda kutafuta mafanikio kwenye giza kinachotokea ni kwamba kama nuru itakua na nguvu kuliko giza basi nuru italifunika giza na yenyewe itaangaza na kama giza litakua na nguvu kuliko nuru basi giza litafunika nuru na lenyewe litatawala na endapo giza na nuru vyote vitakua na nguvu sawa, basi vitaweka hali ya kufifia fulani, yaani giza sio giza wala mwanga sio mwanga.
Na wakati huo huo, ili uweze kufanikiwa unatakiwa kunyanyua nguvu iliyopo ndani ya roho yako ili iweze kutoa mitetemo ya juu sana ambayo itapelekea uweze kuwasiliana moja kwa moja na huo ulimwengu wa kiroho pamoja na kufuata ile njia ielekeayo kwenye hatima yako, sasa ukiuchukua mwanga ukauongezea giza unachokifanya ni kufanya mwanga uendelee kufifia na si kuufanya uendelee kunyanyuka na ukichukua giza ukalipeleka kwa mwanga utakachokifanya ni kulifanya lififie na si kuliongezea mitetemo hasi na hii ndio hufanya watu hawa waweze kudidimia badala ya kunyanyuka pindi wanapofuata njia ambazo si ziwapasazo kupita.
Lakini mtu mwenye nguvu zenye uwiano katika usawa kwenye upande giza na nuru ukimpeleka kwenye njia za giza lile giza litaenda kufifiisha nuru na kuliongezea nguvu giza liliopo na kumfanya mtu huyu afanikiwe na ukimchukua ukampeleka kwenye nuru basi nuru itaenda kulidhoofisha giza na kuongeza nuru kwa nuru iliyopo na hapa pia utaona anafanikiwa kwa nguvu.
Najua unatamani uwe kwenye hii sifa ya kuwa na nguvu sawa ya nuru na giza lakini ukijiangalia si unaona unavyoteseka kiuchumi, sasa wenzio watu wenye hizo sifa hawateseki kiuchumi labda uwe haujawahi kwenda kwenye nyumba za ibada kabisa pamoja na kwa waganga ila kama unazosifa zote za watu wenye sifa hizi basi umasikini wako unatokana na uvivu wako wakutokutaka kutafuta ufumbuzi wa hali yako ya kiuchumi, au ni kwasababu hujajengewa misingi ya aina yoyote hapo awali, na hata sasa hujafanikiwa kunyanyua nguvu yoyote iliyopo ndani yako yaani kati ya hiyo nguvu hasi na nguvu chanya kwahiyo jitahidi unyanyue moja ila nakushauri sana unyanyue nguvu chanya ili uweze kuishi kwa kufuata sheria za ulimwengu kwani utafanikiwa zaidi.
Watu wenye nguvu hasi kwa wingi na nguvu chanya kidogo na hawa wenye nguvu hasi zilizobalance kiusawa na zile nguvu chanya huwa ndio wanaongoza kufanikiwa, kwasababu huwa kufungua siri za nguvu kwenye ulimwengu wa giza zipo moja kwa moja sana kuliko jinsi ya kufungua siri katika upande chanya yaani ulimwengu wa nuru. Elimu ya kiroho inayojihusisha na mambo ya upande wa giza, siri zake ziko wazi sana na ndio maana iko na wataalam wengi wanaoijua kwahiyo hii imefanya iwe rahisi kwa watu wa upande huo kuweza kupata msaada wa haraka pale wanapohitaji.
Pia hata masharti yake mengi sio yale ya kiroho ila ni yale yanayoonekana katika ulimwengu huu wa damu na nyama kwahiyo hii inafanya watu wengi wa upande huo wayafuate kwa uhakika kwa maana wanakua wanajua kwamba nikifanya hivi ni dhambi na nikifanya hivi si dhambi, wakati upande wa nuru masharti yake mengi ni yale ya rohoni kwahiyo unaweza ukafanya jambo usiwe na uhakika kama umevunja miiko au haujavunja, na ndio maana wengi huwa inawawia vigumu kujua kama wamejinajisi au laa. Na endapo utajua umejinajisi basi tiba yake inaenda kiroho pia, kwahiyo nayo huwa ni ngumu kujua kama umeshafunguliwa au bado, wakati wale wa gizani huwa wakijinajisi tiba zao nyingi ni zile zinazoonekana, kwamba waweza ukaambiwa tiba ya unajisi huu yafaa ulete damu ya kondoo au mnyama yoyote na ukishapeleka basi unafanyiwa dawa na unatoka ukiwa na uhakika wa kusafishika kwenye unajisi ule uliokua nao.
Ukitaka kufungua siri za upande wa nuru unaenda kwa shekhe au mchungaji au padre, na wote hawa watakupa njia tofauti tofauti lakini kubwa ya maombi, na kama tujuavyo ufunguzi wa mambo ya kiroho hautokei kama mtu anaetaka kufunguliwa akiwa hajaiweka roho yake katika hali ya utayari wa kupokea huo ufunguzi wenyewe, na utayari huu mara nyingi huwa unadhihirika kupitia imani, sasa ikitokea ukakosa imani basi mambo yote yatakayo kuwa yanatendeka itakua ni kazi bure, ila ikitokea ukawa na imani kubwa juu ya mambo haya ya kiroho na kuamini mafanikio kwanjia hiyo yanawezekana, basi ukifanikiwa kwa njia hiyo utaenda kuwa na ulinzi wa kutosha utokao kwenye ulimwengu huo wa kiroho. Au kuna wakati huwa inatokea kwamba, wewe ukawa na imani iliyo tukuka, ila ukakutana na watumishi wa Mungu ambao ni walaghai wale ambao hawana kipawa kinachoelekea kwenye hiyo hatima, ila kwakua wako na nguvu hasi zilizo katika uwiano sawa na chanya wakaamua kufoji hatima, basi hapa watakua wanakutia unajisi huku wakikuacha ukididimia kiuchumi.
Mwanzo nilikwambia mtu anaweza kugundua kipawa kitakachompeleka kwenye hatima yake bila ya kunyanyua nguvu za asili zilizomo ndani yake na akafanikiwa, lakini shida ni kwamba kugundua kipawa bila kuwa na ulinzi ni rahisi sana watu kukunajisi, nadhani umeona hapo juu, kwamba kuna watu wamezaliwa hapa duniani kwa lengo la kufanya uharibifu kwenye kila eneo, sasa na kitu kibaya zaidi hawa watu wanaopenda kufanya uharibifu ndio watu ambao huwa ni wakwanza kabisa kujua au kutambua kwamba mtu fulani tayari ameshaipata ile njia inayoenda kwenye hatima yake na muda mchache baadae ataenda kuwa mtu mwenye nguvu au mtu mkubwa sana hapa duniani kiasi cha kunizidi mimi kila kitu, sasa kwakua hawa watu huwa ni watu waliojawa na chuki pamoja na roho mbaya kwa haraka sana wanakunajisi au wanakuroga kama watu wengi walivyozoea kuita, sasa ili uweze kukwepa mitego yao basi unatakiwa ujiwekee ulinzi wa kiroho na ulinzi wa kiroho utaupata kwa kufuata kanuni na taratibu za ulimwengu katika upande huo wa kiroho na kanuni hizi pamoja na taratibu huwa zinapatikana sana kwenye nyumba za ibada.
Na sio hili tu, bali pia unatakiwa uwe mtu mnyenyekevu kwa Mungu wako pamoja na kwa ulimwengu unaoishi, kwasababu endapo utajisahau ni rahisi sana kutoka nje ya reli kwasababu nguvu chanya hazifungamani moja kwa moja na mambo ya kidunia kwahiyo pindi utakapofanikiwa kuziamsha unakua ni mtu mwenye nguvu sana lakini pia ili uendelee kulinda nguvu zako zisiingie kwenye uharibifu basi yakupasa uishi kulingana na matakwa ya imani yako.
Ukienda kinyume na mambo ya imani iliyotumika kuinyanyua hiyo nguvu chanya iliyopo ndani yako basi moja kwa moja utapoteza uelekeo kwa maana nguvu zako zitapungua na hapa unaweza usitetereke kifedha kwasababu bado utakua upo kwenye njia inayoelekea kwenye hatima yako lakini hapa wale watu wenye nia ovu wakitaka kukutia unajisi wanafanikiwa kwa haraka sana.
Nguvu zote za asili zilizopo ndani yetu huwa zinamiiko na miiko ya nguvu hizi huwa zinaanza kutekelezwa pale tu zinapoamshwa, na miiko yake mara nyingi ni kuhakikisha unatekeleza kanuni na taratibu za imani iliyotumika kuinyanyua hiyo nguvu iliyopo ndani yako, na hapa ndio utakuta kuna watu wamenyanyua nguvu zao hasi kupitia kwa waganga wenye uwezo wa kunyanyua nguvu hizo, na baada ya kuzinyanyua wanapewa masharti kadha wa kadha, unakuta mtu anaambiwa asinywe pombe kwa maana mizimu haimuhitaji kufanya hivyo au unakuta mtu anaambiwa atoe sadaka kila baada ya muda fulani na hapa sio sadaka ya damu tu, bali wapo ambao huambiwa watoe sadaka za kuwasaidia watu wenye uhitaji wa chakula mavazi na fedha, na wale waliopo kwenye nguvu chanya kama wamezifungua nguvu zao kupitia msikiti au kwa kupigwa dua na mashekhe ndio utakuta watu hawa wanaambiwa kila ikifika ijumaa hawatakiwi kufungua maduka na ni lazima waende kwenye ibada na kadhalika.
Kwahiyo endapo wewe ukishindwa kufuata hizo kanuni na taratibu za imani ya kiroho iliyotumika kuinyanyua nguvu iliyopo ndani yako, basi kuwa na hakika utajitia unajisi wewe mwenyewe na hii itaenda kufanya mwisho wako kuwa mbaya.
Licha ya utofauti huo ila kuna kitu hapa nataka nikwambie, ya kwamba wapo watu wenye nguvu chanya ambao waliwahi kupata changamoto za kifedha yaani baada ya kuanza kuiendea ile njia inayoelekea kwenye hatima yao huku wakiwa bado hawajafanikiwa kuinyanyua ile nguvu yao ya asili kwaajiri ya ulinzi walikutana na changamoto ya kufanyiwa unajisi yaani kurogwa, na baada ya kurogwa waliamua kwenda kwa wataalam wenye ujuzi na mambo ya kiroho lakini upande wa giza na wakafanikiwa kufunguliwa.
Sasa hii huwa inatokea hivi, kwamba wewe asili yako ni nuru ila nuru hii bado hujaifanya ichomoze ila umebahatika kujua hatima yako ya kuwa hapa duniani na umeanza kuifuata, wakati unaifuata hauna ulinzi na hapo akatokea mtu akakuwekea ukuta au giza katikati ya njia yako na hii hupelekea mito yote ya baraka ishindwe kupitisha maji kuja kwako na hapa ndio huwa watu wanasema nyota yako imechafuliwa, na ukienda kwa mtaalam mwenye ujuzi wa elimu hiyo ya mambo ya giza ambae ni mganga basi atakachofanya ni kuuondoa ule ukuta uliopo kwenye safari yako na wala haangaiki na wewe moja kwa moja, na akifanikiwa kuuondoa ndio pale sasa unakuta mambo yanarudi upya kama mwanzo yaani unafunguliwa, na hapa utasema yule mtaalam ni kiboko, wakati ki uhalisia yeye ni mtu wa giza kwa hiyo alichofanya ni kujihusisha na yale mambo ya giza ambayo yaliwekwa katikati ya safari yako, na wala si kujihusisha na wewe moja kwa moja.
Ubaya wa hiyo njia ni kwamba huwa inawafanya watu wengi wawe ni washirikina sana, kwasababu hawana ulinzi wa kiroho na waganga huwa hawawezi kuwapa ulinzi ili wakienda wasirogwe au kutiwa unajisi tena, na hii ndio huwa inapelekea kila wakienda kwenye maeneo yao ya kazi wanakaa kidogo wanawekewa uzibe tena kwenye zile njia zao, kwa hiyo watarudi tena kwa mganga na hii ndio inakua hivi maisha yao yote hasa kama hawatoshtuka mapema kutafuta namna ya kuinyanyua ile nguvu ya asili iliyopo ndani yao ili wapate ulinzi wa milele.
Pia kuna watu wengine ambao wanatokea upande huo huo wa nguvu chanya ila walishawahi kwenda kwa mganga na wakafanikiwa kutatua shida zao.
Hapa sasa nazungumzia yule mtu ambae hajanyanyua nguvu za asili zilizomo ndani yake na wala hajui hatima yake ni nini, kwa hiyo anapitia kipindi kigumu sana cha maisha ya utafutaji wa fedha, na anaamua aende kwa mganga ambae yeye ni mtaalam wa mambo ya gizani, lakini asili ya waganga wengi huwa hawasemi ukweli kwamba hawezi kukusaidia hasa unapoenda na shida inayohusiana na maswala ya umiliki wa fedha na mali, kwakua wanajua kila mtu katika majira fulani fulani kwenye mwaka ni lazima mto wa vipawa vyake unaoelekea kwenye ile hatima kuu lazima ufurike hadi kufikia zile kingo zake zipasuke na kuanza kusambaza hizo baraka maeneo mbalimbali na kipindi hiki ndio ambacho huwa ni cha bahati, kwani shida zote za kifedha ulizo nazo huwa zinapata ufumbuzi kwenye nyakati hizi, sasa mganga yeye atakachofanya ni kuendelea kukupa dawa huku akiendelea kukupangia tarehe kwamba katumie hii siku saba kama hujaona mafanikio urudi, na mambo yatakua hivi hadi siku moja utaona mafanikio kwa maana yale majira yako ya bahati yanapofika na yanakukuta unatumia dawa za mganga wako msanii, na wewe kwakua haujui unaamini kweli mganga ameweza kupata ufumbuzi wa tatizo lako wakati kiuhalisia hata ungekua umekaa ndani wakati wa majira hayo huwa fedha zinakufuata katika hali ya kushangaza sana na ambayo hujawahi itarajia.
Neno la kuchukua hapa ni kwamba usikubali kupumbazwa na haya mambo, kwa maana hayana muendelezo na yatazidi kukuchelewesha kwenye kufikia lile lengo kuu ambalo wewe umeumbwa uje ulitekeleze hapa duniani, kwa hiyo jitahidi kujitafuta kuanzia sasa ili uweze kujua kipawa chako ni kipi na uanze kukifuata ili ukaishi yale maisha ya hatima yako.
Na pia ningependa nieleweke kwamba, ninaposema imani za kiroho simaanishi kwamba ni lazima ziwe za kanisani, msikitini au kilingeni ila imani za kiroho zipo nyingi kwa maana ukienda India utakutana na watu wenye imani tofauti tofauti za kushangaza, pia ukienda China utakutana na imani nyingi za tofauti tofauti na za kushangaza na hata wewe kwenye ukoo wenu huwa mko na imani zenu tofauti tofauti na za kushangaza, kwahiyo hizi imani zote endapo zikifanikiwa kuamsha ile nguvu iliyopo ndani yako, basi jua nguvu yako ya asili uliyo nayo inafungamana moja kwa moja na imani hiyo kwahiyo unachotakiwa kufanya ni kufuata taratibu za hiyo imani na kama wewe nguvu uliyo nayo si ya upande huo utahangaika kwenye huo upande miaka na miaka ila hautafanikiwa kuinyanyua ile nguvu iliyoko ndani yako.
...Nitaishia hapa kwenye hiki kipande na tukutane kwenye kipande kinachofuata. Bado nitaendelea kuwepo hapa kwenye nguvu za asili kwa maana hii ndio brash kwenye kiatu ulichopaka kiwi na ndio clear kwenye gari ulilopaka rangi, ni mbolea kwa mazao yako shambani, pia ni maji kwenye kiu yako kwa maana kwamba kwa hatima pekee utafanikiwa ila kwa hatima jumlisha nguvu za asili utafanikiwa zaidi.
Wakati unaenda kwa mganga au unaenda kuombewa au kupigwa dua kanisani au msikitini, kinachoombewa si hatima ila kinachoombewa ni nyota.
Nyota iko ndani ya nguvu zako za asili, kwahiyo hizi dua au maombi huwa zinanyanyua mitetemo hasi au chanya ya nguvu za asili ambazo ziko ndani yako.
Kwakufanya hivi ni kwamba ulinzi unaongezeka kwako ila sasa ule uwezo wako wa kipato unaweza usiongezeke au ukaongezeka sana na hii hutegemeana na wewe kama umeanza kuifuata ile njia ya hatima yako au bado, kama umeanza kuifuata basi baada ya hayo maombi au dua mambo yako yatakwenda vizuri sana kwa maana ile mitetemo ya mfumo nyota kutoka ulimwengu wa juu inakua iko juu sana na hapa ndio huwa watu wanasema nyota inang'aa. (Nadhani huwa mnawaskiaga watu wakisema ngoja nikasafishe nyota kidogo kwa maana mambo yangu kama yamesimama hivi) ila kama haujaanza kuielekea ile njia ya hatima yako basi kuwa na uhakika watakuombea na kukupiga dua sana ila hautakua na yale mafanikio ambayo wewe unayatarajia.
Sasa kwanini hatima huwa haiombewi au kupigwa dua ni kwamba hatima ni jambo la kiroho ambalo linamuunganiko na dunia hii ya damu na nyama ila nguvu za asili ni jambo la kiroho ambalo linamuunganiko na ulimwengu wa juu, chukulia huu mfano, mwanajeshi aliyevitani akitaka backup kutoka katika nchi yake yaani makao makuu huwa anatumia redio call kuwasiliana na watu wa makao makuu basi na wewe unapotaka backup kutoka kwa malaika walio katika mfumo nyota wako basi utatumia hayo maombi au dua au matambiko au chochote kile ambacho kimefanikiwa kunyanyua nguvu zako za asili na mara tu unavyofanya hivi basi majibu huwa yanarudi kutoka katika huo ulimwengu wa juu hadi upande wako wa kiroho na kutoka upande wako wa kiroho hadi kwenye dunia hii ya damu na nyama kupitia kiunganishi cha umiliki wa fedha na mali ambacho ni hatima, kwahiyo maombi yote ya kiroho huwa yanaishia kwenye ulimwengu wa kiroho na kutokea pale ndio kiunganishi cha kutokea rohoni hadi ulimwenguni hapa cha mahitaji ya hayo maombi kinapokea, kwahiyo mahitaji ya yale maombi ya umiliki wa mali na fadha kiunganishi chake ndio hatima.
Na hapa ndio nilikuambia sasa kwamba unapoomba maombi ya fedha majibu yake huwa yanarudi moja kwa moja kwenye hatima yako na hapa haijarishi wewe upo huko au haupo huko ila yenyewe yanaenda tu moja kwa moja kama vile mtu aliyeagiza bidhaa mtandaoni na akatoa address yake full basi mtu wa delivery atakachofanya ni kuleta mzigo kwenye address husika bila kujali wewe upo au haupo.
Pia naomba niseme hili jambo hapa, kwamba njia ya kusafisha nyota na kuichafua pia inaweza kufanywa na tendo la ndoa.
Tendo la ndoa ni tendo ambalo hufanyika kwa njia ya mwili wa damu na nyama ila liko na muunganiko wa moja kwa moja na upande wako wa kiroho.
Kila nguvu huwa inamiiko na nguvu hii ya asili miiko yake ni moja na tendo la ndoa, naomba nieleweke hapa kwanza, simaanishi kwamba tendo la ndoa ni jambo baya ila namaanisha si kila mtu afaa kukutana na wewe kimwili yaani kufanya tendo hilo la ndoa.
Kiasili mwanamke aliumbwa kuja kuongeza utimilifu kwa mwanaume hapa duniani, na moja kati ya kitu ambacho mwanamke anaweza kuongeza kwa mwanaume ni mitetemo ya mfumo nyota.
Na si tu mwanamke ndio mwenye uwezo huo wa kuongeza hiyo mitetemo ya mfumo nyota bali hata mwanaume anaouwezo wa kumuongezea mwanamke hiyo mitetemo lakini kiasili kwakua mwanaume ndio mtafutaji na ndio provider basi haifai mwanaume amuongezee mwanamke mitetemo ya mfumo nyota bali yafaa mwanamke ndio afanye hivyo kwa mumewe ili azidi kuifanya nyota ya mumewe iwake zaidi.
Sasa kwakua watu tumeundwa kwa mifumo nyota tofauti tofauti basi pia kaa ukijua kuna watu ambao wanazaliwa wakiwa na utimilifu katika mitetemo ya mifumo nyota yao na hawa huwa tunawaita wachangiaji yaani donors au powerbank.
Lakini pia kuna watu wanazaliwa huku mifumo nyota yao ikiwa si mitimilifu na hawa ndio huwa tunawaita wapokeaji yaani receivers au simu, na watu hawa pia huku kukosa utimilifu baina ya mtu na mtu huwa kunatofautiana kwahiyo huyu anaweza akawa na kasoro hii na huyu akawa na kasoro hii.
Na ninaposema utimilifu na kutokua na utimilifu namaanisha kwamba watu ambao wako timilifu kwenye mfumo nyota wao pindi wanapounganisha mitetemo inakua ya hali ya juu hadi kupelekea nyota kung'aa sana kama umeme ambao ulikata halafu ukarudi kwa wingi na wale ambao hawako na utimilifu huwa nyota zao hazing'ai sana ni kama umeme ulikata halafu ukarudi mdogo sana.
Kitu cha ajabu ni kwamba nilikwambia mwanzo kwamba wale timilifu ndio madonor ila pia kuna nyakati hata watu ambao hawako timilifu huwa wanakua madonor hasa wanapokutana na watu ambao si watimilifu pia.
Sasa angalia hapo yaani wewe umenyanyua nyota yako ikawa inang'aa japo kwa kufifia fifia halafu katika huo huo mfifio anakuja mtu anazidi kukunyonya ili nyota yako izidi kufifia zaidi.
Anyway turudi kwenye mada, kwamba kwakua watu ambao sio watimilifu huwa wanakuja na kasoro za aina tofauti tofauti basi pia hata wale watu wakuwapa huo utimilifu huwa wanakuja wakiwa wa aina tofauti tofauti.
Kwahiyo provider mwenzangu nakuasa hapa kwamba kutokana na jambo hilo ni kwamba si kila mwanamke hapa duniani amekuja kwaajiri ya kukupa utimilifu wewe kwahiyo unatakiwa kuwa makini sana na mwanamke ambae unashiriki nae tendo (hii nitailetea kipande chake cha ziada kwa maana nikiiweka hapa kwa upana itafanya hili andiko liwe refu sana na litakuchosha ila nimeweka hapa kwa uchache ili uelewe kwamba tendo la ndoa laweza kuwa njia mbadala ya kusafisha nyota).
Ila kwa sasa niseme tu kwamba...
Mifumo nyota huwa inatofautiana baina ya mtu na mtu hasa kulingana na nguvu ya asili iliyopo ndani mwake, kwahiyo basi hii inamaanisha kwamba hata njia za kufanikiwa kwenye kuzinyanyua hizi nguvu ili nyota ing'ae huwa hazifanani, sasa how? Soma hapo chini.
KWANINI MTU MWENYE NGUVU CHANYA AKIFUATA NJIA ZA MTU MWENYE NGUVU HASI HAWEZI KUFANIKIWA NA KINYUME CHAKE.
Chukulia mfano wewe unataka kupika ugali, ukaenda kununua unga robo na wakati huo huo jikoni umebandika sufuria ya kilo kumi niambie hapa ugali utapatikana? Jibu ni hapana na inawezekana hata uji usipatikane pia, basi hivyo ndivyo ilivyo hata kwenye hizi nguvu, nilikuambia nguvu chanya inawakilisha nuru na nguvu hasi inawakilisha giza. Sasa ikitokea mtu wa nuru akaenda kutafuta mafanikio kwenye giza kinachotokea ni kwamba kama nuru itakua na nguvu kuliko giza basi nuru italifunika giza na yenyewe itaangaza na kama giza litakua na nguvu kuliko nuru basi giza litafunika nuru na lenyewe litatawala na endapo giza na nuru vyote vitakua na nguvu sawa, basi vitaweka hali ya kufifia fulani, yaani giza sio giza wala mwanga sio mwanga.
Na wakati huo huo, ili uweze kufanikiwa unatakiwa kunyanyua nguvu iliyopo ndani ya roho yako ili iweze kutoa mitetemo ya juu sana ambayo itapelekea uweze kuwasiliana moja kwa moja na huo ulimwengu wa kiroho pamoja na kufuata ile njia ielekeayo kwenye hatima yako, sasa ukiuchukua mwanga ukauongezea giza unachokifanya ni kufanya mwanga uendelee kufifia na si kuufanya uendelee kunyanyuka na ukichukua giza ukalipeleka kwa mwanga utakachokifanya ni kulifanya lififie na si kuliongezea mitetemo hasi na hii ndio hufanya watu hawa waweze kudidimia badala ya kunyanyuka pindi wanapofuata njia ambazo si ziwapasazo kupita.
Lakini mtu mwenye nguvu zenye uwiano katika usawa kwenye upande giza na nuru ukimpeleka kwenye njia za giza lile giza litaenda kufifiisha nuru na kuliongezea nguvu giza liliopo na kumfanya mtu huyu afanikiwe na ukimchukua ukampeleka kwenye nuru basi nuru itaenda kulidhoofisha giza na kuongeza nuru kwa nuru iliyopo na hapa pia utaona anafanikiwa kwa nguvu.
Najua unatamani uwe kwenye hii sifa ya kuwa na nguvu sawa ya nuru na giza lakini ukijiangalia si unaona unavyoteseka kiuchumi, sasa wenzio watu wenye hizo sifa hawateseki kiuchumi labda uwe haujawahi kwenda kwenye nyumba za ibada kabisa pamoja na kwa waganga ila kama unazosifa zote za watu wenye sifa hizi basi umasikini wako unatokana na uvivu wako wakutokutaka kutafuta ufumbuzi wa hali yako ya kiuchumi, au ni kwasababu hujajengewa misingi ya aina yoyote hapo awali, na hata sasa hujafanikiwa kunyanyua nguvu yoyote iliyopo ndani yako yaani kati ya hiyo nguvu hasi na nguvu chanya kwahiyo jitahidi unyanyue moja ila nakushauri sana unyanyue nguvu chanya ili uweze kuishi kwa kufuata sheria za ulimwengu kwani utafanikiwa zaidi.
Watu wenye nguvu hasi kwa wingi na nguvu chanya kidogo na hawa wenye nguvu hasi zilizobalance kiusawa na zile nguvu chanya huwa ndio wanaongoza kufanikiwa, kwasababu huwa kufungua siri za nguvu kwenye ulimwengu wa giza zipo moja kwa moja sana kuliko jinsi ya kufungua siri katika upande chanya yaani ulimwengu wa nuru. Elimu ya kiroho inayojihusisha na mambo ya upande wa giza, siri zake ziko wazi sana na ndio maana iko na wataalam wengi wanaoijua kwahiyo hii imefanya iwe rahisi kwa watu wa upande huo kuweza kupata msaada wa haraka pale wanapohitaji.
Pia hata masharti yake mengi sio yale ya kiroho ila ni yale yanayoonekana katika ulimwengu huu wa damu na nyama kwahiyo hii inafanya watu wengi wa upande huo wayafuate kwa uhakika kwa maana wanakua wanajua kwamba nikifanya hivi ni dhambi na nikifanya hivi si dhambi, wakati upande wa nuru masharti yake mengi ni yale ya rohoni kwahiyo unaweza ukafanya jambo usiwe na uhakika kama umevunja miiko au haujavunja, na ndio maana wengi huwa inawawia vigumu kujua kama wamejinajisi au laa. Na endapo utajua umejinajisi basi tiba yake inaenda kiroho pia, kwahiyo nayo huwa ni ngumu kujua kama umeshafunguliwa au bado, wakati wale wa gizani huwa wakijinajisi tiba zao nyingi ni zile zinazoonekana, kwamba waweza ukaambiwa tiba ya unajisi huu yafaa ulete damu ya kondoo au mnyama yoyote na ukishapeleka basi unafanyiwa dawa na unatoka ukiwa na uhakika wa kusafishika kwenye unajisi ule uliokua nao.
Ukitaka kufungua siri za upande wa nuru unaenda kwa shekhe au mchungaji au padre, na wote hawa watakupa njia tofauti tofauti lakini kubwa ya maombi, na kama tujuavyo ufunguzi wa mambo ya kiroho hautokei kama mtu anaetaka kufunguliwa akiwa hajaiweka roho yake katika hali ya utayari wa kupokea huo ufunguzi wenyewe, na utayari huu mara nyingi huwa unadhihirika kupitia imani, sasa ikitokea ukakosa imani basi mambo yote yatakayo kuwa yanatendeka itakua ni kazi bure, ila ikitokea ukawa na imani kubwa juu ya mambo haya ya kiroho na kuamini mafanikio kwanjia hiyo yanawezekana, basi ukifanikiwa kwa njia hiyo utaenda kuwa na ulinzi wa kutosha utokao kwenye ulimwengu huo wa kiroho. Au kuna wakati huwa inatokea kwamba, wewe ukawa na imani iliyo tukuka, ila ukakutana na watumishi wa Mungu ambao ni walaghai wale ambao hawana kipawa kinachoelekea kwenye hiyo hatima, ila kwakua wako na nguvu hasi zilizo katika uwiano sawa na chanya wakaamua kufoji hatima, basi hapa watakua wanakutia unajisi huku wakikuacha ukididimia kiuchumi.
Mwanzo nilikwambia mtu anaweza kugundua kipawa kitakachompeleka kwenye hatima yake bila ya kunyanyua nguvu za asili zilizomo ndani yake na akafanikiwa, lakini shida ni kwamba kugundua kipawa bila kuwa na ulinzi ni rahisi sana watu kukunajisi, nadhani umeona hapo juu, kwamba kuna watu wamezaliwa hapa duniani kwa lengo la kufanya uharibifu kwenye kila eneo, sasa na kitu kibaya zaidi hawa watu wanaopenda kufanya uharibifu ndio watu ambao huwa ni wakwanza kabisa kujua au kutambua kwamba mtu fulani tayari ameshaipata ile njia inayoenda kwenye hatima yake na muda mchache baadae ataenda kuwa mtu mwenye nguvu au mtu mkubwa sana hapa duniani kiasi cha kunizidi mimi kila kitu, sasa kwakua hawa watu huwa ni watu waliojawa na chuki pamoja na roho mbaya kwa haraka sana wanakunajisi au wanakuroga kama watu wengi walivyozoea kuita, sasa ili uweze kukwepa mitego yao basi unatakiwa ujiwekee ulinzi wa kiroho na ulinzi wa kiroho utaupata kwa kufuata kanuni na taratibu za ulimwengu katika upande huo wa kiroho na kanuni hizi pamoja na taratibu huwa zinapatikana sana kwenye nyumba za ibada.
Na sio hili tu, bali pia unatakiwa uwe mtu mnyenyekevu kwa Mungu wako pamoja na kwa ulimwengu unaoishi, kwasababu endapo utajisahau ni rahisi sana kutoka nje ya reli kwasababu nguvu chanya hazifungamani moja kwa moja na mambo ya kidunia kwahiyo pindi utakapofanikiwa kuziamsha unakua ni mtu mwenye nguvu sana lakini pia ili uendelee kulinda nguvu zako zisiingie kwenye uharibifu basi yakupasa uishi kulingana na matakwa ya imani yako.
Ukienda kinyume na mambo ya imani iliyotumika kuinyanyua hiyo nguvu chanya iliyopo ndani yako basi moja kwa moja utapoteza uelekeo kwa maana nguvu zako zitapungua na hapa unaweza usitetereke kifedha kwasababu bado utakua upo kwenye njia inayoelekea kwenye hatima yako lakini hapa wale watu wenye nia ovu wakitaka kukutia unajisi wanafanikiwa kwa haraka sana.
Nguvu zote za asili zilizopo ndani yetu huwa zinamiiko na miiko ya nguvu hizi huwa zinaanza kutekelezwa pale tu zinapoamshwa, na miiko yake mara nyingi ni kuhakikisha unatekeleza kanuni na taratibu za imani iliyotumika kuinyanyua hiyo nguvu iliyopo ndani yako, na hapa ndio utakuta kuna watu wamenyanyua nguvu zao hasi kupitia kwa waganga wenye uwezo wa kunyanyua nguvu hizo, na baada ya kuzinyanyua wanapewa masharti kadha wa kadha, unakuta mtu anaambiwa asinywe pombe kwa maana mizimu haimuhitaji kufanya hivyo au unakuta mtu anaambiwa atoe sadaka kila baada ya muda fulani na hapa sio sadaka ya damu tu, bali wapo ambao huambiwa watoe sadaka za kuwasaidia watu wenye uhitaji wa chakula mavazi na fedha, na wale waliopo kwenye nguvu chanya kama wamezifungua nguvu zao kupitia msikiti au kwa kupigwa dua na mashekhe ndio utakuta watu hawa wanaambiwa kila ikifika ijumaa hawatakiwi kufungua maduka na ni lazima waende kwenye ibada na kadhalika.
Kwahiyo endapo wewe ukishindwa kufuata hizo kanuni na taratibu za imani ya kiroho iliyotumika kuinyanyua nguvu iliyopo ndani yako, basi kuwa na hakika utajitia unajisi wewe mwenyewe na hii itaenda kufanya mwisho wako kuwa mbaya.
Licha ya utofauti huo ila kuna kitu hapa nataka nikwambie, ya kwamba wapo watu wenye nguvu chanya ambao waliwahi kupata changamoto za kifedha yaani baada ya kuanza kuiendea ile njia inayoelekea kwenye hatima yao huku wakiwa bado hawajafanikiwa kuinyanyua ile nguvu yao ya asili kwaajiri ya ulinzi walikutana na changamoto ya kufanyiwa unajisi yaani kurogwa, na baada ya kurogwa waliamua kwenda kwa wataalam wenye ujuzi na mambo ya kiroho lakini upande wa giza na wakafanikiwa kufunguliwa.
Sasa hii huwa inatokea hivi, kwamba wewe asili yako ni nuru ila nuru hii bado hujaifanya ichomoze ila umebahatika kujua hatima yako ya kuwa hapa duniani na umeanza kuifuata, wakati unaifuata hauna ulinzi na hapo akatokea mtu akakuwekea ukuta au giza katikati ya njia yako na hii hupelekea mito yote ya baraka ishindwe kupitisha maji kuja kwako na hapa ndio huwa watu wanasema nyota yako imechafuliwa, na ukienda kwa mtaalam mwenye ujuzi wa elimu hiyo ya mambo ya giza ambae ni mganga basi atakachofanya ni kuuondoa ule ukuta uliopo kwenye safari yako na wala haangaiki na wewe moja kwa moja, na akifanikiwa kuuondoa ndio pale sasa unakuta mambo yanarudi upya kama mwanzo yaani unafunguliwa, na hapa utasema yule mtaalam ni kiboko, wakati ki uhalisia yeye ni mtu wa giza kwa hiyo alichofanya ni kujihusisha na yale mambo ya giza ambayo yaliwekwa katikati ya safari yako, na wala si kujihusisha na wewe moja kwa moja.
Ubaya wa hiyo njia ni kwamba huwa inawafanya watu wengi wawe ni washirikina sana, kwasababu hawana ulinzi wa kiroho na waganga huwa hawawezi kuwapa ulinzi ili wakienda wasirogwe au kutiwa unajisi tena, na hii ndio huwa inapelekea kila wakienda kwenye maeneo yao ya kazi wanakaa kidogo wanawekewa uzibe tena kwenye zile njia zao, kwa hiyo watarudi tena kwa mganga na hii ndio inakua hivi maisha yao yote hasa kama hawatoshtuka mapema kutafuta namna ya kuinyanyua ile nguvu ya asili iliyopo ndani yao ili wapate ulinzi wa milele.
Pia kuna watu wengine ambao wanatokea upande huo huo wa nguvu chanya ila walishawahi kwenda kwa mganga na wakafanikiwa kutatua shida zao.
Hapa sasa nazungumzia yule mtu ambae hajanyanyua nguvu za asili zilizomo ndani yake na wala hajui hatima yake ni nini, kwa hiyo anapitia kipindi kigumu sana cha maisha ya utafutaji wa fedha, na anaamua aende kwa mganga ambae yeye ni mtaalam wa mambo ya gizani, lakini asili ya waganga wengi huwa hawasemi ukweli kwamba hawezi kukusaidia hasa unapoenda na shida inayohusiana na maswala ya umiliki wa fedha na mali, kwakua wanajua kila mtu katika majira fulani fulani kwenye mwaka ni lazima mto wa vipawa vyake unaoelekea kwenye ile hatima kuu lazima ufurike hadi kufikia zile kingo zake zipasuke na kuanza kusambaza hizo baraka maeneo mbalimbali na kipindi hiki ndio ambacho huwa ni cha bahati, kwani shida zote za kifedha ulizo nazo huwa zinapata ufumbuzi kwenye nyakati hizi, sasa mganga yeye atakachofanya ni kuendelea kukupa dawa huku akiendelea kukupangia tarehe kwamba katumie hii siku saba kama hujaona mafanikio urudi, na mambo yatakua hivi hadi siku moja utaona mafanikio kwa maana yale majira yako ya bahati yanapofika na yanakukuta unatumia dawa za mganga wako msanii, na wewe kwakua haujui unaamini kweli mganga ameweza kupata ufumbuzi wa tatizo lako wakati kiuhalisia hata ungekua umekaa ndani wakati wa majira hayo huwa fedha zinakufuata katika hali ya kushangaza sana na ambayo hujawahi itarajia.
Neno la kuchukua hapa ni kwamba usikubali kupumbazwa na haya mambo, kwa maana hayana muendelezo na yatazidi kukuchelewesha kwenye kufikia lile lengo kuu ambalo wewe umeumbwa uje ulitekeleze hapa duniani, kwa hiyo jitahidi kujitafuta kuanzia sasa ili uweze kujua kipawa chako ni kipi na uanze kukifuata ili ukaishi yale maisha ya hatima yako.
Na pia ningependa nieleweke kwamba, ninaposema imani za kiroho simaanishi kwamba ni lazima ziwe za kanisani, msikitini au kilingeni ila imani za kiroho zipo nyingi kwa maana ukienda India utakutana na watu wenye imani tofauti tofauti za kushangaza, pia ukienda China utakutana na imani nyingi za tofauti tofauti na za kushangaza na hata wewe kwenye ukoo wenu huwa mko na imani zenu tofauti tofauti na za kushangaza, kwahiyo hizi imani zote endapo zikifanikiwa kuamsha ile nguvu iliyopo ndani yako, basi jua nguvu yako ya asili uliyo nayo inafungamana moja kwa moja na imani hiyo kwahiyo unachotakiwa kufanya ni kufuata taratibu za hiyo imani na kama wewe nguvu uliyo nayo si ya upande huo utahangaika kwenye huo upande miaka na miaka ila hautafanikiwa kuinyanyua ile nguvu iliyoko ndani yako.
...Nitaishia hapa kwenye hiki kipande na tukutane kwenye kipande kinachofuata. Bado nitaendelea kuwepo hapa kwenye nguvu za asili kwa maana hii ndio brash kwenye kiatu ulichopaka kiwi na ndio clear kwenye gari ulilopaka rangi, ni mbolea kwa mazao yako shambani, pia ni maji kwenye kiu yako kwa maana kwamba kwa hatima pekee utafanikiwa ila kwa hatima jumlisha nguvu za asili utafanikiwa zaidi.