Sambusa kavu
JF-Expert Member
- May 4, 2015
- 806
- 1,296
Mkuu...ningependa nikuweke sawa apo unaposema kroos ni kiungo Wa kawaida kumlinganisha eti na pogba na fabregas unakosea...sasa Huyo jamaa ndo kabisa huwa uwepo wake kwenye match ni kama vile hayupo ila akitolewaga tu utagundua dimba pale kati limepwaya...hii ilijidhihirisha baada ya kroos kutolewa na sub katika 2nd-leg ya atletico kwenye ligi ambapo game iliisha 1-1,so far pale kati dimbani Madrid kuna viungo Wa maana si mchezo...tukianza na Kroos ni Master pass na penetration kuntu(HUYU NI MZURI ZAIDI TIMU IKIWA INASHAMBULIA),MODRIC ni mmiliki mzuri wa mpira na hutuliza pressure ya mpira pale dimbani(HUYU NI MZURI ZAIDI TIMU INAPO POSSESS MPIRA)...Pia kuna CASEMIRO huyu ni mkabaji makini(HUYU NI MUHIMU SANA TIMU IKIWA INASHAMBULIWA)...Na kila mmoja ana umuhimu wake kwa mfano Casemiro akitokaga na timu ikiwa inashambuliwa lazima Ramos adungwe RED...tafsiri yake mabeki wameelemewa na pale kati kumekuwa uchochoro,Modric asipokuwepo utaona kabisa midfilders za timu pinzani wanamiliki Mpira kuliko madrid na mipira mingi huwa inapotea sana pale kati(hapa naona Isco sherehe hii ya kumiliki Mpira pale kati anaweza ifanya vyema sikuizi isipokuwa tatizo lake huwa anapoza sana mipira anayopewa na wenzie maana hadi afanye udambwi wake ule ndo atoe Pasi...muda mwengine hii hukata morale ya timu) na Kroos asipokuwepo utagundua utoaji wa pasi za mwisho na penetration ni ovyo ila Kroos huwa sio mzuri pale Ramos anapopataga RED ambapo Casemiro inamlazimu arudi pale nyuma kumsaidia varane/nacho na hivyo inawalazimu Kroos na modric kubaki pale kati...apa mzigo huwa unamwelemea sana modric kwa kuwa Kroos si mkabaji kivile bora modric na kwa kuwa timu haipandi kama awali Kroos anashindwa kufanya kazi yake anayoifanyaga ya kutoa pasi za mwisho(katika situation kama hii kroos anakuwaga mzigo na huchoka vibaya kwa kuwa dimba huchafukwa na wao pale kati wapo Wawili tu yeye na luka...ukizingatia kukaba sana sio haiba yake...na apa mara nyingi sub inayoingia badala yake utaona ni Kovacic ana afadhali kwenye kukaba kuliko Kroos).
Aiseeee!!! mkuu inabidi umrithi Mourinho pale OT......maana sio kwa mitactics iyo!!