Duniani Kuna vituko: Awashtaki wazazi wake Kwa kumzaa

Duniani Kuna vituko: Awashtaki wazazi wake Kwa kumzaa

Mwanamume wa miaka 27 wa India anapanga kuwashtaki wazazi wake kwa sababu hawakuomba ridhaa yake ili azaliwe.

Raphael Samuel, mfanyabiashara mwenye makazi yake Mumbai, aliambia BBC kuwa haikuwa sahihi kuleta mtoto duniani na kuishia matatizoni maisha yake yote.

Anaelewa kuwa haiwezekani kuuliza maono kutoka kwa mtu ambaye hajaja ulimwenguni, lakini anasisitiza ‘’uamuzi wetu sio kuzaliwa’’.

Hatua hiyo inaweza kusababisha mabishano katika familia yoyote, lakini inaonekana familia yake inaifanyia mzaha.

Katika taarifa iliyotolewa na mamake Kavita Karnad Samuel alisema alimpongeza mwanawe kwa kumpeleka mahakamani, akijua kuwa wote ni mawakili.

Samuel anaomba mahakama iamuru alipwe fidia na wazazi wake.

Wazo la mtu huyu linatokana na mtazamo wa kifalsafa kwamba maisha ni magumu, na kwa hiyo ametelekezwa

Chanzo: BBC swahili
...Amepanga kuwafikisha Wazazi wake Mahakamani... Kichwa Cha Uzi wako kinamaanisha Ameisha Wafikisha tayari??
 
kuna kipindi katika maisha yangu nilikuwa mtu wa kutumia logic sana, mungu wangu kumbe logic na maisha ni kama Russia na Ukraine.

..yatosha, acha kesi zao zijisumbukie zenyewe, kwani una nini nao!?
 
Hapa mtatoa povu ila yuko sahihi, unajijua maisha yako ya kuunga si uvae condom? Kwa nini ulete kiumbe duniani kukitesa bure? Yuko sahihi kabisa na mahakama itowe haki
Nimesikia hospitali ya mirembe wameanza kuwasaka wenye matatizo ya afya ya akili mitaani. Hivi hawana wawakilishi humu JF?
 
Nimesikia hospitali ya mirembe wameanza kuwasaka wenye matatizo ya afya ya akili mitaani. Hivi hawana wawakilishi humu JF?
Pelekwa wewe mirembe, binafsi siwezi ruhusu zaa mtoto kama sina uakika wa mkumlea.
 
Rukiacha masuala ya Imani,hapa kuna hoja.
Wengi kesi hii wataihusisha na urukwaji wa akili,Sidhani!

Kwani hizi njia za uzazi wa mpango si ni kama zinamwelekeo wa bwana Raphael? Au mi pia nimerukwa??

Ikiwa ng'ombe tu tunaambiwa tufuge wale tunaoweza kuwamudu,iweje kwa kiumbe chenye mahitaji lukuki(binadamu).Hapa ukweli usemwe KAMA HUNA UWEZO USIZAE,SUBIRI!
Mbona ukinunua gari alafu uanze kugongea pesa ya kiwese unaonekana hujielewi?

Imani ipo ila isitupofushe kufanya vitu hata tusivyonauwezo navyo!

HII KESI IENDESHWE BILA MZAHA ILI IWE FUNZO KWA WAZAZI WATARAJIWA WASIO NA MALENGO KTK NZAO ZAO!
 
Back
Top Bottom