..hivi huoni Polisi wanaoonekana ktk video wanavyojitahidi kutuliza maandamano kwa uangalifu mkubwa?
unaweza kulinganisha na UKATILI unaofanywa na Polisi wetu?
..umeona jinsi wanavyowakamata waandamanaji? umelinganisha na jinsi polisi wetu wanavyokamata waandamanaji?
..Ingekuwa hapa kwetu waandamanaji wangepigwa RISASI ZA MOTO, au wangelipuliwa na MAGURUNETI kama ilivyotokea kwa DAUDI MWANGOSI.
cc
tindo
Majuzi kuna tukio limetokea Marekani katika mall, kuna mtu kaua watu kwa risasi. Katika kutafuta mhusika Polisi wakampiga risasi kijana mwingine
Leo Polisi wamekiri kuua mtu asiyehusika na kwamba, Polisi aliyeua anachunguzwa
Kuna video ya Polisi aliyetoa maneno ya kibaguzi, amewajibishwa kwa kufukuzwa kazi
Kwa wenzetu kila mmoja yupo ndani ya sheria. Inapotokea makosa, wahusika wanakiri
Uchunguzi huru unafanyika na mwenye makosa anafikishwa mbele ya sheria
Tatizo letu ni Polisi kupoteza imani kwa wananchi kwa taarifa nyingi zinazotofautiana na uhalisia wa tukio
Tukio la Mwangosi RIP, tuliambiwa watu waliokuwa katika mkutano walitupa kitu cha ncha kali
Ushahidi ulipotoka ni Polisi tena wakiwa na wakubwa wao
Kuna matukio ya majambazi ''kuwatoroka'' Polisi wakiwaonyesha walipoficha silaha au wenzao walipo.
Unaweza kujiuliza, hivi Jambazi linaachwaje huru bila pingu kiasi cha kujaribu kutoroka!
Utajiuliza, jambazi linawezaje kutoroka likiwa na pingu, na kama halikufungwa ni kwanini
Suala la Kijana Nondo, Polisi walimleta mbele ya TV kwa mbwembwe.
Polisi wakaacha kazi ya uchunguzi wakajikita katika siasa.
Hilo walifanya wakijua ''mtu hana hatia hadi mahakama itakapomtia hatiani''.
Kulikuwa na ulazima gani wa ''kumhukumu'' mtu bila haki ya kusikilizwa
Mwisho wa siku hawakuweza kutoa ushahidi wa kumtia hatiani, walishamhukumu mbele ya umma ''court of public opinion''. Nondo yupo huru, hakudhalilika. Polisi wanatoa taswira gani kwa umma!
Polisi walituonyesha silaha zilizotumika na watuhumiwa kumuua Dr
Wote wameachiwa. Kazi ya hukumu ilikuwa ya nini? Na je ni kazi ya Polisi kutoa hukumu katika media
Tukio la Tarime la kuuawa nduguye Heche lilionyesha weledi wa Polisi msimamizi
Alijitokeza na kusema ni kweli aliuawa na Polisi. Baada ya hapo kumekuwa na amani, wananchi wameshamwamini Mkuu wa Polisi Tarime. Just kusema ni kweli na ni sisi Polisi ni weledi mkubwa
Kuna taarifa nyingine zinashangaza. Polisi wanasema ' watu wenye ushahidi wa tukio' wapeleke habari kwao. Tukio la Nape kunyooshewa silaha picha za wahusika zipo wazi. Nini kilifuata? Hakuna
Kesho wakiomba ushahidi nani atakyedhani wapo serious na taarifa wanazopewa
Imefika mahali watu wanaogopa kutoa taarifa za matukio kwa hofu ya 'kusaidia Polisi''
Kwa nchi za wenzetu, within an hour kunaweza kuwa na tips zaidi ya 1000.
Polisi kufanya makosa kama taaluma nyingine si tatizo pekee, kila mahali makosa yanatokea
Kwetu sisi imekuwa kama mtindo, kutoa taarifa zingine zikipingana na ukweli ulio wazi.
Kulinganisha utendaji wa Polisi wetu na wenzetu si haki. Huko kwingine hukamatwi hadi uwepo ushahidi wa kutosha. Hupelekwi kwenye TV kama mhusika bali utatajwa kama mtuhumiwa kukiwa na ushahidi
Polisi hawezi kukuweka mahabusu kesho akakuachia huru kwasababu tu alitaka.
Hawezi kukuweka mahabusu kwasababu ni Ijumaa ili ulale hadi Jumatatu bila kusomewa mashtaka.
UK maandamano ya Brexit kila siku tena yakiwa na ulinzi