Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Wanajamvi
Katika mabandiko 4 yajayo tutangaalia hali ya kisiasa mbali na BMK
Tutajadili mbinu na mikakati inayotarajiwa siku za karibuni
Namna CCM wanavyohaingaika kujinusuru
Na namna UKAWA walipo, njia panda na mitego inayowakabili.
Huu ni mwendelezo wa nyuzi hizi
https://www.jamiiforums.com/great-t...ji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika-25.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...historia-ya-juisi-ya-maembe-kujirudia-13.html
Tumeonelea umuhumi wa kuwa na bandiko mahususi kufuatilia tahmini ya mambo yanayoendelea, mbele na nyuma ya pazia.
Sehemu ya I
UKAWA
Ukawa ni ushirika ulioundwa wa vyama kukabliana na nguvu kubwa nay a kibabe ya CCM
Kwa miaka 20 vyama vya upinzani vimejaribu kupigana na CCM kila mmoja kivyake bila mafanikio
CCM imetumia udhaifu wa vyama kutawala kwa hila au halali.
Udhaifu upo miongoni mwa wapinzani zaidi ya hasimu wao CCM.
Uundwaji wa vyama ni matokeo ya mafarakano ndani ya wapinzani.
Hilo lilisaidwa na uwepo wa mapandikizi katika upinzani.
Imefika mahali katibu mkuu wa chama au Mbunge anaporudi CCM ni kuonyesha
Kukamilika kwa kazi aliyotumwa.
Kila ulipotokea mzozo, matokeo ni kuacha udhaifu mkubwa. Mifano ni NCCR vs TLP, CUF.
Uhasama umeondoa maridhiano ya pamoja.Mifano ni mzozo wa CDM vs CUF bungeni ulioleta mapasuko.
Chanzo cha mzozo ni udhaifu uliotumiwa na CCM baada ya kuundwa ndoa ya GNU Zanzibar
CDM waliona CUF kama CCM-b, CUF wakiwaona CDM kama wapiga kelele wasiowatakia mema.
NCCR nao wakilalamika kuwa nje ya kambi ya upinzani.
Mvurugano ukawa mkubwa,kwamba ni rahisi Cuf kuunga mkono CCM au CDM kuungana
na CCM katika mazingira ya kukomoana.
Kambi ya upinzani ikagawanyika vipande, CCM wakatumia udhifu huo katika miswada ukiwemo wa kuandika katiba mpya.
Wapinzani wakirushiana maneno CCM walipanga mbinu zao kwa amani.
Sheria ya katiba ilifanyiwa marekebisho upinzani ukiwa ni CDM na kwa mbali NCCR
Mwenyekiti wa CCM akatumia udhaifu kuwaita kwa mafungu, na mwisho wa siku kuwapiga chenga,akitumia maneno baadhi yao wamekubali baadhi hawataki.
Wapinzani wakaelekea bunge la katiba(BMK) wakiwa na agenda zao binafsi dhidi ya CCM.
Uhuni wa CCM ukaanza kuuma kila upande na wapinzani kubaini tatizo si wao Mbaya wao ni CCM.
Ndipo ikazaliwa UKAWA, nguvu za kudai haki ya kuandika katiba ya nchi.
Muda mfupi wakabaini wamebeba agenda ya wananchi mamilioni nyuma yao.
Kuundwa kwa ukawa ni makubaliano ya viongozi wa vyama vya siasa.
Walichogundua ‘mbaya' wao ni CCM anayewatumia kutimiza azma ya hila na mbinu zake.
Na katika kuendeleza maridhiano, viongozi wakakubaliana kuunda kambi ya pamoja ya upinzani ili ushirika uwe endelevu ndani ya BMK na baada ya hapo.
Umoja huo unaungwa mkono na sehemu kubwa sana ya jamii.
Hata hivyo, jamii imekuja nyuma ya viongozi hao kwa vile agenda ya wananchi imekuwa ni moja, kumaliza ubabaishaji wa miaka 50 na kuweka agenda mpya.
UKAWA ni matokeo ya maridhiano ya viongozi si wananchi.
Kinachowaunganisha wananchi na UKAWA ni agenda ya kitaifa iliyopo mbele, katiba mpya.
Ni kwa muktadha huo UKAWA wana fursa iliyopataikana ya kuwaunganisha kwa kutumia
agenda ya katiba mpya.
Lakini hilo ni suala la muda, bado wana changamoto(challenges) wanazohitaji kuzifanyia kazi sasa na siku za baadaye.
Katiba mpya imetengeneza tanuru(template) ya agenda kubwa na wala katiba si agenda yenyewe kwa mtazamo wa wananchi.
Na wala UKAWA wasidhani CCM wanafarijika na umoja huo. UKAWA ni mwiba unaoangaliwa na CCM na kila mbinu itafanyika kuhakikisha, ima inatibua mipango yao au ina wavuruga.
Tuangalie changamoto zinazoikabili UKAWA
Inaendelea
Katika mabandiko 4 yajayo tutangaalia hali ya kisiasa mbali na BMK
Tutajadili mbinu na mikakati inayotarajiwa siku za karibuni
Namna CCM wanavyohaingaika kujinusuru
Na namna UKAWA walipo, njia panda na mitego inayowakabili.
Huu ni mwendelezo wa nyuzi hizi
https://www.jamiiforums.com/great-t...ji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika-25.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...historia-ya-juisi-ya-maembe-kujirudia-13.html
Tumeonelea umuhumi wa kuwa na bandiko mahususi kufuatilia tahmini ya mambo yanayoendelea, mbele na nyuma ya pazia.
Sehemu ya I
UKAWA
Ukawa ni ushirika ulioundwa wa vyama kukabliana na nguvu kubwa nay a kibabe ya CCM
Kwa miaka 20 vyama vya upinzani vimejaribu kupigana na CCM kila mmoja kivyake bila mafanikio
CCM imetumia udhaifu wa vyama kutawala kwa hila au halali.
Udhaifu upo miongoni mwa wapinzani zaidi ya hasimu wao CCM.
Uundwaji wa vyama ni matokeo ya mafarakano ndani ya wapinzani.
Hilo lilisaidwa na uwepo wa mapandikizi katika upinzani.
Imefika mahali katibu mkuu wa chama au Mbunge anaporudi CCM ni kuonyesha
Kukamilika kwa kazi aliyotumwa.
Kila ulipotokea mzozo, matokeo ni kuacha udhaifu mkubwa. Mifano ni NCCR vs TLP, CUF.
Uhasama umeondoa maridhiano ya pamoja.Mifano ni mzozo wa CDM vs CUF bungeni ulioleta mapasuko.
Chanzo cha mzozo ni udhaifu uliotumiwa na CCM baada ya kuundwa ndoa ya GNU Zanzibar
CDM waliona CUF kama CCM-b, CUF wakiwaona CDM kama wapiga kelele wasiowatakia mema.
NCCR nao wakilalamika kuwa nje ya kambi ya upinzani.
Mvurugano ukawa mkubwa,kwamba ni rahisi Cuf kuunga mkono CCM au CDM kuungana
na CCM katika mazingira ya kukomoana.
Kambi ya upinzani ikagawanyika vipande, CCM wakatumia udhifu huo katika miswada ukiwemo wa kuandika katiba mpya.
Wapinzani wakirushiana maneno CCM walipanga mbinu zao kwa amani.
Sheria ya katiba ilifanyiwa marekebisho upinzani ukiwa ni CDM na kwa mbali NCCR
Mwenyekiti wa CCM akatumia udhaifu kuwaita kwa mafungu, na mwisho wa siku kuwapiga chenga,akitumia maneno baadhi yao wamekubali baadhi hawataki.
Wapinzani wakaelekea bunge la katiba(BMK) wakiwa na agenda zao binafsi dhidi ya CCM.
Uhuni wa CCM ukaanza kuuma kila upande na wapinzani kubaini tatizo si wao Mbaya wao ni CCM.
Ndipo ikazaliwa UKAWA, nguvu za kudai haki ya kuandika katiba ya nchi.
Muda mfupi wakabaini wamebeba agenda ya wananchi mamilioni nyuma yao.
Kuundwa kwa ukawa ni makubaliano ya viongozi wa vyama vya siasa.
Walichogundua ‘mbaya' wao ni CCM anayewatumia kutimiza azma ya hila na mbinu zake.
Na katika kuendeleza maridhiano, viongozi wakakubaliana kuunda kambi ya pamoja ya upinzani ili ushirika uwe endelevu ndani ya BMK na baada ya hapo.
Umoja huo unaungwa mkono na sehemu kubwa sana ya jamii.
Hata hivyo, jamii imekuja nyuma ya viongozi hao kwa vile agenda ya wananchi imekuwa ni moja, kumaliza ubabaishaji wa miaka 50 na kuweka agenda mpya.
UKAWA ni matokeo ya maridhiano ya viongozi si wananchi.
Kinachowaunganisha wananchi na UKAWA ni agenda ya kitaifa iliyopo mbele, katiba mpya.
Ni kwa muktadha huo UKAWA wana fursa iliyopataikana ya kuwaunganisha kwa kutumia
agenda ya katiba mpya.
Lakini hilo ni suala la muda, bado wana changamoto(challenges) wanazohitaji kuzifanyia kazi sasa na siku za baadaye.
Katiba mpya imetengeneza tanuru(template) ya agenda kubwa na wala katiba si agenda yenyewe kwa mtazamo wa wananchi.
Na wala UKAWA wasidhani CCM wanafarijika na umoja huo. UKAWA ni mwiba unaoangaliwa na CCM na kila mbinu itafanyika kuhakikisha, ima inatibua mipango yao au ina wavuruga.
Tuangalie changamoto zinazoikabili UKAWA
Inaendelea