Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #21
XX
PESA ZA MFUKO WA JIMBO KUTOKA BUNGE LA JMT KWENDA ZANZIBAR
Tukirejea bandiko I , II na III tumeona Bunge na idadi ya Wabunge ambao ni 393 akiwemo AG
Kwa upande wa Zanzibar yapo majimbo 50 ya Wabunge wa kuchaguliwa, Wabunge 5 wa Baraza la Wawakilishi, na Wabunge wa Kuteuliwa, na mwisho Wauteuliwa na Rais Kwa muktadha idadi ya Wabunge wa Zanzibar si chini ya 80.
Rejea gazeti la Serikali la Jan 5 2023.
Kwa mujibu wa Katiba ya JMT kama tulivyoonyesha, kuna mambo ya Muungano yanahitaji 2/3 ya kila upande.
Kwa minajili ya mjala ikiwa Wabunge wa Zanzibar ni 80, takribani inahitajika Wabunge 53 kupitisha jambo.
Pili, Wabunge wa Zanzibar wana KURA yenye nguvu sawa na Wabunge wengine wa Bunge la JMT.
Wabunge wa Zanzibar wana KURA kwa yasiyo ya Muungano kama Elimu, Afya, Utalii, Madini, Ujenzi, Uchukuzi, Mifugo, Kilimo , Ardhi n.k. wakiwa ndani ya Bunge. Haya ni mambo ya Tanganyika.
Mfano, Mswada unaohusu ARDHI unaweza kupita au kupingwa na kura za Wazanzibar.
Wazanzibar wana turufu ya kuamua mambo ya Tanganyika,yale yale wanayolalamika yasiwe ya Muungano.
Tuna suala la Bandari, Wabunge wa Zanzibar wamesema HALIWAHUSU lakini walipiga kura kuhusu suala hilo hilo.
Ikitokea Wabunge wa Zanzibar wana interest ya suala lisilo na masilahi na Tanganyika lakini lina masilahi yao, kura zao zinzaweza kuamua mustakabali wa Tanganyika.
Ukiacha nguvu ya TURUFU ya kura yao , kuna nguvu nyingine waliyo nayo.
Wabunge wa Zanzibar wanachaguliwa na idadi ndogo sana ya Wapiga kura.
Kwa mujibu wa Gazeti la Serikali la Jan 5, 2023 tutaonyesha idadi ya kura za Washindi tu katika kujenga hoja.
Hapa ni mifano michache
Mkoa wa kusini Pemba ( Zanzibar) - Mshindi alipata kura 4, 136.
Jimbo la Kawe Dar (Tanganyika )- Mshindi alipata kura 194, 833
Jimbo la Uchaguzi Konde (Zanzibar) - Mshindi alipata kura 1,552
Jimbo la Tanga mjini ( Tanganyika ) -Mshindi alipata kura 114,445
Mifano hiyo halisi ina maana .
Kwanza, Ikiwa kila Jimbo la Zanzibar litapewa wapiga kura 10,000 (idadi ya juu sana) itahitaji Wabunge 19 ili kupata idadi sawa ya wapiga kura wa Jimbo la KAWE.
Itahitajika Wabunge 11 kutoka Zanzibar ili idadi iwe sawa na iliyomchagua Mbunge wa TANGA MJINI.
Wabunge wa Zanzibar wanaochaguliwa na watu 1,500 kama yule wa KONDE wana haki ya kuzuia Bajeti ya Afya, Ardhi, Madini au Mifugo ya Tanganyika kinyume na Matakwa ya Wabunge wa Kawe na Tanga.
Wabunge wa Zanzibar wanapata pesa za Mfuko wa Jimbo sawa na Wabunge wengine wa Tanganyika.
Tunasisitiza Tanganyika kwasababu hakuna Mbunge aliyechaguliwa na Watu chini ya 20,000
Lakini pia pesa za Mfuko wa Jimbo zinatoka Mfuko wa Hazina Kuu Dar es Salaam ambao unakusanya fedha za Tanganyika peke yake na kuzifanya za Muungano.
Rais Mwinyi katoa ushuhuda kwamba Zanzibar haichangii chochote na kodi zote zinabaki huko.
Mfuko wa Jimbo la Kawe la walipa kodi 194,833 ni sawa na Mfuko wa Jimbo la Kusini pemba la watu 4,136( wasiolipa kodi Hazina Kuu Dar es Salaa) Kwa mujibu wa Rais Mwinyi ( Gazeti la Mwananchi December 11,2022).
Mfuko wa Jimbo la Mbunge wa Tanga Mjini aliyechaguliwa na walipa kodi 114,445 ni sawa na Mbunge wa Konde aliyechaguliwa na watu 1,552 (wasiolipa kodi Mfuko Mkuu wa Hazina Dar es Salaam) .
Wabunge wa Zanzibar wanapaswa kulipiwa gharama na SMZ kwasababu wanakuja kwa ajili ya Zanzibar, kinyume chake wanazawadiwa pesa kutoka Hazina Kuu Dar es Salaam kwenda kwenye majimbo ya Zanzibar.
Kama Zanzibar hawana Mchango Hazina Kuu Dar es Salaam kwa mujibu wa Rais Hussein Mwinyi na aliyekuwa gavana wa BoT Ndulu, kwanini kodi za Wapiga kura wa Kawe na Tanga mjini ziende majimbo Zanzibar?
Itaendelea
PESA ZA MFUKO WA JIMBO KUTOKA BUNGE LA JMT KWENDA ZANZIBAR
Tukirejea bandiko I , II na III tumeona Bunge na idadi ya Wabunge ambao ni 393 akiwemo AG
Kwa upande wa Zanzibar yapo majimbo 50 ya Wabunge wa kuchaguliwa, Wabunge 5 wa Baraza la Wawakilishi, na Wabunge wa Kuteuliwa, na mwisho Wauteuliwa na Rais Kwa muktadha idadi ya Wabunge wa Zanzibar si chini ya 80.
Rejea gazeti la Serikali la Jan 5 2023.
Kwa mujibu wa Katiba ya JMT kama tulivyoonyesha, kuna mambo ya Muungano yanahitaji 2/3 ya kila upande.
Kwa minajili ya mjala ikiwa Wabunge wa Zanzibar ni 80, takribani inahitajika Wabunge 53 kupitisha jambo.
Pili, Wabunge wa Zanzibar wana KURA yenye nguvu sawa na Wabunge wengine wa Bunge la JMT.
Wabunge wa Zanzibar wana KURA kwa yasiyo ya Muungano kama Elimu, Afya, Utalii, Madini, Ujenzi, Uchukuzi, Mifugo, Kilimo , Ardhi n.k. wakiwa ndani ya Bunge. Haya ni mambo ya Tanganyika.
Mfano, Mswada unaohusu ARDHI unaweza kupita au kupingwa na kura za Wazanzibar.
Wazanzibar wana turufu ya kuamua mambo ya Tanganyika,yale yale wanayolalamika yasiwe ya Muungano.
Tuna suala la Bandari, Wabunge wa Zanzibar wamesema HALIWAHUSU lakini walipiga kura kuhusu suala hilo hilo.
Ikitokea Wabunge wa Zanzibar wana interest ya suala lisilo na masilahi na Tanganyika lakini lina masilahi yao, kura zao zinzaweza kuamua mustakabali wa Tanganyika.
Ukiacha nguvu ya TURUFU ya kura yao , kuna nguvu nyingine waliyo nayo.
Wabunge wa Zanzibar wanachaguliwa na idadi ndogo sana ya Wapiga kura.
Kwa mujibu wa Gazeti la Serikali la Jan 5, 2023 tutaonyesha idadi ya kura za Washindi tu katika kujenga hoja.
Hapa ni mifano michache
Mkoa wa kusini Pemba ( Zanzibar) - Mshindi alipata kura 4, 136.
Jimbo la Kawe Dar (Tanganyika )- Mshindi alipata kura 194, 833
Jimbo la Uchaguzi Konde (Zanzibar) - Mshindi alipata kura 1,552
Jimbo la Tanga mjini ( Tanganyika ) -Mshindi alipata kura 114,445
Mifano hiyo halisi ina maana .
Kwanza, Ikiwa kila Jimbo la Zanzibar litapewa wapiga kura 10,000 (idadi ya juu sana) itahitaji Wabunge 19 ili kupata idadi sawa ya wapiga kura wa Jimbo la KAWE.
Itahitajika Wabunge 11 kutoka Zanzibar ili idadi iwe sawa na iliyomchagua Mbunge wa TANGA MJINI.
Wabunge wa Zanzibar wanaochaguliwa na watu 1,500 kama yule wa KONDE wana haki ya kuzuia Bajeti ya Afya, Ardhi, Madini au Mifugo ya Tanganyika kinyume na Matakwa ya Wabunge wa Kawe na Tanga.
Wabunge wa Zanzibar wanapata pesa za Mfuko wa Jimbo sawa na Wabunge wengine wa Tanganyika.
Tunasisitiza Tanganyika kwasababu hakuna Mbunge aliyechaguliwa na Watu chini ya 20,000
Lakini pia pesa za Mfuko wa Jimbo zinatoka Mfuko wa Hazina Kuu Dar es Salaam ambao unakusanya fedha za Tanganyika peke yake na kuzifanya za Muungano.
Rais Mwinyi katoa ushuhuda kwamba Zanzibar haichangii chochote na kodi zote zinabaki huko.
Mfuko wa Jimbo la Kawe la walipa kodi 194,833 ni sawa na Mfuko wa Jimbo la Kusini pemba la watu 4,136( wasiolipa kodi Hazina Kuu Dar es Salaa) Kwa mujibu wa Rais Mwinyi ( Gazeti la Mwananchi December 11,2022).
Mfuko wa Jimbo la Mbunge wa Tanga Mjini aliyechaguliwa na walipa kodi 114,445 ni sawa na Mbunge wa Konde aliyechaguliwa na watu 1,552 (wasiolipa kodi Mfuko Mkuu wa Hazina Dar es Salaam) .
Wabunge wa Zanzibar wanapaswa kulipiwa gharama na SMZ kwasababu wanakuja kwa ajili ya Zanzibar, kinyume chake wanazawadiwa pesa kutoka Hazina Kuu Dar es Salaam kwenda kwenye majimbo ya Zanzibar.
Kama Zanzibar hawana Mchango Hazina Kuu Dar es Salaam kwa mujibu wa Rais Hussein Mwinyi na aliyekuwa gavana wa BoT Ndulu, kwanini kodi za Wapiga kura wa Kawe na Tanga mjini ziende majimbo Zanzibar?
Itaendelea