Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #341
Mkuu upo sahihi, experience inaonyesha tulipokuwa na vyuo vichache ubora ulitiliwa maanani kuliko wingi.Mkuu Nguruvi3
Sidhani kama wingi wa vyuo maana yake ni kuwa na vyuo visivyokidhi ubora. Unaweza kuwa na vyuo vingi na vyote vikakidhi ubora au unaweza kuwa na vyuo vichache lakini bado vikawa bogus vilevile.
Kuhusisha mambo haya mawili sidhani kama ni sahihi na kwa namna moja au nyingine ni upotoshwaji.
Tangu tumeanza vyuo holela suala si ubora bali kufaulisha wanafunzi katika viwango vya chini
Chuo kinafundishwa na wahitimu wa degree ya kwanza. Hii si UPE nyingine kweli
Ukisoma vizuri hatukusema tuwe na vyuo vichache, tulichosema ni kuwa ni afadhali kuwa na vichache bora hata kama idadi itapungua kuliko kuwa na utitiri usiokidhi haja.
Hivyo jitihada za kuchuja vibovu ni nzuri hata kama tutabaki na viwili bora
Lakini pia milango haijafungwa kwa vile vtakavyomudu ushindani na kuonyesha Ubora
Pili, hatuna sababu za kuwa na chuo kikuu tunapoweza kufanya ''college' bila kuathiri idadi ya wanafunzi. Tuna maana kuwa ubora wa vyuo hutegemea uzoefu wake pia
Mkuu labda nikuulize, chuo kikuu Singida kinatoa wahitimu gani na future ya wahitimu hao ipo wapi? Bukoba University na Songea University nani anavitambua nchini na katika dunia hii?
Hivi navyo vinahitaji wanafunzi wa HESLB kwasababu tu kuna pesa, kinyume chake vinakufa
Kwanini wanafunzi walazimishwe kwenda kusoma 'highschool' halafu wapewe shahada za Chuo?
Hatua ya serikali kuhakikisha vina survive kwa ubora na si pesa za HESLB ni ya kupongezwa
Ni katika mambo mazuri sana wizara imeyaona.