Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
MBINU ZIMEKWISHA, SASA NI UPOTOSHAJI
WALENGWA NI VIJANA NA WANANCHI WA KAWAIDA MITAANI NA VIJIJINI
Bunge la katiba linaendelea Dodoma kukiwa na msuguano mkubwa ndani ya CCM.
Nje ya CCM kuna upinzani dhidi ya wahafidhina wa CCM wanaotaka kulitekea bunge kwa masilahi yao
Msuguano wa CCM unatokana na chama kupungukiwa na udhibiti miongoni mwa wanachama.
Awali, CCM ilidhani mbinu za kuuteka zingefanikiwa kama tulivyoeleza mwaka jana.
Matumaini ya CCM yalikuwa udhibiti wa tume ya Warioba itekeleze matakwa yao, na matumizi ya wingi wa wabunge wakisaidiwa na Spika wa bunge la katiba
Udhibiti kwa njia hizo unaonekana kutokuwa na mafanikio kutokana na hali ya kisiasa nchini na mwamko wa wananchi katika baadhi ya mambo kama hili la katiba.
Baadhi ya wanaCCM hawakubaliani na chama hasa suala la muungano.
Mbinu za kupotosha rasimu kama kutumia hoja ya gharama za serikali 3 imeshindikana.
Na suala la kutumia kura ya wazi linaleta tatizo
Mbinu za kutumia rasimu mbadala ya Nape na Andrea haionekanani kuwa na matumaini.
Rasimu mbadala inaonyesha CCM wanaunga mkono serikali 3 kwa muundo wa Warioba. Wasichokubaliana nacho ni kupunguza nguvu za kisiasa
Nguvu ya hoja za kuizindua Tanganyika inazidi kushika kasi.
CCM imeanza kutumia mbinu za kuwatisha wabunge na wananchi
Mbinu za mwanzo ni ile ya Rais kubadili msimamo wa kuheshimu mawazo ya wananchi kupitia tume, ghafala akarudi katika serikali 2, na makamu wa rais kutumwa kuongea na vyama vya siasa akisistiza serikali 2
Wiki hii, Rais Shein wa SMZ akiwa na makamu wawili, Seif Hamad na Idd Seif walizundua logo na kauli mbiu za maazimisho ya miaka 50 ya muungano.
Katika hali ya kawaida hili halikuwahi kutokea siku za nyuma, ni wazi shinikizo la muungano linazidi.
Rais Shein amesema msimamo ni serikali 2 kinyume na matakwa ya wazanzibar ambao ndio hasa walioanzisha sakata la uzinduzi wa Tanganyika.
Katika hali ya kuchanganyikiwa ndani ya CCM hasa kuzinduka kwa Tanganyika, viongozi wameanza mbinu za kupotosha wananchi. Wanawalaghai vijana wadogo waliozaliwa nyakati za Tanzania, na wale wa mitaani ambao tofauti kati ya Tanzania na Tanganyika kwao haipo uwazi.
Waziri mkuu Pinda amenukuliwa akiuliza wanaotaka Tanganyika wanataka ipi ya 1961 hadi 1964 au ya Mkoloni? Hoja hii imelenga kupotosha umma,Tanganyikailiyokuwepo miaka ya 1800 na hadi leo
Kama umetusoma vema, hatutumii neno kurudisha Tanganyika kwasababu ipo,neno muafaka ni kuizundua. Kwa maneno ya kisayansi Tanganyika ni ‘recessive' ndani ya Tanzania.
Recessive ni kitu kilichopo ambacho hakionekani kwa uwazi.
Kinachotakiwa kufanywa ni kuifanya ionekane kwa uwazi na majukumu yake ‘dominant'.
Kabla hatujarudi kwenye historia kuonyesha uwepo wa Tanganyika moja bila kujali miaka, tungependa kuwaelewesha watu kuwa Tanganyika ipo ndani ya Tanzania hadi leo hii.
Kinachotakiwa ni kuizindua kutoka katika ‘nusu kaputi' ili itekeleze majukumu yake.
Pinda anapotosha kwa kile Mchambuzi anachokisema kuwa ‘even magician runs out of trick'
kwamba wacheza mazingaombwe kuna nyakati huishiwa mbinu.
Kwa Muktadha huo ni jambo la hatari kupuuza kauli za Pinda zilizolenga kuupotosha umma.
Duru tunauona ukumuhimu wa kukabiliana na hoja potofu
Ni makosa mgonjwa aliye katika dawa ya usingizi kumwita marehemu, Tanganyika si marehemu. Tutakuwa na mwendelezo wa kufafanua kuhusu Tanganyika, tofauti kati yake na Tanzania n.k.
Tutaeleza umuhimu wake kwa nyakati za sasa na kutemebelea hoja zinazoambantana na mada.
Tutaanza na sehemu ya I hadi ya V, tunaomba uvumilivu ili tuwe na mtiririko mzuri wakati tutakapoanza mjadala.
Sehemu ya kwanza inafuata
WALENGWA NI VIJANA NA WANANCHI WA KAWAIDA MITAANI NA VIJIJINI
Bunge la katiba linaendelea Dodoma kukiwa na msuguano mkubwa ndani ya CCM.
Nje ya CCM kuna upinzani dhidi ya wahafidhina wa CCM wanaotaka kulitekea bunge kwa masilahi yao
Msuguano wa CCM unatokana na chama kupungukiwa na udhibiti miongoni mwa wanachama.
Awali, CCM ilidhani mbinu za kuuteka zingefanikiwa kama tulivyoeleza mwaka jana.
Matumaini ya CCM yalikuwa udhibiti wa tume ya Warioba itekeleze matakwa yao, na matumizi ya wingi wa wabunge wakisaidiwa na Spika wa bunge la katiba
Udhibiti kwa njia hizo unaonekana kutokuwa na mafanikio kutokana na hali ya kisiasa nchini na mwamko wa wananchi katika baadhi ya mambo kama hili la katiba.
Baadhi ya wanaCCM hawakubaliani na chama hasa suala la muungano.
Mbinu za kupotosha rasimu kama kutumia hoja ya gharama za serikali 3 imeshindikana.
Na suala la kutumia kura ya wazi linaleta tatizo
Mbinu za kutumia rasimu mbadala ya Nape na Andrea haionekanani kuwa na matumaini.
Rasimu mbadala inaonyesha CCM wanaunga mkono serikali 3 kwa muundo wa Warioba. Wasichokubaliana nacho ni kupunguza nguvu za kisiasa
Nguvu ya hoja za kuizindua Tanganyika inazidi kushika kasi.
CCM imeanza kutumia mbinu za kuwatisha wabunge na wananchi
Mbinu za mwanzo ni ile ya Rais kubadili msimamo wa kuheshimu mawazo ya wananchi kupitia tume, ghafala akarudi katika serikali 2, na makamu wa rais kutumwa kuongea na vyama vya siasa akisistiza serikali 2
Wiki hii, Rais Shein wa SMZ akiwa na makamu wawili, Seif Hamad na Idd Seif walizundua logo na kauli mbiu za maazimisho ya miaka 50 ya muungano.
Katika hali ya kawaida hili halikuwahi kutokea siku za nyuma, ni wazi shinikizo la muungano linazidi.
Rais Shein amesema msimamo ni serikali 2 kinyume na matakwa ya wazanzibar ambao ndio hasa walioanzisha sakata la uzinduzi wa Tanganyika.
Katika hali ya kuchanganyikiwa ndani ya CCM hasa kuzinduka kwa Tanganyika, viongozi wameanza mbinu za kupotosha wananchi. Wanawalaghai vijana wadogo waliozaliwa nyakati za Tanzania, na wale wa mitaani ambao tofauti kati ya Tanzania na Tanganyika kwao haipo uwazi.
Waziri mkuu Pinda amenukuliwa akiuliza wanaotaka Tanganyika wanataka ipi ya 1961 hadi 1964 au ya Mkoloni? Hoja hii imelenga kupotosha umma,Tanganyikailiyokuwepo miaka ya 1800 na hadi leo
Kama umetusoma vema, hatutumii neno kurudisha Tanganyika kwasababu ipo,neno muafaka ni kuizundua. Kwa maneno ya kisayansi Tanganyika ni ‘recessive' ndani ya Tanzania.
Recessive ni kitu kilichopo ambacho hakionekani kwa uwazi.
Kinachotakiwa kufanywa ni kuifanya ionekane kwa uwazi na majukumu yake ‘dominant'.
Kabla hatujarudi kwenye historia kuonyesha uwepo wa Tanganyika moja bila kujali miaka, tungependa kuwaelewesha watu kuwa Tanganyika ipo ndani ya Tanzania hadi leo hii.
Kinachotakiwa ni kuizindua kutoka katika ‘nusu kaputi' ili itekeleze majukumu yake.
Pinda anapotosha kwa kile Mchambuzi anachokisema kuwa ‘even magician runs out of trick'
kwamba wacheza mazingaombwe kuna nyakati huishiwa mbinu.
Kwa Muktadha huo ni jambo la hatari kupuuza kauli za Pinda zilizolenga kuupotosha umma.
Duru tunauona ukumuhimu wa kukabiliana na hoja potofu
Ni makosa mgonjwa aliye katika dawa ya usingizi kumwita marehemu, Tanganyika si marehemu. Tutakuwa na mwendelezo wa kufafanua kuhusu Tanganyika, tofauti kati yake na Tanzania n.k.
Tutaeleza umuhimu wake kwa nyakati za sasa na kutemebelea hoja zinazoambantana na mada.
Tutaanza na sehemu ya I hadi ya V, tunaomba uvumilivu ili tuwe na mtiririko mzuri wakati tutakapoanza mjadala.
Sehemu ya kwanza inafuata