Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu Mkandara, mkeo akiitwa Mrs au kubaki na binti ABC haina taabu bado atakuwa mkeo.Mkuu wangu nina swali moja tu.. Hivi mkeo akiitwa Mrs.Nguruvi3 atakuwa amepoteza Ubinadamu wake? Kuna tofauti ipi baina ya kuitwa Mrs. au laa!
Mkandara nikushukuru kwa maneno haya ambayo nitayaeleza kama ifuatavyo.Na masema hivi kwa sababu imenishangaza sana kuona wajumbe waloteuliwa kuongoza kongamano hili la baraza la katiba hakuna hata mtu mmoja alovaa pini ya bendera ama ngao yetu kuonyesha Uzalendo wao kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sasa ikiwa hawa watu wameshindwa kuitukuza nchi yao kwa kuvaa pini tu ktk makoti yao, mashati yao leo wanabishaa juu ya mavazi sijui mashati gani yavaliwe utadhani kuna red carpet basi ujue huko bungeni kuna Ubinafsi na kupendeza zaidi ya Utaifa!
Ahahahah! sasa ulipenda um[paramie tu meo upendavyo? Mkuu sisi waswahili mkeo unamuomba kwa mapenzi ya zawadi na kadhalika, unaomba kaa unaomba kazi na akifarajia ndipo unaingia ila wewe hutakiwi kumkatalia kwa sababu umechoka na kazi.Mkuu Mkandara, mkeo akiitwa Mrs au kubaki na binti ABC haina taabu bado atakuwa mkeo.
Tatizo ni pale mkeo atakaposhindwa kuheshimu makubaliano ya ndoa yawe rasmi au mliokubaliana wawili.
Mkeo anapoamua kuondoka na kitanda,majiko na kuchukua funguo za nyumba na kukutaka umpigie simu ili akuruhusu kuingia ndani ya nyumba yako huyo si mke ni mhuni.
Tena uhuni wake ni zaidi ya changudoa maana yeye anakutumia kwa jina la mume akikuumiza zaidi kuliko kukusaidia.
Huyu mke anayesubiri ujaze friji aseme ni vyakula vyetu wakati chenji yake akinunua lip stick za wadogo zake si mke ni gubeli.
Huyu mke anayesema mna account ya pamoja wakati umechangia 100 amechangia sh 0 si mke.
Mke anyekupiga busu wakati mnaenda benki na mkishagawana hiyo 100 anakurushia matusi si mke ni tatizo.
Huyu mke anayeishi nyumbani kwako wakati anadai ana vitenge vyake, nyimbo za taarabu na sasa anataka balozi wa nyumba kumi amtambue kuwa ni mwenye nyumba yako, si mke ni baradhuli
Mkuu katika hili zanzibar wanaitambua tanzania vizuri sana. wanaitambua ndoa hii na ndio maana wanaitaka taraka kisheria laa sivyo wangeingia msituni. Hiyo katiba yao ni ya mambo ya kike ambayo umetokana na mume kushindwa kutimiza majukumu ya mume.Mkandara nikushukuru kwa maneno haya ambayo nitayaeleza kama ifuatavyo.
Mwenyekiti wa muda kificho ana waraka unaoitaka serikali 3, akiwa ndani ya CCM anataka serikali 2.
Hivi kificho atavaa pini ya nembo gani? Tanzania, united republic of Tanganyika and Zanzibar au Republic of Zanzibar?
Wajumbe kutoka Zanzibar haiwatambui JMT, na hilo si kosa lao kwasababu katiba ya znz ya mwaka 2010 inawapa haki.
Znz ni nchi na pale Dodoma wamekuja kwa ajili ya posho na masufuru, mioyo yao ipo kwa Zanzibar.
Ndio maana ya maneno znz kwanza.
Kuwalazimisha kuvaa nembo ya JMT ni kuwatukana, katiba ya nchi yao haisemi hivyo.
Wala hiyo JMT hawaitambui kabisa isipokuwa pesa za posho zinapogawanywa.
Wajumbe wa Tanzania wamechanganyikiwa, hawajui wavae nembo ya nchi gani. Je wavae nembo ya taifa jipya la Tanzania bara aliliovumbua Nape na Pinda, au wavae nembo ya JMT ambayo hawajui imeungana na nchi gani kwasababu wao ndio JMT peke yao.
Hawajui ni nembo ile ya adam na hawa ya Tanganyika au watengeneze nembo nyingine haraka haraka.
Wabunge wa Tanganyika wengine wanajiuliza, endapo bunge la JMT linajadili miswada na kuidhinishwa na BLW kwa kukubali au kukataa, wavae nembo ipi ? Ya SMZ yenye BLW linaloongoza Tanzania au JMT inayoongozwa na BLW.
Mimi nawashauri Wabunge wa Tanganyika wasichangayikiwe, warudi na kujiuliza siku ile Nyerere alipokabidhiwa nchi na Malikia walikuwa na nembo ya nchi gani.
sijui kama nitakuwa sahihi sana ama kama nimekuelewa sijui, nafikiri NCHI ni eneo lenye mipaka yake (country =is a region legally identified as a distinct entity in political geography)
na TAIFA ni watu wenye tamaduni, lugha na historia katika eneo husika, (NATION =a large body of people united by common descent, history, culture, or language inhabiting a particular state or territory )
na serikali ni muundo
...na hilo bunge lililotajwa na rais litakuwa na mamlaka juu ya mambo hayo kwa ajili ya jamhuri ya muungano, hii ni ziada juu ya mamlaka kuhusiana na mambo yote yanayohusiana na Tanganyika
12(1) Mamlaka yote ya serikali juu ya mambo ya muungano kuhusu na mengine yote ndani ya tanganyika yamewekwa chini ya rais
Mamlaka ya kutunga sheria juu ya mambo yote yalio ya muungano na mambo mengine yote ndani na juu ya Tanganyika yanawekwa chini ya bunge.
Mamlaka ya serikali ya jamhuri ya muungano kuhusiana na jamhuri ya muungano na mambo yote ya muungano yanawekwa mikononi mwa rais
Kutakuwa na serikali ya zanzibar inayojulikana kama serikali ya mapinduzi ya zanziba ambayo itakuwa na mamlaka katika zanzibar juu ya mambo yote yasiyo mambo ya muungano kwa mujibu wa masharti ya katiba hii
Chama ndicho chenye madaraka ya mwisho katika mambo yote kwa mujibu wa katiba hii na katiba ya chama.
Shughuli zote za vyombo vya serikali ya muungano zitatekelezwa kwa mujibu wa matakwa ya chama.
3 (1) Kutakuwa na chama kimoja cha siasa katika Tanzania.
(2) Mpaka hapo TANU itakapoungana na ASP na kuunda chama kimoja cha siasa, chama hicho kwa Tanganyika kitakuwa ni TANU na kwa zanzibar kitakuwa ni ASP.
(4) Katiba iliyoonyeshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba hii itakuwa katiba ya TANU na katiba inaweza kurekebishwa wakati wowote (na masharti yaliyomo ndani yake ba baada ya muungano wa TANU na ASP kwa mujibu wa masharti yaliyopo ndani ya katiba hiyo
Shughuli zote za kisiasa zaidi ya zile zilizo chini ya serikali ya muungano, vyombo vya serikali na vya kutunga sheria zanzibar au serikali za mitaa zilizoanzishwa kwa au chini ya sheria zilizopo, zitaendeshwa na kusimamiwa na serikali
Eneo la jamhuri ya muungani ni eneo lote la Tanzanua bara na eneo lote la zanzibar pamoja na eneo la bahari
Transition kwenda serikali moja imeshindikana kwasababu, kwanza ulafi wa viongozi kimadaraka.Inashangaza CCM wameacha kuongelea masilahi ya wakulima, wafanya, akina mama na watoto wamekwenda kujifungia kuandika kurasa 22 za kuboresha kile walichoshindwa kwa miaka 20 iliyopita.Muundo wa serikali mbili ulikuwa uko skewed sana kuilea Zanzibar baada ya mapinduzi isionekane kuwa Tanganyika ndiyo iliyoendesha mapinduzi yale lakini ulikuwa ni transitional ili baadaye tufikie kuwa ni nchi moja yenye serikali moja. Miaka ya sabini kabla ya vita ya Kagera tulikuwa tumekaribia sana lengo hilo, hasa baada ya TANU na ASP kuanza kwa kuungana; lakini baada ya vita mambo yakaharibika sana.
Kwa dunia ya leo hii, nadhani ni ndoto ya alinacha kudhani kuwa lengo hilo litafikiwa tena hasa kwa vile tuna umma mkubwa sana wa wanasiasa wanaofikiria madaraka kuliko well being ya nchi. Kwa hali hiyo muundo wa serikali tatu utabaki ndiyo njia pekee ya kuendesha nchi hii. Kukosekana kwa viongozi wenye ushawishi wa kuunganisha nguvu ni ombwe ambalo linafungua chumba kikubwa sana kuwepo kwa muundo wa serikali tatu ambazo ndiyo njia pekee iliyobaki. Ni ama serikali moja au serikali tatu; ile transtional structure ya serikali mbili imeshindwa kabisa hasa wakati huu tunapofikia miaka hamsini bado kukiwa na friction za kimadaraka baina ya pande mbili za muungano.
Effort yoyote ya kuendelea kutuacha kwenye transitional system ni matumizi mabaya ya raslimali zetu
Na siku tutakapo fahamu na kuzingatia ya kwamba huyu mke tumeshindwa kumpamba hadi wamekuja Wazungu sijui Wataliani na Waarabu tena kwa mlango wa nyuma kumhudumia tuliposhindwa, sasa kwa nini asidai taraka?...
Mkuu Mkandara, talaka ipo kwa kadhi, kadhi kaingia mjini wanao omba hawaonekani.Nachowaomba Watanganyika, haswa sis Wadanganyika wa bara na visiwani, Tujirudi wakuu zangu. Kama kweli ni sehemu ya Tanzania na tunathamini huu muungano wetu hiyo bajeti yetu ya maendeleo itazame pia upande wa mama hasa pale tunapotegemea zaidi mikopo na misaada toka nje
Na katiba ni mali ya kila mwananchi. Katiba ya nchi si mali ya Chama.1. CCM haina uwezo wowote wa kisheria (locus standi) wa kujiingiza kisheria na kulazimisha haki na wajibu wa muungano kwa upande wa zanzibar, Tanganyika au jamhuri ya muungano wa Tanzania.
2. CCM haikuwa sehemu ya mkataba wa muungano kwahiyo haiwezi kisheria kudai kupata manufaa yoyote chini ya mkataba wa 1964 kwa kuzinyonya, kuzilalia au kwa hasara ya Tanganyika na zanzibar ambazo ni sehemu ya mkataba wa muungano. Hata mahakama ya kimataifa itakubali kwamba huu ni ukiukwaji wa wazi wa mkataba wa kimataifa.
Na katiba ni mali ya kila mwananchi. Katiba ya nchi si mali ya Chama.
CCM haikuwepo wakati wa muungano, wala wazazi wake TANU na ASP hawakushirikishwa.
Hata mchakato uliopo CCM haina ufahamu nao. Mchakato haukupitia ngazi yoyote ya chama na wala hakukuwa na uhalali kwa mali ya wananchi kuhodhiwa na kundi la watu katika vyama
Nape na Pinda kwa miaka 8 hawana cha kutuonyesha kuhusu suluhu ya kero za muungano.
Leo wanakuja na hadithi za kufikirika wakitegemea Tanzania ya Nnauye ndiyo ya leo.
Ndio mna vyombo vya dola na mnaweza kuvitumia kuhujumu jambo lolote.
Ninachowakumbusha ni kuwa historia haiandikwi inanukuliwa baada ya kujiandika.
Ipo siku mtashindwa kusimama mitaani kwasababu historia itawatenga, matakuwa on the wrong side of the history.
Labda mtueleze, ni wapi na lini duniani nguvu ya umma iliwahi kushindwa na dola?
Kabla sijachangia hoja niliyoinukuu, niwarudishe wanajamvi nyuma kidogo kuhusu upotoshaji wa Pinda. Waziri mkuu anasema rais wa shirikisho atakuwa hana ardhi katika mfumo wa serikali 3.Tuanze na suala alilojadili Nguruvi3 hapo juu - gharama za kuendesha muungano. CCM imependekeza kufunguliwa kwa akaunti ya fedha ya pamoja ambazo zitatokana na mapato ya vyanzo vya muungano na kwamba kuwekwe utaratibu wa kisheria ambao utatekeleza uendeshaji wa akaunti hiyo na kuweka mgawanyo wa mapato kwa pande mbili za muungano.
Kwanza kwa sentensi hii tu, maana yake ni kwamba ccm imekubali serikali tatu kwani inataja muungano na inataja pande mbili za muungano.
Swali linalofuata ni je kuna uwezekano wa kuwepo kwa pande mbili za muungano bila kuwepo kwa serikali ya Tanganyika? jibu ni hapana, vinginevyo ni muendelezo wa mazingaombwe ya chama.
Nikirudi kwenye pendekezo hili la ccm, suala la "kufunguliwa kwa akaunti ya pamoja ya fedha zitokanazo na mapato ya vyanzo vya muungano" ni suala ambalo halitekelezeki chini ya mfumo wa serikali mbili. Isitoshe akaunti hiyo imekuwepo kwa miaka ishirini sasa lakini malalamiko juu ya mgawanyiko wa mapato ya fedha hayajaisha. Swali la kumuuliza Nape Nnauye na Ccm ni je:
*Hayo mapato ya muungano yapo wapi chini ya serikali mbili wakati chombo cha kusimammia mapato tajwa kwa nchi inayoitwa Tanzania bara, chombo hicho hakipo? kutakuwa na ZRA, TRA na chombo gani?
Ni vigumu kuelewa kwanini kina nape na ccm wanafanya watanzania ni wajinga.
Lakini pengine wanadhania kwamba legitimacy ya serikali ya ccm bado chanzo chake ni masuala nje ya katiba kama nilivyojadili elsewhere kwani mapendekezo kama haya yatatekelezeka iwapo tu umma wa watanzania utakiamini ccm na kukipa uhalali wa kuendelea kuongoza nchi bila ya kujalisha constitutionalism.
Pengine kina nape hawaelewi (pengine) kwamba chini ya mfumo wa serikali mbili hakuna kitu kinachoitwa mapato ya nchi mbili kwani kuna mmapato ya zanzibar na mapato ya muungano. Kwa hili tu, tunaona jinsi gani kwa hoja za nguruvi3 hapo juu, pengine ni kwa miaka miwili tu kina nape na ccm watafanikisha malengo yao haya ya ajabu ajabu kwani muda sio mrefu "raia" wa "Tanzania Bara" watawazuia "raia wa Zanzibar" wasitumie kisichowahusu. Kwa upande wa zanzibar, wao wataendelea na malalamiko yao kwamba wanadhulumiwa mapato yao, kisa? Kukosekana kwa chombo cha kusimamia mapato ya "Tanzania bara".
Lakini nadhani ccm wanaelewa kabisa kwamba kuunda chombo cha kusimamia mapato ya Tanzania bara haiwezekani kwa sababu kufanya hivyo kutahitaji uundwaji wa serikali ya Tanzania bara (Tanganyika).