Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)


unanichosha unapukua mtabiri wa maisha ya Zitto
 
Mkuu pamoja na Mkandara kwanza muelewe neno supreme leader lina maana 'kiongozi mkuu''. ACT kwa mujibu wa katiba yao wamelitumia neno kiongozi mkuu.

Hivyo supreme leader ni mbadala wa kiingereza wa neno kiongozi mkuu, sioni sababu za kuhamaki

Pili, nadhani CCM siyo tatizo kwa Zitto. Anapokaa nao jukwaa moja akiwasumanga wananchi wasio na hatia wa mikoa ya kaskazini, then CCM haijawa tatizo kwake

Kwa miaka 50 CCM ndio wenye serikali, ndio wanaoamua mustakabali wa wananchi wa Kilimanjaro, Shinyanga, Mwanza na Arusha.

Wananchi wa mikoa hiyo hawana nguvu za kuamua mustakabali wa wenzi wao

Kurusha tuhuma nzito kwa watu wa kanda za kaskazini ni jambo la kusikitisha sana, tena akiwa meza moja na wale aliopaswa kuwaeleza alichosema

Tatu, hili la kwisha kisiasa sina uhakika nalo, ninachojua ni kuwa Zitto wa issue za kitaifa siyo Zitto huyu wa kugawanya wananchi kikanda na kuchochea chuki miongoni mwao.

Hivi inapofikia mahali anaeneza chuki badala ya issue hapo kisiasa anakuwa kundi gani? Ana paa au ndio mwanzo wa muflisi?
 
Na Mwenyekiti sio Supreme kulingana na katiba za CCM, Chadema CUF na NCCR?
 
Na Mwenyekiti sio Supreme kulingana na katiba za CCM, Chadema CUF na NCCR?
Chairperson siyo supreme leader, ndio maana anaitwa chair

Anna M ni chair wa ACT kama wale wa CCM, CUF na Chadema.
Juu yake yupo kiongozi mkuu a.k.a supreme leader ambaye ni Zitto

Ni kama Iran, yupo Rais wa nchi halafu kuna kiongozi mkuu (supreme leader)
Kwa Iran supreme hachaguliwi na watu, anateuliwa na jopo kama model ya ACT kwa namna fulani(24hr kabla ya uchaguzi) jopo likja na jina

Ni maneno tu mkuu wala yasituondoe katika mjadala. Ukimwita kiongozi mkuu au mhusika mkuu na mwingine supreme leader kama tunaelewana sote tunaongelea nini sioni tatizo mkuu.
 
Mkuu majina hutoka kwasababu nzuri au mbaya. Kwa upande wa supreme, majina hayatungwi na watu , yanaletwa na ACT. Kwa mfano, katika waraka supreme leader ametambuliwa kwa jina la Mhusika mkuu(MM). Jina hilo wamaelitoa akina Mwigamba na Kitila.
Katiba ya ACT inamtaja kama kiongozi mkuu, sisi wengine tunasema ni supreme leader kwa maana ile ile ile ya kiongozi mkuu . Mbona una hamaki?

Pili, nichepuke kidogo kuhusu katiba. Framework ya katiba ipo katika muundo. Period.
Hatukuwahi kuwa na tatizo la haki za binadamu, makundi ya kijamii n.k. Tumekuwa na tatizo la muundo na hilo ndilo chanzo cha mengine yote. Hivyo, muundo ni lazima uwe addreesed ili kuweza ku address mengine

Mkuu, huanzi kuvaa suruali halafu ile ya ndani, itakuwa kituko. Unaanza na ile ya ndani halafu suruali, shati, koti na sombrero, utapendeza

Kuhusu mawazo ya kina Zitto ya kulimega taifa, kama unaona ni mazuri hewalaa!
Sisi tunao yaona ni fyongo tutakemea kwa nguvu zote. Zitto amezaliwa awe raia siyo kiungo cha vurugu.

Tunauliza, hivi mawazo ya wananchi wa kanda ya kaskazini kuwapora wenzao wa kanda ya kati na ziwa rasilimali ni ya kweli? Yana mantiki? Yanaingia akilini hata kwa bahati mbaya?
 
Nyie watetezi wa kauli ya zitto ya kulimega taifa, please njooni na takwimu alizotumia Supreme leader, fafanueni takwimu hizo kwa hoja na mnatiki ili mtushawishi kuwa supreme leader alilenga kujenga taifa na si kulivuruga kwa kuchochea chuki miongoni mwa wananchi
 
Acha uhuni mkuu wangu kwa kutumia majina ya kuondoa maana. Unataka kunambia Kikwete kwa sababu anaitwa Rais ana nguvu za kiutawala serikalini kuliko Prime Minister wa Canada? Tunaijua nguvu ya JK, Mbowe na Lipumba ndani ya vhama na ndio wasemaji wakuu na wala mimi sioni ubaya ikiwa tu kanuni inaruhusu hivyo lakini wakubali vyeo vyao kushindaniwa na kwisha kama kanuni inavyotaka hapa ndipo tunapogomba. Itifaki za vyama vyote hivi wanaandika tu kama utaratibu wa kikatiba lakini nguvu ya watu hawa ni tofauti kabisa na ukweli uliopo na ndio itifaki.

Na lile neno MM lilikuwa MHUSIKA MKUU ina mana gani kuwa ndio Supreme! Kwa hiyo ttunapojadili hapa na Mhusika mkuu ni Zitto inamfanya yeye Supreme wa mada hii sio? Halafu ile e-mail, huwezi kuweka jina la Zitto e- mail inapokwenda lakini aloituma kajiandika Chademampya kuficha jina lake. Mnatunga mengi sana tuone kuna ukweli kwani huyu mtu aloweza kuficha jina lake lakini akatumia anuani ya Zitto huoni kama hii haikukaa sawa? Zitto mjinga kiasi gani atumie e-mail yake wakati anayemtumia kajificha wakati anayetakiwa kufichwa ni Zitto.
 

Thanks mkuu...stay blessed

Naona wananiongezea hamasa ya kupata ukombozi sahihi na genuine; sio ukombozi wa ukipofu kwa ubovu wa CCM

I will support zitto, akikosea nitakuwa wa kwanza kumwambia hapa umekosea!! kwa hili la cdm na zito, Zito yuko sahihi kwa mizani zote

sipati picha kama cdm ingekuwa ccm na ingewezaje ku handle makundi yaliyomo ccm

sipati picha cdm ikishika dola itawezaje ku resolve conflicts zinazotokea za wafanyakazi, jeshi, wanafunzi n.k

Zitto ni kinyago cha chadema kimetengenezwa na kulelewa na chadema! ni mtoto wao wa kumzaa sio wa kutoka vyama vingine-CCM kazaa vyama vingi baadae wakajifunza...CDM kaanza na huyu firstborn

wale wazee wa busara wako wapi? wale wa kutatua migogoro walikuwa wapi? no...hapana! kinachoendelea sasa ni historia, imeandikwa na inaandikwa tutakutana hapa hapa

CDM were supposed to be proud by having him, zitto ndio kahamasisha vijana kupenda upinzani na kujenga hoja...before that wala vijana hawakuwepo wala kuwa interested na siasa

CDM, chacha wangwe ilikuwaje? kafulila? machali? n.k cant someone stand up and say tujitazame ndani ya cdm? nguvu ya pesa ya mbowe kweli imewafanya watu wasiuseme ukweli?? wasione tatizo...bado tunajiita wasomi kweli?

nani sio msaliti ndani ya cdm? cdm ni chama cha wasaliti? nani anaaminika? tuwe wa kweli

Vyama vyetu vyote vya siasa vina wenyewe...when and how these parties can be a place to accomodate anyone? when can our kids take these parties be a place where they can dream being presidents and ministers??

mkuu; tutasubiri sana sana yaaani hata cdm wakiingia ikulu kesho bado haitabadilisha hiki hapa juu
 
Yaani wangelijua kwamba kwa kila wanachoandika Kibaya juu ya Zitto ndivyo wanavyomkweza juu na kucvuna wananchama wasinge endelea. Inakuwa kama Buhari rais mpya wa Nigeria alipandishwa chat na chama tawakla wenyewe kwa matusi na vijembe wananchi wakaipata picha halisi, wakafanya mambo. Nguruvi3 Mimi naona kweli mpango mzima ACT ningekuwa Bongo ningeitafuta kadi yao..
 
Last edited by a moderator:
Wanaukumbi.

Hebu tuwasome kiduchu hawa matapeli wa kisiasa ambao tunaambiwa wanataka kuwakomboa wadanganyika.

Kwa siku za karibuni, umezuka mjadala mkali ndani ya mitandao ya kijamii- hasa baada ya-Samson Mwigamba-ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha kuwatuhumu viongozi wa kitaifa wa CHADEMA kuwa wamebadilisha katiba kinyemela kwa kuondoa ukomo wa uongozi wa awamu mbili ili waendelee kubaki madarakani.-Mwigamba alitoa shutuma hizo akitumia jina bandia la-Maskini Mkulima. Katika shutuma zake Mwigamba alisema yafuatayo;"Wakati tukifanya mabadiliko ya katiba mwaka 2006 hatukugusa kipengele kinachomzuia kiongozi kuongoza kwenye nafasi moja kwa zaidi ya vipindi viwili vya miaka mitanomitano.-"Lakini wakati katiba inachapwa chini ya uongozi uliopo, kipengele hicho kiliondolewa kinyemela. Mambo yanayotokea hivi leo yanaonyesha dhahiri kipengele hicho kiliondolewa kwa makusudi kwa maslahi na kwa faida ya viongozi waliopo madarakani kwa sasa.-"Hiki kinaweza kuchukuliwa kama kitendo kidogo lakini kama viongozi wetu wanaweza kutokuwa waaminifu katika jambo kama hili, ni dhahiri hawawezi kuaminika na wanaweza kufanya mambo mengine makubwa nayenye athari zisizomithirika kwa chama.-"Ni muhimu wanachadema mkafahamu kwamba kitendo cha kuondolewa kwa kipengele hicho ndicho kinacholeta mpasuko leo kwenye chama unaotokana na Mbowe na Zitto kupigania uenyekiti."Kama kingekuwepoleo Mbowe alikuwa anakatazwa na katiba kugombea kipindi cha tatu na hivyo vita iliyopo kati yake na Zitto isingekuwepo na chama kingekuwa imara zaidi.-"Ni dhahiri Mbowe aliondoa kipengele hicho kwa makusudi ili aweze kuendelea kugombea bila mwisho na huu ni udikteta kama ule tu wa akina Lyatonga Mrema, John Cheyo na wengineo, na wanachadema hatupaswi kuuruhusu si kwa Mbowe tu bali kwa yeyote atakayepata nafasi ya kuwa mwenyekiti wa chama chetu."Mara baada ya taarifa hiyo ambayo ilibebwa kwa jina la-Wito kwa wana CHADEMA wote!-ambayo ilieleza madhaifu ya chama na kubadilishwa kwa vipengele vya katiba kinyemela, Dr Slaa, Katibu Mkuu wa CHADEMA alitoa ufafanuzi ufuatao;"Nataka kuwahakikishia wanachadema wote kuwa- nimekuwa ndani ya Chadema kuanzia 1998 ambapo nilikuwa Makamu Mwenyekiti Bara, na baadaye 2003 Kaimu Katibu Mkuu, na hatimaye Katibu Mkuu, hivyo nimeshiriki kikamilifu kuandaa Katiba ya 2004 na pia Katiba ya 2006 baada ya Rebranding ya Chama.-"Nataka niwahakikishie wanachadema, hakuna toleo lolote la Katiba ndani ya Chadema imeweka " muda wa Uongozi kuwa vipindi viwili tu", kuanzia Katiba aliyoiasisi Mzee Mtei na kupitishwa na Mkutano Mkuu, wala si ya 2004 au ya 2006.-"Kama kuna mtu anasema ilikuwepo na imeondolewa kinyemela, basi aonyeshe kifungu hicho kwenye Katiba yeyote ile, au miniti za kikao chochote kile."Hata hivyo, majibu hayo ya Dr Slaa yanaonekana kutofautiana na yale ya JOHN MNYIKA aliposema kuwa kwenye katiba ya 2004 kipengele cha ukomo wa uongozi kiliwekwa lakini hakikuingizwa kwenye katiba ya 2006. John Mnyika anasema- yafuatayo;"Kuhusu Katiba, nina nakala mango (hard copy) tu ya katiba ya 2004, ilikuwa na kipengele cha vipindi viwili vya nafasi ile ile. Hata hivyo, katiba mpya iliyoandikwa mwaka 2006 haikuwa na kipengele hicho. Hivyo, sio kwamba kimeondolewa kinyemela ila hakikuwepo kwenye katiba mpya. "Baada ya malumbano hayo, nilifanya utafiti mdogo ili kujiridhisha na hoja zilizotolewa na viongozi hao. Kwa msaada mkubwa kutoka kwa wadau muhimu ndani ya CHADEMA, nimefanikiwa kupata nyaraka zifuatazoNakala ya Katiba ya CHADEMA ya mwaka 2004 iliyoandikwa kwa lugha ya KiingerezaNakala ya Katiba ya CHADEMA ya mwaka 2006 iliyoandikwa kwa lugha ya kiswahiliMuhtasari wa Mkutano Mkuu Maalum wa CHADEMA uliofanyika katika ukumbi wa PTA Dar es Salaam tarehe 13, Agosti 2006Nitajaribu kuweka vipengele muhimu mahsusi kwa mjadala huu. Nitajikita kwenye hoja moja tu ya Mwigamba kuwa Viongozi wamefanya marekebisho ya katiba kinyemela kwa kuondoa ukomo wa madaraka ili waendelee kuwepo madarakani.--Katiba ya mwaka 2004 ipo wazi kabisa katika hoja ya ukomo wa madaraka. Ibara ya 6.3.2 kipengele cha (c) kinasema ifuatavyo;-''Leaders who finish their term of office can be eligible for re-election provided he qualifies but-no leader can hold the same post at the same level of the party structure for more than two terms.-Kutokana na kipengele hiki, kauli ya Dr Slaa kuwa hakuna katiba ya CHADEMA iliyoweka ukomo wa madaraka ni ya kushangaza ikizingatiwa kuwa yeye ni Katibu Mkuu na hakupaswa kusema uongo mbele ya watu ambao wanaelewa mengi kuhusu katiba hizo.Katika Mkutano Mkuu Maalum wa mwaka 2006 ambao ulikuwa na ajenda 4 ambazo ni;Kufungua MkutanoMaboresho ya KatibaMaazimio juu ya Katiba Mpya naKufunga Kikaoulijadili vifungu 10 ambavyo vimefanyiwa marekebisho kutoka kwenye katiba ya 2004. Kati ya vipengele hivyo, kipengele cha ukomo wa madaraka hakimo na hii ni kusema kuwa hoja hiyo haikuwa na marekebisho. Vipengele vilivyofanyiwa marekebisho kwa mujibu wa muhtasari huo vimeambatishwa na taarifa hii.--Katiba ya Mwaka 2006 ndiyo inayolalamikiwa kuchakachuliwa kwa vile kipengele cha ukomo wa madaraka hakimo na hakuna mkutano uliojadili hoja hiyo.---Kutokana na hali hiyo, ni wazi kuwa hoja za Samson Mwigamba ni sahihi na viongozi wa CHADEMA hususan DR WILBROAD SLAA NA JOHN MNYIKA wametoa majibu ya uongo kupinga hoja za kweli. Kwa mantiki hiyo,-ni wazi kuwa katiba imechakachuliwa kwa maslahi ya wanaotetea uchakachuaji huo.--
 
Kuna Supreme Leader mwingine mbona unamsahu au ndiyo mahaba niuwe.

Mbowe, huyu ni supreme leader Chadema, na ni mwenyekiti wa maisha wa Chadema.

Lakini hauwezi kumtaja hapa unahofia mkate wako mkuu.

Katiba ya Chadema inamkataza Mbowe kugombea uenyekiti vipindi vitatu lakini wapi Supreme Leader kaishaamua kuondelea kuongoza mpaka atakapchoka.

Naona karamu zenu mmezificha mchagoni nyie mnalia na Zitto tu, lakini inasaidia sana mnazidi kumpa promo.
 
Mkuu hizi sifa za kutengeneza kwa Zitto ndizo Mchambuzi amezitolea ufafanuzi

Pius Msekwa akiwa katibu mtendaji wa TANU(alikuwa katika 20s)
Akina Warioba walianza kuwa viongozi wakiwa vijana wadogo, tena wakitandikwa viboko

Hawa akina Samwel Sitta, Malecela na wenzao hawakuanza siasa uzeeni. Wameanza wakiwa wadogo

Nyerere akiwa na miaka 26 alikuwa tayari kaanza harakati za kisiasa kuwaunganisha Watanzania dhidi ya adui, akiwa katika 30s anakwenda kudai uhuru. Katika umri huo supreme Leader anapita kugawa wananchi kwa misingi ya ukanda

Kila kitabu na zama zake. Kwa wale wa karibuni supreme ni hero wao. Kwa wengine tulio ona mengi supreme ni tatiZO.
IKifika mahali mtu anakosa cha kuongelea bali kuwagawa wananchi, kama si tatiZo sijui ni nini

ukumbuke,wazee niliowataja walikuwa na kazi ya kuwatengeneza vijana, leo wengi ni viongozi.
Zitto amehamasisha vurugu, utakubali kuwa makundi ya vijana ndani ya CDM wakiwemo Kafulilawametaja supreme kama kiungo

Wametaja namna walivyotoa sehemu zao za haja kubwa ili walimwe chale na matatibu wa kienyeji
Hatuwezi ku qualify hiyo kama uhamasishaji, ni uharibifu

Hayo ya ugomvi na chama chake wanayajua wao. Tunachokijua sisi ni kile tulichokiona, Waraka

Ni nyaraka iliyojaa matusi na kashfa kwa viongozi wenzake. Huwezi kuwa na makundi ya kisiasa ya matusi

Leo tunafahamu kuwa ule waraka uliandikwa kwa chuki. Ushahidi ni pale waraka uliposema ' Akili ya mwenyekiti ni ndogo'

Kinachoshangaza hatujui uwezo wa mwenyekiti Anna hata hivyo tuna kumbu kumbu za kukataliwa kila mahali.
Hatuna uhakika kama ndio akili kubwa akina Mwigamba, Kitila na Zitto walioyokuwa wanaitamani. Hiyo ni juu yao wenyewe

Pengine sisi wengine tuongelee unafiki. Hakuna chembe ya shaka huyu bwana ni mnafiki.

Alipokuwa CDM alilaani ukanda na kusema ndilo tatizo. Leo anasimama katika vipaza sauti mikoa miwili akitengeneza ukanda hadharani na wala si kusika. Huo unafiki mnauita ushaujaa, well, wengine hatuna shaka ni unafiki mkubwa

Waraka ulilaani kuchezewa katiba na watu. Ni supreme leader amekubali katiba ya chama kwa ajili ya wanachama ibadilishwe ili kukidhi haja yake ya kuwa kiongozi mkuu na ukipenda supreme leader. Huu kama si unafiki, sijui ni kitu gani

Zitto akatoka nje ya BMLK kama wenzake. Wiki chache anasimama na kusema walikosea kutoka. T

umemeuuliza Mkandara, lengo lake la kutoka lilikuwa ni nini, na alifikia lengo gani?

Ukiangali hiyo ni tabia ya kutenda jambo moja akiamini jambo jingine, yaani unafiki mkubwa

Huyu huyu akaita wenzake wasaka tonge. Siku chache akataka kufanya kazi na wasaka tonge.
Unafiki ni tabia tu, huwa inatulia lakini haipotei kabisa. Ni kitu kilichopo kwenye damu.

Akaenda mahakamani akiwa na chama kingine. Kasema anasimamia haki na sheria.
Kumbe haki ni kuvuta muda wa ubunge wake. Ni tabia tu, muda ukifika hujidhiri. Unafiki!

Hili la kwenda mikoani na kuanza kulimega taifa, hatutakaa kimya. Tabia hiyo ameiona Kigoma kutoka ng'ambo ya nchi.

Hata kama ana vinasaba, haijuzu kututia katika matatizo kwasababu Tanzania itakuwepo bila Zitto
Hatutakubali taifa limegwe na waroho

Keshaonja tamu ya kufarakanisha watu kuanzia vijana hadi wazee, sasa anakwenda next level kulichonganisha taifa

Hapana! unafiki anaweza kuendelea nao, Taifa ni letu atuachie taifa na nchi yetu salama.

Hakuna data wa support ya hoja zake za Shinyanga, kama zipo wekeni hapa!

Hatukubali taifa liingie matatani sababu ni supreme. Hapana! alipogusa taifa tutakomaa naye tu.
 
Last edited by a moderator:
Ritz yote haya hata mimi niliyapitia na ndio msingi wa hoja zangu kwa sababu najua makosa yalifanyika halafu baada ya kufanya makosa wanakuwa wakali wao. Hii inanikumbusha hata jamaa zangu nawapa mtaji wanakula, utawafungulia Biashara watakula hadi mtaji. Nikiwauliza sababu wao wanakuwa wakali tena hata kusema undugu ufe basi, hi akili kweli? . Mbona mimi namjua namba 2 (M2), na hadi kesho bado yupo Chadema au yeye alikuwa mpelelezi?

Kauli kama hizi zinatisha na wengine hutukumbusha mbali sana na hii ndio exactly picha ya Zitto na kina Mwigamba. Ukweli tunaujua tatizo hawa watu wanataka kuongopa na ndio maana kila siku lazima watafute mchawi maana kuuzima uongo kazi kubwa sana.
 
Mkuu, maadamu upo hapa GT, jitahidi walau kuandika kwa utaratibu mzuri. Yaani haijulikani umeanzia wapi na umemalizia wapi. Heshima mbele lakini.

Wanaukumbi.

Hebu tuwasome kiduchu hawa matapeli wa kisiasa ambao tunaambiwa wanataka kuwakomboa wadanganyika
 
Jamani kama wapo ma supreme hao hatuwajui kwasababu hawajatangazwa au kujitangaza

Katiba ya ACT inataja Kiongozi mkuu. Kwa lugha ya kiingereza ni supreme leader
Kuna Mwenyekiti (chairperson)wa ACT Anna M, na kiongozi mkuu (supreme leader). Hii ni kwa mujibu wa katiba ya ACT

Kwamba, wana mfumo tofauti kama alivyoeleza Kitila gazetini. Sisi tunafuata tu maelekezo ya mshauri wa chama
Sasa kama kutumia neno supreme leader ni maudhi, wakulaumiwa ni katiba iliyompa nafasi hiyo tena kwa njia za express

Hatuna tatizo kama watakuwepo ma supreme wengine, muhimu ni wao au katiba zao zijieleze kama walivyojieleza ACT

Kwani Zitto kuitwa supreme inawachefua sana kuliko Zitto kusema K'njaroArusha wanachangia kidoogo, wanapewa sana. Mwanza/Shinyanga wanachangia saaaana wanapewa kidogo. Kwamba wapo waporaji na waporwaji!

Tupeni takwimu alizotumia, facts na support za kauli zake. Kama hamna basi tuacheni tuensdelee kukemea uovu, unafiki na uroho
 
Nguruvi3,
Pengine wewe unakijua kiswahili vizuri kuliko sisi, ebu tuambie kama chama kinatumia neno viongozi, itifaki ya Uongozi wa chama Kitaifa toka juu utasemaje? maana akiitwa Rais wa chama ndio mtammaliza kabisa kwamba aliutaka urais kajipa chamani..Sasa ulitaka watumie jina gani haswa..
 
Mkuu, maadamu upo hapa GT, jitahidi walau kuandika kwa utaratibu mzuri. Yaani haijulikani umeanzia wapi na umemalizia wapi. Heshima mbele lakini.
Usiwe punguani wewe mimi siyo mara ya kwanza kuandika kwenye ili jukwaa tabia zako za kike peleka jukwaa la siasa usitake tuchafue jukwaa wewe nani humu kupangia watu cha kuandika unajipa majukumu ambayo siyo yako.
 

Kwa watu tunaoamini demokrasia ya vyama na ndani ya vyama, hatuwezi kusema kuwa ilikuwa dhambi kwa ZZK kuutaka uenyekiti. Lakini kitu kimoja tunachotakiwa kujua ni kuwa ndani ya chama au kundi lolote, kuna wakati busara inatakiwa kuongoza na sio maslahi binafsi na tamaa.

Tangu ZZK alipoteuliwa kuingia PAC alijiona kuwa yeye ni mkubwa kuliko CDM, au naweza kusema tangu alipoonja tamu ya usaliti, na kuanza kui-expose CDM kwa wasio wanachadema, akaota pembe na sharubu na kujiona yeye ni sehemu ya watawala na anatakiwa kutawala. But that does not work in the group that thinks as a team.

As bad as it is, kujadili watu ni cheap, tunatakiwa kujadili issues and policies, lakini tunapokuwa na wanachama wanaoweka mashali yao binafsi na personal ambitions juu ya chama, wao wenyewe wanasababisha watu tuingie kujadili ujinga.

Alichofanya ZZK ni sawa na alichofanya AL Mrema. Na mwisho wake utakuwa ni sawa na wa Mrema. Mrema alikosa uenyekiti CCM, akaufuata NCCR na TLP. ZZK alikosa uenyekiti CDM sasa tuangalie na hiyo ACT yake atafanya nini kabla ya October, likely ataanza kubadilisha jina la chama na baadaye ataanza sarakasi na ataishia kama Mrema tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…