Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)


Mkandara nilitaka kukuonyesha kuwa takwimu za Mchambuzi zililetwa hapa baada ya wewe kuziomba..Ni hilo tu turudi kwenye hoja.

Ukisoma maelezo ya Nguvuri3, unaona mjadala uliokuwa humu JF na ambao wewe ulishiriki ulizua sintofahamu nyingi, ulileta chuki za wazi, wachaga walidhalilishwa,kejeriuwa, baadhi ya watu walifikiri kuwa wao hawathaminiwi na taifa lao maana kila kitu kinakwenda KLM na nk. Na katika hili KAMA lengo la Zitto lilikuwa si kuchonganisha basi alitakiwa aje elezee alichomaanisha na awaombe watanzania kwa kuzusha uchonganishi miongoni mwao maana halikuwa lengo lake. Tungemuelewa na Tungemsamehe na kusonga mbele, lakini kinyume chake ZItto alikaa kimya akaacha watanzania wakiparuana wenyewe kwa wenyewe na si ajabu moyoni mwake alikuwa anasema "Matanzani majinga tu ona yanavyuparuana yenyewe kwa yenyewe huku akishusha moja moto moja baridi.. Siasa za namna hii ni za "KIITARAHAMWE"

Zitto ni mchumi tena mchumi Tanzania nzima hakuna mchumi kama yeye, Zitto ana akili sana, na Zitto ana siasa za kistaarabu, Sasa basi elimu yake ilishindwa kujua kuwa "uchangiaji wa pato la Taifa hauna usihano wa moja kwa moja na maendeleo ya mikoa husika? Alishindwa kujua kuwa Migodi kutosaidia kuleta vichocheo vya maendeleo si kwa sababu kuna mkoa unaoitwa KLM bali ni uzembe wa Mkapa na serikali yake? mbona wewe umegàmua hilo? Hivi alishindwa kuelewa kuwa umasikini wa Shinyanga hautokani na watu wa Arusha?

Kama swala ilikuwa ni kuongelea mikoa yenye maendeleo/uchangiaji wa pato la Taifa mbona ameiacha Lindi mkoa ambao ni kati ya mikoa inayochangia kwa kiasi kidogo sana katika pato la Taifa lakni ni mkoa wa 9 kimaendeleo? Sikiliza hiyo Video kataja Tabora inachangia pato la Taifa ikiwa ya 10 baada ya hapo kaenda kupanga mikoa yenye maendeleo, katafuta Klm ilipo kaikuta ni 9 kuchangia pato la Taifa kaishiki bango, mbona asitumwambie mkoa wa 10 ni hupi? si kaanzia chini? kwa hiyo utaona hapa alichokuwa anatafuta Kilimanjaro tu si kingine.

Na kama angekuwa anamaanisha kitu kingine angekuwa ameisha ingia humu na kutueleza lengo lake likuwa nini? maana mara ya mwisho kuingia humu ilikuwa jana tu. Haji hapa maana lengo lilikuwa chuki zake kwa watu hawa.

Kama hisingekuwa chuki basi angeanza na Lindi mkoa ambao ni kati ya mikoa inayochangia kwa kiasi kidogo sana katika pato lakni ni ya 9 kimaendeleo.. Na hapa kama mwanasiasa angejiuliza ni kwanini Lindi wanaweza na Tabora, Shinyanga wasiweze hali wanalima pamba, mchele, wana mifungo na nk.

Kwa hiyo tatizo angelikuta kwa wenyeji wa mkoa huu elimu bado ni ndogo sana, pia miundo mbinu ni kikwazo kwa ajiri ya kusafirishaji wa mazao yao, Na sote tunafahamu bila elimu hakuna maendeleo ndo maana dada yangu gfwinson ametueleza kuwa watu wa vijijini wakati mwingine wanapesa kuliko watu wa mjini lakini kutoka na elimu ndogo mtu hafahamu hizo hela hazitumieje. matokeo yake ni kuongezea wanawake, kulewea pombe na nk. Sasa hapa ndipo tunapotegemea viongozi ambao ni wanasiasa kuwaeleza watu muhimu wa kujiletea maendeleo badala ya kuanza kuwachonganisha.

Hebu niambie leo Shinyanga ni maskini lakni wakazi wa vijijini wana mali yenye thamani kubwa kuliko wa watu wa mjini. unakuta mtu wa kijijini ana ardhi kubwa tu, ana mifungo mtu mmoja ana zaidi ya Ng'ombe 1000 mbuzi husiseme, kuku na nk. Hivi huyu mtu ni masikni kweli? au amekosa elimu ya kufahamu vitu alivyonavyo vinaweza kumsaidia kuwa na maisha mazuri kuliko mtu wa mjini. maana anaweza kabisa kujenga nyumba ya kisasa, kuweka solar, kupeleka mtoto wake shule kusaidia shughuli mbali mbali katika eneo analoishi kama kujenga barabara (si lami) kujenga visima,choo na nk. kwa mtaji wa Ng´ombe 500, mbuzi, na kuku pamoja na uuzaji wa maziwa.

Tanzania kama Kilimanjaro wameweza, kama Lindi wameweza nina imani hata mikoa mengine wakipata viongozi ambao wanauchungu na matatizo ya wananchi wao basi wataweza kujiletea maendeleo.

Wanasiasa waache uchonganishi, waache porojo wao ndo wanakomba hazina ya taifa kwa kujilimbikizia mIshahara minono na malulupa yasiokuwa na maana. Kama hiyo mil200 wanazokopeshwa kila mbunge zingepelekwa kwa wakulima, kwa wafugaji, kwa vijana wenye viwanda vidogo vidogo, wakapewa elimu, wakapewa watu wa kuwasimamia, miundo mbinu ikatengenezea basi Tanzania tungepiga hatua tena kubwa tu katika swala zima la maendeleo. Sasa anapojitokeza wanasiasa anayelipwa mamilioni ya shilngi hasiyostahili na akaona hilo halitoshi na kuanza kutuchonganisha huyu HATUTAMPA NAFASI.
 

Kawachonganisha kina nani zaidi ya nyinyi kumlisha maneno,yeye kazungumzia huu lazima ubadilike,nyie mnaleta tafsiri zetu,atawajibika kwa alichokisema sio mlicho tafsiri nyinyi
 
Kawachonganisha kina nani zaidi ya nyinyi kumlisha maneno,yeye kazungumzia huu lazima ubadilike,nyie mnaleta tafsiri zetu,atawajibika kwa alichokisema sio mlicho tafsiri nyinyi
Hewalaa, tulitumia maneno yako na Supreme leader kukuuliza haya Tukaomba ufafanuzi wa hoja zako kwa kukuuliza haya Ukajibu hivi
nitakujibumkuu
Hadi leo!!!

Unawezaje kusema supreme leader kalishwa maneno ikiwa weweuliyemnukuu huwezi kuandika hata mstari kwa kile ulichonukuu?
Rudi katafute majibu kwanza, huu mjadala ni mkubwa kidogo

 
Alinda katika bandiko lako 1081 , umeweka misumari mizito sana

Supreme leader alizungumzia Kilimanjaro katika njia mbili kuu.
Kwanza, kutafuta wapiga kura akiamini chuki ingempa fursa ya kuijijenga.

N ingumu kufanya ‘attack' kwa CCM kwasababu zisizo wazi, Supreme alienga upinzani, ndio maana tunasema ACT ni mpini


Pili,SL anaeleza hisia za mgogoro wake na viongoziwa zamani akifikiri ni njia rahisi ya kupata kuungwa mkono.

Alifanya bila kujali athari zinazoweza kutokea kwa taifa. Kukaa kimya ni makusudi, umesikia kachukua form bila kuita waandishi. Alifahamu swali litaulizwa, na hawezi kulijibu kinyume na dhamira yake.

Kuhusu Lindi, mfano wake haukuzingatia ‘sampling' kwa ufasaha
Historia inaonyesha anashambulia mikoa ya kaskazini, sampe yake ilikusudia na wala si bahati mbaya.

Tazama, Lindi inachangia kidogo sana, lakini kwa maendeleo ipo juu kuliko Shinyanga.

Hawezi kuzungumzia Lindi kwasababu si ‘target' yake.Mfano wake haukidhi haja kwa anayetumia sehemu ya fuvu kufikiri


Watetezi wake wanasema, kila mkoa upate kulingana na uchangiaji wa pato.
Halafu wanasema serikali iendeleza maeneno yaliyo nyuma kwa kutoa kipaumbele

Kama hiyo ndiyo hoja, mikoa inayoshika nafasi ya 20 kuendelea haipaswi kuunga mkono ACT.
Maana yake ni kuwa masikini asiyeweza kuchangia atapewa kidogo. Hiyo inaua hoja ya kueneza maendeleo maeneo kote.

Hoja ya elimu ni muhimu sana. Watu hawaelewi k'njaro nimkoa masikini kutokana na uhaba wa rasilimali kama ardhi.
Zao la kahawalimekufa. Kinachouweka mkoa ule mbele ni mwamko wa wananchi na mbinu zakutafuta maendeleo.

Sehemu kubwa ya mapato ya watu ni remittance ,
kama zao la uwekezaji katika elimu kwa watoto wao walioko nje, na watoto hao kujali kurejea na kujenga kwao


Wananchi wa kijiji cha Nronga, wamejenga barabara kwa kuchangisha wanaoishi mikoani kutoka kijiji hicho( milioni100)

SL, Diamond, Ally n.k. wanaweza kuchanga kiasi hicho,achilia mbali maelfu ya wana Kigoma wanaoishi nje.

SL alipaswa kueleza ukweli, si kushambulia wananchi kama wa Nronga. Hatafanikiwa kwa fitna,bali mawazo huru na pana.


Supreme alitakiwa atumie mfano wa Nronga kuhamisisha, na si chuki binafsi na kufanya mgogoro wa kanda, mikoa n.k.

Hawezi kuomba radhi, ndivyo alivyokusudia na inafanya kazi kama alivyotaka, kugawa taifa na kuleta mtafaruku.

Swali la kujiuliza, atakapokwenda
Kagera, Singida, Mtwara na Morogoro mchawi atakuwa nani?
 
Mkuu mimi sikwepi swali la mtu kinachotakiwa ni wewe kunisoma ukanielewa. Swala la Shinyanga kama alivyoelewa Abunuas, ndivyo mlivyoelewa nyie achana kwanza na watu wa vijijini. Huwezi kumlaumu Abunuas kuzungumzia upande wa Zitto kwa fikra hizo hizo wakati nyie pia mnaamini maneno yale yale kuwa Zitto alimaanisha Wachagga wanawadhulumu Wasukuma. Mnapotofautiana ni kuunga mkono au kupinga!..

Kwa hiyo sio swala la watu wa vijijini watafikiri nini bali nyie wenyewe mmefikiri nini kiasi kwamba Abunuas upande wa pili ni mkosa wakati nyie wenyewe ni wakosa - Nyote mna fikira za Ukabila na nyie ndio mloshika mtutu kueneza Ukabila kwa hoja zenu juu ya Hotuba ambayo haina Ukabila.

Tofauti yenu na Abunuas ni upande gani kila mtu kasimama wakati mimi napingana na nyie wote ya kwamba maelezo ya Zitto hayana Ukabila kwa sababu Kilimanjaro sio ya Mkoa wa Wachagga na wala Shinyanga ya Wasukuma kwani watu wa makabila yote wanaishi mikoa hiyo. Mbali na hivyo hotuba yake imezungumzia mikoa mingi ikiwemo Dar, Arusha na Kilimanjaro kuwa juu na mahala pekee alipolinganisha ktk hotuba hiyo ni Mkoa wa Lindi na Shinyanga. Neno mkoa mkilifanya la Kabila fulani wenye matatizo ni nyie sio Zitto.

Muda wote huu nimetaka mjifanyie wenyewe reality check, inatakiwa kujitazama nyie wenyewe kwa sababu hata Mbowe katumia tena kabila la Wasukuma kuwa wako nyuma kwa sababu blaaa blaa blaa! msione ubaya katika maneno hayo isipokuwa ya Zitto hapa hamuoni kama nyie ndio mna tatizo? kwa nini mchague mtu wakati maneno ya Mbowe yameenda ndani zaidi ya Mkoa hadi kutaja Kabila haikuwa shida kwenu kuelewa? Kwa sababu mnaamini kwamba Wasukuma wako nyuma kweli kuliko nyie msokuwa Wasukuma na mnazijenga sababu kuwa Kilimanjaro wana miradi mingi ya kwao na kadhalika kisha mkasema kwa nini Shinyanga wako nyuma na mkajenga sababu wa watu sio Policy mkasahau kwamba walozungumza ni viongozi wa vyama wanauza Policies zao sio reasons! Kama huu wenu sio Ukabila, huo Ukabila ni kitu gani?

Nitazidi kuwapeni mfano wa Mishahara, Hivi mwanasiasa akisema mathlan akiwatetea Waalimu na Madaktari kwamba wanastahili mshahara mkubwa zaidi na akatolea mfano mchango wao na Jeshi au mambo ya Nje atakuwa anakosea kwamba anataka kuchonganisha waajiriwa wa wizara hizo?. Mimi sidhani hivyo isipokuwa tutazame kama kweli waalimu na Madaktari wanastahili mishahara mizuri kutokana na mchango wao kwa Taifa japo sii fedha.
 
Mkandara,

..siasa za kuchonganisha jamii moja vs nyingine ni mbaya na tusizipe nafasi.

..hata kulinganisha taaluma moja vs nyingine ni siasa za hatari hapa Tz.

..tena hiyo ya kuchonganisha madaktari na wanajeshi ndiyo hatari zaidi kwa nchi kama yetu.

..kila taaluma ina umuhimu wake hapa Tz.

..lingine baya zaidi ni kuchonganisha dini moja vs dini nyingine.

..wameishatugawa kwa dini zetu, sasa mnataka watugawe kwa makabila na mikoa tunayotoka!! tunaipeleka wapi nchi??

..Zitto alikosea kutoa kauli zile kule Shinyanga.
 
Wakabila hupenda kuona Ukabila kwa wenzao, Kwa Maisha ya sasa nchini kila Mkoa una watu wa Makabila yote, Anachokizungumza Zitto siyo suala la Wachaga vs Wasukuma, bali ni mikoa mbalimbali vs mingine katika uchangiaji wa pato la taifa na kunufaika nalo. Wenye hisia za kikabila na kumsukumizia Zitto ni reflection ya ukabila walio nao
 
Kawachonganisha kina nani zaidi ya nyinyi kumlisha maneno,yeye kazungumzia huu lazima ubadilike,nyie mnaleta tafsiri zetu,atawajibika kwa alichokisema sio mlicho tafsiri nyinyi



. 1. Labda tuanzie hapa nini maana ya hii sentensi?

"""Hata hivyo Shinyanga ni moja ya mikoa yenye Umaskini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia pato la Taifa,Mikoa yenye Maendeleo Zaidi ni Arusha,Kilimanjaro na Dar es salaam.
Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7 kuchangia Pato la Taifa."

2. Ukakasi huko hapo kwenye nyekundu, Je ni kitu gani alitaka kueleza? Kwamba kwa vile KLM na Arusha wanachangia wakiwa mikoa no.9 na 7 hawastahili kuwa na maendeleo au?


3. Pia tupeni shule "kiduchu" kwa uelewa wenu uchangiaji katika pato la Taifa unachangiaje maendeleo ya mikoa husika?

Kwa tafsiri yenu maendeleo ni nini?


 
Well ndivyo unavyotazama wewe swala hili lakini kwangu miye kama kuna Upendeleo unatakiwa kufanyika ama umegfanyika - tuseme juu ya mahakama ya kadhi ionekane ni upendeleo kwa waislaam, Mkristu anaweza kabisa kuzungumzia swala hilo kwa uwazi kabisa sababu tayari upande mmoja unatazamwa zaidi ya mwingine na ndivyo niivyosema kuhusu Apartheid, Wanaume dhidi ya wanawake na kadhalika.

Kama wanajeshi wanapokea mshahara mkubwa kuliko walimu na madaktari ipo haja ya kulitazama swala hilo na lizungumziwe kwa uwazi pasipo kufichwa na hasa Wanasiasa. Hatari ni pande zote, wananchi wako wanaweza kuuawa kwa mtutu ama kwa kukosa huduma ya Afya, mwanasiasa unatazama maslahi ya wananchi wako sio yako ama chama chako.

Nakumbuka wakati wa Mwalimu graduate wa University wote walikuwa na mshahara sawa haijalishi unaingia wapi isipokuwa unaweza panda mshahara kutokana na unavypopanda cheo. wakati ule nakumbuka vizuri sana 1982 ilikuwa Ukimaliza University mshahara utakao anzia ilikuwa Tsh. 2,020 au 2,040. Sheria inasema tu mhitimu wa chuo kikuu atapokea kiasi kadhaa sasa iwe Luteni, Mchumi au Daktari hapo ndipo unapoanzia, na hapa ndio unaweza kusema kila mmoja wao ana umuhimu wake.

Kwa hiyo katika Ubepari huu ambao nchi maskini kama yetu yenye vipaumbele tofauti, tukisema UMASKINI, ELIMU na AFYA kuwa ndio uti wa mgongo, halafu tunapinda shingo, ukaweka mahitaji ya wanajeshi mbele ya kila kitu wakati hatuna Vita, Kwanza wanakula bure, wanalala bure, usafiri bure huwezi kutoyatazama yote haya ukatazama mishahara ya Walimu na Madaktari. Umuhimu wa kila kitu unatokana na mahitaji yenu, sio kupendelea watu kwa sababu unaogopa kupinduliwa ama kuwaridhisha.

Ni hatari sana katika uchumi wa nchi kuongoza kwa fadhila na tumeona viongozi wangapi wakipewa madaraka wasiyostahili kwa sababu tu ni washikaji wa Mkulu. Kwa nini tusiseme kuogope italeta kuulizana ni dini gani au kabila gani? Wenye matatizo ni wale watakao fikiria mtoa hoja ana Udini ama Ukabila kwa mwajiriwa badala ya kutazama malalamiko yanahusu nini? TRA imelalamikiwa kwa kujaza Wachagga..itakuwa sio Ukabila ikiwa kuna Ukweli. Zamani nakumbuka Bima ililalamikiwa kwa kujazwa Wanyakyusa, haya ni mambo ambayo serikali inatakiwa kuyatazama kama yalivyo na sii kuhofia Ukabila. Ukabila ama Udini unaanza na yule mwenye kutenda ama mwenye kutafsiri hivyo mahala hakuna.

Isipokuwa kuna habari za Uzushi zenye lengo la kujenga Ukabila na Zitto hakufanya hivyo wala Mbowe isipokuwa nyie mlotafsiri ndio mlikuwa na Ukabila nyuma ya hoja yenu. Zitto hakukosea kwa sababu kaeleza jinsi gani michango ya mikoa inavyochangia mfuko wa Taifa na mikoa mingine imeachwa nyumba hapo hakuna cha Mchagga, Wamwela, Wamachinga wala Msukuma. It is the fact na sii sera tu za chama zinaweza kubadilisha mfumo huo isipokuwa ITIKADI ya chama yenye kutambua haki, vipaumbele na matumizi bora ya fedha za Umma katika uwekezaji ili kuuza ajira. Zitto aliahidi kuubomoa mfumo huo aidha mnalalamika kwa sababu mnafikiri Zitto kusema hivyo basi Kilimanjaro itapunguziwa mgao wake.
 
Thank You.....
 
 
NdivyoTulivyo yaani ukitaka kuwajua wadanganyika zungumzia chake tu utasikia.
Na saa hii habari ya UJAMAA matumbo moto maana wanajua UNYONYAJI utapigwavita hata iwe mkoa kwa mkoa .
Gambala Nyoka , hivi unamwelewa huyo uliye nyuma yake? Msome Mkandara, leo anaandika hiki kesho anakikana, keshokutwa anakirudia. Ndio maana Mag3 alikuambia soma kwanza uelewe nini kinaongelewa.

Unaona hoja zako zinavyobomoka kama barafu





 

Wewe hukubaliananinkwa sababu
Gamba la Nyoka, Mkandara anasema ukweli wa makabila kama alivyosema Zittousemwe tu. Soma maandishi mekundu. Huyu ndiye upo nyuma yake, mkuu huoniunavyoadhirika

Kuhusu ukabila, sisi tujmeongelea mikoa. Lipo bandikonimemuonya Mkandara kwa kumwambia Kilimanjaro si wachagga, nkampa mfano waWapare, Wakamba. Nikasema Arusha ina makabila ya Waaerusaa, wameru, wabarabaig,wamasai n.k. Hivyo mashambulizi ya Zitto dhidi ya mikoa ya kaskazini ni hatarikisiasa kwakwe na ni hatari kwa taifa. (kama utahitaji ushahidi upo

Sasa endelea tu maana tuna nondo za kutosha za kuonyeshaukabila, udini wa Mkandara.

Tuna nondo za kutosha kuonyesha flip flop ya Mkandarakatika mada. Hayo hapo juu ni kifungua kinywa, kama utahitaji Lunch na Dinner,hewalaa
Ulaghai wa supreme ni ule wa wafuasi wake
 
Eh hizi sasa Sarakasi, Ilianza ACT ikahama , Ishu Ikageuka na kuwa Zitto, Sasa siyo Zitto tena bali imegeuka na kuwa Mkandara.....Hamna hoja hapo ni vioja tu!
 
Eh hizi sasa Sarakasi, Ilianza ACT ikahama , Ishu Ikageuka na kuwa Zitto, Sasa siyo Zitto tena bali imegeuka na kuwa Mkandara.....Hamna hoja hapo ni vioja tu!
Tunakujibu maana ulianza 'small mind' ghafla umerudi na kutetea alichosema.

Tunajua wazi kuwa Zitto aana mashambulizi kwa mikoa ya kaskazini kutokana na chuki zake.

Na Supreme anafanya hivyo kwasababu maalumu


Ulikuwa ujumbe kwako kuwa usidandie bus usilojua linakwenda wapi. Umeona mwenzako alivyokuvua !

ACT mpini wa kumaliza upinzani unaendelea

- Kauli za kufarakanisha taifa za Zitto zilaaniwe, zikemewe na zipigwe vita
- Vita kati ya ACT/SUpreme na Mikoa ya kaskazini si njema kwa mustakabali wa taifa
- Mifano aliyotoa ya kuzomea wananchi wanaojiletea maendeleo ni ya kupigwa vita
 
Eh hizi sasa Sarakasi, Ilianza ACT ikahama , Ishu Ikageuka na kuwa Zitto, Sasa siyo Zitto tena bali imegeuka na kuwa Mkandara.....Hamna hoja hapo ni vioja tu!
Mtu kama huyu Nguruvi3 sitoweza jadili naye kwa sababu haelewi maana na hata siku moja hatambui mipaka ya hoja. Unapoandika juu ya Ukabila na jinsi ya Kuupiga vita atasema kumbe unakubali kuna Ukabila. Na ukisema hakuna Ukabila atasema kwa nini ulisema kuna Ukabila. hajui kabisa kutenganisha hoja moja kwenda nyingine hata kama unazungumzia hoja ilotangulia mbele yako. Hoja hujibu na hoja iliyopo na ukiulizwa swali jingine utajibu hoja hiyo kulinganana swali hilo sio kuchukua majibu ya huku ukayaweka kule.

Leo nikisema ACT itaupiga vita Unyonyaji hata iwe mkoa kwa mkoa, kwake ina maana tayari upo Unyonyaji wa mkoa kwa mkoa. Nikisema hakuna Unyonyaji wa mkoa kwa mkoa ila serikali ndio yenye mfumo unaopendelea kaelewa vingine kwamba nimejichanganya. Kupendelea na Unyonyaji kwake ni jambo lile lile..

Huyu mtu ni mbaguzi sana yaani yupo tayari kuitenga Zanzibar kwa sababu hizi hizi na lugha ya wazi kabisa lakini kuja kwenye swala la Zitto anaona vibaya na kutunga tafsiri zake kwa sababu yeye mwenyewe ndiye mwenye fikra za Kibaguzi. Sisi tunajua wanaomchukia Zitto basi inaweza kuwa kweli ni watu wa kaskazini maana Zitto ana matatizo na Chadema ghafla imekuwa yeye ndiye mwenye chuki na watu wa Kaskazini. Ni kina nani hao?

Hivi Chadema ni chama cha watu wa kaskazini maana nijuavyo Zitto ana mgogoro na Chadema, iweje leo Zitto awachukie watu wa Kaskazini kwani walimfanyia nini?. huyu jamaa yetu Ubaguzi anauona tu pale panapomfaidisha yeye kujitia unyonge hapa lakini namjua vizuri na maandishi yake humu yanajionyesha wazi. Kwa hiyo nimechoka kujadili naye na kama nilivyosema sitomjibu hoja zake maana haelewi maana na hataweza kunielewa.
 
Na upo sahihi kuhusu Zanzibar.
Nipo katika rekodi nikisema kuwa znz haina mchango katika taifa hili. Na kwamba wao ni tegemezi.Nina sababu za kusema hayo

1. Hakuna mkoa wenye bunge, baraza la wawailishi, Rais, bendera, wimbo wa taifa au uwezo wa kukopa kama taifa. Hakuna mkoa wenye vyombo nje ya vile tuavyojua sote. Znz wana kila chombo, taasisi na mashirika yao

Zanzibar wana hayo yote, na tulikuwabaliana ni nchi na ni taifa kama wanavyodai wao. Hakuna tofauti

2. Kigoma, Kilimanjaro, Mtwara, Kagera Singida n.k. sote tunachangia katika kapu moja.
Hivyo, chetu ni chetu hakuna chetu ni chetu chao ni chetu. Unaelewa maana yake nadhani

3. Hakuna mkoa unaopewa nafasi maalumu kama ilivyo ZNZ. Hakuna kiongozi anayepatikana kwa umkoa wake kama ilivyo ZNZ. Hakuna wananchi wanaopewa kipaumbele maalumu kama znz. Na hakuna mkoa unopewa hadhi tofauti na nyinginen kama znz

3. Znz wanasema ni washirika sawa wa muungano, hivyo ni partner na wanataka haki ya ubia wa muungano. Hakuna mkoa unaodai hadhi na ubia sawa ndani ya Tanganyika. Mikoa yote ni mipaka tu, sisi ni wamoja alpha and omega.

Hivyo ZNZ ni habari nyingine. Wakitaka kuwa sawa na Kigoma lazima wawe sawa ka kila kitu kinyume chake, wanatakiwa wachangie kama hadhi yao inavyowapa haki. Hakuna sababu za Mtanganyika kulipa gharama za taasisi, shirika au serikali ya nchi nyingine ya Zanzibar. Hatufanyi hivyo kwa Kenya, Uganda, Msumbiji au Malawi.

Huo ndio msingi wa kusema, wao wanasema si Watanzania ni wazanzibar.
Wanakuwa Watanzania pale tu wanapotaka mafao, kinyume chake hawakubali Utanzania.

Ni kwasababu hizo, with great power comes great responsibilities.
Kwa mantiki hiyo lazima walinde hadhi zao kwa ushiriki wa kuchangia na si vinginevyo. Hawawezi kuwa na hadhi wasioweza kuitetea kicuhumi. Wanapodai vyeo wanadai kama nchi, ikija kuchangia wanataka mlango wa uani. Huu upuuzi unaelekea mwisho

Mwaka jana wamekopa Bilioni takribani 388 lkwenda znz ni si kwingineko. Mtanganyika amebeba 88% ya mzigo usiomhusu
Tunakopa kama Tanganyika hatuangalii kama pesa inatumika kujenga Maragasi, Lumbulu, au Kibiti

Anachosema supreme leader ni kutaka kugawa wananchi wa Tanganyika katika misingi ya ukanda, umikoa na hata ukabila kutokana na matatizo yake ya kisiasa.

Hilo hatutanyamazia, tutalikemea kwasababu linalenga kuimega nchi moja ya Tanganyika katika misingi ya kubomoa taifa.

Zanzibar wanaweza kuondoka katika muungano,tutabaki Tanganyika.
Hatuwezi kuondoa mkoa mmoja kwasababu hiakuwa hivyo na haikubaliki. Unaelewa maana ya hili?

Ukija upande wako, wewe ni mtetezi wa znz kutochangia katika pato la taifa. Halafu unageuka na kumuunga mkono Zitto kuwa kila mtu apate kutokana na mchango wake. Well, znz kama nchi inapaswa zaidi kabla hujazungumzia mkoa wowote

Ukiangalia utaona tunasimama katika hoja bila kwenda mbele na nyuma.

Wewe unabadilika mara mikoa ichangie na igawiwe kutokana na Mchango.
Halafu unasema ZNZ iachwe tu licha yaa upendeleo na hadhi kubwa iliyo nayo. Unaona mkuu unavyojichanganya

Turudi kwa ACT na supreme na harakati zao za kutaka kuwagawa wananchi wa Tanganyika.
 

Ndugu Mkandara, Kujibishana na Yule bwana ni kujitafutia headache, hana nguvu ya hoja bali anatumia hoja za nguvu, za kulazimisha
Hoja zake hazina sophistication yoyote ya kimantiki au takwimu, Ya Ukweli wala usahihi.
Kinachomuongoza yeye ni chuki kali sana dhidi ya Zitto, na matokeo yake amepoteza focus ya mjadala.
Mwenzake japo naye ana chuki dhidi ya ZZK, lakini angalau anafanya tafiti na anatafakari, japo naye tafsiri yake huwa ni tenge.
Hawa watu Wanaichukia sana Zanzibar ambayo ni sehemu ya Tanzania, Lakini wanajifanya wanaipenda sana Tanzania hata kufikia kuhoji kwa nini Kilimanjaro na Arusha vimekuwa singled out?.
Japo kiukweli hii mikoa haijawa Singled out ukifuatilia long version ya hoja ya Zitto katika speech yake, Kiufupi hata Lindi nayo imetajwa!.
 
Supreme yupo katika rekodi akiwashambulia wananchi wa mikoa ya kaskazini kabla ya kauli ya Shinyanga na zingine. Hivyo, historia peke yake inamweka katika jicho baya dhidi ya mikoa ya kaskazini.

Sina uhakika Chadema inaingiaje hapa maana mjadala ni kuhusu AC/Supreme na shambulio la kisiasa dhidi ya mikoa inayojitahidi kimaendeleo. Upo katika rekodi ukisema mikoa ya kaskazini imewezeshwa, hujaeleza ni kwa namna gani imewezeshwa. Kumbu kumbu zipo kuwa kuna maji, bila hata ya kuangalia jiografia inasemaje. Maji yanatiririka kutoka ardhi wewe na suprem mnalifanya suala la kuwezeshwa.

Hatuwezi kukubali utetezi usio na mashiko. Kauli za ACT dhidi ya kugawa taifa ni hatari na zi kemewe na watu wenye mapenzi mema.

Nimekuonyesha jinsi ulivyobabaika na kudai ACT inakuja na ujamaa kuondoa unyonyaji wa mikoa. Kwamba mikoa yenye maendeleo itakabailiwa na wakati mgumu mbele ya safari. Well, kisiasa sijui kama ni mkakati mzuri

Sampling ya supreme leader ililenga mikoa ya kaskazini ambayo haipo katika top katika uchangiaji wala maendeleo
Aliichukua ili kujenga taswira ya kisiasa jambo la hatari sana kisiasa na kwa muskabali wa taifa

Nafasi aliyo nayo ni kutoka hadharani na kuomba radhi, kinyume ataishi na kauli hiyo kwa muda mrefu ujao.

Sisi tunasema, hapana! hatukubali taifa ligawanywe na watu wachache
 
Well, kauli ya supreme imezua mitafaraku sana. Sijui kama mnaliona hilo

ZNZ wanasema si Tanzania, hakuna chuki. Kama chuki ipo ni znz dhidi ya Tanzania. Lini uliwahi kusikia hoja ya Tanganyika kutaka kujiondoa katika muungano? Wanaotaka ni wznz, na ni haki yao, chuki ipo wapi?

Je, si kweli znz wanadai wanaonewa katika muungano
Je, si kweli kuwa wanadai muungano ume wavia kimaendeleo?
Je, si kweli kuwa wana vyombo kama nchi na taifa

Kama ni Watanzania, iweje wawe tofauti na Watanzania wengine?

Kama kuna chuki dhidi ys supreme, onyesheni chuki hiyo.
Kilichosababisha uzi huu ukamuongelea supreme ni baada ya kuona vijana wakitupiana matusi ya kikabila kutokana na kauli ya supreme, hamuoni hatari hiyo?


Nadhani manapaswa kuongozwa na hoja na si hisia. Kama ipo chuki onyesha tutaomba radhi.
Hata hivyo, ukweli usiwe chuki., bila kujali ni mchungu kiasi gani, mnapaswa kuumeza. Ni dawa na hakuna choice

Nimekuwekea kauli za flip flop za nduguyo, badala ya kutetea unasema kuna chuki

Twit za Zitto zipo, badala ya kutetea mmnasema tunaojadili tuna chuki.

Hakuna chuki kubwa kama ile ya kufarakanisha wananchi wa mkoa mmoja na mwingine
Pitia nyuzi uone jinsi watu wanavyolumbana kutokana na kauli ya mtu mmoja. Eti tukae kimya tu taifa likimemegwa!

Elezeni, ni sampling gani ametumia kuchomoa mikoa miwili iliyo kati kati ya vigezo vyote?
Data zote zilizoletwa hapa hakuna hata moja inayomtetea supreme, sasa chuki ipo wapi

Watu wote wazima wenye heshima zao JF wamesimama na kusema, no ! supreme alichosema ni kibaya! Hamuoni hilo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…