Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Mimi nafikiri Nguruv na Mwenzie Alinda wameshaelewa, Tukisema watu wa Shinyanga tunazungumzia Watanzania, na Ikisemwa watu wa Arusha inazungumzia Watanzania..Wote wana haki sawa na Stahili zao mbele ya Serikali na kwa mujibu wa hoja ya Zitto Stahili hiyo inabidi ibase katika uchangiaji katika pato la Taifa.
Wenye hoja wanaipinga hoja ya Zitto kwa hoja mbadala. Wasio na hoja wanamlisha maneno Zitto eti anaibagua mikoa ya Kaskazini. Huu ni mtizamo usio sahihi, na kulishana maneno.

Sijaona mahali katika kauli ya Zitto akizungumzia kuwa Kabila fulani limenyimwa haki, Au kabila fulani limependelewa, Hicho kitu hakipo.

Leo hii Watanzania wanaishi sehemu zote za nchi hii, Kwa hiyo Serikali ikipanga mipango mibovu katika sehemu fulani, wanaoathirika ni Watanzania wote!

Alinda na Nguruv, Msitake kuyapa maneno ya Zitto Tafsiri yenu mnayoipenda wenyewe!

Sijakujibu muda wote kwa sababu sikutumia neno "Stahiki" katika ile hoja yangu ya awali, bali nilitumia neno "Stahili"
Rekebisha kwanza swali halafu uniulize tena, tusilishane maneno!.


Haina shaka naondoa "Stahiki" na badala yake "Stahili" Unamaanisha nini hapo kwenye nyekundu..?
 
Tena si kuwa wanaimba wimbo wa kodi kodi kodi, wameacha kabisa kuzungumzia GDP

Kila hoja wanayotaka tuiongelee kwa mtazamo wao sisi tunakubali, baada ya dakika tano wanahamisha goli, hatujui watasingizia nini sasa. Twambieni tuongelee hoja za kiongozi mkuu kwa kutumia nini GDP au Kodi? Tupo tayari kwenda mnakotaka

1. Alinda kaibua lingine, anauliza hivi kama DGP alizotumia supreme kuonyesha unyonyanyaji wa mikoa ya Aeusha na Kilimanjaro kwa kuchangia kidogo na kuwa na maendeleo, vipi Lindi ambayo inachangia kidogo lakini ipo juu ya Shinyanga?
(Hii ni kwa mujibu wa maelezo ya Adharusi, Ritz(hotuba ya Shinyanga) Kapwela n.k. Hapa ''hatujamwekea maneno'' ni yenu


2. Nimeshangazwa na mkuu mmoja akisema mipango ya serikali na bajeti inategemea wafadhaili.
Huyu anaishi first world, sijui huko Canada bajeti inategemea wafadhili na ni wapi hao. Nimeskikitila sana , naye aje kuhamisha goli

3. Mchambuzi kasema, kwani Shinyanga inapaswa ipate kiasi gani cha kodi ili kuongeza 0.46% ya sasa?

4. Nguruvi3 anauliza kama kigezo ni madini na corporate tax, zile xa Tanzanite zinaachwa Arusha au zinakwenda Dar?

5 Alinda akauliza, Gamba la Nyoka aliposema Shinyanga haipati 'stahili'(Alinda nasahihisha kwa niaba) au stahiki kama Mknadara anavyosema alimaanisha nini? Tunaona wanatafita hifadhi ya spelling na maneno!

Hadi hapo kama hakuna majibu ya maana(uchambuzi na utambuzi), basi watu wakae kimya wenye hoja tuendelee

Wakati nasubiri Alinda arekebishe swali lake na aniombe msamaha kwa kunilisha maneno, Naendelea kusubiri ndugu yangu Nguruv utuletee hotuba ya ZZK kule Mwanza na Shinyanga, Hata hivyo kwa kuwa wewe hutaki rejea za kifacebook basi huna haki ya kuchangia bandiko ambalo rejea yake ni bandiko lililo huko!
 
Haina shaka naondoa "Stahiki" na badala yake "Stahili" Unamaanisha nini hapo kwenye nyekundu..?

You see unaona sasa, Kama mimi mtu wa kawaida Ulinilisha maneno, tutashindwaje kuamini kuwa hata Zitto Kabwe naye Unamlisha maneno kama ulivyonifanyia mimi?

Mimi naamini umefanya hivi makusudi ili nionekane nimetamka kitu ambacho sijakitamka
Kwa hali ya kawaida unaweza kuona ni kitu kidogo, lakini Kunukuu neno tofauti na lile mtamkaji alilotamka ni distortation, ni dishonesty, It is wrong!


Alinda mimi nitakujibu but you have to apologise for that first!
 
He mara hii Zitto mwenye kulaumiwa kwa kusema Kilimanjaro kuinyonya shinyanga, eti anazungumzia na Kilimanjaro Kunyonywa pia.

je hii si ni ushahidi wa Wazi wa Zitto kutaka fair distribution ya keki ya taifa? na si issue ya ubaguzi?.

Tupe ufafanuzi hapo, kivipi unataka fair distribution na kwa vigezo vipi? tupe shule kwa uelewa wako..Lakini kabla ya hapo pata shule kutoka kwa Mchambuzi..


Husisahau na ili swali maana ufafanuzi wako ni muhimu katika mjadala huu
 
He mara hii Zitto mwenye kulaumiwa kwa kusema Kilimanjaro kuinyonya shinyanga, eti anazungumzia na Kilimanjaro Kunyonywa pia.

je hii si ni ushahidi wa Wazi wa Zitto kutaka fair distribution ya keki ya taifa? na si issue ya ubaguzi?.

You see unaona sasa, Kama mimi mtu wa kawaida Ulinilisha maneno, tutashindwaje kuamini kuwa hata Zitto Kabwe naye Unamlisha maneno kama ulivyonifanyia mimi?

Mimi naamini umefanya hivi makusudi ili nionekane nimetamka kitu ambacho sijakitamka
Kwa hali ya kawaida unaweza kuona ni kitu kidogo, lakini Kunukuu neno tofauti na lile mtamkaji alilotamka ni distortation, ni dishonesty, It is wrong!


Alinda mimi nitakujibu but you have to apologise for that first!

Kama swala ni kuomba msamaha ili wanaukumbi tupate shule ya uhakika kutoka kwako.. Basi Gamba la Nyoka naomba msamaha kwa kutaka ufafanuzi wa neno Stahiki badala la Stahili.. Natumaini msamaha wangu umepokelewa.. Hivyo wanaduru tukae mkao mzuri shule yaja.. Haya Gamba la Nyoka uwanja ni wako...
 
Last edited by a moderator:
Hakuna aliyesema tatizo ni Kodi na siyo GDP, Usiwalishe wana Ukumbi Maneno.

Again, Tatizo siyo Kilimanjaro kama mkoa na watu wake, Tatizo ni serikali isiyo Fair, ambayo ina mipango mibovu katika ugawaji wa pato la taifa, Serikali ambayo hapo juu Ritz amekuonyesha hata Mbunge wa Shinyanga akilalamika kuwa Serikali imeuacha nyuma mno huo mkoa ktk suala la afya na Elimu.

Hakuna mwenye ugomvi na Kilimanjaro, kama serikali imepeleka maendeleo Kilimanjaro kuliko mikoa mingine, then wa kuwa questioned ajibu kwa nini ni serikali. Toka awali nafuatilia huu mjadala, hiki ndicho haswa ZZK alichokifanya.

Gamba la Nyoka
tuko pamoja katika mjadala huu? Pato la Taifa linagawiwa na Serikali?? Hebu tupe ufafanuzi jinsi serikali inavyogawa pato la taifa..

Somo la Uchumi hata mie naona mbili mbili ila wewe mwenzangu ni funga kazi..Unafahamu kitu kama ukifahamu waache wenye huo ujuzi watoe darasa, pale husipoelewa uliza swali ili upate mwanga zaidi.. Na hii si vibaya maana si lazima watu wote tuwe wachumi.. Ila unapojitutumua kuelezea kitu ambacho hata wewe kinakutia aibu.. huu ni...
 
Kama swala ni kuomba msamaha ili wanaukumbi tupate shule ya uhakika kutoka kwako.. Basi Gamba la Nyoka naomba msamaha kwa kutaka ufafanuzi wa neno Stahiki badala la Stahili.. Natumaini msamaha wangu umepokelewa.. Hivyo wanaduru tukae mkao mzuri shule yaja.. Haya Gamba la Nyoka uwanja ni wako...

Asante sana kwa kuwa Muungwana dada, Laiti na mwenzio Nguruv angekuwa na uungwana kama uliounyesha basi mnakasha huu angeutendea haki!, Usihofu Alinda nitakujibu ngoja nipate nafasi ya utulivu ambapo naweza kutype kwa utulivu then Jibu langu utaliona!
 
Hawana hoja wana vioja kama kiongozi mkuu. Hayo ndiyo matatizo ya kutetea kisichowezekana

Wamekuja na kila aina ya hotuba, hadi ya Shinyanga wameweka wenyewe.

Tumekwenda kila wanapotaka, sasa hivi wanarukia herufi kuonyesha walivyolowa

Haya ndiyo tunasema kila siku kuwa ni uchonganishi uliofanywa wa wazi na kiongozi mkuu

Hakukuwa na suala la uchumi wala ukweli, isipokuwa aliongozwa na hasira tu za kushambulia mikoa kwa uchonganishi

Tumeonyesha GDP na kuuliza mahusiano yake na maendeleo kama alivyotumia kiongozi mkuu.
Hakuna anayesimama kutetea hata mmoja, wanaishia kutafuta spelling

Tumeonyesha kodi wanazokimbilia kujadili , hakuna anayeweza kusimama na kutetea kauli za kiongozi wao hata mmoja

Tumeuliza hoja, zimebaki viporo hakuna anayesimama kujibu mapigo, kutetea au kuzungumzia

Wamekimbia wanasubiri uzi usonge mbele waje na vioja, waje na hoja za kitoto, waje na matusi na kejeli, huko ndiko utaalamu ulipo.

Tunasema, hapa sasa hivi ni hoja tu kwenda kwa mbele

Jamvi linaona kwa macho walivyotimka wakisubiri vihoja vya kipuuzi warudi kwa nguvu. Yes watarudi na vijigoja vya kipuuzi

Hakuna mkoa unaonyanya mwingine, hakuna mkoa unaonyonywa na mwingine bali zipo Fitna za wanasiasa muflisi kama kiongozi big

Kiongozi mkuu anajua alichokisema hakina ukweli na ni fitna, sasa tunasikia anataka kutaja majina aliyokaa nayo miaka kifuani
Hizo zote ni kutuondoa katika mjadala muhimu unaomgusa baada ya kuchaonganisha na kuliletea taifa usumbufu usio wa lazima

Hatuwezi kukaa kimya Fitna ikienezwa, ;;uhutu na utusi'' ukipandwa kwa nguvu na wanasiasa uchwara wasiolitakia taifa hili mema.

Wanasiasa walio tayari kuona taifa linamegeka ili wapande ngazi

Hawa hawafai hata kama wanakuja na dhahabu mikoni. Wakemewe, waonywe , wasotwe madole ili tunusuru taifa


Kama kuna mwenye hoja maswali ya Mchambuzi, Alinda na Nguruvi3 TUJITEGEMEE n.k. yapo hapo juu

Endapo hakuna, basi watu waendelee kupata darsa kwa wenye hoja si viroja.
 
Last edited by a moderator:
Ndiyo maana Mwl. Nyerere alikuwa anasisitiza ukusanyaji kodi na suala la miundombinu kwa ajiri ya maendeleo, na kulinda wafanyabihashara wenye viwanda hapa nchini kwa serikali kutoza kodi kwa haki. Mwl. Nyerere hakuimiza GDP...! Nadhani alikuwa amezielewa dhana hizi za Kodi na GDP. Waweza kumsikiliza katika clip mbili hapa chini. Clip ya kwanza isikilize yote na ya pili msikilize mwalimu kuanzia dk 2.40 mpaka ya 5.00.

Clip 1


Clip 2


============================== ============================== ====

Nawashukuru nyote mlionisaidia kulielewa suala la Kodi na GDP kwa undani zaidi. Nimejua kuwa, kwa kutambua sehemu husika ilinapa kodi na tozo kiasi gani na inachangia kiasi gani kwenye GDP ndiyo unaweza kupima mchango wa sehemu hiyo katika maendeleo ya sehemu yenyewe na nchi kwa ujumla.

Baadaye nimeenda mbali kwenda kutafuta ubora wa kipimo hiki cha GDP. Kwanza nimeelezwa, GDP hutumiwa na wachumi kwa shughuli hii (kama nilivyoinukuu): Economists use GDP to measure the relative wealth and prosperity of different nations, as well as to measure the overall growth or decline of a nation's economy.

Pia nikakumbana na vitu vinavyopunguza ubora wa kipimo hiki cha GDP (nanukuu): But there are a number of shortcomings to using GDP. Here are just a few:

1. GDP doesn't count unpaid volunteer work: .......
2. Disasters can raise GDP: Wars require soldiers, oil spills require cleanup, and natural disasters require health workers, builders, and all manner of helping hands. Rebuilding after a disaster or war can greatly increase economic activity and boost GDP.
3.GDP doesn't account for quality of goods: Consumers may buy cheap, low-quality, short-lived products repeatedly instead of buying more expensive, longer-lasting goods (Hili nadhani limeelezwa).

Sasa kwenye namba mbili hapo ndiyo pamenistua kweli, kumbe yawezekana tunaambiwa (mfano) Shinyanga ama Kilimanjaro zinachangia sana kwenye pato la Taifa (GDP). Kumbe mikoa inaongeza matumizi tu ya kwenye pato hilo labda kutokana na majanga yaliyoikumba mikoa hiyo...!! Na bado mtu anakwambia Mkoa fulani unachangia sana kwenye GDP lakini hauna maendeleo...! lakini mwingine unachangia kidogo lakini unamendeleo! Kauli hii isipofafanuliwa zaidi kujua mikoa hiyo inachangiaje GDP (majanga ama uzalishaji?), inapotosha sana umma ambao hawajui maana ya pato la taifa (GDP). Na hapa ndipo S.L anapotiwa hatiani kuwa alitoa kauli za kichonganishi. Mimi siyo mchumi ila kama nimetafsiri maelezo yale ya wanauchumi kwa usahihi, basi na sisitiza S.L (Zitto) anahatia.

Chanzo cha nukuu zangu ni>>>>What are the advantages and disadvantages of Gross Domestic Product?


Well said TUJITEGEMEE. Kwa kuongezea kidogo:

1. Pato la taifa (GDP) halina maana Kama serikali haichumi kodi; wazalishaji wakizalisha huduma na bidhaa na kula faida yote in private, na kutolipa kodi, Je Wana Ana uhalali gani wa kudai Public services? Ndio maana Bado nasubiri majibu kwa maswali yangu kwa Ritz kuhusu mchango wa Shinyanga Kwenye kodi kitaifa. Itatusaidie tujue haki ya wanashinyanga inakosekana Wapi. Kwa bahati mbaya, badala ya kukubali kwamba Hana uelewa wa kutosha ili tusaidiane majibu, anazidi kukoroga mambo kwa lengo la kumtetea zitto Ambae indirectly, keshasema kwamba zitto alikosea. Directly, hoja yake ni kwamba zitto yupo sahihi.

Suala lingine la kuongezea katika hoja yako ni kwamba:

2. Pato la taifa (GDP) halina maana Kama uzalishaji hauzai ajira kwa wananchi. Hao wazalishaji wanataka haki Yao in terms of social Services, lakini Je what's their contribution socially?

Mwisho, nilijadili kitu kinaitwa Tax to GDP ratio. Huu ni uwiano Kati ya KODI na PATO LA TAIFA. Akina Ritz, Mkandara wanashindwa kuona kwamba matumizi ya such a ratio ni ushahidi kwamba PATO la TAIFA na mapato ya serikali (KODI) ni vitu viwili tofauti kabisa.

The higher the ratio, the more desirable, na tukafanya mahesabu ya mikoa kadhaa na kuona kwamba shinyanga, kigoma ratio ipo chini kuliko Arusha, Kilimanjaro. Binafsi nadhani tungekuwa tunajenga zaidi kwa kuangalia mambo Kama haya.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;13165014]
Kwa hiyo usipolipa kodi serikalini, bado fedha ulokuwa nayo itahesabika kuwa mchango wako katk GDP pengine wewe umeongeza ukubwa shamba na upo Shinyanga ina maana unategemea kutakuwa na ongezeko la mapato yako mwaka kesho.

Ulipaji kodi ni muhimu kwa sababu unaiwezesha serikali kukabiri makadirio uloyafanya katika matumizi yake na kikubwa zaidi ni kutokuwa tegemezi la misaada ya nje badala ya wananchi wenyewe kuwa msingi wa pato lake.

Lakini katika mipango yake haiwezi kuzuiwa kwa sababu Shinyanga wamechangia kidogo kwani asilimia kubwa ya mipango ama bajeti ya nchi inatangulia mapato ya kodi itakayo kusanya.
Serikali inapanga mwaka 2015 - 2016 itafanya mambo gani mbele ya pato watalokusanya..

Shule, barabara, Umeme ni mipango ya serikali inayopangwa kabla ya kodi yako haijapokelewa.


Katika upangaji wa utekelezaji huo tunategemea misaada kupitia wafadhili wa nje ambao hutuwekea mikataba mibovu ikiwa ni pamoja na maliasili zetu zimilikiwe na mashirika yao pasipo masharti magumu.
Haya, hapa hajawekewa maneno mtu!

Kazi ya kodi ni kuiwezesha serikali kutoa huduma kwa jamii au kugharamia huduma za jamii siyo kukwepa utegemezi kama anavyotuaminisha mkuu Mkandara.

Kuhusu wafadhili sijui alitaka kuaonisha nini kati ya ufadhili, kodi na GDP!

Kuhusu kulipa kodi, moja ya hoja za critics wa definition ya GDP ni ile wanayosema haizingatia ''transaction za chini
Hivyo kuna wakati GDP inaweza isitupe hasa hali ilivyo''
 
============================== ============================== ====

Nawashukuru nyote mlionisaidia kulielewa suala la Kodi na GDP kwa undani zaidi. Nimejua kuwa, kwa kutambua sehemu husika ilinapa kodi na tozo kiasi gani na inachangia kiasi gani kwenye GDP ndiyo unaweza kupima mchango wa sehemu hiyo katika maendeleo ya sehemu yenyewe na nchi kwa ujumla.

Baadaye nimeenda mbali kwenda kutafuta ubora wa kipimo hiki cha GDP. Kwanza nimeelezwa, GDP hutumiwa na wachumi kwa shughuli hii (kama nilivyoinukuu): Economists use GDP to measure the relative wealth and prosperity of different nations, as well as to measure the overall growth or decline of a nation's economy.

Pia nikakumbana na vitu vinavyopunguza ubora wa kipimo hiki cha GDP (nanukuu): But there are a number of shortcomings to using GDP. Here are just a few:

1. GDP doesn't count unpaid volunteer work: .......
2. Disasters can raise GDP: Wars require soldiers, oil spills require cleanup, and natural disasters require health workers, builders, and all manner of helping hands. Rebuilding after a disaster or war can greatly increase economic activity and boost GDP.
3.GDP doesn't account for quality of goods: Consumers may buy cheap, low-quality, short-lived products repeatedly instead of buying more expensive, longer-lasting goods (Hili nadhani limeelezwa).

Sasa kwenye namba mbili hapo ndiyo pamenistua kweli, kumbe yawezekana tunaambiwa (mfano) Shinyanga ama Kilimanjaro zinachangia sana kwenye pato la Taifa (GDP). Kumbe mikoa inaongeza matumizi tu ya kwenye pato hilo labda kutokana na majanga yaliyoikumba mikoa hiyo...!! Na bado mtu anakwambia Mkoa fulani unachangia sana kwenye GDP lakini hauna maendeleo...! lakini mwingine unachangia kidogo lakini unamendeleo! Kauli hii isipofafanuliwa zaidi kujua mikoa hiyo inachangiaje GDP (majanga ama uzalishaji?), inapotosha sana umma ambao hawajui maana ya pato la taifa (GDP). Na hapa ndipo S.L anapotiwa hatiani kuwa alitoa kauli za kichonganishi. Mimi siyo mchumi ila kama nimetafsiri maelezo yale ya wanauchumi kwa usahihi, basi na sisitiza S.L (Zitto) anahatia.

Chanzo cha nukuu zangu ni>>>>What are the advantages and disadvantages of Gross Domestic Product?

Mkuu TUJITEGEMEE hiyo video ya Mwl imekuja tukiambiwa wakati wa Nyerere hakukuwa na kodi!
Real, mtu anaandika hayo ili tu kujenga hoja za kumtetea SL. Unaweza kuona ukubwa wa tatizo!

Pili, watu wanasahau masharti ya IMF kwa serikali ilikuwa kukusanya kodi. Serikali ya Mwinyi inalaumiwa . Na Mkapa ilibidi atende.

Tatu, watetezi wa kiongozi mkuu hakuna hata mmoja anayetuonyesha uhusiano wa GDP na Maendeleo.
In fact wamekimbi huko sasa wamerudi kule Mchambuzi alipowaambia ni sahihi 1.e kodi.

Tunaulliza kodi zinaathiri vipi Shinyanga? Utetezi ni migodi ya madini 'kuwepo Dar' Tukauliza ile ya Arusha ina makao yao wapi? Kimya

Nne, tukauliza nini ambacho Shinyanga na Arusha wanatofautiana katika shughuli za kijamii.

Tunaona ufafanano. Tukahoji iweje Shinyanga ichangie kodi 0.46% tofauti na Arusha. Wamekimbia wanatafuta spelling

Tano, tukasema turudi kwenye GDP wanayoelewa wao. Tukauliza, kama GDP ni kigezo cha maendeleo, shughuli za kijamii zinahudumiwaje kwa kutumia GDP? Hakuna jibu, wote tutweee ! wanatafuta mistari yenye herufi waibuke

Sita, tukasema kama GDP inapima nani apate nini ili kuendelea, vipi Mbona Lindi ina GDP ndogo sana ukilinganisha na Kilimanjaro na Arusha, kimaendeleo ipo juu ya Shinyanga? Nako kimya, wamejibanza wanatafuta vijherufi vilivyokosewa waibuke

Saba, tukauliza tuelezwe mantiki za kauli za kiongozi mkuu kulinganisha mikoa, kuchagua baaadhi na kuinanika, kauli za ' hata hivyo, maendeleo zaidi, kuchangia zaidi au kidogo zililenga nini'' tunaambiwa asambaza uzalendo! Uhuni unapakwa rangi

Wengine tulishamtia hatiani siku nyingi. Kauli zake za takwimu za kulinganisha jamii, kwa mtu mwenye weledi na mature hawezi kuzikubali bila ushawishi. Ni kauli za kipuuzi sana kwa mwanasiasa mwenye miaka 15+ katika chombo kama bunge

Ni kauli zinazotakiwa zitolewe na mtu anayejiunga siasa. Kuanza comparison ya jamii ni kuleta 'uhutu na utusi' bila sababu

Tunadhani jamvi limeona wanavyotafuta nahau na methali . Hawana hoja, wamehamisha magoli sasa goli lipo karibu na jukwaa kuu

Ukirudi nyuma tulieleza makundi matatu , la kwanza linaloamini katika kiongozi mkuu.
Hili tulisema limelishwa yamini au limbwata. Lipo tayari kujitoa fahamu na kuuza utu na akili ilimradi tu kukaa mbele na kumsikiliza

Kundi la pili, ni lile lisilokubaliana naye kwasababu keshapoteza imani, haaminiki na linamuona ni laghai hatari kwa usalama na umoja

Kundi la tatu, ni lenye mashaka. Hili halimfahamu. Kundi lipo karibu kupotea, hakuna shaka tena juu yake.
Ni ima kundi la kwanza au la pili. Hakuna mashaka kwa mtu anayelenga kuchonganisha jamii

Leo tunaona ukweli, Shinyanga haina matatizo yoyote na Kilimanjaro au Arusha.

Na kwamba matatizo yapo katika dude la miaka 50. Tunaona hakuna ushahidi wa kitakwimu kuwa mkoa mmoja unaonya mwingine.

Tuna maelezo ya kichonganishi kuhusu hilo yakitolewa na mtu muflisi wa kisiasa, asiyejali nchi tna aliye tayari kuiutumbukiza katika matatizo.

Wamekmibia hoja, wamejificha, 'make no mistake'! uzi ukisonga hoja zikiwa mbali wataibuka na spelling check, watakuja wakiwa na wamebeba paste zao, na tutasikia 'mzee mawazo kasema haya.., Msikie Shemahonge, Hapa chini ni Maliwaza, Ngolile kasema'' n.k Hakuna uchambuzi wala utambuzi . Ni waviziaji,wapo bize wanatafuta vimistari na spelling vya kuanzia mada

Kwa hili Kiongozi mkuu alikuwa na nia ovu na mikoa ya kaskazini, nia ovu kabisa! Tunasema ni ovu kijamii, kimantiki, kisiasa na kitakwimu.

Wenye hoja waendelee, wenye viroja toeni nafasi
 
Well said TUJITEGEMEE. Kwa kuongezea kidogo:

1. Pato la taifa (GDP) halina maana Kama serikali haichumi kodi; wazalishaji wakizalisha huduma na bidhaa na kula faida yote in private, na kutolipa kodi, Je Wana Ana uhalali gani wa kudai Public services? Ndio maana Bado nasubiri majibu kwa maswali yangu kwa Ritz kuhusu mchango wa Shinyanga Kwenye kodi kitaifa. Itatusaidie tujue haki ya wanashinyanga inakosekana Wapi. Kwa bahati mbaya, badala ya kukubali kwamba Hana uelewa wa kutosha ili tusaidiane majibu, anazidi kukoroga mambo kwa lengo la kumtetea zitto Ambae indirectly, keshasema kwamba zitto alikosea. Directly, hoja yake ni kwamba zitto yupo sahihi.

Suala lingine la kuongezea katika hoja yako ni kwamba:

2. Pato la taifa (GDP) halina maana Kama uzalishaji hauzai ajira kwa wananchi. Hao wazalishaji wanataka haki Yao in terms of social Services, lakini Je what's their contribution socially?

Mwisho, nilijadili kitu kinaitwa Tax to GDP ratio. Huu ni uwiano Kati ya KODI na PATO LA TAIFA. Akina Ritz, Mkandara wanashindwa kuona kwamba matumizi ya such a ratio ni ushahidi kwamba PATO la TAIFA na mapato ya serikali (KODI) ni vitu viwili tofauti kabisa.

The higher the ratio, the more desirable, na tukafanya mahesabu ya mikoa kadhaa na kuona kwamba shinyanga, kigoma ratio ipo chini kuliko Arusha, Kilimanjaro. Binafsi nadhani tungekuwa tunajenga zaidi kwa kuangalia mambo Kama haya.
Mchambuzi, Hivi haya madai yenu yote yana msingi gani haswa? kwa sababu swala la kodi halihusiani kabisa na mjadala huu kwani mnaanza kutunga vitu ilihali Ukusanyaji wa kodi unatokana na usajili wa shughuli za uzalishaji iwe wafanyakazi, wakulima na biashara zilizopo na zaidi ya hapo ukiacha wafanyakazi inategema kama biashara hizo zinatengeneza faida. Nitawachosha kidogo lakini nawaomba mnisome kwa makini na taratibu kwa sababu sijui kuandika maneno machache nikafikisha Ujumbe upaswavyo..Please tuvumiliane..

Pengine wewe sii mhasibu hujawahi ku file Tax unatumia dhana tu kuonyesha ukusanyaji wa kodi mkubwa wa Kilimanjaro dhidi ya Shinyanga wakati kinachozungumzwa na Mwalimu Nyerere na viongozi wengine ni kuhsu wale watu wanaokwepa kulipa kodi. Hakuna ushahidi wowote mlokuwa nao kudhihirisha kwamba wafanyakazi, wakulima na wafanya biashara wa Shinyanga ama Kilimanjaro wanakwepa kulipa kodi zaidi ya kutazama namba.

Licha ya hivyo unaweza kuwa na biashara kubwa tu lakini kutokana na mahesabu ya revenue against expenses na investmane ikaonekana hudaiwi. Nni asilimia ndogo sana ya watu wanao file Tax Revenue zao TRA na mfumo uliopo ni wa Kifisadi kwa sababu TRA wanatoza Kodi hata kabla kujaanza biashara wala hujapata faida. Kodi kwa mfanya biashara hutokana na Income sio Revenue..(kumbuka lile swala lako)

Kwa hiyo unakosea unaposema Tax zikatwe kulingana na makisio ya thamani ya bidhaa na huduma GDP wakati sivyo, Na hata kodi za VAT sisi sote tunalipa kwa kila unaponunua na kukusanya kila unapouza, hivyo maadam watu wananunua na kuuza toka kila kona ya nchi, hii haimaanishi wananchi wa Shinyanga hawalipi VAT, point kubwa hapa ni kwamba VAT huwa included kwa kila kitu unachonunua na kuuza! haijalishi wewe mkazi wa wapi isipokuwa umenunua wapi au umeuza wapi,.

Ku file tax ni ile check and balance kwa kila mwananchi hii haina maana watu hawalipi kodi kwa sababu kodi hukatwa kila wanapopokea mishahara yao ama kwa wafanya biashara unatakiwa ku file kwa ajili ya kulipa on income lakini tayari wameshalipa VAT kwa kila wanaponunua bidhaa au huduma, na hukusanywa kodi kila wanapouza kitu kwa sababu VAT is included katika bei ya bidhaa ama huduma. Kwa hiyo mfanyabiashara Unapo file tax wanatazama kuhakikisha unalipa kodi on income (profit) jambo ambalo watu wengi hawafanyi ama wanaofanya wanahakikisha biashara zao zina faida kidogo ama hasara.

Labda nikupeni mfano mdogo, Naweza kuwa na biashara yenye mauzo (Sales - Gross Income) ya Bil.10, nachotakiwa kulipa kodi ni asilimia 20 ya net - income, lakini baada ya mahesabu ya matumizi yangu na investment, ikaonekana sidaiwi nimepata hasara wakati biashara imesimama safi kabisa na VAT ikaonekana nimelipa kodi zaidi ya zile nilizopokea, hivyo mimi naidai serikali kodi ya ziada kwenye VAT. Wakati wewe una biashara yako ya Mil.10 lakini kulingana na matumizi na investment zako unadaiwa kodi ya Tsh mil. 3 kulingana na mahesabu ya Matumizi vs Sales ukawa na faida kubwa na umelipa VAT kidogo kuliio ulivyokusanya..

Hivyo maadam kodi zimo katika upatikanaji wa faida huwezi kujua nani alopata faida au hasara hadi ame file, na VAT ni kwa kila unachonunua kwa maana ya kwamba unaponunua kitu chochote ama kuagiza kitu chochote kodi za serikali tayari is included huwezi chukulia huu kama mfano bora. Ila kimfumo tuna tatizo kubwa la ufuatiliaji wa kodi kuhakikisha kila Mtanzania ana file Tax na swla hili nimelizungumzia toka miaka ile ya Mkapa akisifiwa kuweka mfumo huu wa kodi ambao haujengi isipokuwa ni mzigo kwa wananchi na haswa wafanyabiashara wadogo na wananchi wenye mishahara midogo.. Baadhi ya matatizo ya Ulipaji kodi nchini yanatokana na:-

1. Kutokuwa na mfumo mzuri wa kila mtu ku file tax zake mwisho wa mwaka,
2. Biashara nyingi kuwa unregistered.
3. Wananchi wengi hawana TIN namba hivyo mishahara inatolewa chini ya meza na unrecorded.
4. Malipo mengi yanafanywa na cash bila kupitia benki hivyo inakuwa vigumu kwa serikali ku verify revenues za kila mtu..
5.. Pia hata ufuatiliaji wa kila mtu mwenye TIN namba ni mgumu kutokana na ukosekanaji wa mawasiliano baina ya vymbo vya serikali na wananchi wake. watu hawana makazi maalum ama ukosekanaji wa address.

Kwa hiyo kuna sababu nyingi sana ambazo zinatakiwa kufanyiwa marekebisho makuubwa ili kufanisi ukusanyaji kodi na hili sio swala la Shinyanga wala Kilimanjaro kwa sababu Inaweza kabisa kuwa mkazi wa Shinyanga kwenda Dar au Kilimanjaro kununua mali zake badala ya mali hizo kupatikana Shinyanga!. Na naweza tumia mfano wa maji kukosekana Shinyanga ikatokea kuwa wafanya biashara wa Shinyanga huenda Kilimanjaro kununua Maji ili wayasambaze (wauze) SHY. Kwa hiyo swali letu hapa sio kodi yake imelipwa wapi bali kwa nini Shinyanga haina Maji?.

Uchumi wa nchi yetu haujengwi na mchango wa ulipaji wa kodi mkubwa isipokuwa kodi hizo kutumiwa vizuri ktk kulipia gharama za mipango ya maendeleo ilokwisha simamishwa na haya huwa tayari yamekwisha wekezwa na serikali kuu. Kama serikali ikipanga mwaka kesho itajenga mradi wa maji Shinyanga, haijalishi malipo yake yatatokana na kodi ilokusanywa wapi. Kama mradi wa kupeleka maji au ujenzi wa Chuo SHY unapotangazwa, fedha za mradi huo huchotwa hazina na kulipia, pale hazina hakuna kabati ya fungu lilokusanywa Kilimanjaro au Shinyanga hivyo lisiende mahala popote isipokuwa mikoa hiyo...

Anyway nimeandika mengi na nadhani tunaanza kutoka nje kabisa ya mjadala huu kwa sababu Kodi tunayolipa inakuja lipia matumizi ya serikali ambayo tayari ilikwisha yapangia, na kikubwa zaidi kodi yako inalipia zaidi matumizi ya kawaida ya mihimili yetu ya serikali na wizara, idara, taasisi na mashirika yake, gharama za bunge na Mahakama kwa kulipia mishahara, magari, mafuta, safari zao, madudu kibao na kadhalika.

Kodi tunazolipa sisi wananchi hazitoshi kulipia gharama za hawa waheshimiwa, sasa iweje kweli wewe Mchambuzi utumie hili neno kodi kuwakilisha hoja ya maendeleo ya mkoa wa Shinyanga au Kilimanjaro wakati Unajua fika kwamba hata hiyo kodi inayokusanywa Kilimanjaro haitoshi kuendesha mahitaji ya ofisi za mihimili hiyo zilizopp Kilimanjaro, bado kuna fungu linatakiwa kutoka nje au mikopo benki kuendesha shughuli za utawala kwa mkoa huo acha mbali kabisa maendeleo ya mkoa huo.

Kifupi mnasikitisha sana kutafuta hizi sababu kwa kujenga hoja ambayo haihusiki kabisa kusaidia mkoa wa Shinyanga kwa sababu wanaweza kukusanya kodi zaidi ya Kilimanjaro na bado fedha hiz zikaenda kugharamia matumizi ya mkoa wa Dar au Lindi kulingana na mahitaji ya mkoa huo. Labda mngesema hivi Kilimanjaro inapewa mgao zaidi kwa sababu kuna gharama kubwa zaidi kuliko Shinyanga, ukichukua hata walimu tu, Kilimanjaro inaweza kuwa na walimu 3,000 wakati Shinyanga ina walimu 1,000, unafikiri serikali itapeleka wapi fedha zaidi? na hili sio swala tunalozungumzia hapa isipokuwa mpango wa maendeleo kwa mkoa wa Shinyanga!
 
Umeona sasa mkuu Ritz, hii disparity sijui kwa nini Mchambuzi haioni. Kutokana na weakness katika taxation regime, ambapo kodi kutoka sehemu moja ya nchi zinakusanywa sehemu nyingine,ni vigumu kuchukulia kodi ya mahala pekee as an indicator ya sehemu hiyo ya kuchangia katika mapato ya serikali compared na sehemu nyinginezo.

Indicator nzuri zaidi, ni kutumia kipimo cha overall production of goods and services ya sehemu fulani kwa mwaka

..migodi ipo Shinyanga lakini wananchi wa mikoa hiyo siyo wanaochimba madini ktk migodi hiyo.

..kwa maneno mengine mchango wa wananchi wa Shinyanga ktk Mapato yanayokusanywa toka mikoa huo, particularly sekta ya madini, ni mdogo sana.

..hata kama kodi toka migodini itakusanywa huko huko Shinyanga bado ukweli huo nilioueleza hapo juu hauwezi kubadilika.

..Sasa hakuna haja ya kulaumu Kilimanjaro na Arusha kutokana na ugumu wa maisha na umasikini uliotamalaki Shinyanga. Kinachotakiwa kufanyika ni kuziboresha sekta za pamba, ufugaji, na uvuvi, ambazo wananchi wa Shinyanga wanashiriki moja kwa moja.

cc Mkandara, Mchambuzi, Alinda, Nguruvi3
 
..migodi ipo Shinyanga lakini wananchi wa mikoa hiyo siyo wanaochimba madini ktk migodi hiyo.

..kwa maneno mengine mchango wa wananchi wa Shinyanga ktk Mapato yanayokusanywa toka mikoa huo, particularly sekta ya madini, ni mdogo sana.

..hata kama kodi toka migodini itakusanywa huko huko Shinyanga bado ukweli huo nilioueleza hapo juu hauwezi kubadilika.

..Sasa hakuna haja ya kulaumu Kilimanjaro na Arusha kutokana na ugumu wa maisha na umasikini uliotamalaki Shinyanga. Kinachotakiwa kufanyika ni kuziboresha sekta za pamba, ufugaji, na uvuvi, ambazo wananchi wa Shinyanga wanashiriki moja kwa moja.

cc Mkandara, Mchambuzi, Alinda, Nguruvi3
Mkuu hata kama wananchi wanachimba wenyewe bado haiwezi kunyanyua maisha ya wananchi wa Shinyanga kwa sababu migodini zinatumika mashine zaidi na wafanyakazi ni wachache sana. Na sidhani kama umewahi kutembelea migodini kwa sababu ni wananchi ndio wanaifanya kazi ya uchimbaji wakisimamiwa na hao mabwana wakubwa, wenye mali, ila namba haijitoshelezi na mali zio yetu.

Kwa hiyo uchangiaji hautokani na wingi wa wafanyakazi bali mfumo bora unaowezesha mikoa na taifa kunufaika na madini hayo. States kama Texas au ukija Canada unakuta Province kama Alberta hutakuta wafanyakazi wengi katika migodi ya mafuta au madini isipokuwa mzunguko wa utajiri huo una impact kubwa na moja kwa moja katika mafao ya sehemu hizo.

Tazama waarabu na mafuta ukienda katika machimbo yao utakuta WaSaudia wachache sana kazini, wafanyakazi karibu wote ni wageni lakini utajiri wake umeweza kubadilisha maisha ya Wasaudia wote. Tusiende mbali Botswana ile pale, kule juu kwenye madini hakuna mtu wala maendeleo ni jangwa tupu lkn shuka chini Gabarone hadi mpakani na South utajiri wote upo huku wale watu wa porini kwenye madini hawana hata nguo! God must be crazy kweli..

Hivyo yawezekana huu mfumo wa Central Government tulonao kuwa ndio sababu ya kutoleta mafanikio, wananchi wa Shinyanga na sisi wenyewe tumetumiwa kama Nigeria na Sudan izinavyowafanya wananchi wake japo wana machimbo ya mafuta. Kwa nini Nigeria kulikuwa na Biafra, maisha ya watu wa South ni mabaya kuliko North? Hiyo South Sudan kwa nini tunawaunga mkono ikiwa hakuna sababu nyingine maana waloajiriwa sii watu kutoka North ni wenyeji na wakazi wa majimbo hayo maskini..

Ni lazima ifike wakati tuyaangalie haya waswala kwa kina zaidi kwa sababu hata Chadema waliposisitiza utawala wa majimbo ni kutokana na kuepuka Utawala wa juu kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya maslahi yao badala ya kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya ustawi wa jamii yetu. Na pengine kugawanya majimbo ingesaidia kuondoa Unyonyaji unaoendelea nchini. Lazima tukubali kuna kitu hakipo sawa na tukiendelea kubishana juu ya Shinyanga na Kilimanjaro itaonyesha ni jinsi gani sisi wenyewe tulivyopikwa kiakili kuwa watumwa wa makabila yetu..
- Msemo wa Nyani Ngabu - MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO
 
Mkuu hata kama wananchi wanachimba wenyewe bado haiwezi kunyanyua maisha ya wananchi wa Shinyanga kwa sababu migodini zinatumika mashine zaidi na wafanyakazi ni wachache sana. Na sidhani kama umewahi kutembelea migodini kwa sababu ni wananchi ndio wanaifanya kazi ya uchimbaji wakisimamiwa na hao mabwana wakubwa, wenye mali, ila namba haijitoshelezi na mali zio yetu.

Kwa hiyo uchangiaji hautokani na wingi wa wafanyakazi bali mfumo bora unaowezesha mikoa na taifa kunufaika na madini hayo. States kama Texas au ukija Canada unakuta Province kama Alberta hutakuta wafanyakazi wengi katika migodi ya mafuta au madini isipokuwa mzunguko wa utajiri huo una impact kubwa na moja kwa moja katika mafao ya sehemu hizo.

Tazama waarabu na mafuta ukienda katika machimbo yao utakuta WaSaudia wachache sana kazini, wafanyakazi karibu wote ni wageni lakini utajiri wake umeweza kubadilisha maisha ya Wasaudia wote. Tusiende mbali Botswana ile pale, kule juu kwenye madini hakuna mtu wala maendeleo ni jangwa tupu lkn shuka chini Gabarone hadi mpakani na South utajiri wote upo huku wale watu wa porini kwenye madini hawana hata nguo! God must be crazy kweli..

Hivyo yawezekana huu mfumo wa Central Government tulonao kuwa ndio sababu ya kutoleta mafanikio, wananchi wa Shinyanga na sisi wenyewe tumetumiwa kama Nigeria na Sudan izinavyowafanya wananchi wake japo wana machimbo ya mafuta. Kwa nini Nigeria kulikuwa na Biafra, maisha ya watu wa South ni mabaya kuliko North? Hiyo South Sudan kwa nini tunawaunga mkono ikiwa hakuna sababu nyingine maana waloajiriwa sii watu kutoka North ni wenyeji na wakazi wa majimbo hayo maskini..

Ni lazima ifike wakati tuyaangalie haya waswala kwa kina zaidi kwa sababu hata Chadema waliposisitiza utawala wa majimbo ni kutokana na kuepuka Utawala wa juu kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya maslahi yao badala ya kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya ustawi wa jamii yetu. Na pengine kugawanya majimbo ingesaidia kuondoa Unyonyaji unaoendelea nchini. Lazima tukubali kuna kitu hakipo sawa na tukiendelea kubishana juu ya Shinyanga na Kilimanjaro itaonyesha ni jinsi gani sisi wenyewe tulivyopikwa kiakili kuwa watumwa wa makabila yetu..
- Msemo wa Nyani Ngabu - MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO

..Arusha imechangamka kutokana na wananchi kuchimba tanzanite.

..Shinyanga pako tofauti. Serikali imenyanganya migodi yote na kuwapa wawekezaji toka nje.

..kosa lingine ni kwamba serikali imesaini mikataba mibovu na inayoinyonya nchi.

..Tanzania imo ktk 5 bora Afrika ktk uzalishaji wa dhahabu, na Shinyanga Ina migodi miwili mikubwa. Tatizo ni mikataba mibovu iliyosainiwa.

..Zitto alikuwa mjumbe wa tume ya Jaji Bomani ambayo ilipewa jukumu la kuchunguza mapungufu ya mikataba yetu ya madini na kuishauri serikali kuhusu hatua za kuchukua. Kwa hiyo huyu ni mtu anayeelewa umasikini wa Shinyanga Chanzo chake ni nini . binafsi amenishangaza na haya madai yake kwamba Kilimanjaro wanawanyonya ndugu zao wa Shinyanga.
 
Mkuu JokaKuu

Akiwa mjumbe aliwahi kueleza jinsi mikataba inavyotupa mirahaba mibovu.
Alikuwa kinara wa hoja ya Buzwagi, anajua tatizo lipo wapi.

Hii habari ya ulinganisha jamii moja na kuonyesha inaonewa na jamii nyingine inasikitisha


Lakini pia tukifuata dhana ya kuchangia GDP na kupata zaidi,tunaeleza mapungufu yetu ya kufikiri.

Kwa maneno mengine badala ya kusaidia walio nyuma, tunajenga ufa kwa kuwanyima.
Mbona hajaeleza GDP ya Kigoma na tax revenue zake?


Wakati huo huo anaeleza mafanikio yaliyopatikana kwa ujenziwa miundo mbinu katika kipindi chake.

Miundo mbinu hiyo imejengwa kwa rasilimali zipi? Za Kigoma peke yake au kutoka kona zote za nchi?
Unyonyaji unaosemwa upo wapi?


Ni makossa kueleza dhana ya maendeleo kwa kutumia kigezo kimoja.

Tumeeleza factors kwa uchache zinazochangia maendeleo ya eneo.
Kwamfano rahisi sana, Kenya ilipokuwa na matatizo, Arusha ilionekana ku panic kuliko mikoa mingine ''Spillover effects ''

Siasa za kugawa watu ni mbaya sana, tuzikemee kabla hazijaota mizizi.

Umasikini wa Tanzania unaweza kuelezwa
kwa njia zaidi ya 100 bila kuleta tafrani miongoni mwa jamii.
 
Miongoni wa udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye thread hii ni watu kukomaa na vitu ambavyo havipo na matokeo yake kukosa ata haki ya kujadili, NO RESEARCH, NO DATA, NO RIGHT TO SPEAK.

Bila kufuatilia na kujua ACT/Zitto wamesema nin hasa na kuishia kuibua/tutunga/kupinga/kulalama juu ya kisichokuwepo itakuwa ni kama kupiga ngumi hewani, hamtaweza kutimiza lengo.

Mchambuzi,Nguruvi, Alinda, mnaweza mkaliepuka hilo leo kwa kufuatilia mkutano LIVE kutokea Mwembeyanga Temeke kupitia Azam TV, Channel 10, na EFM Radio kuanzia saa 10 jioni.

Aksanteni sana na Kwaherini!
 
Miongoni wa udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye thread hii ni watu kukomaa na vitu ambavyo havipo na matokeo yake kukosa ata haki ya kujadili, NO RESEARCH, NO DATA, NO RIGHT TO SPEAK.

Bila kufuatilia na kujua ACT/Zitto wamesema nin hasa na kuishia kuibua/tutunga/kupinga/kulalama juu ya kisichokuwepo itakuwa ni kama kupiga ngumi hewani, hamtaweza kutimiza lengo.

Mchambuzi,Nguruvi, Alinda, mnaweza mkaliepuka hilo leo kwa kufuatilia mkutano LIVE kutokea Mwembeyanga Temeke kupitia Azam TV, Channel 10, na EFM Radio kuanzia saa 10 jioni.

Aksanteni sana na Kwaherini!

Mkuu hata hivyo lengo la thread ni kujadili ACT kama mpini wa CCM kumaliza upinzani, sidhani kama ukichek heading, hata hivyo tutafuatilia pia ya mwembe yanga, hapatakosekana neno lingine la kujadili kutokea huko.
 
Miongoni wa udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye thread hii ni watu kukomaa na vitu ambavyo havipo na matokeo yake kukosa ata haki ya kujadili, NO RESEARCH, NO DATA, NO RIGHT TO SPEAK.

Bila kufuatilia na kujua ACT/Zitto wamesema nin hasa na kuishia kuibua/tutunga/kupinga/kulalama juu ya kisichokuwepo itakuwa ni kama kupiga ngumi hewani, hamtaweza kutimiza lengo.

Mchambuzi,Nguruvi, Alinda, mnaweza mkaliepuka hilo leo kwa kufuatilia mkutano LIVE kutokea Mwembeyanga Temeke kupitia Azam TV, Channel 10, na EFM Radio kuanzia saa 10 jioni.

Aksanteni sana na Kwaherini!


Sikia kama unataka kujadili hoja ningependelea uwe unazungumzia mawazio yako wewe na sio kuniongoza mimi niseme nini? Mmi sii mtoto mdogo najua nilichokiandika na kwa maana yake. Mbona nyie mnamwita Zitto Ayatola, mnamuita Zitto Msaliti hili neno msaliti mnalichukulia dogo kwa upande wenu, na hata sisi kutupa majina na makundi lakini hamtaki kutiwa doa lolote.

Hizi fikra za kufikiria unaweza kuwaongoza watu na kuwachagulia waseme nini, kunichukulia mimi kama mwanao ama mtoto mdogo wa kuongozwa ndizo zinazotushinda sisi wengine!. JF ni uwanja huru na kila mwenye mawazo anayaweka wazi, hoja hujibiwa kwa hoja, kosa ni kumtukana mtu. Neno MIJITU ina maana ya watu walokosa UTU katika maamuzi yao ama matendo yao haina maana zaidi ya hiyo na hatupo darasani kiasi kwamba unapomsoma mtu unatafuta makosa yake katika maandishi ili kumfundiusha kuandika vizuri huu ni mjadala pokea hoja na jibu hoja ya mtu, kazi nyingine waachie moderators.. Sorry kama nimekukwaza but please usitake kuniongoza niandike nini humu., sote watu wazima hapa..

Nafikri hili jibu linakufaa....
 
Miongoni wa udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye thread hii ni watu kukomaa na vitu ambavyo havipo na matokeo yake kukosa ata haki ya kujadili, NO RESEARCH, NO DATA, NO RIGHT TO SPEAK.

Bila kufuatilia na kujua ACT/Zitto wamesema nin hasa na kuishia kuibua/tutunga/kupinga/kulalama juu ya kisichokuwepo itakuwa ni kama kupiga ngumi hewani, hamtaweza kutimiza lengo.

Mchambuzi,Nguruvi, Alinda, mnaweza mkaliepuka hilo leo kwa kufuatilia mkutano LIVE kutokea Mwembeyanga Temeke kupitia Azam TV, Channel 10, na EFM Radio kuanzia saa 10 jioni.

Aksanteni sana na Kwaherini!
Tumeonyesha kila kona, wamekuja na kila takwimu. Tumetumia takwimu na hoja zao kuwaonyesha kiongozi wao mkuu alikwenda fyongo, anavyoichimba nchi na kupanda mbegu za kibaguzi.

Wabe alisema sisi tunahutubia watu 10 kiongozi mkuu watu 10,000.
Tulimwambia atuache na watu 10 kwasababu tunatumia haki yetu na kati ya 10 yupo Sup,Kapwela ,Wabe..


Hili la Mwembe Yanga tunalijua na tunashukuru umetualika nasi tutajumuika.
Pengine tukuache tu na kionjo


1 Kwenda Mwembe Yanga ilikuwa kutoa Rev B ya list of shame baada ya ile 11

2 Lengo la M/Yanga ni kutaka wananchi wasahau ‘ubaguzi aliouanzisha' Kisiasa wanasema political stunt.Madhumuni ni kuondoa ukakasi wa maneno ya kibaguzi dhidi ya kanda na mikoa ili apate namna ya kuingia huko hasira zikiwa chini

3 Ni namna ya kujikarabati kwani kila alipopita amekumbana na hukumu ya wananchi.
Hivyo anachokifanya ni re-brand . Anafahamu amepoteza mashiko mbele ya umma


4 Ni kutaka kujenga public trust yupo upande wa wananchi,kuondoa shaka kubwa inayozidi kutanda
Kumbuka huyu ana makando kando ya
‘kuzungumzia ' mambo ya kitaifa Ikulu.
Hajaweka sawa hilo na bado lipo masikioni mwa wananchi


Kuna hili la EL kuhamia ACT linalohusishwa kwa namna ..

5 Mwisho ni kutaka kuondoa wingu la usaliti, kwamba yule mpambanaji hajabadilika.
Unakumbuka tuhuma za usaliti zinavyozizima miongoni mwa jamii


Kapwela usihofu, tupo hapa tutafanya research na data ikiwezekana ili tukamilishe azma yetu ya right to speak.


Ahsante kutuaga , safari njema. Sisi tupo hapa
 
Back
Top Bottom