Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
HOTUBA YA RAIS 2013 DEC 31
https://www.jamiiforums.com/great-t...iasa-hotuba-ya-jk-mwisho-wa-mwaka-2013-a.html
KIFO CHA MANDELA NA YALIYOTOKEA
https://www.jamiiforums.com/newthread.php?do=newthread&f=11
SAKATA LA MAWAZIRI KUFUKUZWA NA KUJIUZLU
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/572764-duru-za-siasa-sakata-la-mwaziri.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...pecial-mgogoro-kambi-ya-upinzani-chadema.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/308989-duru-za-siasa-matukio.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/167157-duru-za-siasa-mgongano-wa-mawazo.html
DURU III: KIFO CHA MANDELA
Wana duru za Siasa
Yatakuwepo mabandiko matano mfululizo yakizungumzia tukio kubwa la kifo cha mwanaharakati na mwanasiasa Nelson Madiba Mandela.
Madiba alifariki tarehe 5 Dec na anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Qunu siku ya Jumapili.
Maadhimisho ya kifo chake yamefanyika na yanaendelea kufanyika katika miji ya Johanesburg na Pretoria kuelekea Cape Town katika viunga vya Qunu atakapopumzishwa milele.
Maadhimisho na kuenziwa kwa Mandela ni moja ya matukio makubwa kuwahi kutokea duniani kwa kuwakutanisha viongozi wa mataifa zaidi ya 100 marafiki na mahasimu.Vyombo vyote vikubwa vya habari duniani vilibeba habari inayomhusu Nelson Mandela.
Kumbu kumbu katika alama zinazojulikana kama London tower, Eiffel Tower, Dow Jones, English Premier league na nyingi zilisimamisha shughuli kwa heshima ya Mandela.
Ni tukio lenye mvuto wa aina yake ambalo sasa linazua maswali zaidi kuliko ilivyodhaniwa.
Wapo wanaohoji ni kwanini Mandela aliyekuwa gerezani nchi zikikombolewa Afrika apewe heshima kubwa kiasi hicho.
Zipo hoja, lipi kubwa alilofanya Mandela akilinganishwa na Manguli wengine duniani wa harakati za haki na usawa.
Mandela ana tofauti gani kubwa zaidi ya wanaharakati na viongozi wengine duniani.
Madiba amefanya nini katika kipindi cha miaka 5 ya uongozi kama rais kiasi cha kupewa heshima hiyo ya kushangaza
Je, alikuwa mpigani haki na usawa au alibadilika kuwa mamluki wa nchi za Magharibi
Je, kulikuwa na mkataba kati yake na makaburu wa kulindana baada ya kuachiwa kutoka kifungoni(usaliti)
Je, Mandela ameisadia vipi jamii ya Afrika kusini iliyoishi kwa mateso kwa karne nyingi za ubaguzi wa rangi.
Maswali ambayo ni 'intriguing' yanahitaji mjadala endelevu.
Tatizo linaloonekana kwa baadhi yetu ni kuchukua jambo moja na kulifanya kama legacy ya Mandela.
Mathalani, wapo wanaodai umasikini haujabalika Afrika kusini na hilo ni dalili ya kushindwa kwa sera za Madiba.
Wapo wanaomtazama Madiba kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita na kufikia hitimisho kuhusu legacy yake.
Wapo wanaojaribu kuweka viongozi wa kisiasa katika mizani kama jiwe la kupimia na sukari upande mwingine.
Zipo hoja zisizo na takwimu zinazomhukumu Madiba.
Katika mfululizo wa mabadiko yajayo tutajaribu kuangalia historia ya Madiba kwa ufupi na kuaiangalia nchi hiyo kabla na baada ya Madiba. Tutaangalia hali na nyakati mbali mbali tukizingatia hoja zilizotolewa hapo juu kumhusu Madiba na kupitia moja baada ya nyingine kwa kupanuana mawazo na fikra.
Tutaangalia kama tuna cha kujifunza kutokana na maisha ya Madiba, harakati na ujumla wa matukio yaliyojiri.
Baada ya hapo wanajamvi mtakaribishwa ili tusemezane.
Kama ada ni hoja kwa hoja, kupingana bila kupigana, kuheshimu hoja ya mwingine hata kama hukubaliani nayo na kukosoana bila kukoseana.
Let us get started, mabandiko yataanza jioni hii na siku zinavyoendelea, tunaomba uvumulivu.
Karibuni sana.
https://www.jamiiforums.com/great-t...iasa-hotuba-ya-jk-mwisho-wa-mwaka-2013-a.html
KIFO CHA MANDELA NA YALIYOTOKEA
https://www.jamiiforums.com/newthread.php?do=newthread&f=11
SAKATA LA MAWAZIRI KUFUKUZWA NA KUJIUZLU
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/572764-duru-za-siasa-sakata-la-mwaziri.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...pecial-mgogoro-kambi-ya-upinzani-chadema.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/308989-duru-za-siasa-matukio.html
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/167157-duru-za-siasa-mgongano-wa-mawazo.html
DURU III: KIFO CHA MANDELA
Wana duru za Siasa
Yatakuwepo mabandiko matano mfululizo yakizungumzia tukio kubwa la kifo cha mwanaharakati na mwanasiasa Nelson Madiba Mandela.
Madiba alifariki tarehe 5 Dec na anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Qunu siku ya Jumapili.
Maadhimisho ya kifo chake yamefanyika na yanaendelea kufanyika katika miji ya Johanesburg na Pretoria kuelekea Cape Town katika viunga vya Qunu atakapopumzishwa milele.
Maadhimisho na kuenziwa kwa Mandela ni moja ya matukio makubwa kuwahi kutokea duniani kwa kuwakutanisha viongozi wa mataifa zaidi ya 100 marafiki na mahasimu.Vyombo vyote vikubwa vya habari duniani vilibeba habari inayomhusu Nelson Mandela.
Kumbu kumbu katika alama zinazojulikana kama London tower, Eiffel Tower, Dow Jones, English Premier league na nyingi zilisimamisha shughuli kwa heshima ya Mandela.
Ni tukio lenye mvuto wa aina yake ambalo sasa linazua maswali zaidi kuliko ilivyodhaniwa.
Wapo wanaohoji ni kwanini Mandela aliyekuwa gerezani nchi zikikombolewa Afrika apewe heshima kubwa kiasi hicho.
Zipo hoja, lipi kubwa alilofanya Mandela akilinganishwa na Manguli wengine duniani wa harakati za haki na usawa.
Mandela ana tofauti gani kubwa zaidi ya wanaharakati na viongozi wengine duniani.
Madiba amefanya nini katika kipindi cha miaka 5 ya uongozi kama rais kiasi cha kupewa heshima hiyo ya kushangaza
Je, alikuwa mpigani haki na usawa au alibadilika kuwa mamluki wa nchi za Magharibi
Je, kulikuwa na mkataba kati yake na makaburu wa kulindana baada ya kuachiwa kutoka kifungoni(usaliti)
Je, Mandela ameisadia vipi jamii ya Afrika kusini iliyoishi kwa mateso kwa karne nyingi za ubaguzi wa rangi.
Maswali ambayo ni 'intriguing' yanahitaji mjadala endelevu.
Tatizo linaloonekana kwa baadhi yetu ni kuchukua jambo moja na kulifanya kama legacy ya Mandela.
Mathalani, wapo wanaodai umasikini haujabalika Afrika kusini na hilo ni dalili ya kushindwa kwa sera za Madiba.
Wapo wanaomtazama Madiba kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita na kufikia hitimisho kuhusu legacy yake.
Wapo wanaojaribu kuweka viongozi wa kisiasa katika mizani kama jiwe la kupimia na sukari upande mwingine.
Zipo hoja zisizo na takwimu zinazomhukumu Madiba.
Katika mfululizo wa mabadiko yajayo tutajaribu kuangalia historia ya Madiba kwa ufupi na kuaiangalia nchi hiyo kabla na baada ya Madiba. Tutaangalia hali na nyakati mbali mbali tukizingatia hoja zilizotolewa hapo juu kumhusu Madiba na kupitia moja baada ya nyingine kwa kupanuana mawazo na fikra.
Tutaangalia kama tuna cha kujifunza kutokana na maisha ya Madiba, harakati na ujumla wa matukio yaliyojiri.
Baada ya hapo wanajamvi mtakaribishwa ili tusemezane.
Kama ada ni hoja kwa hoja, kupingana bila kupigana, kuheshimu hoja ya mwingine hata kama hukubaliani nayo na kukosoana bila kukoseana.
Let us get started, mabandiko yataanza jioni hii na siku zinavyoendelea, tunaomba uvumulivu.
Karibuni sana.