Duru za siasa iii: Kifo cha mandela na yaliyotokea

Duru za siasa iii: Kifo cha mandela na yaliyotokea

Mkandara;

Tatizo lako unataka watanzania wawaandikie wasauzi historia yao. Msaada wa Tanzania ni mkubwa lakini hautoi fursa ya Tanzania kufanya hivyo. Nimeangalia shughuli za mazishi na sikuona kuwa wasauzi wana kinyongo na Mandela. Kama nchi za magharibi zinampa sifa Mandela, watu wake wanampa mara 1000 moja ya hizo. Kitu gani zaidi unataka?

Katika kipindi cha miaka mitano ya mwanzo wa utawala wake, Nyerere hakubalidisha chochote katika masuala ya kiuchumi. Hivyo sioni sababu ya wewe kumlaumu Mandela wakati alikaa madarakani miaka mitano tu?

Kuhusiana na jela, hujawahi kukaa jela. Hivyo huwezi kusema kuwa kukaa jela sio big deal. Rafiki yako ni thug na huwezi kulinganisha kukaa kwake jela na kifungo cha Mandela.

Mandela anastahili sifa zote anazopewa. Tatizo lako kila anaposifiwa Mandela, unaona anasifiwa zaidi kuliko Nyerere.
Zakumi 1964 mutiny iliyozaa Africanization ilikuwa ni matokeo ya watu kutoona mabadiliko kwa miaka 4 tangu madaraka ya ndani na uhuru.

Hakuna lilichobadilika katika ardhi hadi 1967 baada ya uchaguzi wa kwanza.
Watu walitaka kuona maajabu katika miaka 5 ya Mandela tena katika nchi iliyokuwa na matatizo makubwa ya ubaguzi na ukabila. Mandela asingeweza kufanya lolote bila kuwa na harmony, peace and tringuility.
Ndicho alichokifanya.

Wakati wanamlaani Mandela kwa ardhi, Watanzania wapo bize kutoa ardhi kwa makaburu waliokimbizwa na Mandela.
Ndicho walichokifanya msumbiji baada ya Mugabe kuwatimua.

Tuondoe boriti kwanza ili tupate fursa ya kuondoa vibanzi katika macho ya wenzetu.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;

Tatizo lako unataka watanzania wawaandikie wasauzi historia yao. Msaada wa Tanzania ni mkubwa lakini hautoi fursa ya Tanzania kufanya hivyo. Nimeangalia shughuli za mazishi na sikuona kuwa wasauzi wana kinyongo na Mandela. Kama nchi za magharibi zinampa sifa Mandela, watu wake wanampa mara 1000 moja ya hizo. Kitu gani zaidi unataka?

Katika kipindi cha miaka mitano ya mwanzo wa utawala wake, Nyerere hakubalidisha chochote katika masuala ya kiuchumi. Hivyo sioni sababu ya wewe kumlaumu Mandela wakati alikaa madarakani miaka mitano tu?

Kuhusiana na jela, hujawahi kukaa jela. Hivyo huwezi kusema kuwa kukaa jela sio big deal. Rafiki yako ni thug na huwezi kulinganisha kukaa kwake jela na kifungo cha Mandela.

Mandela anastahili sifa zote anazopewa. Tatizo lako kila anaposifiwa Mandela, unaona anasifiwa zaidi kuliko Nyerere.
Kwanza kabisa nataka kukueleza ya kwamba hakuna mahala popote nilipo ama napowalinganisha Mandela na Nyerere. nachoandika hapa ni FACTS sasa wewe unaweza kuzipa alama vyovyote upendanyo ktk maono yako na wasomaji wengine.

Sijasema sisi tunataka kuwaandikia Wasouth Historia isipokuwa Historia ni UKWELI wa EVENTS zilizotokea hapa tunaandika tu the after math. Na wala sijasema Mandela hastahili sifa anazopewa isipokuwa nachosema ni sisi tuelewe hizi sifa zinazotoka nchi za magharibi zimetazama nini haswa na sisi tunatazama nini. Sijasema mahala popote ya kwamba hata wewe unatakiwa kumsifia Mandela kwa sifa za wazungu ama usimsifie kwa lolote. Mbona unamchambua Nyerere ambaye alikupa wewe Uhuru kwa mtazamo wako na wala sii FACTS na tunajadili hiyo mitazamo yako?... Mimi isweki mtazamo wangu hapa bali ni facts tupu kuwa Mandela anasifiwa na wazungu kwa kuwaachia wao kuendelea kutawala njia kuu za uchumi. sasa iwe ni vema au vibaya hapa ndipo tunaweza kujadili kwa mitazamo yetu.

Mandela alipotoka Jela alibadilika, Mandela alokuwa Mkomunist alikuwa mpole na kutaka tu kuondoka kwa Apartheid tofauti kabisa na Mandela alojiunga ANC na kupiga kampeni za - Amandla. Hapa nitakujibu wewe pamoja na Nguruvi3, maana naona sasa watu mnataka kupotosha ukweli na lengo hilisi la UHURU wa South kama ilivyoanishwa ktk Charter of Freedom ya South. Na siku zote hili neno UHURU hutumiwa vibaya sana na watu kama vile UHURU ni kumwondoa mtawala mkoloni mweupe na kumweka mweusi badala ya UHURU kuwa ni hali ambayo Taifa au wananchi wake wanakuwa sii WATUMWA wa mtu ama utawala bila kujali rangi wala asili(irrespective of colour, race or nationality). Mtu mweusi anaweza pia kuwa mkoloni na mbaya zaidi ya mtu mweupe.

Nkuu Nguruvi3 ebu tuitazame hotuba ya Mandela aliposema haya:- During my lifetime I have dedicated my life to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination. I have cherished the ideal of a democratic and free society in which all persons will live together in harmony and with equal opportunities. It is an ideal for which I hope to live for and to see realised. But, My Lord, if it needs be, it is an ideal for which I am prepared to die'

mkuu wangu nguruvi3, Mandela anaposema WHITE DOMINATION au BLACK DOMINATION alikuwa na maana gani?..

Hivyo wangu, nchi inaweza kuwa na utumwa ikitawaliwa na mtu mweusi vile vile, na zikafanyika harakati za kuuondoa utawala huo, yakafanyika mapinduzi kwa sababu hizo hizo ambazo tuliutaka Uhuru kutoka kwa wakoloni weupe. Kila binadamu anataka kuwa huru - independent of fate or necessity, kuondokana na Utumwa. Hapa ndipo tunapoanzia kuutazama UHURU wa mtu ama taifa.

Hili neno UTUMWA unapolitafsiri ndipo unaweza kuipata siri ya UHURU maana Mtumwa mara zote sii mmiliki wa ardhi ama mali bali ni mjakazi, ni mtu wa chini ambaye kudai haki za Ubinadamu pasipo kwanza kupigania kuondokana na Utumwa huo ni sawa na kutwanga maji ktk kinu. Hii ni Imani yangu mimi sii lazima nawe uamini hivyo ila naweza kukupa mifano.

Sasa turudi wa Mandela, nachoelewa mimi ni kwamba ule wito wa wasouth unaosema AMANDLA - AWETHU (POWER TO THE PEOPLE) ina maana moja tu nayo ni kujikomboa toka ktk hali ya Utumwa. Ni madai ya kuwa HURU. Ile power of self determination attributed to the will au sio?. Kwa hiyo kuungwa mkono Mandela na wahindi wayahudi na wazungu haina maana ya kwamba wahindi na wazungu wote wanapenda kuona mfumo wa kitumwa isipokuwa mtu mweusi tu. Itakuwa uongo mkubwa tukisema sisi hatupendi Utunmwa wakati kwa mrazamo wangu hakuna race inayopenda Ubwana kama sisi tena tunapitiliza kwa kuwaweka utumwani watu weusi wenzatu.

Zakumi, hata siku moja siwezi kupingana na ukweli kwamba Mandela alijitoa Mhanga kupigana haki za WaSouth hilo ni fact na tunamsifia kwa hilo kama kina Martin Luther King. Lakini pia ni muhimu kwetu ku clarify the fact kwamba watu Wasouth bado wanatawaliwa, hawako huru isipokuwa wamepewa haki za binadamu kimaandishi na uhuru wa bendera pasipo kuwezeshwa umiliki wa aedhi ama mali.

Sijasema wala sintothubutu kusema Mandela hastahili sifa zote alizopewa. Anastahili sana ila nachosema tu ni kwamba kuna mitazamo miwili hapa. Sisi tukimsifia kwa jingine na wazungu wakimsifia kwa jingine ambalo ndilo limempa umaarufu zaidi kuliko sifia zetu sisi. na siwezi sema Mandela alitakiwa afanye nini ktk miaka mitano alokuwa rais kuhalalisha mtazamo tofauti. Isipokuwa ukweli utabakia ya kwamba Mandela alokuwa Mkomunist kabla ya kwenda jela, alipotoka jela alikuwa amebadilika kabisa na kudai tu haki za binadamu Ile Power to the people ikabakia kuwa kielelezo cha mtu mweusi kuwa IKULU wakati wananchi wake bado wapo utumwani kiuchumi.

Ni sawa kabisa nikisema Historia ya Nyerere kabla ya UHURU alionekana kupiga vita Ukomunist na alikuwa pamoja na CIA na MI6 kuhakikisha ukomunist haupewi nafasi East Afrika, lakini mara tu baada ya UHURU wetu, Nyerere alibadilka na kuwa Mkomunist. Hii ndio sababu kubwa ya Nyerere kupoteza sifa na umaarufu wake kwa wazungu japo wapo wazungu wachache wanaomfagilia. These are FACTS, sio simulizi za kufikirika or my perspective!

BTW. Niwe Mohammed Said kwa chati - nauliza tu kutaka kujua... Hivi Mandela alitumikia Jela peke yake ama walikuwa viongozi wengine wa ANC? Je kwa nini hawa wengine hawapewi sifa hizo wala hakuna historia ya mateso na maisha yao wakiwa Jela ama baada yaa japo walitumikia pia miaka 27 au hawa hawastahili sifa hizo!
 
Last edited by a moderator:
Kwanza kabisa nataka kukueleza ya kwamba hakuna mahala popote nilipo ama napowalinganisha Mandela na Nyerere. nachoandika hapa ni FACTS sasa wewe unaweza kuzipa alama vyovyote upendanyo ktk maono yako na wasomaji wengine.

Sijasema sisi tunataka kuwaandikia Wasouth Historia isipokuwa Historia ni UKWELI wa EVENTS zilizotokea hapa tunaandika tu the after math. Na wala sijasema Mandela hastahili sifa anazopewa isipokuwa nachosema ni sisi tuelewe hizi sifa zinazotoka nchi za magharibi zimetazama nini haswa na sisi tunatazama nini. Sijasema mahala popote ya kwamba hata wewe unatakiwa kumsifia Mandela kwa sifa za wazungu ama usimsifie kwa lolote. Mbona unamchambua Nyerere ambaye alikupa wewe Uhuru kwa mtazamo wako na wala sii FACTS na tunajadili hiyo mitazamo yako?... Mimi isweki mtazamo wangu hapa bali ni facts tupu kuwa Mandela anasifiwa na wazungu kwa kuwaachia wao kuendelea kutawala njia kuu za uchumi. sasa iwe ni vema au vibaya hapa ndipo tunaweza kujadili kwa mitazamo yetu.

Mandela alipotoka Jela alibadilika, Mandela alokuwa Mkomunist alikuwa mpole na kutaka tu kuondoka kwa Apartheid tofauti kabisa na Mandela alojiunga ANC na kupiga kampeni za - Amandla. Hapa nitakujibu wewe pamoja na Nguruvi3, maana naona sasa watu mnataka kupotosha ukweli na lengo hilisi la UHURU wa South kama ilivyoanishwa ktk Charter of Freedom ya South. Na siku zote hili neno UHURU hutumiwa vibaya sana na watu kama vile UHURU ni kumwondoa mtawala mkoloni mweupe na kumweka mweusi badala ya UHURU kuwa ni hali ambayo Taifa au wananchi wake wanakuwa sii WATUMWA wa mtu ama utawala bila kujali rangi wala asili(irrespective of colour, race or nationality). Mtu mweusi anaweza pia kuwa mkoloni na mbaya zaidi ya mtu mweupe.

Nkuu Nguruvi3 ebu tuitazame hotuba ya Mandela aliposema haya:- During my lifetime I have dedicated my life to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination. I have cherished the ideal of a democratic and free society in which all persons will live together in harmony and with equal opportunities. It is an ideal for which I hope to live for and to see realised. But, My Lord, if it needs be, it is an ideal for which I am prepared to die'

mkuu wangu nguruvi3, Mandela anaposema WHITE DOMINATION au BLACK DOMINATION alikuwa na maana gani?..

Hivyo wangu, nchi inaweza kuwa na utumwa ikitawaliwa na mtu mweusi vile vile, na zikafanyika harakati za kuuondoa utawala huo, yakafanyika mapinduzi kwa sababu hizo hizo ambazo tuliutaka Uhuru kutoka kwa wakoloni weupe. Kila binadamu anataka kuwa huru - independent of fate or necessity, kuondokana na Utumwa. Hapa ndipo tunapoanzia kuutazama UHURU wa mtu ama taifa.

Hili neno UTUMWA unapolitafsiri ndipo unaweza kuipata siri ya UHURU maana Mtumwa mara zote sii mmiliki wa ardhi ama mali bali ni mjakazi, ni mtu wa chini ambaye kudai haki za Ubinadamu pasipo kwanza kupigania kuondokana na Utumwa huo ni sawa na kutwanga maji ktk kinu. Hii ni Imani yangu mimi sii lazima nawe uamini hivyo ila naweza kukupa mifano.

Sasa turudi wa Mandela, nachoelewa mimi ni kwamba ule wito wa wasouth unaosema AMANDLA - AWETHU (POWER TO THE PEOPLE) ina maana moja tu nayo ni kujikomboa toka ktk hali ya Utumwa. Ni madai ya kuwa HURU. Ile power of self determination attributed to the will au sio?. Kwa hiyo kuungwa mkono Mandela na wahindi wayahudi na wazungu haina maana ya kwamba wahindi na wazungu wote wanapenda kuona mfumo wa kitumwa isipokuwa mtu mweusi tu. Itakuwa uongo mkubwa tukisema sisi hatupendi Utunmwa wakati kwa mrazamo wangu hakuna race inayopenda Ubwana kama sisi tena tunapitiliza kwa kuwaweka utumwani watu weusi wenzatu.

Zakumi, hata siku moja siwezi kupingana na ukweli kwamba Mandela alijitoa Mhanga kupigana haki za WaSouth hilo ni fact na tunamsifia kwa hilo kama kina Martin Luther King. Lakini pia ni muhimu kwetu ku clarify the fact kwamba watu Wasouth bado wanatawaliwa, hawako huru isipokuwa wamepewa haki za binadamu kimaandishi na uhuru wa bendera pasipo kuwezeshwa umiliki wa aedhi ama mali.

Sijasema wala sintothubutu kusema Mandela hastahili sifa zote alizopewa. Anastahili sana ila nachosema tu ni kwamba kuna mitazamo miwili hapa. Sisi tukimsifia kwa jingine na wazungu wakimsifia kwa jingine ambalo ndilo limempa umaarufu zaidi kuliko sifia zetu sisi. na siwezi sema Mandela alitakiwa afanye nini ktk miaka mitano alokuwa rais kuhalalisha mtazamo tofauti. Isipokuwa ukweli utabakia ya kwamba Mandela alokuwa Mkomunist kabla ya kwenda jela, alipotoka jela alikuwa amebadilika kabisa na kudai tu haki za binadamu Ile Power to the people ikabakia kuwa kielelezo cha mtu mweusi kuwa IKULU wakati wananchi wake bado wapo utumwani kiuchumi.

Ni sawa kabisa nikisema Historia ya Nyerere kabla ya UHURU alionekana kupiga vita Ukomunist na alikuwa pamoja na CIA na MI6 kuhakikisha ukomunist haupewi nafasi East Afrika, lakini mara tu baada ya UHURU wetu, Nyerere alibadilka na kuwa Mkomunist. Hii ndio sababu kubwa ya Nyerere kupoteza sifa na umaarufu wake kwa wazungu japo wapo wazungu wachache wanaomfagilia. These are FACTS, sio simulizi za kufikirika or my perspective!

BTW. Niwe Mohammed Said kwa chati - nauliza tu kutaka kujua... Hivi Mandela alitumikia Jela peke yake ama walikuwa viongozi wengine wa ANC? Je kwa nini hawa wengine hawapewi sifa hizo wala hakuna historia ya mateso na maisha yao wakiwa Jela ama baada yaa japo walitumikia pia miaka 27 au hawa hawastahili sifa hizo!

Mkandara;

Tatizo la watanzania wengi, wewe ukiwa miongoni mwa wenye mawazo hayo, wanafikiri kuwa AFRICA REVOLVES AROUND TANZANIA. Hivyo matatizo yote ya kumkomboa mtu mweusi barani Afrika ni lazima yaangaliwe kwa kupitia darubini za watanzania.

Ukweli wa mambo watanzania longolongo nyingi sana. Miaka 50 ya uhuru ilitosha kuonyesha jinsi mtanzania alivyokombolewa kwa vitendo. Na hii ndio ingekuwa historical fact ya kumsuta Mandela na wala usingesikia hoja ya kukupinga kutoka kwangu.

Tatizo lako unatumia preconceived truth alizohubiri Nyerere miaka ya 60 kama facts za kumkomboa mwafrika. Na kiongozi yoyote ambaye hajazitumia hizo unamwona ajafanya kazi. Na hii ndio point inayonirudisha kwenye mjadala huu wa Mandela.

Mpaka sasa Afrika kusini inatoa viongozi wengi wenye vipaji kuliko nchi yoyote barani Afrika. Hivyo kazi ya kuondoa umasikini ilikuwa sio ya Mandela pekee yake. Na ndio maana hakukaa zaidi ya miaka mitano madarakani. Afrika kusini sio nchi iliyopata uhuru ikiwa na kuhani mkuu mmoja.

Kuhusiana na facts unazotaka kutumia kunielimisha, ukweli wa mambo hakuna facts. Historia inatuonyesha wazi kuwa hakuna nchi yoyote ya kiafrika iliyoweza kuwawezesha watu wake katika kipindi kifupi. Na zilizojaribu, zilishindwa. Hivyo wa Sauzi walikuwa au wana machaguo mawili tu. Waige waafrika wenzao na baadaye mambo yaende ovyoovyo au wafanye orderly transformation?

Walichagua orderly transformation. Kama wewe unaona wanachofanya si sahihi, basi waletee mifano kutoka bongo. Kumbuka mkono mtupu haulambwi. Mpaka sasa wewe unalalamika tu lakini huna alternative solution to offer.

Kuhusiana na tafsiri ya utumwa na uhuru, acha longolongo. Katika dynamics za uchumi wa sasa, kuna mambo mengi kuliko umilikaji wa ardhi.
 
Mkandara;

Tatizo la watanzania wengi, wewe ukiwa miongoni mwa wenye mawazo hayo, wanafikiri kuwa AFRICA REVOLVES AROUND TANZANIA. Hivyo matatizo yote ya kumkomboa mtu mweusi barani Afrika ni lazima yaangaliwe kwa kupitia darubini za watanzania.

Ukweli wa mambo watanzania longolongo nyingi sana. Miaka 50 ya uhuru ilitosha kuonyesha jinsi mtanzania alivyokombolewa kwa vitendo. Na hii ndio ingekuwa historical fact ya kumsuta Mandela na wala usingesikia hoja ya kukupinga kutoka kwangu.

Tatizo lako unatumia preconceived truth alizohubiri Nyerere miaka ya 60 kama facts za kumkomboa mwafrika. Na kiongozi yoyote ambaye hajazitumia hizo unamwona ajafanya kazi. Na hii ndio point inayonirudisha kwenye mjadala huu wa Mandela.

Mpaka sasa Afrika kusini inatoa viongozi wengi wenye vipaji kuliko nchi yoyote barani Afrika. Hivyo kazi ya kuondoa umasikini ilikuwa sio ya Mandela pekee yake. Na ndio maana hakukaa zaidi ya miaka mitano madarakani. Afrika kusini sio nchi iliyopata uhuru ikiwa na kuhani mkuu mmoja.

Kuhusiana na facts unazotaka kutumia kunielimisha, ukweli wa mambo hakuna facts. Historia inatuonyesha wazi kuwa hakuna nchi yoyote ya kiafrika iliyoweza kuwawezesha watu wake katika kipindi kifupi. Na zilizojaribu, zilishindwa. Hivyo wa Sauzi walikuwa au wana machaguo mawili tu. Waige waafrika wenzao na baadaye mambo yaende ovyoovyo au wafanye orderly transformation?

Walichagua orderly transformation. Kama wewe unaona wanachofanya si sahihi, basi waletee mifano kutoka bongo. Kumbuka mkono mtupu haulambwi. Mpaka sasa wewe unalalamika tu lakini huna alternative solution to offer.

Kuhusiana na tafsiri ya utumwa na uhuru, acha longolongo. Katika dynamics za uchumi wa sasa, kuna mambo mengi kuliko umilikaji wa ardhi.
Kwanza mkuu samahani sana kwa kusema kwamba unakosea sana kumdhania mtu ni ktk kundi gani ama tunafikiri nini kuhusu maswala ya ukombozi Afrika kusini.

Hakuna mahala nimesema ya kwamba ukombozi wa Afrika kusini ulitokana na Tanzania isipokuwa tunazungumzia mchango wa Tanzania ktk ukombozi wa nchi hizo. Nadhani unakumbuka ya kwamba SADC iliundwa makhsusi kwa ajili hiyo na Nyerere akiwa mwenyekiti wake wa kwanza tulihusika sana na ukombozi tofauti na historia inayosambazwa. Hotuba za mwalimu Nyerere UN zilichukuliwa kama hotuba za AhmadinaJad wa Iran wakati huo Reagan na Mama Thatcher wakionekana mabingwa wa mapinduzi ya ukoloni mamboleo(uchumi). Tulivunja uhusiano na nchi zote zinazokoloni wazawa. Tulitishia hadi kuvunja uhusiano na Uingereza kutokana na msimamo wake na kadhalika na hatukuwa sisi peke yetu bali kundi la nchi za SADC zikiwemo nchi huru za Zambia na Botswana. Sasa iwe makosa ama sio tunachokifanya hapa ni kuweka record sawa ya matukio.

Nakuomba tu ufahamu ya kwamba tunachozungumzia hapa ni Nafasi yetu ktk ukombozi wa nchi hizo na sii matokeo ya utawala wa mweusi kiuchumi. Hili ni swala linalohusu UHURU wa mwananchi na nafasi yake ktk kujitawala kiuchumi na sii matokeo ya Uhuru huo umewafikisha wapi. iwe sisi hatukufanikiwa zaidi ya South kama nchi lakini ukweli unabakia sisi tulipewa UHURU na nafasi ya kufanya maamuzi yetu wenyewe ktk mustakabari wa nchi hii.

Unaposhindwa kutazama ni nafasi ya wananchi kiuchumi maana binafsi yangu naamini kuwa UCHUMI wowote unaokua wakati sii wako wakla haukunufaishi huo sii UHURU wa kweli. Huwezi kuhesabu utajiri wa kaka ama baba yako bali utahesabu utajiri unaokunufaisha wewe. Hii dhana ya kwamba maendeleo ya nchi (ukuaji wa GDP) ndio maendeleo ya wananchi sikubaliani nayo isipokuwa nakubaliana na dhana inayosema maendeleo ya mwananchi ndio maendeleo ya nchi. Na mwananxcchi hawezi kuendelea ikiwa hayuko HURU ktk miliki ya ardhi na rasilimali.

Uhuru tuloupata sisi umetuwezesha sisi kuwa na watu kama Bakhresa (mfano mdogo sana) waloanza na kushona viatu leo hii ni matajiri wanaomiliki viwanda, tunao kina Mengi na wengine wengi tu ambao huwezi kuwakuta South. Hata ukienda Kenya, Uganda na nchi nyinginezo utakuta wazawa matajiri walofanikiwa kutokana na kuwa HURU. Uhuru wetu umetupa nafasi sote, iwe mimi au wewe kuweza kuwa kama Bakhresa wakati huko South, mwafrika bado ni mtumishi wa mzungu na itakuwa ndoto kufanikiwa labda aibe au kupitia utawala wa ANC.

Majuzi tu tuliona mgomo wa wachimba migodi walivyopelekeshana na Wawekezaji kuhusu malipo yao, serikali ikishindwa kufanya maamuzi magumu kwa sababu wametawaliwa kiuchumi. Kifupi pamoja na South kuwa mbele kiuchumi, wana GDP kubwa lakini wananchi wake hawafaidiki na hali hiyo bado wako utumwani mafanikio hayo wanayasoma tu ktk magazeti. Wananchi wake bado ni POunda kama wabeba unga wakati wanaofaidika ni mawakala na wenye mitaji. Mapato ya uwekezaji South yanakwenda kuzinufaisha nchi za magharibi na ndiko sisi pia sasa tunakoelekea.

Ni kutokana na mfumo huu wa Ukoloni Mamboleo ambao mtu kama mimi naupiga vita sana. Na bahati mbaya sana nchi yetu imerudi ktk mfumo wa kutawaliwa kiuchumi. Yale madhara ya Ujamaa wa Nyerere mtakuja kuyaona yana nafuu kuliko madhara ya Kutawaliwa kiuchumi. Wee subiri maana hatujawahi ku experience hali hii ndio maana ni rahisi sana kum judge Byerere.

Hivyo sipimi mafanikio ya nchi yetu kwa kutumia ukuaji wa GDP kama wanavyoamini wasomi wetu, bali napima mafanikio ya nchi kiuchumi kupitia mabadaliko ya hali ya maisha ya wananchi wake. Yule mama wa Kariakoo na Kibanda chake cha vyumba sita na shmba lake la hekari 10 Mbezi namuona yuko huru zaidi ya wewe ulopanga nyumba ya kupangisha Upanga huku ukimtumikia mzungu kama dereva wake. Huyo mama ana miliki nyumba na shamba lake hizi ni assets zake ambazo nyie hamzithaminishi isipokuwa mnatazama kavuna nini kwangu yuu huru hata iwe analima na kuvuna mhogo.

Huyo mama ana uhuru wa kufanya maamuzi yoyote na yuko huru kuliko wewe ambaye hupati usingizi vizuri ktk nyumba inayomiliiwa na mtu mwingine. Kila ukisikia mlango ukigongwa unaanza kujiuliza kama ni baba mwenye nyumba, sijui kuna tatizo gani. Ukiitwa na mzungu jasho linakutoka! Ni imani yangu kuwa hata siku moja yule mfanyakazi wako nyumbani amnayekufulia nguo, kata majani hawezi kudai haki ya usawa na wewe mwajiri wake mpaka yeye mwenyewe amekuwa HURU kiuchumi ndipo utamuheshimu. Hizi habari za kwamba miye na treat kijakazi wangu kaa ndugu ni hadithi za kupoza watu lakini ukweli utabakia kuwa huyu mtu ni MTUMWA na hawezi kupewa haki sawa na bwana wake pasipo mtumwa mwenyewe kuwa huru wa nafsi yake ktk maamuzi.

Mkuu wangu, ukiweza kunielewa hapa itakusaidia sana tunapozungumzia tofauti baina ya Uhuru wa bendera na UHURU wa kiuchumi. Hili neno UCHUMI lisikufanye uanze kupima mafanikio ya nchi zetu ktk mafaniko ya upangaji ama umiliki. Kijakazi anayekula vizuri na kulala ktk ghorofa asikufanye ufikiri ana maisha mazuri kuliko Mkandara anayeishi Kariakoo isipokuwa pima uwezekano wa Mkandata kwenda kujenga Mbezi maana analo shamba lake kule.

Kiukweli Watanzania leo hii wanajenga majumba yao wenyewe. Ni Watanzania wanaoibadilisha miji yetu, nenda Msasani, Mbezi, Tabata huko mikoani ni Watanzania wazawa ndio wanajenga maghorofa, wanaomiliki mashamba na mzunguko wa fedha namapato yao unazunguka ndani japo sii kwa kasi sawa na South.

Huko South utatembea hadi miguu ikuvimbe kuliona Ghorofa mjini linamilikiwa na Mmatumbi kama sii mkopo. Na wataweza vipi kujenga ikiwa hawamiliki ardhi?. Hivyo hata hao wanaoonekana wanazo nyumba ni ktk mfumo huu wa Kibepari wa kukopeshwa maana hana ardhi ya kujenga nyumba yake. Ardhi ni ya mzungu na hata mkopo anaupata toka benki ya mzungu ambao wote kwa pamoja wamewekeza makusanyo hayo huko makwao. UBEPARI hauna maana kila kitu kipitie kwa mzungu bali ni mfumo unaowezekana kutumiwa wakati wananchi wake wote wamewezeshwa kumiliki. Hali iliyopo South ni UKOLONI MAMBO LEO yaani uhuru wa kupeperusha Bendera na hata hilo pia wamekataa kutoa zote.

Yalokwisha tokea kwetu Tanzania wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na yanayoendelea kutokea leo ni maamuzi yetu sisi wenyewe tufanye nini na umilikaji huo. Iwe makosa yalifanyika ama yanaendelea kufanyika tutajilaumu sisi wenyewe maana tumeupata UHURU wa kweli kuliko huko South ambako wananchi wake hawana UHURU huo na hawawezi kubadilisha maisha yao hata kama wanapenda.

Anachokifanya JK leo hii ni sawa kabisa na muafaka aloingia Mandela wakati akitoka Jela. JK leo anauza UHURU wetu kiuchumi na ndio maana unaona watu wanauawa huko Loliondo, Bulyanhulu na kadhalika. Na itafika wakati sisi wananchi hatutaruhusiwa hata kuoga beach ama kwenda baadhi ya Hotel, mbuga ama mashamba maana yanamilikiwa na wageni. Na wala hili sii tatizo kubwa bali kuelewa kwamba pato kubwa la uwekezaji huo unakwenda kukuza hali ya maisha ya wananchi wa nchi nyinginezo. Canada, Uingereza, Uhomanzi, Belgium zote hizi zinafaidika zaidi ya South wenyewe ktk mauzo ya ukulima,madini na mbuga za South. Majuzi tu nilikuwa napita mitaa ya Don Mills, Toronto nikalikuta ghorofa kubwa la ofisi za DE BEERS...Nikasema ama kweli haya mashirika ya kigeni ni sawa na World Vision wanaokuja Afrika kutoa misaada kwetu wakati michango inayotolewa asilimia 80 inalipa mishahara ya wafanyakazi wake. Ni less than 10% inayomfikia mtoto ulokusudiwa kupewa - Kweli kabisa unavyosema - Mkono mtupu haulambwi!
 
Kufunga maono yangu, Tanzania ni yetu itakapo kwenda ama tutakapo ipeleka kiuchumi ni maamuzi yetu kama mama yule mwenye shamba anayelima mhogo badala ya ngano. Na tunayo nafasi na uwezo wa kubadili ndio maana pia tunayo haki ya kuwalalamikia viongozi, watendaji na wananchi kwa mapungufu yoyote lakini huko South Afrika huwezi hata kumlalamikia Zuma maana hana nguvu ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi ni mtawala wa bendera acha aendelee kukanyaga vipapi tu, hii ni kutokana na Uhuru walopewa.
 
Kufunga maono yangu, Tanzania ni yetu itakapo kwenda ama tutakapo ipeleka kiuchumi ni maamuzi yetu kama mama yule mwenye shamba anayelima mhogo badala ya ngano. Na tunayo nafasi na uwezo wa kubadili ndio maana pia tunayo haki ya kuwalalamikia viongozi, watendaji na wananchi kwa mapungufu yoyote lakini huko South Afrika huwezi hata kumlalamikia Zuma maana hana nguvu ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi ni mtawala wa bendera acha aendelee kukanyaga vipapi tu, hii ni kutokana na Uhuru walopewa.

Wawekezaji Afrika ususani Tanzania ni BiniMungu sio biniadam
 
Kufunga maono yangu, Tanzania ni yetu itakapo kwenda ama tutakapo ipeleka kiuchumi ni maamuzi yetu kama mama yule mwenye shamba anayelima mhogo badala ya ngano. Na tunayo nafasi na uwezo wa kubadili ndio maana pia tunayo haki ya kuwalalamikia viongozi, watendaji na wananchi kwa mapungufu yoyote lakini huko South Afrika huwezi hata kumlalamikia Zuma maana hana nguvu ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi ni mtawala wa bendera acha aendelee kukanyaga vipapi tu, hii ni kutokana na Uhuru walopewa.


Mkandara;

Nimesoma posti zako. Unaziandika kwa machungu yanayotokana na maisha ya weusi. Lakini kumbuka kuwa kufanya maamuzi kwa kutumia hoja ya uchungu peke yake haitoshi ni lazima busara na utulivu utumike.

Chukua mfano wa Tanzania. Mali binafsi zilitaifishwa. Na wengi waliotaifishiwa mali zao au vizazi vyao vilivyofuatia vinaishi maisha bora kuliko waliochukua mali. Watanzania wazawa waliona kama uchukuaji mali ni njia pekee ya kujikomboa.

Lakini ukweli wa mambo ni kuwa pamoja na wazungu kutumia nguvu na dhuluma kujitajirisha kwa kutumia migongo na rasimali za waafrika, walikuwa na vitu muhimu vilivyochangia katika utajiri wao. Kwanza walikuwa na maarifa katika fani walizotumia kutengeneza utajiri. Pili walitumia sheria kuhalalisha umiliki wa mali zao. Tatu wana-control mfumo wa fedha na maarifa.

Vitu hivi muhimu katika kuchangia utajiri ni sifa muhimu katika jamii yoyote inayotaka maendeleo ya kisasa. Sifa hizi hazipo katika jamii nyingi za kiafrika. Hivi ni nchi gani au jamii gani zinaendelea bila kuwa mfumo mzuri sheria. Makaburu na walowezi wa Zimbabwe walipitisha sheria za kumdhulumu mwaafrika na kuzilinda na kuzifanyia kazi.

Taasisi za elimu katika ngazi mbalimbali, ziliwafanya au zinawafanya wazungu wawe na maarifa na uzoefu wa kupiga maendeleo kwa ufanisi mkubwa huku wakiwa na mfumo mzuri wa kifedha.

Tukirudi kwenye mada, maendeleo ya mwafrika mweusi hayana short cuts. Na kuwa na uchungu kama ulio nao hakutafanya safari iwe fupi na isiyo na maumivu. Umilikaji wa ardhi peke yake hautoshi. Hili afaidike ni lazima mwafrika awe na ingredients za maendeleo. Kwanza ni lazima awe na uhuru wa kutunga sheria ambazo ni lazima zifuatwe na kulindwa. Pili ni lazima awe na taasisi za maarifa, fedha na mambo mengine ya kijamii na kiutawala.

Kwa mtaji huu sioni kwanini bado unaona kuwa juhudi za waSauzi hazitoshi. Uhuru wao sio uhuru wa bendera kama unavyotaka kuweka hapa. Wamepata uhuru wa kujitungia sheria ambazo zinawawezesha kuunda na kulinda taasisi mbalimbali zitakazoleta maendeleo ya nchi na jamii. Hii sio kazi ya muda mfupi. Ni kazi inayochukua kizazi.

Kama unaona ni kazi ya muda mfupi, je Tanzania iliyotaka kujenga maendeleo ya jamii bila kuwa taasisi za kijamii hipo wapi?
 
Mkandara;

Nimesoma posti zako. Unaziandika kwa machungu yanayotokana na maisha ya weusi. Lakini kumbuka kuwa kufanya maamuzi kwa kutumia hoja ya uchungu peke yake haitoshi ni lazima busara na utulivu utumike.

Chukua mfano wa Tanzania. Mali binafsi zilitaifishwa. Na wengi waliotaifishiwa mali zao au vizazi vyao vilivyofuatia vinaishi maisha bora kuliko waliochukua mali. Watanzania wazawa waliona kama uchukuaji mali ni njia pekee ya kujikomboa.

Lakini ukweli wa mambo ni kuwa pamoja na wazungu kutumia nguvu na dhuluma kujitajirisha kwa kutumia migongo na rasimali za waafrika, walikuwa na vitu muhimu vilivyochangia katika utajiri wao. Kwanza walikuwa na maarifa katika fani walizotumia kutengeneza utajiri. Pili walitumia sheria kuhalalisha umiliki wa mali zao. Tatu wana-control mfumo wa fedha na maarifa.

Vitu hivi muhimu katika kuchangia utajiri ni sifa muhimu katika jamii yoyote inayotaka maendeleo ya kisasa. Sifa hizi hazipo katika jamii nyingi za kiafrika. Hivi ni nchi gani au jamii gani zinaendelea bila kuwa mfumo mzuri sheria. Makaburu na walowezi wa Zimbabwe walipitisha sheria za kumdhulumu mwaafrika na kuzilinda na kuzifanyia kazi.

Taasisi za elimu katika ngazi mbalimbali, ziliwafanya au zinawafanya wazungu wawe na maarifa na uzoefu wa kupiga maendeleo kwa ufanisi mkubwa huku wakiwa na mfumo mzuri wa kifedha.

Tukirudi kwenye mada, maendeleo ya mwafrika mweusi hayana short cuts. Na kuwa na uchungu kama ulio nao hakutafanya safari iwe fupi na isiyo na maumivu. Umilikaji wa ardhi peke yake hautoshi. Hili afaidike ni lazima mwafrika awe na ingredients za maendeleo. Kwanza ni lazima awe na uhuru wa kutunga sheria ambazo ni lazima zifuatwe na kulindwa. Pili ni lazima awe na taasisi za maarifa, fedha na mambo mengine ya kijamii na kiutawala.

Kwa mtaji huu sioni kwanini bado unaona kuwa juhudi za waSauzi hazitoshi. Uhuru wao sio uhuru wa bendera kama unavyotaka kuweka hapa. Wamepata uhuru wa kujitungia sheria ambazo zinawawezesha kuunda na kulinda taasisi mbalimbali zitakazoleta maendeleo ya nchi na jamii. Hii sio kazi ya muda mfupi. Ni kazi inayochukua kizazi.

Kama unaona ni kazi ya muda mfupi, je Tanzania iliyotaka kujenga maendeleo ya jamii bila kuwa taasisi za kijamii hipo wapi?
Mkuu wangu hapa nakubaliana na wewe sana ktk yote isipokuwa tu ni pale hoja inapofikia KUTAIFISHA ama KUTOTAIFISHA. Sijui kama ulikuwa na maana gani? ila nitachukulia kana unauliza kutaifisha kumeleta mabadiliko gani ktk jamii yetu, bora tusinge taifisha.

Nachoweza kusema ama kurudia kusema tena ni kwamba hakuna nchi iliacha mali za wakoloni mikononi mwa mkoloni waendelee kumilimi maliasili nna rasilimali zao walipodai UHURU. KIla nchi iliyodai UHURU iwe UINGEREZA au MAREKANI walichopigania ni miliki ya MALIASILI na RASILIMALI sio UHURU wa mipaka na kupeperusha bendera. Ni South pekee duniani ilokubali Uhuru wa Bendera na ndio sifa kubwa alosifiwa Mandela na nchi za magharibi..

Labda nikutonye kidogo, siku yoyote ukisikia Marekani akimsifia rais ama mtu yeyote basi jua mtu huyo amewafaidisha wao. Marekani siku zote hutazama interest zao kwanza ili kusifia ama kukashifu lolote na sii nje ya mahitaji yao wao. They careless ikiwa kiongozi anaua na kuwatesa wananchi wake kama Saadam, Marcus, Mobutu au Mobarak hadi siku atakapo jaribu kuwageuka.

Na sizungumzi kwa Uchungu wa mtu mweusi bali nazungumzia ni ukweli mtupu. Sina ushabiki isipkuwa nasukumwa na HAKI ya mwanadamu iwe mzungu au mwarabu nitatumia mifano hii hii tena basi ingelikuwa vizuri sana kama ungetumia mifano yao KUTAIFISHA mali za wakoloni wao ukaeleza wao walifanya nini kinyume cha sisi weusi. Na hapo ndipo tungelijua sisi tulikosea wapi maana hata wazungu nao walipopata Uhuru wao walitaifisha mali za wakoloni wao. Hivyo basi mkuu, swala la kutaifisha mali za mkoloni haina maelezo kwa sababu kwanza haikuwa ardhi wala rasilimali yao ila WALIPORA ardhi kwa nguvu, kujimilikisha, kisha wakaitumia kujenga utajiri wao. Kudai haki miliki ya ardhi na kila kilichomo ni haki ya mwenye ardhi kama vile mtu kaja kujenga ktk kiwanja chako

Nakuomba tu unielewe kwa njia hii ya KUHALALISHA miliki maana hata wewe hutakubali mtu akija kujenga nyumba ya ghorofa ktk kiwanja chako pasipo ridhaa yako hata kama wewe huna uwezo wa kujenga ghorofa. Swala ni HAKI ya MTU isidhulumiwe kwa sababu ya uwezo wake bali makubaliano baina yao ndio yapewe nafasi na kuhalalishwa. Mkoloni akikubaliana na sisi kuwekeza nchini haitajkuwa na ubaya wowote maadam sisi tumepewa nafasi ya kufikiri na kufanya maamuzi. Na ndio ndio maana leo sisi tunamlaumu JK, hivyo kama kuna makosa hatuwezi kuwalaumu tena wakoloni ama wawekezaji isipokuwa mchawi yuu baina yetu..

Ni kweli kabisa ya kwamba sisi Waafrika hatukuwa na sifa hizo kutokana na kwamba hatukujua UHURU ni kitu gani zaidi ya Bendera. Uhuru wa kumwondoa mtawala mzungu na kumweka mweusi kuwa ndio KUJITAWALA japo binafsi naamini kabisa kwamba Nyerere alijua maana ya UHURU na hakueleweka kutokana na kwamba ndiye pekee alokuwa msomi, alokuwa na exposure ya nchi za nje akajua wenzetu walipopigania Uhuru walitaka umiliki wa kitu gani. kama sikosei hositoria inasema tulipopata Uhuru tulikuwa na wasomi wangapi wenye Phd kama sii Nyerere peke yake?

Na ukumbuke tu ya kwamba wenzetu wanapokuwa na MAHITAJI hutumia kila njia kuhakikisha mahitaji yao yanapata suluhisho - Demand and Supply tofauti na sisi waafrika ambao tumejibweteka pasi utamaduni wa kukidhi mahitaji yetu isipokuwa kwa kupitia njia za vipaji tulojaaliwa zaidi ya maarifa ya ubunifu. Na hapa ndipo tunakuta umuhimu wa darasa, umuhimu wa elimu ya uchumi, tekonologia na sayansi na uwekezaji wake. Tunahitaji Umeme na maji ili viwanda vijengwe ama vilivyopo vifanye kazi, sisi ndio kwanza tunaahidiana wananchi kana vile hili sii swala la kiuchumi ni janga la wananchi ktk majumba yao hawana umeme wala maji - Hatuna MAARIFA ama hatukuelimika maana JK kasomea uchumi.

Hivyo pale wao walipokuwa na maarifa katika fani ilitokana na kutazama mahitaji kwanza. DEMAND and SUPPLY ya bidhaa ndio msingi wa elimu yao ktk kutengeneza UTAJIRI iwe kwa wakati ule ama leo na ndio sababu kubwa ya watu kwenda shule. Wametupiga bao na wataendelea kutupiga mabao kutokana na sisi tunaenda shule ili tupate KUAJIRIWA wakati wao wanakwenda shule ili kukidhi soko la MAHITAJI. Ndio maana kuna usisitizaji mkubwa wa kuongea kiingereza leo hii kuliko sayansi na tekonologia, tukajua hata namna ya kutengeneza juice ya embe na nanasi na kuihifadhi kama kipoza joto la mwili.

Hivyo, tumeanza na mguuu wa shoto ktk utafutaji wa elimu, watu wanasoma lakini hawaelimiki isipokuwa tunajaza madarasa kuleta takwimu nzuri za kufuta ujinga. Na ndio maana wao walijenga viwanda wakati sisi hadi leo tunakidhi mahitaji yetu kwa kuagiza walivyokwisha tengeneza wao iwe hata kutoka China au India. Leo hii mahitaji yetu ni ya kufuata wao kama fashion vile, maana hatuna elimu wala fikra ya kutazama MAHITAJI kuwa msingi wa ujenzi wa uchumi wetu.

Hili la SHERIA kuhalalisha umiliki wa mali ndilo lilotusukuma hata sisi (Nyerere) kutaifisha mali zao na tukajenga mfumo wa fedha na maarifa. Mfumo ambao ulipigwa vita vikali na wakoloni hao hao wakatuita WAKOMUNIST ilihali wao wenyewe walipoanza walitaifisha na walihakikisha uwekezaji wowote nchini mwao ulizifaidisha kwanza nchi zao. Ni kutokana na kibano tulichopewa na hawa wakoloni ilitulazimu kushusha manyanga, ikahesabiwa kwamba tumeshindwa lakini ukweli utabakia kwamba haikuwa mashindano bali tulilazimika kushindwa kutokana na wao kutubana wakihakikisha hatuuzi kitu wala hatupati kitu, Hivyo walitupa kibano, demand ikaendelea kukua bila kutoshelezwa na supply hadi ikafikia kuwa UHABA...Mwisho wa jeuri!

Ebu wewe nambie nchi kama CUBA au KOREA, unategemea vipi nchi hizi zitaweza kupata maendeleo ikiwa zimewekewa vikwazo kwa sababu tu wameamua wao kutawala rasilimali zao wenyewe? I mean, kwa nini nchi za magharibi wasiache uwanja wazi pasipo vikwazo kwa nchi hizi ili tuone huo Ujamaa wao ukishindwa kuwaletea maendeleo. Hivyo utakuta japo CUBA wanavyo vyanzo vya kukidhi mahitaji ya Waamerika ambavyo vingewaletea UTAJIRI, Marekani inahakikisha vitu hivyo haviuziki wala haviruhusiwi kuingizwa nchi mwao na wakati huo huo MAHITAJI ya wa CUBA wanahakikisha vitu hivyo haviingii CUBA..

Kwa hiyo mkuu wangu nilohitisha ndio mtazamo wangu mimi nawe unaitazama picha hii tofauti. Tanzania tuna makosa mengi sana ya kimfumo baada ya UHURU ambayo ndio kikwazo cha maendeleo yetu. Ni Taifa lenye Utajiri pasipo kuwa na ELIMU wala UBINIFU wa kukidhi soko la MAHITAJI isipokuwa kwa kutegemea MZUNGU atuambie anahitaji nini. na ndio maana kwetu tuna majanga, sii swala la MAHITAJI tena bali ni UKOSEFU, UHABA wa supply wa vidhaa zote ktk kukidhi mahitaji yetu. Na ndio maana unazikuta NGOs kama World Vision wamesambaa kila kona kutokana na kwamba mfumo mzima wa kujitawala ni ule wa mtumwa asokuwa na maarifa hivyo Tanzania yetu itaendelea kuonekana Uwanja wa Fisi.
 
Back
Top Bottom