Duru za siasa iii: Kifo cha mandela na yaliyotokea

Duru za siasa iii: Kifo cha mandela na yaliyotokea

Zakumi,
Kumradhini, waswahili wanasema Ashakum sii matusi..
Leo mimi na wewe maana nataka watu wanisikie vizuri kuhusu huyu mwanasheria - The Great Leader. Ni kweli kabisa kapigania haki za binadamu na ndio upeo wake ktk maono tofauti kabisa na Mchumi. Mandela hakutazama sana upande wa miliki ya utajiri wa mali na ardhi kama kina Mugabe,Nyerere, Kaunda na wengineo bali alichogombania zaidi ni weusi wawe treated sawa na wazungu not second or third class citizen.

Kama mwanasheria alipoahidiwa hilo tu mzee wetu alikubali na kushusha gloves, hizi sifa zote anazomiminiwa hasa na nchi za magharibi sii kwa sababu ya mateso yake ama Huruma alokuwa nayo kutolipiza kisasi..Watakuwaje na huruma leo wakati wao ndio walomweka Jela na kumweka ktk list ya Terrorist hadi majuzi tu. Sifa kubwa ya Madiba kwao ni kukubali kuacha Utajiri wa nchi hiyo ukamatwe bado na wakoloni - BASI!

Ni kiongozi pekee duniani alopigania UHURU na akaweza kuwaacha wakoloni waendelee kukamata ardhi na njia kuu za uchumi. Huo ndio mtazamo wa viongozi wa nchi za magharibi, japo hawatasema hivyo ila eti huruma yake kutolipa kisasi maana huo Urais wangeweza kabisa kumnyima nafasi hiyo. Na sidhani kama kuna mtu humu anajua in details yaliyomi ktk Memorandum of Understanding walofanya baina Kaburu,nchi za Magharibi na Mandela kwani hadi anatoka jela ANC ilikuwa bado banned!


Mkandara;

Mandela alikuwa mkomunisti kabla Nyerere hajajua kuwa kuna kitu kinaitwa ukomunisti. Mandela alishachukua mafunzo ya kijeshi. Na alikuja Tanzania kutafuta misaada ya hivyo wewe unavyomlaumu na mkamkatalia. Na alifungwa kifungo cha maisha kwa ugaidi. Hivyo kuna kitu gani Mandela hajajaribu?

Anatoka gerezani anakuta South Afrika imebadilika. Japokuwa waafrika weusi walikuwa wanateswa, nchi ilikuwa imebadilika. Anatembelea Zambia, Tanzania, na nchi zingine anakuta nchi zimebaki vilevile na viongozi wamekuwa wafalme wa mawazo.

Mandela alikuwa na machagua mawili. Afuate mfumo wa Tanzania au Zambia na nchi iporomoke. Au kucheza na wazungu hili awape vizazi vijavyo nafasi. Alikubali kucheza na wazungu.

Alipokuja Tanzania mwaka 1990 baada ya kutoka ndani mlitakiwa kumwonyesha kitu gani mmefanya na ardhi mliyochukua.
 
Mkuu Zakumi
Kwa vile umesema Mandela alikuwa smart katika uongozi kwasababu alikuwa lawyer swali ni kuwa wafuatao hawakuwa ma lawyer, sijui nao unawaongeleje.

Winston Churchil
Roosevelt
Kennedy
G.Washington
Reagan

Mkuu Mkandara
Kuhusu suala la Mandela kuwaacha wakoloni wakimiliki ardhi
a) Mandela alipaswa kufanya nini kuhusu suala la ardhi zaidi ya ilivyo sasa
b) Ni nchi gani iliyowahi kwanyang'anya wakoloni ardhi ikapata mafanikio?

Ahsanteni


Hakuna sehemu niliyosema alikuwa smart kwa sababu alikuwa Lawyer. Nimesema taaluma yake ilichangia yeye kuwa na mtazamo tofauti na viongozi wengi weusi. Lakini hilo sio jambo pekee yake.

Vilevile kwenda jela kulimfanya awe na mtazamo tofauti na viongozi wengine ambao hawakwenda jela. Alipokuwa jela, alijenga urafiki mkubwa na baadhi ya walinzi ambao ulibadilisha mtazamo wake kuhusu wazungu.

Vilevile sijasema kuwa watu wa taaluma zingine sio viongozi wazuri.

Kagame kama military command ambaye aliendesha military campaign, kuna ujeshi-ujeshi katika uongozi wake. Hivyo kuna uhalali wa kusema kuwa Nyerere alikuwa na ualimu ualimu ndani ya uongozi wake. Mwinyi alikuwa na ualimu ualimu. Na Mandela alikuwa na uwanasheria.
 
Mkandara;

Mandela alikuwa mkomunisti kabla Nyerere hajajua kuwa kuna kitu kinaitwa ukomunisti. Mandela alishachukua mafunzo ya kijeshi. Na alikuja Tanzania kutafuta misaada ya hivyo wewe unavyomlaumu na mkamkatalia. Na alifungwa kifungo cha maisha kwa ugaidi. Hivyo kuna kitu gani Mandela hajajaribu?

Anatoka gerezani anakuta South Afrika imebadilika. Japokuwa waafrika weusi walikuwa wanateswa, nchi ilikuwa imebadilika. Anatembelea Zambia, Tanzania, na nchi zingine anakuta nchi zimebaki vilevile na viongozi wamekuwa wafalme wa mawazo.

Mandela alikuwa na machagua mawili. Afuate mfumo wa Tanzania au Zambia na nchi iporomoke. Au kucheza na wazungu hili awape vizazi vijavyo nafasi. Alikubali kucheza na wazungu.

Alipokuja Tanzania mwaka 1990 baada ya kutoka ndani mlitakiwa kumwonyesha kitu gani mmefanya na ardhi mliyochukua.
Ndio maana nimemuuliza Mkandara, angadhani nchi gani ilifanikiwa kwa kwannyang'anya wakoloni ardhi?
Na pili, Mandela alipaswa afanye nini katika suala hilo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara,

Umeelezea point muhimu sana kuhusu msimamo wa Madiba baada ya kutoka gerezani....

Kwa kuongezea tu ni kwamba msimamo huu ulipata upinzani kutoka baadhi ya kada ndani ya ANC ambapo baadhi waliona kuwa ni usaliti baada ya miaka nenda rudi ya mapambano ya kumwondoa kaburu.
Mwalimu makada wa ANC walikuwa na mitazamo tofauti, kwamfano kijana kama Malema haaamini katika Afrika ya kusini ya rainbow yeye ni nationalist. Pamoja na upinzani alioupata ndani ya ANC Mandela alikuwa na mtazamo mkubwa sana kuliko wengi waliozaliwa baada ya yey kwenda jela.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana Nguruvi3 kwa bandiko hili juu ya maisha ya mzee Mandela.
Ni nini mustakabali wa nchi ya Afrika kusini baada ya kifo cha Mandela? Wale wapinzani wa sera zake ndani ya ANC wanaweza kupata nguvu na kulazimisha sera zao zichukue nafasi? Inaonekana waafrika wengi ndani ya SA bado wanajiona kama hawako huru, maana kiuchumi bado wengi wao hawajainuka.
Tukiwaangalia na wale wageni waliokimbilia kule Afrika kusini kusaka maisha baada ya Mandela kuingia madarakani, je hatima yao itakuwa nini. Maana wengi wameanza kuingiwa na hofu ya kushambuliwa na wenyeji kama ilivyotokea hivi karibuni.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana Nguruvi3 kwa bandiko hili juu ya maisha ya mzee Mandela.
Ni nini mustakabali wa nchi ya Afrika kusini baada ya kifo cha Mandela?

Wale wapinzani wa sera zake ndani ya ANC wanaweza kupata nguvu na kulazimisha sera zao zichukue nafasi? Inaonekana waafrika wengi ndani ya SA bado wanajiona kama hawako huru, maana kiuchumi bado wengi wao hawajainuka.

Tukiwaangalia na wale wageni waliokimbilia kule Afrika kusini kusaka maisha baada ya Mandela kuingia madarakani, je hatima yao itakuwa nini. Maana wengi wameanza kuingiwa na hofu ya kushambuliwa na wenyeji kama ilivyotokea hivi karibuni.
Mkuu Katavi legacy ya Mandela italishikilia taifa hilo kwa muda kiasi. Bado wapo washirika wa Mandela wenye sauti ndani ya ANC. Kadri legacy hiyo itakavyokuwa inakwisha hali itabadilika unless watokee watu wenye busara. Inaweza isiwe leo au kesho lakini ndani ya miaka 5 kutakuwa na mabadiliko makubwa sana.

Kuhusu umasikini, SA ni sawa na nchi nyingine duniani. Mategemeo ya kuwa Mandela angeweza kuondoa umasikini kwa miaka 5 zilikuwa ni ndoto. Tanzania pamoja na hali ya utulivu haijaweza kwa miaka 50, kwanini watu wadhani Mandela alikuwa na Mwarobaini wa tatizo hilo!

Hata hivyo takwimu zinaonyesha tangu ubaguzi ufutwe nchini SA kumekuwepo na maendeleo katika baadhi ya mambo ukilinaganisha na hali wakati wa makaburu. Kuna fursa nyingi zimekuwa sawa kwa watu wote, ujenzi wa miundo mbinu na huduma za afya na elimu umeongezeka hasa maeneno yaliyokuwa hayana fursa.

Ni kwasababu hizo za umasikini dira ya kwanza ya Mandela ilikuwa kuweka sheria ya kupata skilled Manpower kwa kuangalia suala la elimu zaidi.

Umasikini wa watu wa SA si kwasababu ya resource, ni kutokana na elimu. Wengi wao hawana elimu ya kukidhi viwango hasa katika ajira na hao ndio wanatengeneza sehemu kubwa ya umasikini.

Kuhusu wageni kushambuliwa, mashambulizi yanatokana na hasira walizo nazo watu wa Afrika kusini katika mambo ya ajira. Tatizo lao ni kutotambua kuwa elimu ndio kikwazo chao kikubwa kama ambavyo ipo Tanzania pia.
Kuondoka kwa Mandela aliyekuwa anaheshimika kuna weka mustakabali wa wageni katika njia panda.

Kuhusu Wapinzani wa sera zilizopo hawa wanaweza kupata nguvu kutokana na lindi la umasikini. Ni kama ilivyo nchi nyingine kuwa ukitaka kufanikiwa lazima utafute kundi la watu wenye kukata tamaa( desperate).
Kinachowaudhi watu wengi ni kuona ANC imekuwa kama kiota cha kuzalishia matajiri hasa wale waliokuwa wanaonekana wazalendo zaidi. Hilo ni tatizo kubwa kama lilivyo kwa CCM hapa nchini. Kwamba ANC na CCM vimeacha misingi yao na kuwa viota vya kuazlishia matycoon.

 
Last edited by a moderator:
Zipo hoja za kwamba baada ya uchaguzi wa kuondoa ubaguzi, Mandela angeweza kufanya manadiliko ili kuwasaidia watu wa Afrika hasa masikini. Na suala kubwa ni ardhi.

Maswali yasiyo na majibu ni haya
a)Je alipaswa kuwafukuza makabauru kuondoka Afrika kusini kabisa?
b) Je, alipaswa kuwanyang'anya ardhi na kuwapa wazawa?
c) Je, alipaswa kufanya mabadiliko bila kuathiri hali ya uchumi hata kama hayatampnedeza kila mtu?

Candid Scope aliwahi kuuliza kipi cha maana alikifanya?
Nami namuuliza alikuwa afanye nini ili afikie matarajio yako?
 
Zipo hoja za kwamba baada ya uchaguzi wa kuondoa ubaguzi, Mandela angeweza kufanya manadiliko ili kuwasaidia watu wa Afrika hasa masikini. Na suala kubwa ni ardhi.

Maswali yasiyo na majibu ni haya
a)Je alipaswa kuwafukuza makabauru kuondoka Afrika kusini kabisa?
b) Je, alipaswa kuwanyang'anya ardhi na kuwapa wazawa?
c) Je, alipaswa kufanya mabadiliko bila kuathiri hali ya uchumi hata kama hayatampnedeza kila mtu?

Candid Scope aliwahi kuuliza kipi cha maana alikifanya?
Nami namuuliza alikuwa afanye nini ili afikie matarajio yako?

Mizani yangu inaonyesha kwamba Madiba amekuzwa tu na vyombo vya nchi za magharibi kwa sababu ya kuwatetea makaburu ambao ni wazungu wenzao, vinginevyo sijaona cha pekee alichofanya Mandela, pengine kinachoongelewa kusamehe ni makosa kwa upande fulani kwa maana kwamba amehalalisha maovu na mauaji yaliyofanywa na makaburu wakati wa mapambono ya ubaguzi wa rangi.

Kilichobadilika tu ni safu ya viongozi wa serikali katika ngazi ya kiifa kushikwa na weuzi badala ya wazungu, lakini kama mdau ulivyosema sijaona cha pekee cha kuwajali waafrika wenzake ambao walihitaji kwa hali na mali kupata ardhi ambayo ndiyo kitu muhimu kinachotegemewa na wengi katika maisha kama alivyofanya Mugabe.

Tazama mangapi aliyofanya Nyerere, Kaunda, Samora na wengineo kwa ukombozi wa bara la Afrika, hakuna hata mmoja wao anayeenziwa na utawala wa nchi za magharibi kwa vile tu waliwanyoshea kidole. Pengine inaweza kutafsirika kwamba Mandela aliiuza South Afrika kwa wazungu imzunguko wao wamebaki tu vibaraka.
 
Mizani yangu inaonyesha kwamba Madiba amekuzwa tu na vyombo vya nchi za magharibi kwa sababu ya kuwatetea makaburu ambao ni wazungu wenzao, vinginevyo sijaona cha pekee alichofanya Mandela, pengine kinachoongelewa kusamehe ni makosa kwa upande fulani kwa maana kwamba amehalalisha maovu na mauaji yaliyofanywa na makaburu wakati wa mapambono ya ubaguzi wa rangi.

Kilichobadilika tu ni safu ya viongozi wa serikali katika ngazi ya kiifa kushikwa na weuzi badala ya wazungu, lakini kama mdau ulivyosema sijaona cha pekee cha kuwajali waafrika wenzake ambao walihitaji kwa hali na mali kupata ardhi ambayo ndiyo kitu muhimu kinachotegemewa na wengi katika maisha kama alivyofanya Mugabe.

Tazama mangapi aliyofanya Nyerere, Kaunda, Samora na wengineo kwa ukombozi wa bara la Afrika, hakuna hata mmoja wao anayeenziwa na utawala wa nchi za magharibi kwa vile tu waliwanyoshea kidole. Pengine inaweza kutafsirika kwamba Mandela aliiuza South Afrika kwa wazungu imzunguko wao wamebaki tu vibaraka.
Kwanza si kweli kuwa ametukuzwa na vyombo vya habari vya magharibi. Kila wakati alipougua habari zake zilipamba vichwa vya habari duniani.

Pengine vyombo vya habari vya Afrika vilaumiwe kwakuandika habari zake zaidi.
Msiba wa Mandela hakuna chombo cha habari kuanzia Tonga hadi Hawaii, Copenhagen hadi Captown kilichoacha habari zake. Mandela alikuwa ni habari kabla ya habari yenyewe.

Umaarufu wa Mandela si kusamehe tu, bali kuleta jamii iliyokuwa na sheria rasmi za kibaguzi, jamii iliyogawanyika kuwa taifa moja. Ni kutokana na Mandela kukaa meza moja na wabaya wake ili wajadili mustakabali wa SA.
Alifanya hivyo hata pale alipojua kuwa hana cha kupoteza tena kwasababu angeweza kufia magereza bila hofu.

Mandela alishapoteza familia na wala hakuwa na matumaini ya kuishi kama baba mwenye familia tena.
Kilichomsukuma zaidi ni kutaka kujenga misingi ya kudumu kwa vizazi vijavyo na msingi huo ni kuwa na usawa

Suala la ardhi nadhani hujaliangalia vizuri. Katika sheria za mwanzo kubadilishwa ni ile ya mwaka 1913 iliyojulikana kama Bantu Land act au Native land act iliyowazuia weusi kumiliki ardhi.
Sheria hiyo ilibadilishwa mwaka 1994 na Land restitution act iliyowapa fursa watu walionyang'anywa ardhi mwaka 1913 kudai ardhi zao. Hii ilifuatiwa na Land reform act ya Mwaka 1996 zote zikimlenga mwananchi wa kawaida.

Mandela alikuwa na choice tatu, kwanza kuwafukuza wazungu kabisa ili Waafrika wamiliki ardhi
pili, kuwanyang'anya wazungu ardhi yote na kuwapa wazawa
Tatu, kuangalia madhara yatokanayo na hatu zisizozingatia hoja mbili za awali.

Mandela alijifunza kutoka sehemu mbali mbali. Mgogoro uliozuka Kenya ni matokeo ya ardhi na ulianza wakati wa Mau Mau. Kwabahati mbaya baada ya uhuru masetla wakamiliki 90 na wachache akiwemo Kenyatta asilimia 10.

Tanzania, iliunda azimio la Arusha na kutaifisha mashamba. Tanzania haikuwa na upungufu wa ardhi bali lkilichoonekana ni madaraja ya watu. Badala ya kuwawezesha wazawa kumiliki na kuendeleza ardhi, chuki ikatawala.
Leo mashamba ya mikonge ni mapori na mashamba mengine yamebaki kuwa mbuga za wanyama.
Vipi kama serikali ingejenga uwezo kwa wazawa kwanza kwa kuwawezesha kumiliki ardhi!

Hata sasa hivi ardhi ipo lakini wangapi wanaweza kuiendeleza?
Kilichobaki ni wakubwa kujigawia mapande ya ardhi kwa kujua sehemu kubwa haina uwezo wa kuendeleza achilia mbali kumiliki.

Mandela alichokifanya ni kuweka sheria ya skills development act ili kwanza kuwajengea uwezo wakati wanawamilikisha ardhi bila kuathiri uchumi kwa namna moja au nyingine,

Zimbabwe, Mugabe amewanyang'anya ardhi. Nashangaa ukisema waafrika wamefaidika.
Sijui wamefadika na nini wakati wanazamia Tanzania na ni deal.

Uchumi wa Zimbabwe mwaka 1980 na 2013 ni sawa na 'mbingu na ardhi'
Hawa wananchi wanaosubiri mahindi kutoka Tanzania wamefaidika vipi na harakati za akina Hunzwe na Mugabe?

Mchango wa akina Samora, Nyerere na Kaunda unathaminiwa.
Unachosahau ni kuwa kwa miaka 27 Mandela alikuwa jela sijui ulitegemea ashiriki vipi katika ukombozi.

Huwezi kulinganisha role za watu mbali mbali kwa kuwaweka katika mizani kama sukari na jiwe la kupimia.
Kwa mfano unamlinganisha vipi Nyerere na Samora.
Nyerere alishiriki kuandaa mazingira, Samora alikuwa msituni.
Na wala huwezi kuweka katika mizani role ya Kaunda na Nyerere katika ukombozi hata Kaunda anakubali hilo

Nimalizie kwa kusema nipe kiongozi wa taifa moja tu duniani aliyewahi kulijenga taifa kwa miaka 5 kwa kukabiliana na kila changamoto aliyokutana nayo

Mandela hakuwa kiongozi wa kujenga taifa , alikuwa kiongozi wa kulileta taifa lililoparaganyika pamoja ili waje watakaoliendeleza.

Na kama tunadhani mandela alifanya makosa ya kutowanyang'anya ardhi wazungu, iweje sisi tuliowanyang'anya miaka 50 iliyopita tunakwenda South Afrika kuwaalika waje tuwamilikishe ardhi.
Je tumeondoa boriti machoni mwetu kwanza kabla ya kuondoa kibanzi kutoka jicho la Mandela?
 
Mwalimu makada wa ANC walikuwa na mitazamo tofauti, kwamfano kijana kama Malema haaamini katika Afrika ya kusini ya rainbow yeye ni nationalist. Pamoja na upinzani alioupata ndani ya ANC Mandela alikuwa na mtazamo mkubwa sana kuliko wengi waliozaliwa baada ya yey kwenda jela.

Mkuu @Nguruvi3

Unadhani mitazamo tofauti ndani ya ANC unatoka kwa vijana pekee (kina Malema) na sio watu wa enzi zake pia?
 
Mkuu Nguruvi3

Unadhani mitazamo tofauti ndani ya ANC unatoka kwa vijana pekee (kina Malema) na sio watu wa enzi zake pia?
Mwalimu, wenye mitazamo ndani ya ANC wapo wazee wengi tu. Tatizo ni vijana kutumiwa na wazee ambao wanachuki kuwashindilia hasira ili walete vurugu zao. Hakukuwa na sababu ya Malema kuwatukana wazungu katika nchi ambayo wazungu hao wanakaribia miaka 500 na ushee.

Ni kwa msingi huo nimesema kuondoka kwa Mandela kutaacha ombwe la wazee wenye hasira kutimiza ndoto zao.
Alichokuwa anapigania Malema ni ubaguzi ule ule ANC iliyoukataa.
Yes, wapo wazee pia ambao ni mentors wa akina Malema
 
Last edited by a moderator:
Mizani yangu inaonyesha kwamba Madiba amekuzwa tu na vyombo vya nchi za magharibi kwa sababu ya kuwatetea makaburu ambao ni wazungu wenzao, vinginevyo sijaona cha pekee alichofanya Mandela, pengine kinachoongelewa kusamehe ni makosa kwa upande fulani kwa maana kwamba amehalalisha maovu na mauaji yaliyofanywa na makaburu wakati wa mapambono ya ubaguzi wa rangi.

Kilichobadilika tu ni safu ya viongozi wa serikali katika ngazi ya kiifa kushikwa na weuzi badala ya wazungu, lakini kama mdau ulivyosema sijaona cha pekee cha kuwajali waafrika wenzake ambao walihitaji kwa hali na mali kupata ardhi ambayo ndiyo kitu muhimu kinachotegemewa na wengi katika maisha kama alivyofanya Mugabe.

Tazama mangapi aliyofanya Nyerere, Kaunda, Samora na wengineo kwa ukombozi wa bara la Afrika, hakuna hata mmoja wao anayeenziwa na utawala wa nchi za magharibi kwa vile tu waliwanyoshea kidole. Pengine inaweza kutafsirika kwamba Mandela aliiuza South Afrika kwa wazungu imzunguko wao wamebaki tu vibaraka.

Kandid Skope, Mwalimu, Nguruv3, Katavi ;

Hivi watanzania ni nani katika kutathmini mafanikio ya Mandela? Nadhani suala hili tuawaachie wananchi wa Afrika kusini? Kwa kuangalia jinsi wananchi wa Afrika kusini walivyopokea kifo cha Mandela, inaonyesha kabisa wamemweka Mandela katika nafasi ya juu. Na wamefanya hivyo sio kwa sababu vyombo vya habari na serikali za nchi za magharibi zimemkubali. Wamefanya hivyo kwa sababu wanajua maana ya kazi aliyofanya kwao.

Ndani ya Afrika ya kusini kulikuwa na mgawanyiko mkubwa. Hata miongozi mwa watu weusi kulikuwa na mgawanyiko wa kikabila. Kwa mfano baadhi ya wazulu walitaka mfumo wao wa uchifu uendelee kuwepo. Katika mjadala huu inaonyesha watu wanakumbuka yale Mandela aliyofanya kati yake na wazungu. Lakini juhudi alizofanya kati yake na viongozi wa jumuia au vyama vingine vya weusi zimesahauliwa.

Kuhusiana na umilikaji wa ardhi, watanzania ni wanafiki wakubwa. Hivi Tanzania imeonyesha mafanikio gani katika suala la kumiliki ardhi. Inaonyesha watanzania wanataka makosa yaliyofanyika Tanzania yarudiwe katika nchi zingine.

Watanzania, Wazimbabwe na watu wa kutoka Msumbiji wamekimbia nchi zao kwenda kufanya kazi mashambani nchi Afrika ya kusini. Kama siasa za ardhi za Kaunda, Samora na Nyerere zilikuwa nzuri, labda weusi kutoka Afrika kusini wangekuwa wanamiminika Tanzania, Zambia na Msumbiji kutafuta kazi.

cc: mkandara, jasusi
 
Kandid Skope, Mwalimu, Nguruv3, Katavi ;

Hivi watanzania ni nani katika kutathmini mafanikio ya Mandela? Nadhani suala hili tuawaachie wananchi wa Afrika kusini? Kwa kuangalia jinsi wananchi wa Afrika kusini walivyopokea kifo cha Mandela, inaonyesha kabisa wamemweka Mandela katika nafasi ya juu. Na wamefanya hivyo sio kwa sababu vyombo vya habari na serikali za nchi za magharibi zimemkubali. Wamefanya hivyo kwa sababu wanajua maana ya kazi aliyofanya kwao.

Ndani ya Afrika ya kusini kulikuwa na mgawanyiko mkubwa. Hata miongozi mwa watu weusi kulikuwa na mgawanyiko wa kikabila. Kwa mfano baadhi ya wazulu walitaka mfumo wao wa uchifu uendelee kuwepo. Katika mjadala huu inaonyesha watu wanakumbuka yale Mandela aliyofanya kati yake na wazungu. Lakini juhudi alizofanya kati yake na viongozi wa jumuia au vyama vingine vya weusi zimesahauliwa.

Kuhusiana na umilikaji wa ardhi, watanzania ni wanafiki wakubwa. Hivi Tanzania imeonyesha mafanikio gani katika suala la kumiliki ardhi. Inaonyesha watanzania wanataka makosa yaliyofanyika Tanzania yarudiwe katika nchi zingine.

Watanzania, Wazimbabwe na watu wa kutoka Msumbiji wamekimbia nchi zao kwenda kufanya kazi mashambani nchi Afrika ya kusini. Kama siasa za ardhi za Kaunda, Samora na Nyerere zilikuwa nzuri, labda weusi kutoka Afrika kusini wangekuwa wanamiminika Tanzania, Zambia na Msumbiji kutafuta kazi.cc: Mkandara, Jasusi
Zakumi nakubaliana nawe kuhusu umaarufu wa Mandela ndani ya Afrika kusini, ndio maana nilisema halikuwa suala la vyombo vya habari vya magharibi, in fact vya Afrika viliandika na kuzungumzia sana kuhusu Mandela.

Pili, nimejadili mzozo uliokuwepo kati ya Zulu na makabila mengine. Kama ulivyosema wazulu walitaka uchifu uendelee na hata kufikia kuunga mkono weupe kwasababu tu walikuwa wanatambua uchifu wao. Waliwatumia sana kuleta machafuko kati ya ANC na IFP cha Buthelezi.

Mandela alipokuwa rais alimkaribisha Burhelezi kama waziri wa mambo ya ndani.
Katika kumbu kumbu Mongusto Buthelezi amekaimu nafasi ya urais di chini ya mara 10 Mandela aliposafiri.
Hiki kitendo hakikuwa popular kwa ANC hardliners waliosema Buthelezi alikuwa kibaraka na kumwalika meza moja ilikuwa kusaliti damu ya wapigania uhuru.

Kuhusu suala la ardhi, nalo pia umeligusia vizuri sana. Sisi tunasema Mandela hakuwasaidia wazawa kupata ardhi.
Tunasahau ukweli kuwa alianza kwa kufanya marekebisho ya sheria ya ardhi ya Native land act ya mwaka 1913 ili weusi walionyang'anywa ardhi wafidiwe. Si kuwa wafidiwe bali wengine walirejeshewa maeneo yao.
Hilo lilifanyika kwa sheria ya restitution act ya mwaka 1994 iliyofanyiwa maboresho mwaka 1996.

Mandela hakutaka kuwanyag'anya ardhi wazungu kwa kuangalia mifano michache ya Tanzania na Zimbabwe ambapo zoezi hilo lilifanyika kisiasa zaidi ya kiuchumi. Matokeo yake ardhi ikatolewa kwa watu wasio na ufahamu wala ujuzi wa kuiendeleza. Mandela aliona ni vema atengeneze sheria ya kuendeleza wazawa kwanza (skilled development act) ili wakati ukifika wamiliki walicho nacho kwa ufundi.

Leo Watanzania wanasema Mandela hajafanya la maana kuhusu ardhi wakati Watanzania hao hao waliomilikishwa ardhi miaka 40 iliyopita wanaalika makaburu kuja kufanya investment katika ardhi.

Inasikitisha kuona tuna mng'ong'a Mandela afukuze watu wake ili sisi tuwape kile tulichomwambia Mandela amefanya kosa. Huu kama si unafiki ni ujuha ulioselelea na unahitaji rebuke ya hali ya juu.

Nimewauliza wachangiaji, Mandela alipaswa kufanya nini hasa kuhusu ardhi, hakuna jibu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi
Kwa vile umesema Mandela alikuwa smart katika uongozi kwasababu alikuwa lawyer swali ni kuwa wafuatao hawakuwa ma lawyer, sijui nao unawaongeleje.

Winston Churchil
Roosevelt
Kennedy
G.Washington
Reagan

Mkuu Mkandara
Kuhusu suala la Mandela kuwaacha wakoloni wakimiliki ardhi
a) Mandela alipaswa kufanya nini kuhusu suala la ardhi zaidi ya ilivyo sasa
b) Ni nchi gani iliyowahi kwanyang'anya wakoloni ardhi ikapata mafanikio?

Ahsanteni
Swala sio alipaswa kufanya nini bali ktk mtazamo wangu mimi UHURU wa mwafrika haukuhitaji zaidi ya Umiliki wa uchumi, au niseme mali. Ukisha kuwa na mali mkononi huo usawa utajiweka wenyewe kwa maana ya kwamba leo hii Tanzania na cnhi nyingine zote tunashindana na hapo wageni kuwekeza japo sisi wenyewe ndio tunajirudisha ktk kutawaliwa. Hii ndio Fikra za kina Lennin Karl Max na wengineo wote.

sababu kubwa ya kukosana baina ya Mandela na Winnie, Mandela na kina Oliver tambo ilikuwa ulazima wa mtu mweusi kumiliki uchumi wa nchi yao kama nchi nyingine zote duniani zilizowahi kutawaliwa. Wazungu hawakuogopa ANC wakichukua nchi watawalipizia kisasi kuwaua isipokuwa waliogopa zaidi ANC wakichukua nchi watawanyang'anya mali zao. Bila Utajiri huwezi kuwa na nguvu wala sauti. na ndicho anachopongezwa kisirisiri Mandela na hawa wazungu na sii kinginecho. Leo Watu weusi nado ni maskini na sidhani kama hesabu ya UmASKINI imepungua toka wapate Uhuru nadhani rate ya literacy na Poverty imeongezeka kwa wazawa sasa hivi kuliko zamani.

2. Jibu la swali hili ni nchi zote zilizowahi kutawaliwa hata Marekani walichukua mali zote za utawala wa Queen na kuzifanya zao kwa identity mpya ya Umarekani.India, Malaysia yaani ni nyigni mno na sidhani kama kuna nchi ambazo hazikuwahi kutawaliwa na wakaja pigania UHURU wao toka kwa wakoloni. Swala ni hakuna ilowahi kuwaachia wakoloni kuendelea kumiliki uchumi wa nchi hiyo HAKUNA isipokuwa South Afrika.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;

Mandela alikuwa mkomunisti kabla Nyerere hajajua kuwa kuna kitu kinaitwa ukomunisti. Mandela alishachukua mafunzo ya kijeshi. Na alikuja Tanzania kutafuta misaada ya hivyo wewe unavyomlaumu na mkamkatalia. Na alifungwa kifungo cha maisha kwa ugaidi. Hivyo kuna kitu gani Mandela hajajaribu?

Anatoka gerezani anakuta South Afrika imebadilika. Japokuwa waafrika weusi walikuwa wanateswa, nchi ilikuwa imebadilika. Anatembelea Zambia, Tanzania, na nchi zingine anakuta nchi zimebaki vilevile na viongozi wamekuwa wafalme wa mawazo.

Mandela alikuwa na machagua mawili. Afuate mfumo wa Tanzania au Zambia na nchi iporomoke. Au kucheza na wazungu hili awape vizazi vijavyo nafasi. Alikubali kucheza na wazungu.

Alipokuja Tanzania mwaka 1990 baada ya kutoka ndani mlitakiwa kumwonyesha kitu gani mmefanya na ardhi mliyochukua.
Zakumi,
hiyo historia uloisema kuhusu Mandela sii ya kweli na ndivyo ANC walivyotaka watu waelewe. Kifupi Hotuba ya JK majuzi huko South ndio imewafumbua macho wetu wengi kwa sababu ilikuwa siti kubwa sana na viongozi wengi sana hasa wazungu walishtuka waliposikia kwamba Mandela alipoondoka South alikuja Tanzania kupitia mpaka wa Mbeya na ndipo MK ilipozaliwa rasmi.

Hawa wazungu na wajuha wengine walivyoambiwa ni kwamba Mandela alikimbilia Botswana na kutoka huko alipenda ndege kwenda Tunisia ambako ndiko alipata mafunzo ya Kijeshi., Unajua vizuri kwamba Tunisia ndio nchi ya kwanza Afrika kuwa huru kabla kabisa ya Ghana. Na waliamini kabisa kwamba Mandela na MK walipata mafunzo ya Kijeshi Ethiopia na kadhalika wakati sisi tunajua fika kwamba kambi za MK zilikuwa Tanzania na hawa jama walipewa haki zote sawa na sisi. Walisoma hadi chuo kikuuu bure na wengine wamebeba passport zetu hadi leo.

Hotuba ya JK ilikuwa kuwakumbusha na wengine kuwajulisha kitu ambacho walifichwa kwa muda mrefu. Tanzania tumeionyesha dunia kwamba huyo Mandela alokuwa akiitwa terrorist hadi mwaka 2008 akiwa ktk list ya magaidi tulikuwa naye toka mwanzo. kambi za Materrorist zilikuwa kwetu na sisi ndio sponsors wakubwa wa mapinduzi ya kusini mwa Afrika.. Nina hakika kuanzia sasa Wasouth watatupa heshima zetu ipaswavyo. maana sio siri tena.

Mandela hakuwa na choice isipokuwa alibadilika alipokuwa Jela.Alipotoka jela yule Mandela waliyemjua kabla ya kwenda Jela hakuwa yule tena maana tayari walikwisha mlisha sumu na kumweka sawa. Alikuwa wakiletewa habari za Winnie Jela kwamba jamaa bwana mdogo ana perfomr kipapi chake wakati mzee Alisha oza kimapenzi na mengine mengi tu. He had the choice kufuata wengine ama kuendelea na mkataba ulomtoa Jela kwa kuahidiwa Urais kwa malipo ya kutotaifisha mali za wazungu.

Kisha mkuu wangu usiifanye Jela kuwa kitu cha maana saana.. Nina rafiki yangu anaoza Jela kwa kuuza unga. Sasa hivi anatumikia kifungo cha miaka 20 hii mara ya pili sijui tatu.. Maisha yake nijela tu toka akiwa na miaka 19 kwa biashara ya unga!. Kuna cha kujivunia hapo? au tunajivunia mafanikio ya jitihada na msimamo wa mtu ktk kuitafuta haki iwe ya watu ama kiuchumi..


Alipokuja Tanzania mwaka 1990 hakuwa na sababu ya kuonyeshwa bali anajua vizuri kwamba wananchi wetu ndio wamiliki wa ardhi yetu. haijalishi tunaitumia vipi ni YETU kama mama mwenye kibanda cha vyumba sita Kariakoo... huyu mama ana Nyumba YAKE, mali yake wakati mimi na wewe kina Mandela tumepanga uhindini huwezi kumsema hovyo mama huyu ila kujitazama sisi wenyewe kwanza - TUNA NINI?

Hivyo wewe nambie hao Wasouth alowakomboa wana nini?
 
Zakumi hiyo historia uloisema kuhusu Mandela sii ya kweli na ndivyo walivyotaka watu waelewe. Kifupi Hotuba ya JK majuzi huko South ndio imewafumbua macho wetu wengi kwa sababu ilikuwa siti kubwa sana na viongozi wengi sana hasa wazungu walishtuka waliposikia kwamba Mandela alipoondoka South alikuja Tanzania kupitia mpaka wa Mbeya.

Wao walivyoambiwa ni kwamba Mandela alikimbilia Botswana na kutoka huko alipenda ndege kwenda Tuniaia ambako ndiko alipata mafunzo ya Kijeshi., Unajua vizuri kwamba Tunisia ndio nchi ya kwanza Afrika kuwa huru kabla kabisa ya Ghana. Na waliamini kabisa kwamba Mandela alipata mafunzo ya Kijeshi Ethiopia na kadhalika wakati sisi tunajua fika kwamba kambi za MK zilikuwa Tanzania na hawa jama walipewa haki zote sawa na sisi. Walisoma hadi chuo kikuuu bure na wengine wamebeba passport zetu hadi leo.

Mandela hakuwa na choice isipokuwa alibadilika alipokuwa Jela.Alipotoka jela yule Mandela waliyemjua kabla ya kwenda Jela hakuwa yule tena maana tayari walikwisha mlisha sumu na kumweka sawa. Walikuwa wakiletea habari za Winnie toka Jela kwamba jamaa bwana mdogo ana perfor kipapi na mengine mengi. He had the choice kufuata wengine ama kuendelea na mktaba ulomtoa Jela kwa kuahidiwa Urais kwa malipo ya kutotaifisha mali za wazungu.

Alipokuja Tanzania mwaka 1990 hakuwa na sababu ya kuonyeshwa bali anajua vizuri kwamba wananchi wetu ndio wamiliki wa ardhi yetu. haijalishi tunaitumia vipi ni YETU kama mama mwenye kibanda cha vyumba sita Kariakoo... huyu mama ana Nyumba YAKE, mali yake wakati mimi na wewe kina Mandela tumepanga uhindini huwezi kumsema hovyo mama huyu ila kujitazama sisi wenyewe kwanza - TUNA NINI?

Hivyo wewe nambie hao Wasouth alowakomboa wana nini?
Mkuu Mkandara naomba niingie kidogo hapa wakati Zakumi anakuja.

Mandela katawala miaka 5, je alipaswa kufanya nini unachodhani kingekuwa tofauti na ilivyo sasa?
Mandela alibadilisha Native land ya mwaka 1913 kwa restitution act ya mwaka 1994, je alitakiwa afanye nini zaidi
Je, Tanzania na Zimbabwe zimefanikiwa vipi kwa hatua za ardhi ambazo Mandela alipaswa kuiga
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara naomba niingie kidogo hapa wakati Zakumi anakuja.

Mandela katawala miaka 5, je alipaswa kufanya nini unachodhani kingekuwa tofauti na ilivyo sasa?
Mandela alibadilisha Native land ya mwaka 1913 kwa restitution act ya mwaka 1994, je alitakiwa afanye nini zaidi
Je, Tanzania na Zimbabwe zimefanikiwa vipi kwa hatua za ardhi ambazo Mandela alipaswa kuiga
Hakutakiwa kufanya lolote zaidi ya alichofanya na ndivyo alivyoandikiwa na amevikwa sifa nyingi za utukufu na kadhalika afanye nini zaidi?..
Nachosema mimi ni kwamba Mandela hasifiwi kwa sababu ya huruma yake kutolipa kisasi kwa wazungu bali sababu ni kuwaachia wakoloni nguvu ya kiuchumi..jambo ambalo halijawahi kutokea dunianina hakuna kiongozi yeyote alowahi kufanya hivyo isipokuwa Mandela. was he right or wrong - hilo sijui bali ni ktk Exploration of reality!
 
Last edited by a moderator:
Hakutakiwa kufanya lolote zaidi ya alichofanya na ndivyo alivyoandikiwa na amevikwa sifa nyingi za utukufu na kadhalika afanye nini zaidi?..
Nachosema mimi ni kwamba Mandela hasifiwi kwa sababu ya huruma yake kutolipa kisasi kwa wazungu bali sababu ni kuwaachia wakoloni nguvu ya kiuchumi..jambo ambalo halijawahi kutokea dunianina hakuna kiongozi yeyote alowahi kufanya hivyo isipokuwa Mandela. was he right or wrong - hilo sijui bali ni ktk Exploration of reality!
Hakutakiwa kufanya lolote zaidi ya alichofanya na ndivyo alivyoandikiwa na amevikwa sifa nyingi za utukufu na kadhalika afanye nini zaidi?..
Nachosema mimi ni kwamba Mandela hasifiwi kwa sababu ya huruma yake kutolipa kisasi kwa wazungu bali sababu ni kuwaachia wakoloni nguvu ya kiuchumi..jambo ambalo halijawahi kutokea dunianina hakuna kiongozi yeyote alowahi kufanya hivyo isipokuwa Mandela. was he right or wrong - hilo sijui bali ni ktk Exploration of reality!
Mkuu Mkandara tatizo la SA halikuwa ukoloni kama historia inavyosema.

Tatizo lilikuwa ubaguzi wa rangi 'Apartheid'
Kuachiwa kwa mandela au kuapishwa kuwa rais hakukuhusu ulokolini, ilikuwa kumaliza kipindi cha ubaguzi.

Ni kutokana na kumaliza ubaguzi Mandela is revered by common south Africans from the village to the city.
Katika vyama vyote hakuna kilichokuwa kinapigania uhuru, vyote vilikuwa vinapinga ubaguzi wa rangi.

PAC ya Sobukwe iliamini katika Uafrika (Nationalist) ambayo Mandela na Lembede kwanza waliamini hivyo.
Miaka ya 1950 Mandela alishindwa katika kura ya Natioanlist vs democratic ideas.

Marafiki wengi wa Mandela walikuwa kutoka katika mchanganyiko wa rangi, tena wengine wakiwa na mchango mkubwa sana. Ahmed Kathrada ni Mhindi na alifungwa na Mandela. Wapo Wayahudi, Wazungu n.k waliopinga ubaguzi wa rangi

Freedom Charter ya mwaka 1956 ilieleza wazi tatizo la SA na haikuzungumzia ukoloni.
Iliongelea rainbow coalition kwasababu ubaguzi uligusa kila rangi kwa namna moja hadi nyingine.

Makaburu waiofika miaka ya 1600 ni raia wa Afrika kusini kama wengine.
Ukiangalia historia makabila mengi yalihamia na kabila la awali lilikuwa khoikhoi.

Hakuna justification ya kuwafukuza wazungu weupe kwa kutumia mwamvuli wa ukoloni.
Hakukuwa na ukoloni kwa maana ya def ya ukoloni. Kilichokuwepo ni ubaguzi wa rangi tena ukiwa official.

Sifa za Mandela ni pale alipoamini kuwa taifa litabadilika weusi wakipata fursa sawa.
Hakuwahi ku denounce harakati na hata alipopewa offer ya kutolewa ili aachane na siasa alikataa.

Ilipotokea fursa ya international pressure and support, Mandela alitoka akijua hiyo ilikuwa window of opportunity ya weusi kuchukua nchi yao. Na ndivyo ilivyotokea baada ya uchaguzi.

Changamoto ya kwanza ya Mandela ilikuwa kulileta taifa lililogawanyika katika misingi ya ukabila na rangi kwa pamoja.
Upande mmoja alipambana na Inkhata waliaoamini katika uchifu zaidi badala ya ubaguzi na upande mwingine weupe ambao SA ni kwao na ambao walikuwa wanakabiliwa na 'death sentence' endapo Mandela angekuwa na feeling kama za Mkandara.

Pili, ilikuwa ni kubadilisha sheria bila kuleta mtafaruku ambao ungeliingiza taifa katika mzozo mwingine wa umwagaji wa damu.

Tatu, ilikuwa kuwawezesha wazawa kujitawala na kujiendeleza kielimu baada ya kutumia muda mwingi katika kufikiria vita. Hadi sasa madhara ya vita na mentality ya vurugu vinaonekana wazi SA.
Mandela akapitisha sheria za ardhi, elimu na skilled development act.

Upo ushahidi wa takwimu kuonyesha kupungua kwa umasikini, kuongezeka kwa elimu na kipato cha mwananchi tangu ubaguzi ukomeshwe. Data hizo zimetoka SA kwenyewe na nitazitafuta niziweke ili tuone trend iliyokuwepo.

Of course watu walitegemea maajabu katika miaka 5 bila kujiuliza Tanzania katika miaka 50 iliyopita ikiwa haina vita, ubaguzi au chochote kwanini iwe na umasikini mkubwa kuliko ule wa SA kwa mujibu wa takwimu za UN.

Mandela hakuwepo ili kujenga nyumba au kupeleka mtoto wa mtu shuleni asubuhi, alichokifanya ni kujenga mazingira ya kuelewana kwanza kama taifa, kulileta pamoja na kuweka misingi ya kuendelea mbele.
Katika kufanya hivyo alisamehe wabaya wake wote wakiwemo waliompinga kama Inkhata ya Buthelezi.

Mandela alionyesha kuwa nchi haijengwi kwa vurugu inajengwa kwa maelewano.
Aliongoza kwa kuangalia mifano ya Tanzania na Zimbabwe ambayo tumekuuliza je ni role model ambayo Mandela angepaswa kuifuata katika ardhi?
 
Last edited by a moderator:
Zakumi nakubaliana nawe kuhusu umaarufu wa Mandela ndani ya Afrika kusini, ndio maana nilisema halikuwa suala la vyombo vya habari vya magharibi, in fact vya Afrika viliandika na kuzungumzia sana kuhusu Mandela.

Pili, nimejadili mzozo uliokuwepo kati ya Zulu na makabila mengine. Kama ulivyosema wazulu walitaka uchifu uendelee na hata kufikia kuunga mkono weupe kwasababu tu walikuwa wanatambua uchifu wao. Waliwatumia sana kuleta machafuko kati ya ANC na IFP cha Buthelezi.

Mandela alipokuwa rais alimkaribisha Burhelezi kama waziri wa mambo ya ndani.
Katika kumbu kumbu Mongusto Buthelezi amekaimu nafasi ya urais di chini ya mara 10 Mandela aliposafiri.
Hiki kitendo hakikuwa popular kwa ANC hardliners waliosema Buthelezi alikuwa kibaraka na kumwalika meza moja ilikuwa kusaliti damu ya wapigania uhuru.

Kuhusu suala la ardhi, nalo pia umeligusia vizuri sana. Sisi tunasema Mandela hakuwasaidia wazawa kupata ardhi.
Tunasahau ukweli kuwa alianza kwa kufanya marekebisho ya sheria ya ardhi ya Native land act ya mwaka 1913 ili weusi walionyang'anywa ardhi wafidiwe. Si kuwa wafidiwe bali wengine walirejeshewa maeneo yao.
Hilo lilifanyika kwa sheria ya restitution act ya mwaka 1994 iliyofanyiwa maboresho mwaka 1996.

Mandela hakutaka kuwanyag'anya ardhi wazungu kwa kuangalia mifano michache ya Tanzania na Zimbabwe ambapo zoezi hilo lilifanyika kisiasa zaidi ya kiuchumi. Matokeo yake ardhi ikatolewa kwa watu wasio na ufahamu wala ujuzi wa kuiendeleza. Mandela aliona ni vema atengeneze sheria ya kuendeleza wazawa kwanza (skilled development act) ili wakati ukifika wamiliki walicho nacho kwa ufundi.

Leo Watanzania wanasema Mandela hajafanya la maana kuhusu ardhi wakati Watanzania hao hao waliomilikishwa ardhi miaka 40 iliyopita wanaalika makaburu kuja kufanya investment katika ardhi.

Inasikitisha kuona tuna mng'ong'a Mandela afukuze watu wake ili sisi tuwape kile tulichomwambia Mandela amefanya kosa. Huu kama si unafiki ni ujuha ulioselelea na unahitaji rebuke ya hali ya juu.

Nimewauliza wachangiaji, Mandela alipaswa kufanya nini hasa kuhusu ardhi, hakuna jibu.


Nguruv3;

Sikujibu posti yako mapema kuachia wakina Mkandara nafasi kwanza. Wakati wa uhuru wa Msumbiji, wazungu zaidi ya 200,000 walikimbia Msumbiji. Hii pekee yake iliacha pengo kubwa wakati Samora amechukua nchi. Huwezi kuendesha nchi bila kuwa na technocrats. Na hili lilikuwa ni pigo kubwa kwa Msumbiji.

Miaka ya mwisho wa utawala wa wazungu nchini Zimbabwe, Robert Mugabe alikataa majadiliano na wazungu. Mugabe alitakaa kupata ushindi wa kivita. Alitaka uhuru upatikane kwa ushindi wa kijeshi na alitaka aingie Salisbury (Harare) akiongoza gwaride la ushindi wa kijeshi na wazungu kusalim amri.

Samora akamlazimisha Mugabe aende Uingereza na asaini mkataba wa uhuru. Na akamwambia kuwa kama hataki, basi serikali ya Msumbiji itafunga kambi za majeshi ya ukombozi wa Zimbabwe. Na uhuru wa Zimbabwe ulipopatikana, Nyerere alimwambia Mugabe "You have inherited a jewel, Keep it that way.”

Ukisoma jinsi Samora alivyomshinikiza Mugabe na Nyerere alivyomshauri Mugabe, utaona kuwa msimamo wa Mandela ulikuwa hauna tofauti na viongozi waliokubali kuwa transformations zao za kumwezesha mwafrika mweusi zilikuwa na makosa.
 
Zakumi,
hiyo historia uloisema kuhusu Mandela sii ya kweli na ndivyo ANC walivyotaka watu waelewe. Kifupi Hotuba ya JK majuzi huko South ndio imewafumbua macho wetu wengi kwa sababu ilikuwa siti kubwa sana na viongozi wengi sana hasa wazungu walishtuka waliposikia kwamba Mandela alipoondoka South alikuja Tanzania kupitia mpaka wa Mbeya na ndipo MK ilipozaliwa rasmi.

Hawa wazungu na wajuha wengine walivyoambiwa ni kwamba Mandela alikimbilia Botswana na kutoka huko alipenda ndege kwenda Tunisia ambako ndiko alipata mafunzo ya Kijeshi., Unajua vizuri kwamba Tunisia ndio nchi ya kwanza Afrika kuwa huru kabla kabisa ya Ghana. Na waliamini kabisa kwamba Mandela na MK walipata mafunzo ya Kijeshi Ethiopia na kadhalika wakati sisi tunajua fika kwamba kambi za MK zilikuwa Tanzania na hawa jama walipewa haki zote sawa na sisi. Walisoma hadi chuo kikuuu bure na wengine wamebeba passport zetu hadi leo.

Hotuba ya JK ilikuwa kuwakumbusha na wengine kuwajulisha kitu ambacho walifichwa kwa muda mrefu. Tanzania tumeionyesha dunia kwamba huyo Mandela alokuwa akiitwa terrorist hadi mwaka 2008 akiwa ktk list ya magaidi tulikuwa naye toka mwanzo. kambi za Materrorist zilikuwa kwetu na sisi ndio sponsors wakubwa wa mapinduzi ya kusini mwa Afrika.. Nina hakika kuanzia sasa Wasouth watatupa heshima zetu ipaswavyo. maana sio siri tena.

Mandela hakuwa na choice isipokuwa alibadilika alipokuwa Jela.Alipotoka jela yule Mandela waliyemjua kabla ya kwenda Jela hakuwa yule tena maana tayari walikwisha mlisha sumu na kumweka sawa. Alikuwa wakiletewa habari za Winnie Jela kwamba jamaa bwana mdogo ana perfomr kipapi chake wakati mzee Alisha oza kimapenzi na mengine mengi tu. He had the choice kufuata wengine ama kuendelea na mkataba ulomtoa Jela kwa kuahidiwa Urais kwa malipo ya kutotaifisha mali za wazungu.

Kisha mkuu wangu usiifanye Jela kuwa kitu cha maana saana.. Nina rafiki yangu anaoza Jela kwa kuuza unga. Sasa hivi anatumikia kifungo cha miaka 20 hii mara ya pili sijui tatu.. Maisha yake nijela tu toka akiwa na miaka 19 kwa biashara ya unga!. Kuna cha kujivunia hapo? au tunajivunia mafanikio ya jitihada na msimamo wa mtu ktk kuitafuta haki iwe ya watu ama kiuchumi..


Alipokuja Tanzania mwaka 1990 hakuwa na sababu ya kuonyeshwa bali anajua vizuri kwamba wananchi wetu ndio wamiliki wa ardhi yetu. haijalishi tunaitumia vipi ni YETU kama mama mwenye kibanda cha vyumba sita Kariakoo... huyu mama ana Nyumba YAKE, mali yake wakati mimi na wewe kina Mandela tumepanga uhindini huwezi kumsema hovyo mama huyu ila kujitazama sisi wenyewe kwanza - TUNA NINI?

Hivyo wewe nambie hao Wasouth alowakomboa wana nini?

Mkandara;

Tatizo lako unataka watanzania wawaandikie wasauzi historia yao. Msaada wa Tanzania ni mkubwa lakini hautoi fursa ya Tanzania kufanya hivyo. Nimeangalia shughuli za mazishi na sikuona kuwa wasauzi wana kinyongo na Mandela. Kama nchi za magharibi zinampa sifa Mandela, watu wake wanampa mara 1000 moja ya hizo. Kitu gani zaidi unataka?

Katika kipindi cha miaka mitano ya mwanzo wa utawala wake, Nyerere hakubalidisha chochote katika masuala ya kiuchumi. Hivyo sioni sababu ya wewe kumlaumu Mandela wakati alikaa madarakani miaka mitano tu?

Kuhusiana na jela, hujawahi kukaa jela. Hivyo huwezi kusema kuwa kukaa jela sio big deal. Rafiki yako ni thug na huwezi kulinganisha kukaa kwake jela na kifungo cha Mandela.

Mandela anastahili sifa zote anazopewa. Tatizo lako kila anaposifiwa Mandela, unaona anasifiwa zaidi kuliko Nyerere.
 
Back
Top Bottom