Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Mkuu kuna mambo yanayotokea ambayo huko nyuma ima hayakuangaliwa, au yaliangaliwa ''for granted'' kwa kuangalia ukubwa wa ofisi n.k.

Katiba imetenga mihimili kwa uwazi, executive, Judicial and Legislative.(co equal branches of government). Kwa mantiki hiyo Rais anaondolewa madarakani kwa njia ya impeachment tu

Impeachment ni utaratibu mgumu sana, kwamba, House itaandika article of impeachment kama inavyotokea sasa hivi.

Halafu article itapelekwa mbele ya senate kwa mjadala.
Kama kutakuwa na mashtaka kutokana na mijadala ya senate, atakaye preside ni Chief Justice

Ipo katika katiba kwamba lazima kupatikane 2/3 ya wajumbe wa senate ambao ni 99 na VP ili kumuondoa Rais.

Hilo liliwezekana zama hizo si kwa nyakati hizi ambapo senate imepoteza ile nguvu yake (inherent powers) kama tunavyoshuhudia sasa hivi.

Katiba haisemi kama Rais anaweza kushtakiwa akiwa madarakani. Watalaam wanasema ingalikuwa haiwezekani basi walioandika katiba wangeweka kifungu cha'' immunity''

Kwa tafsri ya idara ya sheria imekubalika Rais akiwa madarakani hawezi kushtakiwa

Ieleweke kutoshtakiwa ''is not enshrined in the constitution '' ni legal opinion kutoka DOJ na OLC

Kitu kikiwa ''enshrine'' katika katiba hakiwezi kukwepeka, ni andiko lisilo na utata wa kisheria

Ni kwa msingi huo, Robert Mueller akifikisha uchunguzi wa Russia alisema katika kamati ya Bunge kwamba hawakuweza kumshtaki Rais Trump kutokana na ukweli kuwa Rais aliye madarakani hawezi kushtakiwa kama DOJ inavyosema

Alipoulizwa endapo anaweza kushtakiwa baada ya kumaliza muda wake, Mueller alisema ''Yes''

Swali hilo aliulizwa na Nadler mwenyekiti wa kamati ya sheria ya House kwa sasa

Baadhi ya wasomi wanasema kuna utata katiba haikusema hivyo kwahiyo ni suala lililobaki wazi

Wengi wa Wasomi wa sheria wanakubaliana na maoni ya Mueller kwamba anaweza kushtakiwa

Kitu kilichowazi ni kuwa Rais baada ya muda wake anaweza kushtakiwa kwa ''criminal'' kesi kwani muda huo anakuwa Raia na nguvu au kinga inakuwa haiopo.

Huo ndio msingi wa DOJ kusema Rais aliye madarakani hawezi kushtakiwa

Mkuu,
Rais hawezi kushtakiwa baada ya kustaafu?
Kama anakinga ya kutoshtakiwa akiwa madarakani, vipi akimaliza muda wake?
 
Mkuu, Rais hawezi kushtakiwa baada ya kustaafu? Kama anakinga ya kutoshtakiwa akiwa madarakani, vipi akimaliza muda wake?
Mkuu GM sijaona mahali katiba inasema hivyo, labda ipo!
Ndiyo maana nimekupa ''nadharia'' zinazojulikana

Unajua Rais Trump amekuja na vitu tofauti sana na watangulizi wake
Kuna ''tradition'' za WH ambazo Rais Trump anakwenda kinyume na hazikuanishwa

Kwa mfano moja ya makosa ya impeachment ni ''bribery'' au Rushwa.
''Framers'' wa katiba walilenga rushwa kwa maana yake.

Sasa Trump anapoomba quid pro quo kiujanja ujanja ni ngumu kwa upande wa kisheria
Angalia viongozi wa idara nyingine nyeti kama WH, wanaoongoza ni ''acting''

Mfano wapili, Framer walikusudia kwamba Rais ni mtu mwenye heshima na kauli za kuaminika
Leo Trump anamfahamu balozi Sondland, kesho anamkana hamjui, hilo linaingia wapi katika katiba?

Kubwa zaidi, Framers walijua co equal branches zitasuluhisha baadhi ya matatizo

Hawakufikiria kunaweza kutokea timu kama ya ''Republicans'' ya sasa ambayo ni loyal kwa Trump hata kama kunahitajika nguvu zao za kikatiba ''inherent powers''

Kitu walichofikiria hao Framers ni kuwapa wananchi nguvu, na nguvu hiyo ni kupitia House, Senate na WH. Haya yanayoendelea yatakuwa na gharama kwa namna yoyote iwe kwa GOP au Dems. Pia walifikiri kuwa na taasisi imara na hilo kwa sehemu kubwa linasaidia hali iliyopo
 
ANDIKO LA IMPEACHMENT LATIMIA, VIUNGANI DC KWAZIZIMA

TRUMP NI WA ''NNE'' KATIKA MLOLONGO

Ndani ya viunga vya DC mchakato wa kumshtaki Rais Trump unaendelea
Wiki hii wana taaluma na viongozi wa kambi zote walikuwa na mijadala kuhusu suala hilo

Ukweli upo wazi, Republicans wakihamisha magoli na pengine kuishiwa hoja kiasi cha kuomba mchakato usiharakishwe. Hoja za GOP takribani zote zimepatiwa majibu

Pamoja na hayo Rais Trump alipewa fursa ya kueleza binafsi au kupitia wanasheria wake kuhusu upande wa pili wa habari, Trump na WH wamekataa kushiriki

1. Mazungumzo ya simu na ile ''karatasi'' ya maongezi haikuonyesha popote Trump alipozungumzia rushwa Ukraine, isipokuwa uchunguzi wa Biden na mwanae

2. Balozi Gordon Sondland aliyeongea na Trump alikiri kuwepo kwa quid pro quo

3. Hakuna ushahidi wowote wa kwanini msaada ulizuiliwa

4. Rais Trump alikataa ''mashahidi' wake ambao ni watumishi wa WH na SoS kutoa ushahidi
Hawa wangesema wanachokijua, Trump anajua ilikuwa ni kaa la moto katika mfuko wa kanzu

5. Mchakato ulifanyika ''kisiri'', hoja ambayo imekufa baada ya mjadala kuwekwa hadharani
Kuwekwa siri ililenga mashahidi kutowasiliana na pia kuficha mambo nyeti kama yangekuwepo

Mijadala yote ilikuwa ni makusanyo ya ushahidi uliopatikana

Leo imetangazwa na kamati za House kuwa andiko la impeachment liendelee mbele

Kesho kamati ya sheria itapiga kura kabla ya andiko halijaenda mbele ya House

Andiko lina mashtaka 2, kuzuia bunge kufanya kazi zake kisheria ''obstruction of justice'' na pili matumizi mabaya ya ofisi ''abuse of office''. Kuna mjadala kama andiko litakuwa pana zaidi

Kwa mantiki hiyo, Rais Trump anakuwa wa ''nne'' baada ya Andre Johnson, Nixon aliyejiuzulu kabla ya impeachment na Clinton.

Katika kufunika mjadala na kuzuia maongezi, AG Barr mpambe wa Trump alitoa taarifa ya Inspector General wa DOJ kuhusu uchunguzi wa Russia.

Taarifa ilikuwa mbaya kwa Trump kwani imeeleza uchunguzi wa Russia ulikuwa halali, hakukuwa na lengo baya la kisiasa, hakukuwa na spying au treason kutoka Obama admin

IG alichoona ni maafisa wadogo wa FBI kufanya makosa ya kutofuata taratibu, kanuni au sheria
Hayo waliyafanya bila kuwahusisha wakuu wa FBI akina Comey

Kwa maneno mengine, viongozi wa FBI wako salama, kauli mbiu ya Russia Hoax imekufa, hoja ya Obama kufanya spying imeyeyuka, na kwamba hakukuwa na lengo ovu kwa namna yoyote

Taarifa hiyo imemuudhi bosi wa IG bwana Barr ambaye ni AG. Yaani bosi anakerwa na taarifa ya mtumishi wake na hivyo amepanga kuikataa. Hayo ni kama maagizo ya Trump

Wakati huo huo, ile kamati ya kuchunguza wachunguzi wa Russia nayo imekataa taarifa ya IG kabla ya kutoa taarifa yao. Kamati hiyo iliundwa na AG Barr kwa maelekezo ya Rais Trump

Baada ya IG kuua matumaini sasa wanamshambulia na kutegemea taarifa ya uchunguzi wao wanayoipika wenyewe kwa kumtumia Jaji waliyemteua wenyewe na wanayetaka atoe taarifa itakayowapendeza! Hiyo ndiyo US ya Trump!

Leo katika mkutano na wafuasi wake, Trump anawaeleza vitu vya kuchekesha tofauti na taarifa ya IG ambayo inatetewa na FBI Dir Cris Ray.

Trump anamshambulia Rais Obama licha ya ukweli kuwa IG amemteua yeye mwenyewe
Taarifa ya IG imesafisha Obama admin na FBI kwa ujumla

Hayo yakiendelea, ni kwamba baada ya andiko sasa ngoma inahamia katika Seneti ambako Republicans ndio wenye ukanda na tayari mipango ya kuua impeachment inasukwa

Tofauti inajitokeza, McConnel ambaye ni senate majority anataka machakato uishe haraka ili kuepuka maseneta wake kuingia katika rekodi ya kupiga kura.

Kura ni ngumu sana kwani lazima wamkumabatie Trump, lakini majimboni wataadhibiwa

Trump anataka mchakato wa TV ili kuhakikisha Republican wanajibu mapigo ya House

Kwa hali yoyote, House itapiga kura kwa kuegemea vyama ''partisan'' na seneti pia
Trump ameweza kuwaweka Republicans mfuko kiasi kwamba hawawezi kwenda kinyume

Kinachobaki ni kovu kwa Trump, kwamba ana impeachment na hilo litamweka mguu sawa akijua nchi ya Marekani sheria ni kwa kila mtu na kwamba nchi ni ya watu na si mtu

Tusemezane
 
ANDIKO LATUA NDANI YA HOUSE
SENATE WAKENGEUKA!

Mchakato wa kumshtaki Rais Trump unaingia hatua mpya leo kwa House kupiga kura

Andiko limeleta 'mzio' kwa Rais Trump kwa kumwandikia Spika barua ''ya aibu' kwa Rais wa US

Inategemewa kwa wingi wa Democrats andiko litathibitishwa na Donald Trump atakuwa Rais wa 3 wa Marekani kushtakiwa akiwafuata Andrew Johnson na Bill Clinton.

Ikumbukwe Rais Nixon aliachia ngazi kabla ya impeachment kukamilika ndani ya seneti

Kitakachofuata ni andiko kupelekwa mbele ya seneti kwa shtaka litakalosimamiwa na Jaji mkuu

Seneti ina Republicans 53 na Democrats 47.GOP ndio Majority na Dems ni Minority

Kiongozi wa Seneti ni Mitch McConnel ambaye bila haya wala soni na kinyume cha taratibu za seneti amesema wazi hawezi kufuata sera ya kutofungamana.

Yaani ataungana na White House katika mkakati wa kuua suala zima.

Rais Trump alitaka Republican waite mashahidi mbele ya TV kama ilivyokuwa kwa House.

Alitaka Joe Biden na Mwanae pamoja na Whistle Blower.

Wanasheria wa WH na baadhi ya maseneta kama Graham wanasema impeachment ipigiwe kura mara moja ili ife bila mjadala.

Wanaelewa hakuna utetezi,kuendelea kujadili kunachafua hali maseneta wata badili misimamo

Democrats wanasema mashahidi waitwe wakiwemo John Bolton, Pompeo, Mulvaney n.k

Wote hao wamezuliwa na Trump kutoa ushahidi,wamebeba mazito yanayoweza kuhitimisha muhula wa Trump mapema iwezekanavyo

Kwa hofu ya mashahidi hao, Rais Trump 'amechomoa' sasa anaungana na seneti kutaka mchakato mzima uuawe mapema iwezekanavyo.

Wanachotaka kufanya Republican ni kutumia wingi.

Kwanza, itabaidi 'simple majority'',kwamba inatakiwa maseneta 51 ili shtaka liendelee.

GOP wana namba kwani wapo 53. Kura iki[pigwa shtaka linaweza kwisha kabla ya mjadala

Ikiwa namba haitakuwa 51 maana yake shtaka litaendelea likisimamiwa na Jaji Mkuu.

Ili kumuondoa madarakani kunahitajika 2/3 ambayo ni sawa na maseneta 66 yaani 47 wa Democrats na 19 wa Republican.

Hilo halitawezekana kwani Trump amefanikiwa kuzifinyanga akili za Republican.
Wanamuogopa hata kusema uongo ili kumlinda, wanamuogopa sana

Kwa mantiki hiyo, kidonda atakachoishi nacho katika historia ni Impeachment kutoka House

Hakuna matarajio ya yoyote kwamba shtaka litamuondoa madarakani, si zama za GOP ya leo.

Ukweli upo wazi, kwamba hakuna utetezi wowote kwa Trump, ametenda na kuna ushahidi

Republican walidai kutendewa hujuma na House.
Sasa wana nafasi ya kuita mashahidi lakini wanakimbia mchakato.

Hili lina maana moja, kwamba kuendelea kujadili kunamtia Trump matatizo zaidi, suluhu ni kukata na kukimbia kwa kuua mchakato mzima.

Pamoja na yote, viungani DC kunaweza kutokea mauza uza yasiyotarajiwa na ile namba 51 ya kuua mashtaka haraka inaweza kutopatikana kirahisi. Ikitokea mchakato utaendelea.

Kama kuna kitu Republican na WH wasichokitaka ni mchakato kuendelea ndani ya seneti.

Hilo linaweza kufunua uchafu uliofichwa kwa kuwaleta mashahidi waliobeba siri vifuani.

Tusemezane
 
ANDIKO LAKAMILIKIA, RAIS TRUMP NA HISTORIA
ZOGO LAHAMIA SENATE, VUTA NI KUVUTE

Andiko la Impeachment limekamilika na kupigiwa kura.
Andiko limepita kwa uchama licha ya ushahidi na mazonge zonge mengine yaliyojitokeza.

Andiko limekamilisha sehemu tu ya historia kwa Rais Trump kuwa watatu kuwa impeached

Hili limetokea chini ya miaka 50 ya Uhuru wa Marekani wa miaka 200 likitanguliwa na la Bill Clinton na lile la Andre Johnson kabla.

Andiko la Nixon halikufika hatma kwa yeye kubwaga manyanga.

Kukamilika kwa andiko (article of impeachment) ni mwanzo wa mchakato wa safari nyingine

Kwamba sasa andiko linaenda ndani ya senate kwa mchakato wa mashtaka.

Kabla ya andiko kutimia, majority senate leader Mitch McConnel alitamka kuwa anashirikiana na wanasheria wa White House kuandaa mchakato.

Siku chache baadaye akasema hawezi kutochukua upande katika kusimamia suala hilo.

McConnel kama Republican wengine naye ameamua kuhujumu majukumu ya seneti
Kiapo cha sakata zima kinamtaka seneta asimamie haki

McConnel na GOP wanataka andiko liende seneti walipigie kura ya kulikataa haraka.
Hili litazuia seneti kuita mashahidi waliozuiliwa na Trump katika hatua zilizotangulia.

Spika Nancy Pelosi naye kasema hatapeleka andiko hadi Dems watakapojiridhisha kuwa mchakato utafuta taratibu zote ikiwemo kuita mashahidi waliokosekana hapo mwanzo

Hakuna sheria inayomtaka Spika kufikisha andiko katika seneti kwa muda maalumu.

GOP wanachukizwa na hatua ya Pelosi kwasababu walitaka suala hilo limalizike haraka

Hapa kuna karata zinazochezwa viungani DC.

Spika Pelosi anataka kutumia andiko kuwashinikiza GOP wakubaliane na mchakato wa kuita mashahidi waliobeba mazito vifuani na wanaoweza kuhitimisha safari ya Rais Trump

Kuzuia andiko kunamnyima Rais Trump fursa ya kudai ''amesafishwa''

Trump ni mzuri sana kwani anaweza kubadili hoja ukadhani mchakato ulianzia seneti tu

Katika hali hiyo ingawa Republican wanasema hawana cha kupoteza, ukweli , wanakereka kwani hoja iliyopo ni Rais Trump kuwa impeached na si kusafishwa na Seneti.

Kuna swali linaloulizwa, ikiwa Democrats wanajua GOP hawawezi kubadili msimamo na ndio walio wengi ndani ya seneti kwanini basi wameandika andiko hilo?

Democrats na kwa siri sana Republicans wanakubaliana na article kwasababu ni onyo kwa Rais wa Marekani aliyepo na ajaye, Marekani si shirika binafsi kama Trump organization.

Bila kujali matokeo ya mchakato au maudhui yake, kuna la kujifunza.

Kwamba, kwa wenzetu vyombo kama Bunge huweza kutenda bila shinikizo na kwamba siasa za DC ni timing na mahesabu.Ni ukuu wa Demokrasia iliyokomaa hakuna aliye juu ya sheria

Tusemezane
 
Katiba ya Marekani ilindikwa mwaka 1789, halafu imekuwa inafanyiwa mabadiliko madogo madogo madogo (Ammendments) kiasi kuwa mpaka leo hii baada ya miaka 230 kuna mabadiliko 27 tu ambapo ammendment ya mwisho iliyohusu mishahara ya wabunge ilichukua zaid ya miaka 200 kukubaliwa. Katiba hii ni ya kizamani na kama Marekani inataka kuendelea kuwa taifa lenye nguvu na ushawishi duniani itabidi wabadili katiba yao kwa kiwango kikubwa sana kuendana na wakati:
(a) Mahakama imekuwa siyo neutral tena kama ilivyotegemewa, kwa hiyo mahakimu na majaji wote wawe na term limit. Nguvu kubwa inayomsapoti Trump ni kwa sababu yeye anateua mahakimu wa mlengo wao. Wako tayari Trump awalishe kinyesi mradi tu ateue mahakimu na majaji wa mlengo wao. Uteuzi wa mahakimu na majaji wa Marekani leo unafanywa na Federalist Society, Trump yeye anaweka mkono tu, ndiyo maana kuna wateule wengi walioonekana kuwa hawafai kufuatana na taaluma ya sheria lakini wamepita tu
(b)Bunduki kuuzwa kama peremende mitaani imekuwa ni janga linalosababisha mauaji ya kila siku. Ilipotoka Second Amendment mwaka 1791, Marekani haikuwa na jeshi la kitaifa, kwa hiyo ulinzi ulikuwa unafanywa na wanamgambo, na ndiyo maana wakaiweka kwenye katiba kuwa kila raia awe na bunduki kwa ajili ya ulinzi. Marekani ya mwaka 2019 ina jeshi la kisasa lenye matawi ya majini (US Navy), anga (US Air Force), ardhini (US Army), sehemu yoyote (US Seal) na sasa hivi jeshi la anga za juu (US Space force). Majimbo, wilaya, miji na taasisi mbalimbali zina polisi wake wenye vifaa vya kiasasa sama. Kwa hiyoi Marekani haihitaji Mgambo tena, jambo linalofanya Second Ammendement iwe batili kabisa
(c)Adhabu kwa kiongozi anayekikuka maadili ya majukumu yake isiwe ya kisiasa (Congress na Senate tu) bali iwe ya kiasiasa na kisheria (Congress,Senate + Mahakama)
 
Adhabu kwa kiongozi anayekikuka maadili ya majukumu yake isiwe ya kisiasa (Congress na Senate tu) bali iwe ya kiasiasa na kisheria (Congress,Senate + Mahakama)
Katiba ya Marekani ilikuwa na nia nzuri sana wakati wake lakini kwa sasa unaonekana kupitwa na wakati kama lengo ni kuwa na mamlaka inayosimamiwa na wananchi, we the people. Congress (House + Senate) kwa sasa imeonekana kupwaya katika kutimiza majukumu yake ya kulinda demokrasia na hivyo kutoa nafasi japo kiduchu kwa tawala za Kiimla.

Kinachoanza kuleta mtafaruku na kuharibu hali ya siasa Marekani ni chombo kinachoitwa Senate kwa sababu kuu mbili...
  1. Kinapingana na demokrasia kwani uwakilishi wake hauzingatii matakwa ya wananchi walio wengi
  2. Kinatoa mwanya kwa Rais wa nchi hiyo kushinda kwa idadi ndogo ya kura za wananchi wote (popular vote)
Kwa mfano tu...idadi ya watu kwenye jimbo la California inakaribia milioni arobaini (40,000,000) kiasi ambacho ni zaidi ya mara sitini (60 times) ya idadi ya watu jimboni Wyoming inayokaribia laki sita (600,000) tu. Hata hivyo jimbo la California lina wawakilishi wawili tu ndani ya Senate kama lilivyo jimbo dogo la Wyoming.

Kama vile kutia chumvi kwenye kidonda ni kwamba jimbo zima la Wyoming ina idadi ya watu wachache kuliko miji mikubwa 31 ndani ya majimbo makubwa kama California au New York. Rais wa sasa wa Marekani, kwa mfano, aliweza kuchaguliwa ingawa alipata idadi ndogo ya wapiga kura (popular vote) kuliko mpinzani wake.

Nina uhakika hili jambo linaweza kuleta mtafaruku ndani ya taifa hili huko mbele ya safari watakapoanza kujitokeza viongozi wengi kama wa sasa (populists). Pamoja na hilo ni wazi pia kuwa wajumbe wa Senate kutoka chama cha GOP walipigiwa kura na wachache kuliko wale wa Democrats ingawa ndio wengi ndani ya chombo hicho.

Hali hii inapingana kabisa na dhana zima la demokrasia na kuna siku sauti ya walio wengi itatamalaki na haitawezekana kutoisikiliza kwa kuziba masikio. Uzuri wa Marekani ni kwamba nguvu iko kwa mwananchi na funguo za milango ya uhuru wanazo wananchi iwe kwa moja moja, kwa pamoja au kwa makundi...ni swala la muda tu.

Kwa yanayoendelea hivi sasa ni wazi Marekani pia inahitaji mabadiliko makubwa. Nawaacha na kibwagizo hiki...
View attachment Crime-after-crime.mp4
 
Katiba ya Marekani ilikuwa na nia nzuri sana wakati wake lakini kwa sasa unaonekana kupitwa na wakati kama lengo ni kuwa na mamlaka inayosimamiwa na wananchi, we the people. Congress (House + Senate) kwa sasa imeonekana kupwaya katika kutimiza majukumu yake ya kulinda demokrasia na hivyo kutoa nafasi japo kiduchu kwa tawala za Kiimla.

Kinachoanza kuleta mtafaruku na kuharibu hali ya siasa Marekani ni chombo kinachoitwa Senate kwa sababu kuu mbili...
  1. Kinapingana na demokrasia kwani uwakilishi wake hauzingatii matakwa ya wananchi walio wengi
  2. Kinatoa mwanya kwa Rais wa nchi hiyo kushinda kwa idadi ndogo ya kura za wananchi wote (popular vote)
Kwa mfano tu...idadi ya watu kwenye jimbo la California inakaribia milioni arobaini (40,000,000) kiasi ambacho ni zaidi ya mara sitini (60 times) ya idadi ya watu jimboni Wyoming inayokaribia laki sita (600,000) tu. Hata hivyo jimbo la California lina wawakilishi wawili tu ndani ya Senate kama lilivyo jimbo dogo la Wyoming.

Kama vile kutia chumvi kwenye kidonda ni kwamba jimbo zima la Wyoming ina idadi ya watu wachache kuliko miji mikubwa 31 ndani ya majimbo makubwa kama California au New York. Rais wa sasa wa Marekani, kwa mfano, aliweza kuchaguliwa ingawa alipata idadi ndogo ya wapiga kura (popular vote) kuliko mpinzani wake.

Nina uhakika hili jambo linaweza kuleta mtafaruku ndani ya taifa hili huko mbele ya safari watakapoanza kujitokeza viongozi wengi kama wa sasa (populists). Pamoja na hilo ni wazi pia kuwa wajumbe wa Senate kutoka chama cha GOP walipigiwa kura na wachache kuliko wale wa Democrats ingawa ndio wengi ndani ya chombo hicho.

Hali hii inapingana kabisa na dhana zima la demokrasia na kuna siku sauti ya walio wengi itatamalaki na haitawezekana kutoisikiliza kwa kuziba masikio. Uzuri wa Marekani ni kwamba nguvu iko kwa mwananchi na funguo za milango ya uhuru wanazo wananchi iwe kwa moja moja, kwa pamoja au kwa makundi...ni swala la muda tu.

Kwa yanayoendelea hivi sasa ni wazi Marekani pia inahitaji mabadiliko makubwa. Nawaacha na kibwagizo hiki...
View attachment 1300654

Ni kweli; muundo a Senate ya Marekani unahitaji mabadiliko makubwa sana kwani Senate ina nguvu sana ya kuthibitisha uteuzi wowote unaofanywa na rais, na vile vile rais anaposhitakiwa ndiyo pia inayotoa hukumu lakini muundo wake unazipendelea sana state zenye watu wachache na kuzionea state zenye watu wengi. Njia rahisi ni kuweka weight kwenye kura za maseneta, yaani mfano kura ya seneta kutoka Wyoming inakuwa na uzito wa kura moja, wakati kura ya seneta wa California inakuwa na uzito wa kura kumi.
 
Wakuu Kichuguu na Mag3 ahsanteni kwa hoja mujarabu

Framers wa constitution walifikiria kulinda ''federation'' kwa kuangalia uwakilishi wa state

Rais wa Marekani anachaguliwa kwa delegates na si popular vote
House of representatives hupatikana kutokana na population ya state

Kutokana na hilo, ilionekana state zenye population kubwa zitakuwa na delegates wengi wa kumchagua Rais, na state hizo zitakuwa na House Rep wengi na kuathiri maamuzi ya ujumla

Ndipo hoja ya kila kila state ili ishiriki sawa katika utawala iwe na wajumbe sawa
Ndilo chimbuko la senate kuwa na nguvu kubwa katika baadhi ya maamuzi hasa teuzi za Rais.

Pili, Katiba ya Marekani ilisukwa katika kuhakikisha haichezewi cheziwi hovyo akitokea mwendawazimu au kama ilivyo katika third world.
Kwa bahati mbaya katiba hiyo haikutambua uwepo wa ''wandewazimu wenye akili''

Katiba iliweka chujio katika vyama na kwamba hadi kiongozi aingie WH atakuwa na decorum
Framers waliamini pia uwepo wa House na Senate unatosha kuzuia madhara mengine

Hata hivyo nakubaliana na Kichuguu kwamba katiba ilikuwa mufaka sana kwa nyakati zake
Mabadiliko ya dunia kwa ujumla yanalazimisha yawepo marejeo ili iendane na wakati.

Tayari kuna hoja ya popular vote kuwa mwamuzi wa Urais na si delegates wanaopatikana katika uwiano usio sawa kama alivyoonyesha Mag3.

Kwamba, Rais anaweza kupata delegate 270 kwa kuangalia;
California(55), New York(29), Texas(38), Ohio(19), Florida, Penny state(20), illinois(20), New Jersey(14), Indiana(11), Wisconsin(10), N.Carolina (15). Tennessee(11),Michigan(16),Arizona (11), Minesota(10), Vermont(3)

Utaona states 16 kati ya 50 zinaweza kumchagua Rais dhidi ya 34 zilizobaki

Hoja ya popular vote inarindima na sidhani itachukua muda electoral college utafutwa.

Tatu, hoja ya Gun haina utetezi kama alivyoeleza Kichuguu.
Tatizo ni NRA, wana nguvu sana za kuweka wagombea na kushinda katika House na Senate.

Hata kama Rais aliye madarakani atajaribu, hoja itakufa katika House au Senate kwani NRA wamewekeza sana huko.

Hata hivyo kwa matukio yanayoendelea, sidhani kama itachukua muda kwa second amendment kufanyiwa marejeo. Ni wazi wananchi wamechoshwa na hali ya ''mass shooting'' kila uchao
 
Nafuatilia mnakasha unoendelea ndani ya House of Representative sasa hivi na, duh! Wenzetu kweli wana uhuru wa maoni.
Kuna hila zinafanyika katika mifumo ya utoaji haki ndani ya Marekani. Hakuna uhuru hasa katika kutoa maoni kwenye mambo ya msingi. Flynn kakumbana na hilo, je vipi kuhusu raia wa kawaida wa Marekani!!
====

Flynn’s legal team specifically argues that Assistant U.S. Attorney Brandon Van Grack, who negotiated the plea deal, not only demanded the disgraced ex-adviser provides false testimony, but knew perfectly that what he wants Flynn to do was to lie to the authorities.

The document says that once Flynn changed his legal representative and refused to stand by the falsehoods he was forced to make, the prosecution moved to retaliate, including putting his son on the witness stand “solely to harass him and to raise the threat and anxiety of the family at this crucial time.”
 
VIUNGANI DC, ANDIKO LAHAMIA SENATE
NI ''TIMING '' KILA UPANDE

Andiko la Impeachment hatimaye limetua ndani ya senate ya yenye Republicans wengi

Andiko lilizuiliwa na Spika Pelosi akitaka kujua hatma yake na iwapo kutakuwa na ''fair trial''

Senate Majority McConnel alifanya kosa kwa kutangaza atachukua upande'' hatakuwa neutral'

Hilo likamlazimisha Spika Pelosi kuzuia andiko kwa wiki zaidi ya tatu.

Pelosi ni mjuvi wa siasa za viunga vikuu vya DC. Spika alifahamu White House imezuia watu na nyaraka kutumika katika kutoa ushahidi, na kwamba, Republicans walibaki na hoja hiyo.

Republicans walisema hakuna link ya Trump na Ukraine baada ya hoja zingine zote kutota.

Pelosi anafahamu viungani DC siku moja ni ndefu sana na inaweza kubadili mwelekeo.

Kauli ya McConnel ilimpa sababu tu, ukweli ni kuwa Pelosi alikuwa anavuta muda kwasababu;
1. Watu wengi waelewa ni kwanini kuna shtaka dhidi ya Rais kwani kuzuia nyaraka ni habari
2. Kutoa nafasi kwa Democrats kwenda kuweka presha katika majimbo ya maseneta wa GOP
3. Kuelewa kuwa lazima kuna nyaraka zitavuja kadri muda unavyosonga mbele.

Yote hayo amefanikiwa kwa kiasi kwani nyaraka zinazovuja kama zile za Lev Parnas zinawaweka Republicans katika wakati mgumu wa kuamua hatma yao au ya Trump

Ilikuwa wazi Republicans walitaka article of impeachment iende haraka ndani ya senate kwasababu zile zile za hapo juu. GOP walijua kusubiri andiko ni kama kusbiri dhahma.

Walichotaka ni kupiga kura ya haraka ya kumaliza impeachment bila kuita mashahidi na hivyo Trump ajinasibu 'ameshinda''

Mbinu ya Republicans imeingia wahka kwani walitegemea maseneta 51 dhidi ya 47.

Kwa kuchukua muda kuna hati hati ya maseneta 3 au 4 kuungana na Dems kutaka mashahidi

Ikiwa maseneta 4 wataungana na Dems, idadi ni 51 na azimio la kuita mashahidi litapita

Hapa watu kama Bolton, Mulvaney, Pompeo wataitwa.

Hii haitakuwa rahisi, Trump atatumia privilege ya Uraisi kuwazuia wasitoe ushahidi.

Ikitokea hivyo, mzigo utarudi kwa maseneta wa Republicans kueleza kwa wananchi nini kimejiri

Ikiwa maseneta 3 watungana na Dems, kutakuwa na 50/50 na kura ya Jaji mkuu itaamua.

Hili nalo ni gumu kwani katika historia imetokea mara 3 tu impeachment.
Kuna nadharia kuwa ikiwa ni 50/50 hoja ya kuita mashahidi itashindwa.

Ikiwa maseneta 2 wataungana na Dems, basi Republicans wataweza kuua hoja ya mashahidi.

Republicans hawataki kura ya mashahidi kwani inabaki katika kumbu kumbu kama kura ya vita ya Iraq inavyowaumiza Wagombea wa Dems wanaoutaka Urais.

Hapa ieleweke kura inayogombewa ni ya kuita mashahidi si ya kuamua hatma ya Trump.

Kura ya andiko kama aondolewe au la inahitaji 2/3 ambayo ni ngumu sana kuipata hasa kwa zama hizi ambazo Trump amewachukua GOP mfukoni mwake.

Sakata la malumbano ya kisheria linaanza Jumanne kwa pande zote mbili kuwasilisha hoja.

Hoja itakayoleta malumbano ni ya kuita mashahidi, ambayo inazidi kupata nguvu kila uchao.

Katika viunga vya DC siku moja ni ndefu sana na lolote laweza kutokea kati ya leo na Jumanne

Tusemezane
 
SENATE YAANZA MTIFUANO
REPUBLICANS WAKOMAA NA TRUMP

Andiko limeanza kujadiliwa ndani ya seneti. Kwaleo ilikuwa kurekebisha kanuni zilizoandikwa na Senate Majority McConnel kwa kushirikiana na White House.

Kanuni zinazogombewa ni kuhusu kuitwa kwa mashahidi na vielelezo mbele ya senate.

Mbele ya Jaji mkuu, pande zote zimefikisha na zinaendelea kufikisha hoja zao.

Kwa upande wa WH wanasheria wanataka mjadala uanze kisha kura ya endapo mashahidi wataitwa na vielelezo au la. Huu pia ni msimamo wa Republicans.

Hii ni mbinu ya kutaka kesi isikilizwe bila ushahidi ili GOP waseme hakuna kesi na hakuna haja ya kuita mashahidi. Hilo litapelekea upigaji wa kura na vyovyote vile utamnusuru Trump.

Sababu, lazima ipatikane 2/3 yaani GOP 20 Waungane na Dems ili Rais kuondolewa.

Kwa upande wa Democrats wanachotaka ni mashahidi na nyaraka ambazo kwa namna yoyote ile zitamweka Rais Trump katika wakati mgumu na hata maseneta wa GOP

Vielelezo vilivyotolewa na Dems na ushahidi kutoka House hauna chembe ya shaka mashahidi kama Bolton, Maulvanye, Mike Duff na Pompeo watabadili mwenendo

Maana yake, ushahidi utawalazimisha maseneta kuliona tatizo na hata kama wataamua kukomaa na Trump, kura hizo zitabaki donda ndugu mwaishani mwao.

Republicans hawataki ushahidi wala nyaraka, wanataka kulimaliza suala hili kwa kusema Rais amekuwa '' acquitted ' bila kusikiliza hoja yoyote ile.

Katika upigaji kura wa kanuni, kura ni 47 kwa 53 Republicans.

Hakuna uwezekano wa kupata maseneta 4 kutoka GOP kuwezesha kanuni kubadilishwa kama Dems wanavyotaka.

Kwa mantiki, andiko litajadiliwa kwa kutumia kanuni alizoandika McConnel na WH.

Katika wiki moja shauri litakuwa limekwisha kwani Republicans watapiga kura ya ku 'dismiss'' bila ushahidi wa mashahidi ya nyaraka na impeachment itakuwa imeishia hapo.

Dem wanajua hawana namba ya kuwashinda Republican.

Wanatumia fursa kujenga hoja za kuwashawishi wananchi kuna tatizo lakini Republicans wamekomaa na Trump.

Hili litakwenda hadi uchaguzi na wala halitaishia hapo.

Wapo maseneta watakaokwaza mbele ya mahakama ya wananchi.

Lakini pia kura wanazopiga zitabaki katika kumbu kumbu.

Hivi tunavyoongea kura za vita ya Iraq inawatafuna wagombea wa Dems, na hili linalofanyika Republicans watamsaidia Trump kwa muda na kubaki na donda maishani

Ndivyo pia kura House zitakavyohukumu pande zote muda ukifika

Kwa yanayoendelea ni wazi yakuwa ''precedent' kwa siku zijazo.

Ikiwa GOP watataka kumshtaki Rais wa Dems, mfano wa kinachotokea utajirudia.

Katika vitu Trump alivyofanikiwa ni kupoteza ile nguvu ya Demokrasia ya Marekani.
Ni mtu popular kiasi maseneta na House wanajua anachofanya lakini ni waoga kwake.

Tutaendelea kuwajuza kinachoendelea

Tusemezane
 
Katika vitu Trump alivyofanikiwa ni kupoteza ile nguvu ya Demokrasia ya Marekani.
Ni mtu popular kiasi maseneta na House wanajua anachofanya lakini ni waoga kwake.
Umadhubuti wa mfumo wa taasisi ya kidemokrasia unapotelea kwa umaarufu wa Mtu mmoja!? Kwa hiyo ni kweli kuna 1% ya watu wa Marekani inawanyonya 99% ya wenzao kiuchumi na hata kuamua masuala ya msingi ya kijamii ya wamarekani hawa wanyonge(99%). Na hiki ndiyo tunaambiwa tujivunze kwa wenzentu walio'endelea' !

Nilishasema huko nyuma kuwa siasa za nchi zenye nguvu kiuchumi hazitofautiani sana na zile za nchi zenye kukuza nguvu ya uchumi; tofuati ni ujanjaunjanja namna ya kughiribu ulimwengu kwa kutumia 'powerful MSM' kuwa kuna demokrasia kwenye nchi kama Marekani.
 
DEMS WAMALIZA NGWE , SASA NI GOP
Democrats wamemaliza ngwe yao ya kutoa mashtaka mbele ya seneti.
Mashtaka yao yalijikita katika matumiza mabaya ya ofisi na kuzuia Bunge kufanya kazi zake

Kupitia hayo mawili, Dems walijikita kutaka mashahidi waliozuiliwa na utawala la Trump waitwe mbele ya seneti kwa wito wa lazima ikiwa ni pamoja na kulazimisha utawala utoe nyaraka.

Mashtaka ya Dems yalilenga kuishawishi kukubaliana nao wakijenga hoja kwa vithibitisho pasi na shaka. Ilikuwa wazi Democrats walijiandaa na walijua wanafanya nini.

Lengo la Dems lilikuwa, kwanza, kuwaelewesha wananchi nini kilitokea na kupitia kwao washinikize maseneta wa GOP alau 4 ili kura ya kuita mashahidi na nyaraka itimie
Pili, kuwashinikiza na kuwaweka maseneta waliopo katika swing state kukubaliana nao.

Kwa kuangalia nyuma, utaona Spika Nancy Pelosi anajua mchezo wa Viungani DC kwa dhati.
Lengo lake la kutopeleka andiko mapema lilikuwa na mantiki nzuri kwa upande wa Dems
1. Kuvuta muda kwa kujua ushahidi zaidi utajitokeza viungani DC na hil limetimia
Mshirika wa Meya Rud Giuliani, Bw Parnas ametoa nyeti na anaendelea kuzitoa
2. Pelosi alitaka muda ili Democrats wapate muda wa kupanga hoja, nalo limefanikiwa

Kauli za Majority McConnel zilimsaidia sana Nancy kutafuta sababu. Nancy anaujua mchezo

Hoja za Dems hazipingiki kwa jinsi zilivyosheheni ushahidi. Hilo limewaacha Republicans wakisema hata wao wakiomba mashahidi na nyaraka bado Trump atakwenda mahakamani.

Wengine wanakubaliana kwamba ''uvunjaji wa sheria'' ulifanyika lakini si kiwango cha kuondoa Rais. Kwamba, wanakubaliana na mashtaka na ushahidi uliotolewa

Leo ilikuwa zamu ya utetezi wa WH ambao wametumia masaa 2 kwakujua Jumamosi hakuna anayeangalia TV kutokana na uchovu wa weekend. Wataendelea Jutatu na Jumanne.

Upande wa utetezi unataka shauri liishe kura ya kuita au kutoita mashahidi ifanyike wakijua ni ngumu hadi sasa kupata maseneta 4 kuungana na Dems.

Kura hiyo ikielekea upande wa GOP shtaka litafutwa, hakutakuwa na hoja ya kuendelea bila mashahidi. Utetezi unatumia namba ndani ya seneti na si hoja katika sakata zima.

Hoja zilizotolewa dhidi ya Trump hazilingani na tuhuma za Nixon kiasi cha kuonekana kuwa Nixon ''alionewa ''

Swali wanalojiuliza watu, ikiwa hakukuwepo na uhalifu kwanini nyaraka zimefichwa na watu wanazuiliwa na utawala kutoa ushahidi ambao huenda ungemsamehe Trump?

Tusemezane
 
NGWE YA GOP NA UTETEZI
''SIKU MOJA YA SIASA NI SAWA NA MWAKA''

Republicans wameanza utetezi kuhusu shtaka linalmhusu Rais Trump.

Ilitegemewa ushahidi ujikite katika kubomoa hoja za Dems, kinyume chake kinachofanyika ni kuchomeka tuhuma kuanzia Rais Obama na wengine

Wanasheria mashuhuri wa katiba wanaomtetea Rais Trump wamelamba matapishi yao.

Hawa ni Ken Starr aliyemshtaki Rais Trump na Prof Alan Dershwitz.
Wote kwa pamoja wanakwenda kinyume na misimamo yao nyakati za tuhuma za Clinton

Kinachojitokeza ni kutafuta utetezi ambao kisheria ni haki kwa wanasheria wa utetezi kwa kuweka chochote ili kubadili mwelekeo wa maseneta.

Lengo ni kuhakikisha hakuna seneta wa GOP atakayeunga mkono hoja ya kuita mashahidi.

Hili litakuwa na maana moja, shtaka na andiko litapigiwa kura na kumnusuru Trump

WH na Republicans wanaogopa mashahidi.

Kama tulivyowahi kusema huko nyuma, siku moja katika siasa za viunga vya DC ni sawa na mwaka mzima kwani lolote linaweza kujitokeza.

Jana, aliyekuwa mshauri wa ulinzi wa Trump bwana John Bolton anayeandika kitabu baadhi ya maandiko yake yamewekwa wazi.

Bolton anasema ''leak'' hakujua imetokea wapi ingawa hajakanusha maudhui au kuyakubali.

Hili limeongeza wasi wasi ndani ya kambi ya Trump kwasababu maseneta wameonyesha kuchukizwa na jinsi walivyofichwa na WH.

Trump na WH walijua uwepo wa nyaraka bila kuwataarifu maseneta, kujikuta wakiweweseka

Bolton anasema aliambiwa na Rais asitoe pesa za Ukraine hadi wamchunguze Biden.

Huyu ni shahidi anayeua hoja ya GOP ''hakuna aliyepewa maagizo na Rais''

Bolton anaua hoja nyingine kwamba, kulikuwa na quid pro quo.

Bolton ni shahidi anayetakiwa sana na Democrats kwani , kwanza, hayupo WH, pili ni mshauri wa Rais wa Usalama,anajua kuhusu Ukraine na tatu alisikia maagizo ya Rais.

Kwa namna yoyote ile WH na Wanasheria wa Trump hakuna anayetaka shahidi.

Wanajua Rais Trump alitenda na mashahidi wanaweza kubadili mwelekeo wa seneti.

Katika hesabu za GOP, walitaka andiko liende seneti haraka.

Sababu kubwa ilikuwa kuzuia uharibifu unaoweza kujitokeza hasa kwa kujua siasa za viungani ni za ''timing'' na zinahitaji wajuvi waliobobea kama Spika Nancy Pelosi.

Kuna pressure kubwa sana katika kambi ya Republicans, katika kusimamia ukweli au kumlinda Trump. Kwa namna zozote hakuna chaguo rahisi kati ya hayo mawili.

Kesho itakuja na nini kutoka viunga vikuu vya DC?

Siku ya pili ni kesho, tutawajuza nini kinaendelea

Tusemezane
 
KURA YAPIGWA, TRUMP ATAKUWA 'ACQUITTAL'

Acquittal ni neno linalomsafisha mtu kutoka katika tuhuma za 'uhalifu''
Seneti imepiga kura ya kuzuia mashahidi wasiotoe ushuhuda au kupokea nyaraka zozote

Kura ilikuwa 49 kwa 51 Republicans ikimaanisha kuwa maseneta 2 wa GOP waliungana na Democrats kutaka mashahidi na nyaraka, hata hivyo Republicans wamefanikiwa kuzuia.

Hii maana yake ni kuwa baada ya majadiliano ya wanasheria wa WH na mameneja wa mashtaka kutoka House kulambana kwa masaa 24 kwa kugawana.

Kanuni za seneti zilitengenezwa na Mitchel McConne ambaye ni kiongozi wa majority kutoka chama cha Trump Republicans. McConnel aliweka kipengele cha kuzuia kura makusudi kabisa ili kuhakikisha hakuna shahidi wala nyaraka ya ziada

Licha ya mashahidi 17 kutoa ushuhuda wakiwa ni maafisa wa Trump nje ya WH, Trump alizuia mashahidi waliokuwa WH na nyaraka ambao mmoja wao ni John Bolton, mshauri wa usalama

Kuwazuia na kuzuia nyaraka ilikuwa kuficha ushahidi. Bolton alikuwa tayari kutoa ushahidi baada ya mswada wa kitabu chakekuvuja kwamba Rais alitoa maagizo.

Kwa wanaofuatilia ni wazi pasi na shaka kuwa Trump alitenda kosa la kuzuia msaada kwa Ukraine ili kudhuru Joe Biden ambaye kura zote za maoni zinaonyesha kumshinda

Hivyo, hakutakuwa na kesi tena bali kura ya acquittal kwa Trump.

Wanasheria wa Trump hawakujibu hoja zaidi ya kutoa utetezi ambao hata maseneta wa GOP baadhi wamekiri kutendwa kwa kosa.

Kilichowasukuma GOP kupiga kura ya kukataa mashahidi na nyaraka ni hofu dhidi ya Trump.
Kwamba Trump anawatisha kiasi cha kumuogopa na si kuogopa katiba.

Kutakuwa na majadiliano ya maseneta kukamilisha taratibu na kura ya jumatano ni kukamilisha hatua ya mwisho ya kumsafisha Trump kupitia maseneta wa GOP.

Kura ya leo ni muhimu sana. Takribani asilimia 75 ya Wamarekani walitaka mashahidi na nyaraka ili mashtaka yafanyike kwa haki. Miongoni mwa hao 49% ni Republicans na baadhi ni independents.

Kura ya leo itampa ushindi Trump kwamba amesafishwa, hata hivyo maseneta watabaki na kura hiyo maishani mwao. Wale wenye kiu ya Urais na Useneta

Swali litakalowaandama ni moja, mashtaka yanaendeshwa vipi bila mashahidi na nyaraka?
Kwamba Trump amesafishwa kwa mashtaka yapi na kwa mwenendo upi wa kesi?

Hatua moja imakamilika na kama tulivyosema andiko la impeachment limefikia hatma yake.
Ilikuwa wazi Trump asingeweza kuondolewa madarakani kwa maseneta 60 kumkataa
Hilo tulisema siku nyingi na hesabu zilikuwa wazi.

Kinachoshughulisha akili za watu viungani DC ni namna mashtaka yalivyoendeshwa kihuni.
Kwamba kuna kesi bila mashahidi wala nyaraka.

Ulikuwepo uwezekano wa kuita mashahidi na bado ikakosekana namba ya kumuondoa.

Kwasasa suala zima litarudi katika viwanja vya siasa za uchaguzi.

Kuna watakaolipa gharama kubwa kwa kura ya leo

Tusemezane
 
====
IOWA Imewaumbua Democrats.
********

Ms. Pelosi can not handle it. Ha ha haa! These americans are going nut now! This is not funny at all! Na hapa Trump ndiyo anapita kiulaini 2020!
====

Nasubiri uchambuzi makini wa masuala haya mawili.
 
Back
Top Bottom