Ushahidi wa dalili hizi huu hapa chini, ingawa chanzo cha ushahidi kinaweza kuwa kero kwa baadhi yenu lakini huo ndiyo ukweli.
>>>
China beats US in key patents to secure technological dominance – report
Labda nirejee, naona huelewi tatizo lako na nini tunachosema hapa.
Hakuna tatizo kujadili kwa mtazamo tofauti. Hakuna mtu anaye miliki ''facts'' na ni haki kupinga kwa hoja zenye mantiki na weledi na si kupinga tu kwa kuokota unachodhani ni sahihi bila kuchambua, ilimradi kinakupendeza.
Mfano mzuri ni wa bandiko lako ambapo unachukua ''analysis' ya mtu na kuiita ushahidi.
Kwamba, yoyote anayeandika kwako ni facts na ni ushahidi.
Pili, ungelijua siasa za dunia hii usingevamia tu vitu.
Katika kitu kinachoitwa geopolitics Russia ni adversary and Foe kwa United states.
Tangu Trump ameingia madarakani Russia kwa kupitia vyombo vyake kama RT vimefanya kazi nzuri kwa Taifa lao kwa kugeuza propaganda kiasi cha Rais wa Marekani kuvidharau vyombo vyake kama ilivotokea ''Helsinki'
Kwahiyo, unaposoama habari za RT lazima uelewe zinatoka wapi, zinalenga nini na kwanini.
Russia ndiyo waliogeuza suala la Ukraine kwamba ni Ukraine iliyoingilia uchaguzi 2016 na server ya DNC ilikuwa Ukraine. Intelligence za US zimekataa ujinga huo isipokuwa mtu mmoja .
Katika sakata la Impeachment wateuliwa wa Trump walisimama na kukanusha kuhusu Ukraine, ilikuwa wazi.
Hivi tunavyoandika jitihada za AG Barr kuhusu uchuguzi wa Wachunguzi wa ''Russian'' unaongozwa na Jaji aliyeteuliwa na Barr , Jaji Durham unapingwa na Intel community na kwamba ni njama chafu tu.
RT wanasubiri habari ya Durham ili waweze kufanya spinning zao. Hayo sijui kama unayajua
Ili kuhakikisha wanakwepa ukweli wa Intel community, Barr amemteua prosecutor kuchunguza waliochunguza Russia. Hii nayo sijui kama umewahi kuiona kupitia RT ambao kwao ni habari kubwa.
RT wakasema kuhusu Iran na US jambo ulilolileta hapa jamvini. Tulikaa kimya tukiendelea kusoma ''low''
Ulisema hivi '' US walizima radar baada ya kubaini Iran inajiandaa kurusha makombora''
Hii ni crap! hivi kama walijua hilo walikuwa na sababu gani za kuzima radar? Logic tu bila kusubiri maelezo inatosha kukupa picha. Kwavile siasa za dunia bado ni changa, uliona ni jambo la maana sana kulileta hapa
Ni hivi, lazima uzielewe siasa na kujua maana ya 'opinion, analysis na facts''
Tukirudi kwa hoja ulizoelekeza kwa
Mag3 , kwamba Marekani itazidiwa baada ya miaka 20, sina uhakika kama unaijua historia ya Taifa hilo.
Marekani imepita vipindi vingi vigumu ndani na nje.
Kuanzishwa kwa Bretton woods na uwepo wa new world order na NATO ulitokana na upinzani dhidi ya US
Ilichukua miaka 40 kwa US kumaliza cold War na hakuna aliyejua. Wakati huo akina Brezhnev na Gorbachev walikuwa wakiona ukaribu wao kiushindani na US. Mwisho wa siku wakajikuta hawana USSR
Nimalizie kwa kusema, sote tunasoma habari na kuzitafakari, tatizo ni pale unapovuruga mjadala kwa u 'simba na u-Yanga'' badala ya kusaidia wasomaji kuelewa mambo ambayo si kawaida kuyasikia katika mijadala
Ni pale unaposoma habari na kutafuta ''spelling error'' ukiwa huna lolote la kueleza kama mbadala
Hata hivyo u-simba na u-yanga huo kama unatoa tija si tatizo, lakini unapofikia kiwango 'low'' inatia kinyaa
Kiwango low kama hadithi za mitaani za US kuzima radar isione makombora ya Iran, it is unfortunate!