Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #21
Nilikuwa nazirejea nyuzi na kukumbana na maoni mengi. Moja ya hoja zinazosemwa sasa hivi ni kumuondoa Zitto katika mkakati wa waraka na kumwacha Kitila mwenyewe. Ndugu yangu The big show amesema zito hahusiki. Nasema inawezekana hahusiki lakini katajwa. Kutajwa si kuhusika sasa swali linakuja, ni lini waraka huo umeandikwa? Kuna tarehe inayoonyesha hapo?
Ushahidi wa kimazingira unaonyesha waraka ni muda mrefu kidogo.
Ukiusoma kuna sehemu inasema
Sina shaka mawasiliano yalishafanyika na kilichokuwa kinaendelea ni utekelezaji.
Kuna hoja kuwa Zitto ameundiwa Zengwe.
Kwakuhusishwa na waraka huu kama mhusika mkuu na ushahidi wa kimazingira ni wazi alishiriki.
Hata hivyo watetezi wake pamoja na yeye mwenyewe hawajaeleza ushiriki wake katika kundi la Kafulila, Sakata la M7 na wala hakukanusha kuhusika na waraka.
Katika kujenga hoja hafifu watetezi wa Zitto wanasema Mzee Edwin Mtei ndiye tatizo, wengine wakifumba macho na kusema hakuhusika na waraka.
Wanachoshindwa kukisoma katika utetezi wake mwenye (Zitto) ni hiki
Wapo wanaodai kuwa suala la ukaguzi wa fedha ndicho chanzo na wameligeuza kama ndio hoja.
Wamesahau kuwa waraka uliopo unamtia Zitto matatani.
Tatizo walililofanya akina Zitto na Mkumbo si kuandika waraka. Waraka unaweza kuandikwa na mtu yoyote yule.
Tatizo ni aina gani ya waraka, ulikusudia nini ili kuleta nini na kwa akina nani.
Waraka ulikusudia kuleta mapinduzi (coup d'etat). Nisingeona ajabu kama hilo lingetokea TLP.
Kwa chama kinachojinasibu ni cha kidemokrasia hilo halifai kutamka achilia mbali kuliandika.
Huwezi ukahamasisha demokrasia kwa njia zisizo za kidemokrasia.
Huwezi ukachohochea maasi vichochoroni ukijidai unalinda demokrasia.
Huwezi kukaa na kundi la watu wasiozidi 4 mkawa na mkakati wa kumweka kiongozi wenu kwa njia za kificho mkilaghai watu mkadai mnatekeleza demokrasia.
Hawawezi kunyooshea CCM mkono kwa kukandamiza demokrasia nchini ili hali wao wapo tayari kwenda nchi za jirani kufanya mikutano ya kuhamasisha mapinduzi. Hapa kuna demokrasia gani?
Narudia, kuna hoja zao zenye mantiki kwa kuziangalia kwa haraka.
Mathalani Mbowe kukopesha chama kuna element za conflict of interest.
Kunapokuwa hakuna nyaraka ni mbaya zaidi. Mbowe anaposhindwa kutetea hali hiyo ni mbaya kuliko.
Tatizo linakuja pale Zitto na Mkumbo wakiwa hawajawahi kusimama na kusema watajiuzulu kwasababu ya matumizi mabaya ya fedha. Wanachokifanya ni kwenda nchi jirani kwa mikutano baada ya kuhudhuria mikutano ya kamati kuu bila kuonyesha pingamizi.
Kutetea kalenda ya chama kuna mantiki na hapo Dr Slaa anaulizwa utaratibu wa uchaguzi ukoje?
Kama akina Zitto wangefukuzwa kwa hilo ningesema wameonewa.
Ningesema kama nilivyowahi kusema kuhusu kauli za kumpaka matope Zitto.
Niliwahi kusema kuhusu Muungano CDM haijui nini inakitaka isipokuwa Zitto aliyeandika kwa uwazi kuhusu serikali tatu.
Nilismama na kumsema Mbowe na ziara ya Togwa Ikulu na kufikia mahali nilimwita mnafiki.
Nilisimama na kumsema Dr Slaa kwa suala la Rwanda na kauli zake zilizokosa maono.
Kinachotokea mitandaoni kwa mashabiki wa vyama vya siasa ni ushabiki na si kuangalia mambo kwa mantiki.
Hakuna sababu za kuendelea kulea viongozi wasio na maadili.
Lazima vijana wabadilike na wafanye siasa za maendeleo.Muda wa siasa za tunampenda umekwisha.
Leo tukiuliza CDM kinafuata model gani ya uongozi hatuna jibu, lakini ni wepesi kusimama na kutafuta flimsy reasons za kuficha ukweli. Mtei anaingiaje katika waraka ambao haumhusu na washiriki wamekiri wameuandika na makosa?
Leo mada si waraka mada ni Mtei!
Nilitegemea vijana wangekuwa wanatafuta ukweli na kulumbana kuhusu ukweli, naona siasa za mitaani bado hazijawatoka.
Huu si muda wa kupenda maneno ni muda wa ukweli na sera, mission na vision
Amkeni Watanzania
Ushahidi wa kimazingira unaonyesha waraka ni muda mrefu kidogo.
Ukiusoma kuna sehemu inasema
Nadhani siku za karibuni Zitto amekuwa critical kwa mambo kama pesa za Uswiss na kule Bungenitunayemtaka....apunguzeukaribu na viongozi wa serikali na wa chama tawala na awe crical zaidi nautendaji wa serikali nje na ndani ya bunge
Ni siku za karibuni Zitto ameshiriki sana katika kampeni za kanda magharibi. Historia inaonyesha ni muda mrefu tangu afanye hivyoAshirikikikamilifu katika shughuli za taasisi yetu zikiwamo vikao vyote vinavyomhusu,operesheni mbalimbali, chaguzi ndogo, nk.
Sina shaka mawasiliano yalishafanyika na kilichokuwa kinaendelea ni utekelezaji.
Kuna hoja kuwa Zitto ameundiwa Zengwe.
Kwakuhusishwa na waraka huu kama mhusika mkuu na ushahidi wa kimazingira ni wazi alishiriki.
Hata hivyo watetezi wake pamoja na yeye mwenyewe hawajaeleza ushiriki wake katika kundi la Kafulila, Sakata la M7 na wala hakukanusha kuhusika na waraka.
Katika kujenga hoja hafifu watetezi wa Zitto wanasema Mzee Edwin Mtei ndiye tatizo, wengine wakifumba macho na kusema hakuhusika na waraka.
Wanachoshindwa kukisoma katika utetezi wake mwenye (Zitto) ni hiki
Kama mwanasiasa kijana niliyekaa katika siasa kwa muda sasa yapo mengi mazuri nimeyafanya.
Lakini kuna maeneo nilipojikwaa na yapo makosa niliyofanya kisiasa katika maisha yangu ya siasa
Wapo wanaodai kuwa suala la ukaguzi wa fedha ndicho chanzo na wameligeuza kama ndio hoja.
Wamesahau kuwa waraka uliopo unamtia Zitto matatani.
Tatizo walililofanya akina Zitto na Mkumbo si kuandika waraka. Waraka unaweza kuandikwa na mtu yoyote yule.
Tatizo ni aina gani ya waraka, ulikusudia nini ili kuleta nini na kwa akina nani.
Waraka ulikusudia kuleta mapinduzi (coup d'etat). Nisingeona ajabu kama hilo lingetokea TLP.
Kwa chama kinachojinasibu ni cha kidemokrasia hilo halifai kutamka achilia mbali kuliandika.
Huwezi ukahamasisha demokrasia kwa njia zisizo za kidemokrasia.
Huwezi ukachohochea maasi vichochoroni ukijidai unalinda demokrasia.
Huwezi kukaa na kundi la watu wasiozidi 4 mkawa na mkakati wa kumweka kiongozi wenu kwa njia za kificho mkilaghai watu mkadai mnatekeleza demokrasia.
Hawawezi kunyooshea CCM mkono kwa kukandamiza demokrasia nchini ili hali wao wapo tayari kwenda nchi za jirani kufanya mikutano ya kuhamasisha mapinduzi. Hapa kuna demokrasia gani?
Narudia, kuna hoja zao zenye mantiki kwa kuziangalia kwa haraka.
Mathalani Mbowe kukopesha chama kuna element za conflict of interest.
Kunapokuwa hakuna nyaraka ni mbaya zaidi. Mbowe anaposhindwa kutetea hali hiyo ni mbaya kuliko.
Tatizo linakuja pale Zitto na Mkumbo wakiwa hawajawahi kusimama na kusema watajiuzulu kwasababu ya matumizi mabaya ya fedha. Wanachokifanya ni kwenda nchi jirani kwa mikutano baada ya kuhudhuria mikutano ya kamati kuu bila kuonyesha pingamizi.
Kutetea kalenda ya chama kuna mantiki na hapo Dr Slaa anaulizwa utaratibu wa uchaguzi ukoje?
Kama akina Zitto wangefukuzwa kwa hilo ningesema wameonewa.
Ningesema kama nilivyowahi kusema kuhusu kauli za kumpaka matope Zitto.
Niliwahi kusema kuhusu Muungano CDM haijui nini inakitaka isipokuwa Zitto aliyeandika kwa uwazi kuhusu serikali tatu.
Nilismama na kumsema Mbowe na ziara ya Togwa Ikulu na kufikia mahali nilimwita mnafiki.
Nilisimama na kumsema Dr Slaa kwa suala la Rwanda na kauli zake zilizokosa maono.
Kinachotokea mitandaoni kwa mashabiki wa vyama vya siasa ni ushabiki na si kuangalia mambo kwa mantiki.
Hakuna sababu za kuendelea kulea viongozi wasio na maadili.
Lazima vijana wabadilike na wafanye siasa za maendeleo.Muda wa siasa za tunampenda umekwisha.
Leo tukiuliza CDM kinafuata model gani ya uongozi hatuna jibu, lakini ni wepesi kusimama na kutafuta flimsy reasons za kuficha ukweli. Mtei anaingiaje katika waraka ambao haumhusu na washiriki wamekiri wameuandika na makosa?
Leo mada si waraka mada ni Mtei!
Nilitegemea vijana wangekuwa wanatafuta ukweli na kulumbana kuhusu ukweli, naona siasa za mitaani bado hazijawatoka.
Huu si muda wa kupenda maneno ni muda wa ukweli na sera, mission na vision
Amkeni Watanzania