Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Ndugu Nguruvi3 , unasema mimi na Pasco tunahamisha magoli LAKINI UKWELI NI KWAMBA WEWE NDIYE UNAYEBADILI YALIYOANDIKWA KATIKA WARAKA NA KUTUNGA YA KWAKO, MFANO HAKUNA MAHALI KATIKA WARAKA PENYE HIYO SENTENSI NILIYOIWEKEA RANGI NYEKUNDU. hakuna mahali kwenye WARAKA PANAPOSEMA TUNYEMTAKA HANA BUSARA, HAKUNA!. HAYO MANENO UMEYATUNGA MWENYEWE.
Waraka: ''Kuna wakati tunayemtaka hu-respondkwa taharuki kubwa dhidi ya mashambulizi yanayoelekezwa kwake jambo linalomfanya achukue maamuzi yasiyo sahihi kwa wakati huo. Kwa kifupi kuna wakati tunayemtaka huonekana kufanya maamuzi kwaemotion zaidi badala ya kutulia kwanza na kutafakari kwa kina ikiwa ni pamoja na kutafuta ushauri kwa wenzake kabla ya kurespond

Jambo lililoelezwa katika ‘d' hapo juu humfanya tunayemtaka wakati mwingine kuonekana ana jazba sana kwa sababu akishataharuki na kuchukua maamuzi akingali kwenye taharuki huwa ni rahisi sana kuonekana anajibu mapigo kwa jazba sana''

Gamba la Nyoka kufanya jambo bila tafakuri ndiko kukosa busara. Mengine yapo kama nilivyoonyesha.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Mkuu wangu nakupa no! no! no! kabisa na huu uchambuzi wako maana hauendani hata kidogo na mifano ya nyuma. Mtu anazungumzia hili wewe unaweka la waraka ambalo hayafanani isipokuwa yale ya kumnanga Mbowe. Sikia mkuu wangu, waraka unazungumzia uongozi wote kwa ujumla sijaona mahala umeweka huyo jamaa akimzungumzia Zitto na mapungufu yake. Swala la Mbowe na kutokubaliwa na baadhi ya watu halikuanza jana, toka wakati anagombea Urais mwaka 2005 kiasi kwamba ikafikia Mbowe haonekani hata katika sehemu za starehe ama mialiko na mikusanyiko ya marafiki zake nje ya chama.

Na kibaya zaidi ktk mifano yako umeendelea kumtumia Mbowe kuonyesha wazi jinsi unavyomlinda Mbowe wakati mimi binafsi sii tu namkubali Mbowe bali sikubaliani na maamuzi ya kamati kuu juu ya swala hili. Nina hakika hata huyo Mbowe kashawishika tu kiasi kwamba hana jinsi lakini wapo wanapalilia magugu kuoteza mbegu mpya za husda ndani ya chama. Na ningependa ieleweke wazi kwamba kutokubaliana kwangu na kamati kuu hakunifanyi mimi nisiwe na imani na Mbowe maana swala hili limepitishwa na kundi la watu 33 ambao sijui haswa ni nani alokuwa refa.

Hivyo kwa Zitto kutokubaliana na vitendo vya Makao makuu na hasa uzushi wa kujenga uhasama ulozuka baina yake na Mbowe kwa mapishi yenye chunvi nyingi sintoafikiana na yeyote anayekuja na upuuzi huu wa waraka. Kuna wakati Zitto aliwahi kusema tena humu JF ya kwamba yeye na Mbowe watuna ugonvi lakini watu waliendelea kulishikia bango kiasi kwamba Mbowe mwenyewe akaanza kuamini. wakatumia hadi magazeti yake, wengine kujifanya wako karibu na Zitto kumfikinisha ili mradi tu wameahidiwa kupewa nafasi ya kugombea uongozi uchaguzi ujao. Umewahi kumsoma Ben saa nane alivyokuwa akimshutumu Mbowe? sasa jiulize ikiwa kweli huyu kijana alikuwa karibu na Zitto, unafikiri Zitto aliyapokea vipi kashfa hizi za Mbowe na alimuona vipi Mbowe leo hii Mbowe huyo huyo anapokea kashfa za Zitto na watu wanazimeza kama urojo!

Mimi namjua sana Mbowe, nimefanya kazi naye ktk biashara ya club pale Mbowe na yeye ananijua vizuri kuwa sii mtu wa kuburuzwa,nimekuwa kwa mission town hivyo ujanja ujanja wote naujua sana na hata kumsoma mtu akifunua kinywa tu. Tatizo kubwa la Mbowe ni ile tabia yake ya kusikiliza kila mtu anayekuja kwake na habari za udaku. Mbowe sii mtu anayependa kuzungumza sana mbele ya watu, huchambua kila anachokisema kwa wakati na sehemu aliyopo. Ukienda na habari za mjini mtakesha kimjini, lakini uienda na habari za chama atakusikiliza kama vile ana sura mbili.

Mbowe hupenda kusikiliza zaidi na hapo ndipo hunaswa ktk majanga kama haya. Ni kiongoZI mzuri tu ila inapofikia swala la fedha utamwambia nini Mchagga! pengine tutamuonea bure kumlaumu wakati huu ni urithi na jadi yao kujali kilichoko mfukoni. Waswahili wanasema Shillingi ya mjini sii sawa na ya shamba wakiwa na maaana ya kwamba fedha iliyopo mfukoni huwezi kuilinganisha na ile unayotegemea mavuno. Hivyo swala la Mbowe na Umalaya ktk waraka linajibiwa pia na swala na ndoa kwa Zitto ni tusi vile vile lakini kidemokrasia lazima tuyaangalie haya kama ni sababu zinazoweza kutukosesha kura za wananchi.

Haya maswala ya Umalaya, sijui kuna kiongozi gani Tz sii Malaya, hao wote walojaaliwa kupewa nyadhifa ni malaya wake kwa waume. Na kuhusu kuzaa nje ya ndoa sisi sote humu tuna ndugu wasokuwa tumbo moja pande zote mbili hata huyo JK mwenyewe watoto wake wote sii wa ktk ndoa, lakini mbona hazungumzwi? au huyo Mkapa... eeeh mbona wanapewa misifa tu iweje Mbowe ndio awe gumzo la mjini kumrushia mawe ilihali nyote humu ni malaya?. ETUTANA ni laana tuloandikiwa na ndio maana tunaona ngoma kama mafua tu.

Mkuu nguruvi, swala hapa ni maamuzi ya CC toka kuukamata waraka, kuutoa hadharani badala ya kujipima, na kibaya zaidi kutafuta mchawi wakati wachawi ni wao wenyewe na imedhihirika. Kwa mtaji huu nashindwa kabisa kuendelea kuwaamini iwe Mbowe mshikaji, Dr.Slaa, sijui Mnyika ama Tundu Lissu maana inatisha ikiwa watu hawa watakuja kutawala nchi sijui sheria za nchi zitakuwaje!. Ebu jaribu tu kufikiria ikiwa wapo IKULU na wanaonekana hawafai sijui ni nguvu gani watazitumia kwa upinzani ama raia asokubaliana nao maana tayari sisi tumeisha itwa Mapandikizi ya CCM na hatupendwi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara suala la umalaya limeletwa na wahamisha magoli tena nikiambiwa ni hard facts.
Nilichosema ni kuwa umalaya ni across the board hakuna umalaya strong na mwingine soft.
Nikaonyesha jinsi waraka ulivyomrukia Mbowe halafu ukamtetea 'tunayemtaka'

Kwamba,kwa Mbowe ni mbaya sana, tunayemtaka ah! mashallaha anaweza kupita akidonoa donoa maana hana majukumu ya famili kama alivyosema Pasco na Gamba la Nyoka.
Wanasema one night stand haijambo kwa tunayemtaka.

Nimewaonyesha kuwa tatizo ni tatizo tu hasa mambo hayo yanayoharibu taswira ya CDM kama wasemavyo yanapofanyika. Hakuna uzinifu mzuri, bora au mwema. Uzinifu ni uzinifu tu uwe wa mwenyekiti au tunayemtaka.

Kuhusu ugomvi wa ZZK na Mbowe upo. Hivi karibuni ZZK amenukuliwa akimwambia Tundu, yeye hajibu vifaranga anasubiri mama yao na kisha tukaona akivurumisha madongo kisawa sawa.

Mimi nasema swala hapa ni waraka kama ulikuwa na contents, contex na intent njema.
Suala ni waraka kama ndio ilikuwa njia muafaka ya kujenga CDM na njia ya kidemokrasia ya kukuza demokrasia, suala ni waraka ambao tunauangalia kama ulishaingia sokoni au la na madhara yake ni nini.
Suala ni waraka kama haukuwa na elemts za unafiki, watu wakiingia vikaoni huku wakibeza vikao hivyo

Ni waraka ambao tukiuangalia tunajiuliza je ulikidhi haja ya mabadiliko au ulikuwa na mapungufu zaidi yanayoonekana kwa macho bila miwani. Je nia ya waraka ilikuwa njema. Maudhui yalikuwa mema na viwango na ujumbe ulieleweka na ulikusudia nini.
CC na maamuzi ni sehemu ya mjadala wa waraka lakini siyo 'theme'

Mwisho, mkuu hebu nionyeshe wapi nimetetea Mbowe.
 
Bado unahamisha goli, endapo hoja ya umalaya inahusishwa na uongozi wa chama, kwanini hoja ya mapenzi kwa 'tunayemtaka' ipewe uhalali tukijua itahusishwa na chama pia.

The bottom line ni kuwa mapenzi na uongozi havijengi taswira nzuri kwa mujibu wa waraka regardless nani anafanya hivyo. Double standards zina matatizo na ndicho chanzo cha kusema waraka ni too low, haukuandikwa kama muongozo wa kisiasa bali chuki za kujenga uhalali fulani.
Mkuu Nguruvi3, sihamishi goli, naomba kusisitiza kuwa "malaya" ni yule tuu mwenye ndoa, anayetoka nje ya ndoa!. Kijana ambaye bado hajaoa, akibadili mpenzi, its presumed, he is still searching for the right one!. Lazima tukubali the times za enzi za mababu zetu za single choice tena head hunting, ambapo bibi na mama zetu were head hunted and pointed only once and for all tena wakiwa sealed!, they've long gone!.

Mimi nilioa ay 25 years straight from TSJ na wife akiwa ni class mate wangu, darasa letu likiwa na wanafunzi 24 tuu, 12 boys na 12 girls na out of darasa letu six couples walioana!. Hivyo my boys and girls are my friends kama wadogo zangu!. Sasa hao wasichana 12 tuu hapo darasani, kabla couples hazistabilize na kuja kuishia altareni, search, trios and erros za compactibility zilifanyika, jee hizi seach utaziita umalaya?!.

Kwa vile Jemedari is commited, he is expected to practice zero graizing, lakini MM, is not yet commited, so he has the right to graze without being called names!. Nikiwa UDSM, nilimfahamu binti fulani from Christian family, well mannered aliyeamua kufuata mafundisho ya dini, to keep the seal till defloration day!. (Wengine wetu tumejaaliwa a third eye to see the seal!, tulipoanza first year, seals chache ziliweza kuhesabika!, by mwaka wa nne, there was no seal na hakuna ndoa!). Waoaji wa kisasa sio kama wale wa zamani, laliza wavifitishe kwanza viatu kama vina wafit ndipo wanunue na kuvivaa!. Binti wa watu baada ya kuona miaka inapita na umri wa kuolewa unazidi kusogea, akajikuta hana jinsi, bali kukubali kuishi maisha ya ukweli ya dunia hii na sio tuu kufuata maisha ya kufikirika kwenye mafundisho ya duni, mila na desturi!, tulipofika 4th year, akajikuta amekubali kufitisha kiatu kwa hope anayefitisha kitamtosha!, hakikumtosha!, internship akamfitisha mwingine!, hakikumtosha!. Sasa ana kazi nzuri tuu, na amemfitisha mwingine!, sijui kama kitamtosha!, kiukweli huyu binti unaweza kumuita malaya?!.

Kwenye hoja ya umalaya kwenye waraka, nasisitiza hakuna double standards zozote!.

Ila pia Mkuu Nguruvi3, kitendo cha kuubeza waraka kama hivi
The bottom line waraka ni too low, haukuandikwa kama muongozo wa kisiasa bali chuki za kujenga uhalali fulani
sio kuutendea haki!. Kiukweli kila member humu anazo standards zake kwa ma GT mbalimbali humu jf, kwenye list yangu, Mkuu Nguruvi3, umo kwenye top 3!, nilikuambia tatizo lako ni dogo tuu, ume take side!, kitendo ambacho kimepelekea wewe kupata a little blurred vision ya waraka, hivyo kwa kiasi kikubwa umepoteza objectivity na impartiality yako katika kuuhukumu waraka, ndio maana saa zote unauponda!. Nakushauri vua hiyo miwani ya upande unaoigemea, usome tena waraka, nimekueleza waraka ule ni "The Creation of a Winning Coalition", hii ni very valid political theory!, its a great piece of political litarature!, tena namsisitiza Dr. Kitila aifanyie taratibu za kisomi, utumiwe kama "a working document" katika somo la political science kwa vyuo vikuu vya hapa nchini!.

Please don't let me down na wale wenye mawazo kama mimi, nikakusogeza out of the top 3!. Baadhi ya GT wa calibre na level yako humu, waliomua ku take side, wameeleza wazi humu upande wao kisha wamejinyamazia!. Wewe ume take side halafu unaendelea kuubeza waraka, sio kujitendea haki!, please utendee haki waraka!.

Pasco.
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu nakupa no! no! no! kabisa
Haya maswala ya Umalaya, sijui kuna kiongozi gani Tz sii Malaya, hao wote walojaaliwa kupewa nyadhifa ni malaya wake kwa waume. Na kuhusu kuzaa nje ya ndoa sisi sote humu tuna ndugu wasokuwa tumbo moja pande zote mbili hata huyo JK mwenyewe watoto wake wote sii wa ktk ndoa, lakini mbona hazungumzwi? au huyo Mkapa... eeeh mbona wanapewa misifa tu iweje Mbowe ndio awe gumzo la mjini kumrushia mawe ilihali nyote humu ni malaya?. ETUTANA ni laana tuloandikiwa na ndio maana tunaona ngoma kama mafua tu.
Mkuu Mkandara, naomba hili neno umalaya tusiendelee kulitumia!, najisikia vibaya, kwa sababu kwa sisi wengine haswa wa kanda ya Ziwa, hii ni jadi yetu!, Wazungu na dini yao ya Ukristo ndio wametaka kutuhamisha kwenye jadi yetu na kuumbatia uzungu, ila sisi ambao jadi iko kwenye damu, tumehalalisha hayo, na kiukweli kabisa from the bottom of my heart, ni halali yetu kabisa unless we want to live a lie!.

Ukiondoa uzungu, hubu turudini kwenye jadi zetu kama kina Zuma!, tena thank God hii ilikuwa tabia kabla ya ndoa na waliiolewa wanajua, ndio maana nilikuwa na mke hapo Toronto, mke DC na mke bongo! na kote naona ni halali, japo wa altareni ni mmoja, ila anazijua existance zingine, japo hapendi its a facts na watoto wote ninao home saves wale wanaioshi na mama zao!.

Hii ndio jadi ya Waafrika!, please stop this neno "Umalaya!".
Pasco.
 
Mkuu Mkandara suala la umalaya limeletwa na wahamisha magoli tena nikiambiwa ni hard facts.
Nilichosema ni kuwa umalaya ni across the board hakuna umalaya strong na mwingine soft.
Nikaonyesha jinsi waraka ulivyomrukia Mbowe halafu ukamtetea 'tunayemtaka'

Kwamba,kwa Mbowe ni mbaya sana, tunayemtaka ah! mashallaha anaweza kupita akidonoa donoa maana hana majukumu ya famili kama alivyosema Pasco na Gamba la Nyoka.
Wanasema one night stand haijambo kwa tunayemtaka.

Nimewaonyesha kuwa tatizo ni tatizo tu hasa mambo hayo yanayoharibu taswira ya CDM kama wasemavyo yanapofanyika. Hakuna uzinifu mzuri, bora au mwema. Uzinifu ni uzinifu tu uwe wa mwenyekiti au tunayemtaka.

Mkuu Nguruvi3, hakuna cha kuhamisha magoli popote, tofautisha mtu mwenye ugali, na mboga, lakini "anayetaka kubadili mboga" kwa hamu tuu, na yule mwenye ugali tuu sasa ndio anatafuta kitoweo ili na yeye angalau apate mboga aweze kula!.

Yes kitendo ni kuvunja amri ya sita!, kuivunja in search of settlement inaitwa making choices na its justied without being called names!. Kuivunja just for pleasures its unjustified!.

Lets close hiki kipengele maana unazidi kumuaibisha jemedari wakati kiukweli kabisa kwa MM ni halali!.
Pasco.
 
Mkuu Nguruvi3, hakuna cha kuhamisha magoli popote, tofautisha mtu mwenye ugali, na mboga, lakini "anayetaka kubadili mboga" kwa hamu tuu, na yule mwenye ugali tuu sasa ndio anatafuta kitoweo ili na yeye angalau apate mboga aweze kula!.

Yes kitendo ni kuvunja amri ya sita!, kuivunja in search of settlement inaitwa making choices na its justied without being called names!. Kuivunja just for pleasures its unjustified!.

Lets close hiki kipengele maana unazidi kumuaibisha jemedari wakati kiukweli kabisa kwa MM ni halali!.
Pasco.
Naomba nikuulize, ni kwanini waraka ulimtaja jemedari kuhusu hayo majambo.
Kuna uhusuiano gani wa jemedari, waraka na kitu kingine kama kipo.
 
Ndugu yangu unachotaka kunishawishi hapa ni kuwa kuna 'kamimba kadogo na Mimba kamili' wenyewe wanasema 'little bit pregnant'

Nimesema kuwa hoja za waraka bado hizinionodi katika ukweli kuwa naungalia waraka katika hali zote.
Unaposema kuna malaya kwasababu ameoa utakuwa huna ufahamu wa def ya umalaya.
Ni hivi umalaya ni umalaya tu hakuna umalaya wa sheikh, askofu n.k.

Ukisoma waraka kwa macho angavu bila kitambaa cheusi utaona waandikaji wamekerwa sana na tabia ya mwenyekiti inayoathiri taswira ya chama. Halafu wanajisahau na kumshauri 'tunayemtaka' afanye uzinifu kwa siri sana kwasababu uzinifu una nafuu kuliko umalaya! real.

Na hapa tunaona Pasco akisema yule hajaoa akiruka ruka na vibinti vya BAVICHA au akina mama wabunge ni kughafilikiwa lakini haina athari katika taswira.

Gamba la Nyoka anasema aaa! 'tunayemtaka' anaweza kufanya uzinifu kidogo tu 'one night stand' muhimu ajifiche lakini akionekana haina taabu sana kama mwenyekiti.
Real,waungwana kuna classification za uzinifu kweli!

Point ni kwamba waraka upo vague ukiusoma una ji contradict sana.
Nikupe kionjo kingine, waraka unasema mwenyekiti ana akili ndogo na elimu ya magumashi hafai kabisa kuongoza. Waraka huo huo unasema 'tunayemtaka' hana busara na ana jazba.
Kwamba unaodoa mwiba kwa ku replace na msumari. Waraka huo!

Waraka unasema mwenyekiti anatengeneza makundi ndani ya chama.
Waraka umeshindwa kuelewa kuwa Kitila na ZZK wanatengeneza makundi kwa kutumia waraka.
Tena unampamba 'tunayemtaka' hana makundi, uongo mkubwa, ZZ ndiyte mwenye Masalia 7, Juliana, Kafulila n.k.

Usomeni waraka muone jinsi unavyojichanga, kama kuna kitu too low nimekisoma siku za karibuni waraka umeshinda.

Mwigamba na Kitila ni Wakiristo, Bila shaka watakuwa wameathiriwa na mafunzo ya Kikristu, NA KWA MAFUNDISHO YA KIKRISTO, MTU AMBAYE HAJAOA HUWA HAZINI, MZINZI NI YULE MWENYE NDOA.

Japo MM ni Mwislamu na KATIKA UISLAMU UZINZI NI KWA YEYOTE ANAYEFANYA MAPENZI NA ASIYEKUWA MKE/MME WAKE WA NDOA!. LAKINI WAANDAAJI WAKUU WA WARAKA NI WAKIRISTU NA KWA HIVYO MTIZAMO WAO WAO WA UZINZI UTAKUWA KATIKA MISINGI YA IMANI ZAO!

Kwa hiyo basi mfano wako wa Uzinzi hauko mahali pake, MWENYEKITI ANA NDOA, MM BADO ANATAFUTA!!
 
siku
Naomba nikuulize, ni kwanini waraka ulimtaja jemedari kuhusu hayo majambo.
Kuna uhusuiano gani wa jemedari, waraka na kitu kingine kama kipo.
Kanisome vizuri kule nilipoelezea kuhusu the creation of a new winning coalition, as of now Jemedari ndio the winner, baada ya kuyaona madhaifu ya Jemedari, mnaamua kumtengeneza jemedari mwingine, nikakueleza hizi ni vita na mbinu za kivita ndizo zinatumika!. Nikakueleza kuwa ingekuwa ni front line kwenye battle fields, Jemedari goigoi huwa kwanza anatafutiwa his weakest point ku justify elimination, tena siku ya utekelezaji, anapelekewa a very tasty food ya ile confort na kukabiliwa akiwa pants down!.

Nikakueleza once elimination ni successful ndipo 2i/c anaambiwa to take charge!. Hata Zanzibar aliyepindua sio Karume!. Nikakueleza kwa vile hii ni political battle zinatumika political ammunitions, hivyo zile ni silaha za maangamizi, political missiles! to justify shambulizi la elimination, target ilijiingiza yenyewe in a line of fire, its just taken out.Tena anabahati sana Tanzania tumeiga mfumo wa utawala wa Westminster kwa kucopy tuu mifumo na sheria pari material ila hatukucopy morality standards zao!, ile kusikika tuu kuwa ulionekana, licha ya kutotoa, zamani kazi huna!, saa hizi ingekuwa ni kitambo ameisharudia ile kazi yake kukusanya kiingilio kwenye ile deal yake ya NHC !.
Pasco
 
Gamba la Nyoka, sipendi kuingiza mambo ya dini katika majadiliano kwasababu sina utaalamu huo.
Kwa hili ulilosema nalazimika kukujibu kwa kutambua kuwa wewe na Pasco mna mislead public hasa vijana wadogo katika kutafuta justification ya utetezi wa waraka na wahusika.


Adulterium ni extra marital affairs kwamba mtu ameoa au kuolewa na anakwenda nje ya ndoa.
Hilo limekuwa condemned na vitabu vitakatifu vya dini nyingi the least to say.


Kwa waislam na wakristo adultery inajulikana kama uzinifu na mtenda au mtendwa huitwa mzinzi.


Kwa wasilam kuzini pia inachukuliwa kama kitendo kabla ya ndoa.
Na kwa wakristo ingawa sielewi neno la Kiswahili, kwa lugha nyingine inasema ni ‘sexual immorality'

Zote mbili zimelaaniwa katika vitabu vitakatifu vya dini hizo.


The point kuwa MM anatafuta na hivyo anaruhusa ya kufanya lolote haina mashiko kwa njia zozote zile ziwazo.


Gamba la nyoka kuwahusisha akina Kitila na Mwigamba katika mambo ya siasa na dini zao si kuwatendea haki.
Wao walikuwa wanachama wa CDM na walichotaka kufanya ni kwa ajili ya mambo ya kisiasa na si vinginevyo.


Ukweli unabaki kuwa tuhuma za waraka kwa mwenyekiti zililenga kupeleka ujumbe kuwa tabia yake inaathiri taswira ya chama.


Unfortunate waraka huo huo unatoa nafasi kwa ‘tunayemtaka' ambaye ni mwenyekiti mtarajiwa kufanya uzinifu eti kwavile anatafuta na haitakuwa na athari ya taswira kwa chama!!! mnahamisha goli wakuu kwa double standards


Kama hoja ya kutafuta itatumika vibaya kama mnavyo promote, hilo litakuwa tatizo jingine kwa upande wa ‘tunayemtaka'


Tatizo litakuwa kwamba tunayemtaka hajakomaa katika taasisi kama za ndoa na akili yake bado inahangaika kutafuta huku na kule akipewa pass ya kudonoa hovyo.


Hadi hapo hana uwezo wa kuongoza taasisi kubwa kwasababu ni immature katika mambo ya kijamii ya kupewa dhamana kubwa . Ni bora angepewa muda wa kutafuta ili aweze kuzuia jazba na ukosefu wa busara pengine unaotokana na ujana.

Pasco unanipa wakati mgumu sana kukubali kuwa waraka ni super kinyume na ninavyouona ni too low. I am trying to elevate waraka katika status unayopendekeza ingawa akili yangu inanisuta kwasababu nakubaliana na dhamira ya moyo inayopingana na mantiki ya akili.

 
Last edited by a moderator:
Gamba la Nyoka, na Pasco mna mislead public hasa vijana wadogo katika kutafuta justification ya utetezi wa waraka na wahusika.

Pasco unanipa wakati mgumu sana kukubali kuwa waraka ni super kinyume na ninavyouona ni too low. I am trying to elevate waraka katika status unayopendekeza ingawa akili yangu inanisuta kwasababu nakubaliana na dhamira ya moyo inayopingana na mantiki ya akili.
Mkuu Nguruvi3, sikujua kuwa kumbe na wewe ni mbishi!, usibishe tuu for the sake of kubisha tuu lakini kwenye hili la jemedari kubadili mboga, huna hoja!. Naomba weka dini pembeni. Twende kikawaida tuu, kwenda nje ya ndoa sio kosa la jinai, it's a crime against morality, mtu wako hana morals!, ni msaliti wa ndoa, hivyo usaliti ni usaliti tuu!. Kwa mtu kapera kupata ile huduma it's not a crime!, MM, hana kosa lolote!.

Kuhusu waraka wa mabadiliko, naomba nikuhakikishie nimesoma kitu kinaitwa graphology, huu ni uwezo wa kuisoma intent ya mwandishi, kupitia life iliyoko kwenye andishi!. Amiini nakuambia waraka ni good piece of political literary work!. Kitila na Mwigamba, they're both very genuine ila naamini master mind ni Kitila, this is a great mind and among very few valuable jewels Chadema has lost!.

Japo Kitila amesema MM was not briefed, graphology inaniambia alikuwa briefed, hivyo Kitila amekubali kujitoa mhanga kuwajibika ila hata kama MM was briefed, kosa lake ni lipi?!.

Mkuu Nguruvi3, naomba tuufunge huu mjadala kwa mtu kukubaliana kutokukubaliana, nasisitiza waraka sio uhaini, the motive behind ulikuwa na good intentions za kuisaidia Chadema, na waandishi waraka sio wahaini ni very honest and genuine people with good intentions and were acting in good faith!.
Pasco.
 
Pasco mbona unanisoma bila kunielewa!!!
Nimesema wazi kuhusu adultery kidini na kijamii na kusema si jambo linalokubalika.

Hadi hapo tunakubaliana kuwa hilo ni tatizo.


Nikasema waraka ulikusudia kusema kuwa adultery inaharibu taswira ya chama.

Hakuna mahali nimesema hilo si tatizo, ina maana nimkubali maadili ya mtazamo wa jamii kama ulivyoonyeshwa katika waraka.


Nikaonyesha kuwa waraka umetoa fursa kwa ‘tunayentaka' kufanya ufuska kwa siri.

Nikasema hapana, hapo sikubaliani kwasababu bado tunayemtaka akiwa mwenyekiti ataathiri taswira ya chama kama ambavyo mwenyekiti anaathiri.


Naikasema kuwa endapo tunayemtaka akiwa mwenyekiti na wakati huo huo anaruka ruka na vibinti vya BAVICHA au wabunge au wake za watu jamii haitatambua kuwa anatafuta. Jamii itaelewa mwenyekiti(tunayemtaka ni fuska)


Contention yangu ni kuwa kama adultery ni kosa kwa kuathiri taswira ya chama basi iwe across the board. Hata mbunge au diwani wa kawaida akifanya kinyume bado anaharibu taswira ya chama na si muafaka kutafuta sababu za huyu anatafuta bado, yule amepata.


Nikaenda mabali na kusema uongozi wa taasisi ni jambo na jukumu zito sana.

Itakuwa ni kichekesho kama si mahoka mwenyekiti akianza kuzunguka anatafuta.


Ni kwa muktadha huo waraka badala ya kumshauri kufanya mapenzi kwa siri ulipaswa kumshauri ajiunge na taasisi ya ndoa au aache kuruka ruka vinginevyo ‘tunayemtaka'atakuwa bado hajakamilika.


Atatumia muda mwingi kuzunguka na vibinti na wake za watu kama kile kinacholaaniwa sasa hivi na kuathiri taswira badala ya kushughulika na shughuli za taasisi.

Huo ndio mtazamo wangu.


Sioni wapi nimebisha zaidi ya kutoa maoni yangu.

Nina uhakika kabisa leo wangeambiwa waandike waraka ule tena kwa kusoma maoni tu wangekuwa na mtizamo tofauti.


Ni kwa kuzingatia hayo nikahitimisha kuwa waraka haukuangalia mambo katika angle tofauti zaidi ya kumwandama jemadari. Nawe ukaniunga mkono kuwa ni katika medani za vita silaha za maangamizi zinatumika.


Tofauti yangu nawe ni kuwa mimi nasema kosa ni kosa na kusiwe na loophole yoyote.

Wewe unasema Fulani anatafuta athira yake kwa taswira haipo. Ninasema ipo kwasababu huwezi kuwa na mwenyekiti anaruka ruka hovyo kwa kumtetea kuwa anatafuta.


Kwa ujumla mimi nauangalia waraka kwa microscope na kuona chembe za mchele, magugu na mashudu .

Inahitaji uwe na Neuber chamber kubaini kilichomo, kwa macho ya kawaida yenye mahaba ni ngumu sana kuona kilichomo.

 
I think CHADEMA are the victims of their own success. Not long time ago when the party was still in obscurity being the chairman, vice chairman, or the general secretary of the party wasn't a big deal. Back then the party leader could have committed multiple adulteries and nobody could have cared. The party was a just a petty political project for those who couldn't make their marks through the established political system, CCM. So when we speak about CDM, we don't speak about a political party that was built with moral values in mind from the beginning.

As political fortunes of the party reverse, the legitimacy, moral values or competencies of those in power will be scrutinized and tested by internal and external forces. Internally, there will be a power struggle because being a party leader pays off and is a prestige. Externally, the party is a threat to the establishment. Hence, the current leaders have to rise up to the occasion and take necessary steps to save and strengthening the party, even if those steps might come at their expenses.

Externally, CDM leaders should behave in the manner that everybody including members of other political party would like to have them for dinner, lunch or conversation.
 
Gamba la Nyoka, sipendi kuingiza mambo ya dini katika majadiliano kwasababu sina utaalamu huo.
Kwa hili ulilosema nalazimika kukujibu kwa kutambua kuwa wewe na Pasco mna mislead public hasa vijana wadogo katika kutafuta justification ya utetezi wa waraka na wahusika.


Adulterium ni extra marital affairs kwamba mtu ameoa au kuolewa na anakwenda nje ya ndoa.
Hilo limekuwa condemned na vitabu vitakatifu vya dini nyingi the least to say.


Kwa waislam na wakristo adultery inajulikana kama uzinifu na mtenda au mtendwa huitwa mzinzi.


Kwa wasilam kuzini pia inachukuliwa kama kitendo kabla ya ndoa.
Na kwa wakristo ingawa sielewi neno la Kiswahili, kwa lugha nyingine inasema ni ‘sexual immorality’

Zote mbili zimelaaniwa katika vitabu vitakatifu vya dini hizo.


The point kuwa MM anatafuta na hivyo anaruhusa ya kufanya lolote haina mashiko kwa njia zozote zile ziwazo.


Gamba la nyoka kuwahusisha akina Kitila na Mwigamba katika mambo ya siasa na dini zao si kuwatendea haki.
Wao walikuwa wanachama wa CDM na walichotaka kufanya ni kwa ajili ya mambo ya kisiasa na si vinginevyo.


Ukweli unabaki kuwa tuhuma za waraka kwa mwenyekiti zililenga kupeleka ujumbe kuwa tabia yake inaathiri taswira ya chama.


Unfortunate waraka huo huo unatoa nafasi kwa ‘tunayemtaka’ ambaye ni mwenyekiti mtarajiwa kufanya uzinifu eti kwavile anatafuta na haitakuwa na athari ya taswira kwa chama!!! mnahamisha goli wakuu kwa double standards
Kama hoja ya kutafuta itatumika vibaya kama mnavyo promote, hilo litakuwa tatizo jingine kwa upande wa ‘tunayemtaka’

Tatizo litakuwa kwamba tunayemtaka hajakomaa katika taasisi kama za ndoa na akili yake bado inahangaika kutafuta huku na kule akipewa pass ya kudonoa hovyo.


Hadi hapo hana uwezo wa kuongoza taasisi kubwa kwasababu ni immature katika mambo ya kijamii ya kupewa dhamana kubwa . Ni bora angepewa muda wa kutafuta ili aweze kuzuia jazba na ukosefu wa busara pengine unaotokana na ujana.

Pasco unanipa wakati mgumu sana kukubali kuwa waraka ni super kinyume na ninavyouona ni too low. I am trying to elevate waraka katika status unayopendekeza ingawa akili yangu inanisuta kwasababu nakubaliana na dhamira ya moyo inayopingana na mantiki ya akili.



Hapo nilipopigia Msitari na kuweka rangi nyekundu ndipo haswa ninaposimamia, WEWE NGURUVI3 MATHALANI UNAWEZA KUWA UNAAMINI MM KWA KUTEMBEA NA WANAWAKE AMBAO HAJAWAOA KWAMBA ANAZINI. LAKINI TATIZO LA CONCLUSION YAKO NI KWAMBA HAKUNA MSIMAMO MMOJA WA KIJAMII YA KITANZANIA WENYE KUELEZA KWAMBA KUZINI NI NINI?. BALI KUNA MITAZAMO MIWILI MIKUU JUU YA MAANA YA KUZINI, NAYO NI MTAZAMO WA MLENGO WA KIKIRISTU NA MTIZAMO KWA MLENGO WA KIISLAMU

KWA MTIZAMO WA MLENGO WA KIKIRISTU NI KWAMBA MZINZI NI YULE MWENYE NDOA AKATOKA NJE
KWA MTIZAMO WA DINI YA KIISLAMU KUZINI NI KUFANYA NA YEYOTE AMABAE SI WAKO KINDOA

JE KUNA CONCENSUS ISIYO YA KIDINI JUU YA MAANA YA KUZINI KATIKA JAMII YA KITANZANIA?- HAIPO

SASA HOJA YAKO UNAPOSEMA WARAKA UNAFUMBIA MACHO UZINIFU WA MM, UNGETAKIWA UELEZE UMEFIKIA CONCLUSION YAKO HIYO BASED KATIKA MTIZAMO UPI.


VYOVYOTE UTAKAVYOCHAGUA KUBASE MSIMAMO WAKO, BASI HESHIMU PIA NA WENZIO WANAOBASE KUTAFSIRI MAANA YA KUZINI KWA MTIZAMO TOFAUTI, MAANA HAKUNA CONCENSUS JUU YA KUZINI KATIKA JAMII YA KITANZANIA!.

HATA HIVYO KWA CASE YA MWENYEKITI AMBAYE TAYARI ANA NDOA, VYOVYOTE VILE UKIAMUA KUAPPLY MAANA YA KUZINI KWA MLENGO WA KIKRISTU AU UKIAMUA KUAPPLY MAANA YA KUZINI KWA MLENGO WA KIISLAMU, VYOVYOTE VILE ANAFUNGWA NA MAANA HIZO ZOTE MBILI!.

HIYO CONCLUSION YAKO KWAMBA MAADAMU MM HANA NDOA NA HIVYA HAJAKOMAA, HILO NDILO LA KUDISCUSS, HILO NDILO LA KULIANGALIA KIUNDANI. LAKINI JE SI WAMELIWEKA NALO KWENYE SWOT ANALYSIS?, JE WENYE WARAKA SI WAMELIONA HILO KWAMBA NI UPUNGUFU/UDHAIFU WA MM?, LAKINI PIA SI WAMEWEKA VIGEZO VINGINE NDANI YA SWOT ANALYSIS KISHA WAKAJIRIDHISHA KWAMBA VIGEZO HIVYO VINAZIDI NGUVU MAPUNGUFU?.

SASA KWA NINI HUTAKI KUACKNOWLEDGE KWAMBA KUNA INTELLECTUAL HONESTY IMEFANYIKA KATIKA KUUCHAMBUA WARAKA?.

TOFAUTI YAKO NA AKINA KITILA NI KWAMBA WAO WAMEANGALIA VITU VINGI KUFIKIA CONCLUSION YA KWA NINI MM ANAFAA, LAKNI WEWE MATHALANI UNACHUKUA PUNGUFU MOJA LA MM NA KUFIKIA CONCLUSION KWAMBA HAFAI. WENZIO WAMETUMIA SWOT ANALYSIS JE WEWE UMETUMIA ANALYSIS GANI KUFIKIA CONCLUSION YAKO NDUGU NGURUVI3?

Kiufupi ni kwamba Waraka uko poa sana, umesheheni maono yenye maana juu ya chama kinatakiwa kiwe vipi, Hata kama Mbowe na camp yake wanawachukia kina Kitila, ni vyema wakaufanyia kazi Waraka, wanayoona yanafaa wayachukue, wanayoona hawataki wayaweke pembeni kwanza!, lakini ole wao wakatae yale ya msingi!
 
@Gamba la Nyoka , hapop nyuma nimeeleza suala la uzinzi kwa dini na mitazamo yote ya kijamii.
Hili sitarudia kwa sasababu lipo wazi kabisa na kama unahitaji ufafanuzi rejea post yangu ya nyuma.

Pili, unaweza kuwa na gunia la nafaka, katika kilo 100, kilo 40 mchele. kilo 40 mashudu na kilo 20 chuya. Yes, ni gunia la mchele kama kawaida ya ku generalize kwa Watanzania, kwa uhalisia ni gunia la nafaka lililosheheni kilo 40 za mchele, kilo 40 za mashudu na kilo 20 za chuya.

Ili tuwe na mchele safi inabidi tuchuje mashudu na chuya na kuyatupa pembeni.
Kila mmoja ana mtazamo wake, wangu ni kuwa nauangalia waraka kwa contents,context na intent
 
nguruvi,
Kwanza niwaombe samahani nyote kwa kulileta swala hili humu lakini tusipende sana kumhukumu mtu pasipo kujua sababu zake. Swala la Uzinzi pamoja na kwamba limelaaniwa na dini zote hatuwezi kuzitumia dini kumhukumu mtu maana sii kazi yetu. Hatufahamu mhusika amefuata mafundishio yapi, pengine ana open relationship yeye na mkewe ama mkewe hazai tena na kamruhusu kama ya Nabii Ibrahim.

Hivyo basi nilichokisoma mimi ktk waraka nilielewa tofauti na ya kwamba Mbwe kama mwenyekiti kutembea nje ya ndoa ni udhaifu ambao unaondoa KUAMINIKA kwa maana ya kwamba kama haaminiki nyumbani kwake ataweza vipi kuaminiwa nje na wanachama. Na je kiongozi akiwa Malaya utaweza vipi kujenga nidhamu ndani ya chama maana ni sawa na mume aliyetembea na kijakazi, nidhamu haiwezi kuwepo ndani ya nyumba. Hivi ndivyio nilivyoelewa mimi napouzoma waraka.


Mkuu wangu unapochemsha wewe ni pale unapopima Uzinifu wa mtu alokuwa ktk ndoa na Kapela, vitu hivi havilingani hata kidogo maana ukisema hivyo sisi wote humu na asilimia 99 ya Watanzania wote tumetembea kabla ya kuoa/ kuolewa hivyo huwezi kusema MM ni mzinifu ana makosa sawa na alokuwa ktk ndoa wakati wewe mwenyewe uliwahi kuwa mzinifu hujaoa. Na sote tumekuja kuoa/kuolewa na wazinifu wenzetu mambo mswano kabisa! hivyo tusifanya ya nyani na makalio yake. MM (jina jipya hili) ni kapela na he is not responsible to anyone but himself tofauti na Mimi au Mbowe. Hivyo uzito wa makosa ya Mbowe unaelekezwa ktk Betrayal, ile Usaliti, violation ya ndoa ilofungwa tofauti na ZZK ambaye hana contract na mtu..

Binafsi yangu siwezi kumlaumu Mbowe kwa sababu sijui undani wa imani yake ama sababu zilizopelekea na kikubwa zaidi sina kiongozi hata mmoja Tanzania yetu ambaye ni mwanandoa na MSAFI nyumbani kwake! kama nilivyosema viongozi wote sii wasafi wanatembea nje ya ndoa zao na wana watoto nje ya ndoa hivyo swala hili tusilitazame nje ya waraka kwa kufuatia wana CCM wanalijengea hema swala la Mbowe wakati JK mwenyewe ana mtoto nje ya ndoa na bado ni mwenyekiti hazungumzwi!.

Turudi ktk mada yetu tuachane na hili swala la kumpima Mbowe nje ya waraka wenyewe na kuanza kutumia mistari ya imani za dini. Hatumtafuti Sheikh wala Kadinali hivyo tuusome waraka kwa kuingia vichwani mwa waandishi ambao bila shaka wao walimtazama kiongozi wao kuwa mfano bora, mtu anayeweza kuamimika, anayetenda anayofundisha na kadhalika hivyo hoja hiyo ililenga kuonyesha asivyoweza kuaminika, lakini hata hivyo makosa yapo ktk kumlinganisha na Kapela maana CV zao hazifanani. Na Tanzania yetu MSAFI wa ndoa hutampata maana ngono ni ulevi wetu na ukijaaliwa kupata wadhifa basi utaishi kulingana na wadhifa..
 
Last edited by a moderator:
Mkandara , hakika naungana nawe kama nilivyosema hapo awali kuwa masuala ya dini ni mazito sana hivyo tusiyaingize katika maisha ya watu. Huo ndio msimamo wangu tangu awali nashukuru umeliona hilo.

Nilichokifanya ni kuweka sawa maneno ya Gamba la Nyoka kuwa uzinifu umezungumziwa katika dini moja.

Kuna hoja nisiyoeleweka na naomba niiweke sawa hapa. Ni kweli mwenyeikiti anapaswa kuwa role model kwa kila kitu ndani na nje ya nyumba yake.

Japo sisi wote ni victims wa mambo uliyosema, inatosha kusema kuwa Mkandara akijimwagia chai hakuna atakayezyungumzia lakini mwenyekiti wa taasisi kubwa, hiyo ni habari kama tunavyoona

Silinganishi uadilifu unaotakiwa, ninalinganisha nia ya waraka kwa uadilifu uliosemwa.
Kama ipo hoja ya Mwenyekiti kutenda kinyume kama ilivyoelezwa hilo halikuwa na tatizo.
Tatizo ni pale ambapo waraka umedai kuwa MM akifanya mambo ya mapenzi yawe ya siri.

Tunafahamu kuwa waraka ulikuwa umelenga kumwandaa MM kama mwenyekiti baada ya huyu aliyepo. Ukisoma between the lines waraka unatoa loophole ya mwenyekiti mtarajiwa kufanya mambo kwa siri.

Hakuna mahali waraka umeeleza kuwa akishaoa(kama tajaaliwa) aache, la hasha, ulichofanya ni kumshauri mwenyekiti mtarajiwa kufanya mambo ya mapenzi kwa siri.

Ikumbukwe kuwa waraka ilikuwa ni dira ya CDM in future, hivyo kusema MM a.k.a mtarajiwa afanye mapenzi kwa siri ilikuwa ni kumuasa kuwa yeye anapaswa kufanya mambo kwa siri bila kuweka mpaka lini aache.

Kama CDM inataka kujengwa kwa misingi ya imara haiwezekani kuwe na loophole hizo.

Niltaraji waraka ungesihia kwa mwenyekiti na hapo nisingesema kitu kwa kuamini kuwa wanachora mstari wa nidhamu kwa aliyepo na ajaye.

Kitendo cha kusema yeye afanye kwa siri mimi nakitafsiri kuwa mapungufu yake ayafiche asifanye kama huyu wa sasa. Hapo hakuna moral ya kukemea jambo moja na kulifanya kwa mkono mwingine.

Naomba niweke sawa,sina utetezi wala kulinganisha makosa kabisa.Na hakuna mahali nimesema kilichofanyika ni sawa.

Ninachokifanya ni kuuangalia waraka katika muktadha mzuri hasa kipengele cha ''intent.
'
Je nia ya waraka ilikuwa kujenga nidhamu ya kudumu ya CDM? Kama ilikuwa hivyo vipi kuwepo na 'provision' ya kumruhusu Kapera aliyekuwa anaandaliwa kuwa mwenyekiti afanye hivyo?
Je, nani anaweza kusema kwa dhati kuwa laiti angefanikiwa kuwa mwenyekiti basi angekoma katabia hako.

Nani anaweza kusimama na kuniambia kuwa ufuska wa mwenyekiti mwenye ndoa ni mbaya zaidi kwa taswira ya chama kuliko mwenyekiti Kapera?
Nidhamu inaanza na kuishia wapi katika suala la maadili?
 
Last edited by a moderator:
Mkandara , hakika naungana nawe kama nilivyosema hapo awali kuwa masuala ya dini ni mazito sana hivyo tusiyaingize katika maisha ya watu. Huo ndio msimamo wangu tangu awali nashukuru umeliona hilo.

Nilichokifanya ni kuweka sawa maneno ya Gamba la Nyoka kuwa uzinifu umezungumziwa katika dini moja.

Kuna hoja nisiyoeleweka na naomba niiweke sawa hapa. Ni kweli mwenyeikiti anapaswa kuwa role model kwa kila kitu ndani na nje ya nyumba yake.

Japo sisi wote ni victims wa mambo uliyosema, inatosha kusema kuwa Mkandara akijimwagia chai hakuna atakayezyungumzia lakini mwenyekiti wa taasisi kubwa, hiyo ni habari kama tunavyoona

Silinganishi uadilifu unaotakiwa, ninalinganisha nia ya waraka kwa uadilifu uliosemwa.
Kama ipo hoja ya Mwenyekiti kutenda kinyume kama ilivyoelezwa hilo halikuwa na tatizo.
Tatizo ni pale ambapo waraka umedai kuwa MM akifanya mambo ya mapenzi yawe ya siri.

Tunafahamu kuwa waraka ulikuwa umelenga kumwandaa MM kama mwenyekiti baada ya huyu aliyepo. Ukisoma between the lines waraka unatoa loophole ya mwenyekiti mtarajiwa kufanya mambo kwa siri.

Hakuna mahali waraka umeeleza kuwa akishaoa(kama tajaaliwa) aache, la hasha, ulichofanya ni kumshauri mwenyekiti mtarajiwa kufanya mambo ya mapenzi kwa siri.

Ikumbukwe kuwa waraka ilikuwa ni dira ya CDM in future, hivyo kusema MM a.k.a mtarajiwa afanye mapenzi kwa siri ilikuwa ni kumuasa kuwa yeye anapaswa kufanya mambo kwa siri bila kuweka mpaka lini aache.

Kama CDM inataka kujengwa kwa misingi ya imara haiwezekani kuwe na loophole hizo.

Niltaraji waraka ungesihia kwa mwenyekiti na hapo nisingesema kitu kwa kuamini kuwa wanachora mstari wa nidhamu kwa aliyepo na ajaye.

Kitendo cha kusema yeye afanye kwa siri mimi nakitafsiri kuwa mapungufu yake ayafiche asifanye kama huyu wa sasa. Hapo hakuna moral ya kukemea jambo moja na kulifanya kwa mkono mwingine.

Naomba niweke sawa,sina utetezi wala kulinganisha makosa kabisa.Na hakuna mahali nimesema kilichofanyika ni sawa.

Ninachokifanya ni kuuangalia waraka katika muktadha mzuri hasa kipengele cha ''intent.
'
Je nia ya waraka ilikuwa kujenga nidhamu ya kudumu ya CDM? Kama ilikuwa hivyo vipi kuwepo na 'provision' ya kumruhusu Kapera aliyekuwa anaandaliwa kuwa mwenyekiti afanye hivyo?
Je, nani anaweza kusema kwa dhati kuwa laiti angefanikiwa kuwa mwenyekiti basi angekoma katabia hako.

Nani anaweza kusimama na kuniambia kuwa ufuska wa mwenyekiti mwenye ndoa ni mbaya zaidi kwa taswira ya chama kuliko mwenyekiti Kapera?
Nidhamu inaanza na kuishia wapi katika suala la maadili?
nguruvi3,

Mkuu ni bahati mbaya tu huu waraka umewekwa wazi kwa wananchi lakini swala la Usiri ktk maisha ya kila mtu na hasa viongozi ni wajibu. Hata mimi hapa ningemshauri Mbowe afanye mambo yake kwa siri kama ningekuwa ktk washauri wake maana siwezi kumfunga kamba ya shingo kama mbuzi japo itakuwa vizuri sana kama hatafanya kabisa.

Nikuchekeshe, kuna rafiki yangu ujanani nilimwambia asi fall in love na demu alompenda nikijua ni kibaka, Jamaa yangu akanambia hutaki nitembee naye, sasa unataka nitembee na wewe? mkuu nilinywea nikawa mdogo japo miaka ilofuata huyo Binti alimfilisi kisha akatoka na mtu mwingine rafiki yetu vile vile - Jamaa chanu, hakuyaona niloyaona miye! Ushauri kwa wahusika muhimu japo ukiusoma ktk maandishi utahukumu tofauti kabisa.

Kwa hiyo huo waraka ukiusoma ni maandalizi ya kundi hili wakimtaka huyo, awe kiongozi wa aina hgani tofauti na aliyepo maana kufikia mtu kuitwa Malaya ina maana alishindikana. Tuyaache haya kama yalivyo ila tu nasisitiza ya kwamba wewe unausoma waraka huu kwa imani tofauti kama vile unasoma Kuran wakati wewe ni mkristu kutafuta makosa ama sura inayojikanyaga. Utaziona nyingi sana lakini ukipewa darasa na waislaam wenyewe utagundua kuran haikuwa na maana hiyo!..

Mwisho nasema, ktk swala hili kusema kweli tumekoga ktk maji ya tope, na haikutakiwa kabisa kufikia hapa tulipo. ZZK ana kiburi maana anajua uchungu wa hii Chadema mnayoiona leo ambayo wengi ya wakuja wanalia kivulini tu..Na kwa bahati mbaya tumeingia kiburi, Mbowe ana makosa yake kama kiongozi kwa sababu hakuwahi hata siku moja kumtamkia ZZK mbele yake isipokuwa hutumia watu wengine kuanzisha vagi hao kina Lema na wengine ktk gazeti la Daima. Nimekuwa nikifuatilia sana msuguano huu na hivyo ninazo kumbukumbu nyingi sana ambazo nilizifanyia utafiti wangu na kujua kuwa kitulacho kii nguoni mwetu. Chadema kuna Kirusi kama alivyosema Pasco na ipo siku kitadhihirika na watu mtakosa pa kuficha uso wenu japo itakuwa too late!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom