Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Mwalimu # 291 Watu hawataki kujadili contents, context na intent ya waraka kwasababu wanataka kujenga balance ya makosa ya watu.
Wanataka kuweka hoja za uenyekiti ili kumwepusha awaye na tuhuma zinazo mkabili.
JokaKuu # 292 Kuwazuia ZZK na Mbowe hakutaleta amani. Amani ni zao la kufuata sheria, taratibu na maadili.
Lakini pia itajenga bad precedent kuwa ukimchukia kiongozi endesha mapambano ili iwe mwaga mboga mwaga ugali.

CDM kama taasisi ya kisiasa inapaswa iwe na mlolongo wa watu wanaoweza kujaza nafasi za uongozi
Kwa vile CDM imejengwa kwa personality itabidi wapate personality nyingine, jambo la hatari sana na sasa linaonekana wazi.
Mkandara #295 inagawa umenizuia nisiseme option ya kujiuzulu, mimi nikikuta madudu kama uliyoyasema kwanza naweka wazi ili nitimuliwe, ikishindikana najiweka pembeni.
Lakini kwanza nitasema kuna tatizo na kulionyesha. Siwezi kwenda vichochoroni kama kiongozi nikinung'unika .
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wana jamvi na duru za siasa.
Kwanza taarifa hii haijakanushwa na uongozi wa CDM au idara yoyotE na inabaki
ilivyosambazwa katika .
Pili, Chadema wamesema wazi wahusika wamekiri kuhusika na habari hii
Tatu, tunafahamu kuwa watuhumiwa watakuwa na kikao kujibu yaliyoelekezwa kwao na wanahaki ya kusikilizwa ili kupata ‘habari iliyo na uwiano'

Itakapodhihirika kuwa taarifa hii haina ukweli, wahusika kuikana ,uongozi wa CDM utapaswa kujiuzulu kwa sababu ni kosa la kukosa imani, kuvunja uaminifu, kudanganya, kuhadaa na kupaka watu matope.

Kwa wakati huu tutaijadili habari hii kama ilivyoletwa.

Tunafahamu baadhi ya maoni yataweza kutumika katika kujenga au kujibu hoja kwa mikutano kati ya watuhumiwa na wana habari, hilo halitaondoa ukweli kuhusu tunachokiona hakikufanyika, kimefanyika, kina ukweli, kina udanganyifu au upotoshaji.

Tusimame katika ukweli tukiongozwa na fikra wala si hisia, chuki kwakuelewa kuwa upinzani ni sehemu muhimu`ya ustawi wa demokrasia na maendeleo ya nchi yetu.

Post inayofuata tutaanza kuchambua hoja moja baada ya nyingine bila upendeleo au uonevu lakini pia bila huruma au ushawishi wa namna yoyote.

Wana duru lets get strated
Mkuu wangu mbona umeshachagua upande kwa kusema WATUHUMIWA ni kina nani ktk mjadala huu wakati hao unaowaita watuhumiwa ndio waliowatuhumu kwanza viongozi wetu? Kwa nini tusiuzome huo waraka, tuwajua watuhumiwa ambao ni uongozi na wao ndio wajibu maswali yaloanikwa humo kisha ikiwa ni uongo ndio turudi kwa hawa walio andika huo waraka. Na kama kuna ukweli watuhumiwa wajiuzuru wao maana binafsi yangu njia zote zilizotumika ktk kuupata huu waraka na hata kufanya maamuzi ya haraka kupindisha kila kanuni na sheria za chama kinachofuata demokrasia na kweli. Bila shaka tusipokubalianamimi na wewew ni hapa kina nani - WATUHUMIWA.

Pili, nirudi ktk swala langu ulolijibu hapo juu, nafikiri unakumbuka toka enzi ya Chacha hakuna geni liloandikwa ktk waraka huu na kibaya zaidi inanitisha sana maana huyo Chacha ilipojulikana tu kwamba anaandika waraka alitutoka! Sikutaka kuamini kabisa kwamba CDM ilikuwa na madudu haya yakiendelea ndani na kwa jinsi inavyoendela kujitokeza inatupa mashaka zaidi.

Kwa hiyo kama wewe utakuwa waziri wa maliasili na ukajaribu kuweka wazi sijui wapi na katika kikao gani kumshutumu rais, na marais wastaafu,mkuu wangu sidhani kama utaupata hata huo mwanya. Kuna utaratibu wa kichama au vikao ambapo hoja kama hii hufikishwa kwanza kwa Mwenyekiti akaipitisha ili upewe muda wa kuzungumza. Muda huo hutaupata na habari haitaishia hapo bali itawafikia wote wenye hizi deal - hapo UMEKWISHA! kama alivyokwisha dada yetu Amina alosema wazi kwamba anampa rais list ya wauza unga na isipotolewa na rais yeye mwenyewe ataisoma ktk vyombo vya habari. Muda hupo hakupewa na wala sii yeye wa kwanza wapo kina Kolimba, Mwaikambo, Kombe na kadhalika wote hawa walifikiria njia hizo halali na kujiuzuru kuwa ni maamuzi ya busara. Busara hiyo imewapeleka kaburini!

Njia pekee ya kuweza kupambana na Ufisadi kama huu ni kujiandaa na mtandao wa siri ndani ya chama kama walivyofanya kina JK na EL (Boyz to Men) tukidhani kwamba wamekuja kuyaondoa madudu yote ya Mkapa na ndivyo JK alivyotunanga na maahadi yake ya mwanzoni. JK alipata kura nyingi sana uchaguzi wa mwaka 2005 kutokana na dhana hiyo, na haikutokea CCM kumchukulia hatua JK wala Lowassa maana mbinu zilijuliakana mapema kabla ya uchaguzi, na hapa JF tukimwagiwa mboga na Mzee Es nadhani mnakumbuka. Na leo hii bado EL anaendesha kampeni zake ambazo zimetuletea baraza jipya la mawaziri ambao wamepangwa kufuatia uchaguzi wa mwaka 2015 na wasokuwa ktk mtandao wamepigwa chini.

Kwa CCM wao wanajua chama hakina mvuto tena, na hakuna dawa kwa maskini zaidi ya Takrima hivyo Ufisadi wao unakubalika na weng ndani ya chamai. Kwa wanaopinga, watu kama Mnauye hawatapendwa na ninakuhakikishia kwamba huyo Mnauye atachukuliwa kama ZZK wala sii muda, maana walomtangulia wote walifikiri wanaweza kukibadilisha chama ktk kupambana na ufisadi.

Kwa hiyo nyie endeleeni kusubiri sheria butu maana unaposema Upinzani ni sehemu muhimu ya ustawi wa demokrasia wakati Upinzani huo huo unakataliwa usichukue fomu kugombea, unapigwa vita ndani hata kulitaja tu jina la mhusika, kusiwepo na mikakati ya siri wakati upande mwingine wanazo siri zao - sijui ni demokrasia ipi tunayoizungumzia. Tanzania hatuna demokrasia wala hatuna mfumo unao elekea kuwepo kwa demokrasia isipkuwa tunachagua VICHWA na ndio maana leo swala la mgombea binafsi linapewa kipaumbele zaidi.

Mwisho, nakuomba sana rudia kusoma waraka hasa sehemu yenye kichwa cha habari - VIKWAZO DHIDI YA TUNAYEMTAKA. Hapa utaona wazi kwamba wakati waraka huu unaandikwa ZZK alikuwa bado hana Habari wala hajahusishwa na pili utabiri wa mwandishi kwa yanayoduata, umejitokeza wazi kabisa siku za hivi karibuni tena sentesi kwa sentesi kama vile hawa watu walijua kinachokuja. Sipendi kabisa kuamini kwamba Mbowe ni mtu wa aina hiyo maana binafsi nimemkubali toka siku niloongea naye binafsi akiwa DC na pale alipokubali kutogombea urais mwaka 2010 kuwachia Dr.Slaa. Huyu mtu siwezi kuamnini ana uchu wa madaraka hata kidogo japo naanza kuamnishwa na matokeo ya vikao vya kamati kuu ambakjo binafsi naamni kuna Kirusi kama sii virusi.

Ningewaomba tu viongozi wa Chadema na hasa Mbowe na Mbunge Zitto wakae wenyewe wafikirie hili naloandfika sasa hivi:-
Ikiwa kila mmoja wao anazo habari za mwenzake kuhusu kupewa fedha na Mkono, Rostam na sijui CCM wakati kila mmoja wao anajua fika kwamba sii kweli inakuwaje watu hawa wanashindwa kuunganisha kwamba watu wenyewe ndio hao hao inakuwaje watoe huku na huku na habari ziwafikie kila upande kwa wakati tofauti?. I mean kama leo hii mtu anambie Nguruvi3 kahongwa na Mbowe, Chadema ili kuitetea kamati kuuu ya chama ilihali Nguruvi3 anadai ama anajua hakupewa hongo hilo isipokuwa naye kaambiwa na mtu/watu walonambia mimi kuhusu yeye ya kuwa je unajua kwamba Mkandara kahongwa na Zitto na Kitila ili kuwatetea hapa JF?. halafu tuamze kuto aminiana - Jamani hamuoni kama mnachezewa vichwa?..

Mbowe na Zitto nyie sii watoto wadogo, sisi tusokuwa ndani ya uongozi wala huko makao makuu tulizipata habari za mujini ya kuwa Chadema imepokea fedha za CCM kupitia Rostam ili kukiwezesha chama kisimamishe wajumbe zaidi ktk majimbo ya CUF maana hofu kubwa ya CCM ktk upinzani kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005 ilikuwa CUF, na hivyo mbinu ya kuitumia Chadema ili waweze kukimaliza chama hicho cha CUF. Na ndio maana Mbowe akawa jembe kupitia vyombo vya habari na Chadema kuja juu ya CUF tukakamata majimbo hadi ya Kigoma kwa Zitto. Mbona sisi hatukuziamini habari hizi na tumeendelea kuwaamini viongozi?

Sasa iwe kweli habari hizi ama uongo mimi sitaki kujua isipokuwa nachoelewa ni kwamba Chadema imelishwa sumu na hata wakifanya nini chama hakiwezi kupata amani hadi hapo viongozi watakapo jiuliza KWA NINI HATUAMINIANI na nani mchawi wetu? wakisha mpata mchawi watagundua kwamba mbinu za CCM ndizo zimewafikisha hapo walipo. Walichofanya CCM ni kupiga ngoma ya msukule, walocheza ni wachawi na wengine wasojua maana. Msafara wa Mamba hata Kenge wamo!

Mbowe, Zitto na wazee wa Chadema nisomeni na hakika habari za mjini haziwezi kuwa uongo mtupu na tungo isipokuwa kuna ukweli mkubwa kwamba mmechezewa akili na CCM..
 
Last edited by a moderator:
Kuna option nzuri zaidi ya hiyo?
Bila shaka unless unataka kunambia wewe sii Mwanasiasa unayeitakia Tanzania mema na sii kujifikiria wewe binafsi pasipo ushindani maana ukijiuzuru hutabadilisha kitu madudu yataendelea kuimaliza jamii. Tofauti baina yetu sisi na kina Nyerere na Mandela ni hiyo mkuu wangu wao hawakubali kushindwa inapofikia swala la haki,usawa kwa watu wao. Unapokata tamaa basi wewe siasa haikufai wala sii mwanasiasa kabisa katafute profession nyinginezo!
 
Nguruvi3, nafurahi kuwa ni mengi ambayo tunakubaliana tunapokuja yale ambayo yanahusiana na Chadema. Likija suala la Waraka tunapishana padogo tu. Unazungumzia Waraka kuwa haramu na kutupia lawama zote kwa akina Kitila, kwa kukusoma hapa kaka naona kana kwamba hutaki kwenda nje ya (a) Kuona waraka ni Haramu (b)Kulaumu akina Kitila Mkumbo kuuandaa.

Tukienda hatua kwa hatua; hayo mimi nakubaliana nayo (a) & (b) ikiwa tunalitazama hili suala kwa ‘Right’ and ‘Wrong’ ila tu mimi nataka tuende Zaidi ya hapo kaka. I am sorry to say this; ila kiukweli umewapa credit kubwa sana akina Mbowe and Company na kuwanyima kabisa Kitila and Company. Hapa ndipo tunapishana. Mie nakubali waraka ni haramu na waandaaji ni sawa kuadhibiwa – LAKINI naenda a step Zaidi; yaliyomo kweye waraka (tuhuma kwa viongozi) yazingatiwe na kufuatiliwa (na body nje ya uongozi) . Yakizingatiwa yatatoa majibu yote… Naamini hivyo.

Ok, ume insinuate mahala Kitila alipwaswa ajitoe nafasi aliyopo endapo alikua hakubaliani na yale ambayo viongozi waliopo juu yake walikua hawafanyi? Naomba nikuulize haya;


  1. Huoni kama kujitoa ni dalili ya mtu kukata tamaa haraka katika kutaka kuleta mabadiliko chanya? Kwa mtazamo wake aliona kuwa hao viongozi wanaharibu; giving Mkumbo benefit of the doubt (tokana na umakini na busara aliyo onyesha siku zote huko nyuma)ni wazi katumia njia zote ambazo ni sahihi na hazikuzaa matunda – Unaniambia kuachia ngazi ndio ilikua njia sahihi? Nakataliana na wewe katika hilo! Change haiji kirahisi hivyo, ni lazima upiganie kuweza kufanikisha hasa kama imelenga kheri mwisho wa siku. Kuna msemo wa mmoja wa Thomas Jefferson unaingia vizuri hapa! ““The Democracy will cease to exist when you take away from those who are willing to work and give to those who would not.” Hiki ndicho kimetokea Chadema. Na hiki si kwa Chadema tu! Tunapoelekea tokana na kukosa Chama makini ambacho ni mbadala wa CCM ili waweze kung’olewa madarakani, kuna hatari kikatokea kwa upana hata CCM.
  2. Ki mantiki na kwa misingi ya haki; toka kumkamata Mwigamba, kutangwazwa kupatikana kwa Waraka hadi kujulikana kwa MM wote - Nini maoni yako ya namna hili suala lote limeendeshwa na maamuzi yaliyotolewa? Unakubaliana na hatua na maamuzi yote yaliyochukuliwa na viongozi wa Chadema pamoja na CC kwa ujumla?

Tukija suala la Mwigamba; mfano mzuri sana ambao pia Chadema walikurupuka. Mwigamba aliweka mada hapa JamiiForums iliyo gharimu nafasi yake ya Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha kwa kupitia jina ID name ya Maskini Mkulima. Aliweka mada ya “Kwa nini mabadiliko Chadema ni ya Lazima” ikiwa ni mwendelezo wa mada (WITO KWA CHADEMA) October 25, saa 18:56 (kama post inavyo onyesha) - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/540858-wito-kwa-wana-chadema-wote.html#post7652142.

Siku hiyo hiyo saa 23:53 Kurugenzi ya Habari ya Chadema ikatangaza kumsimamisha nafasi ya uongozi - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...baada-ya-kukiri-kusema-uongo.html#post7654260.

Naomba tuliangalie hili na tulitafakari kwa kujiuliza haya;


  1. Ilisemekana kikao cha Baraza la Uongozi kilikaa na kujadili. Baraza la Uongozi wa Chadema ni akina nani? (Kwa haraka haraka habari siku hiyo zinasema aliyekuwepo hapo ni Mbowe, Lema, Israel Natse, na viongozi wengine wa hapo Arusha) ndani ya masaa 3, mhalifu kakamatwa, waamuzi wamesha mobilise na maamuzi kuchukuliwa?
  2. Why maamuzi ya haraka hivyo? Ikiwa tayari walishachukua PC yake, tayari ishajulikana alichofanya, Kiongozi mkubwa kama Mwigamba hasa ukizingatia katoka eneo ambalo Chadema lina influence kuliko sehemu yoyote nchini – Walikua wanakimbizwa? Hapa ndio huwa nashangaa pale followers baadhi wa Chadema waki condemn viongozi wengine kutumia mitandao ya kijamii na hali pia wapo so Active.
  3. Nguruvi, naamini wengi hawajasoma content ya Mwigamba, na wengi hawajajua hasa ni ipi mada ilifukuzisha. Ukisoma hiyo content yake unapata picha ipi kuhusu Chadema na Uongozi wake? Unaichukulia vipi hiyo content – Kweli/Uongo/nusu ukweli ama nusu Uongo?

Disclaimer:-

Uwakilishi wangu wa suala hili la Mwigamba, Sina maana kuwa Mwigamba hakustahili kuvuliwa Uongozi. Nimetaka tuangalie utendaji wa such cases na viongozi wa Chadema na zaidi nataka tuende a step ahead – Kwa nini akili, maoni na maudhui mengi yanaelemea kutaka kuliangalia tendo na mtu mwenye ila hakuna anae taka kurudi kwenye contents za hivi vitu ili kuwaelewa viongozi wa Chadema na Chadema yenyewe?

Nina concern; Kuna mahala ambapo sijakuelewa ama nimekuelewa vibaya. Nguruvi una maana unasema matatizo yote yakivurugu yaliyopo CDM sasa causative ni ZZK? Take note nilipokua naungumzia suala la shades of grey nilikuwa silengi tu Zitto; I meant utendaji wa ujumla..
AshaDii , naomba nizirejee hoja zako hasa tunazokinzana.
Kwanza kabisa mimi nauangalia waraka na waliohusika.
Hakuna mahali nimetoa credit kwa kundi la Mbowe zipo sehemu nimelaumu uongozi kwa ujumla

Pili, nijibu hoja yako na ya Mkandara kwa pamoja.
Kulikuwa na njia nyingi za kufanya ili wao kueleza wasiokubaliana nayo.
Kutumia vikao, Kutumia mikutano, kujiuzulu nafasi zao na hata kuwashawishi viongozi wengine kuona kile wanachodhani ni sahihi. Kwa bahati mbaya baada ya kukamatwa waraka ndipo wakakumbuka kujiuzulu.

Kitendo cha kujiuzulu baada ya waraka kukamatwa kutambua kosa na uharamu wa walichotaka kukifanya. AshaDii tunakubaliana, Mkandara bado anaamini waraka hauna uharamu wala mawaa.

Mkandara, kufanya kampeni za kisiasa ndani ya vyama ni jambo jema.
Kuandaa mkakati wa kampeni ni jambo jema.

Kinachotatiza kwa hili la Mkumbo ni, kwanza contents za waraka hazina chembe ya kampeni zaidi ya mipasho, Pili, maandishi hayana ladha na nia ya waraka ilikuwa mbaya.

Haiwezekani Kitila mshauri wa chama awashauri CDM katika vikao waandamane halafu arudi vichochoroni kukaa na ZZK na kujisifia kuhusu ubaya wa maandamano.
Huu ni unafiki ulipita kiwango achilia mbali udhaifu wa kisiasa.
Hivi kweli huyu mshauri wa CDM angeweza kulaani kile anachowashauri CDM?

Walichotakiwa ni kukaa pembeni kwanza ili waendeshe kampeni. Kitendo cha kukaa katika vikao wasivyokubaliana navyo na kuandika waraka ni kutengeneza kitu haramu.
Kuingia katika vikao halali kunajenga uharamu wa vikao haramu.

AshaDii kujiuzulu nafasi zao hakukuwa na maana ya kuisusa demokrasia. Ironically kulikuwa na maana ya kujenga demokrasia. Jana kiongozi mmoja Uganda amesimama a kusema atagombea dhidi ya M7 au vijana wake. Hakujificha alisimama katika microphone.

Demokrasia si bahari isiyo na ukomo, demokrasia ina taratibu zake ambazo akina zzk hawakuzifuata. Walikumbuka kuzifuata baada ya waraka kukamatwa.

Kitendo cha CC kupitisha hukumu haraka kilitokana na ukweli kuwa walitaka kujiuzulu ili kuficha ukweli, isingekuwa hivyo wasingeandika barua za kujiuzulu.

Kuhusu maamuzi kwa msimamo wangu nilisema CC ilifanya makosa na ninasimama na hoja kwamba, kitendo cha viongozi kuwa ndani ya CC kitawapa wapenzi na manazi wa Zitto na Kitila sababu. Ndicho kinachoonekana sasa hivi.

Nilisema kitafutwe chombo huru ili kuliangalia tatizo kwasababu haitawezekana manazi wa ZZK kukubali hadi watakaposikia pengine kutoka kwa malaika.

Kosa la pili ni kitendo cha kuziba nafasi za ZZK. Hakukuwa na sababu tukizingatia kuwa ZZK alikuwa hana kazi kwa maana alishajitoa. CC hakuhudhuria akijua kuwa walichokifanya ni uhuni. Nilihoji mbona nafasi ya makamu hawajaijaza?

CC ilikaa kwa jazba, na matokeo yake wakafanya kazi nusu nusu na ndicho kinachoendelea.
Kulikuwa na njia mbili, kwanza kushughulikia tatizo na kufikia hatima muda mfupi sana.

Au kutafuta chombo kingine kishughulikie mgogoro huo ili pengine wapenzi wa zzk waone haya kidogo maana hawana soni.

Hawana soni kwasababu hawaamini kuwa ZZK ni tatizo la muda mrefu akijificha nyuma ya watu.
AshaDii katika migogoro iliyowahi kuikumba CDM nipe mmoja tu ambao ZZK hana mkono.

Kuanzia 2011 nimewaonya CDM kuwa ZZK anakuwa zaidi ya chama, sasa wanavuna grey zone walioipalilia kwa muda mrefu.

Kuhusu Mwigamba, la la la, hii nayo ni aibu. Mwenyekiti wa mkoa yupo bize kutoa taarifa za vikao mitandaoni sasa mashabiki watafanya kazi gani. Huyu naye ni shujaa na mwademokrasia kweli!!
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Mkuu wangu waraka ulikuwa siri kama ilivyokuwa siri ktk utendaji kazi na matumizi ya ndani ya chama. Labda nitumie mtazamo wako na kusema ya kwamba Zitto, Kitila na wengineo wanaoitwa kundi la ZZK walifichwa vile vile ktk maswala ambayo waraka umeyagusia. Kama kweli ilikuwa uongo nina hakika kabisa viongozi waliopo wangeweka kila kitu wazi kuwasuta wakionyesha ukweli ili uongo ujitenge lakini wameshindwa na wameshindwa kwa sababu wanajua kuwa siri nzima imefichuka kama alivyoshindwa Kitila ktk kikako cha chama.

Tatizo kubwa la Chadema sasa hivi ni Zitto ambaye hakubali kumalizwa, yuko tayari kumwaga mboga tofauti na kina Kitila. Na hii ndio athari nilikuwa nikiizungumzia kila mara humu JF japo sikuwa muwazi zaidi. Chadema haikutakiwa kufikia hapa ilipo leo kwa sababu tu ya kugombania nafasi ya uongozi. Na nitasema tu kwamba Uharamu wa yote haya ni ile ari ya kila mmoja wao kutaka kuwa kiongozi wa Chadema kutokana na mfumo walokuwa nao ambao unawapa Ulaji. Kiongozi wa chama ndani ya Chadema ni hatua moja mbele inayokupa nguvu kubwa ya kujitangaza majukwaani kupata umaarufu ambao utamsaidia mtu ktk uchaguzi wa kitaifa.

Watazame hata vijana wake utawaona kila siku wanagombea nafasi ya uongozi BAVICHA,na wakishapata tu kesho wanagombea Ubunge! zaidi ya hapo kiongozi yeyote wa chama hata bavicha tu, ana sauti kubwa kitaifa kuliko wanachama wenye uwezo wa kiutendaji. Hivyo basi ni mfumo uliopo ambao unavuta shari zote hizi laa sivyo hakuna mtu angependa kuwa Mwenyekiti wa chama ikiwa mwenyekiti huyo angekuwa mtumishi wa chama tu na sii kuwania Ubunge, Uwaziri ama Urais maana pasipo kujijua hawa watu wanajipanga utafiri Chadema itachukua nchi kesho.

Mwisho labda nikuulize wewe swali moja. Huu ni mfano tu nautoa na sii hali halisi maana sijui ukweli ni upi..
1. Ikitokea Ukateuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, kisha ukakuta kuna madudu yanafanyika humo na wahusika wakuu ni JK, Mwinyi, Mkapa na viongozi wengine wakubwa wa CCM - Utafanya nini?
- Usinambie utajiuzuru tafadhali!
@Mkandara waraka ulikuwa ni siri, umeingia katika public domain kama kidhibiti.
Nasema kila mara, waraka hauna tatizo kama ungeandikwa na mashabiki na manazi. Umeandikwa na Mshauri mkuu wa chama akiwashirikisha Mwenyekiti wa Mkoa na Naibu katibu mkuu. Hawa wote ni viongozi wanaoingia katika vikao vya maamuzi makubwa ambayo hawakubaliani nayo. Kuingia katika vikao ilikuwa kutafuta siri za CDM na wala si kujenga CDM yao. Hapo ndipo uhuni na uharam wa waraka unapoanzia. Huwezi kuwa na halali iliyotokana na haramu mkuu.
Kitendo cha kuingia vikao kama ma spy ni uharamu, sijui wataandika nini chenye uhalali wakati wao wameshatenda uharamu. Hata wao walijua hilo ndio maana walikimbilia kujiuzulu wakijua ni aibu, soni na haya na kwamba umma hautawaelewa isipokuwa wachache waliogoma.

Sidhani kama ZZK anawazo la kumalizwa. Mbona alianza siku nyingi kwa akina Kafulila, Juliana, masalia n.k.

Huyu ndiye anayeimaliza CDM na nakuhakikishia historia haitamwandika ZZK kwa ukamilifu kama haitaeleza jinsi ambavyo amekuwa anajitumia au anatumika kuvuruga Upinzani.
 
Mag3 nashukuru kwa maoni yako. Nakubaliana nayo kabisa, ila bado mie msimamo wangu upo pale pale kua yapaswa hata yaliyomo kwenye waraka kutiliwa maanani in relation na wale walio husishwa.
Ni kwa misingi hiyo silaumu maamuzi ya Viongozi wa Chadema ingawa bado wana mapungufu makubwa kwa namna walivyo liendesha suala zima.

Mag3 naomba nikumbushe kuna tofauti kubwa ya kujenga chama nje ya chama na kujenga chama ndani ya Chama. Upande wa Chadema naweza nikasema wanafanikiwa kujenga chama nje ya chama chao lakini jitihada hizo ni hafifu ndani ya chama kiasi kwamba hata kinawadhoofisha once in a while. Hivyo in this case hatuangalii hilo kwa akina Kitila.

Kuelewa juhudu zao katika kujenga chama ndani ya chama - hapo ndipo tatizo linakuja, hatuwezi kujua ni juhudi zipi zilifanywa bila kuwauliza wao moja kwa moja.

Hilo linatufanya watazamaji tujigawe katika makundi mawili. (a) wale ambao wanaamini Kitila & Co walishafanya juhudi nyingi ikashindikana hadi kuwasukuma kuuandaa waraka. (b) wale ambao wanaamini moja kwa moja kuwa hakufanya juhudi zozote alichagua tu njia ya kuandaa waraka. Whatever the case akina Kitila wanaelewa Zaidi hapa kuliko yeyote anayeweza liwakilisha hapa.

Kuna hoja za kujibu sana; hizo hoja ni nzito na ni hoja ambazo zimekua zikijirudia mara kwa mara. Hoja ambazo ikiwa kuna vielelezo ilipaswa tu viwekwe sawa. Hasa katika vipengele vinavyohusiana na pesa… Mana tunajua fika kiongozi yeyote yule ambaye ni mroho wa pesa na anajiingiza kujinyakulia pesa ambazo si zake kwa njia ambazo si halali – Ufisadi katika uongozi wake hauepukiki! Kwa maneno mengine kiongozi kama huyo akichaguliwa kuiongoza nchi kutakua hakuna tofauti na sasa.

Madai ambayo yanapaswa kufuatiliwa kwa karibu na kutolewa ufafanuzi ni haya;
  1. Matumizi ya pesa ya taasisi – Chadema siyo ya watu watatu tu (so far ndio watu wanaojua matumizi hayo ya pesa yanavyoenda); kwa taasisi kubwa kama hiyo ni lazima iwe accountable hizo pesa zinatumika vipi, na record ya matumizi hayo yawe public (hilo ni wazi na halina ubishi); kama waraka unavyojieleza, maamuzi na matumizi yapo mikononi mwa wachache. Hilo ni tatizo kubwa else kama mnali underestimate ukubwa wake.
  2. Njia haramu za kubaki Madarakani – Na hili kwa mtazamo wangu ndio linaleta matatizo makubwa Chadema; Uongozi wa juu, upatikanaji wake na ushiriki wa wengine katika nafasi hizo. Kwa wale ambao huwa mnafuatilia habari hapa JF mara kwa mara liliwahi kuletwa hili hapa kama tetesi (kua Viongozi wa Chadema kuna kipengele wamekitoa katika katiba ya Chama ili ku prolong muda wa uongozi uliopo), na mdau aliyeleta hii habari alitukanwa sana kuwa katumwa. Kwa haraka sana tokana na udhaifu wa Chadema ya kila mmoja kutaka kuwa msemaji - Hiyo habari ilikanushwa haraka na mmoja wa viongozi wa Chadema. Habari ililetwa tena safari hii ikiwa na ushahidi wa Kipengele kilivyokuwa awali na kilivyo sasa (baada ya kubadilishwa), hapo sasa Chadema wakaja na utetezi wa kwa nini hicho kipengele kilirekebishwa, safari hii wakikubali kua mabadiliko yalifanywa. Mag3 hayo mambo madogo madogo, yakikusanywa ndiyo yanayozidi kui discredit CHADEMA.
  3. Baadhi ya utendaji wa Uongozi mkuu.

Maoni yako haya naomba niende na wewe tofauti. Believe you me Chadema kama taasisi kubwa walikua na uwezo wa kuwamaliza akina Kitila & Co. kwa njia alternatives na taratibu ambazo zingekua ni za kujenga kuliko kubomoa.

Hivi unadhani kuwa baada ya wao kujulikana nia yao wangetengwa huko na kutupiliwa mbali bila kuhusishwa kungekua na tofauti yoyote ile na kama walivyofukuzwa? Inawezekana ndio wamefanya sawa ila huu ulikua si wakati wake. Hawajawa calculative, na ndio narudi pale pale hilo ni tatizo la kutazama mtu badala ya kuitazama taasisi. Na ndio maana kunakua na discussions za kiongozi is bigger than Chadema. Kufika kote huko kwa namna moja ama nyingine hiyo ni insult kwa Chadema as a whole na si sit u kwa viongozi wa CHADEMA.
AshaDii ahsante kwa maoni yako.

Juhudi za kujenga vyama vya siasa ni ndani na nje. Kwa upande wa ndani juhudi hizo zilenge katika kukiimarisha chama na si kukidhoofisha. Akina Kitila hawakuwa na lengo la kuimarisha chama. Ingekuwa ni hivyo wangesimama wazi na hadharani kueleza kile wanachokiona si sahihi ikiwa ni pamoja na hayo uliyoyasema.

Hawakufanya hivyo na kwenda kinyume kabisa cha misingi ya kujenga chama na pengine kujikita katika kukibomoa kama wanavyofanya sasa hivi.

Hizi kauli za akina Kitila kuhusu chama mbadala au za ZZK kuhusu ufisadi ni matokeo ya kile walichokuwa nacho rohoni siku nyingi.

Laiti wangefukuzwa kwa kusema hadharani ningewaelewa sana. Kitendo cha wao kuwa washauri na naibu katibu mkuu, kuingia vikaoni na kwenda vichochoroni kuandika mambo tofauti na yale wanayozungumza katika vikao ni usaliti, upungufu wa maono achilia mbali udhaifu wa kisiasa.

Nimekuwa natolea mfano wa Filkunjombe na Kigwangalla ambao wamesimama hadharani na kusema waziri mkuu wao hafai na wanatapitisha karatasi afukuzwe.

Hawa kwa njia moja au nyingine wanaijenga CCM kwasababu wanaeleza udhaifu wa chama chao jambo lisilowezekana kwa wengine ambao ninawafananisha na fisi.

Kazi ya fisi si kuwinda ni kufuata mizoga, leo tunataka tumwite fisi shujaa mwituni!!

Malalamiko yaliyoletwa hapa JF kuhusu ufujaji wa fedha na kuondolewa vipengele yanaweza kuwa na mantiki kabisa.

Tunauangalia waraka na kugundua kuwa waliokuwa wanaleta malalamiko ima ni akina Kitila and associates au waliwatumia watu. Kilicho wazi ni kuwa waraka unawiana sana na malalamiko hayo.

Sasa mshauri wa chama anapotumia njia za porini na naibu katibu mkuu anapotumika kupita njia za panya huoni hapo kuna tatizo la kujenga chama ndani?

Nani aseme kama si wao na lini basi walisema hayo. Na je kama walisema hawakusikilizwa ilikuwa muafaka kupitia mitandao kusema maneno mazito kama hayo.
Hapo walikuwa wanajenga au wanabomoa.

Kuhusu hoja ya kumaliza mzozo kwa kuwaondoa uongozi au kwa maneno mengine kimya kimya, hilo lisingewezekana hata kidogo. Haliwezekani kwasababu limejaribiwa likashindaikana.
Si ZZK ameongoza vurugu kama za masalia, Kafulila, Juliana na amevumiliwa, je ameweza kufanya tofauti na zamani?

Pili, hawa watu wameshajijenga sana katika CDM na hivyo kuendelea kuwepo kwao pengine kunge paralyse zaidi ya hali ilivyo sasa.

ZZK alipotimuliwa uongozi wakafuta makamu, Chatanda na yule wa Singida. Hao ni wachache tu. Bado wangeendelea na juhudi zao za kufikia malengo yao ya uongozi au kukiporomosha chama. Hizo ndizo nia zao kuu mbili.

Kwa hili nawalaumu sana CDM. Mwaka 2012 niliwambia kuwa CDM imejengwa kwa personality(s) na si wanachama.

Ingawa kinaonekana kukua na kuwa na wanchama wengi bado suala la personality linatangulia mambo mengine.Vinginevyo wasingekuwa hapa walipo.

Huwezi kuwa na chama chenye watu ambao ni zaidi ya chama. Hicho si chama ni mkusanyiko wa watu wenye lengo fulani.
Mchambuzi anasema ni Political movement kwasasababu political party ina utaratibu wake.
Amelisema sana hilo na kuhoji kama CDM imejengwa kama political movement au political party.

Political party inatofautiana na movement kwa njia nyingi. Movement huongozwa na watu kwa malengo fulani. Political party ina malengo yaliyo katika utaratibu yakiratibiwa kwa ufundi na kutekelezwa kwa umakini.

Kukosekana kwa nidhamu ndani ya CDM ambako ni tatizo la muda mrefu ni matokeo ya kushindwa kutofautisha kati ya political party na political movement.

Kama wanataka kuwa taasisi kweli kweli lazima wasimamie nidhamu ambayo haishii kuwafukuza viongozi tu bali kuweka kila jambo katika muktadha sahihi.

Hapa naungana na Mkandara kuwa huwezi kuwa na template ya CCM ukafanya tofauti na CCM. Wameelezwa siku nyingi kuwa wabunge na watendaji wa chama wawe wanapatikana kwa njia tofauti.

Hili ni tatizo kubwa la CDM kwamba imejengwa kwa template ya CCM. Nilitaraji wasomi wangeweza kusimama na kusema, wait a minute, karne hii mambo yanafanyika ABCD na siyo business as usual, like father like son.

Inasikitisha wasomi hao hao badala ya kuyaangalia mambo kutoka angle tofauti nao wanaendesha siasa za July 13 1947.
 
Last edited by a moderator:
Bila shaka unless unataka kunambia wewe sii Mwanasiasa unayeitakia Tanzania mema na sii kujifikiria wewe binafsi pasipo ushindani maana ukijiuzuru hutabadilisha kitu madudu yataendelea kuimaliza jamii. Tofauti baina yetu sisi na kina Nyerere na Mandela ni hiyo mkuu wangu wao hawakubali kushindwa inapofikia swala la haki,usawa kwa watu wao. Unapokata tamaa basi wewe siasa haikufai wala sii mwanasiasa kabisa katafute profession nyinginezo!
Mkuu Mkandara , kutafuta haki ni jambo moja, namna ya kuitafuta ni jambo lingine.
Hao akina Mandela na Nyerere walisimama katika vipaza sauti na kusema hiki ni sawa kile si sawa.

Ninakusoma unapojaribu kuwashauri akina Kitila kuwa haki haitafutwi kwa kujificha ficha na woga. Wao walishakata tamaa ndio maana hawakuweza kusema, wakarudi katika viunga vya minazi kuandika hayo tunayoyaona. Wamekata tamaaa!

Kwa mfano wako huo hatuwezi kuwa na genge la mitaani tukalipa hadhi ya kutafuta haki wakati halikusema linatafuta haki ipi na kwa njia gani. Haki waliyokuwa wanaitafuta ni ile ya 'Tunayemtaka'.

Baada ya kukata tamaa sasa wanasema wanatafuta mbadala.

 
Mkuu Mkandara , kutafuta haki ni jambo moja, namna ya kuitafuta ni jambo lingine.
Hao akina Mandela na Nyerere walisimama katika vipaza sauti na kusema hiki ni sawa kile si sawa.

Ninakusoma unapojaribu kuwashauri akina Kitila kuwa haki haitafutwi kwa kujificha ficha na woga. Wao walishakata tamaa ndio maana hawakuweza kusema, wakarudi katika viunga vya minazi kuandika hayo tunayoyaona. Wamekata tamaaa!

Kwa mfano wako huo hatuwezi kuwa na genge la mitaani tukalipa hadhi ya kutafuta haki wakati halikusema linatafuta haki ipi na kwa njia gani. Haki waliyokuwa wanaitafuta ni ile ya 'Tunayemtaka'.

Baada ya kukata tamaa sasa wanasema wanatafuta mbadala.

Mkuu wangu kusema kweli sikuelewi kabisa maana hao kina Nyerere na Mandela walianza kwa kujiandaa na bila shaka walifanya vikao vya siri na kuandika nyaraka zinazohuzu mabaya ya Ukoloni na wakapata wafuasi ndipo wakaanza kampeni zao.

Na ukweli tunao ktk historia yetu ambapo Nyerere alikuwa mtu waliyemtaka. Nyerere alifuata na kuambiwa kuhusu TAA na wanavyotaka uongozi wake huku akipingwa na kundi la Takadir. Laukama Abdul Wahid na Mwapachu wangesikiliza hizi chuki za kundi hili la Udini tusingekuwa na Nyerere kama rais wetu wa kwanza. Lakini haikuwa hivyo kutokana na busara na hekima zao. TAA haikusambaratika bali walojitoa na kuanzisha chama chao ndio walopoteza. Mandela ni picha hiyo hiyo naye alipendwa( walimtaka) akafuatwa na akaafiki....

Unachowataka kina Kitila ni ati waanze na kujitambulisha ktk vikao vya chama na kufanya kampeni pasipo maandalizi ya awali, jambo ambalo haliwezekani. Na nitarudia tu kusema waraka huu utakuwa na makosa tu ikiwa kuna UONGO katika madai ya hawa jamaa, lakini kama adai yote ni kweli, haya mambo yanatendeka ndani ya Chadema basi waraka ule haukuwa na makosa kabisa maana haukulenga kukivuruga chama bali kukiimarisha kwa kutaka kukomesha udikteta na uwekezaji ndani ya chama.

Mkuu unachekesha sana kuwaita hawa jamaa genge la mtaani unapotaka kufanya hivyo maana huko nyuma umewataja kama viongozi na washauri wa chama ambao walitakiwa kufanya kadhaa. Hii inaonyesha wazi kwamba unatafuta mchawi tu hakuna jingine. Wahuni ni wale wanaoficha hata mapato na matumizi ya chama kiasi kwamba sii kundi hili tu wameulaumu ungozi bali toka Chacha wangwe na kibaya zaidi inasemekana haijawahi kufanyika kikao kinachoelezea mapato na matumizi ya chama toka 2010 halafu mnataka kuarifiwa swala la kawaida kabisa ktk uongozi?.

Na wengine wote walofuatia kupingana na uongozi walikuwa na hoja zao wenyewe alichofanya Zitto ni kukubaliana na hoja zao wakitaka mageuzi. Na mbona mnashindwa kuzisema hoja zao kwanza isipokuwa makosa yao tu ndio hutangulia habari nzima?. Hii ndio demokrasia ndani ya chama mnakubali kukosoana, kurekebisha na kuwa wasikivu wa hoja za wadau msipoweza kufikia maamuzi kirahisi mnapiga kura. Sasa isiwe yule anayeunga mkono hoja msoitaka, naye anakuwa kundi la waharifu.

Haya imekuwa sasa Zitto ndiye anatumiwa kukiharibu chama, ebu tupeni basi ukweli wa taarifa zenu? mbona mnataka sisi tukubali tu kuwa ZZK ni fisadi wa chama na anatumiwa pasipo kutupa ushahidi isipokuwa tungo zenu mnapoamka asubuhi!. KIla siku mnajaribu kumharibia jina lake kwa uongo halafu mnafikiri sisi wote wajinga kama hao wanaokubali kulishwa?

Hivi kweli wewe unaamini toka Chacha Wangwe na viongozi wengine wote walojiuzuru kwa sababu hizi hiz hawakuwahi kuwakilisha maswala haya ktk vikao? na unaona ni vema kwa chama kuwa na hao walojiuzuru kuliko wale wanaotaka mageuzi ili kuhakikisha chama kinafuata sheria?..Hapa kusema kweli tutakesha, ni bora tukubaliane kutokubaliana maana kwangu mimi hadi siku uongozi wa Chadema watakapo wakilisha mahesabu(mapato na Matumizi) ya chama kwa muda ulodaiwa, watakapo badilisha mfumo wa kujuana, watakapo washirikisha viongozi wengine ngazi za taifa kufanya maamuzi ya bajeti ya chama ili kuwepo na mfumo9 unaweza kuonyesha wazi fedha zinatumika vipi na sii habari hizi za kuweka wake zao kuwa ndio wahasibu. Sorry to say that! Chadema inatakiwa kuwa chama cha watu wote na sii kundi la wale wanao aminiana kwa kujuana!
 
Mkuu Mkandara
Mbona sehemu kubwa sana tunakubaliana! Tunapopishana na pale unapoupa waraka uhalali wakati wenyewe walishakubali uharamu. Zzk na Kitila kutaka kujiuzulu ni ushahidi usiona shaka

Unasema walichosema ni ukweli, well, inawezekana.ZZK anatamaka ufisadi baada ya kutimuliwa. Kitila akitaka mbadala baada ya kutimuliwa. Kwamba wanayo mengi waliyahifadhi rohoni ili waendelee na uongozi si kwa nia ya kujenga CDM bali kumpata 'wanayemtaka'.

Nyerere alikuwa anapigana dhidi ya madhalimu, zake na za wenzake zilipaswa kuwa kubwa zaidi.
Unless uniambie ZZK na Kitila nao walikuwa wanapambana na madhalimu sioni sababu ya wao kushindwa kujitokeza na kusema hapa au pale kuna tatizo.

Ufujaji wa pesa au matumizi mbaya unawezekana upo, ZZK ambaye alipaswa kusema ndani ya chama chake akalibeba suala bungeni kupitia PAC. Waraka umeeleza mkakati na ZZK ameufanya. Hivi kweli huyu alikuwa ana lengo jema hata kama ndivyo ilivyokuwa?

Kusema hili ni genge sidhani ni neno baya. Genge ni mkusanyiko wa watu wenye masilahi au malengo fulani yakiwa zaidi ya muda mfupi. Masilahi ya waandika waraka ni kumpata 'tunayemtaka' siyo kiongozi wa CDM.

Genge pia linaweza kuwa na lengo la uhalifu na lina qualify definition.
Wewe na mimi tutakuwa na def tofauti kulingana na mtazamo wetu kwa waraka.

Aman Kaborou aliondoka kuelekea CCM. Kafulila aliondoka taratibu kwenda NCCR. Juliana Shonzo aliondolewa kwa bahati mbaya akiwa mwenyewe na wenzake wakabaki wakiandika waraka. Arifu kaaachia ngazi mwenyewe. Chatanda kaondoka taratibu kurejea nyumbani CCM.
Kitundu kaachia ngazi kwasababu bwanamkubwa ambaye ni mdogo kanyang'anywa wadhifa.

Wote walisema baada ya kuondoka. Mkandara, nasema, hivi kweli mwituni Fisi anapovizia mizoga tunaweza kumwita shujaa? Hata Mbweha watatucheka! of all animals, fisi kweli!

Katika masakata yote ZZK ameshiriki. Sijui hapa mkuu unasemaje na una maoni gani.
Je, alikuwa sahihi kuzusha vurugu zote au alikuwa na njia mbadala.

Na mwisho, unachanganya mambo. Huu waraka si mkakati wa kampeni. Ni mkakati wa kuondoa viongozi kwa njia nyingine. Habari za Waraka zilitumwa mtandaoni na zimeleta sintofahamu na kujenga chuki miongoni mwa wanaCDM.Yote yalikuwa nyuma ya waandika waraka. Hilo nalo unaita kampeni kweli.

Sina tatizo kama wangeachia ngazi na kuanza kampeni. Hawakufanya hivyo waliendelea kuwa katika uongozi halali wakaitengeneza waraka haramu ambao mkuu Mkandara anaupulizia utuli na marashi

Huwezi kuwa na double standards ukishauri maandamano halafu ukarudi magengeni na kulaani maandamano. Huwezi kulaani mauaji ya Polisi kwa wanachama halafu kuonyesha huruma kwa polisi

Huwezi kujenga chama kwa kujenga chuki na kumdhalilisha mpinzani wako.
Hebu niambie 'elimu magumashi, akili kidogo au malaya' yanajenga vipi chama zaidi ya kubomoa.

Habari ya kujuana nadhani Kitila anaweza kuieleza vizuri sana. Si yeye ndiye alitoa formaula ya kupata viongozi kama mshauri wa CDM.


 
Nguruv3;

Naona umeshikilia bango waraka. Ni maana ya waraka? Waraka ni kumbukumbu tu zilizopo kwenye karatasi au chombo cha electronics kama computer au laptop. Waraka unatumika kama kithibitisho kuwa walioandika walikutana na kuzungumzia masuala ya mabadiliko.

Je watuhumiwa wangekuwa wanakutana na kukariri vitu wanavyotaka kufanya bila kuwa na waraka, CDM ingechukua hatua gani?

Kama ulivyoeleza watuhumiwa ni watu wa ngazi za juu ndani ya chama. Hivyo kikao chochote rasmi cha chama walitakiwa kuwepo. Jinsi waraka ulivyopatikana, inaonyesha kuwa kulikuwa na vikao visivyo rasmi vya chama vya kuutafuta waraka ambavyo havikuwahusisha watuhumiwa. Je uoni kuwa uoni kuwa vikao hivi vilikuwa vinakiuka utaratibu wa chama?
 
Nguruv3;

Naona umeshikilia bango waraka. Ni maana ya waraka? Waraka ni kumbukumbu tu zilizopo kwenye karatasi au chombo cha electronics kama computer au laptop. Waraka unatumika kama kithibitisho kuwa walioandika walikutana na kuzungumzia masuala ya mabadiliko.

Je watuhumiwa wangekuwa wanakutana na kukariri vitu wanavyotaka kufanya bila kuwa na waraka, CDM ingechukua hatua gani?

Kama ulivyoeleza watuhumiwa ni watu wa ngazi za juu ndani ya chama. Hivyo kikao chochote rasmi cha chama walitakiwa kuwepo. Jinsi waraka ulivyopatikana, inaonyesha kuwa kulikuwa na vikao visivyo rasmi vya chama vya kuutafuta waraka ambavyo havikuwahusisha watuhumiwa. Je uoni kuwa uoni kuwa vikao hivi vilikuwa vinakiuka utaratibu wa chama?
Upo sahihi kabisa waraka ni kumbu kumbu kama usemavyo. Mimi nauangalia kama kichwa cha habari tu ninachozungumzia ni kile alichokisema Mchambuzi (contents,context na intent). Hivyo ninaposema waraka ninamaanisha hayo nas si karatasi ya kumbu kumbu.

Watuhumiwa wangekuwa hawana waraka CDM wasingechukua hatua nina dhani.
Kwasasa ushahidi upo na bado watu hawaamini sijui kama wangeamini kusikia tu.

Ni kwa njia hiyo ZZK amedumu na vurugu 4 kwasababu hakuna ushahidi hata pale anapotajwa na wahusika kama alivyofanya Juliana, Mtela na Ben Saanane.

Ben alipojitoa mhanga hakuwa katika kikao cha chama, nadhani ndivyo ilivyokuwa kwa Lema.
Kama tutakubaliana kuwa kuvamia laptop ilikuwa kosa, basi kuingia katika vikao halali na kutoa siri au kwenda pembeni kuandika kumbu kumbu zisizokubaliana na vikao hivyo ni uhalifu zaidi.

Unachokiona wewe ni ''mgonjwa'' kufariki kutokana na homa kali(laptop), umesahau kuwa homa ilisababishwa na malaria ya muda mrefu(kuingia katika vikao na kwenda magengeni)
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu kwanza alokubali kuujua waraka ni Kitila pekee ambaye kaonyesha wazi uzalendo wake sijui wewe ulitaka aukane kwanza kama Petro alivyomkana Yesu. Hapana mkuu wangu uharamu wa kitu ni kama angeukana, isipokuwa amekubali kuhusika kitu ambacho yeye anaona umuhimu kifanyike.

Tatizo la mjadala huu tunaruka sana sehemu muhimu ambazo uongozi wa CDM umetuficha na wewe hutaki kuzungumzia upande huo isipokuwa maamuzi yao tu. Kama alivyosema Zakumi kuwa waraka huu ni kumbukumbu kuonyesha DHAMIRA yao lakini maadam hatujaonyeshwa dhamira hiyo ktk hatua za vitendo siwezi kabisa kuwahukumu kama mnavyofanya nyie. Huitendi dhambi kwa kufikiria japo mawazo yanaweza kuwa mabaya.

Nikupe mifano miwili tusipoelewana mimi na wewe. Kuna mpango haramu ambao unaweza kuwa hivi:-
Mimi naweza kabisa kudhamiria kubeba unga na nikaiweka dhamira hiyo ktk maandishi jinsi gani ninatakiwa kuusunda, kuvaa nguo, kuwa na mhusika airport ambaye ataweza kunipitisha na kadhalika. Haya ni mawazo yangu haramu lakini maadam sijabeba unga hayawezi kutumika kama ushahidi wa kunifungulia mashataka ama kuswekwa Jela. Ni mawazo mabaya, hukanywa tu lakini yahawezi kunitia hatiani.

Mfano wa pili wa Halali ni ule ambapo mimi najua kwamba wewe unaliibia shirika letu fedha na kulitumia kama mali yako. Nimekujulisha kuwa mwenendo huo sio mzuri na najua fika kwamba wapo walotangulia kukujulisha na ukawaachisha kazi mapema na wengine wamejiuzuru lakini vitendo hivyo vinaendelea. Mimi japo sipo ktk chama chenu na mnanificha mkijua ni noma, ni mchawi mkiniweka tu nitaharibu ulaji uliopo lakini nawajua wote unaoshirikiana nao ktk njama hizi na hivyo nimeamua kuchukua njia tofauti kabisa kwa sababu nimewekeza nusu ya maisha, mtaji wa hali na mali ktk shirika hilo. Na mpango wenyewe ni kuhakikisha kuwa safari hii nyie ndio mtakao ondoka ama kuondolewa. Huwezi kabisa kuuita mpango huu kuwa ni Haramu hata kama ulikuwa ni siri yangu maana haiwezekani kabisa niwajulishe nachotaka kukifanya kwa uwazi ilihali nia na dhamira yenu sii nzuri toka mwanzo.

Hivyo binafsi nawatazama kina Kitila kwa mfano wa pili sio ule wa kwanza, wakati wewe unawatazama kwa mfano wa kwanza hivyo hatuwezi kufikia kupata jibu moja. Kila napokusoma nakuona ukiepuka (motive) ya madai ya kina Kitila ambayo ndio sababu kubwa ya wao kufikia dhamira walokuwa nayo. Hao kina Kabourou, Kafulila, Juliana Shonzo, Kitundu na Chatanda ni watu walofikiri kama wewe ya kwamba kuwepo kwao Chadema ni AJIRA tu ambayo unaweza kuiacha ukatafuta ajira sehemu nyingineyo.

Kwa maana hiyo hawa wote sio wanasiasa ila wameingia siasa ili wapate ajira lakini mwanasiasa haswa hupaswi kukimbia chama maana unatanguliwa na IMANI. Unakuwa sehemu ya chama na chama ni wewe na wananchi wote sio swala binafsi tena, hivyo hutakubali sehemu ya maisha ya watu idhulumiwe na mtu ama kundi la watu. Na ndivyo walivyokuwa kina Mandela na mashujaa wengine wa kisiasa ambao waliamini ktk harakati zao japo walionekana wakifanya vitendo Haramu. Na kizuri zaidi kama ukiwauliza hawatayakana. Mandela hakukana hadi kapelekwa Jela, Nyerere na TAA walikuwa na vikao vya siri na wakati wowote angeulizwa kuhusika na njama hizo asingeyakana.

Tatizo la mjadala huu tunatazama tu upande wa kina Zitto ambao nina hakika walipeleka malalamiko yao kwa wahusika. bahati nzuri nina kumbukumbu kubwa sana ya maswala ya Chadema na nina hakika kuwasoma viongozi walopita wakiyagusia haya yote yalodaiwa ktk waraka huu. Imefika mahala najiuliza, wait a minute inakuwaje kila kiongozi aliyetoka Chadema madai yao wote yanafanana? halafu sii wote wana uhusiano ama urafiki isipokuwa Zitto amekuwa kati kwa kukubaliana na madai yao maana hata yeye pia katengwa hajui kinachofanyika japo yupo ktk uongozi.

Sii mara moja wala mbili nimewahi kumsikia Zitto akilalamikia uongozi ktk mahesabu ya chama toka 2008 na kina Omariliyastukawadharau na kuwapuuza. Na ilipofikia swala la posho majuzi karibu na uchaguzi mkuu ndio mgogoro umejitokeza wazi kabisa ndani ya chama wakatokea kina Lema na matusi mazito mazito wakapongezwa, na kila siku uongo na uzushi unaongezeka juu ya ZZK ambaye kila kukicha hakosi kuweka record sawa tofauti na viongozi wa CDM wanaoficha matendo yao. Hapo hapo nikajua kuwa lisemwalo lipo!
 
Last edited by a moderator:
Nakuhakikishia kuwa hutaweza kubadili mawazo kabisa kwa sasa.
Utaweza kubadili endapo utaiangalia CDM kama institution inayoongozwa kwa taratibu, kanuni, sheria na maadili.Utafanikiwa kuona kisichoonekana kama utaiangalia taasisi na si Personality.
Utafanikiwa kama utasoma maandishi ukizingati maudhui, nia na mpangilio.
Mkuu Nguruvi3, usemayo ni kweli, nitajaribu kuutazama tena na tena huu waraka in broader perspective, sijaweza kubadili mawazo!. Kwangu mimi huu waraka sio uhaini bali ni creation ya "the winning coalition!". Hakuna uhaini wowote kwa sababu hakukuwa na mpango wowote wa kufanya mapinduzi, bali ni mkakati wa kubadili uongozi kwenye chaguzi halali za ndani ya Chadema!.

Kilichofanywa na waraka wa mabadiliko ni kitu kinaitwa "The selectorate theory" kama kilivyoelezwa kwenye kitabu cha "The Logic of Political Survival" kilichoandikwa na maprofesa wa siasa, Bruce Bueno de Mesquita na Alastair Smith wa New York Univeristy (NYU) kwa ushirikiano na Randolph M. Siverson wa UC Davis na James D. Morrow wa University of Michigan.

Naomba kunukuu, "In selectorate theory, three groups of people affect leaders. These groups are the nominal selectorate, (wale watu wa kwenye waraka wa siri) the real selectorate, (ni wale wapiga kura kuchagua viongozi wapya wa Chadema), ili kupata kundi kubwa la "the winning coalition". The nominal selectorate, also referred to as the interchangeables, includes every person who has some say in choosing the leader (for example, in an American presidential election, all registered voters). The real selectorate, also referred to as the influentials, are those who really choose the leaders (for example, in an American presidential election, those people who cast a vote). The winning coalition, also referred to as the essentials, are those whose support translates into victory (for example, in an American presidential election, those voters that give a candidate 270 electoral votes).

No Mater how good Mwenyekiti Mbowe is, amefikia his optimum!, hapo ndipo mwisho wa uwezo wake!, kama ilivyo saturated solution, it can take no more!. Uwezo wa Mbowe ndio umefika mwisho hapo alipoifikisha Chadema!, hawezi kufanya anything new, hivyo hawezi kuipeleka Chadema Ikulu 2015!. Lazima abadilishwe aje mtu vibrant zaidi wa kulisukuma jahazi la Chadema kuelekea ikulu!. Akiendelea kuwepo, Chadema kitakuwa ni chama cha kudumu cha upinzani, kama Lipumba alivyofikia optimum yake!.

Wale wenye kuona mbali, na wenye nia njema ya dhati na Chadema kuingia ikulu 2015, wameyaona madhaifu yaliyopo!, kuliko kuikosa ikulu, ni bora kufanya mageuzi ya ndani, na ndipo waraka ulipobuniwa!.
Mpango wowote wa mageuzi ya uongozi, lazima uanze kwa siri!, Mwenyekiti Mbowe baada ya kukinyofoa kwa siri kile kipengele cha ukomo wa uongozi ili atawale milele, Kundi linalomuunga mkono Mwenyekiti ni kubwa na hili ndilo "The Wining Coalition!", ili kulivunja nguvu, kazi ya kwanza ndio hiyo ya kuunda "he nominal selectorate" the few people you can trust ambao kazi yao itakuwa kuwa convince "The real selectorate" kuhusu mapungufu ya viongozi waliopo na the real need to change the top leadership kama nia ni kuiondoa CCM na kwenda ikulu!. Waraka huo umekuwa intercepted kwenye early stage!. Hakuna uhaini wowote!.
Wengi wamepongeza hatua zilizochukuliwa na CC ya Chadema, nikawabeza kuwa huko ni kusifu ujinga!. Sijui wangapi angalau hata wamepitia tuu katiba ya Chadema na kuona taratibu za nidhamu!. Kina Shnza walipovuliwa tuu uanachama niliwaomba Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania Come 2015...

hakuna aliyesikia. Simaanishi wahalifu wasiadhibiwe Chadema, bali watendewe haki!. Lilipokuja hili la Zitto na kina Kitilla, Chadema CC, did the same!. Nikawaambia that was "putting the cart before the horse!". CC ya Chadema haikufuata sheria, taratibu na kanuni!, ZZK akaamua kwenda kuitafuta haki kule inakopatikana! ambapo naamini sasa Chadema itashikishwa adabu na kujifunza umuhimu wa kufuata sheria, taratibu na kanuni!.

Hoja zangu nyingine zote kuuhusu waraka ule zimekuwa pre emptied na Wakuu Asha Di na Mag 3!.

Pasco.

 
Mkuu Nguruvi3, usemayo ni kweli, nitajaribu kuutazama tena na tena huu waraka in broader perspective, sijaweza kubadili mawazo!. Kwangu mimi huu waraka sio uhaini bali ni creation ya "the winning coalition!". Hakuna uhaini wowote kwa sababu hakukuwa na mpango wowote wa kufanya mapinduzi, bali ni mkakati wa kubadili uongozi kwenye chaguzi halali za ndani ya Chadema!.

Kilichofanywa na waraka wa mabadiliko ni kitu kinaitwa "The selectorate theory" kama kilivyoelezwa kwenye kitabu cha "The Logic of Political Survival" kilichoandikwa na maprofesa wa siasa, Bruce Bueno de Mesquita na Alastair Smith wa New York Univeristy (NYU) kwa ushirikiano na Randolph M. Siverson wa UC Davis na James D. Morrow wa University of Michigan.

Naomba kunukuu, "In selectorate theory, three groups of people affect leaders. These groups are the nominal selectorate, (wale watu wa kwenye waraka wa siri) the real selectorate, (ni wale wapiga kura kuchagua viongozi wapya wa Chadema), ili kupata kundi kubwa la "the winning coalition". The nominal selectorate, also referred to as the interchangeables, includes every person who has some say in choosing the leader (for example, in an American presidential election, all registered voters). The real selectorate, also referred to as the influentials, are those who really choose the leaders (for example, in an American presidential election, those people who cast a vote). The winning coalition, also referred to as the essentials, are those whose support translates into victory (for example, in an American presidential election, those voters that give a candidate 270 electoral votes).

No Mater how good Mwenyekiti Mbowe is, amefikia his optimum!, hapo ndipo mwisho wa uwezo wake!, kama ilivyo saturated solution, it can take no more!. Uwezo wa Mbowe ndio umefika mwisho hapo alipoifikisha Chadema!, hawezi kufanya anything new, hivyo hawezi kuipeleka Chadema Ikulu 2015!. Lazima abadilishwe aje mtu vibrant zaidi wa kulisukuma jahazi la Chadema kuelekea ikulu!. Akiendelea kuwepo, Chadema kitakuwa ni chama cha kudumu cha upinzani, kama Lipumba alivyofikia optimum yake!.

Wale wenye kuona mbali, na wenye nia njema ya dhati na Chadema kuingia ikulu 2015, wameyaona madhaifu yaliyopo!, kuliko kuikosa ikulu, ni bora kufanya mageuzi ya ndani, na ndipo waraka ulipobuniwa!.
Mpango wowote wa mageuzi ya uongozi, lazima uanze kwa siri!, Mwenyekiti Mbowe baada ya kukinyofoa kwa siri kile kipengele cha ukomo wa uongozi ili atawale milele, Kundi linalomuunga mkono Mwenyekiti ni kubwa na hili ndilo "The Wining Coalition!", ili kulivunja nguvu, kazi ya kwanza ndio hiyo ya kuunda "he nominal selectorate" the few people you can trust ambao kazi yao itakuwa kuwa convince "The real selectorate" kuhusu mapungufu ya viongozi waliopo na the real need to change the top leadership kama nia ni kuiondoa CCM na kwenda ikulu!. Waraka huo umekuwa intercepted kwenye early stage!. Hakuna uhaini wowote!.
Wengi wamepongeza hatua zilizochukuliwa na CC ya Chadema, nikawabeza kuwa huko ni kusifu ujinga!. Sijui wangapi angalau hata wamepitia tuu katiba ya Chadema na kuona taratibu za nidhamu!. Kina Shnza walipovuliwa tuu uanachama niliwaomba Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania Come 2015...

hakuna aliyesikia. Simaanishi wahalifu wasiadhibiwe Chadema, bali watendewe haki!. Lilipokuja hili la Zitto na kina Kitilla, Chadema CC, did the same!. Nikawaambia that was "putting the cart before the horse!". CC ya Chadema haikufuata sheria, taratibu na kanuni!, ZZK akaamua kwenda kuitafuta haki kule inakopatikana! ambapo naamini sasa Chadema itashikishwa adabu na kujifunza umuhimu wa kufuata sheria, taratibu na kanuni!.

Hoja zangu nyingine zote kuuhusu waraka ule zimekuwa pre emptied na Wakuu Asha Di na Mag 3!.

Pasco.



Pasco;

Naona unatupeleka shule sasa :A S thumbs_up: . Katika management kupishana kunasaidia watu kujifunza. Mbowe au Zittto akikaa pembeni atajifunza makosa aliyofanya na vilevile ataangalia makosa ya viongozi wengine. Basi pale anaporudi kwenye madaraka anakuwa na mawazo mapya. Mabadiliko kama haya ndio yanayosababisha kuleta maendeleo kwa kutumia demokrasi kuwezekana katika nchi zilizoendelea. Demokrasia pekee bila kuwa na tabia ya kuwaachia wenzio haina maana yoyote.

Kama Mbowe has reached the plateau, hawezi kubadilika akiendelea kukaa madarakani. Mabadiliko makubwa atayapata pale atakapokiangalia chama from a different perspective.
 
Pasco;
Naona unatupeleka shule sasa :A S thumbs_up: . Katika management kupishana kunasaidia watu kujifunza. Mbowe au Zittto akikaa pembeni atajifunza makosa aliyofanya na vilevile ataangalia makosa ya viongozi wengine. Basi pale anaporudi kwenye madaraka anakuwa na mawazo mapya. Mabadiliko kama haya ndio yanayosababisha kuleta maendeleo kwa kutumia demokrasi kuwezekana katika nchi zilizoendelea. Demokrasia pekee bila kuwa na tabia ya kuwaachia wenzio haina maana yoyote.

Kama Mbowe has reached the plateau, hawezi kubadilika akiendelea kukaa madarakani. Mabadiliko makubwa atayapata pale atakapokiangalia chama from a different perspective.
Mkuu Zakumi, naamini Mhe. Mbowe, hili analijua, ila kuna wengi wa wanachama wa Chadema na baadhi ya viongozi wao, wamewaglorify viongozi wao hadi kuwa sanctify na wengine hadi kuwaona kama demi god au semi god, hivyo kuwaabudia kama miungu watu!. Akijitokeza mtu kusema madhaifu ya hawa viongozi, kwao ni abomination!, mtu huyo has to be ejected aven condened to death!, kwao ni kama kumkufuru Mungu!, ndio maana mmeona jinsi CC ya walivyohamaki na kuweka pembeni baadhi ya sheria taratibu na kanuni zake za nidhamu!.
Pasco.
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu kwanza alokubali kuujua waraka ni Kitila pekee ambaye kaonyesha wazi uzalendo wake sijui wewe ulitaka aukane kwanza kama Petro alivyomkana Yesu. Hapana mkuu wangu uharamu wa kitu ni kama angeukana, isipokuwa amekubali kuhusika kitu ambacho yeye anaona umuhimu kifanyike.

Tatizo la mjadala huu tunaruka sana sehemu muhimu ambazo uongozi wa CDM umetuficha na wewe hutaki kuzungumzia upande huo isipokuwa maamuzi yao tu. Kama alivyosema Zakumi kuwa waraka huu ni kumbukumbu kuonyesha DHAMIRA yao lakini maadam hatujaonyeshwa dhamira hiyo ktk hatua za vitendo siwezi kabisa kuwahukumu kama mnavyofanya nyie. Huitendi dhambi kwa kufikiria japo mawazo yanaweza kuwa mabaya.

Nikupe mifano miwili tusipoelewana mimi na wewe. Kuna mpango haramu ambao unaweza kuwa hivi:-
Mimi naweza kabisa kudhamiria kubeba unga na nikaiweka dhamira hiyo ktk maandishi jinsi gani ninatakiwa kuusunda, kuvaa nguo, kuwa na mhusika airport ambaye ataweza kunipitisha na kadhalika. Haya ni mawazo yangu haramu lakini maadam sijabeba unga hayawezi kutumika kama ushahidi wa kunifungulia mashataka ama kuswekwa Jela. Ni mawazo mabaya, hukanywa tu lakini yahawezi kunitia hatiani.

Mfano wa pili wa Halali ni ule ambapo mimi najua kwamba wewe unaliibia shirika letu fedha na kulitumia kama mali yako. Nimekujulisha kuwa mwenendo huo sio mzuri na najua fika kwamba wapo walotangulia kukujulisha na ukawaachisha kazi mapema na wengine wamejiuzuru lakini vitendo hivyo vinaendelea. Mimi japo sipo ktk chama chenu na mnanificha mkijua ni noma, ni mchawi mkiniweka tu nitaharibu ulaji uliopo lakini nawajua wote unaoshirikiana nao ktk njama hizi na hivyo nimeamua kuchukua njia tofauti kabisa kwa sababu nimewekeza nusu ya maisha, mtaji wa hali na mali ktk shirika hilo. Na mpango wenyewe ni kuhakikisha kuwa safari hii nyie ndio mtakao ondoka ama kuondolewa. Huwezi kabisa kuuita mpango huu kuwa ni Haramu hata kama ulikuwa ni siri yangu maana haiwezekani kabisa niwajulishe nachotaka kukifanya kwa uwazi ilihali nia na dhamira yenu sii nzuri toka mwanzo.

Hivyo binafsi nawatazama kina Kitila kwa mfano wa pili sio ule wa kwanza, wakati wewe unawatazama kwa mfano wa kwanza hivyo hatuwezi kufikia kupata jibu moja. Kila napokusoma nakuona ukiepuka (motive) ya madai ya kina Kitila ambayo ndio sababu kubwa ya wao kufikia dhamira walokuwa nayo. Hao kina Kabourou, Kafulila, Juliana Shonzo, Kitundu na Chatanda ni watu walofikiri kama wewe ya kwamba kuwepo kwao Chadema ni AJIRA tu ambayo unaweza kuiacha ukatafuta ajira sehemu nyingineyo.

Kwa maana hiyo hawa wote sio wanasiasa ila wameingia siasa ili wapate ajira lakini mwanasiasa haswa hupaswi kukimbia chama maana unatanguliwa na IMANI. Unakuwa sehemu ya chama na chama ni wewe na wananchi wote sio swala binafsi tena, hivyo hutakubali sehemu ya maisha ya watu idhulumiwe na mtu ama kundi la watu. Na ndivyo walivyokuwa kina Mandela na mashujaa wengine wa kisiasa ambao waliamini ktk harakati zao japo walionekana wakifanya vitendo Haramu. Na kizuri zaidi kama ukiwauliza hawatayakana. Mandela hakukana hadi kapelekwa Jela, Nyerere na TAA walikuwa na vikao vya siri na wakati wowote angeulizwa kuhusika na njama hizo asingeyakana.

Tatizo la mjadala huu tunatazama tu upande wa kina Zitto ambao nina hakika walipeleka malalamiko yao kwa wahusika. bahati nzuri nina kumbukumbu kubwa sana ya maswala ya Chadema na nina hakika kuwasoma viongozi walopita wakiyagusia haya yote yalodaiwa ktk waraka huu. Imefika mahala najiuliza, wait a minute inakuwaje kila kiongozi aliyetoka Chadema madai yao wote yanafanana? halafu sii wote wana uhusiano ama urafiki isipokuwa Zitto amekuwa kati kwa kukubaliana na madai yao maana hata yeye pia katengwa hajui kinachofanyika japo yupo ktk uongozi.

Sii mara moja wala mbili nimewahi kumsikia Zitto akilalamikia uongozi ktk mahesabu ya chama toka 2008 na kina Omariliyastukawadharau na kuwapuuza. Na ilipofikia swala la posho majuzi karibu na uchaguzi mkuu ndio mgogoro umejitokeza wazi kabisa ndani ya chama wakatokea kina Lema na matusi mazito mazito wakapongezwa, na kila siku uongo na uzushi unaongezeka juu ya ZZK ambaye kila kukicha hakosi kuweka record sawa tofauti na viongozi wa CDM wanaoficha matendo yao. Hapo hapo nikajua kuwa lisemwalo lipo!

Nimependa Mifano yako mkuu
CC
Pasco wa JF
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara
Naomba niseme kuwa 'mwizi si yule aliyeiba ng'ombe ni yule aliyekamatwa na ngozi'
Ngozi ni waraka na waliokamatwa nao wanajulikana tena wakikubali kuwa wameshiriki.

Siepuki motive ya maneno ya waraka kwasababu nimesema nauangalia waraka kwa contents, contexts na intent.

Kitendo cha kujadili yaliyomo ni kuupa uhalali waraka ambao mimi naamini kwa dhati kabisa kuwa ni haramu nikifahamu waliofanya hivyo walikuwa washiriki wa vikao vya CDM na ambao walikuwa na nafasi pana zaidi ya kulieleza tatizo bila kujificha vichochoroni.

Kitila na ZZK wanaamini kwa dhati ulikuwa haramu ndio maana wakataka kujiuzulu bila kuutetea kwa wanachama wao.

Unachojaribu kunishawishi ni kujadili 'mtoto' aliyezaliwa nje ya ndoa atalelewaje, umesahau kuwa tunachojadili hapa ni uzinifu wa wanandoa. Hapo ndipo tunaachana, kwamba kwakuwa mtoto ni binadamu basi tuwaangalie wazazi wake wazinifu kwa jicho la pili. Mimi nasema aa a! tunawajadili wazinifu kwanza.

Wakati ukifika wa kujadili matatizo yanayoikumba CDM tutafanya hivyo. Ninakumbu kumbu nzuri sana za kumkalia Mbowe shingoni katika mambo matatu makubwa. Hotuba yake Hai, alivyosimamia mchakato wa katiba na juisi, Togwa la Obama na mambo mengine.
Hayo siwezi kuyatumia kuhalalisha waraka, ni vitu tofauti,

Dhana kuwa waraka ulikuwa ni dhana inahitaji kwanza kujibiwa ni lini uliandikwa?
Mimi nina ushahidi wangu kuwa uliandikwa muda mrefu. Hoja ya pesa ya ZZK kupitia PAC ilikuwa sehemu ya waraka na mkakati.
Hoja ya ZZK kujihusisha na mikutano hivi karibuni ilikuwa sehemu ya waraka n.k.
Labda hapa unieleze lini waraka uliandikwa ili twende pamoja.
Pasco, waraka haukuwa kampeni ya kuondoa viongozi kwa njia ya kura.
Hoja za waraka zimekuwa mitandaoni neno kwa neno kama nilivyoonyesha bandiko #92 kwa mfano tu. Kampeni haifanywi katika njia za kuvuruga chama.
Kampeni ni kushindanisha sera,maono na mipango.

Kampeni haifanywi kwa kukashifu team mates.
Leo tunajua 'Mbowe ana akili ndogo, ni magumashi na malaya'.

Haya si sehemu ya kampeni za watu waliokomaa kisiasa. Angeyafanya Juliana tusingejali tungesema '' achwe abalehe'Yameandikwa na mshauri wa chama akishirikiana na mwenyekiti wa mkoa ngangari wakimtaka naibu katibu mkuu.Ni aibu the least to say.
Zakumi endapo Mbowe amefikia mwisho wa kufikiri na anahitaji mbadala hilo halina tatizo. Tatizo ni jinsi ya kumuondoa katika nafasi aliyochaguliwa kidemokrasia.

Kuandika waraka na kuutupa mitandaoni halikuwa jambo jema kwa mustakabali wa CDM. Kwa sisi wengine tunasema ni autolysis, yaani unajimaliza mwenyewe.

Sumu ya waraka iliyokuwa inapenyezwa katika mitandao na 'watumishi' wa waraka iliwapa CCM nguvu ya kukishambulia CDM. Je, kulikuwa na busara ya kufanya hivyo.

Leo mnasema hakuna ushahidi wa waraka kuingia sokoni wakati waraka ulishaingia.
Wengi tulifahamu kuwa maneno yote bila kujali uzito au wepesi wake yalikuwa yanachomekwa na watu fulani, thanks to Mwigamba aliyeuza ghala la silaha na kufumbua kitendawili.

Kwa pamoja nimewauliza
1. Kwanini hawakjiuzulu kabla ili kupinga wanachokiona na badala yake wakataka jiuzulu baada ya kuuza silaha?
2. Kwanini hawakutumia mikutano kueleza hali ilivyo kama vikao vilikuwa na mizengwe
3. Ni lini walipeleka agenda ikakataliwa na wao walichukua hatua gani baada ya hapo.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3

Unasema, Mkamatwa na ngozi ndiyo mwizi, sawa kabisa nakubali lakini je ZITTO KABWE KAKAMATWA NA NGOZI IPI?.

Tunachofahamu moja kwa moja ni kwamba Kitila na Mwigamba wao walikiri kushiriki kuuandaa huo waraka, LAKINI HAO HAO WALIKATAA, WALIKANA KWAMBA ZITTO HAUFAHAMU HUO WARAKA, NA WALA HAKUUANDIKA, Na Kitila alikanusha vikali kauli ya Slaa kwamba eti akina Kitila walimbrief Zitto!.

Kwa Mujibu wa Kauli ya Kitila kuhusu kutaka kwake kujiuzulu. Amesema mara nyingi kwamba KUTAKA KWAKE KUJIUZULU SI KWA SABABU AMEONA WARAKA NI KOSA, BALI KWA SABABU ALIONA VIONGOZI ANAOFANYA NAO KAZI HAWANA IMANI NAYE TENA!.

Zitto halikadhalika alisema kutaka kwake kujiuzuru si kwa sababu ya kushiriki katika jambo la waraka, BALI NI KWA SABABU ILIONEKANA VIONGZI WENZIE HAWANA IMANI NAE

Bwana nguruvi hizo ndiyo sababu haswaa za Zitto na Kitila kutaka kujiuzuru.

Si sahihi kuanza kusema ZITTO alianza kuutekeleza waraka kwa sababu ya Ishu ya PAC vs CAG juu ya kukagua vyama , Posho n.k- Kiufupi ni kwamba Zitto alikuwa akitekeleza majukumu yake, na si mara ya kwanza Zitto kusimamia ishu nzito za Kitaifa bungeni. Kwa mantiki unayotumia, maana yake ni kwamba Zitto hata kama angesimamia ishu yoyote ya kitaifa kadri siku zinavyokwenda, watu wenye msimamo na mtizamo kama wewe wangesema "AAH HUYU ANATEKELEZA WARAKA BWANA". Mimi ninafikiri huu siyo mtizamo sahihi, ni hisia, ni speculation.


Kuna Mahali katika mabandiko yako umekiri kwamba ZItto ni mjanja kweli, kwamba haachi ushahidi katika ishu zake!. Well UMUHIMU WA USHAHIDI BADO NI MUHIMU NGURUVI3. Mathalani Haitoshi tu kwamba kina Shonza, Ben Saa nane wawe wamemtaja, WANAHITAJI KUPROVE BEYOND ANY REASONABLE DOUBT!.

Unauliza waraka umeandikwa lini?, Hilo swali anaweza kulijibu Kitila na Mwigamba vizuri zaidi, SWALI HILI KUMUULIZA ZITTO NI KUMUONEA, KWANI YEYE HAJUI!.


Binafsi ninaamini waraka ule hauna tatizo, ni nia, ni malengo tena malengo mazuri, KUUKAMATA WARAKA NI KUKAMATA MALENGO YALIYO NDANI, NA MALENGO YENYEWE YAMEAINISHWA KATIKA PARAGRAPH ZA MWANZO KABISA ZA WARAKA WENYEWE "KUKIBORESHA CHAMA".

Haya mambo ya sijui kutumia lugha mbaya dhidi ya Viongozi wengine, mimi ninachokiona mle ni matumizi ya lugha ambayo siyo matusi , kwa kiingereza inaitwa "FIGURATIVE SPEECH" au kwa kiswahili tunaita "tamathali za semi". unapotumia neno Elimu ya "magumashi", hiyo ni tamathali ya semi maana yake "elimu duni". magumashi siyo tusi, bali neno la msimu lenye maana ya uduni, kutoeleweka eleweka n.k.

Unaputumia kauli kama "yule kichaa wa ars", nayo pia ni tamathali ya semi, Hapa kichaa haisimami kumaanisha "Chizi" ilhali mtu siyo Chizi, bali inasimamia matendo ya mtu, tabia za huyo mtu, nadhani Ugomvi ndani ya vikao na matamshi ya huyo bwana ni ushahidi wa matendo yake yako namna gani!.

Mathalani Mwalimu Nyerere aliposema "Mwendawazimu katuvamia, tutampiga, uwezo wa kumpiga tunao...", alikuwa hamtukani Iddi Amini, bali alikuwa anaelezea matendo ya Amini ni ya kiwenda wazimu. SANAA YA MATUMIZI YA MANENO KWA MAANA YA FASIHI ANDISHI NI MUHIMU SANA KWA MWANASIASA ANAYEJUA KUJENGA HOJA!

INFACT KITU WASICHOTAKA KUACKNOWLEDGE WATU WENYE HOJA HII, NI KWAMBA MM (ZITTO) AMECHAMBULIWA KAMA KARANGA KWELI KWELI MLE NDANI YA WARAKA, Ameitwa mwenye jazba, hana ndoa, hatafuti ushauri kabla ya kujibu mapigo.

Waraka hauna tatizo, tatizo ni CC ya Chadema iliyokurupuka kufanya maamuzi ya Ajabu kabisa!
 
Mkuu Mkandara

Kitendo cha kujadili yaliyomo ni kuupa uhalali waraka ambao mimi naamini kwa dhati kabisa kuwa ni haramu nikifahamu waliofanya hivyo walikuwa washiriki wa vikao vya CDM na ambao walikuwa na nafasi pana zaidi ya kulieleza tatizo bila kujificha vichochoroni.

Kitila na ZZK wanaamini kwa dhati ulikuwa haramu ndio maana wakataka kujiuzulu bila kuutetea kwa wanachama wao.

Unachojaribu kunishawishi ni kujadili 'mtoto' aliyezaliwa nje ya ndoa atalelewaje, umesahau kuwa tunachojadili hapa ni uzinifu wa wanandoa. Hapo ndipo tunaachana, kwamba kwakuwa mtoto ni binadamu basi tuwaangalie wazazi wake wazinifu kwa jicho la pili. Mimi nasema aa a! tunawajadili wazinifu kwanza.
Mkuu Nguruvi3, nimeupenda mfano wako wa mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa, subject matter ni mtoto, sio kilifanyika nini, lini na wapi, kitendo kilichomtengeneza huyo mtoto!, kidini anaitwa mwana haramu!, kwa Sharia law, haruhusiwi hata kurithi mali!, kama ni wa kike, rukhsa baba yake mzazi kumuoa na kumfanya mke!. Kosa la huyu mtoto ni nini?!. waliofanya uzinifu ni kina nani na anaadhibiwa nani!?, Wazinifu wameadhibiwa kwa uzinifu wao na hatimaye an innocent product ya uzinifu huo, who has nothing to do with kilichofanyika hadi kuzaliwa!. Jee is it real fair kumuandibu mwana haramu kwa makosa ya uzinifu wa wazazi wake?!. Wazinifu wamekiri, mtoto hakuujua uzinifu ule, lakini anayeadhibiwa ni mtoto!, is it fair?!.

Comming back to waraka, mkuu Nguruvi 3, jee umeweza kuelewa chochote kuhusu hii
Mkuu Nguruvi3, Kwangu mimi huu waraka sio uhaini bali ni creation ya "the winning coalition!". Hakuna uhaini wowote kwa sababu hakukuwa na mpango wowote wa kufanya mapinduzi, bali ni mkakati wa kubadili uongozi kwenye chaguzi halali za ndani ya Chadema!.

Kilichofanywa na waraka wa mabadiliko ni kitu kinaitwa "The selectorate theory" kama kilivyoelezwa kwenye kitabu cha "The Logic of Political Survival" kilichoandikwa na maprofesa wa siasa, Bruce Bueno de Mesquita na Alastair Smith wa New York Univeristy (NYU) kwa ushirikiano na Randolph M. Siverson wa UC Davis na James D. Morrow wa University of Michigan.

Naomba kunukuu, "In selectorate theory, three groups of people affect leaders. These groups are the nominal selectorate, (wale watu wa kwenye waraka wa siri) the real selectorate, (ni wale wapiga kura kuchagua viongozi wapya wa Chadema), ili kupata kundi kubwa la "the winning coalition". The nominal selectorate, also referred to as the interchangeables, includes every person who has some say in choosing the leader (for example, in an American presidential election, all registered voters). The real selectorate, also referred to as the influentials, are those who really choose the leaders (for example, in an American presidential election, those people who cast a vote). The winning coalition, also referred to as the essentials, are those whose support translates into victory (for example, in an American presidential election, those voters that give a candidate 270 electoral votes).

No Mater how good Mwenyekiti Mbowe is, amefikia his optimum!, hapo ndipo mwisho wa uwezo wake!, kama ilivyo saturated solution, it can take no more!. Uwezo wa Mbowe ndio umefika mwisho hapo alipoifikisha Chadema!, hawezi kufanya anything new, hivyo hawezi kuipeleka Chadema Ikulu 2015!. Lazima abadilishwe aje mtu vibrant zaidi wa kulisukuma jahazi la Chadema kuelekea ikulu!. Akiendelea kuwepo, Chadema kitakuwa ni chama cha kudumu cha upinzani, kama Lipumba alivyofikia optimum yake!.

Wale wenye kuona mbali, na wenye nia njema ya dhati na Chadema kuingia ikulu 2015, wameyaona madhaifu yaliyopo!, kuliko kuikosa ikulu, ni bora kufanya mageuzi ya ndani, na ndipo waraka ulipobuniwa!.
Mpango wowote wa mageuzi ya uongozi, lazima uanze kwa siri!, Mwenyekiti Mbowe baada ya kukinyofoa kwa siri kile kipengele cha ukomo wa uongozi ili atawale milele, Kundi linalomuunga mkono Mwenyekiti ni kubwa na hili ndilo "The Wining Coalition!", ili kulivunja nguvu, kazi ya kwanza ndio hiyo ya kuunda "he nominal selectorate" the few people you can trust ambao kazi yao itakuwa kuwa convince "The real selectorate" kuhusu mapungufu ya viongozi waliopo na the real need to change the top leadership kama nia ni kuiondoa CCM na kwenda ikulu!. Waraka huo umekuwa intercepted kwenye early stage!. Hakuna uhaini wowote!.
Pasco.
au nipige darasa zaidi?.

Pasco, waraka haukuwa kampeni ya kuondoa viongozi kwa njia ya kura.
Mkuu Nguruvi3 ukiisha chagua upande, you've chosen your side, and you'll love, guard, keep and defend your choice!, hivi na wewe, of all the people anaamini waraka ulitaka kufanya mapinduzi na sio kulobby for changing the mind set ya wapiga kura?!. Usiuhukumu kwa mtindo wa pakacha la samaki mmoja akioza, wote wameoza!, what was the motive behind ule waraka?, kweli kabisa Mkuu Nguruvi3 with all due respect unaamini kabisa kwa dhati kuwa lengo la waraka ule ni kufanya mapinduzi nje ya electoral system ya Chadema?!.

Hoja za waraka zimekuwa mitandaoni neno kwa neno kama nilivyoonyesha bandiko #92 kwa mfano tu. Kampeni haifanywi katika njia za kuvuruga chama.
Nani walitaka kuvuruga chama?, nia ya kukiimarisha chama ili kiweze kuishika ikulu ndiko kuvuruga?, Harakati za kisiasa most of the times zinapangwa kisiasa, lakini mashambulizi ndani ya uwanja wa mapambano, yanatekelezwa kijeshi!, naomba niwasaidie baadhi yetu ambao hatukupata fursa ya kupita jeshini hivyo hawajui mbinu za medani!. Waraka uliandaa a political ambush ya kupata viongozi bora, kabla ambush haijafanywa kwanza inafanyika "rake patrol" inafanywa kwa usiri mkubwa!. Hii ilisha fanyika, kisha inafuta planning phase, askari wa kawaida bado hawaambiwi, na jemedari baada ya kuonekana hawezi kushinda vita, watu mko front line, pia hashirikishwi!, na mkiwa vitani mkajiridhisha jemedari hawezi kuongoza mnapaswa ku take kitu kinaitwa "initiatives" ama mkubali kumvumilia jemedari goigoi mshindwe vita muangamizwe, ama kumuondoa jemedari na 2i/c kuongoza mapambano. Wanaoamua kumuondoa jemedari sio 2i/c bali ni askari wa mstari wa mbele "Kitila, Mwigamba na wengine!, tena kuhakikisha mpango ni wa siri sana, unaohusisha watu wachache sana usually wawili, watatu, baada ya kumueliminate comander, ndipo 21/c anaarifiwa rasmi, kuwa jemedari is no more, he must asume the commanding as the new jemedari, there is no time to negotiate au kuuliza what happened, na yeye akisita, he'll be taken out immediately coming to the 3i/c!. Mpango umetibuliwa kabla ya utekelezaji, ila utekelezaji ulikuwa uwe wa kisiasa kupitia uchaguzi halali ndani ya Chadema sio elimination kama vitani!.

Kampeni haifanywi kwa kukashifu team mates
Leo tunajua 'Mbowe ana akili ndogo, ni magumashi na malaya
Huko sio kukashifu hizo ni missiles, silaha za maangamizi!. Kati ya vitu vinavyoturudisha nyuma sana sisi Watanzania ni kutokuwa wakweli, kutosimama na ukweli, na kukumbatia uongo na unafiki!, hayo yaliyoelezwa kumhusu "jemedari" ni "calling a spade a spade!", kwani ni uongo?, amezushiwa?, au amesingiziwa?!. Hizo ni hard facts, ukiwa front line, you have to play by the rules!, if you cross the line of fire you are taken out!. Jemedari crosed the line!, he has to be taken out, you just shoot!. Uliprefer wamsifie?, very bright, very honest!, na mwaminifu sana katika ndoa yake?!, au wamfichie aibu yake mtindo wa kimbuni mbuni kuficha kichwa mchangani?!. Kumbuka the scheme ya waraka, was ment to be top secret! not for public consumption!, hivyo hivyo hizo kashfa hazipo!. Hata mimi, nikiwa na wewe tuu peke yetu kwenye chumba au kwenye lift, nikakutukana bila mtu yoyote kusikia, huwezi kunishitaki eti nimekuvunjia heshima!. Ili nikuvunjie heshima, lazima a third part asikie!. According to to the codes of secrecy za waraka ule, its considered only insiders tuu ndio walijua!. Aliyemkashifu jemedari ni aliyeusambaza, na umesambazwa kwa ill motives ili kuwachonganisha waandishi waonekane wahaini!.

Zamani dada zetu na mama zetu, walibakwa sana ila hawakuthubutu kusema to any third part itakuwa ni aibu!, mbakaji huwa ana strike again and again and again kwa sababu mbakwaji would rather keep quite and make it secret ya kubakwa kuliko aibu ya kusema!. Chadema ndio walio leak huo waraka na kumuibisha jemedari wao!.
Kwa pamoja nimewauliza
1. Kwanini hawakjiuzulu kabla ili kupinga wanachokiona na badala yake wakataka jiuzulu baada ya kuuza silaha?
Siasa ni kama vitani, kuna point ukifika inaitwa "the point of no return" there is no retreat, no surrender, you to fight risasi ya mwisho na tone la mwisho la damu!, this fight, was the fight from within!, huwezi kulikimbia shamba ukawaachia ngedere watafune mahindi!. Nape alipombwatukia Lowassa kwenye issue ya jengo la UVCC nini kilimtokea?!, si alifukuzwa JK akamuokoa!. Alipotangaza vua gamba, nothing was done!, amejiuzulu, si anaendelea ku fight from within!?. Juzi yeye na Kinana walipoibuka na mawaziri mizigo, JK si amewapuuza?!, wamefanya nini?, walipaswa kujiuzulu!, ila wajiuzulu na kuwaachia gedere wamalize shamba?!, its fighting from within!. Si mmemuona Nape kaibuka na ile hangover ya party supremacy ati CCM itawa summons mawaziri na wakuu wa taasisi za umma!?, CCM iwa summon mawaziri hiyo CCM ikiwa ni kama nani?!, kwenye mfumo wa serikali, what the hell is CCM?, Nape anaota ndoto za alinacha mchana kweupe!. Wenye akili na busara baada ya kuona jahazi linakwenda mrama, captain hawezi tena kuongoza jahazi, dawa ni kuabandon jahazi na kujitosa baharini au kum replace captain na kuokoa jahazi?!.

2. Kwanini hawakutumia mikutano kueleza hali ilivyo kama vikao vilikuwa na mizengwe
Chama si kina chain of command, ushindwe kumuondoa jemedari, halafu uende kwa wapiganaji usema jemedari hafai?!. Gimme a break!.
3. Ni lini walipeleka agenda ikakataliwa na wao walichukua hatua gani baada ya hapo
Hayo ni mambo ya ndani, au unataka waendelee kumwaga mboga kwa sababu tuu wenzao wamamwaga ugali?!. Mtafute ZITTO, Kitila na Mwigamba watakueleza one to one!. Siku ile nilipopandisha ile thread ya Chadema kunyofoa kipengele cha ukomo wa madaraka kinyemela, I got a call from one of them, (not ZZK), akanieleza ukweli halisi ulivyo na jinsi Dr anavyotoa uongo!, sikuweza kusema Dr. ni muongo kwa sababu, pamoja na yote namheshimu sana tuu!. Kwenye hili sakata kuna mengi hayajasemwa, yakisemwa yote itakuwa ni aibu!, nimeshauri wasiendeleze adding an insult to an injury to the damage that has already done!.
Pasco.
 
Mkuu Nguruvi3, nimeupenda mfano wako wa mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa, subject matter ni mtoto, sio kilifanyika nini, lini na wapi, kitendo kilichomtengeneza huyo mtoto!, kidini anaitwa mwana haramu!, kwa Sharia law, haruhusiwi hata kuridhi mali!, kama ni wa kike, rukhsa baba yake mzazi kumuoa na kumfanya mke!. Kosa la huyu mtoto ni nini?!. waliofanya uzinifi ni kina nani?, wao wanaadhibiwaje kwa uzifu wao?, is it fair kumuandibu mwana haramu kwa makosa ya uzinifu wa wazazi wake?!. Wazinifu wamekiri, mtoto hakuujua uzinifu ule, lakini anayeadhibiwa ni mtoto!, is it fair?!.

Comming back to waraka, mkuu Nguruvi 3, jee umeweza kuelewa chochote kuhusu hii
au nipige darasa zaidi?.

Mkuu Nguruvi3 ukiisha chagua upande, you've chosen your side, and you'll love, giard, keep and defend your choice!, hivi na wewe, of all the people anaamini waraka ulitaka kufanya mapinduzi na sio kulobby for changing the mind set ya wapiga kura?. Usiuhukumu kwa mtindo wa pakacha la samaki mmoja akioza, wote wameoza!, what was the motive behind ule waraka?, kweli kabisa Mkuu Nguruvi3 with due all that respect unaamini ulikuwa na lengoi la kufanya mapinduzi nje ya electral system ya Chadema?!.

Nani walitaka kuvuruga chama?, nia ya kukiimarisha chama ili kiweze kuishika ikulu ndiko kuvuruga?, Harakati za kisiasa most of the times zinapangwa kisiasa, lakini mashambulizi ndani ya uwanja wa mapambano, yanatekelezwa kijeshi!, naomba niwasaidie baadhi yetu ambao hakupita jeshini hivyo hawajui mbinu za medani!. Warakauliandaa ambush ya kupata viongozi bora, kabla ambush haijafanywa kwanza inafanyika "rake patrol" inafanya kwa usiri mkubwa!. Hii ilisha fanyika, kisha inafuta planing phase, askari wa kawaida hawaambiwi, na jemedari baada ya kuonekana hawezi kushinda vita, watu mko front line, pia hashirikishwi!, na mkiwa vitani mkajiridhisha jemedari hawezi kuongoza mnapaswa ku take kitu kinaitwa "initiatives" ama mkubali kumvumilia jemedari goigio mshindwe vita muangamizwe, ama kumuondoa jemedari na 2i/c kuongoza mapambano. Wanaoamua kumuondoa jemedari sio 2i/c bali ni askari wa mstari wa mbele "Kitila. Mwigamba na wengine!, tena kuhakikisha mpango ni wa siri sana, unaohusisha watu wachache sana usually wawili, watatu, baada ya kumueliminate comander, ndipo 21/c anaarifiwa rasmi, kuwa jemedari is no more, he must asume comanding as the new jemedari, there is no time to negotiate au kuuliza what happened,na yeye akisita, he'll be take out immediately coming to the 3i/c!. Mpango umetibuliwa kabla ya utekelezaji, ila utekelezaji ulikuwa uwe wa kisiasa kupitia uchaguzi halali ndani ya Chadema!.

Huko sio kukashifu hizo ni missiles, silaha za maangamizi!. Kati ya vitu vinavyoturudisha nyuma sana sisi Watanzania ni kutokuwa wakweli, kutosimama na ukweli, na kukumbatia unafiki!, hayo yaliyoelezwa kumhusu "jemedari" kwani ni uongo?, amezushiwa?, amesingiziwa?!. Hizo ni hard facts, ukiwa front line, yoy have to play by the rules, uki cross the line of fire you are taken out!. Jemedari crosed the line!, he has to be taken out, you just shoot!. Uliprefer wamsifie?, very bright, very honest!, na mwaminifu sana katika ndoa?!. Kumbuka the scheme was ment to be top secret! not for public consumption!, hivyo hivyo hizo kashfa hazipo?. Hata mimi, nikiwa na wewe tuu peke yetu kwenye chumba au kwenye lift, nikakutikana bila mtu yoyote kusikia, huwezi kunishitaki eti nimekuvunjia heshima!. Ili nikuvunjie heshima, lazima a third part asikie!. According to to the codes of secrecy za waraka ule, its considered only insiders tuu ndio walijua!. Zamani dada zetu na mama zetu, walibakwa sana ila hawakudhubutu kusema to any third part itakuwa ni aibu!, mbakaji huwa ana strike again and agai and again kwa sababu mbakwaji would radher keep secret ya kubwaka kuliko aibu ya kusema!. Chadema ndio walio leak huo waraka na kumuibisha jemedari wao!.
Siasa ni kama vitani, kuna point ukifika ni no retreat, no surrender, you fight from within!, huwezi kulikimbia shamba ukawaachia ngedere watafune mahindi!. Nape alipombwatukia Lowassa kwenye issue ya UVCC nini kilimtokea?!, si alifukuzwa JK akamuokoa!. Alipotangaza vua gamba, nathing was done!, amejiuzulu, si anaendelea ku fight from within!?. Juzi yeye na Kinana walipoibuka na mawaziri mizigo, JK si amewapuuza?!, wamefanya nini?, walipaswa kujiuzulu!, ila wajiuzulu na kuwaachia gedere wamalize shamba?!, its fighting from within!. Si mmemuona Nape kaibuka na ile hangover ya party supremacy ati CCM itawa summons mawaziri na wakuu wa taasisi za umma!?, CCM iwa simmon mawaziri hiyo CCM ikiwa ni kama nani?, kwenye mfumo wa serikali, what the hell is CCM?, Nape anaota ndoto za alinacha mchana kweupe!. Wenye akili na busara baada ya kuona jahazi linakwenda mrama, captain hawezi tena kuongoza jahazi, dawa ni kuabandon jahazi na kujitosa ndani ya maji au ku replace captain na kuokoa jahazi?!.

Chama si kina chain of command, ushinde kumuondoa jemedari, hali uende kwa wapiganaji usema jemedari hafai?!. Gimme a break!.

Hayo ni mambo ya ndani, au unataka waendelee kumwaga mbiga kwa sababu wenzao wamamwaga ugali?!. Mtafute ZIITO, Kittila na Mwigamba watakueleza one to one!. Siku ile nilipopandisha ile thread ya Chadema kunyofoa kipengele cha ukomo wa madaraka kinyemela, I got a call fro one of them, (not ZZK), kanieleza ukweli ulivyo na jinsi Dr alivyotoa uongo!, sikuweza kusema Dr. ni muongo kwa sababu, pamoja na yote namheshimu sana tuu!. Kwenye hili sakata kuna mengi hayasemwa, nimeshauri wasiendelee adding an insult to an injury to the damage already done!.
Pasco.
Mkuu Pasco umemaliza yote na sinto changa tena kuelezea kitu kile kile ulichomaliza na kufunga darasa!..Niko tayari kukaa ktk mtihani - waulete!
 
Back
Top Bottom