Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

Wakuu mag3 na nguruvi3,mna maoni gani kuhusiana na kura ya turufu ya rais obama kwenye mswada wa JASTA,kukataliwa na bunge la congress,hakuna athari ya moja kwa moja kwenye uchaguzi wa november kwa wagombea hawa wanaochuana vikali!!?? Km mswada utabaki hivi na kuwa sheria,nani atanufaika kati ya Replican na Democrat na km wabunge watabatilisha uamzi wao nani atanufaika!!? Nimesoma mahali baadhi ya wabunge wa replican wameanza kujutia maamuzi yao. Hebu nipeni maoni yenu..
Suala zima limefanyika katika mtazamo wa uchaguzi.

Mswada umepingwa katika hali ya kuchonganisha wananchi na Obama/Democrats

Akiongea na Veterans Obama amelieza vema kwanini ali veto.

Ukiangalia kura ndani ya seneti na congress mswada umepita kirahisi na kwa kura nyingi bila kujali vyama

Hili maana yake ilikuwa kutengeneza mazingira kuwa Democrats wanakataa familia zisiweze kushtaki Saudia.

Kwa maneno mengine ni kuwaweka Democrats wanaogombea seneti na congress katika mazingira ya kushindwa

Nao kwa kuhofia 'backlash' ya wananchi wakapinga veto

Katika mdahalo ujao hili litaulizwa wagombea walitolee ufafanuzi

Clinton ana wakati mgumu kumpinga Obama au kukubaliana na wabunge.

Trump anaweza kusimama nalo limjenge, lakini lazima awe na ufahamu wa kutosha kuhusu mambo ya ulinzi, kinyume chake lita mu'expose' katika mazingira mengine magumu kama ilivyokuwa NATO mdahalo uliopita

Hata hivyo karata zinaweza kuchezwa na Dem ili kuhakikisha haliathiri matokeo ya uchaguzi na haliwi agenda katika siku za mwisho

Obama haku veto kwasababu tu alitaka.
Alifanya hivyo kwa kuzingatia usalama na masilahi ya nchi.

Alikuwa na taarifa kutoka vyombo vya ulinzi na usalama.

Sasa kwamba lina athari katika uchaguzi, hilo ni wazi kwasababu nia nzima ililenga uchaguzi na itaendelea kuwa hivyo.
 
TRUMP ''AKUBALI'' , MDAHALO ALISHINDWA

MAGAZETI MAKUBWA YAFANYA ENDORSEMENT

Bandiko 341 aliloleta Mag3 lilizungumzia kuhusu poll zinazofanyika
Kwa sehemu kubwa uchaguzi wa US ni sehemu ya ''biashara''

Kuna matumizi na mbinu nyingi za teknolojia katika kutafuta ushindi
Tunakumbuka 2012 Polls zikionyesha 'dead heat' kati ya Obama na Romney

Matokeo hayakuwa karibu na 'margin of error' kwa viti zaidi ya 63

Baada ya mdahalo Trump alizunguka akisema ni mshindi kwa 'polls' za online. Alilalamikia ''main stream media'' kuwa biased

Tulisema hapa jamvini, kwa vigezo vyote hakufanya vizuri.

Surrogates na Pundits wake walikubaliana na hilo isipokuwa Trump

Kwa mfano suala la Alicia Machado limeendelea kuwa mazungumzo

Udhaifu wa kuibua hoja, na kwamba alishindwa kumweka HC 'on defense'

Kila hoja aliyoibua ilimrudi vibaya kutokana na maadilizi hafifu

Habari zilizopo, Gavana wa New Jersey Christie atamnoa kwa mdahalo ujao. Hili linaeleza 'amekubali' hakufanya vema

Katika hali nyingine isiyo ya kawaida, gazeti lenye mrengo wa Republican la Dallas, limefanya 'endorsement' kwa kampeni ya Clinton.

Halijawahi kufanya hivyo tangu vita kuu ya pili ya dunia

Gazeti la Arizona lililojulikana awali kama Republican Arizona, limefanya endorsement pia. Hii ni baada ya miaka 120 ya gazeti hilo

Jana, gazeti la Detroit kama hayo mengine limefanya vivyo hivyo

Haya ynaeleza tatizo kwa upande wa Trump kuelekea uchaguzi

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3, the polls are not even close kama wanavyodai mashabiki wa Donald Trump, wameamua tu kumpandisha chati licha ya kampeni yake kudorora. Republicans wako vizuri tu katika kutengeneza polls feki na ndio maana wamebakia kulaumu polls zilizotengenezwa kitaalam.

Mfano ni poll ya juzi ya Nevada kuonesha kuwa asilimia ya wenye asili ya Latino inazidi kuongezeka kumuunga mkono Trump wakati ukweli ni kwamba inazidi kupungua. Juzi baada ya debate walidai Trump anaongoza kwa asilimia kidogo lakini leo imethibitika Clinton yuko mbele kwa pointi 6 (44% kwa 38%)

Huko Florida nako walitengeneza polls zinazoonesha Trump anaongoza lakini imethibitika kuwa Clinton anaongoza kwa pointi 4 (46% kwa 42%). Tusisahau kwamba hizi ni key swing states ambazo Trump hatakiwi kushindwa kwa namna yoyote kama anataka kuukwaa Urais wa Marekani.

Clinton kwa sasa anaongoza jumla ya swing states nne nazo ni Florida, Michigan, Nevada, na New Hampshire. Ndugu yangu magode, amini usiamini kosa kubwa limefanyika kwa Congress kupiga kura kuizima veto ya Rais Obama. Congress ya sasa ni ya hovyo kuliko wakati wowote mwingine ule na uamuzi huu wataujutia.
 
Ha haa haaa mag3 "Huu mchezo hauhitaji hasira". Kwa nini unasema ni kosa kubwa kwa congress kukataa kura ya uamzi ya Rais obama wakati bunge liliamua kusimama na waathirika wa shambulio la 11/09.!!?
 
Ha haa haaa mag3 "Huu mchezo hauhitaji hasira". Kwa nini unasema ni kosa kubwa kwa congress kukataa kura ya uamzi ya Rais obama wakati bunge liliamua kusimama na waathirika wa shambulio la 11/09.!!?
Ingawa ume address kwa Mkuu Mag3, ningependa kuchangia

Obama ali veto mswada kwa kutumia haki yake kikatiba ambayo inamlinda au kumhukumu leo au siku zijazo

Kutumia veto hakutokei tu kwa asubuhi moja. Waathirika wa 9/11 wametenngenezewa utaratibu wa malipo na serikali ya Marekani. Veto ilitokana na ushauri wa vyombo vya ulinzi na usalama ukizingatia masilahi ya US

Congress na Seneti wameleta mswada huu makusudi kutimiza haja za kisiasa bila kuangalia mantiki ya Obama

Hilo limewalazimisha Dem kwenda kinyume na kiongozi wa chama chao, na inaeleweka

Itakuwa ni hatari Zaidi kwa Rais ajaye kuwa na congress na seneti chini ya Republican

Dem wana tuumaini Rais ajaye atatoka chama chao. Wasingependa apate filibuster anazopata Obama

Kwa mswada huu, maana yake ni kuwa na mtafaruku na Saudia.

Hili halionekani kama tatizo kwasas, ieleweke kuwa kuna interest katika suala la ulinzi wa middle east.

Ingawa uhusiano huo ni 'rogue and vague from time to time' ukweli utabaki Saudia ni mshirika mkubwa wa interest za US eneo hilo

Obama alipokataa alizingatia mambo mengi Zaidi ya politics. Mbele ya safari kutakuwa na tatizo

Kusimama na waathirika wa 9/11 kunachagizwa na siasa Zaidi ya long term strategy za ulinzi na usalama

Tusemezane
 
MDAHALO WA VP

Utafanyika leo hii kati ya Tim Kaine na Mike Pence wa Republican

Kwa kawaida midhalo ya VP haina nguvu na matokeo huisha baada ya muda mfupi

Mwaka huu ni tofauti kidogo. Waombea urais Trump na Clinton wana umri mkubwa

VP wao wanaangaliwa kama potential president kama litatokea lisilo tarajiwa

Mike Pence wa Republican ni mzungumzaji mzuri na huenda akatumia nafasi hiyo kuziba pengo la Trump

Tim Kaine si mzungumzaji mzuri 'boring' na hilo linaweza kuleta tatizo kwa Democrat

Hali ilivyo sasa , kura za maoni katika swing states zinampa nafasi HC.

Ile momentum aliyokuwa nayo Trump inaonekana kufunikwa na mawili mbaya.

Kwanza, suala la Alicia Machado limechukua muda mrefu, na pili suala la kodi likaingia kati na kuzorotesha

Mike Pence ana kazi ya kumtetea Trump na kuonyesha kuwa Clinton ni insider na hana mabadiliko

Mike Pence ana nafasi nzuri ya kumshambulia Clinton kwa yale Trump aliyoshindwa

Shida itakuwa ku balance misimamo yake na misimamo ya Trump

Tim Kaine, anatakiwa kutetea rekodi ya Clinton ima kwa mazuri na mabaya.

Atakuwa na kazi ya kumfungamanisha Trump na Pence ili kuendeleza flip flop za Trump

Kwa hali ilivyo, Mike Pence wa GOP anasimama katika nafasi nzuri kushinda mdahalo.

Kwa pence si suala la kushinda kwa uchaguzi huu bali kujenga jina kwa siku za baadaye.

Tutawaletea habari kadri zinavyokuja

Tusemezane
 
Mdahalo unaendelea na kwa mtazamo wa haraka, Seneta Kaine anaonekana kumshambulia mwenzake
Tatizo linalomkabili Gavana Pence ni rekodi ya Trump. Mara nyingi ameshindwa kutetea hoja za Trump

Tathmini inaendelea
 
TATHMINI

Mdahalo uliokuwa na majibishano umemaliza

Yapo yaliyojitokeza kwa VP CANDIDATES

Wote: Inaonekana walifanya 'homework' zao vizuri na kujiandaa

Mikakati
Pence: Alifahamu wazi kuwa Trump ana 'mazonge zonge' yake. Mike Pence alichokifanya ni kujiweka mbali na Trump na mara zote alishindwa kutetea kauli za Trump.

Kaine: Alifanya kazi nzuri sana ya kuwa na facts na aliweza kumtetea Hillary Clinton.
Kazi yake ilikuwa kushambulia Trump na rekodi yake

Matatizo
Pence: Kama tulivyosema bandiko lililotangulia,Pence alichokifanya ni kujenga jina lake na si kutetea tiketi. Kwa Republican wengi wanaona alipaswa kuwa top ticket

Tim Kaine: Inaonekana alijiandaa na alikuwa 'excited'.
Kila mara aliingilia mwenzake alivyozungumza na kuonekana hana subira.
Kwa sehemu Fulani hasa dakika 20 za mwanzo, Kaine alionekana kuwa na papara

Kutokana na kiu ya kujibu hoja, Kaine aliimsaidia Pence kwenye hoja nzito alizotakiwa kujibu. Mjadala ukaondoka kwenye swali (mwiba) na kumwacha Pence amelikwepa

Picha ya mjadala
Inaonekana mshindi ni Mike Pence kutokana na utulivu na alivyoweza kukwepa maswali kwa kubadilisha kibao. Kaine alijichanganya kwa kutokuwa na subira na pili, kumuokoa Pence

Matokeo ya awali yanaonyesha Pence amefanya vema kuliko ilivyotarajiwa kwa ujumla.

Kwa kuangalia nani ametengeneza kesi kwa mpinzani na kisha kumtetea mgombe, Kaine anapewa ushindi

Mjadala huu umemnufaisha Pence, matokeo mabaya kwa Trump, atajenga jina.

Hili nalo lina matatizo, ndani ya kambi ya Trump kuna manung'uniko kuwa Mike Pence ameshindwa kumtetea Trump.

Kwasasa wachambuzi wanafanya facts check na tutawaeletea kila linalojiri.

Huu ni mtazamo wa awali wa mdahalo wa wagombe
 
TATHMINI

Mdahalo uliokuwa na majibishano umemaliza

Yapo yaliyojitokeza kwa VP CANDIDATES

Wote: Inaonekana walifanya 'homework' zao vizuri na kujiandaa

Mikakati
Pence: Alifahamu wazi kuwa Trump ana 'mazonge zonge' yake. Mike Pence alichokifanya ni kujiweka mbali na Trump na mara zote alishindwa kutetea kauli za Trump.

Kaine: Alifanya kazi nzuri sana ya kuwa na facts na aliweza kumtetea Hillary Clinton.
Kazi yake ilikuwa kushambulia Trump na rekodi yake

Matatizo
Pence: Kama tulivyosema bandiko lililotangulia,Pence alichokifanya ni kujenga jina lake na si kutetea tiketi. Kwa Republican wengi wanaona alipaswa kuwa top ticket

Tim Kaine: Inaonekana alijiandaa na alikuwa 'excited'.
Kila mara aliingilia mwenzake alivyozungumza na kuonekana hana subira.
Kwa sehemu Fulani hasa dakika 20 za mwanzo, Kaine alionekana kuwa na papara

Kutokana na kiu ya kujibu hoja, Kaine aliimsaidia Pence kwenye hoja nzito alizotakiwa kujibu. Mjadala ukaondoka kwenye swali (mwiba) na kumwacha Pence amelikwepa

Picha ya mjadala
Inaonekana mshindi ni Mike Pence kutokana na utulivu na alivyoweza kukwepa maswali kwa kubadilisha kibao. Kaine alijichanganya kwa kutokuwa na subira na pili, kumuokoa Pence

Matokeo ya awali yanaonyesha Pence amefanya vema kuliko ilivyotarajiwa kwa ujumla.

Kwa kuangalia nani ametengeneza kesi kwa mpinzani na kisha kumtetea mgombe, Kaine anapewa ushindi

Mjadala huu umemnufaisha Pence, matokeo mabaya kwa Trump, atajenga jina.

Hili nalo lina matatizo, ndani ya kambi ya Trump kuna manung'uniko kuwa Mike Pence ameshindwa kumtetea Trump.

Kwasasa wachambuzi wanafanya facts check na tutawaeletea kila linalojiri.

Huu ni mtazamo wa awali wa mdahalo wa wagombe
Mkuu Nguruvi3
Matokeo ya mdahalo huu wa wagombea wenza utaleta mabadiliko yoyote kwenye kura za maoni? Hususan kwa upande wa Trump performance ya Pence itamsaidia kumpandisha chati kidogo?
 
Mkuu Nguruvi3
Matokeo ya mdahalo huu wa wagombea wenza utaleta mabadiliko yoyote kwenye kura za maoni? Hususan kwa upande wa Trump performance ya Pence itamsaidia kumpandisha chati kidogo?
Mkuu kuna sehemu tatu kuhusu hili.

Kwanza, siku za nyuma VP ni wasindikizaji na midahalo ili base katika policy za wagombea

Wao walikuwa na kazi ya kuonyesha watafanyaje kazi na Seneti tukijua role ya VP

Pili,Kutokana na umri wa wagombea na utata wa haiba zao, inaonekana VP ni muhimu kwasababu anytime anaweza kuwa Rais.

Hilo ndilo limebadili ile hali ya awali kama ilivyogusia aya ya kabla

Tatu,kumekuwa na utata hasa Republican ambao kwao Trump hasimamia agenda

Anaongea kama conservative,kama 'tea party', wakati mwingine PC na Liberal

Kwa mantiki hizo, mjadala wa VP traditionally huisha mapema,mvumo ni kidogo sana

Hata hivyo, kwa 2016 mvumo wake utaendelea kwa muda na hivyo kuwa na impact

Kwa upande wa Dem hauna madhara ya moja kwa moja, Kwa Trump unayo

1. Republican wakimsikiliza Trump na Pence wanaona kwa uhakika Trump ni garasa

2. Kuna Republican wanaomwamini Trump,wamepata imani kuwa Pence atamweka sawa

3. Kuna hoja Kaine wa Dem amezionyesha, Pence hakuzitete.
Maana yake ni kuwa zimemweka Trump vulnerable zaidi.
Alichokifanya Kaine ni kutengeneza kesi ambayo wananchi wanataka majibu

Kwamba mjadala utakuwa na impact ya moja kwa moja kwa undecided au independent, jibu ni hapana

Mjadala umesaidia Trump kampeni, jibu ni ndiyo.
Haukubadilisha msimamo umezuia majereha ya wiki mbili mbaya kwa Trump.
At least kuna different story

Mdahalo umesaidia Dem, jibu ni yes. Utabadili msimamo wa watu, jibu ni hapana.
Walichofanya Dem ni ku prosecute case na Pence ameshindwa kutetea
 
KAMPENI YA CLINTON NA HOFU NYINGINE

Suala la emails, Clinton foundation na Benghaz yanaonekana kupoteza nguvu japo kwa muda
Ingawa yanajirudia rudia, matukio mengine yanayomhusu Trump yanafunika hoja hizo

Kwa mfano, Trump anasema atatoa taarifa zake za kodi Clinton atakapotoa emails, 33,000

Tangu aingie katika harakati za uchaguzi, Trump amesema ana 'audit' si vema kutoa taarifa za kodi.

Wataalam wa mambo ya kodi na idara husika zimesema hakuna sheria inayozuia hilo

Hoja iliyopo ni kuwa Trump atoe taarifa za kodi za nyuma zisizo kaguliwa.

Lipo gazeti limetoa taarifa kuonyesha Trump hajalipa kodi kwa miaka zaidi ya 10

Hili linakinzana na utetezi wake kuhusu emails, na kuonekana hana sababu bali anaficha jambo

Baada ya mdahalo wa kwanza, Clinton anaonekana ku gain katika swing states na national wide

Hata hivyo, kampeni yake imeingiwa na wasi wasi kuhusiana na kauli ya Wikileaks

Wikileaks wanasema watavurumisha dhoruba nyingine ingawa hawakusema ni lini

Tukijua computer zilizokuwa hacked ni za Democrats, ni wazi hilo linawatia wasi wasi

Lini Wikileaks watatoa habari! ni suala linalosubiriwa

Kuna namna tatu wanazoweza kufanya

1. Kutoa taarifa hizo kuelekea mdahalo wa pili ili ziweze kumweka pagumu Bi Clinton
2. Kutoa taarifa hizo kuelekea au baada ya mdahalo wa tatu
3. Kutoa taarifa hizo siku chache kabla ya uchaguzi

Na inaelekea ni 'mabomu' makali yatakayoyumbisha kampeni ya Clinton

Hili linatia hofu na shaka ndani ya kampeni ya Clinton

Tusemezane
 
Katika kinachoitwa the historic move, the Atlantic imem-endorse Hilary Clinton. The Atlantic imewahi kufanya hivyo Mara mbili Tu katika historia ya Marekani.

Mara ya kwanza ililkuwa miaka 104 iliyopita ilipom-endorse Abraham Lincoln. Mara ya pili Ni pale ilipom-endorse LBJ dhidi ya mbaguzi Goldwater.

Na sasa imefanya hivyo kwa Mara nyingine dhidi ya mgombea inayemuona kama wa hovyo kupita wote waliowahi kujitokeza kugombea Urais, Donald Trump.

Kwa kweli nawashangaa wote humu JF wanaompa huyo mhuni nafasi yoyote ya kuiongoza Marekani ninayoifahamu! Kosa kama Hilo haliwezi kutokea huko.

The Atlantic Ni gazeti linaloheshimika lililoanzishwa Mwaka 1857 Boston Massachusetts na limejitahidi kutokuwa na upande kisiasa isipokuwa pale mambo yanapoelekea kuharibika.
 
Na hii mpya imetoka...

Donald Trump's bankruptcy lawyers say he lies so much they could only meet with him is pairs.

Kwa uongo wake hakuna mwanasheria wake aliyekuwa anakubali kuongea na yeye bila kufuatana na mwenzake kama shahidi kwa yaliyozungumzwa. Pamoja na kuwa muongo, yuko tayari kukanusha maneno aliyoyatamka kwa mdomo wake na kukataa hakuyasema.

Huyo ndiye Donald Trump...muongo, tapeli, mdhulumiaji, mbinafsi, asiye na huruma, mjuaji, mwenye majivuno, dharau na asiye na haya. Wamarekani hawawezi kumchagua mtu kama huyu hata iweje.
 
KUELEKEA MDAHALO WA PILI

TIMBWILI LA TRUMP NA VIDEO YA AIBU

CLINTON NA WIKILEAKS

Mdahalo wa pili wa wagombea Urais ni siku ya Jumapili wiki hii. Huu ni mjadala unafuati wa kwanza ambao Trump alifanya vibaya kwa vigezo vyote. Zaidi ya hapo, suala la Alicia Machado likachukua nafasi

Ilikuwa ni wiki nzima ya sakata la Trump ambayo ilileta tatizo kubwa kwa kampeni yake

Trump alichukua muda wa siku tatu kujiandaa na mdahalo kuepuka 'dhahma' iliyomkuta.

Video inayomuonyesha Trump akitoa kauli za dharau kwa mwanamke na wanawake imetokea
Ni habari kubwa iliyovuta hisia katika vyombo vya habari hasa wanawake

Trump ana rekodi mbaya dhidi ya wanawake, hili lilikoleza ile dhana ya misogyny

Tayari viongozi wa Republican wamejitokeza kulaani kitendo hicho. Spika wa Congress amefuta ziara yake Wisconsin alikokusudia kukampeni na Trump. Congressman wa Utah ametangaza kutompigia kura

Kiongozi huyo wa Utah amefikia mahali akitaka GOP wamweke Pence kama mgombea

Trump amejitokeza katika video, akikubali na kuomba msamaha kwa video hiyo. Trump amekwenda mbali na kulihusisha suala hilo na Clinton na Bi Clinton katika jitihada za kupunguza nguvu.

Trump amesahau kuwa Clinton hagombei na hana hukumu katika kampeni hizi. Mkewe ni victim tu

Video hii ilipangwa kutolewa baada ya kampeni, lakini yupo aliyeivujisha masaa 48 kabla ya mdahalo

Damage inayotokana na video hiyo kwa kundi la akina mama ni kubwa sana. Jitihada zinazofanyika ni kuwanusuru maseneta na wabunge wasiadhibiwe kwa makosa ya Trump.

Trump na kundi linalomwamini hawawezi kupoteza wapiga kura kwa upande. Kitakachotokea hawataweza kuongeza wapiga kura hasa wanawake, na indpendents sasa ndio watapukutika.

Ndiyo maana kampeni ina haha sana, kwani kuondoa kundi la wanawake ambalo alikuwa na wapiga kura wachache, kuondoa watu wa rangi na walatino hakutoi namba 270

CLINTON
Bandiko 331 tulisema WikiLeaks watamwaga mzigo kabla ya mdahalo.

Ndicho kimetokea kwa kutoa emails za Clinton zinazopitiwa na wanahabari kwa wakati huu.

Hili lilikuwa ni dhahiri na limepangwa,hata hivyo video ya Trump imechagiza kutolewa hizo emails

Kwa upande huu, Dem wasilaumu WikiLeaks , tulisema mwanzoni mwa mwaka mtu atakayeimaliza Dem si Republican, ni Bernie Sanders.

Huyo ndiye aliwapa kitabu chote na sasa wanakitumia

Hili la email litasaidia sana suala la Trump kupungua nguvu ingawa limegusa sehemu kubwa ya jamii ya akina mama na haliwezi kutokemea kirahisi

Tusemezane
 
Courting rituals change over time, but it was probably never OK to do what Donald Trump told Billy Bush he did to woo an unnamed woman. In 2005, Trump was chatting with the TV anchor without knowing a live mic recorded some graphic comments he made.
Source :RT
========
Duh!! Wameamua kweli. Kushinda na Wall Street ni kazi ngumu. Yaani hapa wanataka Hillary Clinton apite bila kupingwa! !!
 
Mkuu mag3 kitu kimoja usichokielewa ni kwamba,huyo usiyempenda ndo Rais ajaye wa US. Kumbuka Trump kashfa zake zote ni zile za kibinafsi ukilinganisha na makosa HC ya kisiasa. Tatizo umeelekeza sana ushabiki ukaweka pembeni uhalisia. Hakuna asiyejua km trump ni dhaifu,lkn hata Hilary ni dhaifu zaidi..!!

Kinachomsaidia Donald trump,hajawahi kuwa kiongozi wa kisiasa. Ndo maana amesema wakati akiomba radhi kuhusiana na video mpya iliyotoka kumhusu,alisema bill clinton aliwahi kutoa maneno ya kashfa zaidi wakati wakicheza golf. Lkn haikumuondolea sifa ya kuwa Rais. Me nakuhakikishia,uchaguzi wa awamu hii wagombea wote ni dhaifu,lkn bi clinton ni dhaifu zaidi...!!
 
Mkuu mag3 kitu kimoja usichokielewa ni kwamba,huyo usiyempenda ndo Rais ajaye wa US. Kumbuka Trump kashfa zake zote ni zile za kibinafsi ukilinganisha na makosa HC ya kisiasa. Tatizo umeelekeza sana ushabiki ukaweka pembeni uhalisia. Hakuna asiyejua km trump ni dhaifu,lkn hata Hilary ni dhaifu zaidi..!!

Kinachomsaidia Donald trump,hajawahi kuwa kiongozi wa kisiasa. Ndo maana amesema wakati akiomba radhi kuhusiana na video mpya iliyotoka kumhusu,alisema bill clinton aliwahi kutoa maneno ya kashfa zaidi wakati wakicheza golf. Lkn haikumuondolea sifa ya kuwa Rais. Me nakuhakikishia,uchaguzi wa awamu hii wagombea wote ni dhaifu,lkn bi clinton ni dhaifu zaidi...!!
Tatizo lenu wengine ni kwamba mnaufuatilia uchaguzi wa Marekani kwa macho ya Kitanzania. Mtu kama Magufuli hangeweza kuchaguliwa kuwa Rais Marekani hata kwa kutambika.

Kwa ufahamisho wako Rais wa Marekani ajaye tayari atakuwa amejulikana mwisho wa mwezi huu hata kabla ya siku yenyewe ya uchaguzi. Kura za awali zimeshaanza kupigwa na wachambuzi tayari wanauona upepo unakoelekea.

Pamoja na hayo, Je unafuatilia mtifuano unaojitokeza GOP? Bila shaka wewe umejikita kumsikiliza Sean Hannity wa Fox News. Kila mgombea wa GOP anahaha kukaa mbali na huyo mgombea mhuni na tapeli...stay tuned!
 
Kitendo cha kusema tu kuwa atakuwa amejulikana mwishoni mwa mwezi kinathibitisha kwamba ww mwenyewe huna uhakika na unachoongea. Wewe unasubiri wamarekani waamue nani ataliongoza Taifa hilo kwa kipindi cha miaka 4 ijayo km mimi nnavyosubiri.

Yaani km unavyoshangaa ww kwa sisi tunaofikiri trump ana nafuu ukilinganisha na huyo mama!. Na me nakuambia,wamarekani muda wa kuongozwa na mwanamke bado. Watakuja kuongozwa lkn si huyu asiyeaminika!
 
SAKATA LA VIDEO YA TRUMP

'REPUBLICAN RANKING' WATAKA AACHIE NGAZI

RULE 9 YA GOP ITAWEZEKANA?

Kutwa nzima suala la video ya aibu ya Trump limerindima katika anga za habari.

Pamoja na Trump kuomba radhi hali haionekani kutulia hasa kwa Republican

Viongozi waandamizi wamejitokeza kwa wingi 'avalanche' wakitaka mambo mwili

1. Trump ajiuzulu nafasi hiyo na Mike Pence achukue nafasi yake
2. RNC waondoe resource zake na kuuunga mkono wabunge na maseneta wanaogombea

Viongozi hao wali 'disown and disavow' Trump. Hata VP pence ametoa kauli ya kulaani video husika

Trump amekaririwa na wall street journal alisema hatajizulu na leo jioni atakuwa na mkutano

Kutokana na pressure kutoka republican, swali ni je, akijiuzulu inawezekana Pence kuchukua nafasi?

Jibu la swali hilo lipo sehemu mbili, ndiyo na hapana

Ndiyo ni kwasababu ipo rule 9 ya RNC inayorhusu kuwepo kwa mbadala kama ikitokea dharura.
Sheria hii ililenga hasa panapokuwa na dharura ya kifo, lakini siyo limited, inaweza kutumika vinginevyo

Rule 9 inasema ikitokea hivyo basi convention (mkutano mkuu) unaitishwa kupata mgombea.

Kwasasa hilo haliwezekani kwani zinahitaji resource na muda haurusu.
Kumbuka katika convention kila state inawakilishwa na wajumbe, mfano NY 95 au 100.

Rule 9 inasema convention ikishindikana RNC inakutana kwa niaba ya convention.
Katika uchaguzi kila state itakuwa na kura 1 na si idadi ya wajumbe kama convention.

Hii ina maana, na kwa mfano, Ohio ikiwa na wajumbe 60 hiyo ni kura 1 kama watakubaliana wote.

Wasipokubaliana hiyo 60 itagawanywa katika pande kinzani na kisha asilimia itakayotoa 1` itapatikana
Ni sheria ngumu kidogo kuzitafsiri lakini hii ni kwa ajili ya uelewa tu

Jibu la Hapana kama tulivyoeleza linazingatia ukweli kuwa rule 9 inawezekana lakini itakuwa na athari kwa Republican. Tayari kuna state zimeanza kupiga kura 'absentee ballot'

Uwepo wa mgombe mwingine utakuwa na athari katika idadi ya kura atakazopata huyo mpya

Way forward: Ni kama vile GOP wamekubali yaishe kutokana na ukweli unaoambatana na rule 9

Focus yao kwasasa ni kuhakikisha wanapata maseneta na wabunge wengi wa congress

Tutaendelea kuwaletea hali ilivyo kila muda hadi kufikia mdahalo

Tusemezane
 
GOP TURMOIL

BEN CARSON NAYE ALAANI

Democrats na Hillary Clinton wamekaa pembeni makusudi wakiacha GOP wajikaange kwa mafuata yao
Katika hali isiyotarajiwa, mgombea wa zamani Dr Ben Carson ambaye ni mtiifu kwa Trump amelaani tukio

Kinachozua tafrani katika sakata hili ni jinsi linavyohusishwa na Republican.
Tangu video itoke, wapiga debe wakiwemo wa GOP wamezungumzia umuhimu wa GOP kujtakasa na sakata

Ukubwa wake ni pale ulipogusa wanawake kwa ujumla wake. Inaonekana mgombea wa Republican ambaye ametiliwa shaka mara nyingi kuhusu maadili yake sasa anabeba message inayowaumiza Republican

GOP wanachokifanya ni kujitenga na kauli za Trump ili zisiwe za chama kwa ujumla
Athari zake zinaweza kwenda mbali hadi uchaguzi wa maseneta na wabunge

Kama Trump atalihusisha na Clinton hilo litakuwa kosa.

Bill Clinton hagombei Urasi, na Hillary ni victim wa mauza uza ya Bill.
Hivyo atapata sympathy ya wanawake kuliko ku balance, kama Trump anavyodhani

Lakini pia litaibua mjadala mpana wa video ya leo na kuleta uharibifu mkubwa katika mjadala wa kesho kwa upande wa Trump

Tunafuatilia kwa ukaribu hali ilivyo
 
Back
Top Bottom