Duru za siasa: Vijana, katiba mpya na kiu ya uongozi

Duru za siasa: Vijana, katiba mpya na kiu ya uongozi

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
KELELE ZA UJANA NA MBIO ZA UONGOZI
HAWANA MAONO, HAWAJIAMINI, WAMEBAKI KULAMBA MIGUU
WAMEVAA NGOZI ZA CHUI, NI WOGA KAMA FISI, NA WASALITI KAMA YUDA


Sehemu ya I kati ya 2

Wanaduru
Tuliwahi kuambiwa vijana ni taifa la kesho na nguvu ya taifa lijalo.
Ghafla vijana wakacharuka na kusema wao ni taifa la leo na nguvu ya leo.
Usemi huo ukabadilisha mitazamo ya wananchi kwa matumaini makubwa.

Matumaini yaliyojengwa katika ukweli kuwa vijana ni wasomi,wamefunguka, wana maono na nguvu za kulisaidia taifa na kizazi cha leo.

Kauli mbiu ya vijana ikabamba, kila aliyetaka kupambana nao katika anga za siasa aliangaliwa umri na kutupiwa makombora ya uzee.

Wengi wakaogopa hata kutaja umri wao, wengine wakificha mvi zao, uzee ukawa janga.
Ukaingia unyanyapaa kwa wazee, busara zikachukua nafasi ya mwisho baada ya ujana na usomi.

Tuliaminishwa umasikini wa nchi hii unatokana na uzee, kwamba wazee walijifungia wakilewa ulanzi. Tukaaminishwa kuwa sasa ni zama za 'digital' hata vijana ni digital

Nafasi za upendeleo zikaanza kutolewa hata kuwa na mkuu wa Wilaya aliye na umri chini ya miaka 25. Bodi za mashirika na taasisi zikajazwa vijana kwa kile kilichosema wazee hawana jipya, hawana maono, kuteuliwa kwao ni kuweka mvinyo wa zamani katika chupa mpya.

Tambo zikahamia katika majukwaa ya siasa, vijana wakichaguliwa kwasababu ya umri na usomi wao. Bunge likasheheni wasomi wa kila aina na fani, wengi wakiwa ni vijana.

Makala zimeandikwa kuhusu vijana chini ya miaka 40, kama kwamba baada ya hapo uzee umepiga hodi na ndio ukomo wa fikra, maono au busara.

Matumaini yakawa makubwa, wananchi wakiwa na kiu ya kuona mbadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Wala hawakusita kuliangalia bunge kwa mtarajio ya kusikia fikra mpya, zilizotitia kwa maono, kujiamini na kuongoza.

Miaka 50 iliyopita hatukuwahi kuwa na bunge au baraza la mawaziri lililosheheni vijana kuliko miaka 8 iliyopita. Hali ni hiyo katika mashirika na taasisi.

Matumaini yakaanza kujengwa kwa muonekano wa vijana wachache waliosimama kutete nchi na taifa. Hao wakapewa heshima na kila walipotokea walipata mapokezi ya matumaini na furaha.
Kila kijana akitia chumvi ya ujana kwa kujinasabisha na hao wachache

Tukaanza kuwaona wazee kama watu wasiohitajika katika taifa hili.
Tuliwaona kama maadui walioturudisha nyuma, wasio na elimu,weledi na waliojaa inda na fitna.

Pengine bila kujua, Watanzania tumependelewa na mwenyezi mungu.
Kuna mambo yanayokuja kwa sababu maalumu kutusaidia.
Hili la ujana na uongozi ni mojawapo.

Hatuwezi kuona tahadhari kwasababu sisi ni wanadamu, mara nyingi hatujitambui na tunaongozwa na fikra zetu zaidi hata pale hekima inapotaka kuchukua nafasi yake.

Sote tumejikita kutafuta majina ya na umri ili kuliongoza taifa hili siku zijazo.
Tumejaza ujinga eti wazee wamechoka nasi twaitika 'ndiyo'

Leo kila kijana anatamani kuchukua fomu ili aelekee katika kasri la magogoni kuliongoza taifa hili. Shughuli za kuhonga boda boda, kugawa vitenge na kofia zinapamba moto.
Tumefumba macho na kusema hiki ni kizazi kipya, kile cha dijitali na bongoflavor.

Kama tulivyosema awali, vijana wa leo wana degree za kutosha, wamefunguka 'exposure' wanaifahamu dunia, ni wazuri wa kutumia teknolojia na ni mahiri kuchangamana na jamii.

Endapo hayo ndiyo tunaona ni vigezo vya uongozi wa nchi hii, hewala na iwe.
Kama tunataka kukimbia ili kuwafikia wenzetu lazima tuziangalie hekima za mwenyezi mungu.

Hekima hizo ni hizi zinazoendelea sasa katika bunge la katiba.
Bunge lililosheheni vijana na ujana, wa kike na kiume, mabinti na wabwanga.

Swali la kujiuliza, je ule ujana, maono,nguvu na uongozi unaonekana?
Wale tunaoambiwa wataliongoza taifa hili kuanzia Urais hadi ukuu wa wilaya wana sifa za ujana tunazoimba kila siku?

Hebu tuangalie kwa uchache, huu ujana,katiba mpya na uongozi kama vinakidhi haja ya ujana.

Tuwaangalie hao waliopo Dodoma ili kujiridhisha kuwa umri wa ujana unalisaidia taifa hili na tunahitaji vijana zaidi.

Vijana walioko Dodoma, je ni fahari au ni aibu ya taifa? Tunawategemea kwa lipi?
Je, ni wakweli wa mioyo na dhamira au ni mavuvuzela.
Je, wanauchungu na taifa hili au uchungu na matumbo yao kupitia mirija ya vyama vya siasa?

Wale walioko nje kama akina Nape wanatofuati gani na akina Mbatia, Kangi,Halima Mdee au Mwigulu? Wanaduru tuwaangalie vijana bila hila au hiana. Tutawaaalika mmoja baada ya mwingine waje hapa tuhangaike nao.

Hutwezi kuambiwa January wakati January wa mitaani si yule wa Dodoma!!

Kwanini tuwanyanyapaa wazee wanao ona zaidi ya lundo la vijana wasio na macho au masikio?

Itaendelea sehemu ya 2 kabla hatujasemezana.
 
Well, uchambuzi wako no sahihi, lakini zaidi umeegemea ktk kitu wanaita propaganda.Kabla haujaendelea zaidi, fanya kufuatilia, hiyo notion ya ujana ni Taifa la Kesho ilitolewa na nani na ni ktk kipindi gani? Na pia ujaribu kuangalia kwa umakini, ujanja uliozungumziwa ni wa into AMA wa kifikra na Mtazamo ?( maana hata wanaoitwa wazee kwa umri, wanapokuwa machachali ktk hoja, huitwa vijana). Thentutaongea Siasa sasa
 
baadhi ya maneno ya vijana kwa wazee
Quote By Zitto View Post

Let us be serious guys. Mnataka tutambae? Wazee wameishi maisha yao. Wameishi yetu na sasa tunataka kuwakopesha maisha ya watoto wetu?
January makamba, nape nnauye, mwigulu
wazee wameshachoka wanasubiri kufa
Ridhiwani Kikwete
"Kuna watu ambao wameshamaliza muda wao wa kuishi,muda wao wa kucheka hapa duniani lakini ndio wa kwanza kushadadia Serikali tatu, namshangaa Warioba anavyopayuka kuwa anataka Serikali tatu, Kila siku anafanya interview kwenye redio tv na magazeti,ameshikilia maoni ya watu''
 
baadhi ya maneno ya vijana kwa wazee

Hizi zote ni selected lies, AMA political propaganda, ni kama Chambo nyuma Yake ku nakuwa na ndoano, Ukirukia tu umenaswa, but that is how politics is, ila tukiongelea kwa Mtazamo tofauti na siasa, haileti maana, na hata kisiasa tu pia, ukianza kurudi nyuma ktk mizizi na ukaleta ktk uharisia kutokana na mabadiliko ya dhana, bado inaleta utata
 
Hizi zote ni selected lies, AMA political propaganda, ni kama Chambo nyuma Yake ku nakuwa na ndoano, Ukirukia tu umenaswa, but that is how politics is, ila tukiongelea kwa Mtazamo tofauti na siasa, haileti maana, na hata kisiasa tu pia, ukianza kurudi nyuma ktk mizizi na ukaleta ktk uharisia kutokana na mabadiliko ya dhana, bado inaleta utata

Selected Lies au Propaganda ni zipi: zilizowasilishwa na zumbemkuu au hayo maneno ya vijana waliopo kwenye nafasi za uongozi?

Haujaeleweka.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Selected Lies au Propaganda ni zipi: zilizowasilishwa na zumbemkuu au hayo maneno ya vijana waliopo kwenye nafasi za uongozi?

Haujaeleweka.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Selected lies ni Kama hizo quotes hapo juu zinazotumika Kama njia ya ushawishi wa kundi frani la watu( vijana ) kwa umri, kwasababu ya faida ya wingi wao, kwa manufaa ya watu frani.
In other ways ni kwamba, Propaganda Kama siraha kubwa ktk siasa ndiyo iliyotumika pia kupandikiza hiyo dhana ya Vijana ni Taifa la Kesho na kisha, baada ya mabadiliko ya nyakati ikatumika tena kubadili neno na kuwa Vijana ni Taifa la Leo.

Mabadiliko ya nyakati ( kwa jinsi nilivyoichukulia) ni pamoja na kuzingatia idadi ya uwiano Nadia ya vijana na wazee ( kwa umri), pale wanapoonekana kundi moja ni kubwa ndipo Kama njia ya ushawishi wa kuliteka huyengenezwa na hata kwa sasa Vijana ndio wanatumika Kama njia ya mtaji wa kisiasa. Fanya (thought experiment). Dhana ya ujana ipo ktk nchi zenye wingi wa vijana tu, na sio nchi zenye mfumo mzuri wa Democrasia , na sio nchi zenye uchumi imara na endelevu, Kama wanavyoziita third world countries

Kiasi nadhani nimewleweka ( Kama bado, still we can discuss)
 
Selected lies ni Kama hizo quotes hapo juu zinazotumika Kama njia ya ushawishi wa kundi frani la watu( vijana ) kwa umri, kwasababu ya faida ya wingi wao, kwa manufaa ya watu frani.
In other ways ni kwamba, Propaganda Kama siraha kubwa ktk siasa ndiyo iliyotumika pia kupandikiza hiyo dhana ya Vijana ni Taifa la Kesho na kisha, baada ya mabadiliko ya nyakati ikatumika tena kubadili neno na kuwa Vijana ni Taifa la Leo.

Mabadiliko ya nyakati ( kwa jinsi nilivyoichukulia) ni pamoja na kuzingatia idadi ya uwiano Nadia ya vijana na wazee ( kwa umri), pale wanapoonekana kundi moja ni kubwa ndipo Kama njia ya ushawishi wa kuliteka huyengenezwa na hata kwa sasa Vijana ndio wanatumika Kama njia ya mtaji wa kisiasa. Fanya (thought experiment). Dhana ya ujana ipo ktk nchi zenye wingi wa vijana tu, na sio nchi zenye mfumo mzuri wa Democrasia , na sio nchi zenye uchumi imara na endelevu, Kama wanavyoziita third world countries

Kiasi nadhani nimewleweka ( Kama bado, still we can discuss)

Nimekuelewa mkuu,
Ningependa kuchangia lakini kwanza nasubiri mleta mada amalizie sehemu iliyobaki ili mjadala uwe na mtiririko mzuri.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Nimekuelewa mkuu,
Ningependa kuchangia lakini kwanza nasubiri mleta mada amalizie sehemu iliyobaki ili mjadala uwe na mtiririko mzuri.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Karibu sana kiongozi , pia nasubili mleta mada, kwa nyongeza ya pili, bado Nina swali moja katika mabano nadhani linastahili kuwa sambamba na sehem a pili, acha tusubili.
 
Wakati tunamalizia bandiko la mwisho, ningependa kumueleza bwana Nkumbi kuwa hakuna propaganda kwasababu sijasema vijana wa itikadi gani ya kisiasa. Nimesema vijana.
Pili, Nkumbi asome maneno ya Zumbemkuu, hayo si yangu ni ya vijana.

Muhimu sana, angesubiri kwanza tumalize ili aweze kuonyesha propaganda zipo wapi na aelewe msingi wa hoja.
Sijui kama anakumbuka kuwa vijana wamelilia umri upunguzwe ili wapate madaraka.

Sijui anakumbuka kuwa JK alipogombe uongozi kauli mbiu yake ilikuwa ni ‘wakati wa vijana'.
Na sijui kama hakuna ukweli kuwa baraza la mawaziri na wabunge kwa miaka 8 ilyopita wamekuwa ni vijana kuliko wakati mwingine.

Tunashukuru sana kwa maoni yake, tunaomba tuendelee kuwa pamoja. Maana nzima ya mijadala ni kubadilisha maono.
 
Nguvu hapa nadhani umegusa pazuri, ukweli ni kwamba afadhali wazee kuliko hao vijana tunawasema. Na huu ni ushahidi wa statement niliyotanguliza.

Vijana wengi ambao wamepewa nafasi katika ungozi iwe wa kiserikali au kibiashara ama shughuli zisizo na kiserikali wamekuwa mstari wa mbele kujilimbikizia mali na kutafuta kuongeza madaraka pasipo kuwa na vigezo. Haijalishi vijana hawa wawe Chadema au CCM au independent wote wamekuwa na tamaa za kutajirika haraka haraka.

Vijana ambao hawajapata nafasi za uongozi nao wameweka dhamira kwamba kama watapata basi nao watakula, kwani mfumo ndio upo hivyo. Miaka hii kumi tumeona wimbi la vijana wengi wakipata nafasi mbalimbali kwenye sehemu mbalimbali iwe serikali au katika biashara, kilichoendelea ni skendal na ulafi. Tumeona Mh. Zitto alichofanya katika miaka hii 10, tumewaona kina Mwamvita Makamba.

Mfumo ambao umejitokeza kati ya mwaka 1995-mpaka leo ndio sababisho la matatizo, utaifa umepotea miyoni mwa Watanzania, watu wamekuwa wavivu kifikiri na kuamua. Kila mtu anataka kumiliki mali bila kutengeneza mchakato, vijana wajasilimali wamepungua na kila kijana anataka kuvaa tai na kukaa kwenye AC. Mfumo wa 1960s ulikuwa na muamko zaidi kuhusu utaifa kushinda leo.

Hakuna wa kumlaumu, ni sisi wenyewe. Wote tupo kwenye boti moja na tunapiga kasia pamoja. Wote tunataka rushwa iwe tupo kwenye office ya mkoa au kwenye bunge, sote tunajali posho iwe walimu wa sekondari au wabunge wakatiba. Na sote ni wavivu wa kufikiri iwe wanachuo UDSM au Mawaziri kina Nyalandu. Sisis ni zao la sisi sisi.

Hakuna sababu hata moja Tanzania kuwa masikini, nchi yenye watu 44 Million na Natural resources zaidi ya 100 Billion ziko kwenye kila kona. Tanzania ni masikini sababu Watanzania wameamua kuwa masikini. Tuliwapa dhamana hawajui wanachofanya, na wale wenye uweleo hata mdogo hawatakiwi kusikilizwa. Leo hii tumegundua gas, jee umeona mikataba tunayosaini? Vijana hao hao wanaisoma hii mikataba wakiwa na hang over za ajabu, vijana wamekalia Kuangalia Premium League na Champions League usiku kucha, elimu standard sasa imeshuka, halafu mnataka kwenye hii mikataba tukae na watoto waliomaliza Law Georgetown University? Wakati sisi tunawaza 10% wenzetu Kenya wanawaza kuondoa kabisa Umasikini.

Tanzania ni blah blah nyingi. Lazima apatikane raisi ambae atabadilisha mfumo wa kufikiri, tatizo lilopo ni physiological zaidi. Kama tutaendelee na adisiadisi hizi hizi wakati population inakuwa kwa zaidi ya 3% kila mwaka, tutajikuta tunaongeza masikini na speed yetu ya uzalishaji ipo pale pale. Wenye akili wanaenda kuleta toothpick China. I'm sick, cha ajabu no one sees the problem, i mean NO ONE.

Vijana wengi are just lazy, lazy kufikiri, lazy kutenda and worse zaidi lazy kuamua. Vijana ndio wataliangusha hili taifa, mark my word.
 
Inaendelea kutoka bandiko I

Sehemu ya II

Tulisema ni vema tukawaangalia vijana kwa yale yanayoendelea Dodoma. Tunasema Dodoma kwasababu ni nafasi nadra ya umma kuandika nyaraka muhimu ambayo vijana wanaotaka uongozi wanatarajiwa kuapa na kuilinda nyaraka hiyo.

Tunasema vijana bila kubagua itikadi zao za namna yoyote au kuleta jinsia n.k. Wote ni vijana.Wazo la kuandikwa kwa katiba mpya linaonekana kama la vijana.
Ukweli ni kuwa wazo hilo lilianzia kwa wazee baada ya kuona mambo hayaendi. Vijana wakalishikia bango.

Mchakato mzima ulivyoanzishwa ulikuwa na kila dalili ya hujuma.
Tumeshuhudia matatizo yaliyozikumba nchi nyingine kutokana nakatiba.
Vijana wa leo wamesoma, wengine kushuhudia matatizo hayo kwa macho yao.
Tujiulize wangapi walihoji hatari inayolinyemelea taifa kwa sasa?

Kuna hatari nyingi. Mfano, mchakato mzima unaweza kulimega taifa na Tanzania.
Pili, unaweza kuviza demokrasia na uhuni ukachukua nafasi.
Na mwisho, hatari ya taifa kutokuwa na muafaka na pengine kupelekea machafuko.

Tulitegemea vijana wawe mstari wa mbele, waache itikadi, watangulize utaifa.
Hilo halikutokea!!Lakini muhimu, kwasasa mchakato unaendelea, tulitegemea vijana waseme hili 'ndiyo' lile hapana kwasababu kadhaa. Hilo halijatokea.

Hatuhitaji kijana asimame na kutetea seriakli 3, wala kijana atetee serikali 2 au moja. Tunachohitaji ni vijana kutumia zile silaha walizotuahidi za 'nguvu, maarifa, maono na nyakati'.

Kinachoendelea kinasikitisha. Vijana wamefungiwa katika mikutano inayoitwa ya vyama, wakapanua midomo yao na kusomezwa magunia ili wasiseme.

Vijana tunaoambiwa wana nguvu wamekaa kimya wakiambiwa shut up na wazee tuliaombiwa wamechoka.

Lakini wazee wameonyesha busara, pengine ni muhimu ingawa hakuna degree yake. Wazee wamesimama na kusema wanataka ABCD wakitetea hoja zao kwa mantiki.
Si lazima tukubaliane na hoja zao, lakini ni muhimu kuzitambua hoja zao.

Mfano, Wazee akina Salim, Butiku, Warioba na wenzao ambao ni watoto watiifu wa mwalimu na tuliowategemea kutokubali lolote zaidi ya mafunzo ya Mwalimu wao.
Kwa busara zao wamekubali maoni ya wananchi hata kama hawakubaliani nayo.
Wanatetea mawazo hayo kwa mantiki dhidi ya dhamira zao, taifa likiwa kwanza.

Tukiangalia upande wa vijana, tulitegemea ima wawapinge wazee kwa hoja au wajenge hoja za hoja zao kwa mantiki. Hailo halitokei, tunachosikia ni wao kuwa mafundi wa kuwatukana wazee bila kutueleza nini kifanyike.

Mfano, Kijana kama Nape na Janauary wanaposimama na kusema wanataka serikali 2 kwasababu tumeoleana na serikali ya 3 itakuwa ni kuleta usumbufu, inafikirsha.

January ambaye ameonywa na chama chake kuhusu harakati za kugombea uongozi wa nchi(Urais ) hawezi kuja na sababu hafifu kama hizo na baadaye tumkubali tu kwasababu ni kijana. Hatuelezi kwa hoja kwanini serikali 2 bali kumshambulia mwenye hoja za kwanini serikali 3.

Ndivyo Ngeleja alivyosimama na kusema serikali 2 zitaua muungano. Ngeleja hatuelezi zitaua muungano vipi na serikali 2 zinalindaje huo muungano.

Inaendelea.....
 
Inaendelea....

Mfinao zaidi, vijana kama akina masauni wanasema serikali 2 ndizo muafaka. Hawatuelezi ni muafaka kwa kutumia data zipi kutoka znz, na kwamba muafaka huo unakubalika vipi na wznz. Kinyume chake wanamshambulia Warioba na tume kwa kuja na takwimu ingawa wao hawana takwimu.

Kwa upande mwingine, huko vyama kama CUF kuna akina Mtatiro.
Hawa wanaamini katika serikali 3.Wasichotueleza ni kuwa viongozi wao wanaamini katika mkataba. Lini umewasikia wakiwahoji wazee kwa kuwa na pande mbili za shilingi?

Wamekaa kimya, wanataka siku moja watumie ujana kutuongoza hata kama tunajua hawawezi kuhoji kwanini mtu akubali serikali 3 ndani ya kikao cha chama na mkataba katika mikutano ya siasa.

Ndivyo ilivyo kwa CDM ambako vijana wake wamesimama na kusema wanataka serikali 3, wasichotueleza kwa undani ni ushahidi upi wa takwimu za kuonyesha hicho ndicho wananchi wanataka.Leo hawana ushahidi kuwa sample ya Warioba ilikuwa sahihi au la.

Tofauti ya Kingunge na hawa vijana ipo wapi?
Ni kwanini hawatumii wasomi, maktaba na resources zingine kuonyesha ukweli kuhusu sample inayotumika. Nao, mbele ya safari watataka watuongoze kibusa busa. Hatutaki kuwa na rais mwingine atakeysema 'Nimesikia takwimu si sahihi"

Vijana kama akina Halima Mdee ambao ni wanasheria, wameshindwaje kuja na kutufahamisha tofauti kati ya hati ya mkataba na mkataba wa muungano.

Kwanini hawawezi kusimama kwa pamoja CCM,CUF, Chadema n.k. na kusema Samweli Sitta kughushi sahihi ni kosa la kisheria, kimaadili na ni ujinga.

Inapofikia mahali nyaraka za uongoz zinatumika na akina Dr Ndugulile, Dr Kigwangalla, Machali, Zitto, Luheya, Owino, Lema n.k. wamekaa kimya taifa likidanganywa, kesho wanarudi kutuomba kura tena wakiwa wametanguliza ujana.

Huko katika vyama, wapo wanaopata nafasi kwasababu tu ya ujana wao.
Wote wamekaa kimya kwasababu vyama vyao vimewaambia shut up.

Baada ya Dodoma utawasikia wakija na tambo za kukabiliana na rushwa, wakilalamika umasikini, tena wakisema vijana tunaweza.
Mnaweza nini ikiwa mumesokomezwa pamba midomo na hamfurukuti.

Ninyi vijana badala ya kutanguliza utaifa mnaogopa vyama vyenu, kesho mnazunguka mkigawa kofia na boda boda. Hamna hoja yoyote ya maana kuhusu mustakabali wa taifa. Mnategea mtakapoulizwa msema eti 'chama kilisema'

Kujificha nyuma ya vyama ni unafiki mkubwa. Mlituomba kura kama wabunge vijana si vyama. Vyama ni utaratibu tu, wananchi kwanza.

Leo katika unafiki huu mnaoufanya wa kulamba miguu watu wachache wenye hila zao mnataka urais. Urais au Urahisi? Unawezaje kuwa rais na amir jeshi mkuu ikiwa huwezi kusimama na kuetetea unachokiona ni sahihi kwa mantiki na maono yako.

Vijana wapo katika mitandao wakitoa mistari miwili ili kujionyesha wanajua issue.
Ukweli ni kuwa ni woga kama mafisi. Ni chui waliojificha katika ngozi ya kondoo.
Wamebaki kulamba miguu. Ni hawa akina Mwigulu Nchemba ambao watoto wetu wanawatumia kufanya kozi za matusi na si hoja.

Kinachoendelea Dodoma kinatuonyesha jambo moja kubwa, vijana wa taifa hili hawajafikia mahali pa kutuopngoza. Ni kundi lililovaa kanzu nzuri za kufunika mwili na miguu, ndani ni chui, fisi na wasaliti wakubwa.

Kama hamuwezi kumpinga Warioba kwa hoja, shut up. Kama humuwezi kukataa hila za vyama vyenu, shut up. Kama mumeshindwa kutanguliza utaifa kwa kuhofia vyama vyenu, shut up. Tunawasoma, tunawasubiri mje na hoja ya ujana.

Tunaanda mayai viza, matakapokuja mje kama wachawi, mkitanguliza ujana tutawapopoa kama maembe, wanafiki nyie. Leo mnakataa maoni ya umma ili kulinda mikate yenu, kesho mnataka urais na ubunge! wanafiki wakubwa, wasaliti wakubwa wa umma.

Mtakaposimama wenyewe majukwanii na kupokea vipigo vya mayai viza mtatambua nguvu ya umma. Sha wa Iran hakuweza, ninyi hamuwezi.

Wana duru tusemezane.
 
Nguvu kuna usemi wa kiingereza unasema practice makes perfect, kama umewai kudhubutu kufanya maamuzi maagumu na unauwezo wa kufikiri basi unaweza kuendelea tuu kuwa na fikira peke. Tusiwalaumu hawa vijana nadhani huko sio kuwatendea haki, laumuni mfumo uliopo kwamba watu hawawezi kufikiria nje ya sanduku, watu hawana utashi wa kuchambua mambo.

Hili halijalishi, uwe CCM au Chadema. Kuna kina Mnyika Chadema wanafuata mambo kama magoigoi hawana utashi wa kuuliza kwa nini tunafanya hivi na hatufanyi vile. Mfumo wa kivyama ndio mhimili wa siasa zetu za Tanzania, kama Kamati Kuu ikiamua basi na wewe wamekuamulia tayari. Hili lipo CCM, CUF na Chadema. Waulize wanaofuta CUF agenda kwamba serikali ya tatu itatatuwa vipi matatizo ya mama yako mdogo pale Shelui hawana jawabu, sababu tuu Prof wao Lipumba kaamua kwamba hiyo ndio kauli mbili. Waulize CCM kwamba hizi mbili zinatatua vipi kero za Zanzibar, watakwambia Mkutano Mkuu umeamua. Waulize Chadema kwa nini mnasimamia swala la serikali tatu na sio Moja, jee mnajua gharama za uendeshaji, Jee mnajua mfumo wa kikatiba utako tumika, jawabu Mboe na Slaa wameamua. Hakuna independent thinking ndani ya Tanzania. Wewe Jiulize why hakuna chama chochote kinachopigania serikali moja, ndio utaona kwamba akili za kushikiwa ndio zimetawala. Au umemuona nani katika lile bunge akasimama na kusema serikali moja. Au hata aje na agenda ya serikali 1 lakini mabunge matatu? No one. Wanaotaka mbili hawajui why mbili, tatu wengi wanafuata mkumbo tuu na assumption kibao.

Tunaotaka serikali moja tunaoneka kama vile tumewasili jioni hii kutoka sayari ya Jupiter, jawabu la wanaotaka mbili au tatu ni kwamba moja HAIWEZEKANI. Ukiuliza kwa nini, unapewa sababu mfumo uliopo hauwezi kuzikubali. Hivyo tusilaumu vijana nasema tulaumuni mfumo.

Juzi chalinze wamempa kura Ridhiwani kwa 80%, ni kijana ambae anakila aina ya kashfa, rushwa, kuuwa UDA, madawa ya Kulevya, kuzorotesha ufanisi wa Bandari. Lakini vijana wa Chalinze wakishirikiana na vijana wengi kutoka kila kona walikuwepo pale chalinze na wamemsaidia kijana mwenzo kupata kura.

Vijana wengi, sina takwimu lakini wengi hatuna utashi wa kufikiri, wengi tunataka sababu tuu wengine wanataka. Iwe wewe ni January Makamba au Kafulila, wote ni walewale. Uwe umesoma USA au umemaliza Diploma VETA uwezo wa kufikiri unalindwa na Kamati kuu za chama. Vijana wao ni Pesa Mbele mengine nyuma, na kutaka kupata media buzz tuu. Hivyo kaka Nguvu kama tunataka vijana wawe na ari mpya na kasi mpya tubadilishe uwezo wa kufikiri. Nilitegemea kuona Young Caucus ikijikita zaidi kujadili nyanja za kuondoa Rushwa, Kuimarisha misingi ya uongozi bora, kutetea mali asili zetu, kutetea uraia wa kuzaliwa na mengine mengi. Lakini vijana walio kwenye katiba usiku wao wanapiga Tusker Baridi mchana wanakuja kujadili muundo wa serikali. That is very wastage, haijalishi wametoka Chadema au CCM au CUF, wakifungua midomo unaweza kusema mama yangu mzazi hawa ndio taifa la 2020? Hakuna kitu, yaani maboga tuu.

Mwisho, nilisema tangu awali CCM watatupa katiba yao wao, na hakuna kijana wala mzee atakae badilisha hilo, kwani kwa Tanzania ni haramu kufikiria nje ya chama. Kama ingekuwa Chadema ndio chama tawala wangetupa Katiba ya Kichadema sababu huo ndio mfumo wa Tanzania.

Marekani waliotengeneza katiba walkuwa wanaume wachache, sio watu 540+. Huu ni utitiri tuu wa watu ambao wengine hawana biashara yoyote ya kutengeneza katiba, wengine wamekwenda vacation tuu pale. Unamuweka mtu pale achambue mfumo wa serikali na afanye maamuzi wakati hafahamu hata bajeti ya nchi. Hajui nchi inakopa centi 42 katika kila shilingi wanayolipana pale kwa siku. Hawajui nini maana ya katiba. Matokeo yake hawa wanataka katiba pia iamuwe Yanga wajenge Jangwani au Bunju. Yaani tunakopa kuwaweka watu 500+ wajadili mfumo ambao 50% yao hawajui hata serikali inaendeshwaje. If you don't see problem hapa basi kazi bado ipo.
 
hahaha, mkuu Nguruvi3 duru namba 12 ama kwa hakikia nikiisoma ulivyo na hasira nao hawa vijana wangekuwa karibu ungewachapa bakora, ni kweli wanatia hasira sana kwa kuvaa hoja ya ujana kumbe ni undumilakuwili tu, kwakweli R.I.P Set Benjamini , wa wapi tena akina Set Benjamin wa Tanganyika?
 
Last edited by a moderator:
Wakati tunamalizia bandiko la mwisho, ningependa kumueleza bwana Nkumbi kuwa hakuna propaganda kwasababu sijasema vijana wa itikadi gani ya kisiasa. Nimesema vijana.
Pili, Nkumbi asome maneno ya Zumbemkuu, hayo si yangu ni ya vijana.

Muhimu sana, angesubiri kwanza tumalize ili aweze kuonyesha propaganda zipo wapi na aelewe msingi wa hoja.
Sijui kama anakumbuka kuwa vijana wamelilia umri upunguzwe ili wapate madaraka.

Sijui anakumbuka kuwa JK alipogombe uongozi kauli mbiu yake ilikuwa ni ‘wakati wa vijana’.
Na sijui kama hakuna ukweli kuwa baraza la mawaziri na wabunge kwa miaka 8 ilyopita wamekuwa ni vijana kuliko wakati mwingine.

Tunashukuru sana kwa maoni yake, tunaomba tuendelee kuwa pamoja. Maana nzima ya mijadala ni kubadilisha maono.

Ni kweli, unavyosema sikatai, ila nadhani tunaposhana sehemu ndogo sana. Propaganda unapoichukulia kuwa ni dhana ya kiitikadi, na kisha ukafikia tamati , utakuwa umekosea na utakuwa umekatisha mjadala Kabla haujafikia mwisho.

Political propaganda ( nikirudishe nyuma), zilikuwepo na zilitumika wakati wa Ancient Greece, na ndio chanzo cha kifo cha Socrate, na ndipo Plato akaja na ideal state ' republic' na kuikosoa sana Democrasia ya kipindi kile na mpaka sasa. ( na kazi ya kitabu chake ndio hasa imetumika na inatumika ktk kuimarisha siasa) Hapo ndio ujue kuwa propaganda ni jina la sasa ktk modern states, na Kabla ya hapo na Kabla ya Vyama vingi na Democrasia ya sasa ilikuwa inajulikana Kama ( political myth AMA selected lies)... Nadhani nimeeleweka nini namaanisha.

Zumbemkuu, nimepata kuelewa nini anaongelea, lakini hata Kama nisingeelewa, bado nashawishika kuamini kuwa na yeye Ana waslilisha Mtazamo wake tu Kama hapa tunavyofanya kwa sasa. Na ndio maana hata wanafalsafa wa kubwa wa siasa hata wewe bado una nafasi ya kukosoa mitazamo yao Kama haina ushawishi wa kutosha.

Narudi kwenye mada sasa. Sitaki kukushawishi uamini Mawazo yangu, ila nataka tusaidizane kufikia tamati. Nabadilisha uchangiaji natumia njia ya maswali pindi ukipata jibu ukitafakari huenda utapata kujua nini namaanisha.

Ktk siasa, huwa kuna vitu viwili ( kusema na kupata).zaidi ya hapo bado sijaona kingine.

Katika kusema, ndipo tunapata Maneno Kama " vijana ni Taifa la Kesho" nk. Katika kupata naiacha kwa sasa.

Swali la kwanza. Unaposikia kauli Kama hizo, Kabla ya kwenda kuanza kuitekeleza, jiulize, tupo ktk Taifa lenye mfumo gani, jibu ni mfumo wa Democrasia ya vyama vingi, na je misingi ya Democrasia tuliyonayo ni ipi? Umri una nafasi gani ktk Democrasia? (Jibu la hapa litakuongoza kujua nini maana ya propaganda). Naomba nikomee hapa kwanza. Kama bado kuna utata tutaendelea...

Karibu.
 
Sitogusa suala la Seeikali 2 AMA 3, kwa nyongeza ya wachangiaji hapo juu, tunapaswa kwanza tujue nini wajibu wa wananchi ktk nchi Yao na serikali Yao.( Tunaposema vijana nadhani ni kwa maana ya kwamba Tanzania ni Taifa lenye vijana wengi hivyo tukiwasakama watatii wajibu wao Ktk Taifa .) lakini mantiki hapa penye neno vijana palipaswa kuwa na neno Wananchi AMA Watanzania.
Kama Watanzania wangejua nini wajibu wao kwa Taifa nadhani mambo yangekuwa tofauti hivi sasa.

Nagusia kidogo kuhusu Katiba ya Marekani, na ninaungana na wachangiaji hapo juu wanaopinga wazo la kirundika watu zaidi ya 500 kufanya kazi ya watu hata chini ya 10.( inasikitisha sana).

Katiba ya Marekani kwa asilimia kubwa iliandikwa na mtu mmoja tu, raisi wa 3, Thomas Jefferson, na wengine wasiozidi 3 wakaongeza mchango, na wengine wasiozidi 5 wakasaidia kuikamilisha.

Hii ndio Katiba ya Muda mrefu zaidi duniani kwa sasa, ikifuatiwa na Katiba ya Norway.

Katiba ya Marekani hata Thomas Jefferson pia alipata Mawazo na muundo mzima toka ktk Maandiko ya mwanafalsafa muingereza John Locke ktk Maandiko yake ya Mikataba ya serikali ( kwa tafrisi isiyo rasmi) ambapo pia Johne Locke kuandika kwake kulitokana na Biblia( agano la kale).Jeffrrson alikopi misingi mikuu ya uanzishwaji wa serikali ni kulinda Life, liberty and Property, ambapo yeye neno Property alibadilisha na kuwa Persue of happiness, ambayo ndiyo misingi ya democrasia tuliyonayo sasa,na kuanzia hapo, Katiba Nyingine zote zikafuata kwa kuiga na kuongeza Yao, na hata hiyo ya pili kwa umri ( Norway), haikuandikwa kwa utaratibu Kama wetu, wao pia walichukua Katiba ya Marekani na Ufaransa Enzi zile ( french revolution) na kisha wakatengeneza Yao mpaka sasa hawana shida kabisa.

Hivyo, haihitaji watu 500 kupata Katiba nzuri, inahitaji watu wachache wenye maono na watu wa kuiga mifano ya Katiba imara na kisha kubadilisha machache kulingana na historia na utamaduni wa Taifa letu basi.

Mwanafalsafa mmoja maarufu sana- Aristotle, katika kazi Yake ya siasa, aliifanya kwa kukusanya Katiba tofauti tofauti zaidi ya 150, na kuanzia hapoakaandika vitu muhimu sana ktk siasa ya sasa. Tunashindwaje jamani? Hii Katiba watakayopata lazima itarudiwa tena I promise you wadau.

Respect kwa Mawazo ya , Mchambuzi, zumbemkuu, nguvu 3, na mtanganyika.
 
hahaha, mkuu Nguruvi3 duru namba 12 ama kwa hakikia nikiisoma ulivyo na hasira nao hawa vijana wangekuwa karibu ungewachapa bakora, ni kweli wanatia hasira sana kwa kuvaa hoja ya ujana kumbe ni undumilakuwili tu, kwakweli R.I.P Set Benjamini , wa wapi tena akina Set Benjamin wa Tanganyika?
Kwakweli inatia hasira.

Leo tunasikia January 2015, ana maono, ana fikra mpya, ni mkweli,kijana, anafahamu matatizo ya nchi n.k.

Nafasi ya kutuonyesha imepatikana, wote wamejificha nyuma ya kivuli cha chama.
Kiongozi anaongoza, hajifichi nyuma anatangulia mbele.

Sina tatizo na msimamo au maoni yao, nina tatizo na ukweli kuwa hawasemi chochote kama kiongozi.

January ni kijana kama walivyojaa ndani ya bunge la katiba.
Wamekaa kimya wakishangilia wazee kama Salim, Warioba, Butiku n.k. wakitukwanwa.

Hawana hoja za kuwapinga hawa wazee, hoja zao ni majibu ya shule za awali.
Hivi mtu anaposema serikali 2 zitavunja muungano, hilo ni jibu kweli.

Wengine kila siku katika face book kama si face look, wanapiga vijembe kwa mistari miwili, hatujui wanasimamia wapi.

Wameficha rekodi zao wakisubiri kuwa opportunists, kesho wanakuja na hoja, ni vijana, wana maono na fikra mpya.

Swali nani ana maono na fikra mpya, Warioba, Salim na wenzao au hili kundi la vijana lililobaki likipiga meza kushangilia wazee hawa wanapotukanwa.

Ujana ni nguvu, aje mtu hapa jamvini anionyeshe tofauti ya vijana waliopo na akina mzee Songambele, Marehemu Gama, Nyng'anyi n.k. iko wapi.

Akina mzee Songambele walithubutu hata kama hawakuwa sahihi, hawa vijana wanaobaki kupiga makofi na kujivunia laptop na iphone wana nini pale Dodoma leo siku ya 30.

Vijana tunao ongelea ni hawa akina Mwigulu ambao wakipewa nafasi ya kuongea wanaleta hoja za chekechea.

Leo kijana anasema serikali 3 zitaleta ushoga, hawezi kusimamia hiyo hoja achilia mbali kukosa ukweli.Huyu naye anasema ni kijana tena mchumi nambari moja. Ndivyo wanavyolaghai umma.

Ifike mahali tuwawajibishe. Angalia genge la vijana kama wa CCM ndani ya bunge.
Wameitwa na kuambiwa shut up na kweli wakasimama na kusema kisicho moyoni mwao.

Pembeni na vijiweni tukiwauliza ni kwanini na kwa vipi, wanasema hata wao wapo pamoja na sisi lakini chama kimeamua.

Ni wabunge hao tunaongea nao. Wapi maono? wapi fikra kama si unafiki mkubwa.
Hawa ndio tatizo la taifa si wazee.

Kama huwezi kujibu hoja ya mzee wewe ndiye tatizo si hoja ya mzee.

 
Mimi ninatatizwa na jambo moja na namuomba yeyote yule anayejua anipe timeline; uzee unaanzia wapi na ujana unamalizikia wapi? Je kama Muungano wetu huu wa serikali mbili ungechukua umbo la kibinadamu, kwa umri huu wa miaka 50, ungekuwa bado Muungano kijana au mzee? Kwa nini nauliza hivi? Ni kwa sababu hawa tunaowaita vijana, wengi wao hawajafikisha miaka hiyo kiumri na hawakuwahi kuishi nje ya huu Muungano. Hii ina maana gani? Ina maana kwamba vijana hawa wamezaliwa baada ya 1964 au kwa maneno mengine wamezaliwa ndani ya Muungano wa serikali mbili na kwa msingi huo hawajawahi kuonja maisha nje ya huu Muungano feki!

Hawa vijana wakati wanazaliwa kero za Muungano wa serikali mbili walizikuta, wakati wanakua kero zilikuwapo, wakati wanasoma matatizo yalikuwapo na sasa wakati wanakaribia kutoka ujanani matatizo yameendelea kuwapo. Mwanzoni, pamoja na kuwa na serikali mbili ndani ya nchi moja, matatizo yalikuwapo lakini siku zilivyosogea matatizo yalizidi kuongezeka na hadi sasa tunazo serikali mbili ndani ya nchi mbili. Hali hii inaashiria nini? Inashiria kwamba ufa wa utengano kama taifa moja unazidi kupanuka. Zamani ulihitaji tu kupiga hatua moja kuvuka kamtaro kutoka bara hadi visiwani, siku hizi unahitaji kuota mbawa uweze kuruka bahari kufika ng'ambo ya pili.

Hawa vijana wakati wanazaliwa, waliwakuta wazee wao wakitoa ahadi za kuzimaliza kero za Muungano na sasa wakiwa wanakaribia kuupa kisogo ujana, na wao sasa wanatoa ahadi hizo hizo. Wengine wao wameshavuka hata umri wa wazazi wao wakati Muungano wa serikali mbili unazaliwa...Mwalimu Nyerere alikuwa na miaka 42! Halafu, bila hata aibu, eti wanadai serikali tatu itavunja muungano! Hii dhana potofu wanaitoa wapi? Cha ajabu ni kwamba hapa wako pamoja na wale wale wazee wao walioshindwa kwa miaka 50 kutatua kero za Muungano na wameamua kuwaunga mkono! Hapa tusidanganyane hawa vijana kawalitakii mema taifa hili!

Nakumbuka mwanzoni mwa 1990, wakati upepo wa magaeuzi ulipotua Tanzania, wimbo na msimamo wa chama tawala ullikuwa huo huo; mfumo wa vyama vingi utaleta vita na kulisambaratisha taifa! Vipindi vya redio na TV vilikuwa na ajenda moja tu, kuwaogopesha wananchi kuwa vyama vingi vitatuingiza kwenye hatari ya vita! Picha na habari zilizooneshwa zilikuwa za nchi zilizo vitani! Bila Mwalimu kuwakemea CCM, sijui hali ingekuwaje. Leo miaka ishirini baadaye...mchezo uleule, mbinu zile zile, njama zile zile, ujinga ule ule... my God! Hata aibu hawana hawa jamaa. Muungano kama ulivyo umegota kwenye lindi la tope...njia ya kujikwamua ni kugeuza njia, nothing less!

Swali kwa vijana, je hapa tulipofikia, mfumo wa serikali mbili utaudumishaje Muungano? Kwa kumdhalilisha Mh. Jaji Warioba? Kwa kupuuzia maoni ya wananchi kupitia Tume? Mbona huko ni kujidanganya! Kwa risasi na mabomu? Nasikia kuna mpango wa kanuni kubadilishwa kwa kuondoa kipengele cha maamuzi kupitia theluthi mbili na kuwa tu wengi wape hata kama ni asilimia 50.1%! Juzi tu tumevua nguo kwa kuweka rekodi mpya ya kutumia kura ya aina mbili, ya wazi na siri, na sasa tunataka kuweka rekodi nyingine duniani kwa kupitisha katiba ya nchi kwa kura chini ya theluthi mbili! Huo ndio msimamo CCM kama chama unaoungwa mkono na eti Vijana wake!

Vijana wa CCM, je mnataka na nyie siku zenu zikifika muwaachie watoto wenu hizo kero za Muungano kama mlivyoachiwa na babu zao?
 
Nguvu hapa nadhani umegusa pazuri, ukweli ni kwamba afadhali wazee kuliko hao vijana tunawasema. Na huu ni ushahidi wa statement niliyotanguliza.
Vijana wengi ambao wamepewa nafasi katika ungozi iwe wa kiserikali au kibiashara ama shughuli zisizo na kiserikali wamekuwa mstari wa mbele kujilimbikizia mali na kutafuta kuongeza madaraka pasipo kuwa na vigezo. Haijalishi vijana hawa wawe Chadema au CCM au independent wote wamekuwa na tamaa za kutajirika haraka haraka.

Vijana ambao hawajapata nafasi za uongozi nao wameweka dhamira kwamba kama watapata basi nao watakula, kwani mfumo ndio upo hivyo. Miaka hii kumi tumeona wimbi la vijana wengi wakipata nafasi mbalimbali kwenye sehemu mbalimbali iwe serikali au katika biashara, kilichoendelea ni skendal na ulafi. Tumeona Mh. Zitto alichofanya katika miaka hii 10, tumewaona kina Mwamvita Makamba.

Mfumo ambao umejitokeza kati ya mwaka 1995-mpaka leo ndio sababisho la matatizo, utaifa umepotea miyoni mwa Watanzania, watu wamekuwa wavivu kifikiri na kuamua. Kila mtu anataka kumiliki mali bila kutengeneza mchakato, vijana wajasilimali wamepungua na kila kijana anataka kuvaa tai na kukaa kwenye AC. Mfumo wa 1960s ulikuwa na muamko zaidi kuhusu utaifa kushinda leo.

Hakuna wa kumlaumu, ni sisi wenyewe. Wote tupo kwenye boti moja na tunapiga kasia pamoja. Wote tunataka rushwa iwe tupo kwenye office ya mkoa au kwenye bunge, sote tunajali posho iwe walimu wa sekondari au wabunge wakatiba. Na sote ni wavivu wa kufikiri iwe wanachuo UDSM au Mawaziri kina Nyalandu. Sisis ni zao la sisi sisi.

Hakuna sababu hata moja Tanzania kuwa masikini, nchi yenye watu 44 Million na Natural resources zaidi ya 100 Billion ziko kwenye kila kona. Tanzania ni masikini sababu Watanzania wameamua kuwa masikini.

Tuliwapa dhamana hawajui wanachofanya, na wale wenye uweleo hata mdogo hawatakiwi kusikilizwa. Leo hii tumegundua gas, jee umeona mikataba tunayosaini? Vijana hao hao wanaisoma hii mikataba wakiwa na hang over za ajabu, vijana wamekalia Kuangalia Premium League na Champions League usiku kucha, elimu standard sasa imeshuka, halafu mnataka kwenye hii mikataba tukae na watoto waliomaliza Law Georgetown University? Wakati sisi tunawaza 10% wenzetu Kenya wanawaza kuondoa kabisa Umasikini.

Tanzania ni blah blah nyingi. Lazima apatikane raisi ambae atabadilisha mfumo wa kufikiri, tatizo lilopo ni physiological zaidi. Kama tutaendelee na adisiadisi hizi hizi wakati population inakuwa kwa zaidi ya 3% kila mwaka, tutajikuta tunaongeza masikini na speed yetu ya uzalishaji ipo pale pale. Wenye akili wanaenda kuleta toothpick China. I'm sick, cha ajabu no one sees the problem, i mean NO ONE.

Vijana wengi are just lazy, lazy kufikiri, lazy kutenda and worse zaidi lazy kuamua. Vijana ndio wataliangusha hili taifa, mark my word.
Umenikumbusha waziri mmoja kijana aliyepewa unaibu waziri. Miaka 2 tu akawa anamiliki milioni 700 sawa na dola takribani nlakini 5.
Dola lakini 5 ni pesa ambazo waziri wa uingereza, Ufaransa hanayo.

Kumililki milioni 700 kwa mtu mwenye shughuli zake si jambo baya, tunajua huyu waziri kijana katoka shule wala hajawahi kufanya ujasirimali, kazipata wapi haraka hivyo.

Jibu ni kuwa katumia ofisi ya umma kuuza kazi za umma, iwe tender au mikataba kufikia malengo yake.Hawa ndio tunaaminishwa wanaweza, ni makini na wana maono

Kuhusu umasikini, sijui hata kama wanaweza kueleza umasikini ni kitu gani. Sijui kwasababu hakuna anayejaribu hata kugusia jambo hilo. Kila siku katika facebook utawasikia na hoja rojorojo tena kwa mistari miwili. Una

Kuhusu mfumo wa elimu, nakubaliana nawe pia kwasababu hawa akina Warioba waliosimama na kumpa Nyerere ultimatum ndio waliopanda ngazi na kuwa mawaziri wakuu. Ultimatum halikuwa jambo baya kwasababu ilikuwa ni mwanzo wa fikra na ushujaa wa kueleza maoni na maono yao. Hata kama walikosea, tunaona uwezo wao wa kujenga hoja

Wazee kama Warioba ndio waliosimamia serikali 2 lakini kwa kutumia elimu, muda na mazingira wametafakari na kuona upo umuhimu wa kusikiliza wananchi, kupima hoja zao kulingana na mazingira na nyakati.

Vijana tunaoambiwa wanamjibu Warioba kwa matusi.
Hata wanaotukanwa, vijana wetu wameshindwa kusimama na kusema , mh rais tunataka hoja dhidi ya Warioba, tupo kutafuta hatima ya taifa.

Kinyume chake vijana wa kike wakapiga vigelele wakiume wakitwanga meza kwa furaha ya matusi.

Tunawasikia akina Mwigulu wakiwashambulia akina Warioba kwa wajihi na sifa zao kama wanadamu, hawashambulii hoja.

Mwigulu Nchemba anaposimama na kusema serikali 3 zitaleta ushoga, ni uvivu wa kufikiri, udanganyifu na ulaghai usio na chembe ya aibu. Hakueleza mfumo wa serikali 3 unaleta vipi ushoga, Alichokifanya ni kuwatisha wananchi , eti hayo tunaambiwa ni maono.

Kwakweli katika vijana wetu waliopo uongozini kitu kinachoitwa critical thinking, visio na bold decision hakuna.
 
Back
Top Bottom