Duru za siasa: Vijana, katiba mpya na kiu ya uongozi

Duru za siasa: Vijana, katiba mpya na kiu ya uongozi

Mimi ninatatizwa na jambo moja na namuomba yeyote yule anayejua anipe timeline; uzee unaanzia wapi na ujana unamalizikia wapi? Je kama Muungano wetu huu wa serikali mbili ungechukua umbo la kibinadamu, kwa umri huu wa miaka 50, ungekuwa bado Muungano kijana au mzee? Kwa nini nauliza hivi? Ni kwa sababu hawa tunaowaita vijana, wengi wao hawajafikisha miaka hiyo kiumri na hawakuwahi kuishi nje ya huu Muungano. Hii ina maana gani? Ina maana kwamba vijana hawa wamezaliwa baada ya 1964 au kwa maneno mengine wamezaliwa ndani ya Muungano wa serikali mbili na kwa msingi huo hawajawahi kuonja maisha nje ya huu Muungano feki!

Hawa vijana wakati wanazaliwa kero za Muungano wa serikali mbili walizikuta, wakati wanakua kero zilikuwapo, wakati wanasoma matatizo yalikuwapo na sasa wakati wanakaribia kutoka ujanani matatizo yameendelea kuwapo. Mwanzoni, pamoja na kuwa na serikali mbili ndani ya nchi moja, matatizo yalikuwapo lakini siku zilivyosogea matatizo yalizidi kuongezeka na hadi sasa tunazo serikali mbili ndani ya nchi mbili. Hali hii inaashiria nini? Inashiria kwamba ufa wa utengano kama taifa moja unazidi kupanuka. Zamani ulihitaji tu kupiga hatua moja kuvuka kamtaro kutoka bara hadi visiwani, siku hizi unahitaji kuota mbawa uweze kuruka bahari kufika ng'ambo ya pili.

Hawa vijana wakati wanazaliwa, waliwakuta wazee wao wakitoa ahadi za kuzimaliza kero za Muungano na sasa wakiwa wanakaribia kuupa kisogo ujana, na wao sasa wanatoa ahadi hizo hizo. Wengine wao wameshavuka hata umri wa wazazi wao wakati Muungano wa serikali mbili unazaliwa...Mwalimu Nyerere alikuwa na miaka 42! Halafu, bila hata aibu, eti wanadai serikali tatu itavunja muungano! Hii dhana potofu wanaitoa wapi? Cha ajabu ni kwamba hapa wako pamoja na wale wale wazee wao walioshindwa kwa miaka 50 kutatua kero za Muungano na wameamua kuwaunga mkono! Hapa tusidanganyane hawa vijana kawalitakii mema taifa hili!

Nakumbuka mwanzoni mwa 1990, wakati upepo wa magaeuzi ulipotua Tanzania, wimbo na msimamo wa chama tawala ullikuwa huo huo; mfumo wa vyama vingi utaleta vita na kulisambaratisha taifa! Vipindi vya redio na TV vilikuwa na ajenda moja tu, kuwaogopesha wananchi kuwa vyama vingi vitatuingiza kwenye hatari ya vita! Picha na habari zilizooneshwa zilikuwa za nchi zilizo vitani! Bila Mwalimu kuwakemea CCM, sijui hali ingekuwaje. Leo miaka ishirini baadaye...mchezo uleule, mbinu zile zile, njama zile zile, ujinga ule ule... my God! Hata aibu hawana hawa jamaa. Muungano kama ulivyo umegota kwenye lindi la tope...njia ya kujikwamua ni kugeuza njia, nothing less!

Swali kwa vijana, je hapa tulipofikia, mfumo wa serikali mbili utaudumishaje Muungano? Kwa kumdhalilisha Mh. Jaji Warioba? Kwa kupuuzia maoni ya wananchi kupitia Tume? Mbona huko ni kujidanganya! Kwa risasi na mabomu? Nasikia kuna mpango wa kanuni kubadilishwa kwa kuondoa kipengele cha maamuzi kupitia theluthi mbili na kuwa tu wengi wape hata kama ni asilimia 50.1%! Juzi tu tumevua nguo kwa kuweka rekodi mpya ya kutumia kura ya aina mbili, ya wazi na siri, na sasa tunataka kuweka rekodi nyingine duniani kwa kupitisha katiba ya nchi kwa kura chini ya theluthi mbili! Huo ndio msimamo CCM kama chama unaoungwa mkono na eti Vijana wake!

Vijana wa CCM, je mnataka na nyie siku zenu zikifika muwaachie watoto wenu hizo kero za Muungano kama mlivyoachiwa na babu zao?
Mkubwa, hawa vijana wanatumia neno hilo kwasababu kuu mbili
1. Kuwavutia vijana wenzao wasio na bahati ya kuona kule wanakokuona
2. Hawana fikra za namna nyingine za kujenga hoja bila kutumia ujana.

Vijana hao ambao umri wao hatuufahamu ni kuanzia wapi na kuishia wapi, ndio wanakalishwa kitako na akina Pinda wakiambiwa Tanganyika ipi inayotakiwa, ya mkoloni, wakati wa kupigania uhuru au baada ya uhuru. Eti wanaambiwa kulikuwa na evolution ya Tanganyika.

Na kwa kujua kuwa hawana uwezo wa kujenga hoja, Pinda kawaita na kuwaambia wafunge vinywa vyao. Nao kwavile ni watu wasiojua wanataka nini , wote across the board wakafungia degree zao za ubachela, master and baster, PhD na kumsikiliza yule mtu ambaye hajui Tanganyika ipi ingawa cheti chake cha kuzaliwa ni cha Tanganyika

Kama ulivyosema, hao vijana wapo sambamba na wazee waliosemwa wamechoka tena wazee hao wakiwapeleka mputa.Wamefungwa bendeji za kusema na pale wanaporuhusiwa wameshauriwa wazungumzie matusi kama akina Nchemba.

Vijana hao wametuingiza katika aibu ya dunia. Leo John Mnyika anakubali kuwe na kura ya wazi na siri.
Anaambiwa kura hiyo ilitumika mwaka 1962 wakati huo nchi ikiitwa Tanganyika. Halafu wazee hao inaosemekana wamechoka wanarudi upande wa pili na kuwaambia Tanganyika haikuwepo wakati wanazaliwa.Kama haikuwepo na kura ya wazi haikuwepo inakuwaje ukubali kitu kimoja kingine ikikane?

Vijana hao wameshindwa kujua tofauti ya mkataba na hati ya mkataba. Wameletewa karatasi za kughushi na Mzee Samwel Sitta, wakajua ni za kughushi na bado wakamuacha tu aendelee kuwadanganya.

Eti wanatumia kisingizo cha taifa na nchi kwanza. Hiyo ndiyo hoja ja James Mbatia siku zote.
Ni james huyo ndiye aliyeongoza kampeni ya OMO alipokuwa UDSM.
Leo amesahau utaifa ule kwasababu kamegewa keki ya kuteuliwa.
Ni utaifa gani unaotekelezwa na upande mmoja?

Msekwa kasema saini si yake. Vijana hawashtuki kuwa hilo ni kosa la kisheria na kimaadili. Wamekaa kimya mambo yakiharibika. Wamekumbatia UCCM na Uchadema, UCUF na uTLP bila kujua vyama ni majina nchi ipo hata bila ya vyama.

Vijana wanaaminishwa kwa dhati kuwa mfumo wa serikali mbili ulioshindwa miaka 50 sasa umeapatiwa dawa kutoka Milpark hospital.
Kwamba, kufumba na kufumbua tatizo la muungano litakuwa limekwaisha.

Wameshindwa kutambua kuwa serikali inayotaka kumaliza kero kwa serikali 2 iliyoshindwa miaka 50 ndio hiyo iliytoshindwa kutatua tatizo la umeme kwa miaka 8.

Woga umewajaa, wamepoteza intellect, fikra zao zimejikita kumsubiri Kikwete aje kumsumanga Warioba huku wakilipuka kwa nderemo na vifijo.

Kesho,wanarudi mitaani wakiwa na logo yao ya ujana. Ahadi za kuleta maendeleo, kununua boda boda na udhaifu mwingine kama huo. Tunaambiwa ni wakati wao.

Hapo Dodoma wapo wakibadilishana CD za bongoflavor na Bongo Movie. Hwajui wapi wapate taarifa na tafiti. Tunawasikia wazee akina Lipumba wakilipuka kwa takwimu.
Vijana wetu wanaambiwa hakuna sample ya watu elfu 20, wanalipuka kwa makofi.

Hii dhana ya ujana sasa imefika mwisho. Tunasema, wakija kutomba kura waje kama wachawi au wanga. Wakija na neno ujana tutahamasisha wavurushwe kwa mayai viza.
Vijana wana maono, nia na dhamira. Vijana wanaongoza siyo hawa chui na fisi tunaowaona Dodoma.
 
Misingi ya Uongozi iliyojengwa na Vijana wa awali (chini ya Utawala wa Mwalimu Nyerere), misingi hii, mmoja baada ya mwingine, imekuwa inazidi kubobolewa, huku vijana wanaojadiliwa wakiwa ni kiungo muhimu “kimikakati”, ya Ubomoaji huo. Ni kutokana na hali hii, leo hii kama taifa, Serikali ya Muungano/Tanzania Bara” (ambayo ni Tanganyika), inakimbilia kujiunga na ligi kuu ya “FAILED STATES”. Kwa mujibu wa Wikipeda, maana ya dhana ya “failed state” ni pamoja na hii ifuatayo:

A failed state is a state perceived as having failed at some of the basic conditions and responsibilities of a sovereign government.

Hatupo mbali kukidhi sifa na vigezo vyote vya “a failed state”. Na hii ni kwa sababu, Muungano uliopo leo, ni ule ambao haukuachwa na Vijana wa Awali (ikiwa ni pamoja na Mwalimu Nyerere). Mwalimu hakuacha Muungano wa NCHI MBILI, SERIKALI MBILI. Hali hii imejitokeza under CCM’s watch (uvunjwaji wa wazi wa katiba ya JMT). Chini ya mfumo wa sasa, uamuzi wa CCM wa kuendelea kupuuzia mgogoro uliojitokeza, hasa kuendelea kuinyima Tanganyika haki zake ambazo ziliheshimiwa na Mkataba wa Muungano (1964), zikalindwa na katiba ya muda ya Muungano (1965), na kuja kubomolewa na katiba ya Kudumu ya JMT (1977), taifa letu kugeuka kuwa “a failed state”, ni suala la muda tu.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, idadi ya watanzania wenye umri kuanzia Mwaka Mmoja hadi miaka 35 (Ujana unapotajwa kuwa kikomo), kundi hili linakaribia kuwa ni 70% ya jumla ya watanzania wote. Hata tukiamua kuziweka pembeni takwimu za idadi ya watu Zanzibar, bado takwimu ya 70% itaendelea kusomeka hivyo kwa Tanganyika (Tanzania Bara). Hii ni kwa sababu, zaidi ya nusu ya mikoa ya Tanzania Bara ina jumla ya wananchi wengi kuliko jumla ya wananchi wa Zanzibar. Kwa maana hii, idadi ya wananchi katika hili (kwa Tanganyika/Tanzania Bara), ni zaidi ya MILIONI 30 kati ya jumla ya watanzania wote (Tanzania bara na Zanzibar) wanaokadiriwa kufika MILIONI 45.

Kufikia mwaka 2015, wengi ya wananchi wa rika hili:
· Watakuwa wameishi katika mazingira ya mfumo wa vyama vingi;
· Watakuwa wameguswa zaidi kisiasa, kiuchumi na kijamii na migogoro na kero za muungano kuliko kuona matunda ya muungano kisiasa, kiuchumi na kijamii.
· Watakuwa wanaishi mijini (population trends points towards urban in the future).
· Watakuwa ni wananchi wenye uelewa na ufahamu (exposure and knowledge) kuhusu dhana ya “Uongozi wa Umma”, na jinsi gani dhana hii inatofautiana na ile ya “uongozi katika kampuni binafsi”.
· Na muhimu zaidi, wengi wanaijua tarehe ya Uhuru wa Tanganyika na umuhimu wake katika maisha ya kila siku (kisiasa, kiuchumi na kijamii), kuliko tarehe ya Muungano.

Hili la tarehe ya “uhuru wa Tanganyika” na tarehe ya “Muungano wa Tanganyika na Zanzibar”, ni suala ambalo hivi sasa nipo katika kulifanyia utafiti zaidi, na nikikamilisha utafiti huu, nitauwasilisha . Mbali ya utafiti wangu, naweza kutoa ushahidi mwingine juu ya hoja hii. Tofauti na wengi wanavyofikiri (hasa makada wa CCM wenye msimamo na serikali mbili), watoto wengi wa Tanzania ya leo wana ufahamu mkubwa kuhusu TANGANYIKA. Kwa mfano, kila wiki, kuna kipindi kimoja kinachorushwa na kituo cha televisheni cha EATV kinachoitwa “SKONGA” Dhumuni la kipindi hiki ni kutembelea watoto waliopo kwenye shule mbalimbali za sekondari na kubadilishana nao mawazo juu ya masuala mbalimbali ya kisiasa na kijamii kwa ujumla. Hivi karibuni, nilibahatika kutazama kipindi hiki, na mazungumzo kati ya mwanafunzi wa kidato cha kwanza na mtangazaji wa EATV yalikuwa kama ifuatavyo:

Mtangazaji: Tanganyika ilipata uhuru mwaka gani?

Mwanafunzi: Mwaka 1961.

Mtangazaji: Je Tanzania ilipata uhuru mwaka gani?

Mwanafunzi: Hakuna uhuru wa Tanzania, Tanzania haijawahi kupata uhuru.

Mtangazaji: Je kuna nchi inayoitwa Tanganyika?

Mwanafunzi: Ndio, ipo.

Mtangazaji:Tanzania ni nchi gani?

Mwanafunzi: Tanzania ni Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Mtangazaji: Nani ni Rais wa Tanzania?

Mwanafunzi: Kikwete.

Mtangazaji: Nani ni Rais wa Tanganyika?

Mwanafunzi: Ali Hassan Mwinyi.

Hapa tunajifunza nini?
1. Licha ya Katiba ya JMT (1977) pamoja na sera za CCM kuwekeza sana katika kuuelezea Muungano kwamba umetokana na “Tanzania Bara na Zanzibar”, bado watoto na wadogo zetu wengi mitaani wanatambua kwamba Muungano uliopo ni wa “Tanganyika na Zanzibar”.
2. Jina la Tanganyika” sio jina geni hata kwa watoto wenye umri chini ya miaka 15, licha ya hoja za kina Pinda na wengine kwamba wananchi wengi wamezaliwa ndani ya Tanzania, na sio Tanganyika.
3. Mafanikio ya Kuizindua Tanganyika yatachangiwa sana na watoto na wadogo zetu hawa ambao ndio wengi nchini.
4. Vijana wanaojadiliwa humu (viongozi) kama wasaliti wa vijana wenzao watapata wakati mgumu sana wa kushawishi watoto na wadogo zetu kwanini na wao wapewe nafasi na waaminiwe katika kuijenga Tanganyika tutakayoizindua muda sio mrefu.

Wengi ya wananchi wa rika hili (chini ya umri wa miaka 35), wamekuwa wakijifunza (mashuleni, majumbani na mitaani) jinsi gani vijana waliowatangulia ambao sasa na baba, babu, mama, na bibi zao, walivyutumia muda mkubwa wa UJANA wao kuwa “VANGUARDS” wa taifa lao. Na wanazidi kujifunza kwamba – tofauti na vijana wa enzi za Mwalimu, wanashuhudia jinsi gani Vijana wa leo waliopo kwenye uongozi wanavyoshirikiana na watawala kuwa “VANDALS” wa taifa lao (la vijana), na muhimu zaidi, jinsi gani viongozi waliopata nyadhifa zao za sasa kwa kete ya “ujana”, wakishiriki kikamilifu katika hii Vandalism of the state.

Kama alivyojadili nguruvi3, umahiri na uzalendo wa “viongozi vijana” ulitakiwa uonekana katika mchakato wa katiba. Lakini badala yake, vijana hawa (viongozi) waliopo katika vyama vya siasa, lakini hasa ndani ya CCM (Kamati Kuu na NEC), wameshaamua waziwazi kuwasaliti vijana wa rika tulilojadili hapo juu, na badala yake, wameamua kuunga mkono “even further vandalism of the state” kupitia mfumo wa Muungano wa Serikali Mbili, Nchi mbili. Such Vandalism imejadiliwa vyema sana na Professor Lipumba hivi karibuni bungeni, na muda ukiruhusu, tutaweka maelezo ya Lipumba humu.

Nguruvi3 amejadili vyema sana kwamba, awali kulikuwa na vilio vingi sana kwamba uongozi wa nchi na mfumo wa utawala (vyama vya siasa na serikali) umekuwa hauwashirikishi vijana katika uongozi na ngazi za maamuzi kitaifa. Hii ikawa moja ya hoja za msingi zilizojengwa juu ya kwanini “taifa letu” limeshindwa kupiga hatua ya kimaendeleo, hasa wajenga hoja wakiwashambulia wazee waliopo kwenye uongozi na nafasi za maamuzi kitaifa kwamba mawazo yao yamechoka, yamepitwa na wakati, na hayawezi tena kubuni mikakati mipya ya maendeleo. Hoja hii pia inajadiliwa na watafiti mbalimbali wa masuala ya siasa na demokrasia, kwa mfano, Aminata Faye Kassé (2003) anasema kwamba:

A true democracy is characterized by the full and equal participation of women and men in the formulation and implementation of decisions in all spheres of public life”. Moreover, “No country can call itself democratic if half of the population is excluded from the decision-making process.

Women and youth are widely underrepresented in many African opposition political parties. This is true not only to the opposition parties, but also to the incumbent parties.

Baada ya vilio vya muda mrefu, vijana wakaanza kushirikishwa katika uongozi na ngazi za maamuzi kwa kasi kubwa katika vyama vya siasa, na uongozi wa nchi kwa ujumla. Lakini badala ya mabadiliko haya kuanza kuwa na tija na kuleta manufaa kwa wananchi walio wengi (ambao ni vijana wenzao), matokeo yake ni kwamba - kasi ya taifa letu kuelekea kuwa “a failed state”, imezidi kushika kasi baada ya ujio wa Vijana hawa kwenye uongozi wa nchi. Vijana wa awali (kina Mwalimu Nyerere) walitumia ujana wao katika ujenzi wa Tanganyika as a “a nation-state”, lakini vijana wa leo waliopo madarakani wanatumia muda wao mwingi kuipeleka Tanzania/TanzaniaBara/Tanganyika towards “a failed state.”

Mbaya zaidi, badala ya vijana hawa kutumua ujana wao kupigania na kutetea dhana ya DEMOCRACY, Vijana hawa wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika ujenzi wa:
· CORRUPTOCRACY
· CHAOSOCRACY &
· TERROROCRACY

Vijana wengine wamekuwa wakienda mbali na kushiriki kikamilifu katika “Criminalization of the State”. Wanafanya hivyo kwa sababu, kwa uelewa wao, uongozi ni pamoja na:

· Dispensing patrimony.
· Recycling of elites.
· Utilization of state power and resources to consolidate political and economic power.

Nadhani pia kuna haja ya kujadili:

· Dhana ya “Uongozi” na kuitofautisha na uongozi wa kisiasa.
· Dhana ya “Ujana” na nafasi yake katika the Renascence of Tanganyika.
· Kwanini waliojadiliwa wanaonekana kuwa na nguvu na ushawishi ndani ya jamii.
· Hatima ya Taifa (Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii) iwapo tutaendelea kuwategemea Vijana wa aina ya hawa waliojadiliwa.
 
Mchambuzi katika bandiko lako hapo juu kuna hoja moja ambayo vijana wengi hawaielewi.
Kuna kiongozi halafu kiongozi wa kisiasa.

Upo uwezekano wa kiongozi wa siasa kuwa kiongozi.
Mfano, Nyerere alikuwa politician na wakati huo huo akiwa statesman.

Nakumbuka katika tribute za msiba wake, CCN walisema Nayerere ... one of the Africa statesman.
Hapa walimpa sifa ya uongozi.
Ndivyo alivykuwa Mandela, William Tobert na wengine wengi tu.

Si lazima kila mwanasiasa awe statesman. Ni kitu kigumu kupata hadhi ya kuwa statesman.
Kwa muktadha wa mjadala tumeonyesha dhana hizo mbili ili kujenga hoja ifuatayo.

Vijana walioko Dodoma wamesahau kuwa wao ni viongozi kwanza kabla ya kuwa viongozi wanasiasa. Wanapokuwa katika kampeni wao ni viongozi wanasiasa kwasababu mfumo umejengwa hivyo kuelekea katika uongozi.

Wakiwa bungeni wanajisahau kuwa wale wananchi wa majimbo yao ni wao bila kujali nani alimchagua nani alimkataa.

Wananchi wa jimbo wanamwangalia mbunge kama kiongozi na wala si mwanasiasa. Ni kwa msingi huo yanapotokea matatizo,wananchi huenda kwa kiongozi wao na wala si kiongozi wa siasa.

Vijana hao hawawezi kuzitofatisha hali hizo mbili.Viongozi wa kisiasa wanaumia umbu mbu wa wazee kuwaburuza kwa kiasi wanachotaka. Utasikia wanaitwa katika vikao na kupewa maagizo.

Huo si uongozi ni uongozi wa siasa kwa kiongozi wa kisiasa.
Imefika mahali hawajali tena hadhra iliyowapeleka Dodoma, wanakuwa loyal kwa kundi la watu 105 wakiacha milion kadhaa zinazowategemea zikiwa hazina majibu ya matatizo yao.


Kwavile hawawezi kutenganisha uongozi na kiongozi wa kisiasa, mara zote wamekuwa wakijificha nyuma ya chama ili misimamo yao isijulikane.
Siku zote wamekuwa woga wa nafsi zao na si za wale waliowatuma.


Vijana wanalazimika kutumikia 'hayawani' na kujitia uhayawani ili kuendelea na nafasi zao na si nafasi za uongozi.

Hayo unayaona pale kijana kama January anaposimama na kusema serikali 2, tatu hazifai.
Huyu hawezi kutueleza kwanini serikali 2 na kwanini si tatu, leo anataka kuwa kiongozi.

Huwezi kuwa kiongozi usiyeweza, kwanza kuhrshimu wananchi na pili kujua mipaka ya kiongozi na kiongozi wa siasa.
 
Msingi wa hoja ya Nguruvi3 kuhusiana na vijana, katiba mpya na kiu ya uongozi umeanza kuwa wazi. Katika michango yao kama wajumbe wa bunge BLK, January Makamba, Hamis Kigwangala na Vita Kawawa wamesikitisha vijana wengi sana. Niliamua kwenda kwenye mgahawa kinondoni kusikiliza bunge huko ili nipate mwanga juu ya jinsi gani suala la serikali tatu linavyojadiliwa mitaani. Kwa kweli wananchi wengi sana wanazidi kuamka, na kuna vijana wengi walikerwa sana za hoja za vijana wenzao niliowataja. Kinyume cha matarajio ya wengi, Maria Sarungi kama mjumbe mwingine kijana katika BLK aliwafungua sana watazamaji kwa darasa lake juu ya jinsi gani hivi tunavyozungumza, serikali tatu zipo na kwamba zitazidi kuwepo hata ccm wakifanikiwa kuleta mfumo wanaosema wa "serikali mbili zilizoboreshwa".

Kati ya wajumbe wote, January alienda mbali na kujadili kwamba yeye ni mmoja wa viongozi wa baadae wa taifa hili ambao wana nia ya kuendeleza misingi yote iliyoachwa na waasisi wa muungano wetu. Kwa maana nyingine, vijana waliopo kwenye nafasi za kusaidia mabadiliko wameamua kuweka wazi kwamba wao hawatakuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Ni vigumu kuelewa chama gani cha siasa kinaweza endelea kudumu kwa kuwa na mawazo yale yale kwa miaka 50.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi, nguvu 3 na wengine. Sijui huenda binafsi nitakuwa sielewi AMA naelewa kwa namna Nyingine , Mantiki ya vijana Kama jinsi mlolongo wa Uchambuzi wa mada hii ulivyoanzia toka juu.

Ni kweli Changamoto ni kubwa na Mimi naona vijana hasa ndio wanalengwa kwasababu ya wingi wao ktk idadi ya watu wa Taifa letu. Hii ni sawa lakini binafsi nahisi sasa ni wakati wa kujadili namna ya kupata ufumbuzi wa tatizo la uongozi na mwenendo wa nchi yetu kwa ujumla.

Ninaposema kujadili suala la kubaini tatizo la uongozi ni nini kabla ta kuegemea mawaO yetu baina ya wazee na vijana tunapaswa kujiuliza pia mambo yafuatayo

1.Tunapoizungumzia Tanzania Kama nchi ya Democrasia, je kuna Democrasia kweli AMA ni dhana ya kukalilishwa? Ikiwa tutakubaliana ya kuwa kuna Democrasia nchini Tanzania, AMA tunataka Democrasia ( Kama haipo), tutambue kabisa kuwa Democrasia ya kweli haihushishi Umri wa vijana na wazee, hapa ndipo sasa tunapaswa kutambua kuwa tunapaswa kuelekeza Mawazo yetu kwa wananchi. ( labda tutumie neno, wananchi walio wengi- kwa maana ya vijana). Tuki generalize neno vijana hata wasio vijana watatumia mwanya huo na hata walio vijana watautumia pia, ( kwa maana zote, nzuri na mbaya)

2.inapaswa tutambue kuwa, ktk nchi yetu tuna wananchi wengi na wazalendo wachache sana, na hili ni tatizo ambalo lime kuwepo karne kadhaa sasa na ni tatizo ambalo lilikumba kila Taifa lililokuwa na Democrasia changa, Hapa tatizo kubwa ni Elimu, kwa maana ya Elimu ya uraia.( wananchi wa Ufaransa baada ya kupata Elimu , ndipo tukapata French Revolution, hawakuamka tu wakaamua)

Ni ukweli tu ulio wazi kuwa Nchi yetu inatatizo la kuwa na mashabiki wa siasa na sio wana siasa, wengi wao ndio wamebahatika hizo nafasi walizonazo kutokana na wananchi wengi kuwa na Uelewa mdogo wa Siasa, hili sio tatizo kwetu tu, lilianza zamani, na ndio maana kipindi furani nchini ugiriki walipinga sana hii dhana ya wanasiasa kutumia mwanya wa wananchi walio na Uelewa mdogo ktk siasa kwa kujipatia kura na hivyo wakapendekeza uchaguzi wa viongozi bora uwe unafanywa kwa rotary.
Hivyo, nadhani ni wazi tu tutambue kwamba, Enzi za Mwalimu, hadi kutufikisha hapa ni kwasababu tu, alikuwa mzalendo wa kweli na alikuwa ameona mbali hata akaja na azimio la Arusha , ambalo lilimlazimu hata kutumia Democrasia ya herufi ndogo ili mambo yaende. Hayo yote ilitokana na kutambua madhara ya mapokeo ya dhana zisizotambulika chanzo na Kusudio lake( dhana Kama ya Democrasia ya sasa) , ambazo sisi tuliostaarabika tunapokea na kuweka ktk matumizi bila kujua kuwa nyuma ya chambo kuna ndoano.

Hivyo wadau, hebu tuanze kurudi nyuma, wapi tulikosea, na ni vipi tutarekebisha?
 
Andrew Nkumbi
Kwnza ahsante kwa bandiko.
Ningependa niwekejambo moja sawa kabla sijapitia hoja zako 1 na 2.

Tumeweka bandiko la vijana kutokana naudanganyifu unaoendelea. Kwamba, sasa tumefika mahali mtu anayetanguliza ujanani kama CV ya uongozi. Tunasikia watu wakitaka kuwa Marais na sababu nivijana.

Zama zilizopita kulikuwa na vijana katikauongozi waliopatikana kwa sifa zao hata kama walikuwa na umri mdogo.Pius Msekwa, Jenerali ulimwengu, Basil Mramba, Cleopa Msuya, Salim Ahmed,Stephen Wasira tunayemsikia, Samwel Sitta, Marehemu Kolimba, Warioba kwauchache wa kuwataja.

Vijana walipata uongozi kwa kuangaliwa uwezowao na wala si ujana wao. Siku hizi tumewasikia akina January, Ngeleja n.kwakitaka Urais.

Tunauliza kwa lipi hasa? Jibu ni rahisi ni vijana.
Kwamba hatakama mtu aliyeshindwa kazi ya uwaziri ujana unampa nafasi ya Urais ama uongozi.

Hata kama waziri aliyeko madarakani ameshindwa kuzuia bei ya kadi za simu, nayetunaambiwa anafaa kuwa rais. Tunapohoji kwa lipi? Tunaambiwa ni vijana.

Tumewapa 'benefit of doubt' unaona miaka8 iliyopita jinsi nchi hii ikiongozwa na kijana na vijana wenzake ilipo.

Natumaini umeona yanayoendelea bungeni vijana wakiwa wanaongoza kwa upotofu, ututusa na uzumbukuku.

Hoja kubwa si kulinganisha wazee na vijana au kutafuta makundi.
Ni suala la kuueleza umma kuwa hii kauli ya ujana inayotumiwa kama CV ni udhaifu wa watu wasio na hoja.

Tunajaribu kuufahamisha umma kuwa utapeli upo katika form nyingi.
Na wala haina maana tunawasema vijana wote.

1. Ni kweli demokrasia haichagui umri. Ni kwa msingi huo tunasema watu watumie haki zao za kidemokrasia bila kutanguliziwa CV ya ujana.

Demokrasia itoe uhuru wa kuchagua anayefaa na wala si wajihi au jinsia.
Ni kweli pia demokrasia yetu ni changa. Ni vema tukaanza kuilea katka wakati muafaka siyo ikiashaota manyoya. Udongo uwahi ungali maji.

2. Nakubaliana nawe kuhusu suala la elimu.
Niongezee kuwa elimu lazima ianze kuanzia utotoni kwenda mbele.

Tunachokiona ni matokeo mabaya ya mtayarisho ya vijana wetu.
Lakini hata hili la kuonyesha kuwa CV ya mtu haijalishi jinsia, wajihi au umri si elimu pia.

Tatizo lipo katika elimu kuanzia sekondari hadi vyuo vikuu.
Elimu yetu haipo katika kumjenga mtoto kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Elimu yetu ni ya kutayarisha wafanyakazi na siyo wahitimu.
Mhitimu hawezi kushindwa kufanya research ndogo kujua Tanzania imeanzia wapi, Tanganyika ni kitu gani.

Matokeo ya elimu finyu ni pale watu wanapofungiwa na kuambiwa shut up! ni pale Pinda anaposema Tanganyika haijui ingawa ana cheti cha kuzaliwa cha Tanganyika, na kwa bahati mbaya vijana wanapiga makofi.

Kwa ujumla yote uliyoyasema ni kweli, lakini pia usisahau kuwa kutafuta suluhu bila kukemea ni kutia maji ndani ya ndoo.

Tukemee kwanza halafu tuangalie suluhu, kukalia uzumbu kumbu unaonedelea Dodoma ni kutoa baraka za ubaradhuli kutamalaki.



 
Nguvu3

Ahsante sana kwa bandiko hapo juu na maelekezo, sasa nimepata vyema, na tunaweza kuendelea kukemea kwa pamoja sasa.

Nimefurahi sana ulipogusia suala la Elimu kwa ujumla. Ingawa Mimi nili gusia Elimu kwa maana ya elimu ya uraia, elimu ya kuwajenga wananchi wawe wazalendo wa kuipenda nchi Yao na kukemea mabaya kulingana na historia ya utamaduni halisi wa Mtanzania.

Naendelea kukemea sasa

Elimu yetu, hasa ndio matokeo ya haya tunatoyaona kwa hivi sasa. Elimu yetu inaandaa vijana na matabaka ktk jamii yetu, na ndio inatumika Kama siraha angamizi. Dhana ya ujana, pamoja na Elimu yetu ( ya idadi ya milango ya madarasa- naiita hivyo).

Nafupisha Hadithi tu kwamba, Kama tunataka mfumo bora wa ki uongozi wa kisiasa na kijamii ktk Taifa letu, binafsi nasema mabadiliko ya mfumo wa Elimu yetu ndio kitu ambacho kilipashwa kupewa kipaumbele kwanza Kabla ya mengine yote.

Nadhani hata Kabla ya hili la Katiba ( kwa Mtazamo wangu) nadhani tungeanzia mabadiliko ktk Elimu ( Kama kipaumbele cha kwanza) kisha yakaja mengine, nadhani hata Katiba tungepata nzuri sana.

Kuna vitu vingine, huwa vinakuwa ni misamiati migumu sana kueleza na ukaeleweka kwa Mtanzania wa sasa( ambaye anapokea mapokeo bila kuchuja jema na baya). Mfano nchi ya Denmark, haina chombo Kama PCCB hapa kwetu, same as Norway na kwingine kwingi, dhana ya uwajibikaji, imewaingia sana kiasi kwamba hata vizazi vipya vinazaliwa na kukutu utamaduni huo na kuuendeleza.

Huu ni ukweli mchungu tu kuwa CCM, kuna mengi sana walikosea na kwa masrah ya Taifa ni vyema sasa wakubaliane na matokeo kuwa walikosea na wanahitaji marekebisho Kama sio mabadiliko ( yawe ya wanaofahamu vyema na sio wa kuja kuendeleza yaliyopo).

Ukiangalia mfano wa hizo nchi, kiutawala zikoje, utagundua ndani Yake zina kila dalili ya kile sisi tulitupa kando ( azimio la Arusha). Tulikosea sana , hatukupaswa kutupa jongoo na mti wake. Lakini ni wazi tu kuwa, bado nafasi ni kubwa sana endapo tutaivaa uzalendo na tukaacha kuegemea itikadi ya vyama ( chanzo cha tatizo), mambo yanasonga , wananchi wetu ni wazuri sana endapo wakipata viongozi wenye maono. Hawa wanaojiita vijana ni SIFURI, Enzi za Mwalimu, hawafai hata kuwa watendaji wa serikali za Mitaa.
 
Andrew Nkumbi , elimu ya uraia peke yake sidhani kama ni jibu sahihi sana.
Ninadhani elimu kwa ujumla wake ni jibu.

Nitakupa mfano, katika miaka ya 70 na 80 Chuo kikuu kilikuwa ni sehemu ya chimbuko la fikra. Ingawa watu wanasema Nyerere aliwabana watu, akiwa mkuu wa chuo aliruhusu kanuni za uhuru wa kitaaluma kufanya kazi.

Ni wakati huo shughuli za wapigania uhuru, mawazo ya Pan Africanism, Neo colonialism n.k. yalikuwa yanajadiliwa kwa undani.

Kupitia mijadala hiyo uzalendo ulikuwa unajengeka bila kuwa na somo. Ilikuwa ni kawaida kuwakuta wanafunzi wawe wa engineering, law au art wakijadiliana kwa undani kabisa.

Nadhani unakumbuka akina Henry Kissinger walipotaka kufanya ziara Tanzania.
Chuo kikuu ilikuwa mahali pa fikra mpya na chemchem ya mawazo.
Kutokana na hofu ya watawala, maeneo ya vyuo yamebaki kuwa ni sehemu za fizikia, kemia n.k.

Linapofika suala la kujitambua na kupambanua wanafunzi wanakuwa watupu.
Ndio zao tunaloliona sasa hivi Bungeni.

Hili limeathiri sana hata uwezo wa wanafunzi na wahitimu kuingia katika ushindani wa soko la kimataifa.

Kwa ufupi ni kuwa kuna tatizo la elimu ambalo ni kubwa na linapaswa kuangaliwa.
Tatizo kubwa zaidi ya hilo ni viongozi wanaopatikana kwa ujanja na si merits.

Kwa kutambua hilo lazima tuwe na mahali pa kuanzia. Na kwa kutambua kuwa kuna mahali pa kuanzia viongozi ndio wameingilia mchakato wa nyaraka inayotupa mwelekeo mpya yaani katiba.
Hivyo watu wanapozungumzia katiba si suala la muungano tu, ni zaidi ya hapo.

Katiba haiwezi kuwa panacea ya matatizo yote likiwemo hili la elimu.
Inaweza kuwa msingi wa ufumbuzi wa matatizo tuliyo nayo.
 
Last edited by a moderator:
Ni vigumu kuelewa kwanini Vijana wa aina hii wanakubaliana na hoja kwamba 80 percent ya watanzania wamezaliwa ndani ya muungano kwahiyo hawana sababu za msingi to question muungano walioukuta. Hali hii inathibitisha kwamba uwezo wao wa kuchambua mambo ni mdogo, ndio maana wanachukua yale ya kuchambuliwa.

Scotland iliungana na Uingereza mwaka 1603 kama sikosei, hivyo kufanya muungano huo kudumu kwa miaka takribani 400. Vijana leo hii (wananchi chini ya umri wa miaka 35) nchi scotland wanakaribia asilimia 40. Lakini pamoja na hayo, wao, baba zao, babu zao, na nyanya zao, wote wamezaliwa ndani ya muungano. Kwa maana nyingine, asilimia mia moja ya wa-scottish wanaokaribia jumla ya milioni sita, wote wamezaliwa ndani ya muungano. Lakini pamoja na hayo, bado wananchi wengi wanazidi kujiunga na upande wa kutafuta political and fiscal autonomy kutoka UK. Hali hii imechangiwa na mapungufu ya Unitary System iliyopo UK, same system imposed on us in 1964. Ni kutokana na mapungufu ya mfumo wa muungano (tofauti na mfumo wa shirikisho), UK ilishuhudia "Ireland" ikijitoa in 1920s, UK ilishuhudia ugaidi na vita vya ireland ya kaskazini, na sasa ya scotland nayo yanatimia. Ni kutokana na hali hii, Uingereza imeanza kuangalia uwezekano wa kuleta shirikisho.

Kinachoshangaza, vijana waliopo kwenye BLK, pamoja na access yao to researches and studies mbalimbali, bado wanakuja na hoja za kushangaza sana. Tulitegemea wata waelimisha wazee na kuongoza wimbi la mabadiliko.

Unamsikiliza January, Mwigulu, Kigwangalla, Serukamba, Vita Kawawa, Masauni, inakuwa vigumu kuelewa vijana hawa wakipewa dhamana ya kuliongoza taifa letu watatupeleka wapi?!

Kwa kweli hatutawahitaji katika ujenzi wa Tanganyika yetu, mchango wao utakuwa na thamani katika maeneo mengine ya kijamii na kiuchumi, lakini sio uongozi. Hatuwezi kuwapa uongozi Tanganyika ikizinduliwa kwa sababu hatutawaamini - hawa ni wasaliti wa Tanganyika.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Unamsikiliza January, Mwigulu, Kigwangalla, Serukamba, Vita Kawawa, Masauni, inakuwa vigumu kuelewa vijana hawa wakipewa dhamana ya kuliongoza taifa letu watatupeleka wapi?!

Kwa kweli hatutawahitaji katika ujenzi wa Tanganyika yetu, mchango wao utakuwa na thamani katika maeneo mengine ya kijamii na kiuchumi, lakini sio uongozi. Hatuwezi kuwapa uongozi Tanganyika ikizinduliwa kwa sababu hatutawaamini - hawa ni wasaliti wa Tanganyika
Na huyu umemsahau
- Kumuita Baba wa Taifa kuwa alikuwa Tapeli kama Papa Msoffe na Alex MAssawe unasema sio matusi? Sasa nini maana ya matusi kaka?

Le Mutuz System
Well, heshima mbele sana JF,

- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?

- Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!

- Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!

- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!

RESPECT PEOPLE!

Mr. Willie @DSM City!
Ni mtu mmoja huyo na ID ni ile ile
 
W.J.Malecele,


Azimio la Arusha linapozungumziwa sio kwamba tunataka kurudi ktk azimio la Arusha, Bali tunahitaji kufanya mabadiliko kutokea hapo ktk aZimio la Arusha ili kuendana na wakati wa mabadiliko ya sasa, hiyo ndio moja ya hatua ktk kuendelea, huwezi kuanza na SIFURI, ukafikia nne Kisha ukasitisha na kuanza SIFURI tena itakugharimu Muda mwingi na uchovu na kukata tamaa ili kufikia kumi.

Tunapotaka kunyanyua kuta ili iwe nyumba, huwa tunaweka tofari katika msingi uliokwisha kujengwa imara.

Msingi wa Taifa letu ni Azimio la Arusha ( halikwepeki), hii ni document ya maana sana aisee. kuanzia hapa ndipo tunaiona Tanzania ya sasa na ndipo tunagundua madhaifu ya sasa. Bila azimio la Arusha Leo hii hayo Madini usingeyakuta, gesi mtwara nchi hii ingekuwa ni uwanja wa mapigano zaidi ya Nigeria baada ya Mafuta.

Tambua kwamba Tanzania ni nchi yenye makabila zaidi ya 100, bila azimio la Arusha na sera ya Ujamaa Leo nchi hii ingekuwa ni uwanja wa Mapambano baina ya makabila , angalia Rwanda na Burundi na kwingine kwingi.

Falsafa ya nchi ni ipi kwa sasa baada ya kuua azimio la Arusha? Tumebaki kuwa tunaunda sera kupitia Falsafa za wenzetu na ndicho wanataka, unadhani kwa dhana hii Ushoga utaukwepea wapi, unyonyaji kwa sera ya Maendeleo ( free market) utaukwepea wapi? Tunaingia kichwa kichwa tu, tunavamia chambo kumbe nyuma Yake kuna ndoano.

Hii nchi iko pabaya hakuna pa kukwepea Kama hatutaweza kirudi ktk azimio la Arusha na kuanzia hapo.
 
wakuu Nguruvi3 na Andrew Nkumbi,

msitarajie malecela junior, january, mwigulu, nape wakaja kwenye mjadala huu kwa sababu wanajua kwamba hawana hoja za kujibu. Mijadala hii sio size yao, thats the bottom line. kama huyo malecela hapo juu, ni mnafiki tu, unamteteaje baba wa taifa kwa upande mmoja wa ubongo wako halafu kwa upande mwingine unasema alikuwa mdhaifu katika masuala ya sheria na uchumi? Tungefarijika sana kama angepata udhubutu wa kuja na kujadiliana kwa hoja humu na kwa kufafanua hili. Lakini itakuwa kazi bure kwani katika mjadala wake huo juu ya azimio la arusha, alikiri kwamba hajalisoma, huku akijitapa kwamba hana haja ya kusoma kitu ambacho tayari anaona ni "failure". Ndio hawa wanapigana vikumbo kudai wao ni viongozi wa kitaifa, taifa lipi? eti mashuhuri, wapambanaji, kwa yepi yenye tija kwa taifa, hasa vijana wenzao ambao ndio wengi katika nchi yetu? Hakuna kitu. Ukweli lazima usemwe bila unafiki. Vijana hawa ni mizigo kwa vijana wenzao walio wengi katika taifa hili. Iwapo wanakataa, jukwaa lipo wazi kwa wao kuja tuelewesha kwanini hatupo sahihi juu ya hili. Zipo hoja nyingi ambazo tumezijadili awali katika uzi huu, wazipitie, kisha warudi na hoja. Most likely hawatathubutu, kwani as i said earlier, mijadala kama hii sio size yao. Lakini ni dhahiri kwamba ujumbe unawafikia. Hilo ni dhahiri.
 
W. J. Malecela;9325468]- Kumuita Baba wa Taifa kuwa alikuwa Tapeli kama Papa Msoffe na Alex MAssawe unasema sio matusi? Sasa nini maana ya matusi kaka?
Maana ya matusi ni unafiki, uongo na kumtumia Nyerere kwa kung'ong'a.

Viwanda alivyowaachia Watanzania mumevigeuza maghala ya chumvi.
Leo Mwalimu 'angerejea' akaona Mang'ula machine inavyotumia kuhifadhi chumvi wala asingehitaji tusi lingine.

Mwalimu angeona jinsi reli ya Dar-Tanga aliyejenga ilivyoota majani kwa kushindwa kuweka mabehewa asingehitaji tusi jingine.

Mwalimu angeamka na kuona wezi wa mali ya umma ndio wajumbe wa kamati kuu na ndio wanaoandika katiba, pengine angeomba arejee alikopunzika haraka.

Mwalimu angeona jinsi serikali inavyotuma watu makanisani kwenda kuchochea vurugu za katiba na watu hao bado wanaitwa mwaziri angekata rufaa kama ni kurudi arudishwe nchi nyingine si hii aliyoiacha.


Wala Mwalimu asingesikitika kama ametukanwa, angewasikitikia watanzania wanavyoteswa na wahuni wengine aliowakataa akiwa hai.

Angeshangaa ni lipi tusiloliona hata pale wezi wanatamani Ikulu?

Mwalimu angechanganyikiwa si kwa matusi bali kwa jinsi nchi aliyoipigania ilivyo na inavyoelekea porini.

Mwalimu angelia sana kwa kuona hata wasio na macho kama William nao sasa ni viongozi wa chama alichoasisi.
W. J. Malecela;3773289]Well, heshima mbele sana JF,
- Ninaomba kusema tena na tena, we were Dead wrong na idea za Azimio La Arusha, infact ndilo limetufikisha hapa tulipo yaani tumekwama hili taifa, hatujui tunakokwenda wala tulikotoka. Halafu wanatokea wasomi wanaodai eti turudi kwenye Azimio, hilo Azimio limetushinda mwanzoni kwa nini kuna wanaoamini tutaliweza sasa?
Hata mimi nashangaa kama wewe! Kama wasomi wameona azimio haliwezekani, kwanini wasomi hao hao waone muungano wa serikali 2 ulioasisiwa kabla ya azimio na ambao umetufikisha hapa kwamba tutauweza!
Nami ninashangaa wasomi kama wewe!

Recently, nimeona wale wengi walioachwa kwenye uongozi wa juu yaani kwenye mlo, wakililia Azimio, halafu ninachukizwa sana ninapoona media inawapa free lunch hawa waliokosa mlo, sijawahi kuwasikia wakisema Azimio liliwahi kumfunga kiongozi gani wa juu mwizi, sijawasikia wakisema Azimio lilifanya nini cha maaana mpaka wanalilia!
Waliokosa mlo ni wapi hao? Hata mzee baba aliwahi kusema tumeacha azimio, sijui kwavile alikosa mlo huenda ndio unamsumanga kama unavyomsumanga na hoja yake ya serikali 3. Wee mwana unalaana wewe! Mzazi hatukanwi.


Ni miaka zaidi ya 25 baada ya kifo cha azimio la Arusha kilichotokea Zanzibar na mazishi yakawa Dodoma. Katika muda huo hakuna aliyefungwa kwa wizi.

Na si kufungwa hata kutajwa tu kwa bahati mbaya.
William, nani alichukua pesa hazina na kununua Radar?
Bunge hili la chama chako limeshindwa kutaja jina hata moja.

William, unajua EPA pesa zilichukuliwa na nani? Unajua nani yupo nyuma ya Dowans n.k. Vipi leo usote vidole azimio wakati hata kupiga uyowe wa mwiiizi mumeshindwa.
Mwalimu, yes was the greatest ever, lakini Mwalimu alikuwa na mapungufu makubwa mawili, hakujua;- !. Uchumi 2. Sheria, hivi vitu viwili Mwalimu simply hakuvijua kama alivijiua basi hakuvitilia maanani, na ndivyo vinavyolitafuna taifa letu sasa akiwa hayupo!
Mwalimu hakujua uchumi?
Baada ya Mwalimu wamefuata viongozi 3. Niambie jambo gani ambalo viongozi hao kwa pamoja wamefanya ambalo Mwalimu hakulifanya.

Kuhusu sheria, najua sentiment yako. Damu ni nzito kuliko maji bwana! Mwalimu alikosea sheria pale alipomwita mzee mhuni. Alitakiwa akae kimya wahuni waanze kazi mapema.
Kwani huoni baada ya kifo chake wahuni wakapata mwanya.
- WA-TANZANIA, KAMA TUNATAKA KUSONGA MBELE NA KIJIREKEBISHA TUACHANE NA MANENO YA AZIMIO LA ARUSHA, KWA SABABU NDILO HASA LIMETURUDISHA NYUMA SANA, LISIRUDI, LIENDE ZAKE, NA TUSILIJADILI MAANA NI SHETANI LILILOTURUDISHA NYUMA SANA, SASA TWENDE MBELE NA UBEPARI NA UTAWALA UNAOHESHIMU SHERIA NDIO THE BEST WAY MBELE!
Ungeanza na katiba ya chama chako, katiba ya nchi zinazotambua sisi kama taifa la kijamaa.
Umekaa kimya halafu unazungumzia marehemu azimio la Arusha.


Taifa hili lina matatizo sana, hawa akina Le Mutuz wana exposure sana tu, kama ukiwasoma utajiuliza hivi huko vijijini hali ikoje.

Huyu mzazi wake alikuwa makamu wa kwanza wa rais, tulitegemea uwezo wake uwe wa maana sana. Disappointment kwenda kwa mbele.

Guess what ipo siku utamsikia ni waziri. Si unaona alijaribu kuwa mbunge wa EAC.

Mungu ni mkubwa, wanadamu hatuna shukrani.
Tuanze na kumshukuru mungu kwa kutuepusha na mbalaa na balaa.
Mungu inusuru nchi hii. Tunusuru Watanzania na kipindu pindu, mafuriko, kiangazi na hawa!

 
W.J.Malecele,


Azimio la Arusha linapozungumziwa sio kwamba tunataka kurudi ktk azimio la Arusha, Bali tunahitaji kufanya mabadiliko kutokea hapo ktk aZimio la Arusha ili kuendana na wakati wa mabadiliko ya sasa, hiyo ndio moja ya hatua ktk kuendelea, huwezi kuanza na SIFURI, ukafikia nne Kisha ukasitisha na kuanza SIFURI tena itakugharimu Muda mwingi na uchovu na kukata tamaa ili kufikia kumi.

Tunapotaka kunyanyua kuta ili iwe nyumba, huwa tunaweka tofari katika msingi uliokwisha kujengwa imara.

Msingi wa Taifa letu ni Azimio la Arusha ( halikwepeki), hii ni document ya maana sana aisee. kuanzia hapa ndipo tunaiona Tanzania ya sasa na ndipo tunagundua madhaifu ya sasa. Bila azimio la Arusha Leo hii hayo Madini usingeyakuta, gesi mtwara nchi hii ingekuwa ni uwanja wa mapigano zaidi ya Nigeria baada ya Mafuta.

Tambua kwamba Tanzania ni nchi yenye makabila zaidi ya 100, bila azimio la Arusha na sera ya Ujamaa Leo nchi hii ingekuwa ni uwanja wa Mapambano baina ya makabila , angalia Rwanda na Burundi na kwingine kwingi.

Falsafa ya nchi ni ipi kwa sasa baada ya kuua azimio la Arusha? Tumebaki kuwa tunaunda sera kupitia Falsafa za wenzetu na ndicho wanataka, unadhani kwa dhana hii Ushoga utaukwepea wapi, unyonyaji kwa sera ya Maendeleo ( free market) utaukwepea wapi? Tunaingia kichwa kichwa tu, tunavamia chambo kumbe nyuma Yake kuna ndoano.

Hii nchi iko pabaya hakuna pa kukwepea Kama hatutaweza kirudi ktk azimio la Arusha na kuanzia hapo.
Andrew Nkumbi , msingi uliopo sasa ni kuzunguka duniani tukipitisha bakuli la kuomba omba.
Kuuza wanyama kupitia KIA
Msingi wa sasa ni kuzalisha wezi, kushindwa kusimamia hata kilichokuwepo na kuishi gizani.

Msingi wa sasa kuuza wanyama kupitia KIA.

Mwalimu alijenga msingi 'mbaya' wa nishati kwa kujenga mabwawa ya kuazlisha umeme.
Sasa hivi tuna msingi mzuri, kata umeme singizia kiangazi watu waagize mafuta! alah.
Mwaka mzima bwawa halikauki, sisi tutaagiza mafuta wapi!

Mwalimu aliacha taifa likiwa na mwanga, mwaka wa 8 hawawezi kukabiliana na mgao. Nao tunawaweka meza moja na Mwalimu kwa pamoja wakisema ni viongozi
 
Andrew Nkumbi , msingi uliopo sasa ni kuzunguka duniani tukipitisha bakuli la kuomba omba.
Kuuza wanyama kupitia KIA
Msingi wa sasa ni kuzalisha wezi, kushindwa kusimamia hata kilichokuwepo na kuishi gizani.

Msingi wa sasa kuuza wanyama kupitia KIA.

Mwalimu alijenga msingi 'mbaya' wa nishati kwa kujenga mabwawa ya kuazlisha umeme.
Sasa hivi tuna msingi mzuri, kata umeme singizia kiangazi watu waagize mafuta! alah.
Mwaka mzima bwawa halikauki, sisi tutaagiza mafuta wapi!

Mwalimu aliacha taifa likiwa na mwanga, mwaka wa 8 hawawezi kukabiliana na mgao. Nao tunawaweka meza moja na Mwalimu kwa pamoja wakisema ni viongozi

Asante sana kwa mjadala huu Nguruvi3, Mungu awabariki sana.

Unazungumzia Mgao ambao pia ulinufaisha watu wakavuna kupitia janga hilo na watu hao hao ambao Mwl.Nyerere akiwa hai hawakuthubutu kufungua mdomo na kuuutaka Urais tangu walipojaribu hivyo kwa mara ya kwanza.Leo wanaamini kabisa wanatosha na wale wanaojifanya wanamuenzi Mwl.Nyerere wanawapigia kampeni.

-Baadhi ya vijana wamesababusha vijana wengine washindwe kuaminika.Ni traitors waliopindukia kwa sababu ya woga na unafiki tu

-Kilichobaki ni vijana tulioko nye ya Bunge sasa kuipigania hatima ya nchi na vijana waliopo ndani ya Bunge tuwapimie kwa kipimo kile kile tutakachowapimia wale wazee waliolifikisha Taifa hapa

-Vijana kama January na Kigwangala hawawezi kusimamia mabadiliko maana wameamua kupelekwa kulingana na mkondo wa mfumo na hawataki kutoka kwenye comfort zone.

Kifalsafa na kisaikolojia,mtu asiyependa kutoka ndani ya comfort zone ni mwoga na mpinzani wa mabadiliko.Hawa ni maadui wa change hata kama wana exposure na elimu
 
Last edited by a moderator:
Andrew Nkumbi , msingi uliopo sasa ni kuzunguka duniani tukipitisha bakuli la kuomba omba.
Kuuza wanyama kupitia KIA
Msingi wa sasa ni kuzalisha wezi, kushindwa kusimamia hata kilichokuwepo na kuishi gizani.

Msingi wa sasa kuuza wanyama kupitia KIA.

Mwalimu alijenga msingi 'mbaya' wa nishati kwa kujenga mabwawa ya kuazlisha umeme.
Sasa hivi tuna msingi mzuri, kata umeme singizia kiangazi watu waagize mafuta! alah.
Mwaka mzima bwawa halikauki, sisi tutaagiza mafuta wapi!

Mwalimu aliacha taifa likiwa na mwanga, mwaka wa 8 hawawezi kukabiliana na mgao. Nao tunawaweka meza moja na Mwalimu kwa pamoja wakisema ni viongozi


Nguruv3:

Nyerere hakuacha Taifa likiwa na mwanga. Na hakuacha nchi ikiwa katika nafasi nzuri kiuchumi. Kitu Nyerere alichoacha na ambacho hata wapenzi wake wanashindwa kukifanya ni kuelewa maana ya utumishi wa umma. Utumishi wa umma hata katika nchi za kibepari hautaki kukata kona, kupiga chenga, au kutengeneza dili.
 
Asante sana kwa mjadala huu Nguruvi3, Mungu awabariki sana.

Unazungumzia Mgao ambao pia ulinufaisha watu wakavuna kupitia janga hilo na watu hao hao ambao Mwl.Nyerere akiwa hai hawakuthubutu kufungua mdomo na kuuutaka Urais tangu walipojaribu hivyo kwa mara ya kwanza.Leo wanaamini kabisa wanatosha na wale wanaojifanya wanamuenzi Mwl.Nyerere wanawapigia kampeni.

-Baadhi ya vijana wamesababusha vijana wengine washindwe kuaminika.Ni traitors waliopindukia kwa sababu ya woga na unafiki tu

-Kilichobaki ni vijana tulioko nye ya Bunge sasa kuipigania hatima ya nchi na vijana waliopo ndani ya Bunge tuwapimie kwa kipimo kile kile tutakachowapimia wale wazee waliolifikisha Taifa hapa

-Vijana kama January na Kigwangala hawawezi kusimamia mabadiliko maana wameamua kupelekwa kulingana na mkondo wa mfumo na hawataki kutoka kwenye comfort zone.

Kifalsafa na kisaikolojia,mtu asiyependa kutoka ndani ya comfort zone ni mwoga na mpinzani wa mabadiliko.Hawa ni maadui wa change hata kama wana exposure na elimu
Ben , kuna bwana Buchanan anayetumia haki yake ya kidemokrasia kutetea hata yasiyoweza kutetewa.

Nadhani tusome hapa chini kisha tutafakari huyu kijana amepataje nafasi ya kuwa kiongozi wa kundi lolote achilia mbali ujumbe wa bunge la katiba.

Ukimsoma huyu kijana hutakawia kubaini kuwa tuna tatizo kubwa sana nchi hii.
Kwa mfumo wetu ulivyo kuna uwezekano mkubwa akawa waziri siku moja.

https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/647862-nje-ya-bunge-hakuna-katiba-ya-wananchi.html
 
Ben , kuna bwana Buchanan anayetumia haki yake ya kidemokrasia kutetea hata yasiyoweza kutetewa.

Nadhani tusome hapa chini kisha tutafakari huyu kijana amepataje nafasi ya kuwa kiongozi wa kundi lolote achilia mbali ujumbe wa bunge la katiba.

Ukimsoma huyu kijana hutakawia kubaini kuwa tuna tatizo kubwa sana nchi hii.
Kwa mfumo wetu ulivyo kuna uwezekano mkubwa akawa waziri siku moja.

https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/647862-nje-ya-bunge-hakuna-katiba-ya-wananchi.html

Nguruvi3, huyu Kijana wa ccm, kwa Socratic term ni ' SATISFIED FOOL' Huyu hafai hata kuwa mjumbe wa serikali ya mtaa, siku zote usipojua unapoelekea njia yoyote itakufikisha, kijana anaenda enda tu, anasukumwa sukumwa tu nae anaenda.

Sincerely speaking, Kijana huwa anaongea hata hajui anaongea nini. Nahisi sampuri hii ndio moja Kati ya zile zilizochukuliwa randomly ktk kuchunguza IQ za Watanzania.

Washkaji wake AMA kwa yeyote anayefahamiana nae, amuombe aje tu siku moja ktk jukwaa hili, tusemezane kidogo.
 
W.J.Malecele,


Azimio la Arusha linapozungumziwa sio kwamba tunataka kurudi ktk azimio la Arusha, Bali tunahitaji kufanya mabadiliko kutokea hapo ktk aZimio la Arusha ili kuendana na wakati wa mabadiliko ya sasa, hiyo ndio moja ya hatua ktk kuendelea, huwezi kuanza na SIFURI, ukafikia nne Kisha ukasitisha na kuanza SIFURI tena itakugharimu Muda mwingi na uchovu na kukata tamaa ili kufikia kumi.

Tunapotaka kunyanyua kuta ili iwe nyumba, huwa tunaweka tofari katika msingi uliokwisha kujengwa imara.

Msingi wa Taifa letu ni Azimio la Arusha ( halikwepeki), hii ni document ya maana sana aisee. kuanzia hapa ndipo tunaiona Tanzania ya sasa na ndipo tunagundua madhaifu ya sasa. Bila azimio la Arusha Leo hii hayo Madini usingeyakuta, gesi mtwara nchi hii ingekuwa ni uwanja wa mapigano zaidi ya Nigeria baada ya Mafuta.

Tambua kwamba Tanzania ni nchi yenye makabila zaidi ya 100, bila azimio la Arusha na sera ya Ujamaa Leo nchi hii ingekuwa ni uwanja wa Mapambano baina ya makabila , angalia Rwanda na Burundi na kwingine kwingi.

Falsafa ya nchi ni ipi kwa sasa baada ya kuua azimio la Arusha? Tumebaki kuwa tunaunda sera kupitia Falsafa za wenzetu na ndicho wanataka, unadhani kwa dhana hii Ushoga utaukwepea wapi, unyonyaji kwa sera ya Maendeleo ( free market) utaukwepea wapi? Tunaingia kichwa kichwa tu, tunavamia chambo kumbe nyuma Yake kuna ndoano.

Hii nchi iko pabaya hakuna pa kukwepea Kama hatutaweza kirudi ktk azimio la Arusha na kuanzia hapo.

Bila ya Azimio la Arusha madini ungeyakuta. Kuna mambo mengi yaliofanya madini uyakute. Moja ya ni technologia. Nikiwa shule ramani ya Tanzania ilionyesha sehemu nyingi zenye madini. Lakini sababu kubwa iliyosababisha kuto-extract rasilimali hiyo ilikuwa ni initial investment costs. Hata serikali ilijaribu wakati wa Nyerere lakini costs were prohibitive.

Miaka ya karibuni maendeleo ya kitechnologia na kuibuka kwa China kumefanya mambo mengi kuwezekana. Hivyo kusifu Azimio la Arusha wakati kulikuwa na pingamizi la kimitaji na kitechnologia itakuwa tunapoteza hoja.

Kuhusiana na Azimio la Arusha, ukweli wa mambo sio lazima litumike hili mambo mazuri yafanyike. Nimelisoma na sioni kitu chochote kipya au cha ajabu. Unaweza kulitumia kujipatia umaarufu wa kisiasa kwa umma masikini. Lakini huwezi kulitumia kama msingi wa kuwasaidia masikini wenyewe.

Azimio la Arusha ilikuwa ni kazi ya mtu mmoja. Lilikuja kama amri za Mungu zilizoletwa na Nabii Musa pale alivyotelemka kutoka kwenye mlima Sinai. Watanzania hawakuwa na mchango wowote. Hivyo kuwapa watanzania ownership ya kitu ambacho sio chao si kuwatendea haki. Azimio la Arusha ni mali ya chama cha mapinduzi, libakie huko huko lilipo.

Kama unaliona linafaa unaweza kulifuata. Unaweza kufuata miiko yake. Unaweza kujenga vijiji vya ujamaa na kuishi huko. Kama utafanikiwa tutakufuata.

Kuhusiana na ujenzi wa taifa. Umefika wakati mnaolipenda Azimio la Arusha, kukubali kuwa kuna watu hatuliamini Azimio hilo kama msingi wa maendeleo na tuna haki zetu za kikatiba. Pili nchi inaongozwa kwa kutumia katiba na sheria za nchi. Azimio la Arusha sio sehemu ya katiba au sheria ya nchi. Ulikuwa ni mwongozo wa TANU na CCM. Tusio wanachama wa CCM mwongozo huo hautuhusu.
 
Back
Top Bottom