East Coast of Africa Music HQ- The Empire of Tanzania

East Coast of Africa Music HQ- The Empire of Tanzania

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,887
Karibuni Sana.
Katika thread hii nitaongelea uwezo na nguvu ya muziki wa kitanzania katika pwani hii ya mashariki ya Africa. Nguvu na mabadiliko ya kijamii mara nyingi yanahamasishwa na muziki.

Uzuri wa muziki ni mpangilio wa sauti, vyombo vya muziki na fasihi iliyojificha ndani ya muziki. Kwa upande wa pwani hii ya mashariki, Tanzania ndio makao makuu ya mziki mtamu na wa kuvutia. Mziki wa mwambao huu wa pwani ya mashariki umebatizwa kwa jina la Bongo Flava.

Bongo Flava limetokana na neno Ubongo au kwa maana nyingine akili, kwamba jiji la Dar es salaam linaitwa Bongo. Kwamba Dar es salaam inawakilisha Tanzania. Kwahiyo muziki wa Bongo Flava ni muziki wa akili.

Mashairi ya Muziki wa Bongo Flava mara nyingi yanakuwa katika mpangilio wa vina huku yakijaa maneno ya tafsida na tamathali za semi mbalimbali. Nahau, misemo, misamiati na methali huwa zinaunganishwa katika mashairi ya muziki wa bongo flava ili kunogesha na kufanya wimbo upendeze.

Sauti nyororo na za kubamba za vijana wa bongo zinafanya muziki huu uibuke kidedea na kutetea pwani ya mashariki mwa africa kwa hapa africa na dunia nzima. Mashairi mengi ya Bongo flava yanaandikwa kwa lugha ya kiswahili; kitendo hicho kinawafanya wale ambao hawajui kiswahili wapate hamasa ya kujifunza kiswahili kwa kunguvu ikizingatiwa kwamba kiswahili ni lugha adhimu duniani. Inasadikika kwamba lugha hii ndiyo Adam na Eva walikuwa wakiongea wakiwa bustani ya Aden. Baadhi ya maneno ya kiswahili yanasadiifu ukweli huu kwamba kiswahili ndiyo lugha ya kwanza ya binadamu.

Katika thread hii nitajikita kuonesha ubora wa sauti nzuri za watu wa tanzania katika muziki. Nitaonesha mashairi mbali mbali na kuweka video tofauti tofauti kisha kuzielezea.

Zaidi ya kuwa muziki ni burudani, kuelimisha na kuliwaza, mziki umekuwa biashara na vijana wengi wamekuwa wakijiingizia kipato.

Mungu ibariki Bogo Flava, Mungu Ibariki Tanzania.
Karibuni wenzangu kutoka Kenya muweze kujifunza hapa badala ya kuanza kutoa matusi.
"Usivione Vyaelea Vimeundwa"
 
Kiswahili ni lugha ya kwanza umeitoa wapi hii. ..
 
Diamond Platnumz ft Hawa - Nitarejea


Vipi mizigo umeshaweka tayari
Sijechelewa nkaachwa na gari
Basi jikaze usilie mpenzi
Mi nitarudi niombee kwa mwenyezi

Zile taabu na njaa msimu mzima mavuno hakuna
Huwa nakosa raha pale mkikosa cha kutafuna
Roho yangu inauma, sema ntafanya nini na pesa sina
nakuonea na huruma, bora niende mjini kusaka tumaa

Chorus
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
wadanganye na vibagia, waambie pipi ntawaletea
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
nawe usichoke kuvumilia, na kila siku kuniombea


Wanajua kwamba nafsi na roho vitakuwa na wasiwasi
ukumbuke na moyo utajawa na simanzi
ntakapokuwa nakwenda shambani afu niko peke yangu honey
ntapokuja kuwa na majirani ntaumia aaah
pale napotoka kisimani ama nipo na kuni kichwani
sina wakunitua nyumbani ntaliaa

maneno yako yananfanya nakosa raha na mawazo
hata mwenzako sijawahi kufika dar huu ndo mwanzo
vile nakwenda na sijui pa kukaaa wala mavazi ooh
we niombee niepushwe na balaa na maradhi ooh

Chorus
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
wadanganye na vibagia, waambie pipi ntawaletea
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
nawe usichoke kuvumilia na kila siku kuniombea


Unapokwenda kama ukifika salama, utukumbuke na sisi
usisahau kama mkeo na wana, umetuacha na dhiki
vile usijali ila naomba chunga sana, ogopa na marafiki
wakikulaghai hata kwa mbegu za mtama, waambie sidanganyiki

Unapokwenda kama ukifika salama, utukumbuke na sisi
Kumbuka mkeo na wana nyumbani, umetuacha na dhiki ooh
vile usijali ila naomba chunga sana, ogopa na marafiki
wakikulaghai hata kwa mbegu za mtama, waambie sidanganyiki

ntarejea mama
niombee nirude salama
ohhh watoto wadanganye
ihh, ohh

Chorus
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
wadanganye na vibagia, waambie pipi ntawaletea
Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea
nawe usichoke kuvumilia, na kila siku kuniombea
 
uzi mzuri, ila juzi nmeshanga hili ndilo jeshi lenu la zima moto! straight outta tanga baby[emoji3] [emoji3] [emoji109]
IMG_20170610_145108.jpg
 
Mbona wanamuziki wa tanzania huwa hawa shoot muziki zao nyingi tz? alafu jana nimeskia Rayvanny akisema anataka ku relocate Kenya kwa interview ya Citizen TV...Rose Muhando ana toroka...Wema sepetu pia nimeskia akiwa na interest ya kuhamia nairobi...Diamond na mkewe wanaishi Afrika Kusini...Hivi, Bongo kunani?
 
Mbona wanamuziki wa tanzania huwa hawa shoot muziki zao nyingi tz? alafu jana nimeskia Rayvanny akisema anataka ku relocate Kenya kwa interview ya Citizen TV...Rose Muhando ana toroka...Wema sepetu pia nimeskia akiwa na interest ya kuhamia nairobi...Diamond na mkewe wanaishi Afrika Kusini...Hivi, Bongo kunani?


Hizo ni story za kuokoteza
Tanzania inawasanii wengi sana
Tupe hizo video zinazo tengenezwa nje ya Bongo!!
Ukiona video moja iliyo tengenezewa nje ya Bongo ujue kuna video 10 huyo msanii katengeneza bongo
 
Hizo ni story za kuokoteza
Tanzania inawasanii wengi sana
Tupe hizo video zinazo tengenezwa nje ya Bongo!!
Ukiona video moja iliyo tengenezewa nje ya Bongo ujue kuna video 10 huyo msanii katengeneza bongo
fair enough.....unaeza kuwa unasema ukweli ila mbona wengine wachahe wana relocate either SA or Kenya...wakienda SA ama Nigeria nitaelewa kwani nchi hizi zina music industry zenye nguvu...ila mbona kenya...Kenya's music is not better than Bongo's...sielewi..pengine iwe govt yenu inawanyanyasa sijui...ndio maana nikauliza...sina ubaya wowote..kuuliza tu..thread nzuri hii
 
Mapenzi Yana-run Dunia By Alikiba



Sikatai yule muonyesha wivu ndiye mwenye mapenzi ya kweli kwa mwenza
lakini pia uvumilivu na vitendo vya karaha vilimuumiza
mwenzio mimi ni mtulivu na kuiba mali ya mtu sijafunzwa
ona dhambi lawama ulonipa mimi leo inaniuma eh

fikira ziko vibaya za kudhani ya kwamba yule demu nilimpenda
ni kweli nilimpenda, lakini ni kama rafiki wa kima
haya uliyofanya leo, ikifika kesho utajibu nini kiama
kwa yale yote mapendo ni kama kioo aliyokupa niliyaona

ukadhani anakusaliti kutoka kwako na kuwa mimi naye..
mimi na yeye
kutokana na wako wivu ukadariki kumuacha ajiue
kwanini why, unatema Big G kwa karanga za kuonjeshwa
najua mwanamke akipenda, huwa...kapenda kweli

mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run duniaaaa

mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run duniaaaa

feel free to love
feel free to love

wajua kuna waliobadilisha dini na yote sababu ya kupenda
na kuna waliokimbia... hii dunia... sababu hiyohiyo kupenda
yule alikupenda sana, ninajua na mambo mengi umefanya ilala
Best wangu nilimpendaaaa.. umefanya mpaka sasa kajiua

fikira ziko vibaya za kudhani ya kwamba yule demu nilimpenda
ni kweli nilimpenda, lakini ni kama rafiki wa kima
haya uliyofanya leo, ikifika kesho utajibu nini kiama
kwa yale yote mapendo ni kama kioo aliyokupa niliyaona

ukadhani anakusaliti kutoka kwako na kuwa mimi naye..
mimi na yeye
kutokana na wako wivu ukadariki kumuacha ajiue
kwanini why, unatema Big G kwa karanga za kuonjeshwa
najua mwanamke akipenda, huwa...kapenda kweli

mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run duniaaaa

mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run dunia, mapenzi yana-run dunia
mapenzi yana-run duniaaaa

feel free to love
feel free to love​
 
fair enough.....unaeza kuwa unasema ukweli ila mbona wengine wachahe wana relocate either SA or Kenya...wakienda SA ama Nigeria nitaelewa kwani nchi hizi zina music industry zenye nguvu...ila mbona kenya...Kenya's music is not better than Bongo's...sielewi..pengine iwe govt yenu inawanyanyasa sijui...ndio maana nikauliza...sina ubaya wowote..kuuliza tu..thread nzuri hii
Unapiga povu sana. Mtu mzima ukivuliwa nguo ni vyema kuchutama.
 
Shika Adabu Yako - Ney wa Mitego


Intro
Wanabebwa na refa na bado nacheza rafu
Mi siogopi kufa, ngoja kwanza nipige pafu
Sss, ehe-hee pumbavu!
Wapinzani wajipange round hii ni ligi ndefu

Haya najisikia kuwachana (wachane)
Niwachane? (Wachane!)
Najisikia kutukana (watukane)
Eh, niwatukane? (Watukane!)

Verse 1
Haya naanza kuchana, kuhusu wasichana
Hawa ndio mama zetu ila sometimes hawana maana
Wapo wanaofanya mziki na mziki hauwalipi
Dada zetu wa mjini siku hizi hawavai chupi
Najiuliza ni joto au fashion
Au biashara ndo wanafanya promotion?
Aliokanja nikanjue, niwachane hawa ma-boy
We ni moto uliyewashwa, usiyezimwa hata kwa fire
Bongo Movie imekufa wamebaki kuuza sura
Wote wanataka kuimba ka Shilole na Snura
Ray Kigosi kawa mkongo hadi leo anaishi kwao
Hela za kuuza movie zote ananunua mkorogo
Kama ni umri umeshaenda, au bado anajiona dogo?
Diva Supermario, ana gari ya milioni 10
Hajawahi miliki ghetto
Anaishi tu kwa mademu, gari lake ndo ghetto
Huu ndio wendawazimu!
Kumiliki gari sijui ndo yake ndoto!
Mnaopanga kunishitaki nawapa dole la kati
Mkashtaki hata kwa Magu na bado ntawapa facts
Si wamekuchagua wenyewe Magu waonyeshe maujuzi
Vunja mpaka ikulu wakikuletea upuuzi
Aah! Sifanyi beef mimi na watoto wa juzi

Chorus
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)

Mi sitaki tugombane
Nia nikurekebishe, haya mambo yaishe
Mi sitaki tugombane
Nia nikurekebishe, haya mambo yaishe

Bridge 1
Nataka kwenda Msanga, oh nauli na bure
Chakachaka, chakachaka, oh nauli na bure
Nataka kwenda Msanga, oh nauli na bure
Chakachaka, chakachaka, oh nauli na bure

Verse 2
Kama ni vumbi litaruka na mikia watafyata
Hizi taarifa zangu na ziwafikie BASATA
Nyie ni kuku au bata? Msumeno usiokata
Kazi kufungia nyimbo, mnajua shida tunazopata?
Hamjui wajibu wenu, mngekuwa watoto nshawachapa
Na Mungu hakunyimi vyote lazima atakupa chako
Demu ana sura mbaya ila ana bonge la tako
Na wasanii wadananda, ila Shetta kazidi
Huyo ndo baba Qaila (okay!)
Gari kapewa na Chief Kiumbe utasikia, “my new ride!”
Kwenye kazi ongeza bidii
Maadui ni wengi ongeza speed
Ah, siku hizi kusoma chuo, wala sio sifa tena
Ni kama maonyesho ya urembo, miksa na u-modal
“Dada unafanya kazi gani?”
“Mi mwanafunzi wa chuo”
“Kila siku uko batani!”
“Ndo maisha yetu wanavyuo”

Chorus
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)

Mi sitaki tugombane
Nia nikurekebishe, haya mambo yaishe
Mi sitaki tugombane
Nia nikurekebishe, haya mambo yaishe

Bridge 2
Haya ni ruksa, kunyonga kidogo nipe cha Arusha, hey
Naongea na pusha, mzuka umepanda mbona unanirusha?!
The True Boy is in a building!

Verse 3
Tushazoea wasanii ndo watu wanaopenda kiki
Ila round hii, ligi serikalini
Hii serikali ya “Kazi Tu”, kwani inaendeshwa vipi?
Kila kiongozi ana muandishi, wanashindana magazetini
Huyu jamaa anajiita Dimpoz, Pose kwa Pose
Wanae wanalalamika hawamjui shemeji
Kitaani kuna tetesi mwana hapigi mechi
Mara oh jogoo hawiki, huwa haonyeshi shemeji
DJ Choka daily bata, hivi hauna familia?
Nasikia hata nyumbani huna godoro la kulalia
Wema Sepetu una mimba kweli, au ndo kiki za msimu?
Miezi tisa sio mingi, isije ikakugharimu
Na siku hazigandi tayari ushakuwa bibi
Na unakoelekea utatafuta kiki hadi kwa Fid

Chorus
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)
Haya wewe, haya wee
(Shi-shi-shika adabu yako!)

Outro
Haya ni ruksa, kunyonga kidogo nipe cha Arusha, hey
Naongea na pusha, mzuka umepanda mbona unanirusha?!
The True Boy is in a building!​
 
Mbona wanamuziki wa tanzania huwa hawa shoot muziki zao nyingi tz? alafu jana nimeskia Rayvanny akisema anataka ku relocate Kenya kwa interview ya Citizen TV...Rose Muhando ana toroka...Wema sepetu pia nimeskia akiwa na interest ya kuhamia nairobi...Diamond na mkewe wanaishi Afrika Kusini...Hivi, Bongo kunani?

Yaani wazalishaji wa mziki wa bongo unawafaninisha na walioko huko kwenu?

Unatakiwa ujue watu wa hapa kimziki wanashindana na watu wa magharibi na hili najua unalijua, si wasanii wala wazalishaji wa mziki.
 
Matatizo -
Harmonize



[Verse 1]
Alfajiri imefika anga ina ng’aa
Mvua inaanza katika ghafla tumbo la njaa
Naweka sauti kwa spika npate umbea wa Dar
Mara simu inaita, jina la anko Twaha, akisema…
“Mama yu hoi kitandani, kama si wa leo, wa kesho
Na kupona sidhani, upate japo neno la mwisho”

[Pre-Chorus]
Mi ndo mtoto wa pekee nyumbani wananitegemea
Mdogo wangu wa kike hali duni alishagaolewa
Tizama jasho langu la mnyonge, kipato hakikidhi mahitaji
Napiga moyo konde, Yarabi Mola ndo mpaji

[Chorus]
Matatizo
Matatizo yatakwisha lini?
Matatizo, kila siku mimi
Ewe Mola
Matatizo yatakwisha lini?
Japo likizo, nifurahi na mimi

[Verse 2]
Mola aliniumba na subira, imani pekee ngao yangu
Mbona nishasali sana ila mambo bado tafarani
Mama kanifunza kikabila, nikunde sanda aimu yangu
Tena nijitume sana na vya watu nisivitamani
Hata mupenzi nilonae, najua siku atanikimbia
Itanitesa ye ndo nguzo
Zile “ngoja kesho” baadae atazichoka kuzivumilia
Anakosa hata matunzo
(Ona)
Nataiwa kodi nlipopanga
Nashinda road nikianda
Nshapiga hodi kwa wanga
(Kwa kuhisi nalogwa)
Nikauza maji na karanga
Nikawa dobi kwa viwanda
Ila kote zero ni majanga
(Mtindo mmoja)

[Pre-Chorus]
Mi ndo mtoto wa pekee nyumbani wananitegemea
Mdogo wangu wa kike hali duni alishagaolewa
Tizama jasho langu la mnyonge, kipato hakikidhi mahitaji
Napiga moyo konde, Yarabi Mola ndo mpaji

[Chorus x2]
Matatizo
Matatizo yatakwisha lini?
Ewe Mola
Matatizo, kila siku mimi
Jamani matatizo!
Matatizo yatakwisha lini?
Japo likizo, nifurahi na mimi​
 
Mbona wanamuziki wa tanzania huwa hawa shoot muziki zao nyingi tz? alafu jana nimeskia Rayvanny akisema anataka ku relocate Kenya kwa interview ya Citizen TV...Rose Muhando ana toroka...Wema sepetu pia nimeskia akiwa na interest ya kuhamia nairobi...Diamond na mkewe wanaishi Afrika Kusini...Hivi, Bongo kunani?

Wasanii ambao hawashoot Tz ni wachache kushinda ambao wanashoot Tz na hata ambao hawashoot Tz ni kwa vile wanawafuata directors huko waliko na hiyo ni namna ya kupunguza gharama. Ni kama Eddy Kenzo na wimbo wa Shauri yako alivyoamua kuja kushootia Tz, akiwa anamfuata Director.

Bongo Bahati Mbaya, Tupa Shuka, One day na Tuachane ni miongoni mwa nyimbo mpya ambazo zimefanyiwa shooting Tz.
 
Zoba- Banana Zorro



Mafunzo yote! Pozi zote! Mauzo yote!
Eti binti hanitaki
Nimesubiri sana, nimechukua za uso, kuda deki!
Si uzoba huu? Aiyey!
Chorus
Subira yangu ndiyo iliyoniponza
Ngoja, ngoja, naonekana Zoba
Subira yangu ndiyo iliyoniponza
Ngoja, ngoja, naonekana mjinga
Kwa sababu nilimpenda kweli (4x)
Verse 1
Mawazo, mawazo yatawala kichwa changu, ee
Maumivu, maumivu yamevunja moyo wangu ee
Kusubiri, kusubiri, nimekusubiri mpenzi wangu ee
Lakini umekuja kuuvunja moyo wangu ee
Nilikuwa nikamili nisifanye jambo lolote nawe
Mpaka tuje tufunge ndoa, umalize na masomo
Huko umekwenda huko chuoni ee
Umebadilika mama, umebadilika, umebadilika sana
Mama yo, mama yo
Mama yo, mama yo, mama yo
Unaniona mimi Zoba, Zoo-oba ee
Chorus
Subira yangu ndiyo iliyoniponza (Imeniponza miye ee)
Ngoja, ngoja, naonekana Zoba (Zoba la mapenzi ee)
Subira yangu ndiyo iliyoniponza (Nimepotezwa miye ee)
Ngoja, ngoja, naonekana mjinga (Sijui la kufanya ee)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Kweli eee)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Nilimpenda kweli)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Nilimpenda kweli ooo)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Mama yo, mama yo)
Verse 2
Inauma sana, mpenzi wako
Wampenda sana, wamlinda sana,
Wapata habari, kumbe mwenzako
Kampenda sana, rafiki yako
Ndo maana juzi, umeacha mazoezi
Ndo maana siku hizi hutaki kuwa na mimi
Mapenzi (mapenzi) yananiumiza (yananiumiza)
Mapenzi (mapenzi) yananitesa (nitakulinda wewe)
Maumivi ya mapenzi, zaidi ya mwiba
Sikitiko la mahaba, la shinda msiba
Nitakulinda mama
Nitafanya jambo lolote kwa ajili yako nahakikisha nakuwa na wewe, wewe ee
Mama yo, mama yo, mama yo
Unaniona mimi Zoba, Zoo-oba ee
Chorus
Subira yangu ndiyo iliyoniponza (Imeniponza miye ee)
Ngoja, ngoja, naonekana Zoba (Zoba la mapenzi ee)
Subira yangu ndiyo iliyoniponza (Nimepotezwa miye ee)
Ngoja, ngoja, naonekana mjinga (Sijui la kufanya ee)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Kweli ee)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Nilimpenda kweli ee)
Kwa sababu nilimpenda kweli (Nilimpenda kweli oo)
Kwa sababu nilimpenda kweli
Mama yo, mama yo (3x)
Nitakulinda wewe, mpenzi wangu wewe
Hii ni ahadi naiweka kwako wewe
Wewe oo, wewe oo
Upo kwa ajili yangu ee
Nitasubiri siku zote
Litunze penzi langu mama
Mapenzi, mapenzi, mapenzi, mapenzi, mapenzi, mapenzi, mapenzi, mapenzi mabaya
Mapenzi mabaya, mapenzi mabaya, mapenzi mabaya, mapenzi mabaya
Lakini mpenzi wangu, mapenzi, umalize masomo tuwe wapenzi kweli
Tufunge ndo na we mama nakupenda
Nakupenda kama wali wa nazi (I love you)
Mbona mwenyewe,
Nimeamua kusubiri oo, kusubiri
Usifanye mama, nikaonekana Zoba
Nikija kungoja, siku zote mama​
 
Back
Top Bottom