Ebrahim Raisi atakumbukwa kama kiongozi jasiri zaidi wa Iran aliyeikuza nchi yake kiteknolojia

Ebrahim Raisi atakumbukwa kama kiongozi jasiri zaidi wa Iran aliyeikuza nchi yake kiteknolojia

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Pamoja na kukalia kiti cha uraisi kwa kipindi kifupi, marehemu Ebrahim Raisi wa Iran aliyekufa kwa ajali ya helkopta atakumbukwa kama mmoja wa viongozi mashujaa wa nchi hiyo.

Katika kipindi chake vitu vingi visivyotarajiwa kufanywa na nchi ambayo haijatajwa kama nchi iliyoendelea kama zile za bara la Ulaya na Marekani yaliweza kutokea. Miongoni mwao kwa kumbukumbu zangu ni haya yafuatayo.

Aliweza kuikoa nchi ya Venezuala kutokana na shida kubwa ya mafuta japokuwa ni nchi mzalishaji mkubwa wa bidhaa hiyo duniani.

Shida ya Venezuela ni kutokana na kuwekewa vikwazo na Marekani kiasi kwamba viwanda vyote vya uchakataji wa bidhaa hiyo vilikuwa kama magofu kutokana na ukosefu wa vipuri.

Wakati wa uongozi wa Ebrahim raisi alifanikisha malengo ya mtangulizi wake kwa kuipelelekea mafuta ya msaada nchi hiyo sambamba na vipuri vya kufufua viwanda vyake. Meli zilipoleka misaada hiyo zilipitia ugumu wa hali ya juu katika safari,lakini hata hivyo kwa kutumia mbinu tofauti hatimae ziliweza kufikisha mafuta na vipuri.

Katika kipindi hicho hicho cha Ebrahim ilikuwa ni kisa mkasa.Meli ya Iran ikizuiwa kwa sababu yoyote ile na wao wanazuia meli ya taifa lililongoza kwenye utekaji wa meli zao.

Kipindi hicho kilishuhudia nchi hiyo ikiuza vifaa vya kivita vilivyotengenezwa Iran kwa mataifa mengine na hasa taifa kubwa la Urusi katika kuiadhibu Ukraine. Ukali wa droni za Iran aina ya shaheed zilililala mikiwa mno na Ukraine kuonesha kuwa zilifanya kazi zilizokusudiwa. Hilo halikuwa kufikiriwa kutoka kwa nchi kama Iran.

Kubwa kuliko yote ni ujasiri wa kuipiga Israel kwa makombora ya masafa marefu ambayo yaliweza kutua kwenye uwanja mkubwa wa kijeshi wa Israel na maeneo mengine na kuleta madhara na muadhara kwa nchi hiyo inayoogopewa na mataifa karibu yote ya kiarabu.

Ujasiri wa kuipiga Israel ulikuja baada ya Israel kuyashambulia na kuyaharibu majengo ya ubalozi wa Iran nchini Syria
 
Wananchi wa Iran waliumizwa sana kipindi chake kuliko wakati mwingine wowote. Mtu anajiita "mchinjaji wa Tehran"; sio mchinja nguruwe! Bali muuwaji wa wenye mtazamo kinzani na genge lao wanavyoamini!
 
Wananchi wa Iran waliumizwa sana kipindi chake kuliko wakati mwingine wowote. Mtu anajiita "mchinjaji wa Tehran"; sio mchinja nguruwe! Bali muuwaji wa wenye mtazamo kinzani na genge lao wanavyoamini!
Daaah! Kubwa la magaidi ya kidini
 
... makundi ya kigaidi yalifadhiliwa sana na serikali ya Iran kipindi chake kuliko wakati mwingine wowote.
makundi ya kigaidi kwa mtazamo wa nani.Wengine wanayaita vikosi vya ukombozi wa maeneo yao.
 
Pamoja na kukalia kiti cha uraisi kwa kipindi kifupi, marehemu Ebrahim Raisi wa Iran aliyekufa kwa ajali ya helkopta atakumbukwa kama mmoja wa viongozi mashujaa wa nchi hiyo.

Katika kipindi chake vitu vingi visivyotarajiwa kufanywa na nchi ambayo haijatajwa kama nchi iliyoendelea kama zile za bara la Ulaya na Marekani yaliweza kutokea. Miongoni mwao kwa kumbukumbu zangu ni haya yafuatayo.

Aliweza kuikoa nchi ya Venezuala kutokana na shida kubwa ya mafuta japokuwa ni nchi mzalishaji mkubwa wa bidhaa hiyo duniani.

Shida ya Venezuela ni kutokana na kuwekewa vikwazo na Marekani kiasi kwamba viwanda vyote vya uchakataji wa bidhaa hiyo vilikuwa kama magofu kutokana na ukosefu wa vipuri.

Wakati wa uongozi wa Ebrahim raisi alifanikisha malengo ya mtangulizi wake kwa kuipelelekea mafuta ya msaada nchi hiyo sambamba na vipuri vya kufufua viwanda vyake. Meli zilipoleka misaada hiyo zilipitia ugumu wa hali ya juu katika safari,lakini hata hivyo kwa kutumia mbinu tofauti hatimae ziliweza kufikisha mafuta na vipuri.

Katika kipindi hicho hicho cha Ebrahim ilikuwa ni kisa mkasa.Meli ya Iran ikizuiwa kwa sababu yoyote ile na wao wanazuia meli ya taifa lililongoza kwenye utekaji wa meli zao.

Kipindi hicho kilishuhudia nchi hiyo ikiuza vifaa vya kivita vilivyotengenezwa Iran kwa mataifa mengine na hasa taifa kubwa la Urusi katika kuiadhibu Ukraine. Ukali wa droni za Iran aina ya shaheed zilililala mikiwa mno na Ukraine kuonesha kuwa zilifanya kazi zilizokusudiwa. Hilo halikuwa kufikiriwa kutoka kwa nchi kama Iran.

Kubwa kuliko yote ni ujasiri wa kuipiga Israel kwa makombora ya masafa marefu ambayo yaliweza kutua kwenye uwanja mkubwa wa kijeshi wa Israel na maeneo mengine na kuleta madhara na muadhara kwa nchi hiyo inayoogopewa na mataifa karibu yote ya kiarabu.

Ujasiri wa kuipiga Israel ulikuja baada ya Israel kuyashambulia na kuyaharibu majengo ya ubalozi wa Iran nchini Syria
Umesema vizuri japo ni kweli zaidi kuwa credit pekee kwa marehemu Ibrahimu Raisi ni kufungua zaidi sera ya mambo ya nje ila hayo mengine yote hana credit mengi ni longterm strategy za Iran kilichomkuta Venezuela ndio alihangaika nacho Ahmad Nejad akiwa raisi na wao kama taifa wakaweka nadhiri ya kuhakikisha wanapata technolojia ya oil refinery na kuhakikisha hawawi tegemezi
Kwa wairan huwa wanapanga na kwa kutumia vyuo vyao vikuu na decree ya Ayatollah kila mwaka wao mpyaa ukianza hawafati hizi kalenda zetu wanakuwa na maazimio ya jinsi gani ya kupunguza utegemezi wa technolojia au bidhaa toka nje na ndio maana wanaenjoy true freedom.
 
Umesema vizuri japo ni kweli zaidi kuwa credit pekee kwa marehemu Ibrahimu Raisi ni kufungua zaidi sera ya mambo ya nje ila hayo mengine yote hana credit mengi ni longterm strategy za Iran kilichomkuta Venezuela ndio alihangaika nacho Ahmad Nejad akiwa raisi na wao kama taifa wakaweka nadhiri ya kuhakikisha wanapata technolojia ya oil refinery na kuhakikisha hawawi tegemezi
Kwa wairan huwa wanapanga na kwa kutumia vyuo vyao vikuu na decree ya Ayatollah kila mwaka wao mpyaa ukianza hawafati hizi kalenda zetu wanakuwa na maazimio ya jinsi gani ya kupunguza utegemezi wa technolojia au bidhaa toka nje na ndio maana wanaenjoy true freedom.
tuombe hata raisi mpya awe na moyo kama wa Ahmed Nejad na marehemu Ebrahim Raisi.Au awe shujaa kuliko hao.
 
Atakumbukwa kwa kutoa hukumu ya kifo kwa maelfu ya wafungwa wa iran na waandamanaji
Ni mahakama ya Iran ingawaje na yeye aliridhia kulingana ukubwa wa makosa waliyotenda wahalifu.
 
tuombe hata raisi mpya awe na moyo kama wa Ahmed Nejad na marehemu Ebrahim Raisi.Au awe shujaa kuliko hao.
Ni kweli kwa system ya iran mirengo ni miwili reformist vs conservative
Ahmad Nejad na Raisi wanatokea mrengo wa conservative ila watu kama Rouhani au Khatami walitokea mrengo wa reformist ila mwishowe wote ni sawa hawa reformist wanachofanya ni kupunguza tu kuongea kwa ukali zaidi ila sera na siasa huwa zinakuwa ni zile zile
 
Ebrahim Raissi was a ruthless tyrant who prisided over the massacre of thousands of innocent Iranians and death is the only thing he deserved.

Now that he is perpetually gone maybe this will present a rare opportunity for the limbless people of Iran to have a respite albeit not for foreseeable future.
 
Hayo yote akafa akiwa kwenye helikopter ya miaka 40 iliyokosa vipuri, duh.
 
Hayo yote akafa akiwa kwenye helikopter ya miaka 40 iliyokosa vipuri, duh.
Ni kipimo cha ushujaa nacho.Hakuogopa kupanda helikopta.Kuna viongozi katika dunia ambao kwa kujipenda na kuogopa kufa basi wanekataa kupanda helikopta aina hiyo.
Kiongozi kama Mohammed Sleman wa Saudi Arabia kwa jeuri yake nadhani hata kuonana na maraisi wa dunia basi huwa anachagua.
Au yule kiongozi wa Ethiopia alipokwenda mazikoni London,hakukubali kupandishwa basi moja na maraisi wenzake wa kiafrika.
 
Ni kipimo cha ushujaa nacho.Hakuogopa kupanda helikopta.Kuna viongozi katika dunia ambao kwa kujipenda na kuogopa kufa basi wanekataa kupanda helikopta aina hiyo.
Kiongozi kama Mohammed Sleman wa Saudi Arabia kwa jeuri yake nadhani hata kuonana na maraisi wa dunia basi huwa anachagua.
Au yule kiongozi wa Ethiopia alipokwenda mazikoni London,hakukubali kupandishwa basi moja na maraisi wenzake wa kiafrika.
Hahah sasa ukifa ushujaa unatoka wapi hapo? Yeye ni kiongozi wa taifa, ana wataalam na washauri, hawa walipaswa kufanya kazi yao kabla kiongozi hajaingia au kusafiri na chombo kibovu. Kufa siyo ujasiri, ni safari yetu sote hakuna shujaa wala mzembe kufa ni kufa tu.
Ila yeye kwa nafasi yake, alikosea.
 
Atakumbukwa kwa kuwapoteza wanawake wengi waliopinga uvaaji wa hijabu
 
Back
Top Bottom