Ebu tujadiliane hili suala mara moja wakuu

Ebu tujadiliane hili suala mara moja wakuu

Yofav

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
4,236
Reaction score
7,583
Naishi Hapa Dar mtaa fulani, Nina kama mwaka hivi sasa, Na mahali nilipopanga ni pana mazingira mzuri kiasi chake maana mwenye nyumba wetu ni mtu pia anaependa mali zake hivyo basi hayupo nyuma kutuhakikishia tunapata yale mahitaji ya msingi Kama maji kwa haraka zaidi na marekebisho ya dharura.

So, issue ipo hivi mtaro unaotumika kupitisha maji machafu katika eneo letu (namaanisha huu mtaro upo kwa nje ya geti ambapo umepakana na barabara) Ni mtaro unaotumika na watu wengi ikiwemo hata majirani zetu, So ni mtaro ambao unasaidi sana hapa kitaa maana unayatoa maji kuyaelekeza ulipo mto wa maji.

Mwenye nyumba wetu aliutengeneza mtaro na kuuweka wa kisasa zaidi pale yalipo mazingira yetu lakini kule maji yanapoelekea umbali kama hatua 100 hivi ni eneo wanaloishi watu wengine ila ni kidizain fulani kama hapajatengenezwa kisasa bali pako hovyo jambo linalofanya maji yale kushindwa ku-flow vizuri na kutuama.

Sasa jambo ambalo limenishangaza ambalo ninahitaji tulijadili hapa ni kwamba hii issue imefika serikalini according to mwenye nyumba so inavyodaiwa viongozi wa mtaa wamekaa kikao so sisi watu wote ambao tunahusika kutumia ule mtaro wanapaswa kuchanga pesa ule mtaro utengenezwe kisasa zaidi.

Sikupinga kupata taarifa hiyo maana jambo la kimaendeleo ni vizuri kushiirikiana ila taabu imekuwa kwenye gharama ambazo tunapaswa kuchangia, According to wao ni kwamba tunaotumia huo mtaro tupo 82 so ili tupate budget ya kuutengeneza huo mtaro basi kila mmpangaji anatakiwa kutoa sh.36,000/=, Jambo hili limeleta utata kwa kuwa baadhi ya wapangaji wanahoji kwamba wao wanapita tuu na walipanga nyumba na kufuata maelekezo ya mwenye nyumba wapi wamwage maji taka, So jukumu la masuala ya maji yataelekea wapi au mtaro una shida gani ni issue ambayo inamuhisisha mjenzi (mwenye nyumba)

Then kingine ni hiyo gharama ambayo inapaswa kuchangiwa, Imagine 36,000 kwa kila mpangaji kweli!!? Na hali hii?

Ebu wataalamu mnijuze kwa issue kama hii imekaaje na mimi nipate kuelewa, Hili jukumu ni la mpangaji au mwenye nyumba maana mwenye nyumba anasema yeye sio mmwagaji maji wanamwaga wapangaji, Na mpangaji anahoji kwamba inawezekanaje mjenzi ajenge nyumba asitengeneze mazingira yanayoeleweka ya kumwaga maji ikiwa kama jukumu lake?

Kwa mimi sijataka kupinga suala hili maana ni vizuri kusaidiana hata kama tunapita ila hiyo gharama kiukweli ni kubwa ni heri wangesema hata 10,000/= kwa kila mpangaji.

Uzi umeisha.
 
Kama nyie ni walipa kodi basi jukumu la kujenga miundombinu ni la serikali
 
Hapo ni suala la kujiongeza tu, Mtaro endapo unatuamisha maji maaana yake eneo lenu lina Mbu wa Kutosha kwa hiyo Maralia haiwaishi na hata dawa kama Rungu, Hit nk kwako ni kila wiki elfu 10 inatoka. Pili harufu mbaya hapo Mtaani kwenu imejaaaa na muda wooote matumbo yamejaaa gesi kwa harufu mbaya ya Maji ya Mtaro watoto wanacheza humo humo na kwa hiyo magonjwa ya Kichocho, Minyoo, Kuhara na mwishowe Kipindupindu hapo Mtaaani kwako ni kawaida. Tatu Mazingira hayo yanakufedhehesha kama Mpenda ustaarabu na kukunyima amani kukaribisha ndugu, jamaa na marafiki maaana mwisho wa siku wataona kama unaishi dampo.
Jiulize, .elfu 36 unayodaiwa na hizo kadhia kipi ni kipi?? Wakati mwingine tutumie akili kubwa kutanzua yanayotuzonga kuliko kutanguliza kujua kwiiiiiiingi na harakati nyiiiiingi? Hiyo 36 unayopiga kelele ni gharamaa ya dawa za mbu unazonunua ndani ya mwezi 1 kutokana na maji ya mtaro huo kufuga mbu wanaokuzonga?? Je umejitibia maralia mara ngapi na kiasi gani?? Je, kadhia ya harufu mbaya imekuathiri kiasi gani???
Anyway subirin Serikali itatengeneza mwaka 2026
 
Wameondoa tozo na sisi tumekuja na mbinu mbadaLa ya kupiga pesa
hahaha
Hapo ni suala la kujiongeza tu, Mtaro endapo unatuamisha maji maaana yake eneo lenu lina Mbu wa Kutosha kwa hiyo Maralia haiwaishi na hata dawa kama Rungu, Hit nk kwako ni kila wiki elfu 10 inatoka. Pili harufu mbaya hapo Mtaani kwenu imejaaaa na muda wooote matumbo yamejaaa gesi kwa harufu mbaya ya Maji ya Mtaro watoto wanacheza humo humo na kwa hiyo magonjwa ya Kichocho, Minyoo, Kuhara na mwishowe Kipindupindu hapo Mtaaani kwako ni kawaida. Tatu Mazingira hayo yanakufedhehesha kama Mpenda ustaarabu na kukunyima amani kukaribisha ndugu, jamaa na marafiki maaana mwisho wa siku wataona kama unaishi dampo.
Jiulize, .elfu 36 unayodaiwa na hizo kadhia kipi ni kipi?? Wakati mwingine tutumie akili kubwa kutanzua yanayotuzonga kuliko kutanguliza kujua kwiiiiiiingi na harakati nyiiiiingi? Hiyo 36 unayopiga kelele ni gharamaa ya dawa za mbu unazonunua ndani ya mwezi 1 kutokana na maji ya mtaro huo kufuga mbu wanaokuzonga?? Je umejitibia maralia mara ngapi na kiasi gani?? Je, kadhia ya harufu mbaya imekuathiri kiasi gani???
Anyway subirin Serikali itatengeneza mwaka 2026
mkuu umesoma vizuri ukaelewa? me, nikitoa hiyo 36 wengine hawana uwezo wa kutoa so, issue ni kwamba viongozi wanatakiwa wakae wajadiliane kiwango ambacho wote tunaweza kutoa bila malumbano hiyo 36 kuna wengine hapahapa mtaani kwao ni kodi ya mwezi
 
Inategemea na aina ya ujenzi wa huo mtaro; kama mtashindwa kutoa inabidi nyie muwe vibarua kwa mkandarasi
 
Kwani hayo maji anamwaga mwenye nyumba au nyinyi


Kamwageni mnapopajua msilete hio kadhia
 
Mwenye nyumba amewajengea miundombinu, nyie ndo mnaitumia.

Unadhani ni sahihi mwenye nyumba atoe hela ya kutengeneza mtaro ilihali wanaomwaga maji ni wapangaji wake?

Kuna wakati mnajiongeza tu. Kama 36k ni kubwa, ombeni mlipe kwa awamu hata 4.

Kwenye maendeleo kuna wengine inabidi muumie.
 
Back
Top Bottom