Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Magufuli na Polepole.

Hawa watu wawili walitushambulia sana eti mafisadi yamewakimbia na yamehamia Chadema. Sisi kweli kama Chadema tulibanwa sana kuhusu Lowassa ila tulijikongoja tuu. Kiuhalisia mwaka 2015 tulipoteza uhalisia wetu kichama ingawa Lowassa kweli alikuwa mtu wa watu. Tulilazimika kuwafanya wengine kukaa kimya maana kama chama tuliua agenda zetu kuu. Hatimaye sasa tutapumua.

Nimeshangazwa sana na mapokezi ya kifalme aliyopewa Lowassa huku serikali kuu zaidi ya nusu wakihamia Lumumba kwenda kumpokea mkubwa yule. Ni kwa mara ya kwanza kuona mtu akipokewa na viongozi wote wakuu wa chama na serikali. Mtu ambaye watu hao hao walidai kawakimbia! Leo wao ndiyo waliomkimbilia! Mbaya zaidi Magufuli anampokea Lowassa huku akiwa kasimamiwa na zee la mipango aka Rostam Aziz. Dah kweli dunia ina mambo.

Lowassa najua amerudi CCM ili kulinda fursa zake kibiashara pamoja na hatima yake ya uzeeni. Ni hayo tu.

Nasubiri kuona sasa mapovu ya kina Polepole na Bashiru baada ya madon kujihakikishia kuwa sasa wamemzunguka mkubwa wao. Acha kabisa siasa hizi za kibongo. Pia nasubiri neno la Slaa (Najua hatosema chochote maana anatumikia)
Mgonjwa amepona ama amevishwa ponpon?
 
Tangu jana mpaka muda vijana wa bavicha wamepandisha nyuzi nyingi sana kumuhusu Lowassa,
Kuhama kwake wengi wanajifanya kutoshangazwa wala kushitushwa na uondokaji wake.
Lakini kitendo cha kufungua nyuzi mfululizo linatoa picha ni jinsi gani hili jambo limewauma kuliko hata shambulizi la Lissu kupigwa risasi,

Shambulizi baya mlengaji amepiga pigo moja lenye uzani na uchungu mwingi,kila wakikumbuka walivyomtetea na kutukana watu,walivyodeki barabara,waliamua kumtosa mtu muhimu dkt slaa kwa mustakabali wa matumbo yao na tamaa ya kuingia ikulu kwa kutumia silaha yeyote iliyopo mbele.

Ama kwa hakika vijana wamechanganyikiwa ndio kwanza hakusubiri mbowe atoke gerezani, ndio kwanza ametuonyesha Lowassa alikuwa peke yake ndani ya chadema.
Kama alivyoibuka ikulu bila itelejensia kujua ,ndivyo alivyopata mualiko katika ufunguzi wa maktaba ya chuo kikuu ,na ndivyo alivyoondoka jana na kuibukia Lumumba.
Alishawambia mkiona mtu anahama chama vuteni shuka zenu mjifunike mpaka usoni.
Bavicha wamepaniki rasmi wameamua kurudisha jina lake pendwa fisadi wakati alipokuwepo huko walimtetea kwa kila hali!
Vijana mmepaniki!
 
Hapana Retired; usimuone hivi Lowassa na nadhani si haki kumuona hivyo. Wale wote waliomuunga mkono na kumtumia alipokuja inapaswa kumshukuru tu na kumtakia kila la kheri. Haya mengine si ya lazima. Sidhani kama kurudi kwake ni jambo la kushangaza au kushtua vile. Kwamba alibakia kwa miaka mitatu lazima mumpe hongera na shukrani zake.
Nimeandika kuwa Lowasa kuja CDM huwezi kusema ni hasara. CDM ilinufaika sana na ujio wake.. wabunge, madiwani, wenyeviti/mitaa/vitongoji, Chama kikuu cha upinzania. ruzuku, to mention but a few.
Hoja yangu: Mtu mzima na umri wake unakuwa na msimami thabiti! Unaangalia kitendo kipi nikifanye na kipi nisikifanye kwa heshima yangu muda uliobaki. Alichokifanya kinampa "umalaya" wa aina fulani ya kisiasa. Angelikuwa in his thirties, even forties ningelimuunga mkono kuwa still he has time ngoja aangalie opportunities. Sasa anatafuta kweli opportunities? NO!
Labda for a rescue of SIOI SUMARI, mkwe wake! Hilo huwezi kumlaumu sana maana mpendwa wake yuko jela anateseka. When an avenue for rescue comes, you grab it! at the peril of your honor!
 
kura za uraisi nipatie mimi na wabunge wengi wa ccm..huyu mamvi huwa simwelewi kabisa.
alimzuia mke wake asiteuliwe viti maalum,akamzuia mtoto wake asigombee kwenye marudio ya uchaguzi kumbe alikuwa na la kwake jambo.
Unadhani ana njaa ya pesa kama we!!
 
Mimi nimeshangaa kuona mpaka Uncle amampokea huyo kinyonga, Kiukweli mimi naona kurudi kwake jamaa hakuna nia njema hata kidogo wacha tusubiri 2020
 
Mbona kila anayeandika humu anaona negative impact kwa ccm tu,vipi negative impact kwa CDM mbona haziandikwi au kusemwaswmwa sana
Si useme wewe sasa !.

Tawala za ki Africa zinatumia mbinu chafu kwa wapinzani wao. Badala ya kubadilisha sera na uongozi kuvutia wapiga kura, zenyewe hutumia vyombo vya Dola kudhibiti wapinzani wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ndo udhaifu wa upinzani CDM na hichi chama kife tu ktk raman za siasa Tz. HICHI CHAMA HAKINA HATA MTU MWENYE SIFA ZA KUWA RAISI.
 
Kama hilo uliliona mkuu nakupa big up. Lakini bado hatuko salama tumeonesha Chadema tunakumbatia ufisadi ukiwa tu na maslahi.
Damage 2020 huyu jamaa ataongea sana atataja hata kwa exagration kuwa ndani ya CDM kuna uozo ikiwemo hati miliki ya vyeo kama mwenyekiti, Ukanda , Ruzuku nk
Kwa ma Ccm mapokezi yao ni yale ya "The spy is Back" atakaa tu akila popcorn movie ikiendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani ana Uwezo wa kuongea ,hujaona jana kaongea Sentensi moja tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom