Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa Amerejea Rasmi CCM Leo.

Amepokelewa Lumumba Makao Makuu Madogo Ya Chama Cha Mapinduzi Na Katibu Mkuu Dr Bashiru Ally.

Aidha, katika mapokezi hayo walikuwepo Rais Magufuli, Rostam Aziz, Mzee Phillip Mangula, Waziri Mkuu Majaliwa Kassim, Humphrey Polepole n.k

Habari zaidi...

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amerejea Chama cha Mapinduzi (CCM) Ijumaa, nchini Tanzania. Lowassa alikuwa mgombea wa kinyang’anyiro cha urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na vyama vinavyounda umoja wa UKAWA katika Uchaguzi mkuu 2015.

Kurejea kwa Lowassa kulikuwa kukitabiriwa na baadhi ya watu, lakini mara kadhaa Lowassa alikanusha kuwa anampango wa kurudi katika chama hicho.

Vyanzo vya habari vinasema hatua hiyo imewashitua watu wengi, kwa sababu ya kile ambacho kilisababisha yeye kuhama chama hicho.

Lowassa baada ya kuitumikia CCM kwa kipindi kirefu alikihama chama cha hicho kufuatia mvutano uliotokea baada ya kutoidhinishwa na chama hicho kuwa mgombea wa urais.

Sherehe za mapokezi yake wakati akirejea rasmi Ijumaa zilifanyika katika ofisi ndogo ya CCM iliyoko Lumumba Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa chama hicho John Magufuli.

Lowassa mara kadhaa amefanya mazungumzo na Rais John Magufuli, Ikulu ya Tanzania.

Kumekuwa na wimbi la wanachama wa upinzani kuingia CCM tangu Magufuli achaguliwe 2015, kitu ambacho kimekuwa kikizungumziwa katika duru za siasa kwamba kinadhoofisha upinzani.



View attachment 1035375
View attachment 1035459
View attachment 1035448

Unaweza soma pia:

Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM - JamiiForums

Edward Lowassa: Wanaodhani nitarudi CCM wanapiga porojo na kuota ndoto - JamiiForums

Lowassa hana namna zaidi ya kuipigia magoti CCM, Mkwewe Sioi Sumari mpaka sasa yupo lockup - JamiiForums
Link Godbless Lema: Kuna siku mtavililia vyama vya Upinzani viwasemee hamtavipata. - JamiiForums

Link2. Lowassa kurejea CCM: CHADEMA imepata penati dakika za lala salama! - JamiiForums

Je Dr. Mihogo bin Silaha atasutwa na nafsi yake?

Je Mbowe na Sumaye watamfuata Lowassa kwenda "kuunga mkono" juhudi za mwenyekiti za kuwanyoosha na kuwanyonga wanyonge?
 
Kwanza kbs lazima tukubariane JPM ameshinda kwa sasa. Kingine Upinzani ktk Africa yetu una gharama kubwa sna za kulipa ambayo Mzee Wetu Lowasa ameshindwa fikiria khs mkwewe mwaka na zaidi yupo Jera ambae nina hakika baada mienzi kadhaa tu atakuwa Huru tusisahau khs mdogo wa swaiba wake Rostam Aziz na kesi ya ujangili iliyochukua mwenzi mmoja kuisha baada ndugu Rostam kwenda kumsalimia mkuu mgogoni lipo pia la kumkomoa Mzee wa msonga maana chini kapeti Mzee wa msonga na Jamaa wa Magogoni ss hv wanaishi sna kichina...
tapatalk_1551511150075.jpeg
tapatalk_jpeg_1551473509930.jpeg
D0lRIbbXgAAk7qc.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee Wa Msoga Alishindwa Nini Kumpa Jamaa Wa Enzi Za Boys To Men Mpaka Akachafuliwa Na Yale Matope? Rafiki Yake Angekuwa Magogoni Mzee Wa Msoga Angejilimia Nanasi Zake Fresh Tu Bila Stress Za Kuchafuliwa Legacy Yake.
 
Ni vema kupambanua kati ya kumpokea
Mheshimiwa Lowasa Chadema na kumteua kuwa mgombea wa Urais. Kumpokea chamani halikuwa kosa, lakini kumpa nafasi ya uongozi lilikuwa kosa kubwa sana.

Kuna mhimili wa maadili unaosema "the end does not justify the means". Lilikuwa kosa la msingi kwa Chadema kutaka kuchukua Urais kwa njia yoyote. Kumsimamisha mtu ambaye walikuwa wanadai ni fisadi kulitoa ujumbe kwamba wao hawana msimamo hata kidogo.

Kosa kubwa huleta madhara makubwa. Chadema ilijiimarisha kwa "narative" ya kupinga ufisadi. Baada ya kumtaka yule waliyekuwa wakidai ni fisadi papa kuwa mgombea wa Urais, wamejibomolea hiyo narative. Hawana narative sasa. Matokeo yake ni msambaratiko ambao uko sasa.
 
Mwanzoni CDM walikuwa wanasema fisadi papa 2015 wakazunguka nchi nzima kumsafisha. Upande wa pili CCM jangwani pale Kikwete akasema fisadi ameenda upande mwingine leo hii mtu asiye wataka mafisadi kampokea bira shida na kamsafisha.
Ama kweli huyu mzee yuko na akili sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanzoni CDM walikuwa wanasema fisadi papa 2015 wakazunguka nchi nzima kumsafisha. Upande wa pili CCM jangwani pale Kikwete akasema fisadi ameenda upande mwingine leo hii mtu asiye wataka mafisadi kampokea bira shida na kamsafisha.
Ama kweli huyu mzee yuko na akili sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Katubu bin kaungama karudi nyumbani huku akiangaliwa haswa ni mwana kondoo au igizo.
 
Ungekuwa unafuatilia ninachoandika humu usingeandika huu upuuzi wako. Siku zote huyu akiwa ccm au Chadema kwangu alikuwa ni fisadi tu na kumkaribisha chadema ilikuwa ni makosa makubwa sana. Pole pole wa chakubanga anamuita hadi malaya wa kisiasa.

Hana ukiboko wowote huyu fisadi mchumia tumbo anayejali tumbo lake.

Kweli Lowassa kavuruga watu.
Ha ha ha ha Lowassa kiboko yao na kawaweza.

Chadema walimwita Fisadi weeeee akahamia kwao...wakalamba matapishi na wakanywea balaa.
We fikiria Lissu na mdomo wake ule akanywea.
Lema na mdomo wake ule na viapo vyote kuwa ni haki toka kwa Mungu kumzomea Lowassa akanywea na kunyenyekea.

Alivoenda Chadema , CCM wakamsema weee, kina Polepole wakamwita malaya na fisadi wee..
Sasa karudi. Ccm wote ziii...Polepole kanywea..ccm imenywea.

Hivi sasa ngoma droo. Hakuna ccm wala chadema anayeweza muita Lowassa fisadi. Wamebaki kama BAK na mwenzie wanavyotifuana kwa kitu kile kile...

Lowassa kiboko..jamaa korofi sana ha ha ha
 
Mi simlaumu huyu mzee.Hivi mnadhani mwanasalsafa mmoja alisemaga siasa ni mchezo mchafu alikosea?kumbukeni Mareham Chief Abdala Saidi Fundikira alikuwa waziri wa sheria wa kwanza baada ya uhuru na walisoma na Nyerere Makerere.
Na ndio muasisi wa vyama vya upinzani kupitia UMD lakini Nyerere alivofariki alirudi CCM kwa madai muasisi mwenzake wa Uhuru amefariki hivyo amerudi kumuenzi.
Msije shangaa Mbowe akirudi CCM kumbukeni baba yake marehem Haikaeli Mbowe walikuwa waasisi wa Uhuru na kina Lazaro Bomani na Rupia na ndio walikuwa wanampa Nyerere nauli ya kwenda UNO
Hiyo ndio inaitwa siasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amefika mwisho wa siasa anaona afadhali azikwe kwa heshima ya chama na serikali.
 
Tupo kwenye kipindi kigumu kidemokrasia na jinsi watanzania wengi wasivyokuwa wapiganaji, wengi watajiunga na ccm kwasababu ya udhaifu wao.
 
Wanajamvi kumekuwa na sherehekeo katika maeneo mawili ya kisiasa kwa Nchi yetu, Upinzani na Chama Tawala. Kutokana na hatua ya Edward Ngoyai Lowasa kurudi Ccm.

Mimi binafsi naliona Jambo hili kwa mtazamo mwingine Ccm ilikuwa na ugonjwa Mbaya Sana wa ufisadi na uwizi wa Mali za umma ukiongozwa na mdudu Mbaya ENL.!
Baadae kama kwa bahati Njema wazazi(wananchi)wakapiga kelele wakisaidiwa na majirani (upinzani) Mgonjwa akajitambua (Ccm) akaanza kujikongoja ahsante (JM.kikwete). Hatimaye wakapata dawa ya kutibu tatizo baadhi ya bakteria wakafa. Kirusi mkuu na chanzo cha tatizo akahamia kwa jirani kama kipindupindu. Baada ya jirani kula matapishi ya mgonjwa.! Naye jirani (Upinzani) akaondoka katika hali bora ya Afya aliyokuwa nayo akaanza kuugua ugonjwa uleule wa Kirusi kilekile ENL. Akaanza kutoa harufu ileile jamii (wananchi) wakaanza kukerwa na harufu ile wengi wakaondoa makazi yao jirani na Jirani hao.! Baada ya miaka kadhaa hali ikawa mbaya zaidi kwa jirani (upinzani)
Ccm akiwa amepona ananawiri na kupendeza kila mtu anamsifia kwa ubora wake.
Bahati mbaya iliyoje Mdudu yule yule ENL baada ya kuharibu kule, amefanikiwa kutoka na kurudi tena kwa Mgonjwa aliye pona na akanawiri na kupendeza. Bila shaka safari hii hata utafunaji wake utakuwa mkubwa zaidi na

" anguko la safari hii la CCM litakuwa kubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote"

Sabbu mdudu huyu ameshakuwa sugu na amejifunza mbinu mpya za kukabiliana na dawa zote na bila shaka ataanza kushambulia kutokea ndani sio nje kama ilivyokuwa awali, Biblia inasema


"Shetani akimtoka mtu huenda akitangatanga jangwani kutafuta makazi akikosa husema ntarejea nyumbani kwangu. Akirudi akakuta nyumba ni safi huleta shetani wenzie saba na hali ya mtu huyo huwa mbaya mara saba zaidi ya ile ya awali"

Poleni sana Ccm poleni sana Watanzania poleni sana wote tulio anza kuona matumaini kwa Nchi yetu, kurejea kwa Edward Ngoyai Lowasa Ccm ni msiba mwingine kwa CCM na Taifa letu kwa Ujumla.
Tuliokuwa na matumaini na Ccm taratiibu tunaanza kujiweka pembeni. Yale maumivu tuliyo pitia awali hatustahili kuyapata tena.

Poleni wana Ccm, Poleni Watanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mzee slaaa alimfananisha lowasa na Choo cha kiafrika, Sasa alichoo kiita Choo boss wake slaa (jiwe)anakiita lulu.

Swali ni slaaa alikikimbia choooo leo choo kimemfuata mzee slaa.atakikimbia Tena hicho choooo. ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanajuana vyema wale wote.kiufupi tz hakuna upinzani...
kapewa ubalizi Slaa na ccm na kakubali ujuwe huyo tayari ni ccm... lowasa naye anarudi...
walikula pesa nzuri sana kipindi cha uchaguzi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom